MWANDISHI: NYEMO CHILONGANIEndelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com“Utamuweza lakini?” Mwanaume mmoja aliyekuwa na misuli alimuuliza Dominick ambaye alikuwa amevaa miwani mikubwa iliyokuwa na rangi nyeusi.
“Kwa nini nisiweze. Ebu niangalie, unanionaje?” Dominick alimuuliza kijana yule.
Muziki bado ulikuwa ukiendelea katika klabu hiyo ya Raspinho, taa hafifu ndizo ambazo zilikuwa zikiwaka. Wanawake mbalimbali wazuri ambao kazi yao ilikuwa ni kujiuza walikuwa wamesimama pembeni huku wakijaribu kufanya matangazo kwa kila mvulana ambaye alikuwa akiwaangalia katika klabu ile.
“Nakuuliza tena..utaweza?” Mwanaume yule bado alikuwa akimuuliza Dominick.
“Nitaweza bwana. Mimi ndiye Maliki Mtanga. Nimezaliwa kwa ajili ya kufanya ngono tu” Dominick aliongea huku akijisifia.
“Kumbe umetokea Tanga”
“Ndio. Kule Handeni”
“Basi wewe utakuwa unaweza. Manake mwanamke mwenyewe hataki niwaletee vijana legelege. Kama ndio hivyo basi poa” Mwanaume yule alimwambia Dominick pasipo kumfahamu kutokana na uhafifu wa taa pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa.
Dominick hakuwa kabisa mtu wa klabu, ila alifika mahali hapo kwa ajili ya kazi kubwa ambayo alikuwa nayo mbele yake. Alizifahamu vilivyo tetesi alizokuwa nazo Bi Magdalena, alifahamu vilivyo kwamba mwanamke huyo alikuwa na pepo la ngono.
Hakuwa akimpenda, lakini alitakiwa kufanya hivyo kwa kuwa alihitaji sana kukamilisha kile ambacho alikuwa amekipanga. Kamwe Dominick hakuwa mtu wa pombe lakini siku hiyo pombe aina ya Kilimanjaro ilikuwa katika kaunta huku akijfanya anainywa.
“Huyo hapo. Ngoja nikaongee nae” Mwanaume yule alimwambia Dominick katika kipindi ambacho Bi Magdalena alikuwa akiingia pamoja na binti yake, Sara.
Dominick akaonekana kutabasamu. Yule mwanaume ambaye alionekana kuwa mlinzi wa klabu ile mule ndani akaanza kumfuata Bi Magdalena na kisha kuanza kuongea nae. Walitumia dakika kumi kuongea, mwanaume yule akaanza kumrudia Dominick huku akionekana kutabasamu.
“Vipi?” Dominick alimuuliza huku akiwa na shauku ya kutaka kufahamu.
“Tayari. Kila kitu kipo fresh ingawa alikuwa akikaza. Si unajua hataki skendo” Mwanaume yule alimwambia Dominick
“Kwa hiyo fresh kabisa?” Dominick aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Fresh. Nilipomwambia kwamba umetoka Tanga, alipagawa kinoma”
“Kweli?”
“Ndio hivyo”
“Kwa hiyo nini kinafuata?”
“Ngoja kwanza. Kila kitu kitakuwa fresh”
Dominick akaamua kutulia, akaangalia saa yake, saa ilikuwa ikionyesha kuwa tayari ilikuwa saa saba na nusu usiku. Aliendelea kuzuga kunywa pombe ile mpaka saa nane ilipotimia na Bi Magdalena kumtuma mwanaume yule kumuita Dominick ambaye alikuwa amejitambulisha kwa jina la Maliki.
Kwa haraka haraka Dominick akainuka na kuanza kuelekea kule alipokuwa Bi Magdalena. Akamsalimia kwa salamu kama ambavyo mara kwa mara alikuwa akiwasalimia vijana wenzake. Akakaribishwa kiti na kutulia. Hapo ndipo maongezi yalipoanza.
