Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

WEMA SEPETU ASHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA

$
0
0

Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akijiandaa kukata keki yake ya siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake Kijitonyama.
 
Wema Isaac Sepetu akiongea na wageni wake (hawapo pichani) kabla ya kukata Ndafu.
 
Martin Kadinda (kushoto) akimuonesha Wema Sepetu kadi ya gari.
 
Gari aina ya Nissan Murano alilozawadiwa Wema Sepetu na mpenzi wake Diamond Platnumz. 
Gari aina ya BMW alilozawadiwa Wema Sepetu na meneja wake Martin Kadinda.


A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 05

$
0
0

“Yaani bado walikuwa na kisasi na maisha yangu mpaka wakaiangamiza familia yangu?” Dominick aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Edmund...Edmund...yaani watu hawa ndio waliiangaliza familia yangu? Ni lazima niwaue, ni lazima niangamize familia zao pia kama walivyoiangamiza yangu. Tena nitaziangamiza kwa kuzichoma moto na kisha kuwaua wao wenyewe. Ni lazima Edmund. NI LAZIMA……!!!” Dominick alimwambia Edmind huku akilia kama mtoto. Mwili wake ukabaki ukitetemeka kwa hasira, kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo alizidi kutetemeka kwa hasira.
“NI LAZIMA NIWAUE….” Dominick alisema kwa hasira huku akiondoka mahali hapo kwa mwendo wa kasi kuelekea kule walipolipaki gari.
                                                              **********
5
Dominick hakuonekana kuwa na raha kabisa, huzuni ambayo alikuwa nayo katika kipindi cha nyuma ilikuwa imeongezeka zaidi. Kitendo cha kuwafahamu wabaya wake kilionekana kumuumiza kupita kawaida. Hakuamini kama wale mawaziri ndio ambao wangeweza kumfanyia kitu kama kile.
Kila siku mawaziri wale walikuwa wakijifanya kuwa karibu na waandishi wa habari lakini kumbe walikuwa ni watu hatari ambao wala hawakutakiwa kusogelewa. Kila siku ambazo Dominick alikuwa akiwaona wakiongea katika vipindi mbalimbali vya televisheni, alibaki akiumia tu.
Akaamua kujipanga, alitaka kutekeleza kila kitu pasipo wasiwasi wowote wala kujulikana na mtu yeyote. Hakuona sababu ya watu wale kuendelea kuishi na wakati walikuwa wamemuumiza kwa kuiteketeza familia yake kwa kuichoma moto.
Alipanga kuwaua wote, tena si wao tu, angeanza na familia zao na kisha kuwaua wao wenyewe. Alitaka sana nao kwanza waanze kuumia kabla ya kuwamaliza. Alitamani wayaonje maumivu ambayo alikuwa ameyasikia hata kabla hawajaonja mauti.
“Nitaanza na nani sasa” Dominick alibaki akijiuliza.
“Walijiita BoT, nami nitaanza na majina yao kama jinsi yalivyo, ni lazima niwaue” Dominick alisema kwa hasira huku akijifunika shuka na kulala.
Siku iliyofuata Dominick akaanza kufanya maandalizi ya kazi yake ambayo alikuwa ameipanga kuifanya, alitamani kuifanya haraka sana hata kabla hakijaharibika kitu chochote kile. Hakuonekana kuwa na pupa, alitaka kuifanya taratibu lakini kwa umakini mkubwa sana.
Kitu cha kwanza alichokifanya ni kuchukua kitabu kikubwa cha simu za mezani na kuanza kuziangalia namba za simu za ofisini mwao, alipozipata, akaziandika sehemu. Dominick hakuridhika, akaangalia na namba za simu za mezani za nyumbani kwao, nazo akaziandika pembeni pia.
“Nitahitaji unisaidie kitu kimoja” Dominick alimwambia Edmund.
“Kitu gani tena? Kukusaidia kazi yako?”
“Hapana. Kazi hii wala haihitaji msaada wa mtu yeyote, nataka kuifanya mimi mwenyewe”
“Sasa unataka nikusaidie nini?”
“Nahitaji mafuta ya petroli ya lita ishirini”
“Hilo si tatizo. Kuna jingine?”
“Labda na kiberiti pamoja na gari lako. Ile bunduki yako si unayo?” Dominick alimuuliza.
“Ninayo. Nayo pia unaitaka?”
“Ndo maana nikaiulizia”
Edmund akainuka na kwenda chumbani kwake ambako akamletea bunduki pamoja na kiberiti. Akachukua pochi yake na kutoa kiasi kilichotosha cha kununua petroli ya lita ishirini na kisha kuondoka kuelekea katika kituo cha kuuzia petroli.
Wala hakuchukua muda mrefu, akarudi, akamgawia Dominick mafuta yale na kisha kumkabidhi ufunguo wa gari lake. Dominick hakutaka kupoteza muda kubaki mahali hapo, moja kwa moja akatoka nje mpaka katika sehemu ya maegesho ya magari na kuchukua gari la Edmund.
“Nitachukua miezi mingi mpaka kurudi hapa. Nitahakikisha kazi inaanza kwa mmoja baada ya mwingine” Dominick alimwambia Edmund.
“Usijali. Kazi njema” Edmund alimwambia Dominick.
Dominick akaondoka na kuelekea katika hoteli ya La Vista Inn na kuchukua chumba. Hakutaka kuendelea kuishi nyumbani kwa Edmund katika wakati ambao atakuwa akiendelea na kazi yake ya kuuridhisha moyo wake. Huko hotelini ndipo sehemu ambayo alipanga kila kitu, namna ya kuanza kazi mpaka kuimaliza.
“Nitaanza na huyu waziri wa wa Utalii na Mali asili, Boniface Akwaiziwe. Nitaanza kuiangamiza familia yake kwanza, ili achanganyikiwe na aje Dar es Salaam kutokea Bungeni” Dominick alijisemea.
Tayari muda ulikuwa umekwenda sana. Saa ya ukutani wala haikuonekana kwenda tofauti na saa yake ya mkononi, zote zilikuwa zikimuonyesha kuwa tayari saa moja na nusu usiku. Akatoka chumbani na moja kwa moja kuanza kushusha ngazi mpaka chini ambako akaingia katika mghahawa wa chakula hapo hotelini na kuagizia chakula.
Kofia kubwa ya Malboro pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa wala haikumfanya kujulikana. Alionekana kuwa mgeni kwa kila mtu ambaye alikuwa akimwangalia. Alipomaliza kula chakula pale mghahawani, akarudi chumbani kwake kuendelea na kazi ya kupanga mbinu mbalimbali za mauaji.
“Nitaanza rasmi kesho. Ila dereva ndiye mtu wa muhimu sana kupatikana” Dominick alijisemea.
Siku iliyofuata ndio ilikuwa siku ambayo alitaka kuanza kazi. Alichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika nyumba ya waziri Boniface ambako akakaa mbali kidogo na geti lile huku macho yake yakiangalia getini. Wala hazikupita dakika nyingi, akamuona mtu mmoja akipiga hodi katika geti lile.
Dominick akayapeleka macho yake katika saa yake, ilikuwa ikimuonyeshea kwamba tayari ilikuwa saa kumi na mbili na robo asubuhi. Hakuwa na shaka kwamba yule aliyekuwa akigonga hodi alikuwa dereva, mtu ambaye alikuwa akimtaka kwa udi na uvumba.
Dominick akaliwahsa gari lake na kuanza kusogea kule geti lilipokuwa, alipomfikia, akateremka na kuanza kumsogelea huku kofia na miwani vikiwa vimemkaa vizuri.
Dereva yule bado alikuwa akisubiri geti lifunguliwe ili aingie ndani, achukue gari na kumpeleka mtoto wa Waziri shuleni. Mara akashtukia kitu kikiwa kimemgusa kisogoni, alipogeuka, akakutana na mdomo wa bunduki.
Dereva akaonekana kushtuka kupita kiasi, mdomo wa bunduki ulimfanya kumuogopesha. Akayapeleka macho yake usoni mwa mtu aliyemnyooshea bunduki, hakumfahamu kabisa kutokana na kofia pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa.
“Ingia ndani ya gari langu haraka” Dominick alimwambia dereva ambaye bila kubisha, na kwa nidhamu zote, akaingia huku akitetemeka.
“Shikilia usukani. Nataka uendeshe gari wewe mwenyewe” Dominick alimwambia dereva ambaye kwa haraka sana, akashikilia usukani.
“Endesha moja kwa moja kuelekea nyumbani kwako” Dominick alimwambia dereva yule.
“Kwa nini kwangu lakini? Nimekufanya nini mkuu?” Dereva aliuliza huku akitetemeka.
“Nisikilize. Sihitaji maswali, fanya kile ambacho ninakuamuru kukifanya. La sivyo, nitatawanyisha ubongo wako sasa hivi” Dominick alimwambia dereva maneno ambayo yalizidi kumtetemesha zaidi
Hakuwa na jinsi zaidi ya kuwasha gari na safari ya kuelekea nyumbani kwake kuanza. Njia nzima alikuwa akitetemeka kwa hofu, kila alipokuwa akiuangalia mdomo wa bunduki, alizidi kutetemeka. Tayari nguo zake zilikuwa zimekwishaloana kwa sababu ya jasho ambalo lilikuwa likimtoka, amani yote ilikuwa imemtoka.
Aliendesha kwa makini sana huku akitii kila kitu ambacho alikuwa akiambiwa. Gari likasimama nje ya nyumba moja ambayo ilikuwa katika ujenzi wa kuuzungushia ukuta. Dereva akasimamisha gari na kumwangalia Dominick kwa wasiwasi.
“Tu..mekw..ish..afik..a” Dereva alimwambia Dominick huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Liingize gari katika eneo la nyumba yako” Dominick alimwambia dereva yule ambaye akatii amri.
“Hautakiwi kuonyesha wasiwasi wowote. Japokuwa haunifahamu, jifanye mimi ni rafiki yako wa muda mrefu. Ukifanya vingine, nitakuua wewe pamoja na familia yako. Umenielewa?” Dominick alimalizia kwa kwa kuuliza swali.
“Nimekuelewa mkuu”
Dominick akaiweka bunduki yake kiunoni na kuifunika na fulana yake. Hakutaka mtu yeyote ajue kama alikuwa na bunduki. Dereva akatulia kama alivyoamrishwa, akaufungua mlango na kuingia ndani. Akaanza kumuita mkewe, ambaye baada ya muda, akafika sebuleni hapo.
“Mbona umerudi tena?” Mkewe, Bi Amina alimuuliza huku akionekana kushangaa.
“Nimekutana na rafiki yangu, nimeamua kuja nae hapa” Dereva, Omari alimwambia mkewe.
“Sawa. Karibu mgeni”
“Asante”
Omari akakaa kochini na kuanza kuangaliana na Dominick ambaye muda wote uso wake ulikuwa umetawaliwa na tabasamu pana. Bi Amina akaondoka mahali hapo na kwenda jikoni kuandaa chai. Omari hakujua ni kitu gani ambacho kilitakiwa kuendelea, akazidi kumuangalia Dominick katika hali ya kutaka kuuliza swali.
“Tumekwishafika. Kuna kingine?”
“Ndio. Nataka uende kwa bosi wako. Ninawataka watoto wake wawili pamoja na mkewe uje nao hapa. Hakikisha unakuja nao” Dominick alimwambia Mrisho.
“Sasa nitawezaje kuja nao wote?. Kwa watoto sawa. Ila kwa mkewe sijui kama itawezekana” Omari alimwambia Dominick.
“Itawezekana tu. Wewe nenda, kama haitowezekana, basi acha nimuue mkeo” Dominick alimwambia Omari ambaye akaonekana kushtuka.
“Umuue mke wangu?”
“Ndio. Sasa si utakuwa umeshindwa kazi. Ni lazima nimuue kama hautoweza kuniletea wote ambao ninataka kuwaona mahali hapa” Dominick alimwambia Omari huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikiongea.
Omari hakuwa na jinsi, akamuita mkewe na kumuaga. Akaondoka mahali hapo huku akimuacha Dominick nyumbani hapo. Njia nzima Omari alionekana kuwa na wasiwasi, hakuamini kama Dominick angeweza kumuacha mkewe kama tu asingekifanya kile ambacho alitaka kifanyike. Akajiapiza ni lazima awachukue wote ambao walihitajika. Hakuonekana kuwa tayari kumpoteza mkewe.
Dominick hakutaka kuendelea kubaki mahali pale, alichokifanya ni kumuaga mkewe Omari kwa kumwambia kuwa alikuwa akielelekea sehemu fulani na baada ya muda angerudi. Dominick akatoka nje ambako akachukua gari lake na kuondoka mpaka hotelini, akaliacha na kurudi nyumbani kwa Omari kwa miguu huku kidumu cha petroli cha lita tano kikiwa mkononi mwake.
Dominick akafika na kukaribishwa tena na Amina, akatulia kochini na kuanza kunywa chai. Hakuonekana kuwa na wasiwasi wowote ule hali ambayo Amina hakumtilia shaka hata kidogo. Kila wakati Dominick alikuwa akiiangalia saa yake, muda ulizidi kwenda lakini wala Omari hakurudi.
“Au atakuwa amekwenda polisi? Hapana hawezi kufanya hivyo” Dominick alijiuliza na kujijibu.
Wala haukuchukua muda mrefu sana, muungurumo wa gari ukaanza kusikikanje ya nyumba. Dominick akachungulia na alipoona ni gari la waziri Boniface, akatoka nje. Kwa haraka sana akaanza kulifuata, alipolifikia, Omari akateremka na Dominick kuingia ndani.
“Kazi nzuri sana. Mkeo yuko salama” Dominick alimwambia Omari huku akiingia garini na Omari akiteremka.
Kitu cha kwanza Dominick akayapeleka macho yake katika kiti cha nyuma, watoto wawili wa kike waliokuwa na sare za shule walikuwa nyuma pamoja na mama yao walikuwa wametulia. Mke wa waziri Boniface, Bi Upendo akaonekana kushtuka, tayari wasiwasi ukaanza kumuingia.
Hakujua sababu iliyompelekea Omari kuteremka na kumwachia gari mtu mwingie ambaye wala hakuwa akimfahamu. Akataka kuufungua mlango na kutoka nje, tayari milango yote ilikuwa imepigwa roki. Akateremsha kioo na kumwangalia Omari kwa uso uliojaa hasira.
“Ndio unafanya nini Omari?. Huyu ni nani na kwa nini unamuachia gari? Haujui kama hili gari ni la mtu mkubwa?” Bi Upendo aliuliza maswali manne mfululizo.
“Nimefanya hivi kwa ajili ya mke wangu mama. Kama nisingefanya hivi basi ni lazima ningempoteza mke wangu” Omari alimwambia Bi Upendo ambaye alionekana kushangaa.
Hata kabla hajauliza swali jingine, gari likaondolewa mahali hapo kwa mwendo wa kasi. Dominick hakutaka kuulizwa swali lolote lile, akaanza kuendesha gari kwa mwendo wa kasi. Lengo lake lilikuwa ni kufika katika ufukwe wa Coco kwani aliamini kwa asubuhi hiyo ya saa moja, kusingekuwa na watu wengi.
Bi Upendo alikuwa akiuliza maswali mengi huku akionekana kuwa kama mtu aliyechanganyikiwa lakini Dominick hakujibu lolote, alikuwa kimya huku akionekana kuwa na hasira. Picha ya familia yake ikaanza kuonekana kichwani mwake, nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea ikaanza kujirudia kichwani kama mkanda wa filamu.
Taswira ya miili ya familia yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto ikaanza kuonekana kichwani mwake. Machozi yakaanza kumtoka, hasira ikazidi kumpanda, akaanza kupaona ufukweni mbali, alitamani gari liwe na mabawa, lipae na kutua ufukweni.
“Nyamazaaaaa….!” Dominick alimwambia Bi Upendo kwa sauti ya kelele iliyojaa hasira.
“Ni lazima niwaue. NI LAZIMA” Dominick alijisemea huku akiyauma meno yake kwa hasira
                                                               ********
Kundi la BoT likaonekana kujipongeza. Kila siku ilionekana kuwa ya furaha kwao. Walipongezana kwa kazi nzito ambayo walikuwa wameifanya. Taarifa za uongo walizoletewa juu ya kifo cha Dominick na kifo cha Saida zilionekana kuwafurahisha kupita kiasi.
Waliambiwa na vijana wale kuwa walimfuata Saida nyumbani kwake ambako wakakutana na Dominick ambaye wakaamua kuondoka nae mpaka porini, na huko ndipo walipoamua kuwaua wote wawili. Taarifa ile ya uongo ilionekana kuwa ya faraja kwao, hakukuwa na mtu ambaye alionekana kubisha na wakati mpaka picha za kutengenezwa walikuwa wamekabidhiwa.
Kila siku kwao ilionekana kuwa kama sikukuu. Walikunywa na kufurahia pamoja. Kila siku muda wa Bunge ulipokuwa ukimalizika, walikuwa wakikutana katika mghahawa ulioitwa Matimya ambao ulikuwa katikakati ya mkoa wa Dodoma na kufurahia pamoja.
Walionekana kukamilisha kazi ndefu ambayo ilikuwa ikiwasumbua vichwa vyao, walijiona kuwa na amani sasa. Glasi zao zilikuwa hewani, wakazigonganisha na kisha kuanza kunywa huku wakiongea maneno mbalimbali yaliyojaa dhihaka juu ya Dominick.
“Kiko wapi sasa? Alijifanya anajua sana” Mzee Boniface aliwaambia wenzake.
“Tusimlaumu jamani. Hakujua kama analeta mzaha kwa watu walio na mikono mirefu”  Waziri Ombeni aliwaambia na wote kuanza kucheka.
“Cheeeeerrs! Kwa ajili ya marehemu Dominick na Saida” Waziri Tumaini alisema huku akinyanyua glasi juu.
“Cheeeeerss….! Bwana Ombeni na Boniface waliitikia.
                                                               ********
Dominick akaingia katika eneo la ufukwe na kulipaki gari lile. Kutokana na wakati kuwa asubuhi sana, hakukuwa na watu ufukweni. Kwa haraka haraka huku akionekana kuwa na hasira akateremka huku mkoni akiwa na kidumu cha mafuta ya petroli.
Bi Upendo akabaki akipiga kelele za kuomba msaada, hali tayari ikaonekana kuwa ya hatari. Alipiga kelele sana lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alizisikia kelele zile. Dominick akaanza kulimwagia petroli gari lile. Kila kitu ambacho alikifanywa kwa wakati huo alikifanya kwa haraka haraka.
Alipomaliza kulimwagia petroli kwa nje, akafungua mlango na kuanza kuwamwagia petroli Bi Upendo pamoja na watoto wake. Wote walikuwa wakilia ndani ya gari lakini wala Dominick hakuonekana kujali. Machozi yalikuwa yakimtoka kwa hasira.
Taswira ya nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea ikaanza kumjia kichwani, hasira zaidi zikampanda kiasi cha kujuta kwa kuja na lita tano, aliziona ndogo sana. Alipomaliza, akachukua kiberiti na kuliwasha moto gari lile. Kelele za Bi Upendo na watoto wake zikazidi kusikika zaidi.
Kila Bi Upendo alipojaribu kuufungua mlango kwa ajili ya kutoka nje, milango ilikuwa imepigwa roki. Harufu za nguo zlizokuwa zikiungua kwa moto ikaanza kusikika kunuka na hatimae harufu ya miili iliyokuwa ikiteketea ikaanza kunuka pia.
Kutokana na upepo kuwa mkubwa ufukweni pale, moto ule ukaonekana kuchochewa. Mara milio ya vitu vitatu vilivyoonekana kupasuka vikasikika kutoka garini, hivyo vilikuwa vichwa ambavyo vilikuwa vimepasuka kutokana na kuteketezwa sana na moto.
Kuteketea kwa gari lile kukawafanya watu waliokuwa mbali kabisa kuanza kuuona moto mkubwa, wakaanza kukimbilia kule ambako moto ule ulipokuwa. Dominick hakuwepo mahali pale, tayari alikuwa amekishaondoka huku moyo wake ukionekana kuridhika kiasi.
Kila mtu aliyefika mahali pale alibaki akishangaa, watu wote walibaki wakiwa wameduwaa tu, hawakujua wafanye nini na wakati gari lilikuwa likizidi kuteketea kwa moto. Baada ya muda watu wakaonekana kurudiwa na akili zao, wakaanza kuchukua maji baharini na kuanza kuuzima moto ule. Moto ukazimika, wakasubiri bodi lipoe ili kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote garini.
Mlango wa gari ukavutwa, kijana mmoja akachungulia garini, kile ambacho alikiona alishindwa kuvumilia, akatoka huku akionekana kuwa na wasiwasi mkubwa. Kila alipokuwa akiulizwa aliona nini, hakuongea kitu chochote kile, alikwenda pembeni na kuanza kutapika.
“Kuna nini? Umeona nini?” Kijana mwingine alimuuliza.
“Nendeni mkaangalie wenyewe. Inatisha”
“Inatisha? Inatisha nini?”
“Nyie kaangalieni tu”
Vijana wengine wakaelekea katika gari lile na kuchungulia ndani. Miili mitatu ilikuwa ikionekana vizuri huku ikiwa imeteketea kwa moto na huku ikitoa moshi. Simu zikaanza kupigwa katika kituo cha polisi cha Oysterbay ili kuwaomba mapolisi kufika mahali hapo haraka iwezekanavyo.

