Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

MADRID YASHINDA KWA MBINDE, RONALDO AKOSA PENALTI, ATLETICO YAITULIZA JUVE

$
0
0

Real Madrid imelazimika kufanya kazi ya ziada kushinda kwa mabao 2-1 dhidi ya timu kibonde ya Ludogoret.

Mabao ya Madrid katika mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya makundi yalifungwa na Cristiano Ronaldo kwa mkwaju wa penalti lakini ikiwa ni baada ya kukosa mkwaju wa kwanza, Madrid ilipata mikwaju miwili ya penalti.
Bao la pili na la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Mfaransa, Karim Benzema.

Katika mechi nyingine, Atletico Madrid ikiwa nyumbani, imeituliza Juventus ya Italia kwa kuitwanga kwa bao 1-0, muuaji akiwa ni Mturuki, Arda Turan, kama unamkubuka ndiyo yule aliyeiua Real Madrid.

MATOKEO MENGINE LEO:
Zenit 0-0 Monaco
B. Leverkusen 3-1 Benfica
Anderlecht 0-3 Borussia Dortmund
Malmo 2-0 Olimpiakos
 

STEVE NYERERE: BONGO MOVIE WATANIKUMBUKA!

$
0
0
MSANII wa filamu Bongo aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amesema kuwa ana mengi ya kujivunia katika klabu hiyo ambayo anaamini yatawafanya wasanii wakumbuke kipindi cha uongozi wake.
 
Msaniiwa filamu Bongo aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’
Akipiga stori na paparazi wetu, Steve alisema kuna vitu vingi ambavyo ameifanyia Klabu ya Bongo Movie ikiwemo kurudisha heshima katika jamii kwa ujumla kuwa klabu hiyo haihusiani na vitendo vya kifuska bali ni wasanii wanaojiheshimu na kuthamini kazi zao kwa kukemea maovu.
“Naamini wasanii wa Bongo Movie watanikumbuka kwa mengi niliyowafanyia, hata kama wanatazama mabaya yangu lakini yapo na mazuri ambayo ni wazi hayapingiki, niliondoa matabaka pamoja na kufanya mambo mbalimbali ya kimaendeleo ni wazi jinsi ilivyo sasa ni tofauti na nilivyoingia madarakani, nimewakutanisha na fursa mbalimbali na kusimamia nidhamu,” alisema Steve.

WAKE WA MARAIS WA AFRIKA WANAOTIKISA

$
0
0
Baada ya wiki iliyopita kuwaletea mabinti warembo wa marais wa nchi kadhaa za Afrika wanaosifika kwa uzuri, wiki hii tunawaletea wake wa marais wa nchi hizo ‘wanaokimbiza’ kwa uzuri, uvaaji nk.

Ana Paula Dos Santos.
Ana Paula Dos Santos
alizaliwa1964, ni mke wa Rais wa Angola, Jose Eduardo Dos Santos, Paula ni mwanamitindo wa zamani, anasifika kwa uzuri na kujua kuvaa.
 
Mama Salma Kikwete.
Mama Salma Kikwete
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, alizaliwa 1963, anatajwa kuwa katika orodha ya wake wazuri wa marais wa Afrika, anasifika kwa mavazi yake ya kitenge.
 
Margaret Wanjiku Kenyatta.
Margaret Wanjiku Kenyatta
Ni mke wa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, anatajwa kuwa na tabasamu zuri ingawa nywele zake zenye rangi ya kijivu ni kivutio kikubwa. Kazaliwa Mwaka 1963.
 
Hinda Deby Itno.
Mialy Razakandisa Rajoelina
Ni miongoni mwa wake vijana wa marais katika Bara la Afrika na anatajwa kuwa na ngozi nzuri na urembo wa asili, ni mke wa Rais Andry Rajoelina wa  Madagascar.
 
Zaineb Jammeh Suma.
Hinda Deby Itno
 Anafahamika kama mrembo wa Chad, pia anatajwa kuwa mmoja wa wanawake wa marais mwenye bashasha na tabasamu la kipekee, mke wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa Chad, Brahim Deby Itno.
 
Sylvia Bongo Ondimba.
Zaineb Jammeh Suma
Ni mke wa Rais wa Gambia, Yahaya Jammeh. Zaineb anatajwa kuwa ndiye mwanamke mrembo kuliko wake wengine wa marais katika Afrika. Amezaliwa1977, Rabat nchini Morocco.

Sylvia Bongo Ondimba
Mke wa Rais wa Gabon, Ali Bongo Ondimba, Sylvia ndiyo jina alilopewa na wazazi wake mwaka 1965, ni mzaliwa wa Paris Ufaransa, anasifiwa kwa uzuri.

KAJALA AMSHTAKI MAMA WEMA! KISA KIPO HAPA

$
0
0
Stori: Mwandishi Wetu
KIMENUKA! Habari ya mjini kwa sasa ni bethidei ya Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu kutimiza miaka 26 tangu kuzaliwa, lakini ndani ya tukio hilo, mengine yameibuka!
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Kajala Masanja.
Miongoni mwa yaliyoibuka kwenye sherehe hiyo iliyofanyika Jumapili iliyopita nyumbani kwa Wema, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar es Salaam ni madai ya mama Wema, Mariam Sepetu kudaiwa kupewa nafasi ya kutoa ‘neno la hekima’ lakini akaitumia kumvurumishia mitusi aliyekuwa shosti wa Wema, Kajala Masanja.
KUNASWA KWA SAUTI NA PICHA
Baada ya sherehe hiyo, Jumatatu na Jumanne, mitandao mingi ya kijamii ilitumbukiza video yenye sauti ikimuonesha mama Wema akimrushia matusi Kajala kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kukorofishana kwa mwanaye na Kajala aliyewahi kumfadhili mahakamani kwa kumlipia faini ya shilingi milioni 13 asiende jela kwa kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa na zuio la kisheria.
 
Wema Sepetu akiwa na mama yake.
KAJALA AAMUA ZITO
Katika kufuatilia sakata hilo, Amani lilinyetishiwa kwamba Kajala baada ya kushindwa kuvumilia, ameamua kumshitaki mahakamani mama Wema.
Chanzo chetu kinadai kuwa Kajala alifikia uamuzi huo baada ya kushauriwa na familia sanjari na wafuasi wake (Timu Kajala) ambapo sasa, timu hiyo na Timu Wema wameingia vitani tena.
“Kajala ameshawasiliana na wanasheria wawili na kutoa maelezo yake, wao wanaandaa faili ili mashitaka yafike mahakamani, amekasirika sana.“Amesema mama Wema ametumia nafasi ya kukutana na watu kumdhalilisha bila kumpa nafasi ya kujitetea, ameona si sawa hata kidogo,” kilisema chanzo hicho ambacho ni jirani na Kajala.
 
Wema Sepetu akiwa na Kajala Masanja.
MATUSI YENYEWE
Katika sauti, mama Wema anasikika akitamka matusi (hayaandikiki gazetini)  huku Wema naye anasikika akimsihi mama yake asimtaje jina Kajala kwa kuwa kufanya hivyo ni kumpaisha. Hapa inamaanisha kwamba, Wema alitaka mama yake afunguke lakini bila kutamka jina la mtu.
AGUNDUA TIMU KAJALA IMO NDANI YA BETHIDEI
Katika hatua nyingine, mama Wema alisema kauli iliyoashiria kwamba Timu Kajala ilikuwemo ndani ya bethidei ya mwanaye. “Nasema haya huku najua humu ndani kuna Timu Kajala, lakini nasema….(matusi mazito)”
KAJALA SASA
Baada ya madai hayo yote, juzi, Amani lilimsaka Kajala kwa njia ya simu ili kumuuliza ukweli wa madai hayo. Licha ya kutopokea simu ya paparazi wetu, alitumiwa ujumbe mfupi wa maneno ‘SMS’ na kuulizwa kila kitu.
Hata hivyo, badala ya kujibu alikaa kimya, baada ya dakika kama kumi na tano  alimrushia kwa simu mwandishi wetu video hiyo ambayo anadai kutukanwa na mama Wema bila kusema chochote hali iliyotafsiriwa kuwa kama alisema; ‘hebu oneni wenyewe jamani, nimemkosea nini mama Wema?’
 
Mama yake Wema Sepetu.
ALICHOKIFANYA MARTIN KADINDA
Katika hatua nyingine siku hiyo, meneja wa Wema, Martin Kadinda alikuwa na kazi ya ziada kuhakikisha, mama Wema na mama Diamond, Sanura Kasim ‘Sandra’ hawakai jirani au meza moja licha ya kwamba watoto wao wamependana.
“Kadinda ana kazi ngumu sana, unajua anatakiwa kuhakikisha kwamba mama Wema na mama Diamond hawakai meza moja. Sijui anaogopa nini, kwani hawa si watu ambao watoto wao wana mpango wa kuoana?” alihoji mwalikwa mmoja.
KUMBUKUMBU MUHIMU
Katika bethidei hiyo, Wema alizawadiwa magari mawili, Nissan Murano lenye thamani ya shilingi milioni 36 alilopewa na Diamond na BMW 545i lenye thamani ya shilingi milioni 56, inadaiwa alizawadiwa na Kadinda!
CHANZO GPL

GARDNER ATAKA JIDE AELEZE UKWELI JUU YA NDOA YAO

$
0
0
Habari ya mjini katika ulimwengu wa mastaa Bongo ni kitendo cha mtangazaji mwenye jina kubwa wa Kipindi cha Maskani cha Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’ kutaka mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ ndiye aeleze ukweli juu ya ndoa yao.

Mtangazaji wa Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’
Akizungumza kwenye Kipindi cha Mkasi kinachorushwa hewani kupitia Televisheni ya EATV chini ya ‘hosti’ wake, Salama Jabir, Jumanne iliyopita, Gardner alikataa kuzungumzia ndoa yake inayodaiwa kuvunjika.
Pamoja na mambo mengine ambayo aliyajibu kwa ufasaha, Gardner alipoulizwa juu ya habari zinazozungumzwa mtaani kuhusu kuvunjika uhusiano wake na Jide au Lady Jaydee, aligoma kulizungumzia kwa kigezo kwamba kipindi hicho kilimhusu yeye tu.
 