Waliongea kwa muda mrefu huku wakitafuta muda wa kuzoeana. Dominick akaamua kuitumia nafasi hiyo kumuonyeshea Bi Magdalena ni kwa kiasi gani alikuwa na uwezo wa kumfanya chochote alichotaka kufanyiwa usiku huo.
“Unajua kuchuma mboga?” Dominick alimuuliza Bi Magdalena.
“Aaaaah! Mbona kila mtu anaijua. Hata binti yangu Sara anaifahamu” Bi Magdalena alisema huku akionekana kuanza kulewa.
“Usijali. Nitakupa nyingine kama kumi hivi. Najua kifo cha mende unaifahamu sana…mimi nitakuwa mwalimu wako leo, nitataka tuandike herufi moja baada ya nyingine” Dominick alimwambia
“Tuandike herufi? Herufi gani?”
“Nimejua tu, bado u mdogo kimapenzi. Nitataka tuchore L kitandani, tukitoka hapo, tunachora C huku tukimalizia na T” Dominick alimwambia Bi Magdalena.
Bi Magdalena akaonekana kuchanganyikiwa, maneno ya kimahaba ambayo aliyaongea Dominick yalionekana kumchanganya. Moyo wake ukawa na shauku kubwa ya kutaka kuondoka nae ili aende akachorwe herufi hizo kitandani.
Akanywa pombe haraka haraka, tayari pepo la ngono lilikuwa limekwishampanda, akachanganyikiwa kabisa. Kila wakati akabaki akimwangalia Dominik kwa macho yaliyojaa mahaba. Akaanza kuupeleka mkono wake katika mapaja ya Dominick na kuanza kuupandisha juu hadi katika sehemu ya zipu.
“Mbona una haraka hivyo? Subiri, malizia pombe kwanza. Leo nataka kukuonyesha kwamba mimi ni mtoto wa Tanga. Tukianza tu…tunasitisha baada ya masaa mawili” Dominick alimwambia Bi Magdalena ambaye akaonekana kushtuka.
“Masaa mawili?”
“Ndio. Tena hapo kama utataka tufanye haraka haraka. Awamu ya pili sitokwambia tutachukua masaa mangapi, manake unaweza ukakataa” Dominick alimwambia Bi Magdalena
Bi Magdalena akaonekana kupagawa zaidi, akili yake ilikuwa ikijiuliza ni kwa jinsi gani kijana aliyekuwa akiongea nae alikuwa na uwezo mkubwa kitandani. Akamuita binti yake, Sara na kuanza kuongea nae kwamba alikuwa akitaka kuondoka mahali hapo.
“Utanipgia simu basi” Sara alimwambia mama yake.
“Sawa” Bi Magdalena alimwambia na kisha kuondoka pamoja na Dominick.
Safari ikaanza huku Dominick ndiye akiwa dereva wa gari la kifahari ambalo alikuja nalo Bi Magdalena na binti yake Sara. Ndani ya gari Bi Magdalena alikuwa akiongea maneno ya mahaba tu, alimuona Dominick akiendesha kwa mwendo mdogo.
Alitamani kufika haraka katika sehemu ambayo angechorwa herufi ambazo Dominick alikuwa amemulezea pasipo kujua mwanaume huyo alikuwa nani. Kila alipokuwa akijaribu kuvuta picha ya mambo ambayo yangefanyika kitandani, Bi Magdalena alibaki kuwa na mshawasha wa kufika haraka.
“Paki gari pembeni” Bi Magdalena alimwambia Dominick ambaye akatii amri kwa kulipaki gari lile pembeni.
“Kuna nini tena?”
“Tunachelewa bwana. Njoo huku nyuma” Bi Magdalna alimwambia Dominick huk akimvuta katiks viti vya nyuma.
“Subir tufike hotelini”
“Hapana. Nimezidiwa. Njoo japo unifanyie herufi moja, halafu nyingine tutazimalizia hotelini” Bi Magdalena alimwambia Dominick ambaye alibaki amechanganyikiwa.