A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 06

$
0
0

 MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

“Yaani bado walikuwa na kisasi na maisha yangu mpaka wakaiangamiza familia yangu?” Dominick aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Edmund...Edmund...yaani watu hawa ndio waliiangaliza familia yangu? Ni lazima niwaue, ni lazima niangamize familia zao pia kama walivyoiangamiza yangu. Tena nitaziangamiza kwa kuzichoma moto na kisha kuwaua wao wenyewe. Ni lazima Edmund. NI LAZIMA……!!!” Dominick alimwambia Edmind huku akilia kama mtoto. Mwili wake ukabaki ukitetemeka kwa hasira, kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo alizidi kutetemeka kwa hasira.
“NI LAZIMA NIWAUE….” Dominick alisema kwa hasira huku akiondoka mahali hapo kwa mwendo wa kasi kuelekea kule walipolipaki gari.
SONGA NAYO...
Dominick hakuonekana kuwa na raha kabisa, huzuni ambayo alikuwa nayo katika kipindi cha nyuma ilikuwa imeongezeka zaidi. Kitendo cha kuwafahamu wabaya wake kilionekana kumuumiza kupita kawaida. Hakuamini kama wale mawaziri ndio ambao wangeweza kumfanyia kitu kama kile.
Kila siku mawaziri wale walikuwa wakijifanya kuwa karibu na waandishi wa habari lakini kumbe walikuwa ni watu hatari ambao wala hawakutakiwa kusogelewa. Kila siku ambazo Dominick alikuwa akiwaona wakiongea katika vipindi mbalimbali vya televisheni, alibaki akiumia tu.
Akaamua kujipanga, alitaka kutekeleza kila kitu pasipo wasiwasi wowote wala kujulikana na mtu yeyote. Hakuona sababu ya watu wale kuendelea kuishi na wakati walikuwa wamemuumiza kwa kuiteketeza familia yake kwa kuichoma moto.
Alipanga kuwaua wote, tena si wao tu, angeanza na familia zao na kisha kuwaua wao wenyewe. Alitaka sana nao kwanza waanze kuumia kabla ya kuwamaliza. Alitamani wayaonje maumivu ambayo alikuwa ameyasikia hata kabla hawajaonja mauti.
“Nitaanza na nani sasa” Dominick alibaki akijiuliza.
“Walijiita BoT, nami nitaanza na majina yao kama jinsi yalivyo, ni lazima niwaue” Dominick alisema kwa hasira huku akijifunika shuka na kulala.
Siku iliyofuata Dominick akaanza kufanya maandalizi ya kazi yake ambayo alikuwa ameipanga kuifanya, alitamani kuifanya haraka sana hata kabla hakijaharibika kitu chochote kile. Hakuonekana kuwa na pupa, alitaka kuifanya taratibu lakini kwa umakini mkubwa sana.
Kitu cha kwanza alichokifanya ni kuchukua kitabu kikubwa cha simu za mezani na kuanza kuziangalia namba za simu za ofisini mwao, alipozipata, akaziandika sehemu. Dominick hakuridhika, akaangalia na namba za simu za mezani za nyumbani kwao, nazo akaziandika pembeni pia.
“Nitahitaji unisaidie kitu kimoja” Dominick alimwambia Edmund.
“Kitu gani tena? Kukusaidia kazi yako?”
“Hapana. Kazi hii wala haihitaji msaada wa mtu yeyote, nataka kuifanya mimi mwenyewe”
“Sasa unataka nikusaidie nini?”
“Nahitaji mafuta ya petroli ya lita ishirini”
“Hilo si tatizo. Kuna jingine?”
“Labda na kiberiti pamoja na gari lako. Ile bunduki yako si unayo?” Dominick alimuuliza.
“Ninayo. Nayo pia unaitaka?”
“Ndo maana nikaiulizia”
Edmund akainuka na kwenda chumbani kwake ambako akamletea bunduki pamoja na kiberiti. Akachukua pochi yake na kutoa kiasi kilichotosha cha kununua petroli ya lita ishirini na kisha kuondoka kuelekea katika kituo cha kuuzia petroli.
Wala hakuchukua muda mrefu, akarudi, akamgawia Dominick mafuta yale na kisha kumkabidhi ufunguo wa gari lake. Dominick hakutaka kupoteza muda kubaki mahali hapo, moja kwa moja akatoka nje mpaka katika sehemu ya maegesho ya magari na kuchukua gari la Edmund.
“Nitachukua miezi mingi mpaka kurudi hapa. Nitahakikisha kazi inaanza kwa mmoja baada ya mwingine” Dominick alimwambia Edmund.
“Usijali. Kazi njema” Edmund alimwambia Dominick.
Dominick akaondoka na kuelekea katika hoteli ya La Vista Inn na kuchukua chumba. Hakutaka kuendelea kuishi nyumbani kwa Edmund katika wakati ambao atakuwa akiendelea na kazi yake ya kuuridhisha moyo wake. Huko hotelini ndipo sehemu ambayo alipanga kila kitu, namna ya kuanza kazi mpaka kuimaliza.
“Nitaanza na huyu waziri wa wa Utalii na Mali asili, Boniface Akwaiziwe. Nitaanza kuiangamiza familia yake kwanza, ili achanganyikiwe na aje Dar es Salaam kutokea Bungeni” Dominick alijisemea.
Tayari muda ulikuwa umekwenda sana. Saa ya ukutani wala haikuonekana kwenda tofauti na saa yake ya mkononi, zote zilikuwa zikimuonyesha kuwa tayari saa moja na nusu usiku. Akatoka chumbani na moja kwa moja kuanza kushusha ngazi mpaka chini ambako akaingia katika mghahawa wa chakula hapo hotelini na kuagizia chakula.
Kofia kubwa ya Malboro pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa wala haikumfanya kujulikana. Alionekana kuwa mgeni kwa kila mtu ambaye alikuwa akimwangalia. Alipomaliza kula chakula pale mghahawani, akarudi chumbani kwake kuendelea na kazi ya kupanga mbinu mbalimbali za mauaji.
“Nitaanza rasmi kesho. Ila dereva ndiye mtu wa muhimu sana kupatikana” Dominick alijisemea.
Siku iliyofuata ndio ilikuwa siku ambayo alitaka kuanza kazi. Alichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika nyumba ya waziri Boniface ambako akakaa mbali kidogo na geti lile huku macho yake yakiangalia getini. Wala hazikupita dakika nyingi, akamuona mtu mmoja akipiga hodi katika geti lile.
Dominick akayapeleka macho yake katika saa yake, ilikuwa ikimuonyeshea kwamba tayari ilikuwa saa kumi na mbili na robo asubuhi. Hakuwa na shaka kwamba yule aliyekuwa akigonga hodi alikuwa dereva, mtu ambaye alikuwa akimtaka kwa udi na uvumba.
Dominick akaliwahsa gari lake na kuanza kusogea kule geti lilipokuwa, alipomfikia, akateremka na kuanza kumsogelea huku kofia na miwani vikiwa vimemkaa vizuri.
Dereva yule bado alikuwa akisubiri geti lifunguliwe ili aingie ndani, achukue gari na kumpeleka mtoto wa Waziri shuleni. Mara akashtukia kitu kikiwa kimemgusa kisogoni, alipogeuka, akakutana na mdomo wa bunduki.
Dereva akaonekana kushtuka kupita kiasi, mdomo wa bunduki ulimfanya kumuogopesha. Akayapeleka macho yake usoni mwa mtu aliyemnyooshea bunduki, hakumfahamu kabisa kutokana na kofia pamoja na miwani ambayo alikuwa ameivaa.
“Ingia ndani ya gari langu haraka” Dominick alimwambia dereva ambaye bila kubisha, na kwa nidhamu zote, akaingia huku akitetemeka.
“Shikilia usukani. Nataka uendeshe gari wewe mwenyewe” Dominick alimwambia dereva ambaye kwa haraka sana, akashikilia usukani.
“Endesha moja kwa moja kuelekea nyumbani kwako” Dominick alimwambia dereva yule.
“Kwa nini kwangu lakini? Nimekufanya nini mkuu?” Dereva aliuliza huku akitetemeka.
“Nisikilize. Sihitaji maswali, fanya kile ambacho ninakuamuru kukifanya. La sivyo, nitatawanyisha ubongo wako sasa hivi” Dominick alimwambia dereva maneno ambayo yalizidi kumtetemesha zaidi
Hakuwa na jinsi zaidi ya kuwasha gari na safari ya kuelekea nyumbani kwake kuanza. Njia nzima alikuwa akitetemeka kwa hofu, kila alipokuwa akiuangalia mdomo wa bunduki, alizidi kutetemeka. Tayari nguo zake zilikuwa zimekwishaloana kwa sababu ya jasho ambalo lilikuwa likimtoka, amani yote ilikuwa imemtoka.
Aliendesha kwa makini sana huku akitii kila kitu ambacho alikuwa akiambiwa. Gari likasimama nje ya nyumba moja ambayo ilikuwa katika ujenzi wa kuuzungushia ukuta. Dereva akasimamisha gari na kumwangalia Dominick kwa wasiwasi.
“Tu..mekw..ish..afik..a” Dereva alimwambia Dominick huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Liingize gari katika eneo la nyumba yako” Dominick alimwambia dereva yule ambaye akatii amri.
“Hautakiwi kuonyesha wasiwasi wowote. Japokuwa haunifahamu, jifanye mimi ni rafiki yako wa muda mrefu. Ukifanya vingine, nitakuua wewe pamoja na familia yako. Umenielewa?” Dominick alimalizia kwa kwa kuuliza swali.
“Nimekuelewa mkuu”
Dominick akaiweka bunduki yake kiunoni na kuifunika na fulana yake. Hakutaka mtu yeyote ajue kama alikuwa na bunduki. Dereva akatulia kama alivyoamrishwa, akaufungua mlango na kuingia ndani. Akaanza kumuita mkewe, ambaye baada ya muda, akafika sebuleni hapo.
“Mbona umerudi tena?” Mkewe, Bi Amina alimuuliza huku akionekana kushangaa.
“Nimekutana na rafiki yangu, nimeamua kuja nae hapa” Dereva, Omari alimwambia mkewe.
“Sawa. Karibu mgeni”
“Asante”
Omari akakaa kochini na kuanza kuangaliana na Dominick ambaye muda wote uso wake ulikuwa umetawaliwa na tabasamu pana. Bi Amina akaondoka mahali hapo na kwenda jikoni kuandaa chai. Omari hakujua ni kitu gani ambacho kilitakiwa kuendelea, akazidi kumuangalia Dominick katika hali ya kutaka kuuliza swali.
“Tumekwishafika. Kuna kingine?”
“Ndio. Nataka uende kwa bosi wako. Ninawataka watoto wake wawili pamoja na mkewe uje nao hapa. Hakikisha unakuja nao” Dominick alimwambia Mrisho.
“Sasa nitawezaje kuja nao wote?. Kwa watoto sawa. Ila kwa mkewe sijui kama itawezekana” Omari alimwambia Dominick.
“Itawezekana tu. Wewe nenda, kama haitowezekana, basi acha nimuue mkeo” Dominick alimwambia Omari ambaye akaonekana kushtuka.
“Umuue mke wangu?”
“Ndio. Sasa si utakuwa umeshindwa kazi. Ni lazima nimuue kama hautoweza kuniletea wote ambao ninataka kuwaona mahali hapa” Dominick alimwambia Omari huku akionekana kumaanisha kile alichokuwa akikiongea.
Omari hakuwa na jinsi, akamuita mkewe na kumuaga. Akaondoka mahali hapo huku akimuacha Dominick nyumbani hapo. Njia nzima Omari alionekana kuwa na wasiwasi, hakuamini kama Dominick angeweza kumuacha mkewe kama tu asingekifanya kile ambacho alitaka kifanyike. Akajiapiza ni lazima awachukue wote ambao walihitajika. Hakuonekana kuwa tayari kumpoteza mkewe.
Dominick hakutaka kuendelea kubaki mahali pale, alichokifanya ni kumuaga mkewe Omari kwa kumwambia kuwa alikuwa akielelekea sehemu fulani na baada ya muda angerudi. Dominick akatoka nje ambako akachukua gari lake na kuondoka mpaka hotelini, akaliacha na kurudi nyumbani kwa Omari kwa miguu huku kidumu cha petroli cha lita tano kikiwa mkononi mwake.
Dominick akafika na kukaribishwa tena na Amina, akatulia kochini na kuanza kunywa chai. Hakuonekana kuwa na wasiwasi wowote ule hali ambayo Amina hakumtilia shaka hata kidogo. Kila wakati Dominick alikuwa akiiangalia saa yake, muda ulizidi kwenda lakini wala Omari hakurudi.
“Au atakuwa amekwenda polisi? Hapana hawezi kufanya hivyo” Dominick alijiuliza na kujijibu.
Wala haukuchukua muda mrefu sana, muungurumo wa gari ukaanza kusikikanje ya nyumba. Dominick akachungulia na alipoona ni gari la waziri Boniface, akatoka nje. Kwa haraka sana akaanza kulifuata, alipolifikia, Omari akateremka na Dominick kuingia ndani.
“Kazi nzuri sana. Mkeo yuko salama” Dominick alimwambia Omari huku akiingia garini na Omari akiteremka.
Kitu cha kwanza Dominick akayapeleka macho yake katika kiti cha nyuma, watoto wawili wa kike waliokuwa na sare za shule walikuwa nyuma pamoja na mama yao walikuwa wametulia. Mke wa waziri Boniface, Bi Upendo akaonekana kushtuka, tayari wasiwasi ukaanza kumuingia.
Hakujua sababu iliyompelekea Omari kuteremka na kumwachia gari mtu mwingie ambaye wala hakuwa akimfahamu. Akataka kuufungua mlango na kutoka nje, tayari milango yote ilikuwa imepigwa roki. Akateremsha kioo na kumwangalia Omari kwa uso uliojaa hasira.
“Ndio unafanya nini Omari?. Huyu ni nani na kwa nini unamuachia gari? Haujui kama hili gari ni la mtu mkubwa?” Bi Upendo aliuliza maswali manne mfululizo.
“Nimefanya hivi kwa ajili ya mke wangu mama. Kama nisingefanya hivi basi ni lazima ningempoteza mke wangu” Omari alimwambia Bi Upendo ambaye alionekana kushangaa.
Hata kabla hajauliza swali jingine, gari likaondolewa mahali hapo kwa mwendo wa kasi. Dominick hakutaka kuulizwa swali lolote lile, akaanza kuendesha gari kwa mwendo wa kasi. Lengo lake lilikuwa ni kufika katika ufukwe wa Coco kwani aliamini kwa asubuhi hiyo ya saa moja, kusingekuwa na watu wengi.
Bi Upendo alikuwa akiuliza maswali mengi huku akionekana kuwa kama mtu aliyechanganyikiwa lakini Dominick hakujibu lolote, alikuwa kimya huku akionekana kuwa na hasira. Picha ya familia yake ikaanza kuonekana kichwani mwake, nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea ikaanza kujirudia kichwani kama mkanda wa filamu.
Taswira ya miili ya familia yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto ikaanza kuonekana kichwani mwake. Machozi yakaanza kumtoka, hasira ikazidi kumpanda, akaanza kupaona ufukweni mbali, alitamani gari liwe na mabawa, lipae na kutua ufukweni.
“Nyamazaaaaa….!” Dominick alimwambia Bi Upendo kwa sauti ya kelele iliyojaa hasira.
“Ni lazima niwaue. NI LAZIMA” Dominick alijisemea huku akiyauma meno yake kwa hasira
                                                               ********
Kundi la BoT likaonekana kujipongeza. Kila siku ilionekana kuwa ya furaha kwao. Walipongezana kwa kazi nzito ambayo walikuwa wameifanya. Taarifa za uongo walizoletewa juu ya kifo cha Dominick na kifo cha Saida zilionekana kuwafurahisha kupita kiasi.
Waliambiwa na vijana wale kuwa walimfuata Saida nyumbani kwake ambako wakakutana na Dominick ambaye wakaamua kuondoka nae mpaka porini, na huko ndipo walipoamua kuwaua wote wawili. Taarifa ile ya uongo ilionekana kuwa ya faraja kwao, hakukuwa na mtu ambaye alionekana kubisha na wakati mpaka picha za kutengenezwa walikuwa wamekabidhiwa.
Kila siku kwao ilionekana kuwa kama sikukuu. Walikunywa na kufurahia pamoja. Kila siku muda wa Bunge ulipokuwa ukimalizika, walikuwa wakikutana katika mghahawa ulioitwa Matimya ambao ulikuwa katikakati ya mkoa wa Dodoma na kufurahia pamoja.
Walionekana kukamilisha kazi ndefu ambayo ilikuwa ikiwasumbua vichwa vyao, walijiona kuwa na amani sasa. Glasi zao zilikuwa hewani, wakazigonganisha na kisha kuanza kunywa huku wakiongea maneno mbalimbali yaliyojaa dhihaka juu ya Dominick.
“Kiko wapi sasa? Alijifanya anajua sana” Mzee Boniface aliwaambia wenzake.
“Tusimlaumu jamani. Hakujua kama analeta mzaha kwa watu walio na mikono mirefu”  Waziri Ombeni aliwaambia na wote kuanza kucheka.
“Cheeeeerrs! Kwa ajili ya marehemu Dominick na Saida” Waziri Tumaini alisema huku akinyanyua glasi juu.
“Cheeeeerss….! Bwana Ombeni na Boniface waliitikia.
                                                               ********
Dominick akaingia katika eneo la ufukwe na kulipaki gari lile. Kutokana na wakati kuwa asubuhi sana, hakukuwa na watu ufukweni. Kwa haraka haraka huku akionekana kuwa na hasira akateremka huku mkoni akiwa na kidumu cha mafuta ya petroli.
Bi Upendo akabaki akipiga kelele za kuomba msaada, hali tayari ikaonekana kuwa ya hatari. Alipiga kelele sana lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alizisikia kelele zile. Dominick akaanza kulimwagia petroli gari lile. Kila kitu ambacho alikifanywa kwa wakati huo alikifanya kwa haraka haraka.
Alipomaliza kulimwagia petroli kwa nje, akafungua mlango na kuanza kuwamwagia petroli Bi Upendo pamoja na watoto wake. Wote walikuwa wakilia ndani ya gari lakini wala Dominick hakuonekana kujali. Machozi yalikuwa yakimtoka kwa hasira.
Taswira ya nyumba ambayo ilikuwa ikiteketea ikaanza kumjia kichwani, hasira zaidi zikampanda kiasi cha kujuta kwa kuja na lita tano, aliziona ndogo sana. Alipomaliza, akachukua kiberiti na kuliwasha moto gari lile. Kelele za Bi Upendo na watoto wake zikazidi kusikika zaidi.
Kila Bi Upendo alipojaribu kuufungua mlango kwa ajili ya kutoka nje, milango ilikuwa imepigwa roki. Harufu za nguo zlizokuwa zikiungua kwa moto ikaanza kusikika kunuka na hatimae harufu ya miili iliyokuwa ikiteketea ikaanza kunuka pia.
Kutokana na upepo kuwa mkubwa ufukweni pale, moto ule ukaonekana kuchochewa. Mara milio ya vitu vitatu vilivyoonekana kupasuka vikasikika kutoka garini, hivyo vilikuwa vichwa ambavyo vilikuwa vimepasuka kutokana na kuteketezwa sana na moto.
Kuteketea kwa gari lile kukawafanya watu waliokuwa mbali kabisa kuanza kuuona moto mkubwa, wakaanza kukimbilia kule ambako moto ule ulipokuwa. Dominick hakuwepo mahali pale, tayari alikuwa amekishaondoka huku moyo wake ukionekana kuridhika kiasi.
Kila mtu aliyefika mahali pale alibaki akishangaa, watu wote walibaki wakiwa wameduwaa tu, hawakujua wafanye nini na wakati gari lilikuwa likizidi kuteketea kwa moto. Baada ya muda watu wakaonekana kurudiwa na akili zao, wakaanza kuchukua maji baharini na kuanza kuuzima moto ule. Moto ukazimika, wakasubiri bodi lipoe ili kuangalia kama kulikuwa na mtu yeyote garini.
Mlango wa gari ukavutwa, kijana mmoja akachungulia garini, kile ambacho alikiona alishindwa kuvumilia, akatoka huku akionekana kuwa na wasiwasi mkubwa. Kila alipokuwa akiulizwa aliona nini, hakuongea kitu chochote kile, alikwenda pembeni na kuanza kutapika.
“Kuna nini? Umeona nini?” Kijana mwingine alimuuliza.
“Nendeni mkaangalie wenyewe. Inatisha”
“Inatisha? Inatisha nini?”
“Nyie kaangalieni tu”
Vijana wengine wakaelekea katika gari lile na kuchungulia ndani. Miili mitatu ilikuwa ikionekana vizuri huku ikiwa imeteketea kwa moto na huku ikitoa moshi. Simu zikaanza kupigwa katika kituo cha polisi cha Oysterbay ili kuwaomba mapolisi kufika mahali hapo haraka iwezekanavyo.
ITAENDELEASIKU YAKESHO

