Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

LIVERPOOL HOI YASHIKWA NA EVERTON

$
0
0
 
Wachezaji wa Everton wakishangilia baada ya Phil Jagielka (kulia) kufunga dakika ya 90 dhidi ya Liverpool na kuambulia sare ya bao 1-1.
 
Alberto Moreno (katikati) na Jordan Henderson (kulia) wakilalamika baada ya kunyimwa penalti na refa Atkinson wakidai kuwa mchezaji wa Everton Barry kashika mpira.
 
Steven Gerrard (kushoto) akishangilia baada ya kufunda bao dakika ya 65 kipindi cha pili.
 
Steven Gerrard akishangilia.
KLABU ya Everton imetoka nyuma na kuambulia sare ya bao 1-1 na Liverpool kwenye Ligi Kuu ya England. Wafungaji ni Steven Gerrard dakika ya 65, Phil Jagielka dakika ya 90.
Liverpool: Mignolet, Manquillo, Lovren, Skrtel, Moreno, Gerrard, Henderson, Markovic, Lallana, Sterling, Balotelli
Substitutes: Jones, Toure, Enrique, Lucas, Suso, Coutinho, Lambert
Everton: Howard, Hibbert, Baines, Jagielka, Stones, Barry, McCarthy, Besic, Mirallas, Naismith, Lukaku
Substitutes: Robles, Gibson, Eto'o, McGeady, Browning, Osman, Alcaraz
(PICHA NA MTANDAO)

USIKU WA KIGODORO - 01

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
“UKO wapi Lina?”
“Kwa dada, ndiyo tunataka kutoka kwenda saluni my dear.”
“Lina usinitibue, kwa dada saa hizi wakati unajua kanisani tunatakiwa saa nane kamili mchana, sasa uende saluni saa sita hii utamaliza muda gani? Kanisani utakuja saa ngapi na ndoa itafungwa saa ngapi au hutaki tufunge ndoa Lina?”
“Nitamaliza mapema tu.”
Mara Lina akakata simu…
“Khaa! Yaani Lina kanikatia simu mimi? Ana maana gani?” alijiuliza James. Alipopiga tena iliita bila kupokelewa…
“Afadhali isingepatikana ningesema chaji imeisha, sasa hapokei ina maana gani?” James aliendelea kuwaza…
“Lakini hili suala la Lina kutopokea simu au kukata litaisha lini? Maana ni kawaida yake. Tunaweza kuongea akakata au akawa hapokei. Huyo dada yake anayesema ni mkali sana, ukali wake ni kama wa simba? Afadhali tufunge hiyo ndoa ili aondoke kwa dada yake tuone.”
***
“Lina ulikuwa ukiongea na nani kwenye simu?” Semi, mume wa Lina alimuuliza baada ya kumsikia akisema anajiandaa kwenda saluni na yupo kwa dada yake tena akaita my dear…
“Ni yule rafiki yangu, Agnes anataka nimpeleke kwenye bethidei, mimi sitaki. Sasa nimemdanganya kwamba nakwenda saluni, itafika mahali atakata tamaa mwenyewe,” alisema Lina.
“Hapana mke wangu, Agnes ni rafiki yako mkubwa, nenda kwenye bethidei yake kama amekualika,” alishauri Semi.
“Mh! Haya baby, basi itabaidi niende saluni kweli halafu baadaye niende kwenye shughuli.”
“Sawa. Hakuna shida.”
Moyoni Lina alifurahi sana kwani ndicho alichokuwa akikitaka.
Alijiandaa akatoka kawaida, njiani alimpigia simu Agnes…
“Egi, dili limetiki. Shemeji yako ameikubali ile kamba. Kwa hiyo wewe uko wapi sasa?”
“Yaani fanya fasta, njoo saluni mimi nimeshafika Lina. Halafu James kanipigia simu, anasema umemkatia simu, nikamwambia kuna sababu shemeji asiwe na wasiwasi. Hebu mpigie ajue unakuja saluni.”
Lina alimpigia simu James…
“My dear nimeshafika saluni.”
“Sasa kwa nini ulikata simu?”
“Kawaida tu my dear, hakukuwa na kitu. Nilijua umemaliza kuzungumza.”
“Oke, fanya haraka mimi namalizia saluni, niko na bestimani wangu. Wewe umeshampata Agnes?”
“Ndiyo.”
Baada ya James kukata simu, Lina alibaki na mawazo kibao…
“Hivi lakini mimi Lina ni kwa nini nimekubali kuuingia mkenge kama huu? Yaani wanaume wawili, tena wote wa ndoa? Nitaishije nao sasa? Kwanza mume wangu Semi akijua, si atanichinja?”
Moyoni alijuta sana lakini kwa hatua aliyofikia, haikuwa rahisi agomee ndoa. Akapanga kwenda kugomea kanisani wakati wa kuulizwa na mchungaji, yeye ajibu hayuko tayari!
***
Kanisa zima lilitulia, maharusi siku hiyo walikuwa watatu. Moses na Lydia, John na Elizabeth na James na Lina.
Mwanamke mmoja ambaye alihudhuria ndoa ya Lina na Semi alikuwepo, akashangaa kumwona Lina anaolewa tena huku akijua bado yupo na Semi, akashtuka sana.
Kabla Lina hajamaliza kusema, alimkodolea macho Agnes huku akionekana kama anataka kutokwa machozi…
“Kanitumia shilingi laki moja yule kaka,” alisema…
“Kweli?”
“Kabisa.”
“Basi amekupata. Maana utakimbilia wapi?”
“Si umeona?”
Ilifika mahali, Lina alihesabu kwa kichwa akitumia kumbukumbu zake na kubaini kwamba, alishakula shilingi milioni moja na laki mbili za James, akajisikia huruma na aibu ya mwenyewe.
Siku moja ya Jumapili, James alimpigia simu Lina na kumwalika kwa lanchi kwenye Hoteli ya Riki, Lina alikubali mwaliko huo na kuwekeana ahadi ya kukutana saa saba mchana.
***
Kabla ya kwenda, Lina alijiuliza maswali mengi sana…
“Je, ikifika mahali akaniambia ananipenda itakuaje?”
“Je, akiniambia anataka kunioa? Maana anaonekana kama hana mke!”
“Mh! Hivi nilivyokubali kirahisi si anaweza kusema mi malaya, kwa nini sikutia ngumu kidogo?”
“Hivi nilivyovaa atanikubali kweli? Kama nipo rafu, si kwa kutoka kwenda hotelini.”
Saa saba juu ya alama Lina alifika kwenye mlango mkubwa wa hoteli hiyo, akasimama na kupiga simu kwa James…
“Nimefika, niko nje hapa.”
“Ingia, ulizia mapokezi sehemu ya baa.”
“Oke poa.”
Lina alisaidia na mfanyakazi mmoja wa hoteli hiyo hadi kwenye ukumbi wa baa, akamkuta James ameshakaa anakunywa wine…
“Mambo Lina?”
“Poa, habari yako James?”
“Mungu ananisaidia.”
“Oke. Pole kwa shughuli.”
“Pole wewe, mimi leo niliamua kupumzika, kwa hiyo sijafika ofisini kwangu.”
“Da! Hongera zenu nyie mliojiajiri wenyewe, mnaamua tu, leo siendi, leo nakwenda.”
James alicheka kidogo kisha akamwangalia Lina kwa macho matamu yaliyoonesha dhahiri kwamba anampenda, Lina akahisi aibu na kuangalia chini kwa mbali…
“Enhe, mambo mengine?” alianza Lina…
“Mambo mengine poa. Mimi nimeshakuagizia chakula, najua utakipenda. Lakini nisikuchukulea muda mrefu sana. Ni hivi Lina, kusema ule ukweli mimi nina ndoto za kufunga ndoa na wewe.”
Lina alishtuka, akamtumbulia macho kwa muda huku moyo wake ukipitisha mambo kibao. Aliwaza kuhusu siku ya ndoa yao, akawaza wamepata mtoto, akawaza wanavyotembea mitaani kama mke na mume…
“James, mbona itakuwa ngumu sana.”
“Nilitegemea hilo jibu, lakini pia nilijiandaa kwa kutaka kuujua huo ugumu.”
“Ugumu ni ugeni kati yetu, utawezaje kuzungumzia ndoa kabla ya kufahamiana kwa undani kwanza?”
“Hilo lipo automatiki. Nadhani kubwa ni kujua inawezekana au la, ndiyo iingie awamu ya kufahamiana.”
Lina aliwaza sana.
Alijiambia kwamba akisema ameolewa, angemkatisha tamaa kijana wa watu ambaye kwa siku kumi na mbili tu ameshamlambisha shilingi milioni moja na laki mbili…
“Oke, niko tayari James.”
James alinyoosha mkono na kumshika mkono Lina, akamwambia…
“Siku ya leo itaingia kwenye kumbukumbu ya maisha yangu.”
“Hata mimi pia James.”
“Lakini kuna jambo moja la msingi sana Lina. Najua wewe ni msichana mrembo, mzuri, unavutia na unaishi kwenye dunia yenye wanaume. Je, huna mpenzi kweli?”
“Mmmm…kusema ukweli nilikuwa naye, lakini tulitofautiana lugha tukaachana.”
“Lini?”
“Kama miezi miwili iliyopita. Kuanzia hapo nikasema sitaki tena wanaume, najipanga kwanza. Ndiyo maana hata wewe uliponiambia habari za kuoana nilikataa kwanza.”
“Pole sana baby. Unaweza kunieleza kwa ufupi historia ya maisha yako?”
“Mmmh! Kifupi mimi ni mtoto wa mwisho katika familia ya mzee Joseph Ambakucha yenye watoto watano. Nimezaliwa Kijiji cha Kilole, Korogwe Tanga.
“Baada ya kumaliza masomo Shule ya Msingi Kilole nilichaguliwa kwenda Sekondari ya Wasichana palepale Korogwe. Nilipomaliza masomo nilikwenda kusomea usekretari Tabora, nilipomaliza nikapata kazi kwenye ofisi za kununua madini ya mtu binafsi, baadaye ndiyo nikajiunga kwa wale wazungu wako pale.”
“Oke, nimekusoma. Mimi kama unavyojua. Naitwa James Wingawinga Nampapara, nilizaliwa Mpitimbi, Ruvuma. Ni mtoto wa tatu katika familia nikiwa ndiyo mtoto wa tatu mwenyewe. Nilisomea Ruvuma msingi na sekondari, baadaye nikaja Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
“Baada ya kumaliza chuo niliamua kuwa mjasiriliamali na kwa kuanzisha kampuni yangu ya kusafirisha nje vinyago, ndiyo inaniweka mjini.
“Nimebahatika, nimejenga nyumba Mbezi Beach, nimenunua magari matatu, nina kiwanja kingine Mbezi Beach. Uzuri sina haja ya kuwajengea wazazi wangu kwani baba yangu ana uwezo mkubwa na ndiye aliyenipa mtaji wa baishara.”
Lina alibaki ametumbua macho tu. Hakujua apongeze au achukue hatua gani!
Uhusiano wa wawili hao ulianzia hapo.
Kwa siku hiyo walipomaliza kula, Lina aliingia kwenye gari la James aina ya Toyota Land Cruiser V8 mpaka ofisini kwake, wakati anashuka, James aligeukia nyuma akachukua brifkesi na kuiweka kwenye mapaja yake na kutoa shilingi laki tano…
“Zitakusaidia kwa siku kadhaa.”
“Jamani sweet, mbona ninazo?”
“Usijali baby.”

