Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

Mbwana Samatta Akutana na Mufti Mkuu Sheikh Zuberi

$
0
0
Jana tarehe 11 January 2016, Mwanasoka Bora Afrika Ndg. Mbwana Samatta alimtembelea Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika ofisi kuu za Bakwata zilizopo Kinondoni Jijini Dar Es Salaam.

Mufti Mkuu mbali na kumpatia zawadi mbalimbali kwa ajili ya kumsaidia katika imani yake pia alipata nafasi ya kumuombea dua ya mafanikio zaidi huko aendako Ulaya na kumpa nasaha asisahau kumuomba Mwenyezi Mungu kila wakati na kufanya ibada muda wote atakaokuwa nje ya mazoezi.

Mwisho Mufti alimtakia mafanikio mema na kumuambia dua za watanzania wote zipo naye. 
Mwanasoka Bora Afrika Ndg. Mbwana Samatta akikabidhiwa baadhi ya zawadi mbalimbali na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika ofisi kuu za Bakwata zilizopo Kinondoni Jijini Dar Es Salaam. 

Mwasiti Ft Queen Darleen - Sema Nae

Wimbo mpya: Diamond Platinumz - Hello

Global yatoa mifuko 100 ya saruji ujenzi sekondari Kinondoni

$
0
0


4DC, Makonda (kulia) akipokea mfuko wa saruji kutoka wawakilishi wa Global, Elvan Stambuli (katikati) na David Mwaipaja (kushoto).
1Wanahabari wakichukua tukio katika hafla hiyo.
7Mifuko ya saruji ikiwa ndani ya gari la Global kabla ya makabidhiano.
6Elvan Stambuli (katikati) akionesha risiti ya makabidhiano hayo kutoka kwa Makonda (kulia), anayeshuhudia kushoto ni Ofisa Masoko wa Global, David Mwaipaja.
5.  Mkuu wa Wilaya, Makonda (kulia), akionekana kutumia nguvu kubeba saruji wakati wa makabidhiano hayo. 8Mwakilishi wa Osyter Bay Pharmacy, Kefa Kijo (kulia) akimkabidhi saruji Makonda.
2Mwakilishi wa Global, Mhariri Mwandamizi, Elvan Stambuli, akihojiwa na wanahabari mara baada ya makabidhiano hayo.
3.DC, Makonda (kulia) akipokea mfuko wa saruji kutoka wawakilishi wa Global, Elvan Stambuli na David Mwaipaja.
KAMPUNI ya Global Publishers Ltd inayozalisha magazeti ya Championi, Uwazi, Amani, Risasi, Ijumaa na Ijumaa Wikienda, mapema leo imechangia mifuko 100 ya saruji katika ujenzi wa shule za sekondari wilayani Kinondoni, Dar.
Mifuko hiyo imekabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, na mwakilishi mwandamizi wa Global, Elvan Stambuli, katika ofisi yake iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam.

“Nikiwa mwakilishi kutoka Global Publishers, ninakabidhi mifuko 100 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa sekondari kwa Wilaya ya Kinondoni kutokana na kuguswa na wito wa mkuu wa wilaya hii alioutoa kwa makampuni na taasisi mbalimbali kusaidia kuongeza shule saba za sekondari wilayani Kinondoni ili vijana waweze kupata elimu vizuri,’’ alisema Stambuli.

Wakati huohuo, naye mwakilishi kutoka kampuni ya Ubapa Limited, Wenceslaus Rwezahula, na mwakilishi wa Oyster Bay Pharmacy, Kefa Kijo, walitoa mifuko ya saruji kuchangia ujenzi huo.
Hata hivyo mara baada ya makabidhiano hayo, Makonda aliishukuru Kampuni ya Global Publishers kwa kuchangia mifuko 100 akisema ni mfano wa kuigwa kwa makampuni mengine, huku akisisitiza kuwa bado taasisi na makampuni mengine yanayo fursa ya kuendelea kuchangia ujenzi huo.
PICHA/HABARI: DENIS MTIMA/GPL

Chadema watuma salamu za rambirambi kifo cha Leticia Nyerere

$
0
0


CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SALAAM ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA LETICIA NYERERE

Tumepokea kwa masikitiko makubwa msiba wa Mhe. Leticia Nyerere uliotokea nchini Marekani.

Tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki katika wakati huu mgumu wa kuondokewa na mpendwa wao.

Mwenyezi Mungu awatie moyo wa ujasiri na subra katika wakati huu mgumu wa majonzi ya msiba huo.

Kama chama tutamkumbuka Marehemu Leticia kwa mchango wake na ushiriki wake wakati wote alipokuwa mwanachama wetu na akiwa miongoni mwa watu waliopata fursa za kuwa wabunge kupitia CHADEMA.

Bwana alitoa, bwana ametwaa, jina la Bwana lihimidiwe.