Mwanamuziki wa Bongo fleva kitambo, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’
Mtangazaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia Salama kwamba amwite Jaydee kwenye kipindi hicho ili alielezee jambo hilo kwa undani.Gardner na Jaydee ambao walifunga ndoa mwaka 2005, wamekuwa wakidaiwa kuwa hawapo pamoja tena huku majukumu ya mtangazaji huyo ambaye alikuwa meneja wa mwanamuziki huyo yakielea.
Kupitia kipindi chake cha Diary of Lady Jaydee kilichokuwa kikisimamiwa na Gardner ambacho sasa kinaongozwa na ndugu wa msanii huyo aitwaye Wakazi, Jumapili iliyopita Jide alionekana kwenye harusi ya ndugu yake aitwaye Lameck Mbibo ‘Dabo’ ambaye pia ni msanii wa Dance Hall akiwa mpweke bila mumewe kama ilivyozoeleka.
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

CHA MPENZI WAKO CHAKO, CHAKO CHAKO, HOW COME?

$
0
0


Ni wiki nyingine tafauti kabisa na wiki zilizopita tunakutana tena kupitia safu hii namba moja kwa kuandika makala ‘hot’ za mapenzi. Ni safu ambayo inaweza kuyafanya maisha yako ya kimapenzi yakawa ya furaha endapo tu utayafanyia kazi yale ambayo huwa nayaandika. 
Kikubwa unachotakiwa kujua ni kwamba, ukikosea kidogo tu kwenye mapenzi huwezi kuwa na furaha kwenye maisha yako. Unaweza kwa na pesa nyingi benki, mali kibao lakini kama mapenzi yanakuzingua, utakosa amani na wakati mwingine kuhisi huna thamani ya kuendelea kuishi.

Waliojiua kwa sababu ya mapenzi wapo, waliochanganyikiwa na kushindwa kufanya kazi zao kwa ufasaha ni wengi sana. Hivyo basi, ili uwe na maisha yenye amani na utulivu, tumia gharama yoyote kujihakikisha maisha ya amani ya kimapenzi ikiwa ni pamoja na kuchagua mwenza sahihi.
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

Mpenzi msomaji wangu, leo nataka kuzungumzia hili suala la baadhi ya watu kuwa wabinafsi, wabahili na wasiowajali wapenzi wao na kusababisha mapenzi yao kuwa dhaifu.

Nilishawahi kuzungumzia suala la baadhi ya wanaume kuwa wabahili kwa wapenzi wao. Yaani wao kutoa pesa zao kuwafanyia ‘shopping’ wapenzi wao, kuwasaidia pale wanapokuwa na matatizo ni wagumu kuliko maelezo.
Unakuta mwanaume anapata mshahara mzuri au katika mishemishe zake anakuwa na bahati ya kupata mshiko wa kutosha lakini ukifuatilia sana utabaini ni mgumu kutoa na mpenzi wake hanufaiki chochote na kipato hicho kizuri.

Akiombwa pesa ya vocha anakuwa mkali sana, akililiwa shida anaweza hata kukata mawasiliano kwa kuhisi eti akitoa pesa yake ataonekana kachunwa. Jamani, labda niseme kwamba, mpenzi wako anayekupenda kwa dhati hawezi kukuchuna. Anapokulilia shida, anajua wewe ndiye mtu sahihi wa kumsaidia. Hawezi kwenda kwa mtu wa pembeni na kuomba msaada wakati wewe upo.

Hivi mpenzi wako akimlilia shida rafiki yako (shemeji yake) na akapewa wakati wewe ulikuwa unaweza kumsaidia utajisikiaje? Mpenzi wako akiwa anavaa midabwada, anaishi kwa kuungaunga wakati wewe mambo yako safi hujisikii vibaya? Usipokuwa wa kwanza kumfanya mpenzi wako ajisikie furaha kwenye maisha yake, unatarajia nani afanye hivyo? 
Sikatai huenda kazi huna na fedha inakupitia kushoto, hilo wala siyo tatizo. Kwa kuwa mpenzi wako anajua naamini ataendelea kuwa na wewe akifahamu kuwa kukosa kwako ni mipango ya Mungu. Tatizo ni pale ambapo unazo na unakuwa bahili bila sababu za msingi. Huku ni kutaka kumfanya mpenzi wako ashawishike kuchepuka.

Atakutana na wanaume wanaoujua kumwaga pesa na wenye ushawishi mkubwa na kwa kuwa wewe humjali, atajikuta amechepuka. Tusitake yatukute hayo!Lakini sasa wakati hilo likiwa hivyo, leo nataka kuwazungumzia baadhi ya wanawake ambao wana katabia f’lani kasikofaa. Nawazungumzia wale wanaofanya kazi zinazowaingizia kipato, hata kama siyo kikubwa kuzidi kile cha waume zao.

Ni kweli mume ana jukumu la kumfanya mkewe ajikisikie furaha ya kuolewa lakini wewe mwanamke ambaye unapata pesa kwa kazi zako au mshahara, ni lini ulisema leo ngoja nimsaidie mpenzi wangu katika hili?

Yaani kwa kuwa umeolewa basi unataka kila kitu mumeo afanye, yeye ndiye anunue chakula, atoe mahitaji muhimu kwa watoto, akuvishe na akulishe, fedha zako wewe unafanyia nini?
Ni lini ulisema leo ngoja ninunue mahitaji ya nyumbani? Ni lini ulimnunulia zawadi mpenzi wako? Mara ya mwisho ni lini kumtumia mumeo vocha? Wewe jifanyie tathmini kisha majibu yako uyawekee vingi viulizo.

Nasema hivyo kwa kuwa, wapo wanawake ambao wanaamini kipato chao wana haki ya kukifanyia chochote ila cha mume ndicho kinachotakiwa kutumika ipasavyo.
Wapo wanawake ambao wako makini sana na mshahara wa waume zao lakini za kwao wakiulizwa wanakuwa wakali, hii siyo sawa!Mnapokuwa wapenzi au mmeoana, mnakuwa kitu kimoja. Mwenzako akiwa na shida f’lani unamsaidia pale inapobidi lakini itakuwa haileti picha nzuri kama pesa yako ni yako lakini ya mpenzi wako unaitolea macho.

Ninachotaka kusema hapa ni kwamba, kama kweli unampenda huyo uliyenaye, usijenge utegemezi uliopitiliza. Usiwe ni mtu wa kila siku kutaka usaidiwe, wakati mwingine umsaidie mwenzako pale ambapo unaona una uwezo na yeye ana shida.

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

WANAWAKE 2 WATAJWA KUVUNJA UCHUMBA WA ROSE NDAUKA

$
0
0

STAA wa filamu Bongo, Rose Ndauka ameanika ukweli kuhusu uhusiano wake na aliyekuwa mchumba wake Malick Bandawe baada ya kuwagundua wanawake wawili aliozaa nao mbali na yeye.
 
Staawa filamu Bongo, Rose Ndauka.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Rose aliamua kufungasha virago vyake na kurudi kwa mama yake mzazi maeneo ya Kigogo baada ya kugundua kwamba mchumba’ake huyo alizaa na wanawake wawili tofauti na yeye ambaye ni wa tatu.
“Alichokizungumza Malick kwamba alishamuweka chini Rose na kuzungumza naye si kweli, ila yeye Rose aliamua kurudi kwao baada ya kugundua jamaa ana wanawake wawili aliozaa nao kabla yake,” kilisema chanzo hicho.
 
Akaongeza: “Kile kilichosemwa na  Malick kuwa anasikitika kuona mtoto wake anakwenda kulelewa na mwanaume mwingine ni kujitetea tu lakini ukweli ni kwamba mwanaye analelewa na yeye mwenyewe kwa sababu yuko nyumbani kwa mama yeke.”
Juzi, paparazi wetu alimtafuta Rose kwa njia ya simu yake ya mkononi, alipopatikana na kusomewa madai hayo alikata simu huku akisikika akisema hayuko tayari kufunguka lolote kwa sasa.

