MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com“Kuna nini? Umeona nini?” Kijana mwingine alimuuliza.
“Nendeni mkaangalie wenyewe. Inatisha”
“Inatisha? Inatisha nini?”
“Nyie kaangalieni tu”
Vijana wengine wakaelekea katika gari lile na kuchungulia ndani. Miili mitatu ilikuwa ikionekana vizuri huku ikiwa imeteketea kwa moto na huku ikitoa moshi. Simu zikaanza kupigwa katika kituo cha polisi cha Oysterbay ili kuwaomba mapolisi kufika mahali hapo haraka iwezekanavyo.
Watu ambao walikusanyika mahali pale walikuwa watano lakini kadri dakika zilivyozidi kwenda na ndivyo watu walivyozidi kuongezeka mpaka kufikia watu zaidi ya mia mbili. Kila aliyefika mahali pale na kuangalia miili ya watu wale, alishikw kichwa kwa huzuni.
Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walivyozidi kuongezeka zaidi na zaidi. Watu ambao walikuwa wakipita katika barabara ya lami wakasimamisha magari yao na kuanza kuelekea pale ambapo gari lile lilipokuwa limeteketezwa kwa moto.
Zilipita dakika thelathini na ndipo waandishi wa habari wakafika katika eneo la tukio hata kabla ya mapolisi. Wakaanza kupiga picha kila kitu kilichokuwa kinaendelea mahali pale huku wakichukua muda wao kuwahoji watu ambao walikuwa katika eneo hilo. Kila aliyekuwa akihojiwa, alikuwa akiongea kwa uchungu, wakinamama walishindwa kujizuia, muda wote walikuwa wakilia.
Mapolisi wakafika mahali hapo na kuwaomba watu kusogea mbali na gari lile, wakaingia ndani na kuanza kuitoa miili ile ya Bi Upendo na watoto wake na kisha kuiweka katika gari lao aina ya Defender. Hawakutaka kubaki mahali hapo, safari ya kuelekea hospitalini ikaanza.
“Hivi ilikuwaje?” Mwandishi mmoja wa habari alimuuliza kijana mmoja ambaye alikuwa mtu wa kwanza kufika mahali hapo.
“Yaani toka gari hili lilipokuwa linafika mahali hapa nilikuwa naliona japo nilikuwa mbali sana” Kijana yule alisema hali iliyowafanya watu wengine kumzunguka kutaka kujua ni kitu gani kilitokea.
“Sikulitilia shaka yoyote ile, nikamuona jamaa mmoja ambaye alikuwa amevaa kofia kubwa ya Malboro akiteremka huku akiwa na chombo kidogo, sijui kilikuwa kidumu kile…wala sikukiona vizuri. Nikamuona akianza kulimwagia gari hili. Nafikiri ilikuwa petroli japokuwa mimi nilifikiri maji huku nikidhani alikuwa akiliosha gari lake.” Kijana yule aliwaambia.
“Eheee..!! Ikawaje sasa?”
“Baaada ya muda nikaamua kwenda kuogelea kama kawaida yangu. Ile napiga mbizi mbili tatu, nikashangaa kuuona moto mkubwa ukiwaka. Unajua nilishtuka sana, nikajikuta nikitoka baharini na kuanza kuja huku” Kijana yule alielezea huku kila mtu akibaki kimya akimsikiliza.
“Kwa hiyo mtu mwenyewe hukumuona tena? Au alisimama pembeni?”
Sikumuona. Yaani sijui alikimbilia wapi”
*******
Wabunge wengi walikuwa Bungeni wakisiliza kwa makini sana namna ambavyo Bajeti ya taifa ilivyokuwa ikisomwa. Muda wote ambao bajeti ilikuwa ikisomwa, mawaziri ambao walijiita BoT walikuwa wakikenua kila wakati, vifo vya watu wawili vilionekana kuwafurahisha sana.
Mzee Boniface akahisi simu yake ikitetemeka mfukoni, akaitoa na kuanza kuangalia namba ya mpigaji. Namba ilikuwa ngeni kabisa machoni mwake. Akatamani kuipuuzia lakini akaamua kuanza kupiga hatua kuelekea nje ili kujua ni nani ambaye alikuwa akimpigia simu.
“Haloooo…!” Mzee Boniface aliita.
“Haloooo…Naongea na mheshimiwa waziri hapo?” Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.
“Ndio. Wewe ni nani na sijui nikusaidie nini?”
“Kuna tatizo mzee. Nakuomba uje Dar es Salaam mara moja”
“Tatizo? Tatizo gani ambalo mpaka mnataka mimi nije huko?” Mzee Bonifasi aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.
“Wewe njoo mzee. Tena ikiwezekana, njoo sasa hivi” Sauti ya upande wa pili ilisema.
“Hilo si tatizo. Nikija hapo Dar es Salaam nielekee wapi sasa?” Mzee Boniface aliuliza.
“Njoo katika hospitali ya Taifa”
“Hospitali ya Taifa?”
“Ndio. Fanya haraka sana” Sauti ya upande wa pili ilisikika na kisha simu kukatwa.
Mzee Boniface akaonekana kuchanganyikiwa, neno hospitali ya Taifa ndio ambalo lilionekana kumtisha zaidi. Tayari akaona kuna tatizo lilikuwa limetokea, hivyo alichokifanya ni kumpigia simu mkewe, simu haikuwa ikipatikana.