Imetolewa leo, Jumanne Januari 12, 2016 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Mapinduzi ya Zanzibar yaibua jambo zito

$
0
0

 Sehemu ya maandamano katika sherehe za Mapinduzi ya 52, wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe wa kibaguzi

MAADHIMISHO ya 52 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar yameibua hoja ya mamlaka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Dk, John Pombe Magufuli na Dk. Ali Mohamedi Shein. Anaandika Josephat Isango…. (endelea).
Wakiwa wanaendelea na sherehe hizo zinazofanyika uwanja wa Amani mjini Zanzibar Magufuli aliwasili uwanjani hapo na kuimbiwa wimbo wa taifa pekee.
Alipowasili Rais wa Zanzibar ndiye aliyepigiwa wimbo wa Taifa wa Zanzibar, na mizinga 21 ambayo Magufuli hakupigiwa.

Hoja ya wimbo wa taifa wa Zanzibar huibua dhana ya kuwepo serikali ya bara na ya visiwani ili ya Muungano ndio iwe serikali kuu na ukubwa wa mamlaka kati ya Rais wa Muungano na Rais wa Zanzibar.
Mapinduzi hayo yaliyopambwa na bendera nyingi za CCM, Bendera ya Taifa na Bendera ya Zanzibar yalishereheshwa pia na gwaride la jeshi pamoja na ngoma mbalimbali za asili.

Wageni waliohudhuria katika maadhimisho hayo ni Marais wa wastaafu wa Jamhuri ya Muungano, Ali Hassani Mwinyi, Benjamini Mkapa, Jakaya Kikwete na Rais mstaafu Amani Abeid Karume.

Wengine ni pamoja na Makamu wa Rais mstaafu Dk. Gharib Bilal, Waziri Mkuu mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, Makamu Rais wa sasa Samia Suluhu Hassani na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa.
Aidha hakuna mabalozi wengi waliohudhuria sherehe hizo

CHANZO: MWANAHALISI ONLINE

Simba yatangaza rasmi kumtimua Kerr na benchi lake lote

$
0
0

Aliyekuwa Kocha Mkuu  wa Simba, Dylan Kerr.

Klabu ya Simba ya Dar es Salam imeamua kuvunja mkata wake na makocha wa timu hiyo akiwemo Kocha Mkuu Dylan Kerr pamoja na kocha wa makipa Idd Salim

Katika uamuzi huo uliofanywa mchana na kikao cha utendaji waliitwa makocha hao kwa pamoja na kukubali kuvunja mkataba kwa faida za pande zote mbili.

REKODI YA DYLAN KERR SIMBA SC;
Jumla ya Mechi; 30
Mechi alizoshinda; 19
Mechi alizofungwa; 5
Mechi alizotoa sare; 6
MATOKEO YA MECHI ZA SIMBA SC CHINI KERR;
Simba SC 2-1 Zanzibar Kombaini (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 4-0 Black Sailor (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 2-0 Polisi (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 3-0 Jang’ombe Boys (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 3-2 KMKM (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 1-0 SC Villa (KIrafiki Simba Day)
Simba SC 2-1 URA (Kirafiki, Dar es Salaam)
Simba SC 0-0 Mwadui FC (Kirafiki, Dar es Salaam)
Simba SC 0-2 JKU (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 3-1 JKU (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 0-0 KVZ (KIrafiki Zanzibar)
Simba SC 1-0 African Sports (Ligi Kuu Mkwakwani)
Simba SC 2-0 JKT Mgambo (Ligi Kuu Tanga)
Simba SC 3-1 Kagera Sugar (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 0-2 Yanga SC (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 1-0 Stand United (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 1-0 Mbeya City (Ligi Kuu Mbeya)
Simba SC 0-1 Prisons (Ligi Kuu Mbeya)
Simba SC 1-0 Coastal Union (Ligi Kuu Mbeya)
Simba SC 6-1 Majimaji FC (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 5-2 Kimbunga FC (Kirafiki Zanzibar)
Simba SC 2-2 Azam FC (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 1-1 Toto Africans (Ligi Kuu Kirumba)
Simba SC 1-3 Geita Gold Mine (Kirafiki Geita)
Simba SC 1-1 Mwadui FC (Ligi Kuu Kambarage)
Simba SC 1-0 Ndanda FC (Ligi Kuu Nangwanda)
Simba SC 2-2 Jamhuri FC (Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 1-0 URA FC (Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 1-0 JKU FC (Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 0-1 Mtibwa Sugar (Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi)

HIKI NDICHO ALICHOKIWEKA KOCHA DYLAN KERR KWENYE UKURASA WAKE WA TWITER LEO ASUBUHI

$
0
0
 
KOCHA WA SIMBA, DYLAN KERR AMBAYE KIBARUA KIMEOTA NYASI, ANAONEKANA KUJUA KILA KITU BAADA YA KUTUPIA MANENO KWENYE UKURASA WAKE WA MTANDAO WA KIJAMII WA TWITTER AKIONYESHA KUWASHUKURU NA KUWAAGA MASHABIKI WA SIMBA NA WATANZANIA KWA UJUMLA.