********
“Unasemaje?” Sara aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Ndio hivyo. Jamaa ametoka Tanga, halafu inaonekana nuksi” Mwanaume yule mlinzi alimwamba Sara ambaye alionekana kuchanganyikiwa.
“Mbona haukuniambia? Au unataka raha azipate peke yake? Yaani leo unanigeuka Dickson” Sara alimwambia Dickson huku akilalamika.
“Mbona unakuwa mkali sana leo. Unanilalamikia sana na wakati muda mwingine nakuitia wewe peke yako” Dickson alimwambia Sara
“Lakini sio kwa mtu wa leo. Mtu ametoka Tanga halafu unampa yule bibi. Haiwezekani, kama mambo bora tupewe wote” Sara alisema huku akitoka ndani ya klabu ile. Akakodi bajaji na kuanza kuelekea katika hoteli ya Supernova ambayo mara zote mama yake alikuwa akiitumia kufanya ngono na vijana.
Njiani Sara alikuwa na mawazo, alitaka kufika haraka hotelini. Kijana ambaye aliondoka nae mama yake tayari alionekana kumchanganya. Pepo la ngo lilikuwa limekwishaanza kmpanda. Muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia nje huku upepo ambao ulikuwa ukimpiga ukionekana kumchanganya kabisa.
“Hebu subiri” Sara alimwambia dereva Bajaji mara baada ya kuiona gari aina ya VX likiwa limepakiwa pembeni mwa barabara. Sara akateremka na kuanza kupiga hatua kuifuata gari ile. Alijua fika kwamba gari lile lilikuwa lile walilokuja nalo, alimjua vilivyo mama yake ambaye mara nyingine alikuwa akifanya ngono garini.
Kadri alivyokuwa akilisogelea na ndivyo ambavyo mwili wake ulivyokuwa ukimsisimka. Nywele zilikuwa zikimsimama huku mshawasha wa kufanya mapenzi ukimshika. Alipolifikia gari lile, akajaribu kuchungulia garini, hakuona kitu chochote kutokana na giza kubwa. Akachukua simu yake ambayo ilikuwa na tochi na kumulika ndani.
“Mungu wangu……….!”
************
“Mbona unalia Ombeni. Yaani niliyefiwa wala silii namna hiyo, wewe ndiye ambaye unalia, kwa nini?” Bwana Boniface alimuuliza mzee Ombeni.
“Haujui kama nami familia yangu imeteketezwa kwa moto? Haujui kama nami pia nimempoteza mke wangu na mtoto wangu?” Mzee Ombeni alimwambia Bwana Boniface.
“Kumbe na wewe pia umeipoteza familia yako? Mungu wangu…….” Bwana Boniface alisema.
Mzee Ombeni akashtuka kutoka kitandani, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka, ndoto ambayo alikuwa ameiota ilionekana kumtisha kupita kawaida. Cha kwanza akaangalia kitandani pale, alikuwa peke yake. Akainuka na kuelekea sebuleni, mkewe pia hakuwepo mahali pale. Wasiwasi ukaanza kumshika, akarudi tena chumbani na kuanza kumpigia simu mkewe lakini simu wala haikupatikana.
Mwili wake ukaanza kumsisi mka, kijasho chembamba kikaaanza kumtoka. Akaamua kutoka na kuelekea katika chumba cha binti yake, akanza kuugonga mlango lakini wala hakukuwa na mtu yeyote aliyemjibu hali iliyoonyesha kuwa hata nae hakuwepo.
Mzee Ombeni akarudi tena chumbani kwake na kutulia. Akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi kupita kiasi. Ingawa mara kwa mara mkewe alikuwa akimtoroka usiku na kwenda katika nyumba za starehe wala hakujali kabisa lakini siku hiyo akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi kupita kiasi.