Mzee Bonifasi akaonekana kuchanganyikiwa. Akapiga katika simu ya mezani, simu ikaanza kuita na baada ya muda ikapokelewa na mfanyakazi wake wa ndani. Tayari kijasho chembamba kilikuwa kinamtoka, akajihisi kuchanganyikiwa kupita kawaida.
“Hallooo…! Mage, mama yako yupo hapo?” Mzee Bniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hayupo. Ametoka”
“Ametoka? Ameelekea wapi asubuhi yote hii?”
“Amewapeleka watoto shule pamoja na dereva”
“Inakuwaje leo amewapeleka shule? Si huwa anawapeleka dereva peke yake?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Hata mimi sifahamu”
“Hakuna tatizo lolote lililotokea hapo nyumbani?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa zaidi.
“Mmmmm…!! Wala hakuna” Mage alisikika akijibu.
“Sawa. Nakuja huko huko”
“Sawa”
Mzee Boniface akaonekana kuchanganyikiwa zaidi. Hakuwa na sababu ya kuaga, moja kwa moja akampigia simu dereva wake ambaye alikuja na kumtaka kumpeleka uwanja wa ndege. Mwili wote ulikuwa ukimtetemeka, jasho ambalo lilikuwa likimtoka lilimfanya shati lake lote kulowana kana kwamba alimwagiwa ndoo ya maji.
“Mbona unaonekana tofauti leo?” Dereva alimuuliza.
“Wewe twende kwanza” Mzee Boniface alimwambia dereva.
Wala hazikupita dakika nyingi, wakafika uwanja wa ndege. Tiketi ya ndege ikakatwa kwa haraka sana. Akaichukua tiketi ile ya ndege na kuanza kuiangalia. Akaamua kumrudia dereva ambaye alikuwa nje ya jengo la uwanja wa ndege.
“Hivi hauwezi kuendesha gari kwa mwendo wa kasi. Yaani baada ya saa moja tuwe tumefika Dar es Salaam?” Mzee Boniface alimuuliza dereva wake.
“Ndani ya saa moja?” Dereva aliuliza huku akionekana kushtuka.
“Sasa unaniuliza ina maana haujanisikia au?”
“Mheshimiwa haiwezekani. Labda kama hapa ingekuwa Morogoro sawa. Ila kumbuka hapa ni Dodoma” Dereva alimwambia mzee Boniface
“Lakini bado haujanijibu swali langu”
“Nimekwishakujibu mzee kwamba haiwezekani. Kutoka hapa Dodoma hadi Dar es Salaam ni mbali sana” Dereva alimwambia mzee Boniface.
Mzee Boniface akabaki kimya. Wasiwasi ukazidi kuongezeka moyoni mwake. Simu ambayo alipigiwa katika kipindi kichache kilichopita tayari ilikuwa imemchanganya. Furaha yote aliyokuwa nayo juu ya kifo cha Dominick na Saida ikapotea moyoni mwake.
Kadri muda ulivyozidi kusonga mbele na ndivyo wasiwasi ulivyozidi kumpanda zaidi. Alibaki katika kiti cha gari lake huku akiwa kimya, mawazo yake yalikuwa yakifikiria mbali sana kwa wakati huo. Kwa haraka sana, akaichukua simu yake na kuanza kubonyeza namba za simu yake ya mezani iliyokuwa nyumbani kwake, simu ikaanza kuita, baada ya muda, Mage akaipokea.
“Kuna kitu chochote kilichoendelea huko? Mzee Boniface alianza kuuliza swali.
“Kitu gani?” Sauti ya Mage ilisikika ikiuliza.
“Chochote kile”
“Hapana. Hakuna chochote kile?”
“Hakuna”
“Yaani hata mtu kuja kuniulizia?”
“Aaaah..! Nimekumbuka. Walikuja mapolisi hapa” Mage alimwambia mzee Boniface.
“Wamesemaje?”
“Hawakuniambia kitu chochote kile zaidi ya kukuulizia wewe”
“Sawa” Mzee Boniface alisema na kukata simu.
Akili yake ikachanganyikiwa zaidi. Dereva hakutaka kuuliza kitu chochote kile, alibaki kimya akimwangalia mzee Boniface alivyochanganyikiwa.
Dakika zilizidi kwenda mbele huku sekunde zikienda katika kasi yak kama kawaida. Saa la kwanza likakatika, na hatimae saa la pili kutimia. Abiria wote wakaitwa katika ndege ambayo walikuwa wakihitajika tayari kwa safari ya kuelekea Dar es Salaam kwa kupitia Morogoro.
Kadri ndege livyokuwa ikisafiri angani kuelekea Dar es Salaam na ndivyo ambavyo wasiwasi wake ulivyozidi kuongezeka zaidi. Amani ikazidi kupotea moyoni mwake. Hakuwa na hamu ya kula kitu chochote kile, kila alipopitishiwa vyakula mbalimbali, alikataa kula, mbaya zaidi, hata maji hakutaka kunywa.
Ndege aliiona ikiendelea na safari kwa mwendo wa taratibu sana, alitamani afike haraka Dar es Salaam na kuelekea katika hositali ya taifa. Safari iliendelea zaidi na zaidi na hatimae kuingia katika uwanja wa ndege saa nne sita asubuhi.