CCM Yaomba Radhi Kutokana na Maneno ya Kibaguzi Kwenye Bango Katika Sherehe za Mapinduzi

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesikitishwa sana na ujumbe wenye maudhui ya ubaguzi ulioandikwa kwenye moja ya Bango lililobebwa na mmoja wa wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya Sherehe za Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaomba radhi kwa ujumbe huo, kinapinga na kinakemea kabisa fikra, hisia na mitazamo yoyote yenye maudhui ya kibaguzi.
Ujumbe huo sio tu kuwa una maudhui ya kibaguzi bali pia unaenda kinyume kabisa na falsafa na Shabaha ya waasisi wa Mapinduzi hayo Matukufu ya mwaka 1964 na unapingana na misingi na itikadi ya CCM inayohimiza Umoja na Mshikamano wa Kitaifa.
Daniel Chongolo
Mkuu wa Mawasiliano na Umma CCM.
12/01/2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Afika Muhimbili Kumjulia Hali Waziri Mkuu Staafu Fredrick Sumaye

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Waziri Mkuu, Mstaafu Frederick Sumaye  ambaye amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu Januari 12, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wapili kushoto) wakizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amnaye amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa Matibabu Januari 12, 2016. Kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Esther Sumaye.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Balozi Hassan 
Kibelloh ambaye naye  amelazwa katika hospitali ya taifa y Muhimbili kwa Matibabu Januari 12, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya January 13, 2016

DPP Akata Rufaa Kupinga Kuachiwa Huru Kwa Shehe Ponda

$
0
0
 MKURUGENZI wa Mashitaka (DPP) ameamua kukata rufaa Mahakama Kuu dhidi ya kesi ya uchochezi inayomkabili mwanaharakati wa Kiislamu Shehe Ponda Issa Ponda.
 
Mwanasheria Mwandamizi katika ofisi ya DPP, Bernard Kongola amesema kuwa Serikali inapinga kuachiwa kwa Shehe Ponda ambaye alishitakiwa kwa makosa ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.

“Tayari tumeomba tupatiwe nakala ya hukumu pamoja na nyaraka za mwenendo wa shauri hilo ili upande wa mashitaka tuweze kuandaa rufaa yetu Mahakama Kuu,” alisema.

Kwa mujibu wa mwanasheria huyo, tangu waombe kupatiwa nakala ya hukumu hiyo katika mahakama hiyo ya hakimu mkazi, hakimu ambaye alikuwa anasikiliza kesi hiyo bado hajawapatia upande wa mashitaka hukumu ambayo imechapwa.

“Hatujui kuna tatizo gani, maana tunapoomba kupatiwa nakala ya hukumu, hakimu amekuwa anatuambia kwamba bado hawajamaliza kuichapa, kwa kweli hii inashangaza,” alisema.

Novemba 30 mwaka uliopita, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Morogoro, Mary Moyo alimwachia huru Shehe Ponda kwa maelezo kuwa upande wa mashitaka ulishindwa kuthibitisha pasi shaka yoyote mashitaka dhidi ya mwanaharakati huyo wa Kiislamu.

Wakati kesi hiyo ilipokuwa inasikilizwa, upande wa mashitaka uliita mashahidi wanane kwa lengo la kuthibitisha makosa dhidi ya Shehe Ponda ambaye alikuwa anatetewa na Mawakili wa kujitegemea Juma Nassoro na Abubakar Salum.

Shehe Ponda alifikishwa katika mahakama hiyo Agosti 19, 2013 akikabiliwa na mashitaka matatu likiwemo la kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu iliyomtaka awe mhubiri amani katika jamii likiwa ni sharti la kifungo cha mwaka mmoja nje baada ya kumtia hatiani katika kesi ya jinai.

Upande wa mashitaka ulidai kuwa Shehe Ponda alitenda kosa Agosti 10, 2013 katika eneo la Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege iliyoko katika Manispaa ya Morogoro.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo kiongozi huyo wa kidini alidaiwa kutoa maneno ya uchochezi ya kuhamasisha jamii kinyume na maelekezo ya mahakama.

Katika mkutano huo Shehe Ponda anadaiwa kusema maneno haya, “Ndugu Waislamu msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti, kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa CCM na Serikali na kama watajitokeza kwenu watu hao na kujitambulisha kwamba wao ni kamati za ulinzi na usalama za msikiti, fungeni milango na madirisha ya misikiti yenu na muwapige sana.”

Kauli hiyo inadaiwa kwenda kinyume cha amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam, iliyotolewa mahakamani hapo na Hakimu Victoria Nongwa, Mei 9, 2013 ambayo ilimtaka ndani ya mwaka mmoja kuhubiri amani na asifanye jambo lolote la uvunjifu wa amani na badala yake ahubiri suala la amani, ambayo ni kinyume cha Kifungu cha Sheria Namba 124 cha Mwaka 2002.

Shitaka la pili lililokuwa likimkabili Shehe Ponda ni uvunjifu wa sheria Kifungu cha 129 cha Makosa ya Jinai kuwa siku hiyo, alitoa maneno ya uchochezi yaliyohatarisha kuathiri imani za watu wengine.