USIKU WA KIGODORO - 05

$
0
0


ILIPOISHIA: Wakati mazungumzo yakiendelea, mume wa Lina alifunga breki nje ya nyumba ya Eg na kupiga honi ana shida na mke wake huyo…
“Pii pii piii!”     
JIRUSHE MWENYEWE SASA…
Eg ndiye aliyechungulia nje baada uya kusikia honi ya gari, akashtuka sana na kusema…
“Ha! Lina, shemeji Semi…”
“Kweli?”
“Mungu tena, amesimamisha gari hapo nje.”
“Mungu wangu, sasa?”
“Hata sijui! Kwani amefuata nini huku?  Au ametonywa ishu nzima?”
“Hapana, atakuwa ana shida na mimi. Lakini sasa nimeshavaa itakuaje? Si ataniona nimekuwa rasmi sana kuliko huyo niliyemsingizia?”
“Na kweli.”
Semi alipiga tena honi, Eg akatoka. Lina alivua gauni la kitchen party na kuvaa alilokwenda nalo kisha naye akatoka. Ndugu na marafiki wa Eg nao wakafuata hadi kwenye gari…
“Shem mambo?” alisalimia Eg…
“Poa, mzima wewe?”
“Mimi mzima. Karibu sana.”
“Asante sana.”
“Huyu ndiye shemeji kwa Lina?” ndugu mmoja wa Eg aliuliza akiamini Semi ndiye bwana harusi mtarajiwa…
“Eee, ndiyo huyu.”
“Oo! Karibu sana shemeji…sisi leo mambo yatakwenda vizuri kabisa ukumbini…bibiye atapendeza kupita kawaida,” aliropoka yule ndugu bila kujua kwamba anakaribia kulipua bomu.
Kilichosaidia ni kwamba, maneno yake yalifunga ufahamu wa Semi kwani kule kusema sisi leo mambo yatakwenda vizuri, Semi alijua ni sherehe ambayo mkewe alishamwambia ipo.
Kule kusema bibiye atapendeza kupita kawaida hakukumfanya Semi ahisi kitu kwani ni kweli mke wake alitoka nyumbani na gauni zuri la kitenge ambalo alisema atalivaa kwenye kitchen party ya rafiki yake, ubaya uko wapi sasa!
“Sawa jamani, nawatakia sherehe njema, nimekuja kumpa maagizo huyu, mimi nakwenda Morogoro nikichelewa nitarudi kesho.”
“Sawa mume wangu,” alisema Lina. Mwanamke mmoja akadakia…
“We, bado hajawa mume wako, atakuwa mumeo ukishafunga naye ndoa.”
Lina na Eg walishtuka sana kwa kauli hiyo, walijua sasa mambo hadharani lakini katika hali isiyotarajiwa, Semi akajibu…
“Tufunge ndoa mara ngapi? Shemeji Eg hujawaambia nini?” akawasha gari na kuondoka huku akicheka.
Mambo yalikuwa mambo, mkorogano ulitawala kila aliyesema, aliyesikia alitafsiri vingine kabisa.
Hata yule mwanamke aliyejibiwa kwamba ‘tufunge ndoa mara ngapi?’
alijua ameambiwa kwa kutaniwa kwani alijua ile kitchen party ya Lina, muoaji mwenyewe ndiye yule. Na Semi naye alijua yule mwanamke ameuliza kwa sababu ya ugeni, hajui kama Lina yupo kwenye ndoa ndiyo maana akamwambia Eg, ‘shemeji Eg hujawaambia nini?’
***
Lina aliendelea kujipamba, magari mawili ya kukodi yakafika kwa ajili ya kupelekwa ukumbini.
Shamrashamra ukumbini zilinoga kama si kuvutia, kwani kila kitu kilikwenda sawasawa. Lina pamoja na kwamba alitegemea michango lakini yeye mwenyewe kwa kupitia kwenye mfuko wa James alichangia fedha kwa kiasi kikubwa na kusababisha bajeti kwenda ilivyopangwa.
Shughuli ilikuwa nzuri, waalikwa walikula la kunywa na wakasaza huku kila mmoja akimpongeza Lina.
Lakini muda mwingi wa sherehe hiyo, Lina alipenda kuinamisha kichwa ili kukwepa macho ya watu akiamini pengine kuna ambaye atakuwa anamjua. Mbali na macho ya watu, awali kabisa Eg alishawatangazia waalikwa kuachana na kupiga picha kwa kutumia kamera za kwenye simu zao. Na wala hakukuwa na mpiga picha aliyekodishwa.
Baada ya shughuli hiyo, Lina alikwenda kulala kwa Eg baada ya kumpigia simu mume wake na akamwambia hatarudi toka Morogoro.
Usiku Lina alianza kuchati na James…
“Baby sherehe ilikuwa nzuri sana, nimemaliza kazi bado kwako ndoa wikiendi ijayo.”
“Niko fiti baby, mipango yote tayari. Tutakwenda fungate wapi baby?” aliuliza James swali lililomuumiza sana Lina kwani alijua kwenda fungate ni kubumbulua mambo kwa mume wake, atamuaga anakwenda wapi!”
“Popote pale my dear,” alijibu Lina.
Kama wangekuwa wanaongea kwa sauti angeshangaa kusikia sauti ya Lina inazungumza kwa unyonge wa hali ya juu.
“Basi niachie mimi, nitachukua hoteli nzuri sana tena kubwa ya hapa mjini. Au unataka twende nje ya mji kama Zenji?”
“Noo! Hata hapa Dar panatosha sana my love.”
Walichati mpaka saa tisa kasoro lakini muda mwingi akili ya Lina ilikuwa haipo sawa. Kuna wakati alitamani hata kufunguka lakini alishindwa kwa sababu walishafika mbali na angesababisha mawazo ya James kuamini kwamba  wanawake ni wabaya sana.
Siku ya ndoa ndiyo ikafika sasa, Lina alikuwa anajiandaa kivyake na James kivyake walikubaliana wakutane kanisani na kuungana kuingia ndani kwa ibada ya ndoa.
 “Uko wapi Lina?”
“Kwa dada, ndiyo tunataka kutoka kwenda saluni my dear.”
“Lina usinitibue, kwa dada saa hizi wakati unajua kanisani tunatakiwa saa nane kamili mchana, sasa uende saluni saa sita hii utamaliza muda gani? Kanisani utakuja saa ngapi na ndoa itafungwa saa ngapi au hutaki tufunge ndoa Lina?”
“Nitamaliza mapema tu.”
Mara Lina akakata simu…
“Khaa! Yaani Lina kanikatia simu mimi? Ana maana gani?” alijiuliza James. Alipopiga tena iliita bila kupokelewa…
“Afadhali isingepatikana ningesema chaji imeisha, sasa hapokei ana maana gani?” James aliendelea kuwaza…
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

LOVE TONE - NINGEWEZA (OFFICIAL VIDEO)

$
0
0

NEW MUSIC VIDEO FROM NORTHWOOD PICTURES, (NITAWEZA - Love Tone- Official Music Video ) MUSIC produced By, - JUMAJA RECORDS- VIDEO Directed by TUMSIFU

KALALE PEMA - MLAPA NG’OSHA (OFFICIAL VIDEO)

$
0
0

 Mojawapo ya picha katika video hiyo.
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva anayekuja kwa kasi, Gabriel Samalu Ng’osha ‘Mlapa Ng’osha' ameachia video yake mpya inayokwenda kwa jina la 'Kalale Pema' aliyoelezea maisha ya mateso anayopata mama mjamzito.


Video hiyo imetengenezwa chini ya prodyuza Melkiadi Oreje 'OJ' wakati audio ikifanywa na Lebo ya Audio Visual ya nchini Kenya chini ya maprodyuza Haptune & Douncher.

MAJONZI, ZLATAN KUIKOSA BARCELONA LIGI YA MABINGWA LEO

$
0
0

PSG watapambana katika mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelona bila ya mshambuliaji wao nyota, Zlatan Ibrahimovic.

Katika mechi hiyo itakayopigwa leo kwenye dimba la Parc des Princes, PSG haitakuwa na Zlatan aliyewahi kuichezea Barcelona.
Uongozi wa matajiri hao wa Ufaransa, umethibitisha kuwa Mswidi huyo ameumia mguu wake, hivyo hataweza kuivaa Barcelona.
Hilo ni pigo kubwa kwa Kocha Laurent Blanc ambaye lazima alimhitaji Zlatan.
Lakini Zlatan pia angefurahi kucheza dhidi ya timu yake hiyo ya zamani aliyowahi kusema wachezaji wake wanaishi kama watoto wa shule.