Hakutaka kuchelewa kubaki uwanjani hapo, kwa haraka haraka huku akionekana kuchanganyikiwa, akachomoka na kuelekea nje ya jengo la uwanja ule ambako akachukua taksi.
“Twende Muhimbili” Alimwambia dereva taksi ambaye alikuwa akimshangaa.
“Elfu kumi na t….”
“Wewe twende bwana. Mbona unataka kunichelewesha” Mzee Boniface alimwambia dereva taksi ambaye kwa haraka sana, akaliwasha gari na kuondoka uwanjani hapo.
Mzee Boniface alimuona dereva taksi akiendesha kwa mwendo wa taratibu sana kiasi ambacho akatamani kushikilia usukani yeye mwenyewe. Kila wakati alikuwa akimuhamasisha dereva kuongeza kasi.
Mpaka wanafika katika hospitali ya Muhimbili, walitumia dakika arobaini na saba njiani. Akamlipa dereva kiasi chake cha fedha alichokihitaji na kwa haraka haraka akateremka na kuanza kuelekea katika eneo la hospitali ile.
Ingawa watu wengi walikuwa wamezuiliwa kutokana na wakati ule kutokuwa muda wa kuwaona wagonjwa, lakini kutokana na kuwa na nyadhifa kubwa serikalini, mzee Boniface akaruhusiwa kupita. Watu wote ambao walikuwa mahali hapo walikuwa wakimshangaa kwa jinsi alivyokuwa akitokwa jasho.
Kila mmoja aliyemuona mzee Boniface alikuwa akijiuliza juu ya hali ambayo alikuwa nayo. Kila mtu alifahamu kuwa kwa wakati huo alihitajika kuwa Bungeni kuwawakilisha wananchi wake, lakini kwa nini wakati ule alikuwa hospitalini, tena akionekana kuwa na haraka huu uso wake ukiwa umejaa wasiwasi?
“Mheshimiwa…!” Alisikia akiitwa. Kwa haraka haraka akageuka, macho yake yakagongana na umati wa mapolisi pamoja na baadhi ya manesi ambao walikuwa wamesimama nje ya chumba kimoja kilichoandikwa Monchwari kwa nje. Mzee Boniface akazidi kushikwa na wasiwasi zaidi, nyuso za watu wale zilikuwa zimejawa na huzuni kupita kawaida.
“Kuna nini? Niambieni kuna nini?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Twende kwanza ofisini” Daktari alimwambia na wote kuanza kwenda katika ofisi ya daktari huku baadhi ya mapolisi wakiwafuata.
Mzunguko wa damu mwilini mwake ulikuwa mkubwa, mapigo ya moyo yalikuwa yakimdunda kupita kiasi. Walipoifikia ofisi ile moja kwa moja wakaingia ndani na kutakiwa kukaa kitini. Macho yake yalikuwa yakimwangalia daktari kwa wasiwasi kupita kawaida.
“Kuna nini daktari? Mbona hamtaki kuniambia?” Mzee Boniface aliuliza huku akionekana kukasirika.
“Kuna habari mbaya. Ila kwa sababu wewe ni mwanaume, ningependa ujipe moyo wa ushujaa kuisikia habari hii” Daktari alimwambia mzee Boniface.
“Mbona unazunguka zunguka? Niambie kwanza” Mzee Boniface alimwambia daktari huku akionekana kuwa na hasira zaidi.
“Kuhusu familia yako”
“Familia yangu? Imefanya nini?”
“Imeteketezwa kwa moto. Mkeo na watoto wako wamefariki kwa kuunguzwa na moto vibaya” Daktari alimwambia mzee Boniface.
Mzee Boniface akaiona presha ikipanda kwa kasi. Akabaki ameganda kna kwamba alikuwa akijitayarisha kupigwa picha. Akailalia meza ya daktari, ghafla akaanguka chini kama mzigo. Hakujua kitu chochote kilichoendelea baada ya hapo. Alionekana kuwa katika hali ya nusu kifo.
*******
Miili ilikuwa imeteketea vibaya kupita kawaida. Kila polisi ambaye alikuwa akiiangalia alibaki kushika tama kwa huzuni. Haikuwa rahisi hata kidogo kuwatambua watu wale ni wakina nani. Walikuwa wakitisha kupita kawaida. Picha ambayo ilikuwa ikionekana mbele yao, ilikuwa ni picha mbaya ambayo ilikuwa ikiwasisimua kupita kawaida.
“Hali inatisha” Polisi mmoja alijikuta akisema.
Gari lile likaenda moja kwa moja hadi katika hospitalini ambacko machela zikaletwa na miili kupakizwa huku ikifunnikwa shuka. Machela zikasukumwa moja kwa moja mpaka katika chumba kikubwa cha kuhifadhia maiti. Mapolisi walibaki nje wakisubiri kuona ni kitu gani kingeendelea mahali hapo.
Mara mzee mmoja ambaye alikuwa na vazi refu jeupe akaanza kuelekea kule waliposimama na kisha kuingia ndani ya chumba kile. Wala hazikupita dakika hata tano, akatoka huku uso wake ukiwa umejawa na huzuni kupita kawaida.
“Kuna ndugu zao wowote mmekuja nao?” Dokta aliwauliza mapolisi.
“Hapana”
“Sasa hata majirani zao mmeshindwa kuja nao? Au walikuwa wanaishi porini?” Dokta aliuliza huku mawazo yake yakimpelekea kuwa ni ajali ya nyumba kuungua ndio ambayo ilikuwa imetokea.