Katika hati ya shitaka hilo, ilinukuu kauli ya Ponda kuwa “Serikali ilipeleka Jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi kwa kuwaua, kuwabaka na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni Waislamu. Lakini Serikali haikufanya hivyo kwa wananchi wa Loliondo walipokataa Mwarabu asipewe kipande cha ardhi ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni Wakristo.”

Shitaka la tatu anadaiwa kutenda kosa kinyume cha sheria kifungu cha 390 na 35 kwa kuchochea maneno dhidi ya wananchi wakati wa kongamano lililofanyika Agosti 10, 2013 Uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.

NYUMA YA MACHOZI - 22

$
0
0

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’

ILIPOISHIA:
Kauli ya Mose ilizidisha machungu moyoni kwa Teddy na kuamini wazo lake na ushahidi aliopata lilikuwa sahihi. Alijitahidi kutengeneza tabasamu la uongo ili kuvuta muda wa kummaliza Mose. Muda wote alionesha mapenzi mazito yaliyomziba masikio asijue nini kilichokuwa kikiendelea. SASA ENDELEA...
Majira ya saa moja na nusu Teddy aliamini ule ulikuwa muda muafaka kwake kufanya alichokikusudia, hakutaka kumuua Mose kwa bastora kwa kuhofia sauti yake unaweza kufika mbali.
Kwa vile alikuwa amefunga dirisha la chumbani na kuamini sauti haitatoka nje aliona kisu kingefanya kazi yake vizuri kutokana na Mose kulewa sana asingeweza kushindana naye. Wakiwa watupu kitandani Teddy alisema kwa sauti ya mahaba: “Samahani mpenzi.”
“Bila samahani,” Mose alijibu kwa sauti ya kilevi.
“Nakuja mara moja,” Teddy alisema huku akinyanyuka kitandani.
“Basi usichelewe mpenzi, leo moyo wangu una furaha ya ajabu.” “Usihofu leo mimi na wewe mpaka lyamba.”
Teddy alikwenda hadi kwenye kabati na kuchukua kisu kikubwa na kurudi nacho kitandani. Wakati huo Mose alikuwa amejilaza chali akiwa amefumba macho kutokana na kunywa kiasi kikubwa cha pombe. Teddy alimkalia tumboni kama anataka kumuandaa kimahaba. Kwa sauti iliyojaa ukatili isiyo na chembe ya huruma alisema: “Wee mbwa Sali sala yako ya mwisho.”
“Vipi tena mpenzi?” Mose aliuliza huku alijitahidi kufumbua macho yaliyokuwa mazito kutokana kunywa pombe nyingi kupita kiasi. Macho yake hayakuamini kuona Teddy amemshikia kisu.
“Ha! Nini tena?” “Unauliza jibu, nilikueleza nini siku moja?”
“Mpenzi mbona sikuelewi.”
“Nilikueleza toka mwanzo kuwa hutaugusa mwili wangu labda maiti yangu, lakini leo umeugusa nikiwa mzima ni ishara ya kifo chako.” “Kwa hiyo unataka kuniua?”
“Si ulitaka kunipoteza? Sasa nakupoteza wewe.”
“Si..si..nimekueleza sa..sa..babu yake,” Mose alijitetea akiwa bado amelala chali mwili haukuwa na nguvu kutokana na kulewa sana.
“Fedha yote niliyopoteza baada ya kukamatwa itanunua kifo chako,”
Teddy alisema huku akikipunga kisu hewani.
“U..u..usi..ni..”
hakumalizia alikutana na mapigo ya kisu mfululizo yaliyompiga bila mpangilio.
Teddy alimshambulia Mose kwa visu mfululizo kama anatengeneza chujio la nazi. Mose kutokana na ulevi wa kupindukia hakuweza kujitetea.
Baada ya kupiga kelele za maumivu kwa muda bila msaada sauti ilizidi kupungua mpaka aliponyamaza kabisa, wakati huo kitanda kizima kilikuwa kimejaa damu kama kachinjwa ng’ombe ambazo zilizomrukia Teddy mwilini.
Teddy baada ya kuamini amemaliza kazi, alinyanyuka na kukimbilia bafuni kuoga kisha alibadili nguo na kuchukua vitu vya muhimu na kuhakikisha picha zake zote ameondoka nazo. Baada ya kubeba mizigo yake alikodi gari hadi uwanja wa ndege.
Alifika ikiwa imebakia nusu saa ndege iondoke, baada ya kupima mizigo alielekea kwenye ndege na kuketi huku akiomba Mungu aondoke kabla ishu haijashtukiwa. Hakujiamini mpaka ndege alipoondoka katika jiji la Sicily, safari yake ilikwenda vizuri mpaka alipotua katika jiji la Turin salama salimini. Alitafuta hotel yenye hadhi ya nyota tano iitwayo Principi di Piemonte.
Baada ya kupata chumba aliagiza chakula na kula kidogo kwani bado picha ya kitendo cha kinyama alichomfanyia shemeji yake ilijirudia akilini mwake. Aliamua kuagiza pombe kali ambayo alikunywa mpaka alipopoteza mawasiliano na kulala alipokuwa amekaa. Alishtushwa siku ya pili na hodi iliyokuwa ikigongwa.