USIKU WA KIGODORO - 07

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ILIPOISHIA :Lina alifika hotelini, akasukuma mlango na kuzama kwenye chumba alichomo mume wake wa pili James.
“Hodi.”
NING’INIA NAYO…
James alifungua mlango, ukawa wazi mpaka mwisho. Lakini alionekana kukunja sura na kupoteza uchangamfu kuliko siku nyingine.
“Karibu.”
Lina aligundua James hakuwa sawa…
“Baby kama haupo sawa, kuna nini?”
“Lina, mimi ni nani kwako?”
“Mume wangu.”
“Unatakiwa kumsikiliza dada ‘ako au mimi?”
“Wewe.”
“Basi naomba unisikilize kuanzia sasa.”
“Kwani sikusikilizi baby? Mbona mimi nakusikiliza sana jamani.”
“Lakini si kwa kiwango kinachotakiwa Lina, ongeza usikivu wako kwangu. Mbona mapema sana kuanza kuonesha si msikivu!”
“Nisamehe mume wangu.”
“Oke, yamepita nakupenda sana.”
“Asante baby, nakupenda pia.”
Walikumbatiana wakaganda kwa muda huku kila mmoja akimtazama mwenzake machoni, mwishowe wakaachia tabasamu laini, wakapanda kitandani ambako Lina ndiye aliyeanzisha kupeana muwashawasha kwa James naye akapokea, wakakukuruka mpaka wakaingia uwanjani kuanza mchezo.
***
Usiku uliingia, Lina alikuwa akipiga mahesabu ni uongo  gani atamwambia mume wake akaeleweka ili asirudi nyumbani siku hiyo. Kwa siku hiyo kumpigia asingeweza maana muda wote James alikuwa yuko naye beneti. Akaamua kutuma meseji.
“Baby, hali ya dada’ke Eg bado si nzuri. Naomba nilale hospitali maana naye Eg ana mgonjwa mwingine pale kwake.”
Baada ya kutuma meseji hiyo, kila sekunde Lina alikuwa akiiangalia simu yake ili kuona kama meseji ya majibu itaingia.
Zilikatika dakika kumi meseji yake haijajibiwa, mwishowe akaanza kuingiwa na wasiwasi kwamba huenda mume wake hajapenda ruhusa hiyo na kama ndivyo, ataagaje kwa James ili arudi nyumbani. Mara, meseji ya mume wake Semi iliingia.
“Sijakubaliana na wewe, Eg aangalie utaratibu mwingine wa mtu wa kulala na mgonjwa wake na si wewe.”
Ni kujikaza tu, lakini Lina alibadilika rangi muda uleule ila alijichangamsha ili kutompa nafasi James kumsoma. Moyoni alijua kuna ugumu mkubwa kwa James kumkubalia aondoke. Kwanza atasema anakwenda wapi?
“Mh! Nimeyavulia nguo mwenyewe, lazima niyaoge sasa,” alijisemea moyoni huku akianza kutetemeka mpaka James akajua.
“Vipi baby mbona kama unatetemeka?”
“Wala, niko fiti tu.”
Kwa mbali Lina alipata akili kwamba, amtumie meseji Eg na kumwambia apige simu kwake aseme kuna shangazi mgonjwa amepelekwa Muhimbili muda huo, awahi Muhimbili.
Baada ya kujiridhisha kwamba itakuwa sawasawa, Lina alituma meseji hiyo kwa Eg ambaye alijibu kwa ufupi poa! Lakini akatuma nyingine akimuuliza apige simu au atume meseji?
“Piga kabisa,” alijibu Lina.
Alijifanya anakwenda chooni ili simu ya Eg ikiingia ipokelewe na James na ikibidi ujumbe huo upokelewe na yeyeyeye James.
Ile anafika chooni tu, simu yake ikaita. James akatupa jicho kwenye skrini, akasoma jina akamwita Lina.
“Baby…”
“Abee…”
“Kaka Semi.”
Kaka Semi ni mume wa Lina. Wakati anakwenda hotelini hapo aliamua kubadii jina la mume wake, badala ya kuandika My Huzband kama ilivyokuwa mwanzo, akaandika kaka Semi akiamini kwamba  anaweza kupiga wakati yeye yupo na James itakuwa soo kuonekana My Huzband!
Lina alitoka mbio huku mapigo ya moyo yakimwenda kasi kwa sababu hakutegemea kama  mumewe angepiga simu muda ule.
Lina aliipokea simu kutoka kwenye mikono ya James akiwa haamini maana alijua kuwa hata kama James angeamua kupokea na kusema ‘mwenye simu yuko mbali’ au ‘subiri kidogo’ ingekuwa soo kwake.
Pia alijua kuwa, James angeweza kuipokea simu hiyo kwa lengo la kusalimiana na shemeji yake huyo aitwaye Semi kwa mujibu wa jina la kwenye skrini ya simu.
Lina alijifanya anaipeleka simu hiyo sikioni huku akiikata halafu akajifanya anaongea.
“Shikamoo kaka Semi…mimi sijambo, za huko? Hawajambo wote? Sisi tunaendelea vizuri, utakuja lini? Haya karibu sana, shemeji yako utamuona tu ukija, yupo! Haya kwa heri kaka.”
Alipomaliza kusema kimagirini, alituma meseji kwa mumewe.
“Kuna daktari kapita wodini, nitakupigia. Lakini pia nitakuja nilikuelewa.”
Alichokitaka Semi ni hicho kujua kwamba,  kukataa kwake Lina asilale hospitali alielewa. Mara, ikaingia simu ya Eg, Lina akiwa amesimama dirishani, James akatupia tena macho na kumwambia...
“Eg anapiga, ngoja nipokee nimsalimie…shemeji mambo? Ee…yupo…nani? Amelazwa..? Hospitali gani? Hebu ongea na Lina huyu hapa shemeji…”

“Haloo…amelazwa? Anaumwa nini? Oke, nakuja basi.”
Lina alikata simu na kumgeukia James…
“Vipi?” aliuliza James…
“Mh! Majanga… itabidi niende hospitali.”
“Ameniambia aisee. Da! Sasa si itabidi nikupeleke?”
“Utanipeleka? Si ulisema unapenda wiki nzima ushinde ndani tu!”
“Ni kweli, lakini sasa wewe utaendaje?”
“Nitachukua Bajaj…”
“Kwanza leo nataka kukwambia jambo, mambo ya kupandapanda Bajaj yaishe, sitaki kuona. Nitakununulia gari tukimaliza fungate, kwa hiyo itabidi ujifunze kuendesha…ila leo nenda na teksi,” alisema James huku akimwagiza Lina kutoa pesa kwenye brifkesi…
“Nichukue shilingi ngapi?”
“Unayoona inatosha.”
Lina alitumbukiza mkono akaibuka na shilingi elfu hamsini…
“Nimechukua hamsini.”
“Sawa, kawape pole wote.”
Lina alichukua Bajaj hadi nyumbani kwake ambapo alimkuta mumewe, Semi. Swali la kwanza alilokumbana nalo kwa mumewe ni kuhusu pete ya ndoa na ya uchumba…
“Baby, hivi hizo pete ulizipeleka tena kwa sonara nini, maana naziona zinang’aa sana siku mbili hizi.”
“Nilipeleka zikaoshwa. Niliona zimeanza kuingia giza.”
“Oke, zimekuwa nzuri sana,” alisema Semi bila kujua kwamba zile ni pete mpya ambazo alizinunua James kwa ajili ya ndoa hiyo.
***
 Lina amefika kwake, kazi ikawa kumsikilizia James akipiga kuulizia kuhusu mgonjwa. Aliumia sana moyoni kiasi kwamba alitamani kumwandikia meseji amwambie ukweli kwamba yeye ni mke wa mtu, tena kwa ndoa lakini kila alipofikiria kuhusu hilo akiamini hata James alifunga naye ndoa alikosa la kufanya.
Eg alimpigia simu Lina na kumuuliza kama dili lao lilitiki au la! Alipoambiwa limetiki, akacheka sana na kukata simu huku moyoni akisema…
“Lakini sisi tuna hatari sana. Ni kweli Lina ataweza kudumu na James kwa muda mrefu bila kujulikana? Sidhani aisee!”
***
Saa kumi na mbili jioni, Lina akiwa chumbani simu yake iliita. Na muda huo aliamua kwa makusudi kuwa chumbani akijua lazima James atapiga…
“Haloo,” alipokea kwa sauti ya chini, mume wake alikuwa amekaa sebuleni…
“Vipi mgonjwa?”
“Mgonjwa hali mbaya James, hivi hapa daktari ndo ameingia sasa hivi.”
“Mh! Sasa itakuaje? Ahamishwe hospitali.”
“Sijajua ndugu watasemaje maana waliondoka na hawajarudi. Hivi nilitaka kukwambia naomba nilale nitoke asubuhi kuja huko.”ITAENDELE KESHO.
“Sawa, lala tu Lina, wale wakija asubuhi wewe unatoka, si ndiyo?”
“Ndiyo.”
“Basi hamna shida.”
Lina alijisikia furaha ya aina yake, kwani alijua amemaliza kazi kubwa sana ya siku hiyo…
“Kibarua cha leo kimeisha, bado cha kesho, keshokutwa, mtondogoo na siku za mbeleni, sijui itakuwaje!”
***
Asubuhi ya saa kumi na mbili, Lina alitoka na simu yake hadi uani, akampigia simu James haraka ili arudi tena kitandani kulala…
“Umeamkaje baby?”
“Nimeamka poa. Vipi mgonjwa?”
“Mgonjwa hivyohivyo tu, hakulala usiku.”
“Da! Poleni sana. Wameshakuja hao?”
“Wako njiani, watafika kwenye saa mojamoja hivi, maana watashinda hapa.”
“Sawa. Sasa ukitoka si unakuja huku?”
“Yeah!”
“Oke poa.”
“Oke, baadaye basi.”
***
Asubuhi ya siku hiyo, Lina alipotoka kuoga na kuvaa ili aende kwa James alipata wakati mgumu kwani isingekuwa kawaida aende akiwa amevaa nguo nyingine wakati James anajua alikwenda hospitali. Lakini pia isingekuwa rahisi avae nguo zilezile mbele ya mume wake. Kwa siku hiyo, mume alijua anakwenda kazini.
Ilibidi avae nguo nyingine, akazichukua za jana yake na kuzitia kwenye mkoba na kuondoka zake.
“Mume wangu baadaye.”
“Sawa, kazi njema.”
“Poa.”
Nje, Lina alichukua Bajaj na kwenda hotelini kwa James. Lakini alimshangaza sana dereva wa Bajaj kwani walipokaribia nje ya hoteli, alimwambia suka huyo asimamishe Bajaj na afungue turubali ili abadili nguo, avae ileile ya jana yake kisha zile alizovaa siku hiyo akaziweka kwenye mkoba…
“Kwani vipi anti, sijakuelewa?”
“We acha tu. Nina mambo makubwa sana, usinione hivi.”
“Mambo gani, siwezi kukusaidia mimi?”
“Huwezi.”
Mara, simu yake ikaita, mumewe alipiga…
“Nakuja hapo ofisini kwako, kuna mzigo nataka kuuacha,” akakata simu.
  

HAPPY BIRTHDAY DIAMOND PLATINUMZ

$
0
0
 
Staa wa muziki wa Bongo Flava Nasibu Abdul 'Diamond Platunumz'.
Leo, Octoba 2, Staa wa muziki wa Bongo Flava Nasibu Abdul 'Diamond Platunumz' anasherehekea siku yake ya kuzaliwa akiwa anatimiza umri wa miaka 25.
Mpenzi wake, Wema Sepetu ambaye wengi wanasubiri kusikia atasema nini au atatoa zawadi gani kwa Diamond ambaye alimpa gari aina ya Nissan Murano, ameandika machache kwenye Instagram na kueleza kuwa anajipanga kuandika ujumbe mzuri zaidi.