MAMBO NDO KWANZA YAMEANZA ITAENDELEA

A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 01

$
0
0



MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
Mambo mengine yakaonekana kufumuka. Watu wakaanza kulitolea macho gazeti la Pamoja ambalo lilikwa na kichwa cha habari kikubwa kilichoonekana kumvutia kila mtu ambaye alikuwa akiliangalia. Habari ile ikaonekana kumshtua kila mtu, hakukuwa na mtu aliyeamini kwamba mambo kama yale yangeweza kutokea kwa mara nyingine.
Gazeti hilo likanunuliwa mtaani kupita kiasi, kila mtu alikuwa akiligombania. Kila mtu alitaka kujua hasa chanzo cha habari ile ambayo ilikuwa ikimvutia kila mtu. Mpaka inafika saa sita mchana, gazeti lile halikuwa likionekana mitaani.
‘VIONGOZI HAWA WATAFUNA MABILIONI YA WATANZANIA’ Kichwa cha habari kilikuwa kinasomeka vizuri mbele kabisa ya gazeti hilo tena huku kikiwa kimeandikwa kwa mwandiko mkubwa ambao hata kwa aliyekuwa na matatizo ya macho angeweza kuusoma.
Shauku ya kutaka kufahamu kwa kina juu ya habari ile ndio ambayo iliwafanya watu kulinunua zaidi gazeti lile. Idadi kubwa ya wananchi ndani ya jiji la Dar es Salaam walikuwa na nakala ya gazeti lile ambalo mara kwa mara lilikuwa likizungumzia mambo yanayofanywa na viongozi wa Serikali
Ununuzi mkubwa wa gazeti hilo haikuwa Dar es Salaam tu, bali hadi katika mikoa ya jirani, gazeti hilo lilikuwa likigombaniwa kupita kiasi. Habari ile ilimsisimua kila aliyekuwa akiiangalia. Hawakuamini kama viongozi ambao walikuwa wakiwaamini ndio ambao walikuwa wamefanya wizi mkubwa wa mabilioni.
Watu hawakutaka kuishia kuisoma habari ile tu, kuna kitu ambacho walitamani kukifahamu zaidi, jina la mwandishi ambaye alijitolea kuandika habari ile. Jina la Dominick Hyera lilikuwa likionekana vizuri, mwandishi huyu ambaye mara kwa mara alikuwa akiyaandika maovu mengi yaliyokuwa yakifanywa na viongozi wengi alionekana kuyatoa sadaka maisha yake.
Kila Mtanzania alimuona mwandishi Dominick kuwa shujaa, shujaa ambaye hakutaka kuona Watanzania wakiibiwa fedha zao ambazo walikuwa wakiziangaikia katika kuzilipia kodi. Dominick alionekana kuwa radhi kupata tatizo lolote lile ili mladi tu Watanzania wafahamu ni watu gani ambao walikuwa wakichukua fedha ambazo walikuwa wakiziangaikia.
“Nitaendelea kuandika mambo haya hadi mwisho. Nitataka watu wote wabaya wajulikane” Hayo yalikuwa maneno ambayo mara kwa mara Dominick alikuwa akimwambia bosi wake.
Dominick hakuonekana kuogopa kitu chochote kile. Maisha ya dhiki ambayo alipita katika kipindi cha nyuma ndio ambayo yalikuwa yakimfanya kuandika mambo hayo. Dominick aliwachukia viongozi wezi kuliko kitu chochote katika maisha yake.
Aliandika mambo mengi kipindi cha nyuma, wizi ambao ulitendeka katika kila sekta nchini. Aliandika mambo mengi kuhusu EPA, Dominick hakufumbia macho, aliandika mambo mengi kuhusu BoT. Dominick hakuishia hapo, kila wizi ambao ulifanyika, aliuandika gazetini pasipo kujali kitu chochote kile.
Jina lake liliendelea kuwa maarufu, kila mtu alitamani kumuona Dominick. Siku ambayo Dominick alionekana akihojiwa katika runinga, hakukuwa na mtu ambaye aliamini kuwa ni yeye. Alikuwa kijana mdogo sana ambaye kwa mtazamo wa haraka haraka alikuwa na miaka ishirini na tano.
Kila siku maisha yake yalikuwa ni kuwaweka wazi watu wote ambao walikuwa wakitumia nyadhifa zao katika kuiba mamilioni ya Watanzania, ambao asilimia zaidi ya tisini na tano walikuwa wakiishi maisha ya kimasikini.
Mtu pekee ambaye alikuwa akimtia moyo katika kazi yake alikuwa mke wake mpendwa, Christina pamoja na mtoto wake, Ibrahim aliyekuwa na miaka mitatu. Kila alipokuwa akiwaangalia watu hao, alijiona kupata nguvu ya kuandika mambo mengi zaidi.
Hakutaka mtoto wake, Ibrahim apate matatizo kama yeye alivyopata matatizo kipindi cha nyuma kwa viongozi kula fedha ambazo zilitolewa kwa ajili ya kuendeleza elimu nchini Tanzania. Alijiona kuwa na jukumu kubwa kuhakikisha wezi anawaweka wazi ili hata nafasi ya kuiba mamilioni ya Elimu isiwepo tena.
Kila kiongozi alikuwa akimuogopa Dominick, alionekana kuwa adui namba moja kwa viongozi ambao kazi yao kubwa ilikuwa ni kuiba mabilioni ya fedha ambazo zilikuwa zikilipiwa kodi kutoka kwa Watanzania.
Siku za Jumanne na Ijumaa hazikuwa zikikalika ofisini, watu walikuwa mitaani kununua gazeti la Pamoja kujua ni mambo gani ambayo yalikuwa yametokea kwa viongozi kwa wakati huo. Kila siku Watanzania walikuwa wakiumia, hawakuamini kama fedha ambazo walikuwa wakizitoa kama kodi zilikuwa zikiliwa kirahisi namna ile.
“Unajua kama leo ni sikukuu ya kuzaliwa ya Ibrahim?” Sauti ya Chrstina ilisikika ikiuliza swali kupitia simu.
“Mungu wangu! Kumbe ni leo! Nilikuwa nimesahau kabisa mpenzi, mambo mengi” Dominick alisema huku mkono wake mmoja akiutumia kushikilia usukani.
“Basi fanya haraka mpenzi. Fanya haraka kwa sababu wote hapa nyumbani tumekumisi, njoo tusherehekee pamoja” Christina alimwambia mumewe, Dominick.
“Usijali. Ngoja nipitie madukani nikanunue zawadi” Dominick alimwambia mkewe.
“Usichelewe....”
“Usijali, nitawahi mpenzi”
“Nakupenda”
“Nakupenda pia” Dominick alijibu na kukata simu.
Ingawa alikuwa safarini kurudi nyumbani, akakata kona na kuanza kuelekea katika maduka ambayo yalikuwa yakiuza vitu mbalimbali ambavyo vilikuwa vikitumika kama zawadi katika sherehe mbalimbali. Mara baada ya kufika katika eneo la maduka hayo, akasimamisha gari na kuteremka.
“Nahitaji midoli kwa ajili ya mtoto wangu, na ni vizuri kama itakuwa na ujumbe wa siku ya kuzaliwa” Dominick alimwambia muuza duka.
“Midoli ipo. Ipo ya aina mbalimbali na yenye jumbe tofauti tofauti” Muuza duka alimwambia Dominick huku akichukua baadhi ya midoli na kumkabidhi.
Dominick akaanza kuiangalia baadhi ya midoli ile, aliyoiona inafaa, akaichukua na kuondoka dukani hapo huku ikiwa imetimia saa kumi na mbili na nusu jioni.
Foleni ya magari kuanzia Ubungo ilikuwa kubwa mpaka Manzese Tip Top. Dominick alionekana kuchoka, tayari alijiona akichelewa kufika nyumbani. Kila wakati alikuwa akilalamika peke yake, foleni ilionekana kumchosha kupita kiasi.
Muda ulizidi kwenda mbele lakini hakukuwa na dalili ya foleni kusogea mbele kutokana na magari ambayo mara kwa mara yalikuwa yakijiingiza. Foleni ilidumu kwa dakika arobaini, magari yakaanza kusogea kwa mwendo wa taratibu.
Magari yalitembea kwa mwendo wa taratibu kwa dakika moja lakini yalikuwa yakisimama kwa dakika ishirini. Mpaka wanafika Ubungo na kupavuka tayari ilikuwa imetimia saa mbili kasoro. Dominick akaonekana kukasirika kupita kiasi.
Kutoka Ubungo mpaka Kimara mwisho wala hakuchukua muda mrefu, ni ndani ya dakika nne tu akawa amekwishafika. Akakata kona na kuanza kuingia barabara ya vumbi na kuendelea na safari ya kuelekea nyumbani.
Huku akiwa njiani, ghafla akasikia king’ora kikilia. Kwa haraka sana akaliegesha gari lake pembeni na gari lile la kitengo cha zima moto kupita.
“Wanajifanya wana haraka sana na wakati utakuta nyumba yenyewe imekwishateketea” Dominick alisema huku akiachia tabasamu la chini.
Akaendelea na safari yake ya kwenda nyumbani. Kila wakati alikuwa akiiangalia midoli aliyoiweka katika kiti cha pembeni. Furaha kubwa ilikuwa moyoni mwake, alimini mkewe, Christina angezifurahia zawadi zile kwa ajili ya mtoto wake, Ibrahim ambaye alikuwa akifikisha umri wa miaka mitatu.
Dominick aliendelea na safari, moshi mkubwa ukaanza kuonekana mbele yake huku mwanga wa moto uliokuwa ukiendelea kuwaka ukizidi kuongezeka. Dominick akaonekana kuwa na wasiwasi, akaongeza kasi ya gari lake.
Akakata kona ya njia ya kuelekea nyumbani kwake. Watu walikuwa wengi wakikimbilia katika njia ambayo alikuwa akiitumia kufika nyumbani kwake. Dominick akapigwa na mshtuko mara baada ya macho yake kutua katika nyumba ambayo ilikuwa ikiteketezwa kwa moto, ilikuwa nyumba yake.
“Christina.....” Dominick akajikuta akiita.
Hakuamini macho yake kama nyumba yake ndio ambayo ilikuwa ikiendelea kuteketea kwa moto. Kwa kasi ya ajabu akateremka kutoka garini na kuanza kupiga hatua kuelekea kule ilipokuwa nyumba yake huku akionekana kuchanganyikiwa.
Majirani zake ambao walikuwa wakiiangalia nyumba ile, walipomuona, wakamzuia. Dominick akaanza kupiga kelele huku akionekana kuchanganyikiwa zaidi. Majirani ambao walikuwa wamemshika upande wa kulia na kushoto wakamshika zaidi.
“Christinaaaaaaa.....Christinaaaaa... Ibrahimmmmm...” Dominick aliita huku akiwa amechanganyikiwa.
Watu kutoka katika kitengo cha Zima moto bado walikuwa wakiendelea na kazi ya kuuzima moto ambao ulikuwa umeiteketeza nyumba ile. Kila mtu akaonekana kuchanganyikiwa, hawakuelewa sababu iliyosababisha moto ule.
“Au shoti ya umeme ilipiga?” Kijana mmoja alimuuliza mwenzake.
“Mmmh! Sidhani. Nafikiri kuna mtu atakuwa ameichoma moto” Kijana mwingine alijibu.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Hauisikii harufu ya petroli?”
“Mhhhh! Inawezekana”
Zoezi la kuzima moto liliendelea zaidi na zaidi. Dominick alikuwa akilia kama mtoto, alitamani achoropoke kutoka katika mikono ya watu waliokuwa wamemshika lakini watu wale walikuwa wamemshika vilivyo.
Moto ulizimwa, hakukuwa na kitu chochote ambacho kilikuwa kimesalia, kila kitu kilikuwa kimeteketezwa kwa moto. Watu wakasubiri joto lipungue na ndipo waingie ndani. Walikaa kwa takribani dakika ishirini baada ya moto kuzimwa na ndipo wakaingia ndani ya nyumba ile ambayo tayari ilikuwa gofu.
Dominick akatamani aingie pamoja nao lakini watu wale waliomshika hawakutaka kumuachia. Baada ya dakika fulani maiti ya Christina na Ibrahim zikatolewa huku zikiwa zimefunikwa kwa kanga. Dominick akajikuta akipata nguvu za ziada, akajitoa mikononi mwa watu wale na kuanza kuwafuata watu wale waliobeba maiti ya mkewe, Christina na mtoto wake, Ibrahim.
“Christina.... Christina mke wangu...” Dominick aliita mara baada ya kuwafikia watu wale waliobeba maiti.
“Christina...Christina...” Dominick aliita huku akiwa haamini kile ambacho kilikuwa kimetokea.
“Ebu angalieni yale maneno pale” Jirani mmoja alisikika akiwaambia wenzake waangalie maneno ambayo yalikuwa yameandikwa getini.
‘BoT’ Maneno yale yalisikika.
Dominick akageuka na kuangalia kule getini, maneno yale yalikuwa yakisomeka vizuri machoni mwake. Akaonekana kugundua ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea kwa wakati huo.
*********
Mara baada ya kukata simu, Christina akaanza kufanya maandalizi kwa ajili ya kusherehekea siku ya kuzaliwa ya mtoto wake, Ibrahim. Kwanza akampeleka kumuogesha na kisha kumvalisha nguo nzuri ambazo zilionekana kumvutia hata yeye mwenyewe.
Christina akaingia jikoni ambako akaandaa chakula kizuri ambacho aliamini kingemfurahisha mumewe. Mara baada ya kumaliza kupika, akakipeleka chakula mezani.
Muda ulizidi kwenda mbele lakini bado Dominick hakuweza kuwasili. Christina aliendelea kusubiri zaidi na zaidi, wakati mwingine alitamani kumpigia simu kujua ni mahali gani alipokuwa na kama zawadi alikwishanunua, lakini kila alipotaka kufanya hivyo, alisita.
Muda ulizidi kusogea, mara kwa mara alikuwa akiangalia mishale ya saa kubwa ya ukutani, hasa mshale wa dakika, aliona muda ukizidi kusogea lakini wala mumewe hakuwa amefika nyumbani.
“Fanya haraka mpenzi...” Christina alijikuta akiongea peke yake.
Wala hazikupita dakika nyingi, akashtukia mlango ukigongwa. Christina akashtuka, hakuelewa ni nani ambaye alikuwa akigonga mlango wakati huo. Wazo la mumewe likamjia kichwani, lakini likapotea ghafla mara baada ya kugundua kuwa hakuwa amesikia muungurumo wa gari wala geti kufunguliwa.
Swali juu ya mtu ambaye alikuwa akigonga mlango lilikuwa likijirudiarudia kichwani mwake kila nukta ambayo ilisogea. Akainuka kutoka katika kiti alichokuwa amekaa na kuufuata mlango.
Christina akapigwa na mshtuko mara baada ya kuufungua mlango na macho yake kutua katika uso ambao ulikuwa umefunikwa kwa kutumia kinyago. Hata kabla Christina hakuchukua uamuzi wa kupiga kelele, akajikuta akizibwa mdomo.
Vijana wengine ambao nao nyuso zao zilikuwa zimefunikwa na vinywago wakaingia ndani. Christina akawekwa kochini na kuamriwa kutokupiga kelele zozote zile. Akabaki akitetemeka kama mtu ambaye alikuwa akisikia baridi kali.
Muda wote Christina alikuwa akilia, hakuelewa ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea mahali hapo. Kijana mmoja akamfuata Ibrahim ambaye alikuwa amewekwa katika kochi la pembeni, alipomfikia, akambeba na kumpelekea Christina.
“Jamani kuna nini tena? Mbona mnanitisha?” Christina aliuliza huku akionekana kutokuelewa chochote.
“Mumeo anafahamu kila kitu. Yaani hakuna hata kigeni asichokifahamu” Mwanaume mmoja alisema kwa sauti nzito iliyojaa mikwaruzo.
“Kitu gani? Mume wangu anafahamu kitu gani?” Christina aliuliza huku akiendelea kutetemeka.
“Anawachafua wazee wetu, anategemea tutamuacha hivi hivi?” Mwanaume mmoja alimuuliza Christina na kuendelea.
“Leo tutataka kumuonyesha ni kwa jinsi gani wazee wetu wamekasirika” Mwanaume yule alimwambia Christina.
Christina akafuatwa na mwanaume mmoja kutoka pale alipokuwa amekaa na kupelekwa jikoni. Huko akafungwa kamba mikononi na miguuni huku mdomo wake ukifungwa na kitambaa. Christina alijitahidi kupiga kelele lakini sauti yake wala haikuweza kusikika popote pale.
“Tuwaue kwa aina gani ya kifo” Mwanaume mmoja aliwauliza wenzake.
“Chochote tu. Ili mladi watu wasijue kama wameuawa”
“Sawa. Hapo nimekuelewa. Nenda kalete petroli garini” mwanaume yule aliagiza na mmoja wao kutoka nje na kuanza kuelekea nje ambako baada ya muda fulani akarudi akiwa na dumu la lita ishirini lililokuwa na mafuta ya petroli.
Wala hawakutaka kupoteza muda wowote ule, wakaanza kummwagia Christina pamoja na mtoto wake, Ibrahim ambaye alikuwa amemkumbatia na kisha kuendelea kumwaga na sehemu nyingine za nyumba ile. Baada ya kuona kila kitu kilikuwa tayari ndani ya mpango wao, mwanaume mmoja akachukua kiberiti na kuwasha.
“Mmmmmhhh.... mmhhhh..” Christina alisikika ndani.
Nyumba ikaanza kuteketea kwa moto hali iliyowafanya baadhi ya majirani kutoka nje ya nyumba zao. Kila mtu ambaye aliiona nyumba ile ilivyokuwa ikiteketea alishindwa kuelewa ni kitu gani ambacho kilisababisha nyumba ile kuteketea.
“Pigeni simu kitengo cha Zimamoto” Mwanamke mmoja aliwaambia wenzake.
“Nimekwishapiga kitambo” Mwanaume mmoja alimwambia.
Mpaka gari la kitengo cha Zimamoto linaingia mahali pale, tayari nyumba yote ilikuwa imeteketezwa wa moto. Hakukuwa na dalili za kupatikana na kitu chochote kile kilichokuwa kizima, kila kitu kilikuwa kimeteketezwa kwa moto.
**********
Dominick alionekana kuchanganyikiwa, tukio la kuchomwa moto kwa nyumba yake lilionekana kumchanganya kupita kiasi. Kila siku alikuwa mtu wa kulia tu, moyoni aliumia kupita kiasi. Picha ya mkewe mpendwa, Christina pamoja na mtoto wake, Ibrahim bado zilibaki kichwani mwake.
Mbele yake akaona giza, hakujua afanye nini ili atoke katika hali ambayo alikuwa nayo. Akili yake tayari ilimwambia kuwa kuna mtu ambaye alikuwa nyuma ya tukio lile, lakini hakuwa akifahamu ni nani hasa alihusika moja kwa moja na tukio la kuumiza moyo wake kupita kiasi.
Maisha yake katika kipindi hicho yalitawaliwa na majonzi, hakujua ni sehemu gani ambako angeweza kupata faraja ambayo ilionekana kupotea moyoni mwake. Kila siku alikuwa akielekea katika kaburi la mke wake na mtoto wake kama ishara kubwa ya kuwakumbuka.
Mara kwa mara alikuwa akiitwa katika kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa baadhi ya maelezo huku upelelezi ukiendelea kufanyika. Kila Mtanzania ambaye alilisikia tukio lile alijua moja kwa moja kwamba kuna mtu ambaye alikuwa amehusika katika kuiteketeza familia ya Dominick.
Maneno ya BoT ndio ambayo yalionekana kumchanganya kila mtu. Kila mmoja alijua fika kuwa kiongozi wa kitengo hicho ambaye aliandikwa sana na magazeti kuhusu wizi aliokuwa ameufanya ndiye ambaye alikuwa amefanya tukio lile.
“Sidhani kama atakuwa ni yeye” Dominick alimwambia kamanda mkuu wa polisi, Bwana Idrisa.
“Kwa nini unadhania hivyo?”
“Hebu jifikirie, kwanza habari kuhusu yeye niliiandika miaka miwili iliyopita, halafu kingine, tayari alikwishafariki. Unalikumbuka hilo mkuu?” Dominick alimwambia na kumalizia na swali.
“Mhhhh... Lakini hapa kuna ukweli”
“Sasa swali linalonijia kichwani juu ya mtu aliyehusika na tukio hili” Dominick alimwambia Bwana Idrisa.
Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo afya ya Dominick ilivyozidi kushuka. Mwili wake ukapungua kupita kiasi, mawazo juu ya familia yake bado yalikuwa yakimsumbua kila siku. Dominick alijiapia kutaka kulipiza kisasi kwa mtu yeyote mbaye alikuwa amehusika kwa namna moja au nyingine katika kumuumiza.
ITAENDELEA SIKU YA KESHO HAPA USIKOSE.
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ARSENAL YACHOMOA MWISHONI IKIPATA SARE YA 1-1 NA TOTTENHAM

$
0
0

Arsenal: Szczesny, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Arteta (Flamini 28), Oxlade-Chamberlain, Ramsey (Cazorla 45), Wilshere (Sanchez 63), Ozil, Welbeck.
Subs Not Used: Rosicky, Podolski, Ospina, Coquelin.
Booked: Oxlade-Chamberlain, Wilshere, Chambers.
Goals: Oxlade-Chamberlain 74.

Tottenham Hotspur: Lloris, Naughton, Kaboul, Vertonghen, Rose (Dier 83), Mason, Capoue, Lamela, Eriksen (Lennon 62), Chadli (Bentaleb 80), Adebayor.
Subs Not Used: Soldado, Vorm, Townsend, Fazio.
Booked: Lamela, Chadli, Adebayor, Lennon, Mason, Rose.
Goals: Chadli 56.
Att: 59,900
Ref: Michael Oliver (Northumberland).








RONALDO APIGA BAO MADRID IKIISHINDA VILLAREAL

$
0
0
Wakati mashabiki wa Manchester United wameendeleza vituko vya kutembeza bango lao la 'COME HOME RONALDO' kwa kutumia ndege katika mechi ya La Liga kati ya wenyeji
Villarreal dhidi ya Real Madrid, mshambuliaji huyo ameendelea kutikisa nyavu.

Cristiano amefunga tena wakati Madrid ikiiangusha Villareal kwa mabao 2-0.
Bao jingine la Madrid lilifungwa na kiungo Luka  Modric.
Ronaldo ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mara mbili ya mabao yake katika kipindi cha wiki sita tu, hiyo ni katika miaka 60 iliyopita.
Tayari ana mabao 187 ya La Liga akiwa na Madrid na kwa misimu yote mitano alitoitumikia Madrid amekuwa kwenye 10 bora ya wafungaji bora wa La Liga.




MESSI APIGA BAO LA 400, NEYMAR APIGA HAT-TRICK BARCELONA IKIICHUBUA GRANADA 6-0

$
0
0

Barcelona: Bravo, Mathieu, Dani Alves, Adriano, Mascherano, Busquets (Bartra 64), Xavi, Rakitic (Sergi 58), Neymar, El Haddadi (Ramirez 71), Messi.
Subs not used: Ter Stegen, Montoya, Pedro, Iniesta.
Goals: Neymar 26,45 & 66, Rakitic 43, Messi 62 & 82.
Bookings: Dani Alves

Granada: Fernandez Alvalleros, Foulquier, Claude Babin, Nyom, Murillo, Yuste Canton (Pascual Israfilov 45), Marquez Moreno, Iturra, Rico Castro (Medina Luna 45), El-Arabi (Martins 73), Success Ajayi.
Subs not used: Olazábal Paredes, Mainz, Nounkeu, Cordoba.
Bookings: Rico Castro, Foulquier.
Referee: Juan Martínez Munuera
Attendance: 72,596.