Alishangaa kujikuta amelala pembeni ya kitanda kwenye zulia. Aliponyanyuka alizidi kujishangaa kukuta haja ndogo aliimalizia pale bila kujielewa kutokana na kunywa pombe nyingi kupita kiasi.
Alinyanyuka na kukimbilia bafuni na kuchukua cha kufutia kisha alifungua mlango.
“Za saizi?” mhudumu alimsalimia. “Nzu..nzuri, karibu.”
“Asante, nilikua naomba kufanya usafi.”
“Kwani sasa hivi ni saa ngapi?”
“Saa tano.” “Ooh! Kumbe nimelala sana.”
“Inaonesha ulikunywa sana.”
“Okay, fanya haraka usafi nataka kupumzika.”
Teddy alimwacha mhudumu afanye usafi, baada ya kufanya usafi alioga na kuagiza kifungua kinywa kisha alizimua kidogo. Akiwa amejipumzisha kwenye sofa huku akinywa whisky taratibu, tukio la jana yake lilimjibu kwenye akili na kujikuta akiwasha luninga labda habari za kifo cha Moze kitatangazwa.
Alifungua luninga ya taifa, alikuta kuna matangazo ya magazeti na moja ya habari iliyotawala kwenye ukurasa wa mbele ilikuwa yake. Kichwa cha habari kilisomeka unyama wa kutisha, juu kulikuwa na picha ya Mose akiwa amelala kitandani mwili wote ukiwa katika dimbwi la damu.
Picha ile ilimtisha alijikuta akifumba macho kwa woga na kuchukua chupa ya whisky na kuipeleka mdomoni kwake na kujaza kiasi kikubwa na kukimeza chote kwa shida huku amefumba macho mpaka mishipa ya kichwa ikamsimama, baada ya kutikisa kichwa alisema kwa sauti ya chini.
“Ooh! Mungu wangu, nimemuua Mose kifo kibaya sana.”
Akiwa ameinamisha kichwa huku akisikitika na machozi kumtoka kutokana na unyama aliofanya, alinyanyua macho na kushtuka kuona Mose hakufa yupo hospitali ila katika chumba cha wagonjwa mahututi. Akiwa bado anatumbulia macho habari za Mose ambaye alionekana mfu.
Alimuona mkuu wa makosa ya jinai akitoa taarifa kuwa mpaka muda ule upelelezi ulikuwa unaendelea ili kujua nani aliyefanya tukio la kikatili kama lile baada ya kukosa ushirikiano wa mgonjwa ambaye alikutwa katika hali mbaya mpaka wakati ule alikuwa akipumua kwa mashine. Taarifa za daktari zilisema mgonjwa kutokana na kupoteza damu nyingi kutokana na kutobolewa na kitu chenye ncha kali aliongezwa damu zaidi ya chupa kumi.
Habari zile hazikumfurahisha hata kidogo Teddy na kuamini kama Mose atapona na kutoa ushahidi basi atamtia kwenye matatizo makubwa na akishikwa adhabu yake ni kifo. Wazo la haraka lilikuwa kuondoka ndani ya nchi ya Italy na kwenda kuishi Afrika kati ya nchi ya Tanzania au Kenya. Aliamini upelelezi lazima utajua kuwa ni yeye mhusika aliwasiliana na washirika wake na kukubaliana akajifiche Kenya mpaka hapo mambo yatakapojulikana yamefikia wapi.
Bila kupoteza muda alipanda ndege moja kwa moja mpaka Kenya na kwenye kujificha katika jiji la Nairobi katika jumba moja la mshirika wao lililokuwa na kila kitu ndani maeneo ya Kasalani. Mwezi mmoja akiwa anaishi kwa kificho katika jiji la Nairobi aliziona habari na picha yake za kutafutwa kwake kuhusiana na jaribio la kutaka kumuua Mose.
Baadhi ya vyombo vya habari na luninga alitoa kila siku sura ya Teddy kutafutwa huku donge nono likitangazwa kwa mtu atakayetoa habari zake na kufanikisha kukamatwa. Taarifa zile zilizidi kumficha Teddy ambaye alikuwa akitoka usiku tu kwenda club za usiku na baada ya hapo alishinda ndani tu. Aliweza kumuona Mose katika hali ya umajeruhi kutokana na shambulio kali la kutaka kumuua.
Mwili wake ilionesha kuharibika vibaya hata kuzungumza kwake alizungumza kwa shida. Katika mahojiano na mwandishi wa habari mmoja alimsikia akisema kuwa akipona atamtafuta popote hata kaburini ili kulipa kisasi.
****
Majira ya saa sita za usiku Kinape alijirudisha nyumbani kwa kuamini muda ule Kilole atakuwa amelala. Alipokaribia nyumbani aliona teksi ikisimama mbele kidogo na nyumbani kwao. Aliendelea kusogea kwa vile alikuwa upande wa giza aliweza kuliona lile gari ambalo hata namba zake hazikuwa ngumu kuzinakili kichwani.
Kabla ya kupiga hatua alishangaa kumuona mwanamke aliyevaa hijabu na nikabu iliyomziba uso wake akitelemka kwenye teksi na kuelekea kwenye geti la nyumba yao na gari ile kuondoka. Alijuliza ni nani aliyevaa vazi lile kuelekea kwao muda kama ule. Ilibidi atembee kwa taadhari ili kujua yule mwanamke anakwenda kufanya nini kwao muda ule.