“Happy Birthday to you my original soul... ngoja nitulie kwanza ndo niandike caption maana nina mengi kwa kweli... ila jua nakupenda sana...”Ameandika Wema. Naye Shetta ameamua kumlipa fadhira ya shukurani Diamond Platinumz kwa mchango wake kwenye maendeleo ya muziki wake ikiwa ni sehemu ya kumtakia heri ya siku ya kuzaliwa.

PICHA TATU ZA WOLPER MENINAHN NA DAGRIS

AMEKUSALITI, LAKINI BADO UNAMPENDA?

$
0
0

Namshukuru Jalali kwa kuniwezesha kukutana tena na wewe msomaji wangu mpendwa wa safu hii nzuri ambapo tunajuzana, kushauriana na kuelimishana kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo uhusiano wa kimapenzi.
 
Mada yetu ya leo, kama inavyojieleza kwenye kichwa cha habari, ni mambo unayopaswa kuyafanya unapogundua mpenzi wako amekusaliti wakati bado unampenda na unahitaji kuendelea kuwa naye katika uhusiano wa kimapenzi.
Vitabu vya dini zote vinaeleza kuwa kosa pekee linaloweza kuivunja ndoa, hata ile iliyofungwa kwa baraka za Mungu, iwe ni madhabahuni au msikitini, ni USALITI. Yaani hata kama ulikuwa unampenda vipi, ikitokea amekusaliti na umegundua ukiwa na ushahidi, una haki zote za msingi za kutoa/kudai talaka au kuachana kabisa (kama bado hamjaoana).
Hata hivyo, kuna mazingira ambayo yanaweza kukutokea, ukagundua mkeo, mumeo, mchumba au mpenzi wako amekusaliti lakini kutoka ndani ya moyo wako, ukawa haupo tayari kuachana naye kwa sabahu bado unampenda sana licha ya kwamba amekukosea.
Kutokana na maombi maalum ya wasomaji wangu kadhaa ambao wamekutana na hali kama hiyo na hawajui cha kufanya, ndiyo maana leo nimeamua tuijadili mada hii na wewe msomaji wangu. 

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
Naamini mimi peke yangu sijui kila kitu wala ushauri wangu hauwezi kuwa wa mwisho lakini nataka kukushirikisha wewe msomaji wangu, hebu niambie utafanya nini unapotokewa na tukio kama hili? Unampenda kwa moyo wako wote, umemfanyia mambo mengi lakini mwisho ukagundua kuwa amekusaliti, utafanya nini?
Mapenzi yamegeuka shubiri, usaliti na maumivu ya moyo yamegeuka na kuwa sehemu ya kawaida katika uhusiano wa kimapenzi. Watu wengi wanalia kwa sababu wanasalitiwa au waliwahi kusalitiwa na wenzi wao, si wanawake, si wanaume, si wanandoa, si wachumba wala wapenzi!
Zipo sababu nyingi zinazosababisha usaliti lakini lengo langu leo siyo kuzungumzia hilo bali ni kujaribu kuiponya mioyo ya wote waliojeruhiwa na watu wanaowapenda sana kwa kuwasaliti.
Yawezekana ulitokea kumpenda sana mwenzi wako, ukaamini wewe ndiyo kila kitu kwake, ukamtimizia kila kilichokuwa ndani ya uwezo wako lakini mwisho, ukaambulia maumivu baada ya kugundua kuwa yupo mwingine anayekuibia mali zako.
Sitaki kupingana na maandiko ya vitabu vitakatifu au sheria ambazo zipo wazi kwamba malipo ya usaliti ni kuvunjika uhusiano lakini nataka tujadiliane, ni lazima kila unapogundua kuwa mwenzi wako amekusaliti dawa yake ni kupeana talaka au kuachana kwa ugomvi?
 
Mathalani umefunga ndoa na kuishi na mwenzi wako kwa kipindi kirefu mkipendana, kujaliana na kuoneshana kila aina ya mahaba lakini akateleza na kukusaliti ilihali bado anakupenda na wewe unampenda, utakapoamua kuachana naye na kwenda kwa mwingine, ukigundua naye anakusaliti utafanya nini? Utaachana na wangapi?
Siyo mara zote talaka au kuachana huwa suluhisho la usaliti ndani ya ndoa. Siwafundishi watu wasaliti ndoa zao au uhusiano wao kwa makusudi wakitegemea kusamehewa, hapana.
Nataka uelewe kwamba hata baada ya mwenzi wako kukusaliti, bado mna nafasi ya kuendelea na maisha yenu ikiwa wote wawili mtaamua kulishughulikia tatizo hilo kwa kina bila kujali watu wa nje wanasemaje.
Usikilize moyo wako, ni kweli amekusaliti! Amekuumiza, unahisi dunia yote imekuelemea, unatamani kufa au kuua, lakini je, moyo wako unakuambia nini? Upo tayari kumruhusu mwizi wako ndiyo awe mmiliki halali wa mwenzi wako ambaye bado unampenda?
Naiweka hoja mezani mpaka wiki ijayo tutakapokutana kwa ajili ya mwendelezo, nataka tujadiliane na wewe msomaji wangu. Fikiria kwa kina kisha uniambie mawazo yako.
Itaendelea wiki ijayo.
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

DOWNLOAD NGOMA KALI KUTOKA KWA RUGA MKALI- JIANDAE

VIDEO: MAMA WEMA AKIMPONDA KAJALA

$
0
0

Mama mzazi wa msanii Wema Sepetu, Miriam Sepetu akimponda aliyekuwa rafiki wa mwanaye Kajala Masanja wakati wa bethidei ya binti yake Kijitonyama jijini Dar Septemba 28, 2014.

BATULI: SIJAVUNJA UCHUMBA WA ROSE NDAUKA

$
0
0



MSANII wa filamu Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ameshangazwa na madai kuwa, anahusika kuvunjika kwa uchumba wa msanii mwenzake Rose Ndauka na kueleza kuwa hayo ni maneno ya watu wasiomtakia mema.
Msanii wa filamu Bongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni kufuatia madai hayo, Batuli alisema hajawahi kuwa na uhusiano wowote na bwana wa Rose (Malick) na kwamba ukaribu wao ni wa kikazi tu.
Msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka.
“Jamani siwezi kutoka na mchumba wa Rose kutokana na kwamba ni mtu ambaye namheshimu sana na tumekuwa tukifanya kazi na Rose bila matatizo yoyote. Hizi taarifa zinanishangaza na najua wanaozieneza hawanitakii mema,” alisema Batuli.

AIBU! MKE, MUME WAZICHAPA WAFUNGA MTAA

$
0
0

Stori: Richard Bukos/GPLHii ni aibu kubwa! Njemba mmoja aliyefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma Mtata, wakazi wa mtaa Mrefu,  Kigogo-Luhanga jijini Dar wamenaswa wakiangusha bonge la timbwili barabarani na kusababisha umati wa watu kujikusanya eneo hilo kujionea ‘sinema’ ya bure.
Timbwili zito likianza kati ya njemba mmoja anayefahamika kwa jina la Zeno na mkewe Mwajuma Mtata.
Tukio hilo lililofananishwa na muvi ya kivita lilitokea usiku wa Jumanne iliyopita ambapo chanzo kimedaiwa kuwa ni mwanamke huyo kutelekeza jikoni kitoweo cha maini ya mbuzi na kwenda baa kupata kilaji.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, siku ya tukio, Zeno alirudi nyumbani mida ya jioni mkononi akiwa na kifurushi chenye maini ya mbuzi pamoja na mazagazaga mengine zikiwemo ndimu, tangawizi, pilipili hoho, nyanya na vitunguu kupokelewa na ‘mai waifu’ wake huyo.
Mke akimlia 'taimingi' kumbwaga mume wake kwa mweleka.
MUME ATOKA KIDOGO
Baada ya Zeno kumkabidhi mkewe mazagazaga hayo kwa ajili ya mlo wa usiku, alimuaga mkewe kuwa anakwenda kutembea ili akirudi akute msosi uko tayari, wale, walale.
“Dakika kadhaa baada ya mumewe kutoka, nasikia bibie naye alichomoka na kwenda baa ya jirani ‘kusukutua mdomo’.
Mara Puuuuu...!! wote chini
“Sasa akiwa pale baa, alizidi kunogewa na masaa yalizidi kupotea ndipo Zeno alirudi nyumbani na kukuta mlango umeegeshwa na mkewe hayupo huku akisikia harufu kali ya kitu kuungua na kumfanya apige chafya.
“Alipokaa sawa alibaini kuwa maini aliyoleta yalikuwa yameungua na kuwa kama mkaa hali iliyompandisha hasira na kuanza kumsaka mkewe,” kilidai chanzo hicho.
Mume (Bw Zeno) akimburuta mkewe kwa ghadhabu.
AMUIBUKIA BAA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, Zeno akiwa katika sakasaka yake ndipo alipombamba mkewe kwenye baa hiyo akimalizia ‘kunyonya’ kilevi kikali.
ZACHAPWA
Bila kuuliza, Zeno alimkunja mkewe na kumtoa nje huku akimpa makofi ndipo Mwajuma akaona kama anaonewa hivyo akamvizia mumewe na kumchota mtama ambapo wote walikwenda chini kutokana na kuwa katika hali ya kuzidiwa na kilaji.
Wote wakichukua uamuzi wa kuzima timbwili hilo.
LAHAMIA NJE YA BAA
Timbwili hilo liliendelea nje ya baa hiyo ambapo vijana wawili wa mtaani hapo waliofahamika kwa majina ya Haidani na Kulwa walihofia yangeweza kutokea machafuko zaidi wakakimbilia kwa mjumbe wa eneo hilo aliyefahamika kwa jina la Shukuru lakini walimkuta mke wa mjumbe ambaye aliwaambia mumewe alikuwa kazini.
Mke(Bi Mwajuma Mtata) akijaribu kuzuia kupigwa picha na kamera za wanahabari.
WARUDI NYUMBANI
Wapenzi hao baada ya kugaragazana vya kutosha ikiwa ni pamoja na kuvuana nguo, mwanaume alianza kumburuza mkewe na kurudi nyumbani kwao ambapo walipofika eneo la Kwamkoma walianza kutifuana tena kabla ya kuamuliwa na wasamaria wema.
Jirani akihoji kulikoni mpaka iwe hivi...
ETI WAMEYAMALIZA!
Taarifa tulizozipata wakati gazeti hili lilipokuwa linakwenda mitamboni juzi, Jumatano, wawili hao walikuwa tayari wameshayamaliza na wanaishi raha mustarehe baada ya kuombana msamaha.