A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 02

$
0
0

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

 “Kwa nini unadhania hivyo?”
   “Hebu jifikirie, kwanza habari kuhusu yeye niliiandika miaka miwili iliyopita, halafu kingine, tayari alikwishafariki. Unalikumbuka hilo mkuu?” Dominick alimwambia na kumalizia na swali.
   “Mhhhh... Lakini hapa kuna ukweli”
   “Sasa swali linalonijia kichwani juu ya mtu aliyehusika na tukio hili” Dominick alimwambia Bwana Idrisa.
   Kadri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo afya ya Dominick ilivyozidi kushuka. Mwili wake ukapungua kupita kiasi, mawazo juu ya familia yake bado yalikuwa yakimsumbua kila siku. Dominick alijiapia kutaka kulipiza kisasi kwa mtu yeyote mbaye alikuwa amehusika kwa namna moja au nyingine katika kumuumiza.
SONGA NAYO...2JIACHIE NDO MPANGO MZIMA
   Katika kipindi hicho hakuwa na nyumba, alikuwa akiishi kwa rafiki yake, Edmund ambaye alikuwa akifanya  kazi ya Uandishi pamoja nae. Maisha yake aliyaona yakianza nyuma kabisa katika pointi ya kwanza ambayo alikuwa akiishi kabla ya kuoa.
   Kila siku Dominick alikuwa akiuliza kuhusu upelelezi ambao ulikuwa bado ukiendelea kufanyika. Aliona kila kitu kikikwenda taratibu sana. Katika kipindi hicho alihitaji hata tetesi ya nani alikuwa amehusika katika kufanya mauaji yale.
   Hakukuwa na tetesi zozote zile alizozisikia kutoka katika kitengo cha polisi cha upelelezi, kila kitu kilionekana kuwa kigumu. Kwa wakati huo, kila gazeti lilikuwa na taarifa zake, waandishi wa habari wakaanza kuingiwa na hofu ya kuandika mambo mengi kuhusiana na wizi ambao ulikuwa ukifanyika katika sekta mbalimbali Serikalini.
   Maisha yaliendelea kama kawaida. Baada ya miezi mitatu ya kujipanga upya, Dominick akajiona kuanza kusahau. Akaanza kufanya kazi kama kawaida japokuwa mara kwa mara alikuwa akiikumbuka familia yake hasa kila alipokuwa akiziangalia picha ambazo walipiga pamoja.
   “Kuna habari kuhusu nini?” Dominick alimuuliza mwanamke ambaye alimpigia simu.
   “Ufisadi. Kuna ufisadi umefanyika katika hili shirika la serikali la nyumba za taifa, NHC. Kuna kamchezo kamefanyika hapa” Sauti ya mwanamke yule ilisikika.
   “Kuna ushahidi wowote juu ya habari hiyo?”
   “Ushahidi upo. Tuna mikanda baadhi ambayo itakudhihirishia hilo” Sauti ya mwanamke yule ilisikika.
   “Sawa. Uko wapi ili nije kuichukua habari hiyo?”
   “Njoo hapa New Africa Hoteli”
   “Nitakuwa hapo baada ya dakika ishirini” Dominick alisema na kukata simu.
   Hakuwa na cha kufanya kwa wakati huo zaidi ya kujiandaa na kisha kuanza safari ya kuelekea katika hoteli ya New Afrika. Dominick alionekana kuwa na hamu kubwa ya kuandika habari ambazo zilikuwa zikihusu wizi ambao ulikuwa ukiendelea kufanyika japokuwa kwa wakati huo tayari ulikuwa umepungua kwa kiasi kikubwa.
   Ingawa saa yake ilikwa ikimwambia kuwa ni saa nne usiku lakini hilo hakuonekana kulijali,kitu ambacho alikuwa akikijali ni kufanya kazi yake tu.
   Mara baada ya kufika Jangwani, akaongeza kasi ya gari lake mpaka alipofika maktaba ya Taifa ambapo akakata kona kulia na kuanza kuelekea Posta. Wala hakuchukua sekunde nyingi, akaaingia katika eneo la hoteli ya New Afrika.
   Huku akiwa hajateremka, ghafla akashtuka baada ya kuwaona vijana watatu wakielekea kule alipokuwa garini. Hata kabla hajajiuliza juu ya watu wale, akashtukia wakiingia ndani ya gari lake.
   “Mbona mnai.....” Dominick aliuliza lakini hata kabla hajaalizia swali lake, akajikuta akiwekwa chini ya ulinzi na mwanaume mmoja ambaye alishika bunduki.
   “Fuata maelekezo yetu kuanzia sasa. Kama utakuwa mkaidi, utaifuata familia yako” Mwanaume yule alimwambia Dominick.
   Hakuwa na la kufanya kwa wakati huo, mdomo wa bunduki ambao alikuwa ameelekezewa ulionekana kumuogopesha kupita kiasi. Akawasha gari lake na kuanza kuelekea kule ambako alitakiwa kwenda kwa wakati huo.
   “Lakini nimefanya nini jamani?” Dominick aliuliza huku akionekana kuogopa.
   “Kwani wewe umekuja hotelini kufanya nini?” Mwanaume mmoja kati ya wale watatu alimuuliza.
   “Nilipigiwa simu ya kikazi. Kama mnataka kuchukua gari, tafadharini, lichukueni ila niachieni niendelee na kazi yangu” Dominick alijitetea.
   “Hakuna. Hakuna kitu kama hicho. Kama magari, tunayo mengi na ya kutosha. Kwa sasa hatuhitaji gari, tunachohitaji ni roho yako tu” Mwanaume yule alisema maneno ambayo yalimshtua Dominick.
   “Unasemaje?” Dominick aliuliza huku aisimamisha gari.
   “Najua umenisikia. Topa, shikiria usukani” Mwanaume yule aliyejiita Kibra alimwambia mwenzake na Dominick kuchukuliwa na kuwekwa katika viti vya nyuma.
   “Jamani. Nimefanya nini, nimefanya nini jamani. Mmeiua familia yangu, hamjalidhika tu mpaka mnataka kuniua na mimi?” Dominick aliuliza huku akianza kutokwa na machozi.
   Hakuwa na tumaini lolote kwa wakati huo, tayari alijiona kuwa kama mfu ambaye alikuwa akitembea, aliuangalia mdomo wa bunduki ile, bado ulionekana kumtisha. Tayari akaanza kuhesabu dakika za yeye kuvuta pumzi ya dunia hii, hakuwa na uhakika kama angeweza kunusurika katika mikono ya watu hao.
   “Lakini ni nani ananifanyia hivi? Kwa nini lakini” Dominick aliuliza.
   “Hata sisi hatumfahamu na wala hatufahamu ni kwa nini anafanya hivi. Sisi tunachokitaka ni utekelezaji tu”  Kibra alimwambia Dominic.
   Njia nzima Dominick alikuwa akilia huku akiwaomba watu wale wamuachie. Hakukuwa na mtu yeyote ambaye alionekana kuelewa chochote kile, kitu ambacho walikuwa wakikitaka kukifanya kwa wakati huo kilikuwa ni utekelezaji wa kile walichotumwa tu.
   Gari likafungwa breki katika msitu wa Nyakipande, Dominick akateremshwa. Giza lilikuwa kubwa wakati huo, moja kwa moja akaanza kuingizwa ndani ya msitu huku akiwa amefungwa kitambaa usoni. Muda wote Dominick alikuwa akilia tu huku akiomba msamaha japokuwa hakuwa amelifahamu kosa lake.
   Dominick akapelekwa mpaka katika sehemu ambayo ilikuwa na nyasi ndefu na kulazwa chini. Kibra akachomoa bunduki yake na kuanza kuisafisha kwa mbwembwe zote. Bado Dominick alikuwa akilia ingawa hakukuwa na mtu yeyote ambaye alionekana kumjali.
   “Tutakuua kifo kilichojaa maumivu, ili utakapokuwa ukiumia, basi ujute kwa nini ulikuwa ukipenda kuandika mambo ya watu gazetini” Kibra alimwambia Dominick huku akimwuelekezea bunduki.
   “Paaaaaa....” Mlio wa risasi ulisikika, Dominick alikuwa akiugulia kwa maumivu huku akiushika mguu wake.
   Damu zilikuwa zikimtoka mguuni, risasi ilikuwa imepenya katika mguu wake. Kilio kikubwa ndicho ambacho kilikuwa kikisikika kutoka kwa Dominick. Kibra na wenzake wakabaki wakicheka, walionekana kuyafurahia maumivu ya Dominick.
   “Tutaendelea hivi hivi mpaka pale utakapoanza safari ya kuifuata familia yako” Kibra alimwambia Dominick huku akiwa amemuelekezea tena bunduki.
   “Paaaaaaa.....” Mlio wa risasi ulisikika kwa mara ya pili.
   “Paaaa... paaaa....paaaa...paaaaa...” Milio mingine ya risasi ikasikika katika eneo hilo, damu zikatapakaa katika eneo hilo, ukimya ukatawala, hakukuwa na sauti yoyote ambayo ilisikika katika kipindi hicho hata ile sauti ya kilio cha Dominick haikusikika tena.
                                                                    ************
   Siku ziliendelea kukatika, wafanyakazi wa kampuni ya magazeti ya Hold on Publishers wakaonekana kuchanganyikiwa. Siku nyingi zilikuwa zimekatika pasipo Dominick kuonekana. Wasiwasi ukazidi kuogezeka zaidi hasa mara baada ya Edmund kusema kwamba hakuwa amelala kwake karibu siku tano.
   Taarifa zikatolewa katika vituo mbalimbali vya polisi na kazi ya kumtafuta Dominick kuanza. Dominick alitafutwa katika sehemu nyingi lakini wala hakupatikana. Taarifa zikatolewa gazetini, kila mtu ambaye aliiona taarifa ile ya kupotea kwa mwandishi ambaye alikuwa akiandika mambo mengi kuhusiana na viongozi wezi alibaki na mshangao.
   Maswali mengi yalikuwa yakimiminika vichwani mwa Watanzania, upotevu wa Dominick ukaonekana kumtia wasiwasi kila mmoja. Tetesi za Dominick kuuawa zikaanza kutapakaa katika kila kona ya jiji la Dar es Salaam. Kila mtu aliamini kuwa Dominick aliuawa na watu ambao walikuwa wameiteketeza familia yake.
   Baada ya miezi mitatu, mazishi yakaanza kufanyika. Watu wengi walishiriki katika mazishi ya Dominick, picha yake kubwa ilikuwa mbele ya jeneza lake. Watu ambao walikuwa na upendo mkubwa kwa Dominick, walilia mpaka wengine kupoteza fahamu.
   Nchi ya Tanzania ikaonekana kumpoteza mtu shujaa, mtu ambaye alikuwa akitaka Watanzania waishi katika maisha mazuri kupitia uandishi kwa kuwataja viongozi ambao walikuwa wakiiba fedha za wananchi. Jeneza likafukiwa katika makaburi ya Kinondoni, hakukuwa na mtu aliyeamini kama Dominick waliyekuwa wakimpenda alikuwa ameuawa.
   “Acha akapumzike na familia yake” Kijana mmoja aliwaambia wenzake huku macho yake yakiwa mekundu.
   Kampuni ya kutengeneza magazeti ya Hold On Publisher ikatoa siku thelethini za kuomboleza. Wafanyakazi wa kampuni hiyo walipunguziwa masaa mawili ya kufanya kazi ndani ya mwezi huo. Siku ziliendelea kukatika mpaka mwaka kuisha, Dominick akasahaulika vichwani mwa watu.
   “Mwaka jana tulikuwa na mwandishi mzuri sana. Aliandika wizi ambao ulikuwa ukifanyika katika sekta mbalimbali, namkumbuka mtu huyu, familia yake iliuawa kabla ya yeye mwenyewe kuuawa na maiti yake kutoonekana mpaka leo” Mwandshi mmoja alimwambia mwenzake mara baada ya kuhitimu masomo yake katika chuo kikubwa cha DSJ (Dar es Salaam School of Journalism).
   “Namkumbuka sana. Si yule Dominick aliyekuwa akiitwa shujaa. Namkumbuka sana, katika maisha yangu sitoweza kumsahau mtu kama yule” Mwandishi mwingine alisema.
   “Mungu Amlaze Pahali Pema Peponi”
   “Amen”
                                                                *************
   Mzee Mrisho alikuwa mtu maarufu sana katika sehemu yote ya Mbezi. Kila mtu ambaye alikuwa akiishi Mbezi alikuwa akimfahamu mzee huyu kutokana na biashara yake aliyokuwa akiifanya ya kuuza nyama katika moja ya bucha lake lililokuwa Mbezi kwa Yusufu.
   Nyama mbalimbali zilikuwa zikipatikana buchani kwake hali ambayo iliwafanya watu wengi kumiminika buchani hapo kununua nyama kwa ajili ya mboga. Nyama nyingi zilikuwa zikipatikana buchani hapo, swala, nyati, mbuzi na ng’ombe zilikuwa ni moja ya nyama ambazo zilikuwa zikipatikana kwa wingi.
   Mzee Mrisho alizaliwa miaka hamsini iliyopita mkoani Shinyanga. Alizaliwa katika familia ya mwindaji, baada ya miaka kadhaa nae akaanza kuelekea kuwinda pamoja na baba yake. Mpaka anakuja kufikisha miaka kumi na nane, Mrisho alikuwa mwindaji mzuri.
   Alipofikisha miaka ishirini, baba yake alifariki dunia, kazi ya uindaji ikabakia kwake, kila siku alikuwa akielekea porini kuwinda. Kila mtu aliyekuwa akiishi Shinyanga alikuwa akimfahamu Mrisho ambaye maisha yake yalikuwa yakiendeshwa na biashara hiyo.