Alisimama nje ya uzio na kuweza kumuona yule mwanamke akifungua mlango kwa taadhari kubwa, alijiuliza yule mwanamke ni nani au mwizi. Hakutaka kumshtua alitulia kutaka kuona mwisho wake, lakini kilichomshangaza kilikuwa kufungwa mlango kwa ndani. Moja kwa moja alijua yule ni Kilole, lakini swali lilikuwa usiku ule anatoka wapi na katika vazi lile ambalo hakuwahi kuliona hata siku moja.
Hakutaka kupitia mlango wa mbale alizunguka nyuma na kuingia chumbani kwake kwa kutumia dirisha. Mara zote anapojua anachelewa kurudi alilitegesha dirisha na aliporudi aliingilia kupitia dirishani.
Baada ya kuingia ndani alibadili nguo na kwenda kuoga na kurudi kulala ili alfajiri awahi kuamka kabla Kilole hajaamka. Alikumbuka muda wote alizima simu ili kumkwepa Kilole asimsumbue, alipowasha haikuchukua muda simu iliita. Ilikuwa simu ya dada ya mchumba wake, aliipokea. “Haloo shemu.”
“She..she..mu,” hakuendelea kuzungumza alivuta kamasi za kilio kitu kilichomshtua Kinape na kutaka kujua kuna nini, kwani simu ilikuwa hewani kwa mbali alisikia sauti kama za vilio.
“Haloo shemu,” aliita lakini upande wa pili haukupokea zaidi ya kuendelea kusikia vilio vya upande wa pili.
Aliamua kukata simu na kupiga, iliitaka kwa muda mfupi ilipokelewa upande wa pili na dada ya mchumba wake.
“Shemu upo wapi?” aliulizwa.
“Nyumbani.”
“Una habari gani za Happy?” “Sina! Amefanya nini?” alishtuka.
“Amefariki.”
“Nini?” Kinape alishtuka. “Amefariki,” kauli ile ilirudiwa. “Muongo acha kunirusha roho shemeji.”
“Si kukurusha roho ukweli ni huo mchumba wake ameuawa saa mbili zilizopita.”
“Hapana sikubali Happy hawezi kufa kirahisi namna hiyo nimeachana naye jioni akiwa na mzima wa afya.”
“Hakufa kwa ugonjwa.”
“Nini kimemuua mpenzi wangu?” “Ameuawa.”
“Nini?”
“Ameuawa.”
“Na nani?”
“Hatujajua ile sasa hivi tunaupeleka mwili wa Happy hospitali.”
“Nakuja sasa hivi.”
Kinape alikata simu na kujikuta akichanganyikiwa kwa kuvaa fulana na taulo. Alikwenda moja kwa moja kugonga katika mlango wa Deus kumjulisha taarifa za mchumba wake Happy.
Aligonga mlango kwa muda, Deus aliyekuwa kama yupo ndotoni alishtuka na kunyanyuka hadi mlango. Alipofungua alikutana na Kinape aliyekuwa akitokwa na mchozi na macho yalikuwa mekundu kuonesha ana tatizo zito.
Deus alishtuka na kutaka kujua rafiki yake kipi kimemsibu usiku mkubwa kama ule.
“Best vipi?” Kinape alishindwa kuzungumza alijitupa kifuani kwa Deus na kuangua kilio bila kusema neno.
“Best kuna nini?”
“Happy.”
“Happy amefanya nini?”
“Amefariki.”
“Wewe! Acha utani, si leo asubuhi mnakwenda kijijini?” Deus alishtuka na kumshika Kinape mabegani na kumsogeza mbele yake ili kumtazama vizuri.
“Ndiyo, lakini nimepigiwa simu muda huu amefariki.”
“Alikuwa akiumwa?” “Hapana.”
“Nini kimemuua?”
“Na..na..sikia.. ameuawa.” “Ameuawa! Na nani?”
“Hata wao hawajui.”
“Mwili wa marehemu upo wapi?” “Wameniambia ndiyo wapo njiani kuupeleka hospitali.”
“Unasema kauawa, kivipi?”
“Hata najua, nakwenda kujua huko huko.”
“Nisubiri basi tuongozane.”
Deus alirudi chumbani kumjulisha mkewe habari za Happy.
“Mke wangu,” alimwita huku akimtikisa.
“A.aa..bee mume wangu.” “Kuna tatizo limetokea.” “Tatizo gani tena?” Kilole aliuliza huku akifikicha macho. “Happy amefariki.”
“Nini?” Kilole aliuliza kwa mshtuko. “Happy amefariki.”
“Acha utani, Happy mchumba wa shemeji Kinape?”
“Ndiyo.”
“Muongo, si kesho wanakwenda kijijini kumtambulisha?”
“Ndiyo.”
“Nini kimemuua?”
“Nasikia ameuawa saa mbili zilizopita.”
“Sasa inatakuwaje, kwani Kinape yupo wapi?” “Yupo ananisubiri twende hospitali.”
“Sasa hospitali kufanya nini ikiwa mnasema amekwisha kufa?”
“Wamesema wanaupeleka mwili wa marehemu.”
“Kwa hiyo twende wote?”
”Hapana nilikuwa nakutaarifu tu.”
Wakati Deus akibadili nguo ili awahi hospitali, Kilole alitoka nje na kilio hadi kwa Kinape na kujitupa kifuani kwake.
“Maskini shemeji yangu nini kimemsibu mke mwenzangu?”
“Ha..ha..ta sijui.”
“Kinape tuwahi nipo tayari,” Deus alisema huku akimtoa Kilole kifuani kwa Kinape.
“Okay twende.”
“Mbona hujabadili nguo?”
“Mbona nipo sawa.”
“Sasa utakwenda na taulo?”
Kinape alipojiangalia akijikuta amejifunga taulo, alikimbilia ndani kubadili kisha walitoka kuwahi hospitali.
Itaendelea