A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 08

$
0
0

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

“Utamuweza lakini?” Mwanaume mmoja aliyekuwa na misuli alimuuliza Dominick ambaye alikuwa amevaa miwani mikubwa iliyokuwa na rangi nyeusi.
“Kwa nini nisiweze. Ebu niangalie, unanionaje?” Dominick alimuuliza kijana yule.
Muziki bado ulikuwa ukiendelea katika klabu hiyo ya Raspinho, taa hafifu ndizo ambazo zilikuwa zikiwaka. Wanawake mbalimbali wazuri ambao kazi yao ilikuwa ni kujiuza walikuwa wamesimama pembeni huku wakijaribu kufanya matangazo kwa kila mvulana ambaye alikuwa akiwaangalia katika klabu ile.
“Nakuuliza tena..utaweza?” Mwanaume yule bado alikuwa akimuuliza Dominick.
“Nitaweza bwana. Mimi ndiye Maliki Mtanga. Nimezaliwa kwa ajili ya kufanya ngono tu” Dominick aliongea huku akijisifia.
“Kumbe umetokea Tanga”
“Ndio. Kule Handeni”
“Basi wewe utakuwa unaweza. Manake mwanamke mwenyewe hataki niwaletee vijana legelege. Kama ndio hivyo basi poa” Mwanaume yule alimwambia Dominick pasipo kumfahamu kutokana na uhafifu wa taa pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa.
Dominick hakuwa kabisa mtu wa klabu, ila alifika mahali hapo kwa ajili ya kazi kubwa ambayo alikuwa nayo mbele yake. Alizifahamu vilivyo tetesi alizokuwa nazo Bi Magdalena, alifahamu vilivyo kwamba mwanamke huyo alikuwa na pepo la ngono.
Hakuwa akimpenda, lakini alitakiwa kufanya hivyo kwa kuwa alihitaji sana kukamilisha kile ambacho alikuwa amekipanga. Kamwe Dominick hakuwa mtu wa pombe lakini siku hiyo pombe aina ya Kilimanjaro ilikuwa katika kaunta huku akijfanya anainywa.
“Huyo hapo. Ngoja nikaongee nae” Mwanaume yule alimwambia Dominick katika kipindi ambacho Bi Magdalena alikuwa akiingia pamoja na binti yake, Sara.
Dominick akaonekana kutabasamu. Yule mwanaume ambaye alionekana kuwa mlinzi wa klabu ile mule ndani akaanza kumfuata Bi Magdalena na kisha kuanza kuongea nae. Walitumia dakika kumi kuongea, mwanaume yule akaanza kumrudia Dominick huku akionekana kutabasamu.
“Vipi?” Dominick alimuuliza huku akiwa na shauku ya kutaka kufahamu.
“Tayari. Kila kitu kipo fresh ingawa alikuwa akikaza. Si unajua hataki skendo” Mwanaume yule alimwambia Dominick
“Kwa hiyo fresh kabisa?” Dominick aliuliza huku akionekana kutokuamini.
“Fresh. Nilipomwambia kwamba umetoka Tanga, alipagawa kinoma”
“Kweli?”
“Ndio hivyo”
“Kwa hiyo nini kinafuata?”
“Ngoja kwanza. Kila kitu kitakuwa fresh”
Dominick akaamua kutulia, akaangalia saa yake, saa ilikuwa ikionyesha kuwa tayari ilikuwa saa saba na nusu usiku. Aliendelea kuzuga kunywa pombe ile mpaka saa nane ilipotimia na Bi Magdalena kumtuma mwanaume yule kumuita Dominick ambaye alikuwa amejitambulisha kwa jina la Maliki.
Kwa haraka haraka Dominick akainuka na kuanza kuelekea kule alipokuwa Bi Magdalena. Akamsalimia kwa salamu kama ambavyo mara kwa mara alikuwa akiwasalimia vijana wenzake. Akakaribishwa kiti na kutulia. Hapo ndipo maongezi yalipoanza.
Waliongea kwa muda mrefu huku wakitafuta muda wa kuzoeana. Dominick akaamua kuitumia nafasi hiyo kumuonyeshea Bi Magdalena ni kwa kiasi gani alikuwa na uwezo wa kumfanya chochote alichotaka kufanyiwa usiku huo.
“Unajua kuchuma mboga?” Dominick alimuuliza Bi Magdalena.
“Aaaaah! Mbona kila mtu anaijua. Hata binti yangu Sara anaifahamu” Bi Magdalena alisema huku akionekana kuanza kulewa.
“Usijali. Nitakupa nyingine kama kumi hivi. Najua kifo cha mende unaifahamu sana…mimi nitakuwa mwalimu wako leo, nitataka tuandike herufi moja baada ya nyingine” Dominick alimwambia
“Tuandike herufi? Herufi gani?”
“Nimejua tu, bado u mdogo kimapenzi. Nitataka tuchore L kitandani, tukitoka hapo, tunachora C huku tukimalizia na T” Dominick alimwambia Bi Magdalena.
Bi Magdalena akaonekana kuchanganyikiwa, maneno ya kimahaba ambayo aliyaongea Dominick yalionekana kumchanganya. Moyo wake ukawa na shauku kubwa ya kutaka kuondoka nae ili aende akachorwe herufi hizo kitandani.
Akanywa pombe haraka haraka, tayari pepo la ngono lilikuwa limekwishampanda, akachanganyikiwa kabisa. Kila wakati akabaki akimwangalia Dominik kwa macho yaliyojaa mahaba. Akaanza kuupeleka mkono wake katika mapaja ya Dominick na kuanza kuupandisha juu hadi katika sehemu ya zipu.
“Mbona una haraka hivyo? Subiri, malizia pombe kwanza. Leo nataka kukuonyesha kwamba mimi ni mtoto wa Tanga. Tukianza tu…tunasitisha baada ya masaa mawili” Dominick alimwambia Bi Magdalena ambaye akaonekana kushtuka.
“Masaa mawili?”
“Ndio. Tena hapo kama utataka tufanye haraka haraka. Awamu ya pili sitokwambia tutachukua masaa mangapi, manake unaweza ukakataa” Dominick alimwambia Bi Magdalena
Bi Magdalena akaonekana kupagawa zaidi, akili yake ilikuwa ikijiuliza ni kwa jinsi gani kijana aliyekuwa akiongea nae alikuwa na uwezo mkubwa kitandani. Akamuita binti yake, Sara na kuanza kuongea nae kwamba alikuwa akitaka kuondoka mahali hapo.
“Utanipgia simu basi” Sara alimwambia mama yake.
“Sawa” Bi Magdalena alimwambia na kisha kuondoka pamoja na Dominick.
Safari ikaanza huku Dominick ndiye akiwa dereva wa gari la kifahari ambalo alikuja nalo Bi Magdalena na binti yake Sara. Ndani ya gari Bi Magdalena alikuwa akiongea maneno ya mahaba tu, alimuona Dominick akiendesha kwa mwendo mdogo.
Alitamani kufika haraka katika sehemu ambayo angechorwa herufi ambazo Dominick alikuwa amemulezea pasipo kujua mwanaume huyo alikuwa nani. Kila alipokuwa akijaribu kuvuta picha ya mambo ambayo yangefanyika kitandani, Bi Magdalena alibaki kuwa na mshawasha wa kufika haraka.
“Paki gari pembeni” Bi Magdalena alimwambia Dominick ambaye akatii amri kwa kulipaki gari lile pembeni.
“Kuna nini tena?”
“Tunachelewa bwana. Njoo huku nyuma” Bi Magdalna alimwambia Dominick huk akimvuta katiks viti vya nyuma.
“Subir tufike hotelini”
“Hapana. Nimezidiwa. Njoo japo unifanyie herufi moja, halafu nyingine tutazimalizia hotelini” Bi Magdalena alimwambia Dominick ambaye alibaki amechanganyikiwa.
                                                                    ********
“Unasemaje?” Sara aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Ndio hivyo. Jamaa ametoka Tanga, halafu inaonekana nuksi” Mwanaume yule mlinzi alimwamba Sara ambaye alionekana kuchanganyikiwa.
“Mbona haukuniambia? Au unataka raha azipate peke yake? Yaani leo unanigeuka Dickson” Sara alimwambia Dickson huku akilalamika.
“Mbona unakuwa mkali sana leo. Unanilalamikia sana na wakati muda mwingine nakuitia wewe peke yako” Dickson alimwambia Sara
“Lakini sio kwa mtu wa leo. Mtu ametoka Tanga halafu unampa yule bibi. Haiwezekani, kama mambo bora tupewe wote” Sara alisema huku akitoka ndani ya klabu ile. Akakodi bajaji na kuanza kuelekea katika hoteli ya Supernova ambayo mara zote mama yake alikuwa akiitumia kufanya ngono na vijana.
Njiani Sara alikuwa na mawazo, alitaka kufika haraka hotelini. Kijana ambaye aliondoka nae mama yake tayari alionekana kumchanganya. Pepo la ngo lilikuwa limekwishaanza kmpanda. Muda wote macho yake yalikuwa yakiangalia nje huku upepo ambao ulikuwa ukimpiga ukionekana kumchanganya kabisa.
“Hebu subiri” Sara alimwambia dereva Bajaji mara baada ya kuiona gari aina ya VX likiwa limepakiwa pembeni mwa barabara. Sara akateremka na kuanza kupiga hatua kuifuata gari ile. Alijua fika kwamba gari lile lilikuwa lile walilokuja nalo, alimjua vilivyo mama yake ambaye mara nyingine alikuwa akifanya ngono garini.
Kadri alivyokuwa akilisogelea na ndivyo ambavyo mwili wake ulivyokuwa ukimsisimka. Nywele zilikuwa zikimsimama huku mshawasha wa kufanya mapenzi ukimshika. Alipolifikia gari lile, akajaribu kuchungulia garini, hakuona kitu chochote kutokana na giza kubwa. Akachukua simu yake ambayo ilikuwa na tochi na kumulika ndani.
“Mungu wangu……….!”
                                                            ************
“Mbona unalia Ombeni. Yaani niliyefiwa wala silii namna hiyo, wewe ndiye ambaye unalia, kwa nini?” Bwana Boniface alimuuliza mzee Ombeni.
“Haujui kama nami familia yangu imeteketezwa kwa moto? Haujui kama nami pia nimempoteza mke wangu na mtoto wangu?” Mzee Ombeni alimwambia Bwana Boniface.
“Kumbe na wewe pia umeipoteza familia yako? Mungu wangu…….” Bwana Boniface alisema.
Mzee Ombeni akashtuka kutoka kitandani, kijasho chembamba kilikuwa kikimtoka, ndoto ambayo alikuwa ameiota ilionekana kumtisha kupita kawaida. Cha kwanza akaangalia kitandani pale, alikuwa peke yake. Akainuka na kuelekea sebuleni, mkewe pia hakuwepo mahali pale. Wasiwasi ukaanza kumshika, akarudi tena chumbani na kuanza kumpigia simu mkewe lakini simu wala haikupatikana.
Mwili wake ukaanza kumsisi mka, kijasho chembamba kikaaanza kumtoka. Akaamua kutoka na kuelekea katika chumba cha binti yake, akanza kuugonga mlango lakini wala hakukuwa na mtu yeyote aliyemjibu hali iliyoonyesha kuwa hata nae hakuwepo.
Mzee Ombeni akarudi tena chumbani kwake na kutulia. Akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi kupita kiasi. Ingawa mara kwa mara mkewe alikuwa akimtoroka usiku na kwenda katika nyumba za starehe wala hakujali kabisa lakini siku hiyo akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi kupita kiasi.