   Kila siku jina la Dar es Salaam lilikuwa kichwani mwake, jiji hilo ambalo alikuwa akilisikia masikioni mwake kutoka kwa watu mbalimbali lilionekana kumvutia. Mrisho akajikuta akitamani kufika jijini Dar es Salaam na kuanza maisha huko.
   Alichokifanya Mrisho ni kuanza kuzihifadhi fedha alizokuwa nazo. Baada ya miaka miwili alikuwa na fedha za kutosha ambazo zilimfanya kusafiri kuelekea Dar es Salaam. Mrisho alionekana kuwa mshamba kwa kila kitu ambacho alikuwa akikiona, majengo mazuri pamoja na mpangilio wa nyumba vilikuwa vitu ambavyo vilimvutia kupita kiasi.
   Mrisho hakutaka kukaa tu nyumbani, akaanza kutafuta kazi. Kazi hazikuwa rahisi kupatikana, alitembea umbali mrefu kutafuta kazi lakini hakukuwa na mafankio yoyote yale. Miaka ilizidi kukatika, Mrisho akaamua kuanza biashara ya kuuza genge.
   Mara baada ya kusikia juu ya wanyama waliokuwa wakipatikana katika msitu wa Nyakipande, Mrisho akavutiwa, akaamua kuhamia Mbezi. Huko ndiko ambako akaanza kazi kama ile ambayo alikuwa akiifanya Shinyanga.
   Kila siku alikuwa akitoka asubuhi kuelekea katika msitu wa Nyakipande ambako alikuwa akiwinda na kurudi jioni huku akiwa na vitoweo vya kutosha. Biashara ya kuuza nyama ikaonekana kuchanganya, akaamua kuanzisha bucha ambalo alikuwa akiuza nyama mbalimbali.
   Watu walikuwa wakimiminika. Kila baada ya siku mbili alikuwa akiingia porini kuwinda. Mrisho akaonekana kuuzoea msitu wa Nyakipande, kila kona za msitu huo alikuwa akizifahamu vilivyo. Mrisho hakuwa akipata kazi kutokana na makazi mengi ya wanyama kuyafahamu.
   Miaka iliendelea kwenda mbele hadi alipokuja kuoa na kupata watoto. Serikali ikakataza uwindaji ambao ulikuwa ukifanyika katika msitu wa Nyakipande, ulinzi mkali ukawekwa. Maisha yalionekana kuwa tofauti kwake lakini baada ya muda, maisha yakaanza kurudi katika hali ya kawaida kama zamani.
   Akaanza kuwinda usiku na kurudi nyumbani asubuhi. Hayo ndio yalikuwa maisha yake, aliingia msituni usiku na kurudi asubuhi. Nyama ambazo alikuwa akizipata porini ndizo ambazo alikuwa akiziuza buchani ambako mtoto wake, Selemani ndiye alikuwa msimamizi wa bucha hilo.
   “Twendeni kule” Sauti ilisikika msituni.
   Mzee Mrisho aliisikia sauti ile vizuri, akachukua gobole lake na kujificha. Tayari akili yake ilikwishamwambia kuwa watu hao ambao walikuwa wakiongea walikuwa mapolisi ambao kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha ulinzi msituni mule.
   Sauti za watu wale ziliendelea kusikika. Mzee Mrisho alitaka kupiga hatua kurudi lakini akajikuta akishindwa kufanya hivyo. Alijikuta akivutiwa zaidi kuwafuatilia watu hao ambao alikuwa na uhakika kuwa hawakuwa walinzi.
   “Hawa sio walinzi, ulinzi gani usiku namna hii?” Mzee Mrisho alijiuliza.
   Akaanza kupiga hatua kuelekea kule ambako watu hao walisikika wakielekea. Mgobole wake ulikuwa makini mkononi mwake, alionekana kutaka kujitetea na hatari yoyote ambao ingeweza kutokea mahali hapo.
   Aliendelea kuwafuatilia watu hao huku akijifichajificha. Safari ya watu wale ikashia katika sehemu ambayo ilikuwa na uwazi mkubwa. Ingawa kulikuwa na giza lakini mzee Mrisho alikuwa akiona kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea.
   Mtu mmoja aliwekwa chini, sauti ya mtu yule haikuwa ikisikika vizuri hali ambayo aliigundua kwamba alikuwa amezibwa mdomo kwa kutumia kitambaa. Mwanaume mmoja akaonekana akichomoa bunduki na kisha kumuelekezea mtu yule ambaye alikuwa chini.
   “Tutakuua kifo kilichojaa maumivu, ili utakapokuwa ukiumia, basi ujute kwa nini ulikuwa ukipenda kuandika mambo ya watu gazetini” Sauti ya mwanaume mmoja ilisikika.
   Mlio wa risasi ukasikika, mwanaume yule aliyekuwa chini alisikika akipiga kelele za maumivu. Tayari mzee Mrisho aliona hakukuwa na amani mahali pale, alijiona kuwa na nafasi ya kufanya chochote ili aokoe maisha ya mwanaume yule.
   Wanaume wale watatu walibaki wakicheka hali iliyoonyesha kwamba walikuwa wakiyafurahia maumivu ya mwanaume yule aliyekuwa akilia. Mwanaume yule ambaye alimpiga risasi mwanaume yule aliyekuwa chini, akamuelekezea tena bunduki tayari kwa kumpiga risasi nyingine.
   Mzee Mrisho akajikuta akichukua mgobole wake na kumwelekezea mwanaume yule aliyekuwa ameshika bunduki. Hakutaka kuchelewa, hapo hapo akamfyatulia risasi ya kichwa, mwanaume yule akaanguka chini kama mzigo wa viazi.
   Hata kabla wale wenzake hawakujua wafanye nini, wakashtukia wakipigwa risasi za vifuani, damu zikatapakaa mahali pale. Wote wakaanguka chini ambako wakaanza kurusha mikono na miguu yao, baada ya muda, wakatulia hali iliyoonyesha  tayari walikuwa wamekufa.
   Mzee Mrisho akachomoka kutoka kichakani na kumfuata mwanaume yule aliyekuwa akilia kwa maumivu makali, akambeba na kuanza kuondoka nae pasipo kuongea nae kitu chochote kile. Safari ya kurudi nyumbani ikaanza, ilikuwa safari ndefu huku mwanaume yule akiwa mgongoni mwake.
   Alitumia masaa mawili, akawa amekwishafika nyumbani huku ikiwa saa tisa usiku. Mkewe akamfungulia mlango, mshangao mkubwa ukampata, hakuelewa ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea mpaka mumewe kurudi na mtu ambaye alionekana kuwa kama maiti.
   “Kuna nini tena mume wangu?” Bi Sikujua aliuliza.
   “Bandika maji jikoni kwanza” Mzee Mrisho alimwambia mkewe.
   Pasipo kuuliza kitu chochote kile, Bi Sikujua akaelekea jikoni ambako akabandika sufuria iliyokuwa na maji na kisha kurudi sebuleni ambako mzee Mrisho akaanza kumuelezea kila kitu kilichotokea.
   “Kwa hiyo haumfahamu kabisa?”
   “Ndio. Niliamua kumsaidia, niliona akiwa katika hali ya hatari” Mzee Mrisho alimwambia mkewe.
   Maji yalipochemka, yakaletwa na mzee Mrisho kuanza kufanya kazi ya kuiondoa risasi katika mguu wa mwanaume yule. Kilio kikubwa kilisikika lakini mzee Mrisho hakuonekana kujali, aliendelea na kazi ile mpaka risasi ilipotoka na kisha kumfunga bandeji.
   “Asubuhi ikifika, tutaelekea hospitalini kumnunulia dawa” Mzee Mrisho alimwambia mkewe, Bi Sikujua.
   “Kwa nini tusimpeleke hospitalini tu?”
   “Hapana. Maisha yake bado nayaona kuwa katika hatari” Mzee Mrisho alimwambia mkewe.
                                                             ************
   Maisha yaliendelea mbele, Dominick hakuruhusiwa kutoka nje, kila siku maisha yake yalikuwa ndani ya nyumba ya mzee Mrisho. Kila kitu alikuwa akikipata ndani ya nyumba ya mzee Mrisho, maisha yake hayauonekana kuwa na amani nje ya nyumba hiyo.
   Kitu alichokuwa akikifahamu ni kwamba kila siku angekuwa akitafutwa kwa lengo moja tu la kuuawa. Hakuamini kama watu ambao waliwatuma vijana wale wangeridhika kama wangepeta taarifa kuwa mtu ambaye alitakiwa kuuawa hakuuawa kama ilivyotakiwa iwe.
   Dominick akajiona kuingia katika vita, vita ambayo alitakiwa kuimaliza kwa mikono yake mwenyewe. Kila siku maombi yake yalikuwa juu ya kumfahamu mtu au watu ambao walikuwa nyuma ya mpango wa kuuawa kwake.
   Kila siku Dominick alikuwa akiyafikiria maneno yale ya BoT ambayo yalikuwa yameandikwa nje ya geti lake katika siku ambayo nyumba yake ilichomwa moto na familia yake yote kuangamia. Maneno yale yalieleweka vizuri na hata makao makuu ya idara ile alipafahamu vilivyo.
   Kitu alichokijua ni kwamba hakukuwa na mtu yeyote kutoka katika idara ile ambaye alihusika kutokana na yule mtu aliyefanya ufisadi kuuawa kwa kulegezewa breki ya gari lake alipokuwa akielekea Dodoma. Bado Dominick alionekana kuchanganyikiwa, hakuelewa kabisa mtu ambaye alikuwa nyuma ya tukio hilo.
   Kila siku alitamani kuwasiliana na marafiki zake ili kuwapa taarifa juu ya uwepo wake katika nyumba ya mzee Mrisho lakini kila alipotaka kufanya hivyo, alisita kwa kuogopa kujulikana kuwa yuko hai.
   Kila siku alikuwa mtu wa kulala ndani, hakutakiwa kutoka nje wala hakutakiwa mtu yeyote kufahamu kuwa yuko ndani ya nyumba ile.
   Mpaka taarifa za kifo chake zilipokuwa zinatangazwa, yeye mwenyewe alikuwa akiangalia katika televisheni. Dominick alibaki akifurahia kwani alijua kuanzia kipindi hicho asingeweza kupata usumbufu wowote ule.
   Siku ziliendelea kukatika mpaka mwezi mmoja kupita, bado Dominick alikuwa akishinda ndani. Hakutakiwa kutoka kabisa nje ya nyumba hiyo, na kama alitaka kutoka, basi kitendo hicho kilitakiwa kufanyika usiku, muda ambao hakukuwa na watu wengi mtaani.
   Hayo ndio maisha ambayo Dominick alikuwa akiishi. Kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea, alikuwa akipata taarifa kupitia televisheni na magazeti ambayo mzee Mrisho alikuwa akiyaleta.
   “Kila mtu anajua kuwa uliuawa, hakuna mtu ambaye anajua kama uko hai” Mzee Mrisho alimwambia Dominick.
   “Kwa hiyo wanachofahamu kuwa kwa sasa nipo kaburini?”
   “Ndio. Tena umeoza kabisa” Mzee Mrisho alimwambia Dominick.
   Dominick hakutaka kuendelea kukaa sebuleni hapo, moja kwa moja akainuka na kuaelekea chumbani. Mzee Mrisho alibaki sebuleni pale akiangalia televisheni. Dakika ziliendelea kukatika, mzee Mrisho hakutaka kwenda chumbani mpaka muda wa taarifa ya habari utimie, aliendelea kusubiri zaidi na zaidi.
   Huku akiendelea kuwa sebuleni hapo, mara umeme ukakatika na giza kutawala mahali hapo. Mzee Mrisho akaonekana kukasirika, akainuka kutoka pale alipokaa na kuelekea kule ilipokuwa soketi ya umeme na kuizima.
   Hata kabla hajapiga hatua kuelekea chumbani, mara akasikia mlango ukigongwa. Mzee Mrisho hakuonekana kuwa na wasiwasi, akaanza kupiga hatua kuufuata mlango na kuufungua.
   Mzee Mrisho akashtuka kupita kawaida, mdomo wa bunduki ulikuwa umeelekezewa usoni mwake na mtu ambaye hakuweza kumhamu kutokana na giza lililokuwa mahali pale. Hata kabla mzee Mrisho hajaamua ni kitu gani alitakiwa kufanya, akaamriwa kuingia ndani.
   “Jamani, kuna nini tena?” Mzee Mrisho aliuliza huku akionekana kuwa na hofu.
   “Tutakachohitaji, tutataka kupatiwa. Na kama hatutopatiwa, milio ya risasi itakwenda kusikika mahali hapa” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho huku wenzake wawili wakiwa wamekwishaingia ndani ya nyumba ile.
   “Mnataka nini? Mnataka nini jamani?” Mzee Mrisho aliuliza huku hofu ikizidi kuongezeka.
   Hata kabla mwanaume yule hajajibu chochote juu ya kile walichokuwa wakikitaka, Bi Sikujua akatokea sebueni pale. Akaamriwa anyamaze kimya, sauti yoyote kutoka kwake isisikike. Mwanaume mmoja alimsogelea na kumvuta katika upande aliokuwa mzee Mrisho.
   “Tunamuhitaji mtu wetu” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho
   “Mtu gani jamani? Mbona mnanichanganya” Mzee Mrisho aliuliza.
   “Unakumbuka nilichokuambia? Unakumbuka nilikwambia nini nilipoingia hapa?” Mwanaume yule aliuliza huku sauti yake ikisikika kama mtu aliyekasirika.
   “Ndio. Ninakumbuka”
   “Basi tunamuhitaji mtu wetu, hatuna muda mwingi wa kukaa mahali hapa” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho.
ITAENDELEA SIKU YA KESHO.