NYUMA YA MACHOZI - 23

$
0
0

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’

ILIPOISHIA:
“Kinape tuwahi nipo tayari,” Deus alisema huku akimtoa Kilole kifuani kwa Kinape.
“Okay twende.”
“Mbona hujabadili nguo?”
“Mbona nipo sawa.”
“Sasa utakwenda na taulo?” Kinape alipojiangalia akijikuta amejifunga taulo, alikimbilia ndani kubadili kisha walitoka kuwahi hospitali.
SASA ENDELEA...
****
Walipofika walikuta mwili wa Happy ndiyo umefikishwa muda mfupi ukiwa bado upo katika gari la polisi, dada yake Happy alipomuona Kinape alimkimbilia na kujitupa kifuani kwake na kuangua kilio cha sauti.
“Ooh! Shemeji mdogo wangu wamemuua.”
“Hapana si kweli Happy hawezi kufa kirahisi namna hiyo,” Kinape alisema kwa sauti ya juu huku akimkumbatia shemeji yake.
“Kweli mdogo wangu amekufa, yaani wamemuua kama jambaziii...amewakosea nini mdogo wangu mimiii,” dada yake Happy aliendelea kulia akiwa bado amejilaza kifuani.
Wakati huo kitanda cha kuuchukulia mwili wa Happy uliokuwa umefunikwa shuka kilikuwa kimesogezwa karibu kabisa na gari la polisi.
Kinape alijitoa kwenye mikono ya dada yake Happy na kwenda kwenye gari la polisi wakati huo askari walikuwa wakiushusha mwili wa Happy uliokuwa ulifunikwa na shuka jeupe lililojaa damu.
Baada ya kuulaza mwili juu ya kitanda cha magurudumu, Kinape alisogea karibu kabisa akiwa bado haamini kama kweli mpenzi wake Happy amekufa. Aliishika shuka upande wa kichwani na kuanza kuifunua huku mikono ikimtetemeka. Macho yake yalikutana na uso wa Happy aliyeonekana kama umelala.
“Happy mpenzi wangu amka,” alimwita kwa sauti huku akimtikisa taratibu.
“Shemeji amekufa mdogo wangu,” dada Happy ambaye alikuwa akilia kuliko watu wote waliokuwa pale alikwenda kuungana na shemeji yake ambaye alikuwa bado akiona kama kiini macho kilichokuwa mbele yake.
“Happy mpenzi wangu amka huwezi kufa kirahisi mpenzi wangu, huwezi kuniacha peke yangu, leo asubuhi tunakwenda kwa wazazi wangu wakakutambue. Hata kaka Deus yupo hapa ametoa gari ili lake la kifahari ili nikupeleke kijijini...Amka mpenzi amka ni wewe peke yako niliyekuchagua... Hapiiiiiiiiii,” Kinape alimtikisa kwa nguvu ili aamke lakini mwili ule haukuwa na uhai. Kinape alilia kwa uchungu, Deus alimchukua na kumuondoa kwenye kitanda na kumpeleka pembeni kumbembeleza.
“Deus niache huu ni unyama wa hali ya juu, inaniuma kwa nini wamuue mpenzi wangu nimewakosea nini?” alisema huku akipiga chini. “Pole rafiki yangu, kazi ya Mungu haina makosa.” “Noooo, hapana hii si kazi ya Mungu ni mashetani wasiopenda kuona Kinape na Happy wanaoana.”
“Basi...basi, wewe mwanaume unatakiwa kuyashinda maumivu ya moyo wako,” Deus aliendelea kumbembeleza. “Yaani Happy...hata siamini haiwezekani Happy hajafa,” Kinape alimponyoka Deus na kukifuata kitanda kilichokuwa kikielekea chumba cha uchunguzi kabla ya kupelekwa Mochwali. Alichepua mwendo huku akimwita kwa sauti kama anamsikia, lilikuwa pigo mujalabu ambalo hakulitegemea kipindi kile.
“Jamani mnampeleka wapi mpenzi wangu, Happy hajafa amelala mwambieni aamke leo asubuhi nakwenda kumtambulisha kwa wazazi,” kifo cha ghafla cha Happy kilimchanganya Kinape na kuonekana kama chizi. Lakini Deus alimuwahi na kumketisha chini rafiki yake.
“Kinape hebu kuna kuwa na moyo wa kiume.”