Ndoto ya kutisha ambayo alikuwa ameiota ndio ambayo ilionekana kumtisha zaidi. Akatoka na moja kwa moja kuelekea nje, gari yake ya VX wala haikuwepo hali iliyoonyesha kwamba kulikuwa na mtu ambaye aliichukua. Hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, moja kwa moja akalifuata gari jingine aina ya Range Rover na kuanza kuondoka mahali hapo.
Kazi yake ilikuwa moja tu, kulitafuta gari lak katika kila klabu ya usiku ambayo alikuwa akiifahamu. Breki ya kwanza ilikuwa San Siro, hakukuwa na gari lake katika sehemu ya kuegeshea magari.
Hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, safari yake ikaendelea zaidi kwenda katika klabu nyingine zaidi. Katika kila klabu ambayo alikwenda, wala gari lake hakuliona. Akajihisi kuchanganyikiwa kupita kiasi. Alitembea katika klabu zaidi ya kumi na tano Dar es Salaam lakini wala hakuliona gari lake.
Akaliegesha gari lile pembeni na kuanza kufikiria kama kulikuwa na klabu yoyote ambayo hakuwa ameitembelea usiku huo. Jina la klabu ambalo lilikuwa limeingia kichwani mwake ilikuwa klabu ya Raspinho. Mzee Ombeni hakutaka kukubaliana na hilo, allijihisi kuchoka sana.
“Haiwezekani wawe kule bwana. Ngoja nirudi nyumbani” Mzee Ombeni alijisemea.
Akageuza gari na kuanza kuelekea nyumbani kwake. Ghafla akalisimamisha gari lake, akakata kona na kuanza kurudi kule alipotoka. Tayari akaonekana kushikwa na machale, hakuwa tayari kurudi nyumbani pasipo kwenda Raspinho Club kuhakikisha kama familia yake haikuwa kule.
Alipofika katika eneo la klabu ile, hakukuwa na gari lake hali iliyomfanya kukata tamaa zaidi. Akaanza kuligeuza, lakini alipoangalia vizuri, idadi ya watu ilikuwa kubwa sana nje hali iliyomfanya kuteremka na kuanza kupiga hatua kuelekea kule watu walipokuwa akikusanyika huku tayari ikiwani saa tisa usiku.
Watu walikuwa wakiongea kwa sauti kubwa sana lakni mara baada ya kumuona mzee Ombeni akiwasogelea, wote wakanyamaza na kuanza kumwangalia mzee huyo ambaye alionekana kutaka kusikia ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea.
“Kuna nini jamani?” Mzee Ombeni aliuliza lakini hakukuwa na mtu aliyejibu chochote kile, umati wote wa watu themanini waliokusanyika mahali pale ulibaki kimya hali iliyoanza kumtia wasiwasi mzee Ombeni.
                                                            **********
Dominick hakutaka kabisa kufanya kufanya mchezo wowte wa ngono hasa na mwanamke yule ambaye alikuwa akionekana kuwa kama mama yake. Alimwangalia Bi Madgalena mara mbili mbili, tayari pepo la ngono lilikuwa limekwishampanda kwa asilimia mia moja.
Mwili wake ulikuwa umemlegea kupita kiasi, akaanza kuchojoa kila nguo ambayo alikuwa ameivaa. Alipomuona Dominick hafanyi kitu chochote kile, akaanza kumvua shati lake. Domonick alikuwa akipapaswa kila seheu ya mwili wake huku Bi Magdalena akitoa milio mbalimbali ya mahaba.
“Mbona una bunduki?” Bi Magdalena alimuuliza Dominick mara alipokuwa akimvua suruali.
“Si unajua mimi mlinzi wa Benki Kuu Tanzania. Nimetoroka kule kwa ajili yako, yaani kuja kukuonyesha ni kwa jinsi gani mapenzi yanavyofanywa, sio kama vijana wengine ambao wanakuvua nguo halafu mambo yao yanakuwa ya kitoto” Dominick alidanganya.
Udanganyifu ule ulimfanya Bi Magdalena kuchanganyikiwa, bado alitamanisana kuuona umakini wa Dominick wa kufanya mchezo wa ngono kitandani. Akamvua suruali haraka haraka na kisha kumvutia kifuani mwake.
Dominick hakuwa akijisikia kabisa kufanya mchezo wa ngono na mwanamke yule ambaye alikuwa taabani. Dominick akachukua bunduki yake na kuiweka vizuri. Akachungulia nje, hakukuwa na gari lolote lililokuwa likipita barabarani kutokana na usiku kuwa mkubwa.
“Bado sijaridhika. Nikimuua huyu, bado na binti yake. Halafu sitaki afe kwa risasi, huyu ni kuchomwa moto tu” Dominick aliwaza.
“Ngoja nimpige risasi hata ya mbavu, sitaki kumuua. Baada ya hapo nitamfuata binti yake kumleta huku” Dominick alijisemea.
Akaikoki bunduki yake vilivyo, Bi Magdalena bado alionekana kuwa katika mahaba mazito. Alichokifanya Dominick ni kuanza kumpapasa Bi Magdalena ili aweze kumvuruga zaidi. Bi Magdalena akachanganyikiwa kupita kawaida, akaanza kukunja kunja vidole vyake vya mguuni kuonyesha ni kwa jinsi gani kwa wakati huo alikwa amechanganyikiwa.
Dominck hakutaka kupoteza muda, hapo hapo akakibonyeza kitufe cha kuruhusu risasi, ukelele mkubwa ukaanza kusikika kutoka kwa Bi Magdalena. Damu nyingi zilikuwa zikimtoka mbavuni. Dominick akaonekana kushtuka, mara baada ya kuchungulia nje na macho yake kuiona Bajaji ikiwa imesimama kwa mbali, mtu msichana mmoja akateremka a kisha Bajaji ile kuondoka.
Kwa haraka haraka huku akiogopa kuonekana, akaufungua mlango wa upande mwingine na kuteremka huku akimvizia kuona msichana yule alikuwa nani. Dominick akashtuka kwa furaha, taa za gari lile ambazo zilikuwa zikiendelea kuwaka zilimuwezesha kumjua msichana ambae alikuwa akisogea mahali kule alipokuwa.
“Mungu wangu! Kweli Mungu yuko pamoja nami” Dominick alijisemea huku akisogea kule nyuma ya gari.
Sara akasogea mpaka katika mlango mmoja wa gari lile na kuanza kuchungulia. Alikuwa na uhakika kuwa mama yake alikuwa amezidiwa na hivyo alihitaji kufanya ngono hata garini kwani mara kwa mara alikuwa akifanya mchezo huo garini.
Hakuona vizuri garini kitu ambacho kilimfanya kuchukua simu yake iliyokuwa na tochi na kisha kuchungulia. Sara akashtuka, alimuona mama yake akiugulia kwa maumivu. Damu nyingi zilikuwa zikimtoka kupita kawaida. Alichokifanya ni kuanza kuufungua mlango ule, mlango ulikuwa umefungwa.
Kwa mwendo wa kasi akaanza kuzunguka nyuma ya gari ili kuufungua mlango mwingine, akashtukia akipigwa ngumi nzito usoni nzito ya kushtukiza ambayo ilimfanya hapo hapo kuanguka chini na kupoteza fahamu.
Kwa haraka haraka Dominick akambeba Sara na kumingiza garini. Akalwasha gari na moja kwa moja kuondoka mahali hapo. Breki ya kwanza ilikuwa katika kituo cha mafuta ya Petroli ambako akateremka na kumfuata muuzaji mmoja.
“Nahitaji mafuta ya petroli lita kumi” Dominick alimwambia muuza mafuta wa kituo cha kuuzia mafuta.
“Sogeza gari basi karibu”
“Hauwezi kuniwekea kwenye dumu? Si unajua nakwenda kuyamiminika katika gari jingine” Dominick alimwambia muuza mafuta
“Daaa! Kazi itakuwa kutafuta dumu”
“Kwa hiyo hakuna madumu kabisa mahali hapa?”
“Yapo ila mwenyewe akijua kwamba nimeyatoa na kumpa mtu mwingine anaweza akanianzishia utata” Muuzaji yule alimwambia Dominick ambaye alibaki kimya kwa muda.
“Huwa anayauza?” Dominick aliuliza
“Ndio. Moja elfu nne”
Dominick hakutaka kupoteza muda, akatoa kiasi cha shilingi elfu tano na kumgawia muuzaji mafuta ambaye akaenda kuchukua hilo dumu na kurudi nalo. Mafuta yakawekwa ndani ya dumu lile na kisha kulipa fedha zote ambazo zilikuwa zikihitajika.
Dominick akalichukua dumu lile na kulipandisha garini. Sauti ya Bi Magdalena ilikuwa ikisikika kwa chini sana, bado damu zilikuwa zikiendelea kumtoka. Sara ambaye alikua pembeni hakuonekana kurudiwa na fahamu, ngumi nzito na ya kushtukiza ilionekana kumuingia vilivyo.
Dominick akaangalia saa yake ambayo ilikuwa ikimuonyesha kuwa tayari saa tisa na nusu usiku. Alichokifanya ni kuendesha kwa kasi kuelekea katika ufukwe wa Coco ambako aliamini kwa muda ule, hakukuwa na mtu yeyote ambaye angekuwepo mahali pale.
Hakukuwa na magari barabarani hali ambayo ilimfanya Dominick kuendesha kwa kasi ambayo alitaka kuendesha. Alipoanza kuingia katika eneo la ufukwe ule, akazima taa zote na kuanza kuelekea katika eneo lile lile ambalo alilichomea gari la Bwana Boniface.
Akalisimamisha gari lile, akaanza kulimwagia mafuta kwa kasi ya ajabu kuanzia nje hadi ndani. Akawamwagia mafuta Bi Magdalena pamoja na binti yake, Sara. Bado sauti ya chini iliyojaa maumivu ilikuwa ikisikika kutoka kwa Bi Magdalena
Dominick hakuonekana kujali, bado aliendelea kuwamwagia petroli. Alipomaliza akaingiza mkono mfukoni na kuchukua kiberiti, akaliwasha gari lile. Moto mkubwa ukaanza kuwaka, Dominick akabaki pembeni akicheka tu. Gari liliendelea kuteketea zaidi na zaidi, uso wake bado ulikuwa umetawaliwa na tabasamu.
Mwanga wa tochi ukammulika usoni, Dominick akaonkana kushtuka kupita kiasi. Alijua kwamba mahali hapo alikuwa peke yake kutokana na usiku kuwa mwingi sana. Tochi ambayo ilimmulika usoni ndio ambayo ikamfanya kuanza kukimbia.
Milio ya mbwa waliokuwa wakija kwa kasi ikaanza kusikika. Dominick akaongeza kasi zaidi na zaidi. Mchanga mwingi wa ufukweni ndio ambao ulimfanya kutokukimbia kwa kasi. Mbwa watano walizidi kumsogelea zaidi na zaidi, ni umbali wa hatua kumi tu ndizo ambazo walikuwa wamebakiza kabla ya kumkamata Dominik ambaye alionekana kuchoka kutokana na mchanga mwingi uliokuwa pale ufukweni ambao ulimfanya kutokumbia kwa kasi.
“Kama kunikamata…acha tu wanikamate…sina ujanja” Dominick alijisemea huku kasi yake ikianza kupungua Tayari alikuwa amekwishakata tamaa kabisa. Aikuwa tayari kukamatwa na mbwa wale, kuumwa na hatimae mtu yule aliyemmulika tochi kumfikia.
                                                               *******
Walinzi  wanne walikuwa wakiendelea na ulinzi katika nyumba ya balozi wa Marekani Bwana Brown Poll. Mbwa wakali ambao walikuwa wamepewa mafunzo ya kutoshwa walikuwa mikononi mwao, tochi pamoja na bunduki zilikuwa mikonon mwao.
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ITAENDELEA SIKU YA KESHO..