“Bora ingekuwa hivyo daktari. Hawa watu wamechomwa moto wakiwa ndani ya gari, gari lenyewe lilikuwa limetelekezwa ufukweni” Polisi mmoja alimwambia daktari ambaye akaonekana kushtuka.
“Wamechomwa moto ndani ya gari?” Daktari aliuliza kwa mshtuko huku akionekana kutokuamini.
“Ndio”
Mapolisi hawakutaka kuendelea kubaki hospitalini hapo, bado walijiona kuwa na kazi ambayo ilibakia kwa ajili ya kumjua mmiliki wa gari lile. Moja kwa moja wakaenda katika kituo chao cha Oysterbay na kisha kuagiza gari lile lililoteketezwa kwa moto kuletwa kituoni pale.
Dakika arobaini na tano gari lile likaletwa kituoni pale. Rangi halisi ya gari lile haikuwa ikijulikana, lilikuwa limeteketezwa vibaya na moto. Walichokifanya ni kwenda mbele ya gari lile kwa ajili ya kuangalia namba za gari, namba hazikuwa zikionekana.
Wakajaribu kufungua milango ya gari lile na kuanza kuangalia kwa ndani, kila kitu kilikuwa kimeteketezwa kwa moto, hali ikaonekana kuwa ngumu kumjua mmiliki halisi wa gari lile. Milango ikafungwa na kwenda nyuma ya gari, namba zilikuwa zikionekana japokuwa hazikuwa zikionekana vizuri.
“Mhhhh!” Polisi mmoja alisikika akiguna.
“Vipi tena? Mbona umeguna?”
“Hizi namba. Naona si za kawaida”
“Kwa nini umesema hivyo?”
“Namba hizi ni za serikali. Nafikiri gari hili litakuwa linamilikiwa na mtu mkubwa serikalini”
Uchunguzi zaidi ukaendelea na zaidi. Namba zile zikaandikwa katika faili na kisha kuanza kuwasiliana na vitengo mbalimbali vya serikali ili kugundua ni nani hasa alikuwa mmiliki wa gari lile. Ndani ya dakika arobaini, simu ikapigwa kituoni na pale na kuambiwa mmiliki halisi wa gari lile.
Kila polisi akaonekana kushtuka, hawakuamini kama waziri Boniface ndiye alikuwa mmiliki wa gari lile. Bado maswali yakaendelea zaidi na zaidi juu ya watu ambao walikuwa ndani ya gari lile. Kitu walichokifanya ni kuanza kuelekea katika nyumba ya mzee Boniface kumuulizia japokuwa walikuwa na uhakika kuwa wasingemkuta kutokana na kikao cha pili cha Bunge kuendelea mkoani Dodoma.
Wakafika nyumbani pale na kumuulizia, hawakumkuta mtu yeyote zaidi ya mfanyakazi wa ndani pamoja na mlinzi ambaye muda wote alikuwa getini akiendelea na ulinzi. Kitu walichokifanya ni kuchukua namba ya mzee Boniface na kisha kurudi ofisini na kumpigia.
******
Dominick akaonekana kuwa na amani japokuwa aliiona kutokukamilika. Alijilaza kitadani huku macho yake yakiangalia televisheni. Shauku yake kubwa ilikuwa ni kutaka kuiona taarifa ile ambayo aliamini ingempa furaha kwa wakati huo.
Muda wa taarifa ya habari ukawadia na habari ya kwanza kutangazwa ilikuwa ile ya gari la waziri kuchomwa moto na watoto wake pamoja na mkewe kuteketezwa kwa moto mpaka kifo. Habari ile ilikuwa inasikitisha na ilisomwa kwa majonzi makubwa lakini kwa Dominick hali ilionekana kuwa tofauti kabisa.
Uso wake ulikuwa umetawaliwa na tabasamu pana, muda wote alikuwa akikenua meno yake kwa furaha huku akishushia juisi nzito ya maembe. Moyo wake haukusikia hukumu kabisa, furaha ndio ambayo ilikwa imemtawala kuliko kitu chochote kile kwa wakati huo.
“Hivi ndivyo ninavyotaka. Nilivyoumia mimi basi nao waumie hivyo hivyo” Dominick alijisemea huku akibadilisha stesheni kuangalia taaarifa nyingine ya habari huku akitaka kuiona kwa mara nyingine habari ile ambayo ilikuwa ikimpa furaha kuiona.
“Ombeni ndiye anayefuata. Nitakwenda hivi hivi, zamu kwa zamu mpaka wote wamalizike” Dominick alisema huku tabasamu likiendelea kuwapo usoni mwake.
*******
Wabunge wote wakaonekana kuchanganyikiwa. Taarifa ya kuchomwa moto kwa gari la mbunge mwenzao ilipotangazwa, kila mtu akabaki kuwa na maswali kichwani. Hawakuamini kama Tanzania kungekuwa na mtu ambaye angekuwa na roho ya kufanya kitendo cha kikatili namna ile.
Kulichoma gari moto kwa makusudi huku watu wakiwa garini kilionekana kuwa kitendo cha kinyama ambacho hakikutakiwa kutokea katika nchi kama Tanzania. Mambo kama hayo yalitakiwa kusikika katka nchi nyingine, hasa katika nchi ambazo walipigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuuana kinyama.