BALOTELLI KAMA PAPAA, ATINGA MITAANI LIVERPOOL AKIWA NA SIMU TATU

$
0
0
Mara baada ya mechi ya watani dhidi ya Everton. Mshambuliaji nyota wa Liverpool, Mario Balotelli aliamua kuingia mitaani.

Alionekana katika jiji la Liverpool akiwa na simu tatu katika mikono yake miwili, utafikiri Papaa.
Mastaa wengi wa nje wamekuwa wakitumia simu moja tu tofauti na Bongo.
Lakini Balotelli aliokuwa tofauti na mambo yake kumbe ni kama Bongo tu.



A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 03

$
0
0

MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

“Mnataka nini? Mnataka nini jamani?” Mzee Mrisho aliuliza huku hofu ikizidi kuongezeka.
   Hata kabla mwanaume yule hajajibu chochote juu ya kile walichokuwa wakikitaka, Bi Sikujua akatokea sebueni pale. Akaamriwa anyamaze kimya, sauti yoyote kutoka kwake isisikike. Mwanaume mmoja alimsogelea na kumvuta katika upande aliokuwa mzee Mrisho.
   “Tunamuhitaji mtu wetu” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho
   “Mtu gani jamani? Mbona mnanichanganya” Mzee Mrisho aliuliza.
   “Unakumbuka nilichokuambia? Unakumbuka nilikwambia nini nilipoingia hapa?” Mwanaume yule aliuliza huku sauti yake ikisikika kama mtu aliyekasirika.
   “Ndio. Ninakumbuka”
   “Basi tunamuhitaji mtu wetu, hatuna muda mwingi wa kukaa mahali hapa” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho.
SONGA NAYO....
   “Jamani, mtu gani ambaye mnataka mimi niwape?” Mzee Mrisho aliuliza huku hofu ikiongezeka kadri muda ulivyozidi kwenda mbele.
   “Tunamuhitaji mwandishi wa habari. Mwandishi yule mbeya” Mwanaume yule alimwambia.
   “Mwandishi gani jamani?”
   Yule mwanaume hakuongea kitu, mpaka muda huo tayari aliona kama anafanyiwa mzaha, akaivuta bunduki yake kwake na kuikoki hali iliyoonyesha alikuwa tayari kumfyatulia risasi mzee Mrisho. Bi Sikujua alikuwa akilia tu, hakuamini kama muda huo walikuwa wamewekwa chini ya ulinzi na watu ambao walionekana hatari, watu waliokuwa wameshika bunduki.
   “Moja... niambie. Mbili.... niambie. Ta...”
   “Subiri baba. Mimi nitakwambia ukweli” Bi Sikujua alimwambia.
   “Ukweli gani?”
   “Juu ya huyo mnayemtafuta”
   “Tuambie yuko wapi?”
   “Chumbani. Yuko chumbani. Naomba mmuache mume wangu” Bi Sikujua alimwambia.
   “Chumba gani?”
   “Chumba cha tatu koridoni upande wa kushoto” Bi Sikujua aliwaambia.
   “Una bahati sana, mkeo ameokoa maisha yako” Mwanaume yule alimwambia mzee Mrisho.
   Hawakutaka kupoteza muda, wote wakaanza kuelekea katika korido ile na kisha kuanza kuufuata mlango wa chumba kila. Walipoufikia, wakajaribu kuufungua, mlango ulikuwa mgumu hali iliyoonyesha kuwa ulifungwa kwa ndani. Wakaanza kuugonga kifujo fujo lakini mlango wala haukufunguka.
   “Tuuvunjeni” Mwanaume yule aliyeonekana kuwa kiongozi aliwaambia wenzake na hatua za kuuvunja mlango kuanza.
   Ni ndani ya dakika moja tu, mlango ukavunjika. Wakawasha tochi ambazo walikuja nazo mahali hapo na kuanza kumulika ndani ya kile chumba alichokuwa Dominick.
“Yule pale kitandani”  Mwanaume mwingine aliwaambia wenzake na wote kuanza kumfuata Domonick kitandani huku bunduki zao zikiwa tayari.
                                                               ***********
  Kikao cha dharura kilikuwa kinaendelea  kufanyika ndani ya chumba kimoja ambacho kilikuwa miongoni mwa vyumba vizuri vilivyokuwa katika nyumba ambayo ilikuwa ikiheshimiwa sana, nyumba ya kifahari iliyojengwa katika mtaa wa kifahari wa Osterbay.
Watu watatu ambao walikuwa wazee wa makamo ndio ambao walikuwa wamejikusanya ndani ya chumba hicho. Bado ajenda ambayo walikuwa wakiizungumzia katika kipindi hicho haikupatiwa muafaka kabisa. Kwa wakati huo, kila mmoja alionekana kuchanganyikiwa.
Dada waliyemtuma katika kufanya kazi ya kumuita Dominick katika hoteli ya New Africa alifanya kazi kama vile ilivyotakiwa kufanywa. Wasiwasi wao bado ulikuwa juu ya vijana wale ambao waliondoka na Dominick kuelekea katika msitu wa Nyakipande.
Bado hawakupata taarifa yoyote juu ya kilichoendelea msituni. Mara kwa mara walikuwa wakijaribu kuwapigia simu, simu hazikuwa zikipokelewa zaidi ya kuita mpaka kuzima. Mambo haya yote yakaonekana kuwatia wasiwasi.
Kikao kikaendelea zaidi na zaidi hadi kufikia muafaka wa kuwatafuta vijana wengine ambao wangeanza kufuatilia ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea msituni. Kutokana na usiku kuwa umekwenda sana, wakaahirisha kikao ambacho kilitarajiwa kufanyika tena kesho.
Siku iliyofuata vijana watatu wakatafutwa na kupewa mavazi ya kipolisi pamoja na kuwa na mbwa mmoja ambaye angetumika katika kunusa nusa ndani ya msitu ule. Safari ya kuelekea katika msitu wa Nyakipande ikaanza mara moja.
Mara baada ya vijana wale kuingia msituni wakaanza kuwatafuta watu wale ambao walikuwa wametumwa kuifanya kazi waliyopewa jana usiku. Walitembea sana msituni huku wakiongozana na mbwa ambaye alikuwa makini kunusa katika kila njia.
   Hakukuwa na dalili zozote za kuwapata vijana wale kitu ambacho kiliwapelekea kumfuata mbwa kila sehemu alipotaka waelekee. Mbwa aliendelea kunusa ardhini huku akipita katika kila njia ambazo aliziona kuwa sahihi kwake. Ni ndani ya dakika tano tu, wakafika katika eneo ambalo lilikuwa na nyasi fupifupi.
Wote wakaanza kuangalia katika eneo hilo, miili ya watu watatu iliyokuwa na michirizi ya damu ilikuwa ikionekana vizuri machoni mwao. Kwa haraka wakapiga simu kwa wazee wale ambao walikuwa wamewatuma na kuwapa taarifa juu ya kile walichokuwa wamekiona.
“Kama ni hivyo, basi rudini” Sauti ya mzee mmoja iliskika.
“Turudi pamoja nayo?”
“Nini?”
“Hii miili”
“Hapana. Iacheni, hatuna kazi nayo”
“Sawa mkuu”
“Kuna bunduki walizokuwa wanazitumia mahali hapo?”
“Ndio”
“Hizo njooni nazo”
“Sawa” Kijana yule alijibu na kisha kukata simu.
Wazee walionekana kuchanganyikiwa, kitendo cha vijana wao kupigwa risasi na kisha Dominick kutoweka kilionekana kuwachanganya zaidi. Kila wakati walikuwa wakijiuliza ni kwa jinsi gani Dominick aliweza kupambana na vijana wao watatu waliokuwa na bunduki na kuwashinda nguvu.
Walichokifanya baada ya vijana wao kurudi ni kuwapa kazi ambayo vijana wale wengine walishindwa kuifanya. Dominick hakutakiwa kuwa hai tena, tayari alionekana kuwa hatari katika maisha yao kama tu wangemwacha aendelee kuvuta pumzi ya dunia hii.
 Wakawatuma mitaani kuhakikisha Dominick anapatikana na kuuawa. Miezi miwili ilipita na ndipo taarifa za Dominick kufa zikaanza kutapakaa. Wazee wa hawakutaka kukubali kabisa. Ukweli waliujua kwamba Dominick hakuwa amekufa kama ilivyotangazwa, alikuwa hai akiwa amejificha sehemu fulani.
“Mtafuteni katika kila sehemu, ila Mbezi ndio muitolee macho sana” Mzee mmoja aliwaambia vijana wale.
“Sawa mkuu”
Dominick akaanza kutafutwa katika maeneo mengi ya Mbezi. Kazi haikuwa nyepesi hata kidogo, katika kila kona ambayo walikuwa wakifika, Dominick hakuwa akionekana kabisa. Siku ziliendelea kukatika lakini bado Dominick alionekana kuwa adimu kupatikana.
“Kuna tetesi zinasikika kuwa kuna nyumba ina mgeni ambaye hutoka nje usiku sana” Mmoja wa vijana wale waliotumwa na wazee wale, Pius aliwaambia wenzake.
“Nyumba gani?”
“Bado sijaifahamu, ila inatubidi tuendelee kuchunguza”
Uchunguzi wa kuigundua nyumba hiyo ukaanza mara moja, mara kwa mara walikuwa wakiwaaita vijana mbalimbali na kuwauliza swali juu ya nyumba hiyo.
“Hata mimi nimesikia. Ila si unajua umbea, kwanza mtu atakaaje na mtu pasipo kumtoa nje. Huo uzushi” Kijana mmoja alimwambia Pius.
“Kwani nyumba yenyewe ipi?”
“Kwani wewe mgeni maeneo haya? Hata nyumbani kwa mzee Mrisho haupafahamu?” Kijana yule alimuuliza Pius huku akionekana kumshangaa.
“Simjui yeyote huku. Bado mimi ni mgeni, nakaa hapo mtaa wa nyuma. Unamjua mzee Ally Mangushi?” Pius alisema na kuuliza swali.
“Yule mzee mfupi mwenye upara?”
“Ndio. Nyumbani kwake ndipo nilipopanga” Pius alimwambia kijana yule.
Pius hakutaka kuacha kuzungumza na kijana yule, muda wote alikuwa akiongea nae kama njia mojawapo ya kutafuta mazoea. Kijana yule akaonekana kumzoea Pius kana kwamba alikuwa rafiki yake wa muda mrefu.
“Ulisema nyumba ipi?”
“Kwa mzee Mrisho. Mzee mwindaji. Subiri akipita nitakuonyeshea”
“Hapana. Usifanye hivyo, kwani nyumba yenyewe iko wapi?”
“Kule mbele, nyumba yenye bucha kwa nje”
“Nimekwishaikumbuka. Kumbe pale ndipo anapokaa?”
“Ndio hapo hapo”
Pius hakutaka kuendelea kukaa mahali hapo, tayari alikwishaonekana kupata kile ambacho alikuwa akitaka ukipata kwa wakati huo. Moja kwa moja akaanza kuwasiliana na wazee ambao walikuwa wamemtuma na kuwapa taarifa juu ya kile kinachoendelea kwa wakati huo.
“Msimcheleweshe. Mkimpata muueni”
“Sawa. Ila hamtaki hata kiungo kimoja kutoka mwilini mwake?”
“Kama itawezekan, tuleteeni kichwa”
Mipango ikaanza kufanyika usiku huo. Pius akawaita wenzake na kuwaambia kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea. Hawakutaka kupoteza muda, walitaka kumtia mikononi Dominick hata kabla siku nyingine haijafika.
Wakapanga mpango mzima na hatimae wazo la kuzima umeme wa nyumba ile kupewa kipaumbele. Walitaka kuzima kwanza umeme wa nyumba ile kutoka katika chuma la umeme la nyumba ile kwa kutoruhusu umeme kuingia ndani na kisha ndipo wavamie.
“Hilo wazo zuri sana. Tufanyeni hivyo hivyo” Kimbetu alimwambia Pius.
Usiku ulipoingia, kazi ikaanza mara moja Wakaelekea katika duka la vifaa mbalimbali na kununua plaizi kwa ajili ya kukata waya wa umeme ambao ulikuwa ukipitisha umeme katika nyumba ya mzee Mrisho. Mara walipopata kila kitu walichokuwa wakikihitaji, wakajiandaa na kazi.
Usiku ulipoingia, wakasubiri mpaka ifike saa mbili. Muda ulipotimia, moja kwa moja wakaanza kupiga hatua kuelekea katika eneo ilipokuwa nyumba ile.
“Kwa hiyo tunaanza kukata waya?”
“Ndio”
“Basi msitake kupoteza muda, mtakapoona umeme umezimika, pigeni hodi” Jonas aliwaambia.
“Poa” Pius aliitikia na kisha yeye na Kimbetu kuanza kuelekea mlangoni.
Jonas akaanza kupanda katika ukuta wa nyumba ile mpaka pale alipolifikia chuma la umeme na kisha kuchukua plaizi na kuukata waya uliokuwa ukipitisha umeme ndani ya nyumba ile. Umeme ndani ya nyumba ile ukakatika.Pius na Kimbetu hawakutaka kupoteza muda, wakaanza kugonga mlango.
                                                                            *********
Dominick alikuwa amechoka kukaa sebuleni, kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea katika vituo mbalimbali vya televisheni aliviona kuwa kama vikimpotezea muda. Akainuka katika kochi alilokuwa amekalia na moja kwa moja kuelekea chumbani huku akimwacha mzee Mrisho sebuleni pale.
Dominick akapanda kitadani, hata kabla hajachukua muda mrefu kitandani pale, akaanza kusikia minong’ono kutoka nje ya nyumba ile karibu kabisa na dirisha la chumba kile. Kwa kasi ya ajabu, Dominick akainukana kufungua pazia kuchungulia nje.
Vijana watatu walikuwa wamesimama nje karibu kabisa na dirisha la chumba chake. Dominick hakutaka kujiuliza watu wale walikuwa ni wakina nani, moja kwa moja akatoka nje ya chumba kile na kuelekea koridoni ambako akaanza kupiga hatua kuelekea jikoni.
Alipofika jikoni akaufungua mlango na kisha kutoka nje. Dominick akaanza kukimbia kuelekea mbali kidogo na nyumba ile, alipofika umbali fulani, akasimama kwa kujificha katika ukuta wa nyumba moja na kuanza kuchungulia kuona ni kitu gani ambacho kilikuwa kinaendelea.
Kwa mbali akamuona mwanaume mmoja akipanda katika ukuta ambao ulikuwa karibu na chuma lililokuwa limeshikiria nyaya iliyokuwa ikiingia ndani ya nyumba ile. Wala hazikupita hata sekunde ishirini, umeme ndani ya nyumba ile ukakatika.
Vijana wawili wakaanza kupiga hatua kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni ambako baada ya kuufikia, wakaanza kugonga. Wala haukupita muda mrefu, mzee Mrisho akaufungua mlango ule.
Kila kitu ambacho kiliendelea baada ya vijana wale kuingia ndani ya nyumba ile wala Dominick hakuwa akikifahamu. Alibaki pale katika kiambaza cha ukuta huku akiendelea kuangalia kule ilipokuwa nyumba ya mzee Mrisho.
Wala hazikupita dakika nyingi, akawaona wanaume wale wakitoka nje ambako mmoja wao akatoa amri wajitawanye mahali hapo.
“Atakuwa yupo karibu na hapa. Mtafuteni” Sauti ya Pius iliskika na vijana wale wawili kutawanyika kumtafuta Dominick ambaye waliamini kwamba hakuwa mbali na mahali hapo.
Dominick hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, tayari alikwishaona kuwa wanaume wale hawakuwa na amani hata kidogo. Kwa kasi ya ajabu nae akaanza kukimbia kuelekea mbele zaidi ya mtaa ule.
Dominick alipofika katika barabara ya lami, akasimamisha taksi moja ya kukodi na kuingia ndani. Kutokana na mwanga hafifu uliokuwepo ndani ya gari lile, dereva hakuweza kumjua kama mteja ambaye alimpakiza alikuwa Dominick, mwandishi ambaye alisemekana kufa miezi mitatu iliyopita.
Taksi ilisimama nje ya nyumba moja ambayo ilikuwa imezungushiwa ukuta pamoja na kuwa na geti kubwa la rangi nyeupe. Dominick akaingiza mkono mfukoni na kutoa kiasi ambacho kilihitajika na dereva yule kisha kuteremka na kuanza kuugonga mlango.
Mlinzi alisikika akielekea getini pale ambako akafungua geti na moja kwa moja kuingia ndani. Mlinzi akamsimamisha Dominick huku akionekana kukasirika na kitendo kile cha kuingia moja kwa moja katika eneo la nyumba ile pasipo hata ruhusa.
“Mbona unaingia moja kwa moja hata bila kuuliza?” Mlinzi alimuuliza Dominik aliyeonekana kuchanganyikiwa.
“Samahani sana. Akili yangu haiko sawa kabisa. Edmund yupo?” Dominick alimuuliza mlinzi.
“Mbona usiku sana. Wewe nani?”
“Rafiki yake, ninafanya kazi pamoja nae”
“Namba yake ya simu si unayo hapo, kwa nini usimpigie?”
“Hapana. Simu yangu haina chaji. Naomba ukaniitie mara moja” Dominick alimwambia mlinzi ambaye pasipo kuuliza swali jingine akaanza kuufuata mlango na kubonyeza kengele.
Wala haikupita hata dakika moja, mlango ukafunguliwa na mfanyakazi wa ndani. Mlinzi akaanza kumuelezea mfanyakazi yule juu ya Dominick. Msichana yule wa kazi akaondoka na kuelekea ndani ambako baada ya muda, Edmund akatokea.
“Kuna mgeni gani?” Edmund alimuuliza mlinzi.
“Mimi hapa”
“Wewe nani?”
“Sogea karibu”
Edmund akaanza kupiga hatua kumfuta Dominick. Edmund hakuamini macho yake mara baada ya kumfikia Dominick. Hofu ilimjaa moyoni huku mapigo yake ya moyo yakiongeza kasi ya udundaji. Mtu ambaye alikuwa akionekana mbele yake, walikwishamzika miezi mitatu iliyopita, kwake, Dominick alionekana kuwa kama mzimu.
“Dominick!” Edmnd aliita huku akionekana dhahiri kutaka kukimbia.
“Ndio mimi, Edmund”
Edmund akapiga hatua zaidi, alipomfikia Dominick, akamkumbatia kwa furaha. Macho yake hayakuamini kabisa, alijiona kuwa kama ndotoni ambako muda mchache ujao angeamka na kujikuta yuko kitandani.
Wote wakaanza kuelekea ndani ambako wakakaa kochini na kisha Dominick kuanza kumuelezea Edmund kila kitu ambacho kilitokea baada ya kupotea kwake. Edmund alibaki akishangaa, hakuamini kama duniani kulikuwa na mtu aliyekuwa na bahati kama aliyokuwa nayo Dominick.
“Kwa hiyo unamaanisha hauwafahamu kabisa watu wanaokutafuta?”
“Hadi sasa sijafahamu. Ila kuna kitu nataka kukifanya na ningependa msaada wako” Dominick alimwambia Edmund.
“Kitu gani?”
“Subiri”
Dominick akaingiza mkono mfukoni na kisha kuitoa simu yake. Akaiwasha na moja kwa moja kwenda katika sehemu ambayo ilikuwa na kumbukumbu juu ya simu zote zilizoingia.
“Kuna namba hii nataka uende ukaiulizie” Dominick alimwambia Edmund huku akimpa simu.
“Namba ya nani hii?”
“Ya mwanamke yule aliyenipigia siku ile”
“Sasa nitamjua vipi?”
“Nenda katika kampuni hii ya simu, ukifika waambie uongo wowote hadi wakwambie namba hii ni ya nani na anakaa wapi. Tukimpata huyu mwanamke, kila kitu kitakuwa rahisi” Dominick alimwambia Edmund.
“Sawa”
                                                                        **********
Pius akakifuata kitanda kile na kulifunua shuka. Kila mtu alikuwa na uhakika kwamba Dominick ndiye ambaye alikuwa amejifunika kitandani pale. Pius akalifunua shuka, ni mito tu ndio ambayo ilikuwa kitandani pale, ilikuwa imepangwa vizuri.
INAENDELEA NDANI YA WEBSITE YETU HII

A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI) - 04

$
0
0




MWANDISHI: NYEMO CHILONGANI
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