Ndoto ya kutisha ambayo alikuwa ameiota ndio ambayo ilionekana kumtisha zaidi. Akatoka na moja kwa moja kuelekea nje, gari yake ya VX wala haikuwepo hali iliyoonyesha kwamba kulikuwa na mtu ambaye aliichukua. Hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, moja kwa moja akalifuata gari jingine aina ya Range Rover na kuanza kuondoka mahali hapo.
Kazi yake ilikuwa moja tu, kulitafuta gari lak katika kila klabu ya usiku ambayo alikuwa akiifahamu. Breki ya kwanza ilikuwa San Siro, hakukuwa na gari lake katika sehemu ya kuegeshea magari.
Hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, safari yake ikaendelea zaidi kwenda katika klabu nyingine zaidi. Katika kila klabu ambayo alikwenda, wala gari lake hakuliona. Akajihisi kuchanganyikiwa kupita kiasi. Alitembea katika klabu zaidi ya kumi na tano Dar es Salaam lakini wala hakuliona gari lake.
Akaliegesha gari lile pembeni na kuanza kufikiria kama kulikuwa na klabu yoyote ambayo hakuwa ameitembelea usiku huo. Jina la klabu ambalo lilikuwa limeingia kichwani mwake ilikuwa klabu ya Raspinho. Mzee Ombeni hakutaka kukubaliana na hilo, allijihisi kuchoka sana.
“Haiwezekani wawe kule bwana. Ngoja nirudi nyumbani” Mzee Ombeni alijisemea.
Akageuza gari na kuanza kuelekea nyumbani kwake. Ghafla akalisimamisha gari lake, akakata kona na kuanza kurudi kule alipotoka. Tayari akaonekana kushikwa na machale, hakuwa tayari kurudi nyumbani pasipo kwenda Raspinho Club kuhakikisha kama familia yake haikuwa kule.
Alipofika katika eneo la klabu ile, hakukuwa na gari lake hali iliyomfanya kukata tamaa zaidi. Akaanza kuligeuza, lakini alipoangalia vizuri, idadi ya watu ilikuwa kubwa sana nje hali iliyomfanya kuteremka na kuanza kupiga hatua kuelekea kule watu walipokuwa akikusanyika huku tayari ikiwani saa tisa usiku.
Watu walikuwa wakiongea kwa sauti kubwa sana lakni mara baada ya kumuona mzee Ombeni akiwasogelea, wote wakanyamaza na kuanza kumwangalia mzee huyo ambaye alionekana kutaka kusikia ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.
“Kuna nini jamani?” Mzee Ombeni aliuliza lakini hakukuwa na mtu aliyejibu chochote kile, umati wote wa watu themanini waliokusanyika mahali pale ulibaki kimya hali iliyoanza kumtia wasiwasi mzee Ombeni.
**********
Dominick hakutaka kabisa kufanya kufanya mchezo wowte wa ngono hasa na mwanamke yule ambaye alikuwa akionekana kuwa kama mama yake. Alimwangalia Bi Madgalena mara mbili mbili, tayari pepo la ngono lilikuwa limekwishampanda kwa asilimia mia moja.
Mwili wake ulikuwa umemlegea kupita kiasi, akaanza kuchojoa kila nguo ambayo alikuwa ameivaa. Alipomuona Dominick hafanyi kitu chochote kile, akaanza kumvua shati lake. Domonick alikuwa akipapaswa kila seheu ya mwili wake huku Bi Magdalena akitoa milio mbalimbali ya mahaba.
“Mbona una bunduki?” Bi Magdalena alimuuliza Dominick mara alipokuwa akimvua suruali.
“Si unajua mimi mlinzi wa Benki Kuu Tanzania. Nimetoroka kule kwa ajili yako, yaani kuja kukuonyesha ni kwa jinsi gani mapenzi yanavyofanywa, sio kama vijana wengine ambao wanakuvua nguo halafu mambo yao yanakuwa ya kitoto” Dominick alidanganya.
Udanganyifu ule ulimfanya Bi Magdalena kuchanganyikiwa, bado alitamanisana kuuona umakini wa Dominick wa kufanya mchezo wa ngono kitandani. Akamvua suruali haraka haraka na kisha kumvutia kifuani mwake.