USIKU WA KIGODORO - 8

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ILIPOISHIA: James alikuwa bafuni akijimwagia maji, Lina akavuta simu yake na kuanza kusachi majina ili alipate la Kindaundau…
“Kindaundau…Kindaundau…Kindaundau…”
Akakumbana nalo limeandikwa…
“Kindaundau 2.”
KANYAGA NAYO…
Haraka sana akaisevu namba hiyo kwenye simu yake na kuirudisha simu mahali pake. Akajibalaguza akifikiria namba ambavyo atawasiliana na mtu huyo na kumwambia chondechonde asije akatumbua jipu kama si kidonda.
***
James alipotoka kuoga alijiweka kwenye kitanda na kumwita Lina mke wake ili ambembeleze kwa mahaba mazito kwa wakati ule ingawa pia, Lina alikuwa na mawazo kichwani ya kuangalia namna atakavyoaga na kurudi kwa mumewe Semi.
“Baby, njoo basi, unajua nimekumisi sana!”
“Hata mimi my love, nimekumisi pia.”
“Basi kumbe tumemisiana.”
“Ni kweli d.”
Kwa muda huo wakiwa juu ya sita kwa sita, James alikuwa fiti kimahaba lakini Lina alionekana kuwa chini kuliko kiwango chake jambo ambalo lilimshangaza sana James, akamuuliza huku mechi ikiendelea…
“Nahisi kama hauko sawa dear.”
“Ni kweli.”
“Kwa nini? Kuna nini kimetokea?”
“Ah! Basi tu, sijui leo nimeamkaje?!”
“Unajisikiaje kwani?”
“Mwili na akili vyote havipo sawasawa.”
“Unawaza nini?”
“Sijui tu.”
James aliposikia hivyo aliamua kujitahidi mwenyewe na alipomaliza safari yake akajiweka pembeni, naye akazama kwenye mawazo kuhusu Lina…
“Hii ndoa ipo haipo? Mbona kama sielewielewi…
“Mtu anasema ana mawazo, mawazo gani sasa wakati mimi nipo na ndiyo kwanza tupo kwenye ndoa mpya tena fungate.”
Lina aliiona hali ya James akajua naye hayuko sawa kama yeye, lakini alishindwa kumuuliza waziwazi.
“Lina,” aliita James…
“Abee.”
“Naomba leo tuondoke kwenda nyumbani, sina amani tena na hapa hotelini.”
Lina alishtuka sana lakini kwa siri ili asijulikane, aliamini kitendo cha kwenda nyumbani kwa James ndiyo mambo yatakuwa wazi mapema sana jambo ambalo hakulipenda…
“Kuna nini kimetokea baby?”
“Nimeamua hivyo tu.”
“Ndiyo umeamua, kuna nini?”
“Hakuna kitu Lina, fuata ninayosema.”
“Oke, sawa! Nimekuelewa!”
“Kama umenielewa vizuri, naomba jiandae kwani tunaondoka muda huuhuu, sioni sababu ya kupoteza muda.”
Lina alijiandaa, akili ilizidi kuvurugika, aibu aliiona mbele ikimnyemelea, angesema nini…
“Hivi likibumbuluka nitasema nini mimi?” alijiuliza mwenyewe.
Walishuka hadi kwenye gari la kifahari la James, wakazama humo na kuondoka hadi nyumbani kwa James ambapo Lina alipokelewa kwa shangwe na wafanyakazi wa ndani wa James wakijua amekwenda rasmi na si kama mchumba. Salamu zikawa nyingi, karibu za kumwaga!
Moyoni Lina alisema…
“Mh! Mngejua nimelikoroga wala msingenishobokea, yaani nyie mko huru kuliko mimi hapa.”
Bado Lina alikuwa na mawazo ya jinsi gani ataaga kurudi kwa Semi. Aliona afadhali walivyokuwa hotelini kuliko pale nyumbani.
“Bosi samahani, alikuja Bryan, akasema ukija muonane, amepata ule mzigo,” alisema mlinzi wa getini akimwambia James.
James aliachia tabasamu kusikia maneno hayo, palepale alimuaga Lina kwamba anaondoka atarudi ndani ya dakika 50 mpaka saa moja.
“Sawa baby.”
***
Baada ya James kuondoka, Lina aliingia chumbani, akatoa simu yake huku akifurahi kwamba atapata nafasi ya kuongea na Kindaundau sasa, akapiga simu hiyo lakini haikuwa hewani!
“Mungu wangu! Au Kindaundau 2 niliyoichukua haitumiki kwa sasa?” alijiuliza mwenyewe Lina huku mapigo ya moyo yakiendelea kumdunda.
***
Katika kuelekea nyumbani kwa Bryan, James alipita mahali akakutana na Eg, rafiki wa Lina akiwa na rafiki zake wawili, wamejikwatua hao mfano hakuna, akasimamisha gari ili kumsalimia…
“Shemu vipi?”
“Shwari shemeji yangu, hajambo Lina?”
“Hajambo, wapi shemeji mbona umependeza sana?”
“Tunakwenda kwenye kikao cha hawa rafiki zangu, kinafanyika Mikocheni.”
“Ooo! Sawa! Mgonjwa anaendeleaje?”
Eg ndiyo akashtuka kusikia habari ya mgonjwa, akakumbuka dili lake na Lina. Kwa jinsi alivyojipara alishindwa kusema mgonjwa bado kalazwa, angeonekana hajali, akasema…
“Mgonjwa katoka mchana wa leo shemeji, hivi hata Lina hajui lolote.”
“Ala! Afadhali, poleni sana,” alisema Lina huku akiingiza mkono kwenye mfuko  wa shati na kutoa shilingi elfu hamsini, akampa…
“Ongezea nauli shemeji.”
“Jamani shemeji, asante sana jamani, Mungu akubariki sana.”
“Usijali shemeji.”
***
Baada ya kuondoka tu, Eg akampigia simu Lina ili kumpa tukio hilo…
Sasa kaondoka, akirudi nitakwambia ili  unipigie simu usingizie yule mgonjwa, kwamba unaniomba nikalale naye ili wewe urudi nyumbani, niweze kurudi kwa Semi la sivyo mwenzio naumbuka…”
“Shoga pole, haitawezekana,” alijibu kwa mkato Eg…
“Eh! Eg, kwa nini? Ni wewe au mwingine?”
“Yaani namaanisha tumekutana na shemeji sasa hivi?”
“Yupi?”
“Si James. Sasa hivi, tunaagana ndiyo na mimi nikaamue kukupigia simu. Amesema anakwenda wapi sijui, lakini kwa rafiki yake.”
“Mh! Alikuuliza kuhusu mgonjwa?”
“Ndiyo swali lake la kwanza. Kauliza vipi mgonjwa shemeji? Na mimi kwa jinsi nilivyovaa na kujipata leo nakwenda kwenye kile kikao cha akina Mama Mumba, nikajikuta nimemwambia mgonjwa katoka.”
“Ayaaaa! Umeniua Eg, nitadanganya nini sasa kwa James mpaka anikubalie kutoka na kwenda kulala hukohuko mpaka kesho?”
“Aisee! Sijui iweje! Halafu mbaya zaidi nilimwambia kabisa kwamba nakwenda kikao cha harusi.”
Lina alikata simu kwa hasira. Alimchukia Eg. Aliamini anaweza kuwa chanzo cha lolote litakalotokea kwake na James na Semi.
“Khaa! Sasa huyu mbona amekata simu?” alijihoji Eg akianza kuingiwa na wasiwasi.
Kwa upande wake, Lina aliamua liwalo kwa siku hiyo na liwe, alishajua kisingizio hakuna tena. Aliamua kupanda kitandani na kujipumzisha huku akiwaza sana kuhusu hatima yake.
“Sijui nini hatima ya hili sakata langu, nahisi Eg naye ameanza kunikimbia, ni kwa nini amwambie anakwenda kwenye kikao cha harusi wakati anajua yeye ndiyo tegemeo langu la kuondokea kwa James?”
***
James alirejea nyumbani hapo saa kumi juu ya alama. Alipoingia ndani tu aliita kwa sauti ya juu…
“Baby wa James.”
Lina alikuwa chumbani kwa hiyo hakusikia, ila mfanyakazi mmoja wa ndani alimwambia bosi wake huyo kwamba, Lina alikuwa chumbani.
Alikwenda chumbani na kusukuma mlango, akazama ndani na kwenda kumkumbatia Lina…
“Baby nimekumisi sana…”
“Mmmh! Jamani baby, hata mimi. Ila sina amani sana dear…”
“Kisa nini tena?”
“Nimetumiwa meseji mama anaumwa sana nyumbani, Korogwe! Si unakumbuka hata kwenye harusi yangu nilikwambia hatakuja?”
“Ndiyo…sasa?”
“Da! Sijui niende?”
“Ah! Lina mke wangu, suala la mama kuumwa ni la kuamua uende au usiende? Unatakiwa kwenda, ikibidi hata kesho asubuhi na mapema.”
“Ooh! Nashukuru kwa ruhusa baby, nilijua hutapenda ukizingatia tumetoka kwenye ndoa juzi tu.”
“Kutoka kwenye ndoa si ishu Lina, uzima wa mama ni wa mbele. Hata kama tungekuwa tumefunga ndoa leo, usiku ukaambiwa mama anaumwa, ingebidi kwenda.”
***
Usiku uliingia, Lina aliamua kuzima simu ili Semi asimpate moja kwa moja. Alijua angepigiwa na angeshindwa kujibu au kudanganya mbele ya James…
“Lakini sasa hatima yake ni nini kama hatanipata hewani? Je, atanitafuta kwa Eg? Na kama atakwenda kule halafu asinikute, nini kitafuata? Da! Huu mzigo ni mkubwa sana kwangu, vigumu kuubeba,” aliwaza moyoni Lina kiasi kwamba, James aligundua hilo…
“Baby, pungumza mawazo. We kesho nenda, asubuhi sana mimi nitakupeleka stendi. Kama ungekuwa unaweza kuendesha gari ungetumia gari moja,” alisema James huku akiwa anamshikashika sehemu mbalimbali mkewe huyo.
Lakini Lina alikumbuka kitu, akawasha simu ili amtumie meseji Eg kumshawishi wapange uongo mpya kwa mumewe, Semi.
Hata hivyo, kabla hajamtumia meseji yoyote, meseji iliingia kwenye simu yake, ilitoka kwa mumewe…
“Baby, pole na kazi! Nimekupigia simu haupo hewani, pole. Mimi niimepata dharura, nakwenda Iringa na wale jamaa wauza madini, tunarudi keshokutwa. Please take care.”
Lina alihisi ameona nyota ya bahati kwa kupata ujumbe ule kwani ndiyo sababu pekee iliyokuwa na uwezo wa kumpa nafasi ya kulala nje ya nyumbani kwake kwa siku hiyo. 
Alimwangalia James kwa macho yaliyojaa furaha, akamkumbatia na kumsogeza kifuani pake kisha kuanza kumpa mabusu mfululizo.
ITAENDELEA SIKU YA KESHO
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