JWTZ MILIONEA ALIVYOUAWA KWA RISASI

$
0
0

Stori: Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’/GPL
NI taharuki iliyojaa majonzi na simanzi kufuatia Jeshi la Wananchi wa Tanzania ‘JWTZ’ Kikosi cha CMTU jijini Dar kuondokewa na mpiganaji wake, Sajenti Yohana  Lugendo Gweso (40) ambaye alikuwa milionea aliyepigwa risasi sita mwilini na kufariki dunia papo hapo.
 
Mwili wa marehemu Sajenti Yohana Lugendo Gweso (40) wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ‘JWTZ’ Kikosi cha CMTU ukiwa kwenye jeneza.
Tukio hilo la kusikitisha, lilijiri saa 1:45 usiku wa Septemba 22, mwaka huu, Ukonga Babana ndani ya baa maarufu ijulikanayo kwa jina la Super Karatu.
UWAZI HATUA KWA HATUA
Kufuatia tukio hilo, Uwazi kama kawaida yake lilifuatilia kwa kina ili kubaini yaliyofichika nyuma ya pazia kama siyo sirini!
 
Gari kubwa la jeshi lililoandaliwa kwa ajili ya kuuchukua mwili wa marehemu Sajenti Yohana  Lugendo Gweso kwenda Bunda kwa mazishi.
Habari zilizopatikana zilidai kuwa, siku ya tukio, marehemu Gweso alipigiwa simu akiwa njiani kurudi nyumbani kwake akitokea Hospitali ya Dar Group iliyoko Tazara jijini Dar.
Ikadaiwa kuwa, baada ya kupata simu hiyo alifika kwanza nyumbani kwake Gongo la Mboto kambini.
“Alipofika alikula chakula cha mchana kisha alipumzika. Ilipofika saa 11 jioni aliondoka kwenda kwenye shughuli zake za biashara. “Alipokuwa huko inadaiwa alipigiwa simu na mtu huyo wa mwanzo na kupanga sehemu ya kukutania ambapo ilikuwa  ni hapo baa,” alisema ndugu mmoja akiomba kusitiriwa jina lake.
 
Wanajeshi wa JWTZ wakiupandisha mwili wa Sajenti Yohana Lugendo Gweso kwenye gari.
AONDOKA NA NDUGU
Mpiganaji huyo inadaiwa wakati anatoka katika biashara zake alikuwa na mtoto wa dada yake aliyetajwa kwa jina moja la Frank ambaye alikuwa akisimamia hesebu zote za biashara. Siku hiyo walikuwa wamekusanya kiasi cha shilingi milioni 42.
Ikadaiwa kuwa, walipofika Banana kabla ya kuingia Baa ya Super Karatu, marehemu ambaye alikuwa akiendesha gari lake aina ya Toyota Prado lenye namba za usajili T 855 BWK, alimshusha Frank na kumtaka atangulie  nyumbani kwani alihitaji kwenda Super Karatu kukutana na mwanamke huyo ambaye baadhi ya watu wanadai ni mweupe, mnene aliyepanda hewani (mrefu).
 
Mjane (mwenye kilemba cheupe) wa marehemu Sajenti Yohana  Lugendo Gweso akisaidiwa na ndugu wa karibu kuingia kwenye gari lililoandaliwa kwa ajili ya safari.
AFIKA ENEO LA MAUAJI YAKE
Habari zaidi zinasema kuwa, marehemu aliwasili kwenye baa hiyo saa 1 usiku na kutafuta  maegesho. Alishuka na kuanza kutembea, lakini ghafla kwa  nyuma aliitwa na watu wawili ambao walimuita; “Gweso tuko hapa.”
Wakati anageuka kuwafuata watu hao, watu wengine walianza kuvunja gari lake vioo hivyo alirudi mbio ili kujua nini kinaendelea.
“Kumbe wau hao walikuwa kundi moja na mashambulizi ya risasi yalianzia hapo.
“Marehemu alimiminiwa risasi sita mwilini, alipigwa kichwani, nyingine kifuani na walimchukulia fedha zote milioni 42 na bastola yake kisha wakatokomea,” aliendelea kusema ndugu huyo.
 
Waombolezaji wakiingia kwenye gari kuelekea kwenye mazishi, Bunda.
MWILI WAKUTWA CHINI
Baada ya tuko hilo ndugu, jamaa na marafiki walijulishwa kuhusiana na kifo cha mjeshi huyo ambapo walifika na kuuchukua  mwili wa marehemu hadi Hospitali ya Rufaa ya Lugalo jijini Dar kwa ajili ya kuuhifadhi.
UTAJIRI WA MAREHEMU
Mpaka kifo chake, marehemu Gweso alikuwa akimiliki magari manne ya kisasa, Toyota Prado (alikuwa nalo siku ya tukio), Toyota Verossa, Suzuki Vitara na VRS.
Aidha, alikuwa akimiliki biashara mbalimbali kama vile baa, duka la bia za jumla na nyumba ya kulala wageni. Vyote vipo Ukonga, Dar.
 
Waombolezaji wakiuchukua mwili wa Sajenti Yohana  Lugendo Gweso kwa ajili ya mazishi.
Baadhi ya waombolezaji siku ya msiba walimtaja marehemu kuwa mwanajeshi milionea aliyehakikisha anapiga hatua kwa biashara kila kukicha.
ALIANZA KUWINDWA MWAKA 2008
Habari zaidi zinadai kuwa, marehemu alianza kuwindwa mwaka 2008 ambapo watu wasiojulikana majina, sura wala nia yao, walivamia nyumbani kwake, Banana (uswahilini) na kumpiga risasi mtoto wa dada yake na kufariki dunia papo hapo.
 
Sajenti Yohana  Lugendo Gweso enzi za uhai wake.
Inadaiwa watu hao waliamini mtoto huyo ni Gweso mwenyewe lakni yeye hakuwepo. Kufuatia tukio hilo, marehemu aliomba kuhamia kambini kwa usalama wake hadi kifo kilipomkuta hivi karibuni.
MAZISHI YAKE
Marehemu Gweso amezikwa Septemba 27,  mwaka huu katika Makaburi ya Kijiji cha Tailo Wilaya ya Bunda Mkoani Mara. Ameacha mke mmoja na watoto wanne.

WANANCHI WAWASUBIRI WARIOBA, SITTA MTAANI

$
0
0
BAADA ya kutokea malumbano kati ya Mwenyekiti wa Tume Maalum ya Kukusanya Maoni ya wananchi juu ya mchakato wa Katiba mpya, Jaji Joseph Warioba na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la katiba, Samuel Sitta, wananchi waliohojiwa wamesema wanawasubiri kwa hamu wanasiasa hao mitaani ili kuwasikiliza maneno yao.

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la katiba, Samuel Sitta.
Mara baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uandishi katika Bunge Maalum la Katiba (BMK) Andrew Chenge kuwasilisha rasimu ya katiba inayopendekezwa, ambayo iliyaacha baadhi ya mambo yaliyokuwa katika rasimu iliyowasilisha na Tume ya Warioba, Waziri huyo mkuu wa zamani wa Tanzania, alisema anamsubiri Sitta mtaani waweze kujieleza mbele ya wananchi, ili hoja zao zipimwe.
“Ni kweli, kama alivyosema Warioba, waje huku mitaani watuambie hoja zao nani tumsikilize na kumfuata, maana sisi wengine tunaona kama wanatuchezea tu akili, rasimu rasimu, yaani wanatuchanganya kabisa,” alisema Tom Sisiri, mfanyabiashara wa nguo za mitumba aliyetakiwa kutoa maoni yake.
 
Mwenyekiti wa Tume Maalum ya Kukusanya Maoni ya wananchi juu ya mchakato wa Katiba mpya, Jaji Joseph Warioba.
Shoyoza Ibrahim, mwanamke mjasiriamali mwenye duka la vyombo Mwenge jijini Dar es Salaam, alisema viongozi wanatakiwa kutoa elimu ya kutosha ili kuwafanya watanzania waelewe kinachojadiliwa, kwani hata maneno yenyewe yanayotumika, ni msamiati mkubwa kwao.
“Utawasikia wanasema sijui rasimu, akidi, muswada, mchakato na mambo mengine kama hayo, watu kama mimi naweza kuwa naelewa wanamaanisha nini wakisema hivyo, lakini ninajua kuna idadi kubwa ya watu hawajui maana ya maneno haya, sasa hii misamiati ingefafanuliwa kwa lugha rahisi za watu kuelewa, halafu ndiyo watoe somo sasa la nini kinachobishaniwa,” alisema.
Bunge Maalum la Katiba ambalo lilikuwa likipitia rasimu ya katiba iliyowasilishwa bungeni na Jaji Warioba, linategemewa kumalizika mwishoni mwa wiki ijayo mjini Dodoma, likiwa na rasimu mpya inayopendekezwa.
 Stori: Ojuku Abraham/GOBAL PUBLISHERS

HII INAKUBALIKA BONGO? ANGALIA VIDEO YA IRINE UWOYA NA RICH WAKIFANYA 'KWELI' KWENYE SCENE YA MAPENZI!

$
0
0

Tasnia ya filamu nchini huenda ikawa na mengi yanayofanyika nyuma ya pazia wakati wa majaribio ya kutafuta shots nzuri zenye uhalisia hasa kwenye scene za mapenzi!
Lakini napata kigugumizi kikali kwa kile kilichoonekana kwenye video hii inayoaminika kuwa ni kipande cha filamu mpya inayotarajia kutoka iliyowakutanisha Rich na Irene Uwoya ambao wanaonekana wakibadilishana mate kwa kiss za uweli.

USIKU WA KIGODORO - 06

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ILIPOISHIA: Lina alichukua Bajaj ambayo ilimfikisha nyumbani kwake akiwa amechoka sana. Ile anaweka simu mezani tu, mumewe Semi akaichukua.
JIACHIE SASA…
“Kuna mtu nataka kumpigia nijue alipo halafu simu yangu haina hela,” alisema akiminya vitufe.
Moyo wa Lina ulilipuka kwani alikumbuka kuwa ndani ya simu hiyo kulikuwa na meseji za James ambazo hakuzifuta na zilisomeka vibaya kama zingeonwa.
Alitaka kupeleka mkono kumpokonya mume wake lakini alijua akifanya hivyo pia angempa picha mbaya kama nia yake haikuwa kupekua meseji.
Semi alipiga simu na kuongea na mtu ambapo alisikika akisema…
“Wee kama nilivyokwambia, hakikisha unatumia kila njia ili tuujue ukweli wa mambo. Unajua hakuna kitu kibaya kama mke awe wako halafu kumbe kuna mwingine anamwona ni mke wake, hiyo ndiyo maana yangu kuu.
“Sawa kaka, sawasawa, fanya uchunguzi wako halafu utanipa majibu.”
Lina aliishiwa nguvu, miguu ilimtetemeka, akataka kukaa lakini akajisikia kuumbuka. Alitamani kuuliza kinachoendelea, pia akashindwa.
Semi hakuwa na nongwa, alimrudishia simu yake huku akimwangalia usoni ambapo Lina aliamua kuukimbiza uso wake pembeni.
“Pole na starehe,” alisalimia Semi, Lina akashindwa acheke au ajibuje…
“Nzuri.”
“Mambo yaliisha salama?”
“Ndiyo.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo, kwani umesikia nini?”
“Nimesikia umenisaliti.”
Lina moyo ukamfanya paa! Mpaka akajishika kifua kwa hofu…
“Mungu wangu,” alisema ndani kwa ndani…
“Pole lakini, maana kulala nje ya nyumbani nako...” Semi alisema huku akicheka, kidogo Lina akajua mumewe anafanya utani kwani kwa anavyomfahamu asingeweza kucheka kama angekuwa analo jambo moyoni.
Lakini bado yale maneno aliyoongea mumewe na mtu kupitia simu yake kwamba achunguze mtu anaweza kusema ni mke wake kumbe kuna mwanaume mwingine naye anasema ni mke wake  yalimtesa akilini.
Alienda chumbani huku akifungua simu kuangalia namba iliyopigwa, akabaini ni ya mtandao ambao anao na yeye hivyo aliisachi…
“Issac Majurila ni nani, mbona sijawahi kumsikia,” aliwaza moyoni. Aliamua kumsaka ili kujua mumewe alimwambia amchunguze nani ambaye anaweza kuwa mke wa mtu kumbe kuna mwingine anasema ni mke wake!
***
“He! Kumbe leo ni Jumapili, nilisahau kabisa, nikajua utachelewa kazini,” alisema Semi akiwa ameingia chumbani ambapo hata Lina mwenyewe alishtuka, akakumbuka kwamba, alifunga ndoa jana yake Jumamosi, amelala na James usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili.
“Mh! Mi mwenyewe kusema za ukweli  nilijua leo ni siku ya kazi,” alisema Lina akiendelea kushangaa. Mara simu yake iliingia meseji, akaisoma chapchap...
“Baby leo ni Jumapili, sasa umeondoka bila kusema utakuja muda gani?”
Lina aliijibu palepale…
“Mchana nitakuwa hapo baby, hata mimi nilisahau kabisa kwamba leo ni Jumapili, sijui ni kwa nini wote tulisahau.”
“Oke, ilitokea tu, uje basi kwa muda huo.”
Bahati nzuri pale nyumbani napo, Semi aliaga anakwenda kwenye shughuli zake hivyo Lina akabaki yeye na msichana wa kazi tu. Ikawa ni nafasi yake ya kurudi hotelini aliko James.
Alikwenda sebuleni, akazima tivii maana alimkuta mumewe Semi ameiwasha akitazama mambo mbalimbali. Lina aliizima kwa sababu alihisi inamchanganya, kwa wakati huo alihitaji kutafakari zaidi kwa kitendo alichokifanya.
Kwanza alijua amemfanyia kitendo kibaya sana James, kufunga naye ndoa ambayo ni batili. Alihisi huruma anatakapogundua wakati mwenzake mapenzi yote aliyaelekeza kwake kama mke.
Pili, alimini kuwa James anajua amejikomboa kwa kupata mke na yeye anapitia sera za kike maana yake ametoa mkosi, sasa kumbe badala ya kuondoa mkosi amejiongezea…
“Hivi huu mtego nitawezaje kujinasua nao? Ni kwa nini nimeuingia? Ni tamaa ya hela au mapenzi ya dhati?” aliwaza Lina. Lakini kwa harakaharaka alipata jibu kwamba, zile laki mojamoja kila kukicha zilimchanganya akili licha ya kwamba ni kweli James ni kijana mtanashati sana.
Lina aliamua kumpigia simu shoga yake, Eg na kumwambia anavyojisikia…
“Halo Lina…”
“Eg…”
“Bee.”
“Naweza kujiua mwenzio.”
“He! Kwa nini Lina, kuna nini kimetokea? Shemeji kajua?”
“Hapana! Ila…”
“Ila nini tena Lina?”
“Unajua nimefanya jambo la kipuuzi sana? James anajua mimi ni mke wake wa ndoa. Halafu sasa, mbaya zaidi ndoa yenyewe ya Kikristo, ni kama loki. Siku akijua nina mume tena wa ndoa nini kitatokea?
“Mtu mwenyewe ana hela, nahisi atanifunga na hakuna wa kunitetea. Najuta Eg, najuta kabisa. Sijui ni kwa nini na wewe rafiki yangu kipenzi hukinikataza?”
“Lina, nisingekukataza mtazamo wako na wangu ni mmoja tu. Kama ni kujuta sasa tujute wote, kwani kwa maneno yako ya saa hizi hata mimi nimegundua hilo…”
“Eg subiri nipokee simu ya James…halooo.”
“Mke wangu Lina…”
“Abee baba.”
“Mwambie dada ukija mchana hakuna kurudi tena huko. Utakuwa unatokea hapa kwenda kazini na kurudi mpaka siku tano tunahamia nyumbani, hivyo ukija beba nguo zako kwenye sanduku chukua teksi.”
“Mh! Sawa baby.”
“Mbona umeguna kwanza?”
“Basi tu, nafikiria jinsi ya kumwambia huyo dada.”
“Unafikiria jinsi ya kumwambia dada? Kwa nini ufikirie? Mimi si mume wako kwa sasa? Tena wa ndoa.”
“Ni kweli my love.”
“Sasa?”
“Oke, nimekuelewa.”
James alikata simu na kumwacha Lina katika mawazo kibao…
“Da! Nimeingia mkenge kwa kweli. Hapa sina cha kujitetea, siwezi kutengua ndoa tena. Imefungwa imefungwa tu. Kinachotakiwa ni kuamua moja, kusuka au kunyoa…
“Semi mume wangu akijua sijui nini kitatokea. Da! Balaa! Hivi kama ni tamaa, tamaa gani ya hivi mimi Lina mimi? Haya mambo si yanaweza kufika kwa wazazi? Yakifika nitajiteteaje?”
Lina alikosa ujasiri wa kufikiria kiasi kwamba alianza kutoa machozi mwenyewe…
“Mungu wangu, nisaidie mimi. Nimekwaa tatizo kubwa.”
Kwa upande wake James baada ya kumkatia simu Lina naye alizama kwenye maswali kibao huku akikosa majibu ya moja kwa moja…
“Ni kwa nini Lina anamuogopa dada yake kiasi hicho? Yeye si mke wangu wa ndoa? Sasa nini kitamfanya huyo dada azuie Lina kuondoka?
“Halafu, kwani mbona siku ya harusi ukumbini sikumwona huyo dada yake akitambulishwa? Maana kama ndiye ameishi naye alitakiwa kutambulishwa kama mzazi wa Lina kwa hapa Dar es Salaam.”
Kifupi wote walikuwa katika wakazi mgumu sana, kila mmoja alikuwa na maswali yake yaliyokosa majibu ya moja kwa moja kwa pale.
***
Mchana ulifika, Lina mapigo ya moyo yaliongezeka kwa sana. Kila dakika ilipokatika aliitupia macho simu yake akiamini James atapiga…
“Huyu atapiga sasa hivi,” alisema moyoni. Aliwaza amwambie nini mume wake, Semi ili aondoke kurudi hotelini aliko James lakini pia alijiuliza akienda bila nguo ataelewekaje kwa mumewe huyo?
Kama aliota, simu ya James iliita. Aliitupia macho kwa dakika moja nzima mpaka akakata. Ikapigwa tena ndipo akapokea…
“Baby…
“Mbona hufiki? Nikufuate?”
“Noo baby, nilikuwa naweka nguo zangu kwenye begi nakuja.”
“Poa.”
James akakata simu kwa dalili zote kwamba amekasirika na mwenendo wa Lina kwa siku ile.
Lina alimpigia simu mume wake ili amdanganye kitu…
“Baby…”
“Ee baby…”
“Kuna balaa juu ya balaa,” alisema Lina…
“Lipi tena baby?”
“Yaani Eg ana dada yake alikuwepo kwenye sherehe ya jana, amefika kwake ameumwa ghafla kakimbizwa Muhimbili…”
“Duu! Balaa. Sasa?”
“Sasa nakuomba ruhusa niende Muhimbili mchana huu maana Eg naye anakwenda.”
“Sawa! Lakini huyo atakuwa amekula kitu kibaya, unajua sherehe sherehe hizi mambo hayo hutokea. Ngoja nikupe namba ya Dokta Matingisha ukifika umpigie ili asaidie.”
“Itakuwa vizuri baby.”
Lina aliachia tabasamu, akapata akili. Alichukua begi, akatoa kwenye kabati lake nguo za zamani kibao na kuziweka kwenye begi.
Kama vile hiyo haitoshi, akafunua godoro ambapo pia mlikuwa na nguo nyingine, nazo akazitia kwenye begi mpaka likavimba. Akachukua Bajaj hadi hotelini alipo James.
***
Eg alikuwa hana hili wala lile, simu ya shemeji yake Semi ikaingia kwake…
“Mh! Huyu shemeji vipi, si kawaida yake kunipigia simu,” alisema moyoni Eg huku akiwaza apokee au la! Akaamua kuipokea…
“Haloo shem…”
“Shemeji poleni sana na mgonjwa jamani! Aisee,” alisema mume wa Lina…
“Mgonjwa?” alihoji Eg…
“Si Lina ameniambia kwamba…”
Eg alikata simu haraka sana. Akampigia Lina…
“Shoga…”
“Ee shoga vipi?” alisema Lina…
“Umemwambia shemeji nina mgonjwa?”
“Ha! Ndiyo Lina, kakupigia? Please mwambie unaye, nimemwambia ni dada yako amelazwa Muhimbili anaumwa sana tumbo la kuendesha na yuko hoi…”
“Oke, tena huyo anapiga ngoja nipokee…
“Haloo shem…”
“Shem, naona mtandao unasumbua…Lina kaniambie una mgonjwa.”
“Eee, unajua nilidhani unasema wewe ndiyo una mgonjwa ndiyo maana nikauliza mgonjwa gani?! Dada yangu bwana, anasumbuliwa na tumbo tukamkimbiza Muhimbili.”
“Da! Poleni sana, lakini Mungu atamsaidia.”
“Asante sana shemeji.”
“Oke shemeji. Sisi tupo, yeye kaniambia anakuja Muhimbili.”
“Ee, na mimi naelekea huko shemeji yangu.”
“Sawa, baadaye.”
***
Lina alifika hotelini, akasukuma mlango na kuzama kwenye chumba alichomo mume wake wa pili James…
“Hodi.”ITAENDELEASIKU YA KESHO.