Dominick hakuwa akijisikia kabisa kufanya mchezo wa ngono na mwanamke yule ambaye alikuwa taabani. Dominick akachukua bunduki yake na kuiweka vizuri. Akachungulia nje, hakukuwa na gari lolote lililokuwa likipita barabarani kutokana na usiku kuwa mkubwa.
“Bado sijaridhika. Nikimuua huyu, bado na binti yake. Halafu sitaki afe kwa risasi, huyu ni kuchomwa moto tu” Dominick aliwaza.
“Ngoja nimpige risasi hata ya mbavu, sitaki kumuua. Baada ya hapo nitamfuata binti yake kumleta huku” Dominick alijisemea.
Akaikoki bunduki yake vilivyo, Bi Magdalena bado alionekana kuwa katika mahaba mazito. Alichokifanya Dominick ni kuanza kumpapasa Bi Magdalena ili aweze kumvuruga zaidi. Bi Magdalena akachanganyikiwa kupita kawaida, akaanza kukunja kunja vidole vyake vya mguuni kuonyesha ni kwa jinsi gani kwa wakati huo alikwa amechanganyikiwa.
Dominck hakutaka kupoteza muda, hapo hapo akakibonyeza kitufe cha kuruhusu risasi, ukelele mkubwa ukaanza kusikika kutoka kwa Bi Magdalena. Damu nyingi zilikuwa zikimtoka mbavuni. Dominick akaonekana kushtuka, mara baada ya kuchungulia nje na macho yake kuiona Bajaji ikiwa imesimama kwa mbali, mtu msichana mmoja akateremka a kisha Bajaji ile kuondoka.
Kwa haraka haraka huku akiogopa kuonekana, akaufungua mlango wa upande mwingine na kuteremka huku akimvizia kuona msichana yule alikuwa nani. Dominick akashtuka kwa furaha, taa za gari lile ambazo zilikuwa zikiendelea kuwaka zilimuwezesha kumjua msichana ambae alikuwa akisogea mahali kule alipokuwa.
“Mungu wangu! Kweli Mungu yuko pamoja nami” Dominick alijisemea huku akisogea kule nyuma ya gari.
Sara akasogea mpaka katika mlango mmoja wa gari lile na kuanza kuchungulia. Alikuwa na uhakika kuwa mama yake alikuwa amezidiwa na hivyo alihitaji kufanya ngono hata garini kwani mara kwa mara alikuwa akifanya mchezo huo garini.
Hakuona vizuri garini kitu ambacho kilimfanya kuchukua simu yake iliyokuwa na tochi na kisha kuchungulia. Sara akashtuka, alimuona mama yake akiugulia kwa maumivu. Damu nyingi zilikuwa zikimtoka kupita kawaida. Alichokifanya ni kuanza kuufungua mlango ule, mlango ulikuwa umefungwa.
Kwa mwendo wa kasi akaanza kuzunguka nyuma ya gari ili kuufungua mlango mwingine, akashtukia akipigwa ngumi nzito usoni nzito ya kushtukiza ambayo ilimfanya hapo hapo kuanguka chini na kupoteza fahamu.
Kwa haraka haraka Dominick akambeba Sara na kumingiza garini. Akalwasha gari na moja kwa moja kuondoka mahali hapo. Breki ya kwanza ilikuwa katika kituo cha mafuta ya Petroli ambako akateremka na kumfuata muuzaji mmoja.
“Nahitaji mafuta ya petroli lita kumi” Dominick alimwambia muuza mafuta wa kituo cha kuuzia mafuta.
“Sogeza gari basi karibu”
“Hauwezi kuniwekea kwenye dumu? Si unajua nakwenda kuyamiminika katika gari jingine” Dominick alimwambia muuza mafuta
“Daaa! Kazi itakuwa kutafuta dumu”
“Kwa hiyo hakuna madumu kabisa mahali hapa?”