Shughuli za Bunge zikaahirishwa, bunge likafungwa na kutolewa siku saba kwa ajili ya kuomboleza pamoja na mbunge mwenzao ambaye pia alikuwa waziri wa Mambo ya Utalii na Maliasili, mzee Boniface. Kila mbunge alikuwa na maoni tofauti juu mauaji yale ya kinyama. Kila walipokuwa wakiongea, maoni yao yalikuwa ni kuwataka mapolisi hasa katika kitengo cha upelelezi kufanya kazi mara moja ya kumtafuta na kumleta kwenye chombo cha dola mtu ambaye alihusika na mauaji yale.
Wazairi wa Miundo Mbinu, Bwana Ombeni akaonekana kuwa na wasiwasi zaidi, hakuonekana kuwa na amani, muda wote alikuwa mnyonge huku akionekana kuwa namawazo. Hakutaka kuendelea kubaki katika hali hiyo, moja kwa moja akampigia simu waziri mwenzake, Bwana Tumaini na kutaka kuonana nae katika hoteli ya Cat iliyokuwa Kariakoo.
Ndani ya dakika arobaini wakawa katika chumba kimoja ndani ya hoteli ile. Kila mmoja akaonekana kuchanganyikiwa, wasiwasi ukaonekana kuanza kuwashika. Mashaka makubwa yalikuwepo juu ya Dominick ambaye akaonekana kuwa nyuma ya mambo yote yale.
“Lakini si wale vijana walimuua?”
“Ndio. Kama aliuawa sasa ni nani ambaye anahusika na mauaji haya?”
Kila wakati walikuwa wakijiuliza juu ya muuaji ambaye aliiteketeza familia ya rafiki wao mkubwa. Akili zao zikaonekana kuchanganyikiwa, hawakuwa na uhakika kama mauaji yale alikuwa ameyafanya Dominick au mtu mwingine. Swali lao halikujibika vichwani mwao zaidi ya kupeana angalizo la kuzilinda familia zao.
“Unajua nae rafiki yetu alikua mtu wa matukio sana, unaweza kukuta kumbe kuna mtu aligombana nae na ndio maana aliamua kufanya kitu hiki” Bwana Tumaini alisema
“Ila inawezekana. Hata mimi nakuunga mkono”
Wakaachana siku hiyo na kila mtu kurudi nyumbani kwake ambako akajiandaa na kuelekea msibani nyumbani kwa mzee Boniface.
******************
Idadi ya watu zaidi ya elfu moja ilikuwa imekusanyika katika eneo la nyumba kubwa ya mzee Boniface. Vilio vilikuwa vimetawala katika kila sehemu nyumbani hapo. Wakina mama walikuwa wakilia kupita kawaida, ndugu ambao walikuwa wametoka mkoani nao pia walishiriki vilivyo msiba huo.
Kila mtu alionekana kuwa na huzuni, hakukuwa na utulivu msibani pale, wakina mama wengine walikuwa wakikimbia huku na kule huku wakiendelea kulia. Siku hiyo ilionekana kuwa siku ya majonzi makubwa maishani mwao, kuwapoteza watu watatu kwa mpigo lilionekana kuwa tukio kubwa ambalo halikuwahi kutokea katika ukoo wao.
Waandishi wa habari hawakuwa mbali, walikuwa wamekusanyika katika msiba huo huku kamera zao zikiwa mikononi wakijaribu kupiga picha na kuandika kila kitu ambacho walikiona kikifaa kuandikwa na kupigwa picha tayari kwa kuitoa habari ile katika magazet yao siku itakayofuata.
Mzee Boniface alikuwa amekaa pamoja na wazee wenzake, muda wote uso wake ulionyesha kuwa na huzuni japokuwa alikuwa akiongea kama hakupatwa na kitu chochote cha kuhuzunisha. Moyo wake ulikuwa ukimuuma zaidi kutokana na watoto wake kuuawa.
Kila siku alikuwa akiwalea katika maisha bora, hakutaka wapate matatizo yoyote yle kiasi ambacho alikuwa akiwalinda sana. Kwa sasa maisha yake yalikuwa kama katika kipindi ambacho hakuoa, mkewe hakuwa pamoja nae, mbaya zaidi, hata watoto wake hawakuwa pamoja nae pia.
Ving’ora vikaanza kusikika kwa mbali, watu wakaanza kuambiwa wakae vizuri mahali hapo. Zikaanza pikipiki mbili kuingia mahali hapo zikiongozana na magari manne. Polisi mmoja akaufungua mlango na kuelekea katika garijingine na kuufungua mlango, rais Emmanuel Moses akaanza kuteremka na moja kwa moja kuelekea kule wafiwa walipokuwa huku akiongozana na mkewe, Jaqueline Mlolo.
Walipomaliza kuwapa pole, mke wa rais, Jaqueline akaenda kukaa na wanawake wenzake huku rais, Emamanuel akienda kukaa pamoja na wanaume.
Wala haukupita muda mrefu, majeneza matatu yakaanza kuletwa mahali hapo. Vilio vikaanza kusikika zaidi na zaidi. Wakina mama na ndugu mbalimbali wa kike wakaanza kulia kwa uchungu huku wakigalagala chini. Mzee Boniface alikuwa akiongea kama kawaida, mara akanyamaza baada ya kuyaona majeneza ya familia yake. Machozi yakaanza kumlenga na hatimae kutiririka mashavuni mwake.