NI RAHISI MWANAMKE ALIYEAJIRIWA KUSALITI!

$
0
0
KWANZA nianze kwa kuwashukuru wasomaji wote wa safu hii, waliowasiliana na mimi kwa namna moja au nyingine, katika kubadilishana mawazo juu ya uhusiano. Ni faraja kugundua kwamba wapo watu wanaofuatilia unachokiandika na kisha kutaka kuchangia neno.

Mada yangu ya leo inaweza kuniletea ugomvi na waajiriwa wenzangu wanawake, lakini panapo ukweli ni vyema tukasema, kwa sababu unasaidia katika kurekebisha na wakati mwingine hata kujua jinsi gani unaweza kujihami, ili kutokusaliti ndoa au uhusiano wako wa kimapenzi.

Nina uzoefu kidogo na mambo ya kazi za ajira maofisini, nimefanya hivi kwa muda mrefu. Wakati flani nilifanya kazi katika ofisi zilizo katikati ya jiji, kule mitaa ya Posta jijini Dar es Salaam.
 

Ofisi nyingi za serikali na watu binafsi zinapatikana mitaa ile. Kutokana na sababu hiyo, kuna idadi kubwa pia ya migahawa, hoteli, mama ntilie, pub na kadhalika.
Kuna mambo mawili makubwa yenye ushawishi mkubwa wa usaliti. Ofa za chakula au vinywaji na usafiri. Kwa kawaida, wafanyakazi wa ofisi moja hupenda kutoka pamoja wakati wa chakula cha mchana, wenyewe tunapendelea zaidi kusema lunch!
Kila mmoja ana sehemu yake anayokula kulingana na kipato chake, wapo wanaokwenda Southern Sun kupata chakula cha mchana, na wapo wanaowafuata mama ntilie wanaojibanza kwenye vichochoro vingi vilivyopo mjini.
Huko ndiko tunakokutana na akina dada waliovalia vizuri na kupendeza, wakitokea katika maofisi mbalimbali, huwezi kujua yupi ni mhudumu wa chai, yupi ni bosi, wote wanang’ara. Na hapa ndipo ofa za misosi zinapoanza kushawishi ngono. 
Kijana mmoja mwenye kipato kikubwa ofisini kwake, atavutiwa na msichana mrembo mwenye mshahara wa wastani. Ili kumsogeza karibu, atalipia chakula cha siku hiyo na kumualika kwa kesho yake. Kulipiwa chakula ni jambo dogo, lakini lenye thamani kubwa sana. Si rahisi mtu aliyekulipia chakula kwa nia njema, ukaacha kumshukuru na hata kumwelekeza unapofanya kazi.
“Mimi nipo pale Oj Traders,” msichana anaweza kujita mbulisha jina na kusema anapofanyia kazi huku mkaka akimweleza kuwa yeye ni mhasibu katika ofisi flani. Watakapo
 

kutana mara ya pili, wataachiana namba za simu.
Baada ya hapo, mkaka atafanya mbwembwe za kuhamahama maeneo ya lunch ili mradi tu mdada wa watu aingie kwenye laini.
Ukimaliza suala la lunch, kuna hii kitu foleni, hasa kwa wakazi wa Dar es Salaam. Raha ya kufanya kazi katikati ya jiji inaingia shubiri kadiri jioni inavyozidi kusogea. Kuanzia saa kumi, ni vurugu katika vituo vya daladala na hasa wakati kama huu ambao bodaboda zimezuiliwa kuingia mjini.

Wenye magari binafsi ndiyo wakati wao wa kujidai, ingawa foleni inawakumba wote. Lakini ni afadhali ukiwa kwenye foleni ndani ya gari dogo, mko wawili kuliko foleni, umeshika bomba kwenye daladala.
 

Siyo rahisi kwa mdada kukataa lifti ya kijana mwenye gari. Na katika foleni ndefu, ni wazi kwamba hadi mwisho wa safari, watakuwa wameshabadilishana namba. Kwa msichana, kuwa na uhakika wa usafiri kila siku ni ukombozi.
Tusidanganyane, hakuna msichana ambaye hatajua kuwa lunch au usafiri anaopewa unahitaji malipo maalum, ambayo ni penzi. Hali hii haiko Dar tu, bali nchi nzima na pengine duniani kote.
 

Mwanamke aliyeajiriwa anakuwa katika mitihani mikubwa zaidi ya kusaliti ndoa au uhusiano wake, kwa sababu hata kama haitakuwa kwenye chakula au usafiri, bado watu anaokutana nao katika utendaji wake, wanaweza kumghasi. Fikiria anakutana na mabosi, marafiki wa mabosi wake, wafanya biashara, atapona kweli?
Hata hivyo, simaanishi kama tabia hii inawakumba waajiriwa wote, isipokuwa nadhani ni sehemu kubwa wanahusika!
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

MAHUSIANO: WADADA SOMO LA BURE KWENU,SOMA HAPA

$
0
0
Jamani wee, kila nikitaka kukaa kimya mdomo unanicheza, siwezi kukaa kimya moja kwa moja lazima nitie neno ili kuhakikisha mambo yanakwenda sawa. Kufunga kwetu bado hakusimamishi  mapenzi ndani ya nyumba zetu, hivyo siwezi kukaa kimya huku naona jahazi  linazama.

Leo wari wangu nataka niwape somo la bure kuhusu kulinda nyumba zetu. Tunalalamika kuwa waume zetu hawaoneshi kufurahia mapenzi tukiwa faragha. Inawezekana uliyenaye ni mgeni wa mambo ya chumbani, nawe kama siyo mbunifu wa kujua uliyenaye ni ‘maimuna wa mapenzi’ basi penzi lenu linakuwa bora liende.

Waweza usione hasara zake mapema, lakini huwa kubwa, ndicho chanzo cha nyumba nyingi  kuyumba au kusambaratika kabisa. Unajua sababu gani?


Nakuuliza acha kunitumbulia mijicho kama fundi saa aliyepoteza lensi. Siku zote wachawi wa uhusiano wetu huwa sisi wenyewe, bila kujua tunaziroga ndoa zetu au uhusiano wetu.

Hebu kaa chini nikupashe ili usichelewe kumpikia futari na uji, basi uongeze cha ziada ili upate zaidi ili panapo majaaliwa umeremete kwenye sikukuu ya idd au usiye muislamu uamshe furaha na kumfanya mwenzako achanganyikiwe na kuona mambo mapya ya kimahaba.

Si wote mmepitia unyagoni na kupata mafunzo ya chumbani, jamani mafunzo ya chumbani ukiyajua nina imani ndoa yako kila siku itakuwa mpya. Katika maisha ya ndoa hasa ya chumbani lazima mwakwetu ujue wanaume wanapenda nini? Na hii utaijua pale mwanaume wako wa kwanza utakayekula naye raha umuulize kijanja vitu gani anapenda siyo kukurupuka kama unatoka kujisaidia kichakani.

Siku zote mjenzi mzuri hujifunza tabia za udongo ili akijenga nyumba isianguke haraka au kuweka nyufa. Hata katika mapenzi ukiwa faragha na mwenzako hebu jenga tabia ya kudadisi.
 

”Mpenzi nikikushika wapi unajisikia raha?” lazima atakujibu vilevile nawe una haki ya kumueleza mpenzi wako kuwa:
“Mpenzi wangu usisumbuke sana kunipapasa mwili mzima mi sehemu zangu hizi, ukinigusa sehemu hizi kama umetwanga pilipili lazima nikohoe.”

Umeona siyo mtu anakushika sehemu nyingine wala hazina msisimko unamuacha pengine naye Maimuna hajui lolote alipokushika ndipo uwezo wake wa kujua sehemu za kumsisimua mwanamke.
 

Kwa vile hajui basi utajikuta mpaka mchezo unaanza mwili wako bariiiidii. Haipendezi hebu basi tuambiane ukweli ili kuifanya nyumba yetu kila mara iwe na furaha.

Kuna maeneo mengi ya mambo ya chumbani unatakiwa kuyajua mkiwa kitandani. Unapoona hutendewi haki mweleze mwenzako ili ajue siyo kukaa kimya unaumia moyoni kumbe ulitakiwa kusema. 

Wengi hulalamika hawajawahi kufurahia tendo la ndoa tangu waolewe hata wengine kudiriki kusema huwa hawafiki mwisho wa safari, mmh! Kioja.

Narudia kauli yangu, siyo wote wanaojua mapenzi, hebu muulize mtu aliyekuzidi amewezaje kufurahia mapenzi muda wote. Akishakueleza basi lifanyie kazi ndani, haki ya nani utashangaa kumuona mtu mzima akilia kama mtoto mdogo, si kwa kupigwa bali kutu ya mapenzi imeondolewa sasa hivi chuma kimekuwa laiiiini raha kila kona.

Utashangaa unapata ambavyo hukuwahi kupewa, la muhimu ni kukubali kujifunza na kuyafanyia kazi, hakika kila siku ndoa yako itakuwa mpya.
Yangu yanatosha, ni mimi Anti Nasra, Shangingi Mstaafu.
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

BARCA WAPIGWA, MAN CITY WABANWA, CHELSEA WAITOA SHOO TIMU YA NANI

$
0
0

Mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya leo zilikuwa na raha yake. Sasa iko hatua ya makundi lakini ushindani uko juu, angalia matokeo ya mechi za leo.



Sporting 0-1 Chelsea:
Sporting Lisbon ikiwa nyumbani, imeshindwa kuonyesha cheche baada ya kulambwa bao 1-0 na wageni wake Chelsea.
Licha ya juhudi za Luis Nani kutaka kuonyesha mchango wake tokea arejee Ureno, kikosi cha Jose Mourinho kilikuwa imara na Nemanja Matic ndiye alikuwa shujaa.

PSG 3-2 Barcelona:
PSG ikiwa nyumbani imefanikiwa kuifunga Barcelona kwa mabao 3-2.
PSG licha ya kucheza bila nahodha wake Zlatan Ibrahimovic ilionyesha soka safi na kufunga mabao matatu kupitia beki David Luiz, Marco Verrati na kiugo mtundu Blaise Matuidi lakini nyota Lionel Messi na Neymar nao wakajitutumua kufunga hayo mawili.

Man City 1-1 AS Roma
Vijana wa Manuel Pellegrini licha ya kuwa nyumbani, waliushindwa mziki wa AS Roma na kujikuta wakilazimishwa sare ya bao 1-1.
Man City walicheza vizuri na kupoteza nafasi nyingi na bao lao moja la Kun Aguero kwa mkwaju wa penalti halikuwasaidia hasa baada ya nahodha wa AS Roma, Francesco Totti kusawazisha.

CSKA Moscow 0-1 Bayern Munich:
Bayern Munich wamezidi kujiongezea pointi baada ya kufikisha sita kutokana na ushindi wa ugenini nchini Urusi.
Bao pekee la Muller, limewapa ushindi kama ule dhidi ya Man City katika mechi iliyopita.

MATOKEO MENGINE:
APOEL NICOSIA 1-1 AJAX 
SCHALKE 1-1 MARIBOR 
BATE 2-1 BILBAO
SHAKTAR 2-2 PORTO

MAPICHA ZAIDI YA ACTION, BAADAYE KIDOGO

BIFU LA FLORA, NISHA LAFIKA PABAYA

$
0
0



WASANII wawili waliowahi kuwa marafiki wa kupika na kupakua, Flora Mvungi na Salma Jabu ‘Nisha’ bifu lao sasa limefika pabaya baada ya hivi karibuni kuwaacha watu midomo wazi kwa kitendo chao cha kupitana kama hawafahamiani.

Msanii wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’.
Ishu hiyo ilitokea wikiendi iliyopita kwenye sherehe ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya staa wa filamu, Wastara Juma iliyofanyika katika ukumbi wa Dar West uliopo Tabata jijini Dar es Salaam. Wawili hao walikutana mlangoni wakati wa kuingia, lakini Flora alimpita Nisha kama hamfahamu na kama hiyo haitoshi, walipoingia ndani, kila mmoja alikaa meza yake.
Wakati sherehe zikiendelea, ukafika wakati wa kufungua shampeni na baada ya tukio hilo, Nisha alipewa jukumu la kuwagawia wageni waalikwa kwa kuwamiminia kwenye grasi zao, lakini alipofika kwenye meza aliyokaa mwenzake, Flora alikataa glasi yake kuwekwa kinywaji hicho.
 
Msanii wa filamu Bongo, Flora Mvungi.
Baada ya tukio hilo, paparazi wetu aliwafuata mastaa hao na kuwauliza kulikoni, na Flora alisema: “Sikumuona Nisha mimi, na shampeni nimekataa kwa sababu huwa siipendi.”
Kwa upande wake, Nisha alisema: “Mimi sikumuona Flora, kuhusu Shampeni mbona nilimimina kwenye glasi zote jamani!”

A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 07

$
0
0

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

“Kuna nini? Umeona nini?” Kijana mwingine alimuuliza.
“Nendeni mkaangalie wenyewe. Inatisha”
“Inatisha? Inatisha nini?”
“Nyie kaangalieni tu”
Vijana wengine wakaelekea katika gari lile na kuchungulia ndani. Miili mitatu ilikuwa ikionekana vizuri huku ikiwa imeteketea kwa moto na huku ikitoa moshi. Simu zikaanza kupigwa katika kituo cha polisi cha Oysterbay ili kuwaomba mapolisi kufika mahali hapo haraka iwezekanavyo.