Dominick akaingiza mkono mfukoni na kisha kuitoa simu yake. Akaiwasha na moja kwa moja kwenda katika sehemu ambayo ilikuwa na kumbukumbu juu ya simu zote zilizoingia.
“Kuna namba hii nataka uende ukaiulizie” Dominick alimwambia Edmund huku akimpa simu.
“Namba ya nani hii?”
“Ya mwanamke yule aliyenipigia siku ile”
“Sasa nitamjua vipi?”
“Nenda katika kampuni hii ya simu, ukifika waambie uongo wowote hadi wakwambie namba hii ni ya nani na anakaa wapi. Tukimpata huyu mwanamke, kila kitu kitakuwa rahisi” Dominick alimwambia Edmund.
“Sawa”
                                                                        **********
Pius akakifuata kitanda kile na kulifunua shuka. Kila mtu alikuwa na uhakika kwamba Dominick ndiye ambaye alikuwa amejifunika kitandani pale. Pius akalifunua shuka, ni mito tu ndio ambayo ilikuwa kitandani pale, ilikuwa imepangwa vizuri.
SONGA NAYOOO
Kila mmoja alionekana kukasirika, hawakuamini kama Dominick angeweza kuwafanyia ujanja ule ambao kwao ulionekana kuwa wa kitoto sana. Walichokifanya baada a hapo ni kuanza kumtafuta katika kila kona ya chumba hicho.
 Walifungua kabati na kutoa nguo zote lakini wala Dominick hakuonekana. Hawakuonekana kuridhika hali iliyowapelekea kutoa kila kitu uvunguni mwa kitanda lakini napo Dominick hakuonekana kabisa.
Kila mmoja alionekana kuchanganyikiwa, kumkosa Dominick ndani ya chumba kile ilionekena kuwashangaza kupita kiasi. Kitu walichokifanya mahali pale ni wote kujitawanya na kuanza kumtafuta Dominick. Amri moja tu ndio ambao ilitolewa mahali hapo, kumuua popote pale watakapomuona.
                                                                  *******
   Siku iliyofuata, Edmund akaanza safari ya kuelekea katika jengo la kampuni ya simu za mkononi ya  Etisalat lililokuwa Posta mpya. Tayari Edmund alikwishajua ni kitu gani ambacho alitakiwa kuongea mara tu atakapofika ndani ya jengo lile.
Mara baada ya kufika katika sehemu ya maulizo, akaulizia sehemu ambayo ilikuwa ikipatikana huduma ile ambayo alikuwa akiihitaji kwa wakati ule. Alipoelekezwa, moja kwa moja akaanza kuelekea kule kulipokuwa na chumba maalum.
“Nikusaidie nini?” Sauti nyembamba ya msichana ilimuuliza mara baada ya salamu.
“Kuna namba ya mtu ambaye ananitisha kila siku, ni namba ngeni kwangu, sifahamu anataka nini” Edmund alimwabia dada yule ambaye alikaa kimya kumsikiliza.
“Nafikiri ametumwa, kila siku sina amani moyoni. Natamani kumfahamu mtu huyu ili nijue ni kwa jinsi gani nitaweza kujilinda” Edmund alimwambia dada yule.
“Unafikiri anaishi hapa hapa Dar es Salaam?”
“Sifahamu. Kwa kweli sifahamu”
“Unafanya kazi wapi?”
“Mimi ni mfanyabiashara, mara kwa mara huwa ninasafiri kwenda nchi mbalimbali” Edmund alidanganya.
“Namba yenyewe iko wapi ya huyo mtu?”
Hapo hapo Edmund akaichukua simu yake na kuiangalia namba ile ambapo baada ya kuipata, akamgawia msichana yule. Kazi ya kuanza kuitafuta katika kompyuta yake iliyokuwa mezani ikaanza. Dakika mbili zikakatika, mtumiaji wa namba ile akapatikana.
“Mwenye namba hiyo anaitwa Saida Hamisi. Anaishi Sinza Makaburini” Msichana yule alimwambia Edmund.
“Kumbe Saida! Ni rafiki yangu ambaye mara kwa mara huwa tunataniana sana. Nafikiri amebadilisha namba. Nikitoka hapa, nitanunua laini nyingine na mimi nianze kumzingua” Edmund alimwambia dada yule huku akijifanya kumfahamu Saida.
“Kumbe unamfahamu?”
“Sanaaa. Nimesoma nae kuanzia msingi mpaka chuoni”
“Chuo gani?”
“I.F.M” Edmund alijibu na kisha kuondoka.
Tayari kazi ambayo alipewa alikuwa amekwishaimaliza. Ujanja alioufanya wa kujifanya kumfahamu Saida ulionekana kuwa ujanja ambao haukushtukiwa na msichana yule. Akaingia ndani ya gari lake na safari ya kuelekea nyumbani kuanza huku moyoni akiwa na shauku ya kumpa Dominick taarifa.
“Vipi?” Dominick aliuliza mara baada ya Edmund kuingia ndani.
“Poa. Nimefanikiwa”
“Kweli?”
“Ndio”
“Ni nani?”
“Msichana mmoja anakaa Sinza Makaburini, anaitwa Saida Hamisi” Edmund alimwambia Dominick.
“Safi sana. Huyu ndiye atakuwa mwanzo wa safari yangu ya kuwagundua wabaya wangu” Dominick alimwambia Edmund.
Kazi ya kumtafuta Saida ikaanza. Wakaanza kujiandaa tayari kwa safari ya kuelekea Sinza. Dakika kumi baadae walikuwa ndani ya gari wakielekea Sinza Makaburini. Ndani ya dakika kumi na tano, gari lao likasimama katika eneo lililo karibu na makaburi ya hapo Sinza.
“Samahani” Edmund alimwambia mwanaume mmoja ambaye alikuwa amekaa nje ya saluni moja.
“Bila samahni”
“Kuna dada yangu namtafuta, anaitwa Saida Hamisi”
“Umeelekezwa anakaa wapi?”
“Hapa Sinza Makaburini. Unamfahamu?”
“Mhhhh! Jina lake si geni masikioni mwangu”
“Ulikwishawahi kulisikia wapi?”
“Hapa hapa. Hebu subiri” Mwanaume yule alimwambia na kisha kuingia ndani ya saluni, alipotoka, alitoka na mwanaume mwingine.
“Kuna Saida Hamisi mmoja tu ndiye ninamfahamu”
“Yupi?”
“Anakaa hapo mbele, nyumba yenye rangi nyeupe isiyokuwa na geti” Mwanaume yule alimwambia Edmund.
Edmund akaridhika na kwa jinsi alivyoelekezwa, akarudi garini na kisha kumfahamisha Dominick kile ambacho kiliendelea mahali pale. Gari likawashwa na kisha safari ya kuelekea katika nyumba ile kuanza.
Huku wakiwa wamebakiza umbali mdogo kuifikia nyumba ile, wakashangaa watu wawili kutoka katika gari jingine lililopaki katika eneo la nyumba ile wakiteremka na kuanza kuingia ndani ya nyumba ile kifujofujo.
Tayari Dominick na Edmund walikwishaanza kuhisi kitu, wakatulia garini na kusubiria kuona ni kitu gani ambacho kingeendelea mahali hapo. Wala hazikupita dakika nyingi, wanaume wale waliokuwa wameingia ndani ya nyumba ile wakaanza kutoka huku wakiwa na Saida ambaye alionekana kuwa chini ya ulinzi wao.
“Mh! Kuna usalama kweli hapa?”
“Wala hakuna, kuna kitu nafikiri kinaendelea”
Gari lile likaendeshwa mpaka barabarani na kisha safari ya kuelekea kusipojulikana kuanza. Dominick na Edmund hawakutaka kubaki mahali pale, tayari waliona kuna kitu ambacho kilikuwa kinaendelea mahali pale, wakaanza kulifuatilia gari lile.
“Hapa kuna kitu, tuendelee kufuatilia hivi hivi” Dominick alimwambia Edmund huku wakiendelea kulifuatilia gari lile ambalo likaanza kuingia katika barabara ya Nyerere kuelekea Bagamoyo.
                                                             ********
Kila kitu kilionekana kwenda tofauti na mipango waliyokuwa wameipanga kabla. Kutokufanikiwa kuuawa kwa Dominick kulionekana kuwachanganya kupita kiasi. Kila siku walikuwa wakikutana na kufanya vikao vya dharura, hawakujua ni wapi walitakiwa kuanzia.
Hawakuelewa ni kwa nini vijana ambao walikuwa wakiwatuma walishindwa kabisa kufanya kazi ile ambayo walitaka ifanyike. Dominick alionekana kuwazidi ujanja vijana wao. Walipewa taarifa juu ya uwepo wa Dominick ndani ya nyumba moja iliyokuwa Mbezi, waliwatuma vijana wao kwenda kumuulia huko huko ndani ya nyumba hiyo, lakini cha ajabu, walishindwa kumuua.
Kila kitu kilionekana kwenda shaghalabaghala. Walijiona kuwa na kazi ya kufanya kuhakikisha Dominick anauawa ndani ya miezi hiyo miwili. Mipango ilikuwa ikiendelea kama kawaida lakini walijiona kutakiwa kufanya kitu ambacho kingewafanya kutokujulikana na mtu yeyote juu ya uovu ambao waliufanya.
“Yule msichana” Mzee mmoja aliwaambia wenzake.
“Msichana gani?”
“Tuliyemwambia ampigie simu Dominick amuite pale New Africa Hotel”
“Amefanya nini sasa? Au anahusika na nini kwa sasa?”
“Anaweza akatoa siri ya kila kitu kinachoendelea, si unajua wasichana walivyo”
“Hiyo kweli. Kwa hiyo mnataka tufanye nini ili kujilinda”
“Tumuueni tu, hiyo ndio salama yetu ya kutokujulikana”
Hayo ndio maamuzi ambayo yaliafikiwa katika chumba ambacho walikuwa wamefanya mkutano wa siri. Benard, mvulana ambaye aliwaunganisha wazee hao watatu na Saida akaitwa na kuelezwa kwamba Saida alikuwa akihitajika kwa kazi nyingine mahali hapo.
Benard  akaanza kuwaelekeza mahali msichana huyo alipokuwa anakaa. Hakukuwa na muda wa kupoteza tena, kila kitu kilitakiwa kufanyika kwa haraka haraka. Simu ikapigwa na baada ya dakika kumi na tano, vijana watatu wakaingia ndani ya nyumba hiyo.
“Kuna kazi moja mnatakiwa kufanya”
“Kazi gani bosi?”
“Kuna msichana tunataka apotee haraka iwezekanavyo”
“Msichana gani”
“Saida”
“Yule ambaye mlimshirikisha kipindi cha nyuma?”
“Ndiye huyo huyo” Mzee huyo aliyeonekana kiongozi kati ya wazee wale aliwaambia.
Akaanza kuwapa maelekezo juu ya mahali ambapo Saida alipokuwa akiishi kwa wakati huo. Maelekezo yalichukua dakika tano, vijana wote wakaonekana kuelewa mahali ambapo Saida alipokuwa akikaa.
“Kwa hiyo tumuue humo humo ndani?”
“Hapana, mchukueni na mumpeleke sahemu yoyote ile. Mtakapomuua, tuwasiliane basi”
“Sawa bosi”
Vijana wale wakaanza safari ya kuelekea Sinza huku akili yao ikiwa na lengo moja tu la kufanya mauaji. Wakaziangalia bunduki zao ambazo zilikuwa na risasi za kutosha. Walichukua dakika kumi na tano mpaka kufika Sinza Makaburini ambapo wakateremka na kuanza kuelekea ndani ya nyumba ile iliyokuwa imepakwa rangi nyeupe. Hawakupiga hodi, wakaingia ndani.
Saida alikuwa amekaa kochini huku akiangalia filamu ya Kitanzania iliyoigizwa na msanii Steven Kanumba. Ghafla akashtuka kuona watu watatu waliokuwa na bunduki wakiingia ndani. Hata kabla hajafanya kitu chochote kile, akashtuka akivamiwa na kuwekwa chini ya ulinzi.
“Ukipiga kelele, ukionyesha mgomo wowote au ukiuliza swali, roho yako itakuwa halali yetu” Pius alimwambia Saida ambaye alikuwa akitetemeka tu.
Wote wakaanza kuelekea nje huku Saida akiendelea kuwa chini ya ulinzi wao. Walipotoka nje, wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea Bagamoyo kuanza. Saida hakuongea ktu chochote kile, alitamani kuulza juu ya kile kilichokuwa kinaendelea mahali hapo lakini kila alipokuwa akikumbuka maneno ambayo aliambiwa, alishindwa kuuliza.
“Mungu nisaidie... Mungu niokoe...” Saida alijikuta akiomba moyoni.
                                                           ************
Dominick na Edmund bado walikuwa wakilifuatilia gari lile ambalo lilikuwa likeonyesha kwamba lilikuwa safarini kuelekea Bagamoyo. Hawakutaka kuliacha zadi ya mita ishirini, walikuwa wakiliangalia katika kila kona.
Bado walikuwa wakimhitaji Saida kuliko mtu yeyote katika kipindi hicho. Safari iliendelea zaidi na zaidi mpaka kufika katika sehemu ambayo kulikuwa na pori la Mapinga. Gari likakata kona, likaacha barabara ya lami na kuingia katika barabara ya vumbi.
Safari iliendelea zaidi na zaidi mpaka kufika katika sehemu ambayo haikuwa na dalili ya uwepo wa nyumba yoyote ile. Pius na wenzake wote wakateremka huku wakiwa na Saida na kisha kuanza kuelekea ndani ya msitu huo.
Dominick na Edmund wakalipita gari lile na kwenda kulisimamisha gari lao mbali na sehemu gari lile lilipokuwa. Wote wakateremka na kuanza kuelekea kule gari la Puis na wenzake liliposimama, walipofika karibu na eneo lile, nao wakaingia ndani ya pori lile kwa mwendo wa kunyata.
Sauti ya Sauda ilikuwa ikisikika ikipiga kelele, Dominick na Edmund wakajificha na kuanza kuchungulia kule kelele zilipokuwa zikisikika. Saida alikuwa amekaa chini huku akilia, Pius na wenzake walikuwa wameshika bunduki, walionekana kujiandaa kummiminia risasi Saida.
“Sali sala yako ya mwisho” Pius alimwambia Saida.
“Nitasali...nitasali ila kuna siri nataka kuwaambia” Saida aliwaambia.
“Unasemaje? Siri? Siri gani?” Pius alimuuliza Saida.
“Mtakaponiua mimi, na ninyi lazima mtauawa” Saida aliwaambia maneno ambayo yalionekana kuwashtua.
“Tutauawa? Kivipi?”
“Wanaona kwamba kama wakiniacha mimi nitatoa siri, lakini kwa upande mwingine, wamepanga kuwamaliza hadi ninyi, kwani watapowaacha siri itavuja juu ya uovu waliomfanyia Dominick. Kwa hiyo na ninyi lazima mtauawa” Saida aliwaambia.
Pius akashusha bunduki yake. Maneno aliyoyaongea Saida yalionekana kuwa na ukweli kabisa. Kila kitu ambacho walikuwa wakikifanya wazee wale kilikuwa siri kubwa ambayo hawakutaka ijulikane na mtu yeyote yule, hiyo ndio sababu ambayo iliwapelekea kuwatuma wao kumuua Saida.
Hawakujua ni nani angeuawa baada ya Saida. Hawakuwa na uhakika kama wazee wale wangewaacha hai kama wangekamilisha kila kitu, walijiona nao wao kuuawa kama alivyosema Saida.
“Ila kweli. Na sisi tunaweza kuuawa” Pius aliwaambia wenzake.
“Kwa hiyo tufanye nini sasa?”
“Tuondokeni”
“Tuondoke pasipo kumuua?”
“Ndio. Hauoni kama ameyaokoa maisha yetu!”
“Na wazee wakituuliza tuseme nini?”
“Kwamba tumeishafanya kazi waliyotutuma”
“Poa”
Pius na wanzake hawaktaka kuendelea kukaa mahali pale, walichokifanya ni kuanza kuondoka kurudi Dar es Salaam. Hawakutaka kuondoka na Saida, walitaka kuondoka peke yao.
“Wewe utarudi Dar peke yako” Pius aliwmwambia Saida na kisha wao kuondoka.
Saida akaanza kusali sala ya shukrani, hakuamini kama alikuwa amenusurika kuuawa katika tukio lile. Mara baada ya kumaliza kusali, akainuka kwa lengo la kuondoka, lakini hata kabala hajaondka, akashtukia akiwekwa chini ya ulinzi.
“Dominick.....!” Saida aliita kwa mshangao.
“Ndio mimi Saida. Sali sala yako ya mwisho. Ni lazima nikuue na ndio niende kuwaua watu waliokutuma” Dominick alimwambia Saida huku akionekana kukasirika.
“Naomba unisamehe Dominick. Naomba usiniue” Saida alimwambia Dominick huku akianza kulia.
“Ni lazima nikuue. Wewe si ulifanya mipango ya mimi kuuawa! Kuna sababu gani ya kukucha hai?” Dominick alimwambia Saida huku akiikoki bunduki yake.
“Naomba unisamehe” Saida alimwambia Dominick huku akipiga magoti mbele yake.
Dominick hakuongea kitu chochote kile, alibaki kimya akimwangalia Saida ambaye alikuwa akilia kama mtoto. Kila akikumbuka shida ambazo alizipata porini pamoja na mambo mengi yaliyotokea maishani mwake, alijiona kuwa na sababu ya kumuua Saida.
“Nisamehe Dominick....naomba unisamehe” Saida aliendelea kuomba msamaha.
“Kama utataka nikusamehe, nijibu juu ya kila swali nitakalokuuliza” Dominick alimwambia Saida huku akitetemeka kwa hasira.
“Nitakwambia. Niulize nitakwambia.....”
“Ni nani yuko nyuma ya haya yote? Ni nani ambaye aliiangamiza familia yangu? Ni nani ambaye anataka kuniua? Niambie maana ya maneno BoT kama kirefu chake si Bank Of Tanzania. Ninaitaka maana yake iliyomaanishwa na wauaji hawa” Dominick aliuliza maswali matatu mfululizo.
“Nitakwambia…nitakwambia Dominick”  Saida alimwambia Dominick na kuendelea
“BoT ni kifupi cha majina matatu ya watu watatu wanayoyafaya haya” Saida alimwambia Dominick huku akiwa amepiga magoti karibu na miguu ya Dominick.
“Watu gani hao? Niambie ni watu gani hao” Dominick aliuliza kwa kukalipia huku akionekana kuwa na hasira.
“Mawaziri, mawaziri. Waziri Bonifasi wa Mali asili na Utalii, waziri Ombeni wa Miundombinu na waziri Tumaini wa Mambo ya Ndani” Saida alimwambia Dominick.
Dominick akaonekana kuchoka, hakuamini kile ambacho alikisikia masikioni mwake. Watu ambao walitajwa mahali hapo aliandika wizi wao wa mamilioni miaka miwili iliyopita, hakujua kama watu hao bado walikuwa na kisasi juu ya maisha yake.
“Yaani bado walikuwa na kisasi na maisha yangu mpaka wakaiangamiza familia yangu?” Dominick aliuliza huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Edmund...Edmund...yaani watu hawa ndio waliiangaliza familia yangu? Ni lazima niwaue, ni lazima niangamize familia zao pia kama walivyoiangamiza yangu. Tena nitaziangamiza kwa kuzichoma moto na kisha kuwaua wao wenyewe. Ni lazima Edmund. NI LAZIMA……!!!” Dominick alimwambia Edmind huku akilia kama mtoto. Mwili wake ukabaki ukitetemeka kwa hasira, kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo alizidi kutetemeka kwa hasira.
“NI LAZIMA NIWAUE….” Dominick alisema kwa hasira huku akiondoka mahali hapo kwa mwendo wa kasi kuelekea kule walipolipaki gari.