DIAMOND ACHARUKA BMW LA WEMA!

$
0
0

Ni sheeedah! Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ amecharukia gari aina ya BMW 545 alilozawadiwa mwandani wake, Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ ambaye ni Miss Tanzania 2006/07, akipinga gari hilo kupewa na meneja wake, Martin Kadinda.
 
Gari aina ya BMW 545i alilozawadiwa Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na meneja wake, Martin Kadinda.
DIAMOND ACHANGANYIKIWA
Habari za kipekepeke zilidai kuwa, taarifa ya Kadinda kumpa zawadi ya gari Wema kwenye pati ya bethidei yake Jumapili iliyopita, nyumbani kwake, Kijitonyama, Dar zilimchanganya Diamond na kudai kwamba ni kitu ambacho hakiwezekani kwa maana anamfahamu vyema Kadinda kuwa hana uwezo huo wa kununua BMW la zaidi Sh. milioni 56 za madafu.
 
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akifungua shampeni katika bethidei yake.
Chanzo hicho kiliweka wazi kwamba mkali huyo anayekimbiza na Ngoma ya Mdogomdogo alihamaki baada ya kupata taarifa kuwa siyo yeye peke yake aliyekabidhi zawadi ya gari (Nissan Murano) kwa maana aliamini mwenye zawadi ya gari alikuwa ni yeye tu ambayo ilikuwa ‘surprise’ kwa mpenzi wake huyo.
 
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’akipokea funguo ya gari la zawadi kutoka kwa Meneja wake.
BOFYA HAPA KUPATA ‘UBUYU’
 “Unaambiwa Diamond kachanganyikiwa kabisa kusikia Wema kapewa gari, tena BMW na mbaya zaidi aliyempa gari ni Kadinda huku yeye akiamini kabisa zawadi aliyotoa kwa mpenzi wake asingeweza kupata kwa mtu mwingine yeyote, mwenyewe anasema amedhalilishwa kwani hawezi kutoa gari kisha mwanaume mwenzake naye atoe gari,” kilidai chanzo hicho.
 
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’
Mpashaji huyo alizidi kufafanua kwamba baada ya kupokea taarifa hizo na kuona kwenye vyombo vya habari na mitandao mbalimbali akiwa nje ya nchi, Diamond alianza kufanya utaratibu wa kurudi nchini akitokea Canada ili kujua vizuri kuhusu undani wa hilo gari.
“Yaani ninyi mtasikia, nakwambia kimenuka maana Diamond aliposikia na kusoma habari za BMW la Wema alianza kufanya utaratibu wa kurudi Bongo ili kupata ufafanuzi zaidi,” kilisema chanzo hicho.
 
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’
KADINDA AKOMAA
Kwa upande wake Kadinda ameendelea kusisitiza kwamba yeye ndiye aliyenunua gari hilo na kumkabidhi Wema ikiwa ni michango ya watu wanaomsapoti mwanadada huyo.
Kuhusu gari hilo, watu kibao wamekuwa wakitajwa kulinunua akiwemo mfanyabiashara Mkongo mwenye jina linaloanza na herufi S na mume wa mtu ambaye ni kigogo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Dar anayetajwa kwa herufi moja ya L.
WEMA VIPI?
Jitihada za kumsikia Wema ziligonga mwamba baada ya simu yake kuita bila kupokelewa na hata alipofuatwa nyumbani kwake hakuwepo hivyo juhudi za kupata lake la moyoni zinaendelea. Stay tuned kwani inavyoonekana nyuma ya pazia ya gari hilo kuna siri kubwa!
(CREDIT: GAZETI LA IJUMAA OCTOBA 3, 2014)

SHEREHE YA BETHIDEI YA DIAMOND PLATINUMZ GOLDEN JUBILEE, DAR

SHIGONGO AZINDUA VITABU VYAKE VIPYA MAREKANI

$
0
0

10 Laws-How to Move From Poverty to Prosperity.

26 Secrets- How to Defeat From Enemies and Make Millions of Dollars.
MKURUGENZI Mtendaji wa Global Publishers, Eric James Shigongo amezindua vitabu vyake viwili vipya vya namna ya kuondokana umaskini vyenye majina ya 10 Laws-How to Move From Poverty to Prosperity na 26 Secrets- How to Defeat From Enemies and Make Millions of Dollars.
Shigongo alizindua vitabu hivyo vya ujasiriamali alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Runinga cha Voice of America (Voa) kwenye Kipindi cha Straight Talk of Africa nchini Marekani juzi.
Kwa mujibu wa Shigongo vitabu hivyo vitakuwa vikiuzwa duniani kote ili kuikomboa jamii kwenye wimbi la umaskini.
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>