Watu ambao walikusanyika mahali pale walikuwa watano lakini kadri dakika zilivyozidi kwenda na ndivyo watu walivyozidi kuongezeka mpaka kufikia watu zaidi ya mia mbili. Kila aliyefika mahali pale na kuangalia miili ya watu wale, alishikw kichwa kwa huzuni.
   Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walivyozidi kuongezeka zaidi na zaidi. Watu ambao walikuwa wakipita katika barabara ya lami wakasimamisha magari yao na kuanza kuelekea pale ambapo gari lile lilipokuwa limeteketezwa kwa moto.
Zilipita dakika thelathini na ndipo waandishi wa habari wakafika katika eneo la tukio hata kabla ya mapolisi. Wakaanza kupiga picha kila kitu kilichokuwa kinaendelea mahali pale huku wakichukua muda wao kuwahoji watu ambao walikuwa katika eneo hilo. Kila aliyekuwa akihojiwa, alikuwa akiongea kwa uchungu, wakinamama walishindwa kujizuia, muda wote walikuwa wakilia.
Mapolisi wakafika mahali hapo na kuwaomba watu kusogea mbali na gari lile, wakaingia ndani na kuanza kuitoa miili ile ya Bi Upendo na watoto wake na kisha kuiweka katika gari lao aina ya Defender. Hawakutaka kubaki mahali hapo, safari ya kuelekea hospitalini ikaanza.
“Hivi ilikuwaje?” Mwandishi mmoja wa habari alimuuliza kijana mmoja ambaye alikuwa mtu wa kwanza kufika mahali hapo.
“Yaani toka gari hili lilipokuwa linafika mahali hapa nilikuwa naliona japo nilikuwa mbali sana” Kijana yule alisema hali iliyowafanya watu wengine kumzunguka kutaka kujua ni kitu gani kilitokea.
“Sikulitilia shaka yoyote ile, nikamuona jamaa mmoja ambaye alikuwa amevaa kofia kubwa ya Malboro akiteremka huku akiwa na chombo kidogo, sijui kilikuwa kidumu kile…wala sikukiona vizuri. Nikamuona akianza kulimwagia gari hili. Nafikiri ilikuwa petroli japokuwa mimi nilifikiri maji huku nikidhani alikuwa akiliosha gari lake.” Kijana yule aliwaambia.
“Eheee..!! Ikawaje sasa?”
“Baaada ya muda nikaamua kwenda kuogelea kama kawaida yangu. Ile napiga mbizi mbili tatu, nikashangaa kuuona moto mkubwa ukiwaka. Unajua nilishtuka sana, nikajikuta nikitoka baharini na kuanza kuja huku” Kijana yule alielezea huku kila mtu akibaki kimya akimsikiliza.
“Kwa hiyo mtu mwenyewe hukumuona tena? Au alisimama pembeni?”
Sikumuona. Yaani sijui alikimbilia wapi”
                                                                 *******
Wabunge wengi walikuwa Bungeni wakisiliza kwa makini sana namna ambavyo Bajeti ya taifa ilivyokuwa ikisomwa. Muda wote ambao bajeti ilikuwa ikisomwa, mawaziri ambao walijiita BoT walikuwa wakikenua kila wakati, vifo vya watu wawili vilionekana kuwafurahisha sana.
Mzee Boniface akahisi simu yake ikitetemeka mfukoni, akaitoa na kuanza kuangalia namba ya mpigaji. Namba ilikuwa ngeni kabisa machoni mwake. Akatamani kuipuuzia lakini akaamua kuanza kupiga hatua kuelekea nje ili kujua ni nani ambaye alikuwa akimpigia simu.
“Haloooo…!” Mzee Boniface aliita.
“Haloooo…Naongea na mheshimiwa waziri hapo?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.
“Ndio. Wewe ni nani na sijui nikusaidie nini?”
“Kuna tatizo mzee. Nakuomba uje Dar es Salaam mara moja”
“Tatizo? Tatizo gani ambalo mpaka mnataka mimi nije huko?” Mzee Bonifasi aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Wewe njoo mzee. Tena ikiwezekana, njoo sasa hivi” Sauti ya upande wa pili ilisema.
“Hilo si tatizo. Nikija hapo Dar es Salaam nielekee wapi sasa?” Mzee Boniface aliuliza.
“Njoo katika hospitali ya Taifa”
“Hospitali ya Taifa?”
“Ndio. Fanya haraka sana” Sauti ya upande wa pili ilisikika na kisha simu kukatwa.
Mzee Boniface akaonekana kuchanganyikiwa, neno hospitali ya Taifa ndio ambalo lilionekana kumtisha zaidi. Tayari akaona kuna tatizo lilikuwa limetokea, hivyo alichokifanya ni kumpigia simu mkewe, simu haikuwa ikipatikana.
Mzee Bonifasi akaonekana kuchanganyikiwa. Akapiga katika simu ya mezani, simu ikaanza kuita na baada ya muda ikapokelewa na mfanyakazi wake wa ndani. Tayari kijasho chembamba kilikuwa kinamtoka, akajihisi kuchanganyikiwa kupita kawaida.
“Hallooo…! Mage, mama yako yupo hapo?” Mzee Bniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hayupo. Ametoka”
“Ametoka? Ameelekea wapi asubuhi yote hii?”
“Amewapeleka watoto shule pamoja na dereva”
“Inakuwaje leo amewapeleka shule? Si huwa anawapeleka dereva peke yake?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hata mimi sifahamu”
“Hakuna tatizo lolote lililotokea hapo nyumbani?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa zaidi.
“Mmmmm…!! Wala hakuna” Mage alisikika akijibu.
“Sawa. Nakuja huko huko”
“Sawa”
Mzee Boniface akaonekana kuchanganyikiwa zaidi. Hakuwa na sababu ya kuaga, moja kwa moja akampigia simu dereva wake ambaye alikuja na kumtaka kumpeleka uwanja wa ndege. Mwili wote ulikuwa ukimtetemeka, jasho ambalo lilikuwa likimtoka lilimfanya shati lake lote kulowana kana kwamba alimwagiwa ndoo ya maji.
“Mbona unaonekana tofauti leo?” Dereva alimuuliza.
“Wewe twende kwanza” Mzee Boniface alimwambia dereva.
Wala hazikupita dakika nyingi, wakafika uwanja wa ndege. Tiketi ya ndege ikakatwa kwa haraka sana. Akaichukua tiketi ile ya ndege na kuanza kuiangalia. Akaamua kumrudia dereva ambaye alikuwa nje ya jengo la uwanja wa ndege.
“Hivi hauwezi kuendesha gari kwa mwendo wa kasi. Yaani baada ya saa moja tuwe tumefika Dar es Salaam?” Mzee Boniface alimuuliza dereva wake.
“Ndani ya saa moja?” Dereva aliuliza huku akionekana kushtuka.
“Sasa unaniuliza ina maana haujanisikia au?”
“Mheshimiwa haiwezekani. Labda kama hapa ingekuwa Morogoro sawa. Ila kumbuka hapa ni Dodoma” Dereva alimwambia mzee Boniface
“Lakini bado haujanijibu swali langu”
“Nimekwishakujibu mzee kwamba haiwezekani. Kutoka hapa Dodoma hadi Dar es Salaam ni mbali sana” Dereva alimwambia mzee Boniface.
Mzee Boniface akabaki kimya. Wasiwasi ukazidi kuongezeka moyoni mwake. Simu ambayo alipigiwa katika kipindi kichache kilichopita tayari ilikuwa imemchanganya. Furaha yote aliyokuwa nayo juu ya kifo cha Dominick na Saida ikapotea moyoni mwake.
Kadri muda ulivyozidi kusonga mbele na ndivyo wasiwasi ulivyozidi kumpanda zaidi. Alibaki katika kiti cha gari lake huku akiwa kimya, mawazo yake yalikuwa yakifikiria mbali sana kwa wakati huo. Kwa haraka sana, akaichukua simu yake na kuanza kubonyeza namba za simu yake ya mezani iliyokuwa nyumbani kwake, simu ikaanza kuita, baada ya muda, Mage akaipokea.
“Kuna kitu chochote kilichoendelea huko? Mzee Boniface alianza kuuliza swali.
“Kitu gani?” Sauti ya Mage ilisikika ikiuliza.
“Chochote kile”
“Hapana. Hakuna chochote kile?”
“Hakuna”
“Yaani hata mtu kuja kuniulizia?”
“Aaaah..! Nimekumbuka. Walikuja mapolisi hapa” Mage alimwambia mzee Boniface.
“Wamesemaje?”
“Hawakuniambia kitu chochote kile zaidi ya kukuulizia wewe”
“Sawa” Mzee Boniface alisema na kukata simu.
Akili yake ikachanganyikiwa zaidi. Dereva hakutaka kuuliza kitu chochote kile, alibaki kimya akimwangalia mzee Boniface alivyochanganyikiwa.
Dakika zilizidi kwenda mbele huku sekunde zikienda katika kasi yak kama kawaida. Saa la kwanza likakatika, na hatimae saa la pili kutimia. Abiria wote wakaitwa katika ndege ambayo walikuwa wakihitajika tayari kwa safari ya kuelekea Dar es Salaam kwa kupitia Morogoro.
Kadri ndege livyokuwa ikisafiri angani kuelekea Dar es Salaam na ndivyo ambavyo wasiwasi wake ulivyozidi kuongezeka zaidi. Amani ikazidi kupotea moyoni mwake. Hakuwa na hamu ya kula kitu chochote kile, kila alipopitishiwa vyakula mbalimbali, alikataa kula, mbaya zaidi, hata maji hakutaka kunywa.
Ndege aliiona ikiendelea na safari kwa mwendo wa taratibu sana, alitamani afike haraka Dar es Salaam na kuelekea katika hositali ya taifa. Safari iliendelea zaidi na zaidi na hatimae kuingia katika uwanja wa ndege saa nne sita asubuhi.
Hakutaka kuchelewa kubaki uwanjani hapo, kwa haraka haraka huku akionekana kuchanganyikiwa, akachomoka na kuelekea nje ya jengo la uwanja ule ambako akachukua taksi.
“Twende Muhimbili” Alimwambia dereva taksi ambaye alikuwa akimshangaa.
“Elfu kumi na t….”
“Wewe twende bwana. Mbona unataka kunichelewesha” Mzee Boniface alimwambia dereva taksi ambaye kwa haraka sana, akaliwasha gari na kuondoka uwanjani hapo.
Mzee Boniface alimuona dereva taksi akiendesha kwa mwendo wa taratibu sana kiasi ambacho akatamani kushikilia usukani yeye mwenyewe. Kila wakati alikuwa akimuhamasisha dereva kuongeza kasi.
Mpaka wanafika katika hospitali ya Muhimbili, walitumia dakika arobaini na saba njiani. Akamlipa dereva kiasi chake cha fedha alichokihitaji na kwa haraka haraka akateremka na kuanza kuelekea katika eneo la hospitali ile.
Ingawa watu wengi walikuwa wamezuiliwa kutokana na wakati ule kutokuwa muda wa kuwaona wagonjwa, lakini kutokana na kuwa na nyadhifa kubwa serikalini, mzee Boniface akaruhusiwa kupita. Watu wote ambao walikuwa mahali hapo walikuwa wakimshangaa kwa jinsi alivyokuwa akitokwa jasho.
Kila mmoja aliyemuona mzee Boniface alikuwa akijiuliza juu ya hali ambayo alikuwa nayo. Kila mtu alifahamu kuwa kwa wakati huo alihitajika kuwa Bungeni kuwawakilisha wananchi wake, lakini kwa nini wakati ule alikuwa hospitalini, tena akionekana kuwa na haraka huu uso wake ukiwa umejaa wasiwasi?
“Mheshimiwa…!” Alisikia akiitwa. Kwa haraka haraka akageuka, macho yake yakagongana na umati wa mapolisi pamoja na baadhi ya manesi ambao walikuwa wamesimama nje ya chumba kimoja kilichoandikwa Monchwari kwa nje. Mzee Boniface akazidi kushikwa na wasiwasi zaidi, nyuso za watu wale zilikuwa zimejawa na huzuni kupita kawaida.
“Kuna nini? Niambieni kuna nini?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Twende kwanza ofisini” Daktari alimwambia na wote kuanza kwenda katika ofisi ya daktari huku baadhi ya mapolisi wakiwafuata.
Mzunguko wa damu mwilini mwake ulikuwa mkubwa, mapigo ya moyo yalikuwa yakimdunda kupita kiasi. Walipoifikia ofisi ile moja kwa moja wakaingia ndani na kutakiwa kukaa kitini. Macho yake yalikuwa yakimwangalia daktari kwa wasiwasi kupita kawaida.
“Kuna nini daktari? Mbona hamtaki kuniambia?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kukasirika.
“Kuna habari mbaya. Ila kwa sababu wewe ni mwanaume, ningependa ujipe moyo wa ushujaa kuisikia habari hii” Daktari alimwambia mzee Boniface.
“Mbona unazunguka zunguka? Niambie kwanza” Mzee Boniface alimwambia daktari huku akionekana kuwa na hasira zaidi.
“Kuhusu familia yako”
“Familia yangu? Imefanya nini?”
“Imeteketezwa kwa moto. Mkeo na watoto wako wamefariki kwa kuunguzwa na moto vibaya” Daktari alimwambia mzee Boniface.
Mzee Boniface akaiona presha ikipanda kwa kasi. Akabaki ameganda kna kwamba alikuwa akijitayarisha kupigwa picha. Akailalia meza ya daktari, ghafla akaanguka chini kama mzigo. Hakujua kitu chochote kilichoendelea baada ya hapo. Alionekana kuwa katika hali ya nusu kifo.
                                                                        *******
Miili ilikuwa imeteketea vibaya kupita kawaida. Kila polisi ambaye alikuwa akiiangalia alibaki kushika tama kwa huzuni. Haikuwa rahisi hata kidogo kuwatambua watu wale ni wakina nani. Walikuwa wakitisha kupita kawaida. Picha ambayo ilikuwa ikionekana mbele yao, ilikuwa ni picha mbaya ambayo ilikuwa ikiwasisimua kupita kawaida.
“Hali inatisha” Polisi mmoja alijikuta akisema.
Gari lile likaenda moja kwa moja hadi katika hospitalini ambacko machela zikaletwa na miili kupakizwa huku ikifunnikwa shuka. Machela zikasukumwa moja kwa moja mpaka katika chumba kikubwa cha kuhifadhia maiti. Mapolisi walibaki nje wakisubiri kuona ni kitu gani kingeendelea mahali hapo.
Mara mzee mmoja ambaye alikuwa na vazi refu jeupe akaanza kuelekea kule waliposimama na kisha kuingia ndani ya chumba kile. Wala hazikupita dakika hata tano, akatoka huku uso wake ukiwa umejawa na huzuni kupita kawaida.
“Kuna ndugu zao wowote mmekuja nao?” Dokta aliwauliza mapolisi.
“Hapana”
“Sasa hata majirani zao mmeshindwa kuja nao? Au walikuwa wanaishi porini?” Dokta aliuliza huku mawazo yake yakimpelekea kuwa ni ajali ya nyumba kuungua ndio ambayo ilikuwa imetokea.
“Bora ingekuwa hivyo daktari. Hawa watu wamechomwa moto wakiwa ndani ya gari, gari lenyewe lilikuwa limetelekezwa ufukweni” Polisi mmoja alimwambia daktari ambaye akaonekana kushtuka.
“Wamechomwa moto ndani ya gari?” Daktari aliuliza kwa mshtuko huku akionekana kutokuamini.
“Ndio”
Mapolisi hawakutaka kuendelea kubaki hospitalini hapo, bado walijiona kuwa na kazi ambayo ilibakia kwa ajili ya kumjua mmiliki wa gari lile. Moja kwa moja wakaenda katika kituo chao cha Oysterbay na kisha kuagiza gari lile lililoteketezwa kwa moto kuletwa kituoni pale.
Dakika arobaini na tano gari lile likaletwa kituoni pale. Rangi halisi ya gari lile haikuwa ikijulikana, lilikuwa limeteketezwa vibaya na moto. Walichokifanya ni kwenda mbele ya gari lile kwa ajili ya kuangalia namba za gari, namba hazikuwa zikionekana.
Wakajaribu kufungua milango ya gari lile na kuanza kuangalia kwa ndani, kila kitu kilikuwa kimeteketezwa kwa moto, hali ikaonekana kuwa ngumu kumjua mmiliki halisi wa gari lile. Milango ikafungwa na kwenda nyuma ya gari, namba zilikuwa zikionekana japokuwa hazikuwa zikionekana vizuri.
“Mhhhh!” Polisi mmoja alisikika akiguna.
“Vipi tena? Mbona umeguna?”
“Hizi namba. Naona si za kawaida”
“Kwa nini umesema hivyo?”
“Namba hizi ni za serikali. Nafikiri gari hili litakuwa linamilikiwa na mtu mkubwa serikalini”
Uchunguzi zaidi ukaendelea na zaidi. Namba zile zikaandikwa katika faili na kisha kuanza kuwasiliana na vitengo mbalimbali vya serikali ili kugundua ni nani hasa alikuwa mmiliki wa gari lile. Ndani ya dakika arobaini, simu ikapigwa kituoni na pale na kuambiwa mmiliki halisi wa gari lile.
Kila polisi akaonekana kushtuka, hawakuamini kama waziri Boniface ndiye alikuwa mmiliki wa gari lile. Bado maswali yakaendelea zaidi na zaidi juu ya watu ambao walikuwa ndani ya gari lile. Kitu walichokifanya ni kuanza kuelekea katika nyumba ya mzee Boniface kumuulizia japokuwa walikuwa na uhakika kuwa wasingemkuta kutokana na kikao cha pili cha Bunge kuendelea mkoani Dodoma.
Wakafika nyumbani pale na kumuulizia, hawakumkuta mtu yeyote zaidi ya mfanyakazi wa ndani pamoja na mlinzi ambaye muda wote alikuwa getini akiendelea na ulinzi. Kitu walichokifanya ni kuchukua namba ya mzee Boniface na kisha kurudi ofisini na kumpigia.
                                                                     ******
Dominick akaonekana kuwa na amani japokuwa aliiona kutokukamilika. Alijilaza kitadani huku macho yake yakiangalia televisheni. Shauku yake kubwa ilikuwa ni kutaka kuiona taarifa ile ambayo aliamini ingempa furaha kwa wakati huo.
Muda wa taarifa ya habari ukawadia na habari ya kwanza kutangazwa ilikuwa ile ya gari la waziri kuchomwa moto na watoto wake pamoja na mkewe kuteketezwa kwa moto mpaka kifo. Habari ile ilikuwa inasikitisha na ilisomwa kwa majonzi makubwa lakini kwa Dominick hali ilionekana kuwa tofauti kabisa.
Uso wake ulikuwa umetawaliwa na tabasamu pana, muda wote alikuwa akikenua meno yake kwa furaha huku akishushia juisi nzito ya maembe. Moyo wake haukusikia hukumu kabisa, furaha ndio ambayo ilikwa imemtawala kuliko kitu chochote kile kwa wakati huo.
“Hivi ndivyo ninavyotaka. Nilivyoumia mimi basi nao waumie hivyo hivyo” Dominick alijisemea huku akibadilisha stesheni kuangalia taaarifa nyingine ya habari huku akitaka kuiona kwa mara nyingine habari ile ambayo ilikuwa ikimpa furaha kuiona.
“Ombeni ndiye anayefuata. Nitakwenda hivi hivi, zamu kwa zamu mpaka wote wamalizike” Dominick alisema huku tabasamu likiendelea kuwapo usoni mwake.
                                                                          *******
 Wabunge wote wakaonekana kuchanganyikiwa. Taarifa ya kuchomwa moto kwa gari la mbunge mwenzao ilipotangazwa, kila mtu akabaki kuwa na maswali kichwani. Hawakuamini kama Tanzania kungekuwa na mtu ambaye angekuwa na roho ya kufanya kitendo cha kikatili namna ile.
Kulichoma gari moto kwa makusudi huku watu wakiwa garini kilionekana kuwa kitendo cha kinyama ambacho hakikutakiwa kutokea katika nchi kama Tanzania. Mambo kama hayo yalitakiwa kusikika katka nchi nyingine, hasa katika nchi ambazo walipigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuuana kinyama.
Shughuli za Bunge zikaahirishwa, bunge likafungwa na kutolewa siku saba kwa ajili ya kuomboleza pamoja na mbunge mwenzao ambaye pia alikuwa waziri wa Mambo ya Utalii na Maliasili, mzee Boniface. Kila mbunge alikuwa na maoni tofauti juu mauaji yale ya kinyama. Kila walipokuwa wakiongea, maoni yao yalikuwa ni kuwataka mapolisi hasa katika kitengo cha upelelezi kufanya kazi mara moja ya kumtafuta na kumleta kwenye chombo cha dola mtu ambaye alihusika na mauaji yale.