USIKU WA KIGODORO - 03

$
0
0

ILIPOISHIA:
Mume wa Lina, Semi alishtuka, akaangalia alipolala mkewe akagundua hayupo na ametoka na simu. Kwa mbali alimsikia akiongelea kutokea chooni, akaamka…
SASA JIACHIE…
ALITEMBEA kuelekea chooni lakini alikutana naye anatoka…
“Vipi, mbona kama unaongea na simu chooni?”
 “Si mama Pendo huyo, saa zile naamka kuja chooni na yeye akapiga sasa nilibanwa na haja ikabidi nije huku naongea naye.”
“Anasemaje muda huu?”
“Anasema hajalala tumbo,  nikiwa na nafasi asubuhi nimpeleke hospitali.”
“Shemeji naye, mbona hospitali ni karibu na kwake? Yaani we utoke huku mpaka kule halafu umchukue kurudi naye hospitali au yu mahututi?”
“Hamna, kwanza mpaka akuambie mwenyewe ndiyo utajua anaumwa, mimi mwenyewe sikujua  mpaka aliponiambia.”
Kulipambazuka kabisa, Lina alijiandaa mumewe naye alijiandaa, wakatoka wote. Lina alishushwa nje ya ofisi yake mumewe akaendelea na safari.
Ile anakaa tu, Lina akashika simu kumpigia James…
“Baby…”
“Yes baby, niambie.”
“Nimeingia job baby.”
“Safi sana, mimi ulivyoniamsha nikaoga lakini sijatoka nyumbani.”
“Oke. Sasa baby nyumbani unaishi na nani?”
“Niko na wasaidizi wa kazi watatu.”
“Watatu wa nini wote hao?”
“Mmoja ni mwanamke mtu mzima, ndiyo huwa anapika na kufua. Wa pili wa kiume kijana, huyu anatunza mazingira na wa tatu ni mlinzi getini.”
“Du! Kweli baby unatakiwa kuoa sasa baby wangu.”
“Kha! Kwani unadhani ni kwa nini nilikuomba uwe mke wangu Lina? Kwanza nimekupenda, pili una sifa za kuwa mke. Wewe Lina ni wife material.”
Lina alicheka kidogo, akafurahi, akaendelea…
“Sasa unatoka saa ngapi?”
“Eee, kuna email nazisubiria kwa hapahapa nyumbani nataka kutuma mzigo Ufaransa kwa hiyo naseti mawasiliano.”
“Naweza kuja?” alisema Lina kwa kusitasita, moyoni aliamini James hawezi kukubali hilo la yeye kwenda kwake.
“Wao, karibu sana Lina, tena nitafurahi sana kukuona hapa kwangu.”
Lina hakuamini masikio yake, akashangaa na kumuuliza James…
“Kweli baby?”
“Yeah! Njoo, chukua teksi nitalipa mimi hapa.”
“Ni wapi?”
“Mbezi.”
Lina alikata simu, akaingia kwa mabosi wake na kuomba ruhusa ya dharura akaruhusiwa, akaondoka.
Alitembea kwa mwendo wa haraka hadi kituo cha teksi, akaingia kwenye mojawapo…
“Twende Mbezi Beach tafadhali.”
Safari ilianza huku Lina akiwa na mshawasha wa moyo, alikuwa na maswali kadhaa…
“Je, James akitaka kuduu na mimi?” alijiuliza mwenyewe.
“Mh! Kwa kweli kwa jinsi alivyonilaza na njaa jana sitakuwa na sababu, nitakubali tu. Maana mh! Hata hivyo, ni nafasi ya pekee ya mimi na yeye kukutana kimwili kwa mara ya kwanza tena nyumbani kwake.
“Ni heshima kubwa sana atakuwa amenipa, maana angekuwa mwanaume mwingine asingekubali kuniita kwake, angeweka kikwazo.”
Lina alipoingia Mbezi ya Tangi Bovu alimpigia simu James akapewa ramani halisi ya kufika kwake. Ilikuwa ramani rahisi sana kwani walifika hadi nje ya geti, honi ikapigwa, geti kubwa likafunguliwa.
“Umeambiwa ingiza gari ndani,” mlinzi alimwambia dereva akimchungulia kwa kutumia kioo cha dirisha.
“Sawa,” teksi ikaingizwa ndani, Lina akashuka.
Ile anashuka tu, James anatokea ndani kwa mlango mkubwa…
“My wife to be,” alisema James akiachia tabasamu pana huku mikono ameipanua tayari kwa kumkumbatia Lina…
“Yes Lina’s husband.”
Walikutana wakakumbatiana, Lina akamuwahi mabusu James kama matatu, naye akarudishiwa, wakaingia ndani huku James amemkumbatia Lina kwenye kiuno.
Lina alishangazwa sana na mazingira ya nyumba hiyo. Licha ya kuambiwa mlikuwa na watu watatu na mwenyewe James wa nne, lakini ilionekana kama wanaishi watu kumi na mbili.
Maana alipozama sebuleni tu, akatokea yule mwanamke, akamkaribisha Lina kwa adabu zote licha ya kwamba alikuwa mama mtu mzima, kabla hajatoka akatokea kijana mtunza mazingira huku mlinzi naye akiingia na boksi na kuliweka sehemu kisha akatoka.
Lina alishangazwa pia na ukubwa wa sebule kwani alikuwa kama yupo kwenye ‘nusu uwanja’ wa table tennis. Mbali na ukubwa huo alishangazwa na samani za ndani licha ya usasa wake lakini hizo hakuwahi kuziona tangu azaliwe.
“Enhee, za kazi baby?”
“Poa, vipi wewe?” aliitika Lina.
“Mimi mzima sana, namshukuru sana Mungu. Lakini namshukuru zaidi kwa kukuleta wewe hapa leo.”
“Mimi mwenyewe nimefurahi sana kwa kunikubalia kuja kwako leo,”
alisema Lina huku akipepesa macho sehemu mbalimbali za sebule hiyo, akampongeza James kwa kuwa na nyumba nzuri kama ile.
Baada ya salamu, James aliwaita wafanyakazi wake wote, wakafika na kukaa kwenye sofa, kila mmoja yake…
“Huyu anaitwa Lina, ni mtoto wa mzee Joseph Ambakucha pale Kijiji cha Kilole, Korogwe Tanga. We mama si umetokea Korogwe pia?” alihoji James akimwangalia mwanamke anayemsaidia kazi za ndani…
“Ndiyo, hapohapo Kilole. Na mzee Joseph Ambakucha namfahamu sana.”
Lina alimtumbulia macho, akahisi kama mwanamke huyo anaweza kuharibu mambo japokuwa yeye hakuwa anamkumbuka kwa sura…
“Na wewe mama umeishi pale?”
“Ee! Mimi nilikuwa naishi Mgandini, wengi wananijua kwa jina la mama Tabu, nyumba yangu iko jirani na ya mzee Hussein, yule ana watoto akina Sakina, Said, Mariam...”
“Ooo! Sakina, Said wote nawakumbuka. Lakini wewe sikukumbuki kabisa…”
“Si rahisi lakini dada zako, kaka zako nawajua. Namjua Kiliana, Josephine, Anna na Yonasi.”
Basi, baada ya hapo, James akaendelea…
“Huyu sasa ndiye mchumba wangu niliyewaambia nimempata mtu wa Korogwe, Tanga ndiyo huyu.”
“Lakini sasa mbona ana pete ya ndoa kwenye kidole?” alidakia yule mwanamke.
Kumbe siku hiyo Lina aliamua kuvaa pete bwana, akasahau kuivua wakati anakwenda nyumbani kwa James.
James alishtuka sana, Lina pia alishtuka lakini akajikaza asijulikane, kilishanuka…
“Mungu wangu…Mungu wangu,” alisema moyoni…
“Eti Lina! Ni nini hiyo mpenzi? Kumbe unanisaliti?”
“Hamna! Kwa sababu nyie hamtembei sana mitaani. Siku hizi wanawake wengi wanavaa pete za ndoa ili kukwepa usumbufu wa wanaume. Mwanaume akikuona una pete ya ndoa heshima inaongezeka kidogo…”
James alitazamana na yule mwanamke anayemsaidia kazi za ndani, mwanamke akasema…
“Hiyo ni kweli, hata mimi nakubaliana na wewe. Japokuwa kuna wanaume hawajali hata kama una pete ya ndoa lakini inasaidia kupunguza upungufu.”
“Ni kweli.”
James alikubaliana na hilo kwa kutingisha kichwa huku akimwangalia Lina kwa macho yaliyojaa mahaba mazito…
“Vipi baby?” aliita Lina akimwangalia James…
“Poa tu.”
Wakati huo wale wote walioitwa kutambulishwa walishaondoka. Walibaki wawili tu.
“Hapa ndiyo nyumbani kwako?”
“Yeah! Hapa ni nyumbani.”
“Da! Bonge la jumba. Ukisikia jumba la kifahari ndiyo hili.”
“Kweli Lina?”
“Sana tu, hongera sana bwana. Kwanza bado kijana mdogo lakini umejitahidi sana.”
“Asante baby, ndiyo maana nataka tufunge ndoa ili uje kuipamba nyumba hii.”
“Hilo tumwombe sana Mungu atupe afya na uzima.”
James alisimama na kwenda chumbani kwake, nyuma Lina akawa anashangaashangaa mapambo ya nyumba hiyo yalivyokuwa na mvuto.
Mara James alitokea. Moyoni aliamini ni siku mwafaka sana kwake kuivunja amri ya sita na Lina lakini alikuwa haamini kama atakubaliwa kwani msichana mwenyewe alitoka kazini na angerudi tena kazini…
“Labda mjaribu, akisema siku nyingine sawa,” sauti ilisema ndani ya moyo wa James.
“Baby sasa, si umechoka sana ukaoge upumzike kidoo kitandani, au?” alisema James huku akiangalia pembeni kwani alijaliwa kitu kinaitwa aibu.
“Poa. Lakini nikioga nitabadili nini sasa?”
“Kwani mpaka ubadili, si unavua hizo, unaoga unavaa taulo ukilala, ukiamka unaoga tena unavaa hizo unaondoka.”
“Poa.”
“Basi simama twende.”
Lina alisimama akatembea huku akiivua ile pete ya ndoa na kusema moyoni…
“Ilitaka kuniletea balaa bure, bahati njema nimepata mwanaume mwelewa.”
Aliingia kwenye chumba cha James na kukutana na vitu vya samani ambavyo hakuvitarajia. Kitanda cha kisasa, sofa moja kubwa, stuli ndogo mbili na kitu kama meza fupi sana kwa ajili ya kupandia kitandani.
Lina alishangaa kuona ndani ya chumba hicho kila kitu ni cheupe au kimechanganywa na rangi ya krimu. Mashuka meupe, pazia jeupe, kapeti krimu, foronya nyeupe, dari nyeupe, mlango hadi madirisha na makabati.
Kilichomshangaza sana Lina na kuona chumba hicho hakina choo na bafu kwa maana ya ‘master bedroom’ kama ambavyo alitarajia…
“Mh! Bonge la chumba, kila kitu kimehusika lakini amekosa kitu kimoja tu, choo cha ndani,” alisema moyoni Lina. Lakini moyoni alisifia chumba hicho kilivyo na nyumba nzima kwa ujumla kwamba ni ya kisasa.
“Sasa ukaoge my love,” alisema James. Lina akasimama na kupokea taulo kutoka kwenye mikono ya kijana huyo. Alichojoa nguo zake zote, akabaki kama alivyozaliwa kisha akajijaladia na taulo sasa, akawa anatembea kwenda mlango mkubwa…
“Bafu liko uani au?” aliuliza Lina…
“Oooh! Sorry, bafu lile pale,” James alimwelekeza Lina bafu ambapo kwa Lina alipoona mara ya kwanza alijua pana kioo kikubwa kumbe ni mlango wa kuingilia bafuni, alijisikia aibu kubwa kwa ushamba.
“He! Sikujua mpenzi wangu, samahani,” alisema Lina huku akimfuata James na kumkumbatia kisha akampiga mabusu mawili ya pande mbili za mashavu.
James alionesha kusisimkwa mwili, naye akamkumbatia, wakatazamana. Ilikuwa ni kitendo cha mara yao ya kwanza tangu waanze kufahamiana siku kadhaa nyuma.
Lina alisisimka sana, James pia. Walijikuta wakigandana na baadaye walipanda kitandani huku Lina akiwa ametupa taulo chini…
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

USIKU WA KIGODORO - 04

$
0
0

 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

“Baby,” aliita Lina kwa sauti tamu sana ambayo kwa mwanaume yeyote rijali angevutwa nayo hata kama angeisikia kwenye simu tu.
“Yes dear,” alipokea James akiwa kwenye macho yaliyojaa ulegevu wa mahaba ingawa hakumshinda Lina ambaye alikuwa mbendembende.
“Nahisi naota.”
“Kwa nini baby?”
“Hivi kweli?”
“Kweli nini?”
“Nipo kitandani na wewe leo?”
“Hata mimi siamini Lina, wewe ni mwanamke niliyetokea kukupenda sana. Napenda ujivunie kwa hilo baby.”
“Asante dear jamani,” alisema Lina akiwa anamshikashika James sehemu ya mgongoni.
Mechi ilianza kwa Lina kumsoma James kwamba ni mwanaume wa namna gani, anayependa nini kwenye ‘uwanja’ na nini hapendi. Kwa hiyo alichokuwa akikifanya Lina na kufanya tukio halafu ‘kumsikilizia’ James kwamba ‘anariakti’ vipi!
Mfano, katika kugalagaza, Lina alipeleka mdomo wake kwenye sikio la kijana huyo na kumpumulia kwa nguvu, James akawa hoi.
Kumbe James naye alikuwa kama Lina. Kwa sababu ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana kwenye mechi,  Naye alijitahidi kusaka sehemu ambazo ni za msisimko kwa Lina. Alipeleka vidole kwenye kifua na kuzishika nido kwenye misumari yake ambapo Lina akawa kama amepoteza fahamu.
Kama vile hiyo haitoshi, James alipotoa mikono kwenye nido akavipeleka kwenye sehemu kuu na kumfanya Lina kuwa hoi bin taaban huku akisema maneno ambayo ili uyasikie ni lazima kulaza sikio kwenye kinywa chake…
“Baby tayari sasa,” James alimsikia akisema hayo baada ya kumsogelea kwa karibu ili kumsikiliza. James hakutaka kumsikiliza, akaamua kwenda mbele zaidi ambapo alipeleka vidole kwenye sehemu ya kukanyangia mguuni kwa Lina, kilio kikubwa kikasikika kutokea chumbani humo lakini kwa jinsi mlango na madirisha yalivyokuwa hata kama mtu angesimama kuemea mlango asingesikia kitu.
James alizidisha manjonjo kwa kumpapasa Lina sehemu ya nyuma ya magoti ambapo Lina alibaki ameduwaa, uwezo wa kusema lolote hakuwa nao tena.
James aliianzisha mechi kwa kupuliza filimbi uwanjani yeye mwenyewe, Lina akaipokea huku akimwimbia nyimbo mbalimbali za mahaba mpenzi wake huyo ilimradi mchezo uwe mzuri huku jasho likifichwa kwa kasi ya utulivu ndani ya uwanja.
Ni ndani ya dakika kumi tu, Lina akatangaza ushindi wake wa kwanza dhidi ya James huku akipokea mashambulizi ya piga nikupige bila kubutua.
Ndani ya dakika tano tena mbele, Lina akatangaza kupata ushindi mwingine wa pili huku James akiendelea kupeleka mashambulizi yenye kumpa ushindi mrembo huyo.
“Baby,” aliita Lina mara baada ya ushindi wa pili…
“Yes…”
“Upo vizuri darling.”
“Kweli?”
“Sana.”
Maneno ya Lina yalimsukuma James ambaye naye papo hapo akapata ushindi wake wa kwanza huku Lina baada ya kumsikia mwanaume wake akiwewesekea ushindi na yeye akaupata wa tatu wa bure kabisa.
Wote wakawa wanahema kwa kasi, hakuna aliyemsemesha mwenzake. Sanasana kuna wakati James alinyoosha mkono na kushika rimoti ya AC na kuongeza kidogo spidi ya kutoa baridi. Hapo, Lina alikuwa akimwangalia James kwa mbali kwa macho ambayo kama anayafumba lakini hajayafumba kabisa, unaweza kusema alikuwa akisinzia.
James alidondoka na kulala ubavuubavu akimwangalia Lina ambaye naye alipeleka mkono wake kwenye kiuno cha mpenzi wake huyo na kukishikashika kama moja ya mbwembwe ndani ya uwanja wa mapenzi.
Baadaye sana, wawili hao walirejea katika ungangari wao, walianza kuzungumza…
“Sweet,” aliita Lina kwa sauti ya chini sana…
“Yes,” James aliitika kwa sauti nzito.
“Nakupanda sana. Sijui itakuwaje?”  alisema Lina huku James akiwa hajui nini maana ya kauli yake hiyo.
“Baby, kwa nini umesema hujui itakuwaje? Kwani si tumeshapanga kufunga ndoa au?”
“Ungejua niko kwenye ndoa mwenzako wala usingesema hivyo,” alisema moyoni Lina lakini kwa sauti akasema…
“Unajua siamini kama hiyo siku itafika dear.”
“Kwa nini isifike my love? Itafika tu, sisi kinachotakiwa ni kumwomba Mungu tu basi,” alisema kwa ujasiri mkubwa James.
***
Saa kumi na mbili, James alimwingiza Lina ndani ya gari kumrudisha nyumbani na si kazini kama alivyotoka. Ndani ya gari, kiyoyozi kilikuwa kwa kiwango cha juu huku Lina akifurahia maisha na kusema moyoni kwamba alipata mwanaume wa kweli na kulaani ni kwa nini aliwahi kuonana na mumewe, Semi na si James.
Lina alimwelekeza James na kuiegesha gari jirani kabisa na nyumbani kwake huku akimwambia…
“Kama nilivyokwambia dear, dada yangu ni noma sana baby, kwa hiyo nishushe hapa.”
“Oke. Lakini baby vumilia tu iko siku yatakwisha mke wangu. Tukifunga ndoa shemeji atatulia, ukali wote utaisha,” alisema James akimkazia macho Lina. Lina aliachia tabasamu laini lakini kila wakati alionesha kutaka kuendelea kuwa na James.
Ukweli ni kwamba, Lina aliamua kushuka pale ili kukwepa mtego wa kukutana na mumewe ambaye alijua akigundua hilo pangechimbika ile mbaya.
Wakati anashuka, Lina alimpa mdomo James, akaachia ulimi, ukapokelewa kwa kuvutwa kwa dakika kama moja nzima huku mrembo huyo akionesha kusisimka sana…
Mara, simu yake iliita, kuangalia namba ni mume wake…
“Haloo baby…”“Nahisi nimekupita ukiwa ndani ya gari upo na nani?”
“Ni rafiki yangu mbona, amekataa kufika nyumbani, ndiyo kageuza sasa hivi hapa,” alisema Lina huku akishuka kwenye gari hilo na kuanza kutembea bila kuagana na James ambaye alishikwa na mshangao.
James hakutaka kumuuliza kitu Lina, akaweka gia ya kurudi nyuma kisha akageuka na kuondoka. Lakini kichwani alipata tabu na kauli ndogo tu ya Lina ukiachilia mbali kule kuondoka. Nayo ni ile aliyoitoa wakati akipokea simu…
“Haloo baby…”
“Huyo baby ni nani? Ina maana Lina ana mwanaume mwingine? Haiwezekani…kama ni kweli nitatumia uwezo wangu wote nisambaratishe penzi lao,” alisema moyoni James huku akiingiza gari lake barabara kuu.
***
Lina aliendelea kuzungumza na mume wake kwa simu akijisafisha huku akikaribia nyumbani lakini alipomaliza ndipo akamkumbuka James na mazingira ya kuachana kwao muda mfupi uliopita…
“Haloo baby…”
“Daaa! Sasa pale si atakuwa ameshangaa, haloo baby, baby ndiyo nani wakati nilimwambia sina mpenzi tuliachana? Nimechemsha kweli. Nilichotakiwa kukifanya pale ni kutopokea simu ya mista,” alisema moyoni Lina, akajikuta akiumia sana.
Alisimama nje ya duka moja kabla hajafika nyumbani kwake, akampigia simu James…
“Lina,” James aliitika kwa sauti nzito…
“Baby nisamehe sana…”
“Kwani kulitokea nini Lina mpenzi?”
“Da! Yaani, unajua nini my love?”
“Ee…”
“Kuna yule jamaa yangu niliyekwambia tumeachana, ndiye aliyenipigia…”
“Sasa baby kama ni yeye, ndiyo uondoke bila kuniaga?”
“Unajua nini my love?”
“Sijui…”
“Alichonitendea, kila akipiga simu nahisi kukasirika.”
“Sasa kama ni hivyo,  mbona ulivyopokea ulisema haloo baby?”
“Da! Ni mazoea yangu, mabaya sana. Napenda sana kusema baby hata kwa mwanaume ambaye si mpenzi wangu.”
“Basi uache tabia hiyo kuanza sasa, sawa Lina?”
“Sawa mpenzi wangu, nisamehe.”
“Poa, yameisha.”
“Nashukuru baby, sasa naingia ndani ukinitaka unitumie sms kama nilivyokwambia sista mnoko kweli, ananifanya mimi kama mtoto wake, tena wa chekechea.”
“Usijali d, ila na wewe ukiwa katika mazingira mazuri nipigie, sawa?”
“Sawa d.”
Lina alizama ndani kwake akiwa na amani baada ya kumaliza ishu nzito na James ambaye alimwita mchumba ingawa wakati mwingine alipokuwa amekaa mwenyewe alijiuliza nini hatima ya uhusiano wake huo.
***
Baada ya hapo, mapenzi yaliimarika zaidi na zaidi hadi ikafika hatua ya kukubaliana kuhusu ndoa ambapo vikao kwa James vilianza na Lina aliwahi kuhudhuria kama mara tano hivi.
Kwa upande wake, Lina aliweka kikao kwa ajili ya kitchen party tu ambapo alimtumia rafiki yake Agnes kumsimamia wakisingizia kwamba, hakuwa na ndugu jijini Dar.
Ndugu wa Agnes, kama mashangazi na rafiki zake wengine, akiwemo mama mkubwa walibeba jukumu la kusimamia sherehe hiyo mwanzo mwisho.
Siku ya kwenda kwenye sherehe ya kitchen party, Lina alimwomba ruhusa mume wake, Semi siku moja nyuma akimwambia kutakuwa na kitchen party ya rafiki yake.
Siku ya shughuli mumewe alimuuliza kisa cha kuondoka akiwa amebeba nguo kwenye begi badala ya kuvalia nyumbani, Lina alisema…
“Hili gauni nikilivalia nyumbani nitakuwa kituko mtaani, nitakwenda kuvalia kwa Eg…”
“Kwani lina nini hilo gauni?”
“Limeshonwa kwa madoido sana baby, linafaa kuvaliwa ukumbini tu.”
“Hebu tulione.”
Lina alisita kwanza akidai muda unakwenda, lakini akalitoa…
“Khaa! Sasa mbona gauni lenyewe limeshonwa kama wewe ndiye bi harusi mtarajiwa?”
“Hamna! Unajua wamealika ngoma ya kigodoro ndiyo maana magauni wamesema yawe hivi.”
“Oke poa.”
Lina aliondoka mpaka kwa Eg, akapokelewa kwa shangwe na ndugu wa Eg ambao walikuwa hawajui kama bi harusi huyo ni mke wa mtu tena kwa ndoa ya kanisani kabisa.
Akiwa kwa Eg, Lina alimpigia simu James…
“Baby, uko wapi?”
“Niko kwa Eg darling.”
“Kwa hiyo ndiyo kama hivyo, leo hatuonani siyo?”
“Hatuonani labda usiku sana maana si unajua kitchen party si ya wanaume baby?”
“Poa, kuna nini kimepungua?”
“Hakuna dear.”
Wakati mazungumzo yakiendelea, mume wa Lina alifunga breki nje ya nyumba ya Eg na kupiga honi ana shida na mke wake huyo…
“Pii pii piii!”    