Moyo wake ulikuwa na maumivu makubwa kupita kiasi zaidi ya kuchomwa kwa msumari wa moto moyoni. Mchungaji akasimama na kuanza kuongea maneno machache. Miili ile haikutakiwa kuagwa kutokana na kuharibika vibaya, na kama ingeagwa kwa kuangaliwa sura ya mwisho, wanandugu wangeumia zaidi na zaidi.
Harakati nyingine zikaendelea na maiti kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni huku idadi ya watu ikiwa imeongezeka zaidi.
“Nitatumia gharama zangu zote kumpata muuaji huyu. Ni lazima nimpate na kumuua kwa mkono wangu mwenyewe” Mzee Boniface alijisemea katika kipindi ambacho maiti za familia yake zilipokuwa zikifukiwa kwa mchanga.
*******
Mapolisi walionekana kuchanganyikiwa kupita kawaida. Taarifa ya gari la waziri kuchomwa moto na mtu hasiyejulikana na kusababisha kuipoteza familia yake ilionekana kuwachanganya. Kamanda mkuu akawaita watu wote ambao walikuwa katika kitengo cha upelelezi na kuanza kuongea nao.
Kamanda mkuu wa polisi, Bwana Innocent Ngomale alionekana kuchanganyikiwa, muda wote alikuwa akikipiga kichwa chake. Tukio lile likaonekana kulitia doa jeshi la polisi kuliko tukio lolote ambalo liliwahi kutokea. Kuchomwa moto kwa nyumba ya Dominick na familia yake wala halikuangaliwa kama tukio kubwa, tukio la kuteketezwa familia ya Waziri wa wa Mali Asili na Utalii, Bwana Boniface ndilo lilionekana tukio kubwa kwa mapolisi.
Kila polisi alibaki akiwa na wasiwasi, siku hiyo kamanda Ngomale alionekana kukasirika kuliko siku zote. Akasimama kutoka kitini kwake na kuanza kuangalia darini, akakaa na kuanza kutapitisha macho yake usoni mwa kila polisi aliyekuwa mahali pale.
“Hii ina maana gani?” Kamanda Ngomale alianza kwa kuuliza swali. Hakukuwa na polisi yeyote ambaye alilijibu swali lile, kila mtu alibaki kimya.
“Ina maana hamfahamu hali hii ina maana gani?” Kamanda Ngomale aliuliza huku akionekana kuwa na hasira. Bado ukimya ukatawala mahali pale, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alijibu kitu chochote kile.
“Hii ina maanisha kwamba tumeshindwa kazi. Ulinzi umekuwa mdogo sana siku hizi. Zaidi ya yote, hii inaonyesha ni jinsi gani tulivyojisahau na kazi zetu” Kamanda Ngomale aliwaambia mapolisi.
Akachukua glasi ya maji ambayo ilikuwa mezani na kupiga fundo moja. Jasho tayari likuwa likimtoka, feni ambayo ilikuwa ikiendelea kupepea ndani ya chumba kile ilionekana kutokufanya kazi yake katika mwili wake. Akayarudisha macho yake katika uso wa kila mmoja na kuanza kuwaangalia tena kwa zamu.
“Muuaji anahitajika haraka sana. Nendeni mkajipange ninyi kama mapolisi wa kitengo cha upelelezi. Tunataka ndani ya mwezi huu muuaji apatikane hata kabla mambo mengine hayajatokea” Kamanda Ngomale aliwaambia.
Kikao kilipokwisha wala hakukuwa na muda wa kupoteza zaidi ya mipango kabambe kuanza kupangwa. Mpelelezi mashughuli ambaye alisomea shughuli za Upelelezi nchini Urusi, Emmanuel Bugabu ndiye ambaye akateuliwa kuanza kushughulikia suala la kumtafuta muuaji.
Mpelelezi Emmanuel Bugabu alizaliwa miaka ishirini na tano iliyopita. Mara baada ya kujiunga na jeshi la polisi, akafanikiwa kuwa miongoni mwa vijana ambao walifuzu mafunzo ya kwenda kufundishwa upelelezi nchini Urusi.
Maisha nchi Urusi yalionekana kuwa magumu kwake, hali ya hewa ambayo alikuwatana nayo ilikuwa tofauti kabisa. Kila siku alikuwa akishinda na jaketi kubwa ambalo lilikuwa juu ya sweta lililokuwa juu ya fulana nzito ambayo ilikuwa juu ya ngozi yake.
Ingawa alikuwa akipata tabu kila siku, Bugabu akavulimilia mpaka pale alipomaliza elimu yake ambayo ilichukua miaka mitatu mpaka kumalizika. Aliporudi nchini Tanzania, Bugabu akaanza kufanya kazi ya upelelezi. Mauaji pamoja na uvamizi mbalimbali ulikuwa ukitokea, Bugabu ndiye ambaye alikuwa akipewa kazi ya kupeleleza. Wala hakuchukua muda mrefu, kila kitu kilikuwa kinakamilika na wahusika kukamatwa.
Sifa hizi ndizo alizokuwa nazo mpelelezi Bugabu, hakushindwa kazi hata moja, kila kazi ya upelelezi aliyopewa ilionekana kuwa ngumu kwa watu wengine lakini kwake yeye aliifanya kwa haraka sana. Kujituma kwake kazini pamoja na umakini mkubwa aliokuwa nao ndio ukapelekea shirika la upelelezi nchini Marekani, F.B.I (Fideral Bureau of Investigation) kutaka kuwa pamoja nao.