Wazairi wa Miundo Mbinu, Bwana Ombeni akaonekana kuwa na wasiwasi zaidi, hakuonekana kuwa na amani, muda wote alikuwa mnyonge huku akionekana kuwa namawazo. Hakutaka kuendelea kubaki katika hali hiyo, moja kwa moja akampigia simu waziri mwenzake, Bwana Tumaini na kutaka kuonana nae katika hoteli ya Cat iliyokuwa Kariakoo.
Ndani ya dakika arobaini wakawa katika chumba kimoja ndani ya hoteli ile. Kila mmoja akaonekana kuchanganyikiwa, wasiwasi ukaonekana kuanza kuwashika. Mashaka makubwa yalikuwepo juu ya Dominick ambaye akaonekana kuwa nyuma ya mambo yote yale.
“Lakini si wale vijana walimuua?”
“Ndio. Kama aliuawa sasa ni nani ambaye anahusika na mauaji haya?”
Kila wakati walikuwa wakijiuliza juu ya muuaji ambaye aliiteketeza familia ya rafiki wao mkubwa. Akili zao zikaonekana kuchanganyikiwa, hawakuwa na uhakika kama mauaji yale alikuwa ameyafanya Dominick au mtu mwingine. Swali lao halikujibika vichwani mwao zaidi ya kupeana angalizo la kuzilinda familia zao.
“Unajua nae rafiki yetu alikua mtu wa matukio sana, unaweza kukuta kumbe kuna mtu aligombana nae na ndio maana aliamua kufanya kitu hiki” Bwana Tumaini alisema
“Ila inawezekana. Hata mimi nakuunga mkono”
Wakaachana siku hiyo na kila mtu kurudi nyumbani kwake ambako akajiandaa na kuelekea msibani nyumbani kwa mzee Boniface.
                                                              ******************
Idadi ya watu zaidi ya elfu moja ilikuwa imekusanyika katika eneo la nyumba kubwa ya mzee Boniface. Vilio vilikuwa vimetawala katika kila sehemu nyumbani hapo. Wakina mama walikuwa wakilia kupita kawaida, ndugu ambao walikuwa wametoka mkoani nao pia walishiriki vilivyo msiba huo.
Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, hakukuwa na utulivu msibani pale, wakina mama wengine walikuwa wakikimbia huku na kule huku wakiendelea kulia. Siku hiyo ilionekana kuwa siku ya majonzi makubwa maishani mwao, kuwapoteza watu watatu kwa mpigo lilionekana kuwa tukio kubwa ambalo halikuwahi kutokea katika ukoo wao.
Waandishi wa habari hawakuwa mbali, walikuwa wamekusanyika katika msiba huo huku kamera zao zikiwa mikononi wakijaribu kupiga picha na kuandika kila kitu ambacho walikiona kikifaa kuandikwa na kupigwa picha tayari kwa kuitoa habari ile katika magazet yao siku itakayofuata.
Mzee Boniface alikuwa amekaa pamoja na wazee wenzake, muda wote uso wake ulionyesha kuwa na huzuni japokuwa alikuwa akiongea kama hakupatwa na kitu chochote cha kuhuzunisha. Moyo wake ulikuwa ukimuuma zaidi kutokana na watoto wake kuuawa.
Kila siku alikuwa akiwalea katika maisha bora, hakutaka wapate matatizo yoyote yle kiasi ambacho alikuwa akiwalinda sana. Kwa sasa maisha yake yalikuwa kama katika kipindi ambacho hakuoa, mkewe hakuwa pamoja nae, mbaya zaidi, hata watoto wake hawakuwa pamoja nae pia.
Ving’ora vikaanza kusikika kwa mbali, watu wakaanza kuambiwa wakae vizuri mahali hapo. Zikaanza pikipiki mbili kuingia mahali hapo zikiongozana na magari manne. Polisi mmoja akaufungua mlango na kuelekea katika garijingine na kuufungua mlango, rais Emmanuel Moses akaanza kuteremka na moja kwa moja kuelekea kule wafiwa walipokuwa huku akiongozana na mkewe, Jaqueline Mlolo.
Walipomaliza kuwapa pole, mke wa rais, Jaqueline akaenda kukaa na wanawake wenzake huku rais, Emamanuel akienda kukaa pamoja na wanaume.
Wala haukupita muda mrefu, majeneza matatu yakaanza kuletwa mahali hapo. Vilio vikaanza kusikika zaidi na zaidi. Wakina mama na ndugu mbalimbali wa kike wakaanza kulia kwa uchungu huku wakigalagala chini. Mzee Boniface alikuwa akiongea kama kawaida, mara akanyamaza baada ya kuyaona majeneza ya familia yake. Machozi yakaanza kumlenga na hatimae kutiririka mashavuni mwake.
Moyo wake ulikuwa na maumivu makubwa kupita kiasi zaidi ya kuchomwa kwa msumari wa moto moyoni. Mchungaji akasimama na kuanza kuongea maneno machache. Miili ile haikutakiwa kuagwa kutokana na kuharibika vibaya, na kama ingeagwa kwa kuangaliwa sura ya mwisho, wanandugu wangeumia zaidi na zaidi.
Harakati nyingine zikaendelea na maiti kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni huku idadi ya watu ikiwa imeongezeka zaidi.
“Nitatumia gharama zangu zote kumpata muuaji huyu. Ni lazima nimpate na kumuua kwa mkono wangu mwenyewe” Mzee Boniface alijisemea katika kipindi ambacho maiti za familia yake zilipokuwa zikifukiwa kwa mchanga.
                                                               *******
Mapolisi walionekana kuchanganyikiwa kupita kawaida. Taarifa ya gari la waziri kuchomwa moto na mtu hasiyejulikana na kusababisha kuipoteza familia yake ilionekana kuwachanganya. Kamanda mkuu akawaita watu wote ambao walikuwa katika kitengo cha upelelezi na kuanza kuongea nao.
Kamanda mkuu wa polisi, Bwana Innocent Ngomale alionekana kuchanganyikiwa, muda wote alikuwa akikipiga kichwa chake. Tukio lile likaonekana kulitia doa jeshi la polisi kuliko tukio lolote ambalo liliwahi kutokea. Kuchomwa moto kwa nyumba ya Dominick na familia yake wala halikuangaliwa kama tukio kubwa, tukio la kuteketezwa familia ya Waziri wa wa Mali Asili na Utalii, Bwana Boniface ndilo lilionekana tukio kubwa kwa mapolisi.
Kila polisi alibaki akiwa na wasiwasi, siku hiyo kamanda Ngomale alionekana kukasirika kuliko siku zote. Akasimama kutoka kitini kwake na kuanza kuangalia darini, akakaa na kuanza kutapitisha macho yake usoni mwa kila polisi aliyekuwa mahali pale.
“Hii ina maana gani?” Kamanda Ngomale alianza kwa kuuliza swali. Hakukuwa na polisi yeyote ambaye alilijibu swali lile, kila mtu alibaki kimya.
“Ina maana hamfahamu hali hii ina maana gani?” Kamanda Ngomale aliuliza huku akionekana kuwa na hasira. Bado ukimya ukatawala mahali pale, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alijibu kitu chochote kile.
“Hii ina maanisha kwamba tumeshindwa kazi. Ulinzi umekuwa mdogo sana siku hizi. Zaidi ya yote, hii inaonyesha ni jinsi gani tulivyojisahau na kazi zetu” Kamanda Ngomale aliwaambia mapolisi.
Akachukua glasi ya maji ambayo ilikuwa mezani na kupiga fundo moja. Jasho tayari likuwa likimtoka, feni ambayo ilikuwa ikiendelea kupepea ndani ya chumba kile ilionekana kutokufanya kazi yake katika mwili wake. Akayarudisha macho yake katika uso wa kila mmoja na kuanza kuwaangalia tena kwa zamu.
“Muuaji anahitajika haraka sana. Nendeni mkajipange ninyi kama mapolisi wa kitengo cha upelelezi. Tunataka ndani ya mwezi huu muuaji apatikane hata kabla mambo mengine hayajatokea” Kamanda Ngomale aliwaambia.
Kikao kilipokwisha wala hakukuwa na muda wa kupoteza zaidi ya mipango kabambe kuanza kupangwa. Mpelelezi mashughuli ambaye alisomea shughuli za Upelelezi nchini Urusi, Emmanuel Bugabu ndiye ambaye akateuliwa kuanza kushughulikia suala la kumtafuta muuaji.
 Mpelelezi Emmanuel Bugabu alizaliwa miaka ishirini na tano iliyopita. Mara baada ya kujiunga na jeshi la polisi, akafanikiwa kuwa miongoni mwa vijana ambao walifuzu mafunzo ya kwenda kufundishwa upelelezi nchini Urusi.
Maisha nchi Urusi yalionekana kuwa magumu kwake, hali ya hewa ambayo alikuwatana nayo ilikuwa tofauti kabisa. Kila siku alikuwa akishinda na jaketi kubwa ambalo lilikuwa juu ya sweta lililokuwa juu ya fulana nzito ambayo ilikuwa juu ya ngozi yake.
Ingawa alikuwa akipata tabu kila siku, Bugabu akavulimilia mpaka pale alipomaliza elimu yake ambayo ilichukua miaka mitatu mpaka kumalizika. Aliporudi nchini Tanzania, Bugabu akaanza kufanya kazi ya upelelezi. Mauaji pamoja na uvamizi mbalimbali ulikuwa ukitokea, Bugabu ndiye ambaye alikuwa akipewa kazi ya kupeleleza. Wala hakuchukua muda mrefu, kila kitu kilikuwa kinakamilika na wahusika kukamatwa.
Sifa hizi ndizo alizokuwa nazo mpelelezi Bugabu, hakushindwa kazi hata moja, kila kazi ya upelelezi aliyopewa ilionekana kuwa ngumu kwa watu wengine lakini kwake yeye aliifanya kwa haraka sana. Kujituma kwake kazini pamoja na umakini mkubwa aliokuwa nao ndio ukapelekea shirika la upelelezi nchini Marekani, F.B.I (Fideral Bureau of Investigation) kutaka kuwa pamoja nao.
Serikali ya Tanzania ikakataa, haikutaka kumuachia Bugabu aende nchini Marekani, alihitajika kubaki nchini Tanzania kuendelea na kazi ya upelelezi. Bugabu alikuwa akiaminika na kila mtu, neno kushindwa kazi kwake wala halikuwepo, kila siku alikuwa akifanikiwa kwa kuwatia watu mikononi mwa vyombo vya dola. 
Kila siku kazi yake ilikuwa ni ya mafanikio makubwa, Umakini wake mkubwa ndio ambao ulikuwa ukimletea sifa za kukubalika katika kila idara za kipolisi kiasi ambacho mara kwa mara alikuwa akiitwa Ikulu kula chakula pamoja na rais. Emmanuel Bugabu huyu huyu ndiye ambaye alikuwa amepewa jukumu kubwa la kuhakikisha muuaji wa familia ya Waziri Boniface anakamatwa na kuletwa katika vyombo vya sheria.
“Nimefanya kazi kubwa tena kubwa mara mia ya hii, zote nikafanikiwa. Hii kazi niliyopewa ni ndogo sana, nitaifanikisha ndani ya mwezi mmoja tu” Bugabu alijisemea huku akionekana kutoa tabasamu la dhihaka.
                                                                  *********
Kila siku Dominick alikuwa mtu wa furaha, mauaji ambayo alikuwa ameyafanya wala hakuyasikitikia, kila siku kwake ilikuwa siku ya furaha. Alifuatilia kila kitu kwa karibu sana, kuonekana kwa mzee Boniface kuwa na hzuni hadi makaburini, kwa Dominick ndio ilikuwa furaha kubwa.
Kamwe moyo wake wala haukujuta, kila siku alikuwa akifurahia. Kila siku magazeti yalikuwa yakimfikia chumbani, picha mbalimbali za watu ambao walikuwa wakionekana kuhuzunika zlimfurahisha. Akaamua kumpigia simu Edmund na kumueleza juu ya kazi ambayo alikuwa ameifanya.
Muda wote Dominick alikuwa akizielezea waziwazi hasira ambazo alikuwa nazo moyoni, hakuona sababu ya watu wale watatu kuendelea kuwa na maisha ya furaha na wakati wao ndio walikuwa wameyarudisha nyuma maisha yake.
Mwezi mmoja ukapita, bado watanzania walikuwa na kumbukumbu vichwani mwao juu ya mauaji yaliokuwa yametokea. Walimhuzunikia sana waziri Boniface ambaye kila siku alikuwa akionekana kuwa na huzuni. Muuaji wa familia yake alikuwa akipokea lawama kila siku pasipo watu kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Dominick bado alijiona kuwa na kazi kubwa ya kufanya, alitaka kukamilisha kila kitu ambacho kilitakiwa kukamilishwa kwa mikono yake. Jina la waziri Ombeni ndilo ambalo lilikuwa likitawala kichwani mwake kwa wakati huo.
Alijiona kuwa na uwezo mkubwa wa kumuua lakini kabla hata hajafanya hivyo alihitaji mzee huyo aumie kwanza, alitamani ayapate maumivu kama ambayo alikuwa ameyapata katika kipindi cha nyuma kwa kuiteketeza familia yake.
Akachukua karatasi na kupanga mipango mbalimbali juu ya namna kazi yake ambavyo angeifanya. Kila hatua ambayo alikuwa ameipanga kwa ajili ya kufanya mauaji, aliiona kutokuwa nzuri. Aliziandika mbinu zaidi ya kumi katika karatasi yake na kisha kuichagua mbinu moja ambayo aliiona kufaa sana.
“Nitaiteka familia yake halafu nitaichoma moto” Dominck alisema.
Akachukua karatasi ambayo alikuwa ameandika namba kadhaa za simu na kuiangalia namba ya simu ya nyumbani kwa waziri Ombeni. Dominick akaichukua ile namba na kuiandika katika simu yake.
“Nitaanza na familia yake” Dominick alisema huku akitabasamu.
                                                                 *********
Kila siku baadhi ya watanzania walikuwa wakikasirika juu ya  tabia ya Bi Magdalena ambaye mara nyingi sana alikuwa akitumia fedha nyingi kwa ajili ya kusafiri sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufanya starehe. Bi Magdalena hakuonekana kuridhika na mumewe, hali ambayo ikamfany kuanza kutembea na vijana wadogo ambao damu zao zilikuwa zikichemka.
Hakuonekana kujitambua alikuwa nani na alikuwa na heshima gani, kitu ambcho alikuwa akikitaka ni kuifurahisha nafsi yake. Ngono na vijana ndio ikawa sehemu ya maisha yake. Mara kwa mara alikuwa akishinda klabu pamoja na vijana wadogo huku wakila na kunywa.
Jina lake lilikuwa kubwa katika kila klabu kubwa jijini Dar es Salaam. Umri wake ulikuwa ni miaka arobaini na mbili lakini kila siku maombi yake yalikuwa ni kutaka kurudishiwa miaka nyuma na kuwa kijana. Hakuutaka uzee, alijiona kuwa na nafasi kubwa ya kustarehe kwani fedha kwake haikuwa na tatizo lolote lile.
Ni mara chache sana alikuwa akilala nyumbani mpaka asubuhi, mara nyingi alikuwa akitoroka na kuelekea katika klabu za usiku. Bi Magdalena alikwenda sambamba na binti yake, Sara. Mara kwa mara walikuwa katika kumbi za starehe, mwanaume ambaye alikuwa akitembea na binti yake, Sara basi nae ilikuwa ni lazima atembee nae.
Pepo la ngono likaonekana kuikumba familia hiyo. Ukimuachilia mumewe, basi wao wawili ndio walikuwa wakiunda familia hiyo. Kila siku pombe na ngono ndio yalikuwa sehemu ya maisha yao. Walichukuana na kujirusha sehemu mbalimbali za starehe.
Kila starehe walitamani kufanya, pepo la ngono likaonekana kuwatawala zaidi hasa pale ambapo wakaamua kusafiri kwenda nchini Marekani ili tu kutafuta kampuni mbalimbali ambazo zilikuwa zikijihusisha na urekodiji wa filamu za ngono, nao walitaka kuigiza.
Kila kitu ambacho walitaka kukifanya kikajulikana, hai ambayo walitakiwa kurudi nchini Tanzania haraka iwezekanavyo. Hawakuonekana kukumbuka maisha ya tabu ambayo walikuwa wamepitia katika kipindi cha nyuma, wao walichokuwa wakikikumbuka ni kipindi ambacho walikuwa wameanza kupata fedha tu.
Familia hii ilionekana kuwa ya hatari hasa katika mchezo wa ngono, kila siku waliwaza ngono kiasi ambacho wakati wmwingine pasipo kufanya ngono, walijisikia wagonjwa. Hii ndio ilikuwa familia ya waziri wa Miundo Mbinu, Bwana Ombeni.
Kila siku Bwana Ombeni alionekana kuwa mtu wa matatizo, alijua kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea juu ya mke wake na mtoto wake lakini wala hakuwa akisema kitu chochote kile. Moyo wake ulikuwa katika mapenzi mazito juu ya mke wake. Alimpenda Bi Magdalena kuliko kitu chochote maishani mwake.
Kila siku Bi Magdalena alikuwa akilalamika juu ya uwezo wa mumewe kitandani, na hiyo ndio sababu iliyompelekea kuanza kutembea na vijana wadogo. Shughuli ambazo alikutana nazo kwa vijana wadogo ambao muda mwingi walikuwa wakitumia kuangalia picha za ngono zilimfanya kumsahau mumewe.
Bwana Ombeni alionekana kuchoka sana kitandani, hakuwa na nguvu zozote za kutosha kiasi ambacho muda mwingi Bi Magdalena alijiona kulala pamoja na mwanamke mwenzake. Fedha ambazo alikuwa nazo ndizo ambazo zilikuwa zikiwavutia vijana wengi kutembea nae.
Hakukuwa na kijana yeyote ambaye asingelala nae kwa usiku mmoja kwa malipo ya shilingi laki mbili. Kwa kila kijana ambaye alikuwa akitembelea klabu za usiku sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam basi ni lazima atakuwa akimfahamu mwanamke huyu.
Ingawa alikuwa akifanya mambo mengi pamoja na binti yake lakini wala hakikuandikwa kitu chochote magazetini. Kwanza waandishi wengi wa habari walikuwa wakiogopa, lakini wakati mwingine walikuwa wakipewa fedha nyingi kwa ajili ya kukaa kimya.
Picha zake na binti yake zilikuwa katika simu nyingi za vijana, tena zilikuwa picha ambazo walikuwa watupu au wakifanya ngono na watu mbalimbali. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kuzikana picha zile ambazo zilikuwa zimesambaa katika kila kona jijini Dar es Salaam.
Yeye ndiye alliyemshauri mumewe kufanya ufisadi wa shilingi bilioni kumi ambazo zilikuwa zikielea elea katika idara yake. Kila siku fedha zile zilikua zikitumika katika kuwahonga vijana ambao alikuwa akitembea nao. Hakuonekana kuwa na wasiwasi na fedha ambazo wala hakuwa amezitolea jasho, kila siku fedha kwake aliziona kustahlli kutumiwa kwa kuwa tu zilikuwa zimetengezwa kwa kazi hiyo.
“Utamuweza lakini?” Mwanaume mmoja aliyekuwa na misuli alimuuliza Dominick ambaye alikuwa amevaa miwani mikubwa iliyokuwa na rangi nyeusi.
“Kwa nini nisiweze. Ebu niangalie, unanionaje?” Dominick alimuuliza kijana yule.
Muziki bado ulikuwa ukiendelea katika klabu hiyo ya Raspinho, taa hafifu ndizo ambazo zilikuwa zikiwaka. Wanawake mbalimbali wazuri ambao kazi yao ilikuwa ni kujiuza walikuwa wamesimama pembeni huku wakijaribu kufanya matangazo kwa kila mvulana ambaye alikuwa akiwaangalia katika klabu ile.
“Nakuuliza tena..utaweza?” Mwanaume yule bado alikuwa akimuuliza Dominick.
“Nitaweza bwana. Mimi ndiye Maliki Mtanga. Nimezaliwa kwa ajili ya kufanya ngono tu” Dominick aliongea huku akijisifia.
“Kumbe umetokea Tanga”
“Ndio. Kule Handeni”
MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