ITAENDELEA SIKU YA KEHOOOOO
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

NINI CHA KUFANYA MPENZI WAKO ANAPOWASILIANA NA EX WAKE?-2

$
0
0
Shukrani ziende kwake Muumba ambaye kwa mara nyingine ametupa nafasi ya kukutana kwenye uwanja wetu huu, tukijuzana, kuelimishana na kubadilishana mawazo kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo uhusiano wa kimapenzi.Wiki iliyopita tulianza kuijadili mada hii kama inavyosomeka kwenye kichwa cha habari kuhusu hatua unazopaswa kuzichukua unapogundua kuwa mpenzi wako, mumeo au mkeo ana mawasiliano na mpenzi wake wa zamani (ex wake).
Tulianza na mfano halisi wa jinsi mwanamke mmoja aliyeishi na mumewe kwa kipindi kirefu na kufanikiwa kupata watoto, alivyoumia baada ya kugundua kuwa mumewe ana mawasiliano na mpenzi wake wa zamani kiasi cha kutamani hata kuyakatisha maisha yake.
Niwashukuru wote waliochangia mada hiyo kwa ujumbe mfupi wa maandishi, nilichokibaini ni kwamba tatizo linalomsumbua mwanamke huyo, linawasumbua watu wengi sana lakini hawana pa kusemea.
Leo tunaendelea kuangalia dalili za hatari ambazo ukiziona kwa mwenzi wako, zinaashiria kwamba bado anampenda ex wake na kuna uwezekano mkubwa bado wanaendelea kuwasiliana. Tulianza na dalili ya kwanza ambayo ni mpenzi wako kumzungumzia ex wake mara kwa mara, iwe kwa mazuri au kwa mabaya.
2. Anazo namba zake za simu. Mapenzi yakishafika mwisho, namba ya simu ya mliyeachana haina umuhimu tena lakini ukiona bado mpenzi wako ameisevu namba ya ex wake kwenye simu yake au ameiandika kwenye diary, hiyo ni dalili mbaya kwamba wanawasiliana. Endelea kuchunguza.
3. Anabadilika ghafla akimuona hata mkiwa pamoja. Yawezekana mpo kwenye matembezi au shughuli za kawaida na mpenzi wako, ghafla ex wake akapita mbele yenu na ghafla mwenzako akabadilika.
Mapigo ya moyo yakaanza kumuenda mbio, akakuachia mkono hata kama mlikuwa mmeshikana kimahaba, akatangulia mbele, kubaki nyuma au akamgeukia ex wake, hiyo ni dalili kwamba bado anampenda na kuna uwezekano mkubwa wakawa wanaendelea kuwasiliana.
4. Anajifanya ni rafiki yake wa kawaida. Hakuna urafiki wa kawaida kati ya mtu na ex wake. Ukiona walishaachana lakini bado wanajifanya ni marafiki wa kawaida, lazima ujue kwamba kuna mchezo unaochezeka nyuma ya kisogo chako. 
5. Anakasirika akisikia ex wake anatoka na mtu mwingine. Hii ni dalili nyingine muhimu, hata kama walishaachana siku nyingi zilizopita, kama bado ana hisia juu ya mpenzi wake wa zamani, atajisikia wivu na kukasirika akisikia anatoka na mtu mwingine. Ataonesha wivu waziwazi, atamchukia, atamsema vibaya na wakati mwingine hata kupigana na mpenzi mpya wa ex wake.
6. Anaendelea kumpa misaada mbalimbali. Ukiona mpenzi wako anaendelea kumsaidia ex wake kama kumtumia muda wa maongezi, fedha za matumizi au kodi ya chumba, ujue bado wanapendana na anafanya hayo kwa sababu anaamini ipo siku watarudiana.
7. Bado anazo zawadi walizokuwa wanapeana kipindi cha nyuma. Ukiona mpenzi wako bado anatunza zawadi walizowahi kupeana na ex wake kipindi cha mapenzi yao, ni dhahiri kwamba bado anampenda na wanaendelea kuwasiliana.
Yawezekana pia kwenye simu yake bado kuna sms au picha walizokuwa wakitumiana kipindi cha nyuma, amezihifadhi hataki kuzifuta! Hiyo ni dalili kwamba bado anampenda.
MBINU ZA KUKABILIANA NA TATIZO HILI
Kuna usemi wa wahenga kwamba ukishalijua tatizo ni rahisi sana kukabiliana nalo ndiyo maana kabla ya kukupa mbinu za kupambana na tatizo la mpenzi wako kuwasilianana ex wake, nimeanza kwa kukupa dalili ambazo ukiziona, ujue bado anampenda ex wake na wanaendelea kuwasiliana.
Wiki jayo tutahitimisha mada yetu kwa kuangalia mbinu za kukabiliana na tatizo hili baada ya kuwa umeshapata uhakika kwamba mpenzi wako bado anampenda ex wake na wanaendelea kuwasiliana.

YANGA WAIKANDAMIZA PRISONS 2-1 TAIFA

$
0
0


COUTINHO AKIPAMBANA NA MABEKI WA PRISONS, JANA

Mshambuliaji wa Yanga, Genilson Santana 'Jaja' akimpongeza mwenzake Andrew Coutinho (wa kwanza kushoto) aliyeifungia Yanga bao la kwanza dhidi ya Prisons katika Uwanja wa Taifa, Dar jana.
 
Mchezaji wa Yanga, Andrew Coutinho akijaribu kuipita ngome ya Prisons.
 
Kikosi cha Prisons kilichoanza dhidi ya Yanga leo.
 
Kikosi cha Yanga kilichoiua Prisons ya Mbeya mabao 2-1.
 
Mchezaji wa Yanga, Andrew Coutinho alilalamika baada ya kufanyiwa madhambi uwanjani.
 
...Andrew Coutinho kazini.
 
Mshambuliaji wa Yanga, Genilson Santana 'Jaja' akifanya yake.
(PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS / GPL)




WEST BROM YAUA 4-0 ENGLAND, BERAHINO APIGA MBILI

$
0
0

Beki mkongwe wa West Bromwich Albion, Michael Duff akimtoka Sessegnon wa Burnley katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana The Hawthorns. West Brom siku ya jana ilishinda 4-0, Saido Berahino akifunga mabao mawili, Craig Dawson moja na Graham Dorrans moja.


WEMA, DIAMOND WANADAIWA KUMWAGANA!

$
0
0

Diamond..Mh! Upepo mbaya unaivumia kapo ya mafahari wawili Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ambapo wanadaiwa kufanyiana ‘taimingi’ ya kumwagana.
 
Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Kwa mujibu wa mnyetishaji wetu makini, wawili hao wamepotezeana kwa muda mrefu huku kila mmoja akifanya yake lakini kila mmoja anashindwa kujitoa mhanga na kusema hawapo pamoja akihofia kuonekana ndiye tatizo.
“Kifupi ni kwamba Wema na Diamond hawapo pamoja kwa kipindi kirefu, yawezekana wanawasiliana lakini si kwa mapenzi labda kwa mambo mengine. Diamond anazuga kama yuko kwenye shoo, hata akirudi Bongo hawana ukaribu na Wema kama ilivyokuwa zamani, anazuga kidogo kisha anaondoka tena.

 Mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platinum.
“Wema naye hivyohivyo, yupo bize na mambo yake, inasemekana yupo na kigogo f’lani hivi Mkongomani ndiye anampa jeuri mjini kama ulivyoona juzikati amemwaga mapesa ukumbini.
“Inasemekana Mkongomani huyo amemfungulia pia ofisi mpya ya kurekodia filamu pamoja na kumnunulia gari jipya,” kilidai chanzo hicho.
Chanzo hicho kilikwenda mbele zaidi kwa kudai kwamba, Jumapili (jana) Wema alipanga kutangaza rasmi kumwagana na Diamond wakati alipokuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa sambamba na kumtangaza mwanaume wake mpya.
“Jumapili (jana) ndiyo kila kitu kitakuwa hadharani maana Wema amepanga kutangaza hadharani kwenye bethidei yake,” kilizidi kudai chanzo hicho.
 
Diamond na Wema wakila ujana.
Mwanahabari wetu alipokutana na Wema nyumbani kwake na kumuuliza kuhusu madai hayo aliyakanusha yote lakini akawa mzito kidogo katika suala la kutoonana muda mrefu na Diamond.
“Madai yote hayo siyajui! Nina bwana mpya? Eti kaninunulia gari! Amenifungulia ofisi! Sijui nimeachana na Diamond! Hayana ukweli wowote,” alisema Wema kwa mshangao mkubwa.
(CREDIT: GPL)
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ROSE NDAUKA MCHUMBA'KE WAACHANA!

$
0
0
Stori: Imelda MtemaOoh…nooo! Wachumba wa muda mrefu, staa wa sinema za Kibongo, Rose Donatus Ndauka na Malick Bandawe ambao maisha yao ya kimapenzi yamekuwa yakitawaliwa na msuguano wa chini kwa chini, hatimaye wameachana, Ijumaa Wikienda linakupa mkanda mzima.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini na cha uhakika kimemwaga data kwamba wachumba hao ambao walivalishana pete kwa mbwembwe miaka mitatu iliyopita huku wakipika na kupakua lakini wamekuwa katika mzozo wa muda mrefu wa kifamilia, ambapo mara kadhaa wameripotiwa kuchapana wameachana.
“Unajua hawa jamaa wamekuwa na maisha ya kutoaminiana sana, nadhani wivu ndiyo sababu kubwa, lakini naona safari hii hali imekuwa mbaya zaidi kwa sababu Rose  ameamua kubeba kilicho chake na kuondoka kwa mwenzake,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Hiyo ndiyo habari ya mjini, bidada karudi kwao (Kigogo, Dar) na mwanaye. Ilikuwa ni lazima ndoa isiwepo kwani licha ya kupata mtoto hakukuwa na furaha hata kidogo.”
TATIZO NI NINI?
Ingawa chanzo hicho hakikuweza kuingia kwa undani kuhusu tatizo hasa lililotokea safari hii, lakini kilibainisha kwamba kabla ya tukio la sasa, mzozo mwingine mkubwa uliibuka kati yao.
“Kuna kipindi hali ilikuwa tete sana, Malick akaamua kuchukua mabegi yake na kutokomea kusikojulikana ambako alikaa kwa muda wa kama wiki mbili.
“Haikujulikana alikuwa wapi kwa muda wote huo, lakini baadaye tukamuona jamaa anarudi na maisha yao yakaendelea.
NDOTO YA NDOA YAYEYUKA
“Lakini wakati bado mambo hayajatulia, kumeibuka tatizo lingine kubwa ambalo limesababisha Rose kuamua kuondoka huku ndoto ya ndoa ikiyeyuka,” kilisema chanzo hicho.
VIPI KUHUSU MTOTO?
Katika mtafaruku huo, Malick alikataa katakata mtoto wake kuondoka na mama yake, lakini kutokana na umri wa mwaka mmoja wa kijana wao huyo, Naveen, alilazimika kuondoka na mama yake kwa vile bado ananyonya.
Rose Ndauka wakati akiwa na mpenzi wake, Malick Bandawe
Rose, mmoja kati ya waigizaji warembo wa filamu Bongo, inasemekana kwamba yupo nyumbani kwa wazazi wake, Kigogo kutoka kwa mchumba wake, anayeishi Tandale, Tanesco jijini Dar.
IJUMAA WIKIENDA MZIGONI
Baada ya kunyetishiwa ‘ubuyu’ huo, Ijumaa Wikienda lilizama mzigoni ambapo stepu ya kwanza ilikuwa ni nyumbani walikokuwa wakiishi wapenzi ambapo hawakuwepo.

JIRANI ANASEMAJE?
Akizungumza na gazeti hili juu ya kuondoka kwa Rose nyumbani hapo, mmoja wa majirani zake aliyejitambulisha kwa jina moja la Sudi alikuwa na haya ya kusema:
“Rose Ndauka ana muda hatumuoni kama miezi sasa lakini ‘mista’ tunamuonaona labda kama amehama ‘but’ sina uhakika sana.”
ROSE VIPI?
Katika kutafuta ukweli alitafutwa Rose kila kona baada ya simu yake ya kiganjani kutokuwa hewani lakini jitihada ziligonga mwamba hivyo zinaendelea.
BOFYA HAPA KUMSIKIA MALICK
Mchumba mtu, Malick alipoulizwa juu ya ukweli wa sakata hilo, alikiri kutokea na kwamba baada ya jitihada zake nyingi za kulinusuru penzi lao kushindikana, amekubali matokeo.
“Nimejitahidi sana kumwelewesha Rose ili apate kunielewa, ajue namna ya maisha yalivyo, lakini imekuwa ni kama kutwanga maji kwenye kinu. Nimekubali yaishe.
“Kinachonisikitisha sana ni kuona kuwa mwanangu anakwenda kulelewa na mwanaume mwingine, inauma sana tena sana,” alisema bila kufafanua maana ya kauli hiyo.
Katika uchumba wao mrefu, Rose na Malick wamejaliwa mtoto mmoja wa kiume aitwaye Naveen.

Staa wa sinema za Kibongo, Rose Ndauka.
CHANZO: IJUMAA WIKIENDA

WEMA AWACHARUKIA WASANII WENYE MAJUNGU

$
0
0

MADAMUUU! Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ amecharuka na kudai anachukizwa kwa kiasi kikubwa na wasanii ambao wanapenda kumfanyia majungu kutokana na chuki zao binafsi.
 
Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Madam alisema anajua wapo wengi wanaomchukia kutokana na sababu zisizo za msingi kwa kudai kuwa anaringa na vyovyote vile wanavyojadili lakini hajali kwa kuwa hakuna ukweli wowote.
“Watu wenye majungu hawanisumbui kichwa kabisa nabaki nawatazama tu, sababu sina maringo wala majivuno kwa mtu yeyote, sasa cha ajabu wengine wanasema naringa, kwa staili hiyo hatutafika mbali maana wasanii wa nchi za wenzetu wana umoja hawana mambo ya aina hiyo,” alisema Wema.

HUSNA MAULED LIVE KITANDANI

$
0
0

KABAANG! Miss Sinza 2001 na aliyekuwa pia mshiriki wa Miss Tanzania 2011, Husna Maulid amenaswa akiwa kimalovee laivu kitandani na modo maarufu Bongo aliyejulikana kwa jina moja la Calisa.
 
Miss Sinza 2001, Husna Maulid akila ujana na modo maarufu Bongo anayejulikana kwa jina moja la Calisa. 
Picha hizo ambazo zinamuonesha Husna na Calisa wakiwa wamekumbatiana zimevuja kiitelejensia na kumfikia paparazi wetu kisha akawauliza kulikoni?  Ni wapenzi?
 
Modo, Calisa
“Siyo kweli sina uhusiano na Calisa, sina boyfriend na sitaki mwanaume kwa sasa, Calisa ni rafiki yangu tu,” alijibu Husna huku Calisa akijibu:
 
Husna Maulid.
“He hebu ngoja kwanza nitakupigia, hizo picha kaleta nani?”
 Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com


CHANZO: GOBALPUBLISHERS

DIAMOND AMKABIDHI WEMA SEPETU GARI KAMA ZAWADI YA BITHDAY

$
0
0
 

Gari aina ya Nissani Murano alilozawadiwa Wema Sepetu na mpenzi wake Diamond Platnumz.
STAA wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz amemzawadia gari aina ya Nissan Muran mpenzi wake Wema Sepetu katika bethidei yake jana.
Kupitia ukaunti yake ya Instagram, Diamond ameandika hivi:

Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>