“Yapo ila mwenyewe akijua kwamba nimeyatoa na kumpa mtu mwingine anaweza akanianzishia utata” Muuzaji yule alimwambia Dominick ambaye alibaki kimya kwa muda.
“Huwa anayauza?” Dominick aliuliza
“Ndio. Moja elfu nne”
Dominick hakutaka kupoteza muda, akatoa kiasi cha shilingi elfu tano na kumgawia muuzaji mafuta ambaye akaenda kuchukua hilo dumu na kurudi nalo. Mafuta yakawekwa ndani ya dumu lile na kisha kulipa fedha zote ambazo zilikuwa zikihitajika.
Dominick akalichukua dumu lile na kulipandisha garini. Sauti ya Bi Magdalena ilikuwa ikisikika kwa chini sana, bado damu zilikuwa zikiendelea kumtoka. Sara ambaye alikua pembeni hakuonekana kurudiwa na fahamu, ngumi nzito na ya kushtukiza ilionekana kumuingia vilivyo.
Dominick akaangalia saa yake ambayo ilikuwa ikimuonyesha kuwa tayari saa tisa na nusu usiku. Alichokifanya ni kuendesha kwa kasi kuelekea katika ufukwe wa Coco ambako aliamini kwa muda ule, hakukuwa na mtu yeyote ambaye angekuwepo mahali pale.
Hakukuwa na magari barabarani hali ambayo ilimfanya Dominick kuendesha kwa kasi ambayo alitaka kuendesha. Alipoanza kuingia katika eneo la ufukwe ule, akazima taa zote na kuanza kuelekea katika eneo lile lile ambalo alilichomea gari la Bwana Boniface.
Akalisimamisha gari lile, akaanza kulimwagia mafuta kwa kasi ya ajabu kuanzia nje hadi ndani. Akawamwagia mafuta Bi Magdalena pamoja na binti yake, Sara. Bado sauti ya chini iliyojaa maumivu ilikuwa ikisikika kutoka kwa Bi Magdalena
Dominick hakuonekana kujali, bado aliendelea kuwamwagia petroli. Alipomaliza akaingiza mkono mfukoni na kuchukua kiberiti, akaliwasha gari lile. Moto mkubwa ukaanza kuwaka, Dominick akabaki pembeni akicheka tu. Gari liliendelea kuteketea zaidi na zaidi, uso wake bado ulikuwa umetawaliwa na tabasamu.
Mwanga wa tochi ukammulika usoni, Dominick akaonkana kushtuka kupita kiasi. Alijua kwamba mahali hapo alikuwa peke yake kutokana na usiku kuwa mwingi sana. Tochi ambayo ilimmulika usoni ndio ambayo ikamfanya kuanza kukimbia.
Milio ya mbwa waliokuwa wakija kwa kasi ikaanza kusikika. Dominick akaongeza kasi zaidi na zaidi. Mchanga mwingi wa ufukweni ndio ambao ulimfanya kutokukimbia kwa kasi. Mbwa watano walizidi kumsogelea zaidi na zaidi, ni umbali wa hatua kumi tu ndizo ambazo walikuwa wamebakiza kabla ya kumkamata Dominik ambaye alionekana kuchoka kutokana na mchanga mwingi uliokuwa pale ufukweni ambao ulimfanya kutokumbia kwa kasi.
“Kama kunikamata…acha tu wanikamate…sina ujanja” Dominick alijisemea huku kasi yake ikianza kupungua Tayari alikuwa amekwishakata tamaa kabisa. Aikuwa tayari kukamatwa na mbwa wale, kuumwa na hatimae mtu yule aliyemmulika tochi kumfikia.
*******
Walinzi wanne walikuwa wakiendelea na ulinzi katika nyumba ya balozi wa Marekani Bwana Brown Poll. Mbwa wakali ambao walikuwa wamepewa mafunzo ya kutoshwa walikuwa mikononi mwao, tochi pamoja na bunduki zilikuwa mikonon mwao.
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.comITAENDELEA SIKU YA KESHO..