BMW LA WEMA UTATA MTUPU, MKONGO ATAJWA!

$
0
0

Achana na lile gari aina ya Nissan Murano alilozawadiwa na mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, gari lingine aina ya BMW 545i aliloletewa Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ kwenye pati ya ‘bethidei’ yake ni utata mtupu na maswali kibao.
 
Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akiwa ndani ya Gari aina ya BMW 545i alilozawadiwa na meneja wake.
NYUMBANI KWA MADAM
Pati hiyo ambayo iliandika historia katika ulimwengu maridhawa wa mastaa iliangushwa nyumbani kwa mwanadada huyo, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar, wikiendi iliyopita ambapo alitimiza umri wa miaka 26.
Katika shughuli hiyo, waalikwa ambao sehemu kubwa walikuwa watu wenye majina, walikula na kunywa kuanzia mchana hadi usiku mnene.
NISSAN MURANO
Akiwa Marekani, Diamond alimuagiza mama yake, Sanura Kassim ‘Sandra’ apeleke gari aina ya Nissan Morano lenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 36 za madafu ikiwa ni zawadi ya jamaa huyo kwa mkewe huyo mtarajiwa.
Gari aina ya BMW 545i alilozawadiwa Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na meneja wake.
Alipoliona gari hilo, Wema alipigwa na butwaa huku akimshukuru Diamond ambaye kwa sasa amempachika jina la Chibu baada ya lile la Dangote ‘kueksipaya’.


MANENO KUNTU
Huku akiambatanisha na picha ya gari hilo, kupitia ukurasa wake wa Instagram alimwandikia Wema: “Nilitazama nikupe vingi huenda ingesaidia kukueleza ni kiasi gani napenda nikuone ukiwa umefurahi kwenye siku yako hii ya kuzaliwa...lakini tu sina uwezo huo Mumy...tafadhali pokea hicho kidogo hiki nilichojaliwa leo.”
BMW UTATA MTUPU!
Gari aina ya BMW alilokabidhiwa na meneja wake, Martin Kadinda ndilo habari ya mjini huku nyuma yake kukiwa na maswali kibao.
 
Martin Kadinda akionyesha funguo ya Gari aina ya BMW aliyomzawadia Wema.
MAMA WEMA AHOJI
Wa kwanza kuhoji alikuwa ni mama mzazi wa Wema, Mariam Sepetu ambaye alikataa kwamba Kadinda hawezi kutoa zawadi ya gari kama hilo hivyo minong’ono ikawa ni mingi.
Baada ya kuona hivyo, Kadinda alitoa kadi ya gari hilo lenye namba spesho za usajili ambapo jina la mmiliki lilisomeka Wema Sepetu.
MKONGO ATAJWA
Hata hivyo, pamoja na utetezi wake, maneno yaliendelea kusambaa kama moto wa kifuu kwamba nyuma ya gari kuna stori kubwa inakuja.
 
 Muonekano wa keki ya ‘bethidei’ ya Wema.
Minong’ono mingine ilikwenda mbele zaidi huku jamaa mmoja mfanyabiashara kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (Mkongomani) akitajwa kulinunua na kumpa Kadinda akakabidhi.
Baada ya kuona gari hilo lenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 56 za madafu zinaleta utata, kama kawaida yake, Kadinda alikimbilia kwenye ukurasa wake wa Instagram akaandika:
“....Gari hili linatokana na kazi ndogo tuzifanyazo na sapoti kubwa ya watu wanaotutakia mema. Peke yangu nisingeweza bila sapoti yao....”
 
Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akimlisha keki mama yake.
MSISITIZO
Akizungumza na gazeti hili juu ya sakata hilo, Kadinda alisema kwa msisitizo: “Ni mimi ndiye nimemnunulia Wema hilo gari.”
MASWALI
Huku Kadinda akisisitiza hivyo, waalikwa walibaki na maswali vichwani likiwemo lile linaloulizwa zaidi kwamba iweje yeye (Kadinda) aendeleshe gari la thamani ndogo aina ya Toyota Corola halafu ampe Wema BMW?
“Hapa pana kitu na kitakapobumburuka itakuwa soo, ni bora Kadinda angefunguka ukweli kuliko kuja kunyooshewa vidole baadaye, ngoja tusubiri,” alisikika mmoja wa mastaa walioalikwa (jina kapuni).
 
...Akimlisha keki mamamkwe wake.
MENGINE YATOKANAYO
Pati hiyo ya Wema iligawanyika mara mbili ambapo ya kwanza ilianza saa 6:00 mchana hadi saa 12:00 huku nyingine iliyohusisha watu maarufu ikianza baadaye hadi ‘kokoriko’.
KEKI 69 MEZANI
Katika hali isiyo ya kawaida, sherehe hiyo ilikuwa na keki zipatazo 69 ambazo zililetwa na baadhi ya mastaa ambao walihudhuria sherehe hiyo huku kukiwa na vinywaji vya kufa mtu (wiski tu), loko bia tupa kule.
 
...Akimlisha keki Jokate.
NDAFU
Kwa upande wa nyama kulikuwa ndafu mzima ambaye watu walimtafuta hadi wakasaza.

MAMA DIAMOND AMTANGAZA RASMI MKWEWE  
Katika sherehe hiyo, mama Diamond alipopewa kipaza sauti ‘maiki’ ili anene chochote alisema kuwa Wema ni mkwe wake wa halali na kwamba anampenda hivyo asiwe na wasiwasi kwani hakuna mkwe mwingine atayatokea zaidi yake.
 
Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akifungua shampeni kwaajili ya shughuli hiyo.
“Jamani huyu ndiye mkwe wangu, Mrs Chibu (Diamond) ndiye mkwe wangu hasaaa...,” alisema mama Chibu huku watu wakishangilia.
MILIONI 10
Kwa mujibu wa Kadinda, shughuli hiyo iligharimu zaidi ya Sh. milioni 10 hadi kukamilika na kuonekana ya tofauti na pati nyingine za mastaa Bongo.
 
...Akiwakaribisha ndugu jamaa na marafiki katika shughuli hiyo.
AMWAGIWA NOTI
Ulipofika muda wa kutunzwa zawadi, watu walijitokeza kumtunza Wema fedha ambazo hazikuweza kupatikana kiasi chake mara moja huku staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiweka rekodi kwa kumwaga ‘minoti’ mingi katika hafla hiyo.
Imeandaliwa na Imelda Mtema, Shani Ramadhan na Mayasa Mariwata.
(CRREDIT: GLOBAL PUBLISHERS, RISASI JUMATANO)

MEYA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MKEWE

$
0
0

Daniel Crespo enzi za uhai wake.
MEYA wa Bell Gardens, California nchini Marekani, Daniel Crespo ameuawa jana kwa kupigwa risasi na mkewe nyumbani kwake.
Crespo alipigwa risasi wakati wa mzozo baina yake na mkewe ambapo mtoto wao wa kiume mwenye miaka 19 alijaribu kuingilia na kusukumwa na baba yake ndipo mtuhumiwa alipofyatua risasi.
Marehemu alipoteza maisha akiwa njiani kupelekwa katika hospitali iliyo karibu na nyumbani kwake.
Mke wa marehemu,  Levette Crespo anashikiliwa na polisi kwa tukio hilo.

SHEHE: AUNT EZEKIEL HANA NDOA

$
0
0
 
Stori: Gladness Mallya na Chande Abdallah 
SHEIKH Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa ameweka wazi kuwa msanii nyota wa filamu, Aunt Ezekiel ambaye aliolewa na Sunday Demonte hana ndoa kutokana na kukaa mbali na mumewe kwa zaidi ya miezi sita.
 
Sheikh Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa akizungumza jambo.
“Hakuna ndoa kati ya mtu yeyote ambaye amezidi miezi 6 bila kukutana na mumewe kwa mujibu wa dini ya kiislamu.
 
Msanii nyota wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel
“Kwa kawaida mwanamke ambaye hajakutana na mumewe kwa miezi 6 au zaidi baada ya ndoa yao, hupaswa kwenda mara moja Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) kulalamika na hatimaye kudai talaka, ikiwa mwanamke ameridhika na hali hiyo, naye akaamua kukaa kimya huku akifanya mambo yake na kuanzisha uhusiano na wanaume wengine maana yake amejitoa mwenyewe kwenye mamlaka ya mumewe, hivyo hapo kunakuwa hakuna ndoa tena,”alisema Shehe.

ARSENAL YAUA, WELBECK AGONGA HAT-TRICK

$
0
0

Mshambuliaji Danny Welbeck akishangilia baada ya kupiga 'hat-trick'.
 
Alexis Sanchez akiifungia Arsenal bao la tatu dhidi ya Galatasaray.
 
Welbeck akitupia bao la nne.
 
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ametimiza miaka 18 akiwa meneja wa klabu hiyo.
KLABU ya Arsenal imetoa kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya Galatasaray kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopigwa Uwanja wa Emirates jijini London usiku huu.
Mshambuliaji Danny Welbeck ametupia kambani mabao matatu 'hat-trick' huku bao la tatu likiwekwa kimianai na Alexis Sanchez. Katika mtanange huo, kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny alizawadiwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mshambuliaji wa Galatasaray, Burak Yilmaz.
Ushindi wa leo wa Arsenal umeongeza furaha kwa Meneja wa timu hiyo, Arsene Wenger aliyetimiza miaka 18 akiwa kocha wa klabu hiyo leo.
VIKOSI:
Arsenal: Szczesny, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Cazorla, Ozil (Wilshere 77), Sanchez (Ospina 62), Oxlade-Chamberlain (Rosicky 68), Welbeck.
Waliokuwa benchi: Coquelin, Bellerin, Campbell, Podolski.
Galatasaray: Muslera, Chedjou, Felipe Melo, Semih Kaya, Veysel (Bulut 68), Yekta (Altintop 46), Dzemaili, Telles, Sneijder, Pandev (Bruma 68), Burak Yılmaz.
Waliokuwa benchi: Bolat, Balta, Adin, Camdal.

Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>