Serikali ya Tanzania ikakataa, haikutaka kumuachia Bugabu aende nchini Marekani, alihitajika kubaki nchini Tanzania kuendelea na kazi ya upelelezi. Bugabu alikuwa akiaminika na kila mtu, neno kushindwa kazi kwake wala halikuwepo, kila siku alikuwa akifanikiwa kwa kuwatia watu mikononi mwa vyombo vya dola.
Kila siku kazi yake ilikuwa ni ya mafanikio makubwa, Umakini wake mkubwa ndio ambao ulikuwa ukimletea sifa za kukubalika katika kila idara za kipolisi kiasi ambacho mara kwa mara alikuwa akiitwa Ikulu kula chakula pamoja na rais. Emmanuel Bugabu huyu huyu ndiye ambaye alikuwa amepewa jukumu kubwa la kuhakikisha muuaji wa familia ya Waziri Boniface anakamatwa na kuletwa katika vyombo vya sheria.
“Nimefanya kazi kubwa tena kubwa mara mia ya hii, zote nikafanikiwa. Hii kazi niliyopewa ni ndogo sana, nitaifanikisha ndani ya mwezi mmoja tu” Bugabu alijisemea huku akionekana kutoa tabasamu la dhihaka.
*********
Kila siku Dominick alikuwa mtu wa furaha, mauaji ambayo alikuwa ameyafanya wala hakuyasikitikia, kila siku kwake ilikuwa siku ya furaha. Alifuatilia kila kitu kwa karibu sana, kuonekana kwa mzee Boniface kuwa na hzuni hadi makaburini, kwa Dominick ndio ilikuwa furaha kubwa.
Kamwe moyo wake wala haukujuta, kila siku alikuwa akifurahia. Kila siku magazeti yalikuwa yakimfikia chumbani, picha mbalimbali za watu ambao walikuwa wakionekana kuhuzunika zlimfurahisha. Akaamua kumpigia simu Edmund na kumueleza juu ya kazi ambayo alikuwa ameifanya.
Muda wote Dominick alikuwa akizielezea waziwazi hasira ambazo alikuwa nazo moyoni, hakuona sababu ya watu wale watatu kuendelea kuwa na maisha ya furaha na wakati wao ndio walikuwa wameyarudisha nyuma maisha yake.
Mwezi mmoja ukapita, bado watanzania walikuwa na kumbukumbu vichwani mwao juu ya mauaji yaliokuwa yametokea. Walimhuzunikia sana waziri Boniface ambaye kila siku alikuwa akionekana kuwa na huzuni. Muuaji wa familia yake alikuwa akipokea lawama kila siku pasipo watu kujua ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Dominick bado alijiona kuwa na kazi kubwa ya kufanya, alitaka kukamilisha kila kitu ambacho kilitakiwa kukamilishwa kwa mikono yake. Jina la waziri Ombeni ndilo ambalo lilikuwa likitawala kichwani mwake kwa wakati huo.
Alijiona kuwa na uwezo mkubwa wa kumuua lakini kabla hata hajafanya hivyo alihitaji mzee huyo aumie kwanza, alitamani ayapate maumivu kama ambayo alikuwa ameyapata katika kipindi cha nyuma kwa kuiteketeza familia yake.
Akachukua karatasi na kupanga mipango mbalimbali juu ya namna kazi yake ambavyo angeifanya. Kila hatua ambayo alikuwa ameipanga kwa ajili ya kufanya mauaji, aliiona kutokuwa nzuri. Aliziandika mbinu zaidi ya kumi katika karatasi yake na kisha kuichagua mbinu moja ambayo aliiona kufaa sana.
“Nitaiteka familia yake halafu nitaichoma moto” Dominck alisema.
Akachukua karatasi ambayo alikuwa ameandika namba kadhaa za simu na kuiangalia namba ya simu ya nyumbani kwa waziri Ombeni. Dominick akaichukua ile namba na kuiandika katika simu yake.
“Nitaanza na familia yake” Dominick alisema huku akitabasamu.
*********
Kila siku baadhi ya watanzania walikuwa wakikasirika juu ya tabia ya Bi Magdalena ambaye mara nyingi sana alikuwa akitumia fedha nyingi kwa ajili ya kusafiri sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufanya starehe. Bi Magdalena hakuonekana kuridhika na mumewe, hali ambayo ikamfany kuanza kutembea na vijana wadogo ambao damu zao zilikuwa zikichemka.
Hakuonekana kujitambua alikuwa nani na alikuwa na heshima gani, kitu ambcho alikuwa akikitaka ni kuifurahisha nafsi yake. Ngono na vijana ndio ikawa sehemu ya maisha yake. Mara kwa mara alikuwa akishinda klabu pamoja na vijana wadogo huku wakila na kunywa.
Jina lake lilikuwa kubwa katika kila klabu kubwa jijini Dar es Salaam. Umri wake ulikuwa ni miaka arobaini na mbili lakini kila siku maombi yake yalikuwa ni kutaka kurudishiwa miaka nyuma na kuwa kijana. Hakuutaka uzee, alijiona kuwa na nafasi kubwa ya kustarehe kwani fedha kwake haikuwa na tatizo lolote lile.
Ni mara chache sana alikuwa akilala nyumbani mpaka asubuhi, mara nyingi alikuwa akitoroka na kuelekea katika klabu za usiku. Bi Magdalena alikwenda sambamba na binti yake, Sara. Mara kwa mara walikuwa katika kumbi za starehe, mwanaume ambaye alikuwa akitembea na binti yake, Sara basi nae ilikuwa ni lazima atembee nae.
Pepo la ngono likaonekana kuikumba familia hiyo. Ukimuachilia mumewe, basi wao wawili ndio walikuwa wakiunda familia hiyo. Kila siku pombe na ngono ndio yalikuwa sehemu ya maisha yao. Walichukuana na kujirusha sehemu mbalimbali za starehe.
Kila starehe walitamani kufanya, pepo la ngono likaonekana kuwatawala zaidi hasa pale ambapo wakaamua kusafiri kwenda nchini Marekani ili tu kutafuta kampuni mbalimbali ambazo zilikuwa zikijihusisha na urekodiji wa filamu za ngono, nao walitaka kuigiza.
Kila kitu ambacho walitaka kukifanya kikajulikana, hai ambayo walitakiwa kurudi nchini Tanzania haraka iwezekanavyo. Hawakuonekana kukumbuka maisha ya tabu ambayo walikuwa wamepitia katika kipindi cha nyuma, wao walichokuwa wakikikumbuka ni kipindi ambacho walikuwa wameanza kupata fedha tu.
Familia hii ilionekana kuwa ya hatari hasa katika mchezo wa ngono, kila siku waliwaza ngono kiasi ambacho wakati wmwingine pasipo kufanya ngono, walijisikia wagonjwa. Hii ndio ilikuwa familia ya waziri wa Miundo Mbinu, Bwana Ombeni.
Kila siku Bwana Ombeni alionekana kuwa mtu wa matatizo, alijua kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea juu ya mke wake na mtoto wake lakini wala hakuwa akisema kitu chochote kile. Moyo wake ulikuwa katika mapenzi mazito juu ya mke wake. Alimpenda Bi Magdalena kuliko kitu chochote maishani mwake.
Kila siku Bi Magdalena alikuwa akilalamika juu ya uwezo wa mumewe kitandani, na hiyo ndio sababu iliyompelekea kuanza kutembea na vijana wadogo. Shughuli ambazo alikutana nazo kwa vijana wadogo ambao muda mwingi walikuwa wakitumia kuangalia picha za ngono zilimfanya kumsahau mumewe.
Bwana Ombeni alionekana kuchoka sana kitandani, hakuwa na nguvu zozote za kutosha kiasi ambacho muda mwingi Bi Magdalena alijiona kulala pamoja na mwanamke mwenzake. Fedha ambazo alikuwa nazo ndizo ambazo zilikuwa zikiwavutia vijana wengi kutembea nae.
Hakukuwa na kijana yeyote ambaye asingelala nae kwa usiku mmoja kwa malipo ya shilingi laki mbili. Kwa kila kijana ambaye alikuwa akitembelea klabu za usiku sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam basi ni lazima atakuwa akimfahamu mwanamke huyu.
Ingawa alikuwa akifanya mambo mengi pamoja na binti yake lakini wala hakikuandikwa kitu chochote magazetini. Kwanza waandishi wengi wa habari walikuwa wakiogopa, lakini wakati mwingine walikuwa wakipewa fedha nyingi kwa ajili ya kukaa kimya.
Picha zake na binti yake zilikuwa katika simu nyingi za vijana, tena zilikuwa picha ambazo walikuwa watupu au wakifanya ngono na watu mbalimbali. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kuzikana picha zile ambazo zilikuwa zimesambaa katika kila kona jijini Dar es Salaam.
Yeye ndiye alliyemshauri mumewe kufanya ufisadi wa shilingi bilioni kumi ambazo zilikuwa zikielea elea katika idara yake. Kila siku fedha zile zilikua zikitumika katika kuwahonga vijana ambao alikuwa akitembea nao. Hakuonekana kuwa na wasiwasi na fedha ambazo wala hakuwa amezitolea jasho, kila siku fedha kwake aliziona kustahlli kutumiwa kwa kuwa tu zilikuwa zimetengezwa kwa kazi hiyo.
“Utamuweza lakini?” Mwanaume mmoja aliyekuwa na misuli alimuuliza Dominick ambaye alikuwa amevaa miwani mikubwa iliyokuwa na rangi nyeusi.
“Kwa nini nisiweze. Ebu niangalie, unanionaje?” Dominick alimuuliza kijana yule.
Muziki bado ulikuwa ukiendelea katika klabu hiyo ya Raspinho, taa hafifu ndizo ambazo zilikuwa zikiwaka. Wanawake mbalimbali wazuri ambao kazi yao ilikuwa ni kujiuza walikuwa wamesimama pembeni huku wakijaribu kufanya matangazo kwa kila mvulana ambaye alikuwa akiwaangalia katika klabu ile.
“Nakuuliza tena..utaweza?” Mwanaume yule bado alikuwa akimuuliza Dominick.
“Nitaweza bwana. Mimi ndiye Maliki Mtanga. Nimezaliwa kwa ajili ya kufanya ngono tu” Dominick aliongea huku akijisifia.
“Kumbe umetokea Tanga”
“Ndio. Kule Handeni”
MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com