“Siwezi, siwezi Deus inauma sana.” “Najua inauma lakini imekwisha tokea kinachotakiwa kutafuta chanzo cha kifo chake.”
Baada ya kuufanyia uchunguzi mwili wa Happy alipelekwa mochwali kwa ajili ya kusubiri kuchukuliwa na kwenda kuzikwa.
****
Kilole alijikuta akijigeuzageuza kitandani akiyakumbuka matukio yote aliyoyafanya usiku ule. Moyo ulimuuma kwa kitendo cha kikatili lakini hakuwa na jinsi ilikuwa lazima afanye vile ili kupata anachokitaka. Matukio yalipokuwa yakijirudia kichwani alikwenda hadi kwenye friji ndogo ya chumbani na kuchukua chupa ya pombe kali na kunywa glasi nzima.
Baada ya kunywa alijikuta akipitiwa na usingizi na kujilaza nusu ya kitanda, Deus aliporudi toka hospitali alishangaa kumkuta mkewe aliyemwacha amelala akiwa katika hali ya ulevi. Alimshtua toka usingizini kwa kumwita na kumtikisa ili alale vizuri.
“Mke wangu.”
“Tafadhali, mimi sijamuua Happy,” Kilole alikurupuka usingizini baada ya kumuona mumewe amemsimamia mbele yake. “Nani kakuambia umemuua?”
“Sa..sa mahani mume wangu,” Kilole alijibu kwa sauti ya kilevi. “Mbona umekunywa pombe?”
“Hivi kweli Happy amekufa?”
“Kweli amekufa.”
“Basi kila dakika ananijia ndotoni, nikaamua bora ninywe pombe kali nilale fofofo.”
“Ooh! Pole sana.”
“Umefikia wapi?”
“Tumerudi kila kitu kitakuwa asubuhi ya leo.”
****
Siku ya pili asubuhi wakiwa sebuleni Kilole na Deus wakimsubiri Kinape atoke chumbani ili wawahi msibani huku macho yao yalikuwa kwenye runinga katika taarifa ya habari ya asubuhi ile. Katika taarifa ile ya habari vilitangazwa vifo vya watu watatu vilivyotokea usiku wa kuamkia siku ile waliouawa kwa risasi.
Mmoja wa maiti hizo alikuwemo mchumba wa Kinape, Happy, wengine waliouawa ni Jimmy mpiga picha na rafiki yake Rich. Deus alishtuka kuona na Jimmy amekufa mtu aliyekuwa akimfahamu kwa kumpiga picha nyingi zikiwemo za birthday na mkewe.
Taarifa ya habari ilielezea kwa ufasaha vifo vile kuwa mwili wa Happy ilikutwa nje ya geti la nyuma yao na miili mingine ya wanaume wawili Jimmy na Rich ilikutwa katika chumba cha Jimmy wote wakiwa wameuawa kwa risasi.
Pia taarifa iliongeza kupitia mashahidi majirani wa nyumba ile kuwa usiku wa saa sita walimuona mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa hijabu iliyomziba mwili wote aliyeingia mule ndani.
Kwa vile hawakuwa na wasiwasi naye hawakujishughulisha naye lakini baadaye katikati ya usiku waligundua Jimmy hajafunga mlango kitu ambacho hakikuwa kawaida yake. Walipokwenda ndani ndipo walipokuta tukio lile la kutisha. Zilioneshwa picha za Jimmy na Rich zilivyokuwa zimelala kwenye kochi na sakafuni.
Lakini maiti ya Happy haikuonekana kutokana na kuchelewa kwa taarifa kufika kwenye vyombo vya habari. Kinape aliyekuwa ndiyo anafika sebuleni aliliona tukio lile. Kilichomshtua ni picha ya Jimmy.
“Jamani huyu si Jimmy mpiga picha?”
“Ndiye mwenyewe.”
“Mungu wangu na yeye kafanya nini?”
“Tena nasikia muuaji ni mwanamke,” Deus alimwambia Kinape aliyekuwa amesimama nyuma ya kochi waliokalia. “Mwanamke!” Kinape alishtuka.
“Ndiyo, tena alikuwa amevaa hijabu iliyomzima mwili wote.”
“Unataka kuniambia ndiye aliyemuua Happy?”
“Walaa, mume wangu hawakusema yule mwanamke ni muuaji bali ndiye aliyeingia chumbani kwa Jimmy,” Kilole alipinga kauli ya mumewe.
“Kwa nini ujifiche lazima atakuwa muuaji.”
“Jamani tuachane na hayo tuwahi msibani tukajue nini kinaendelea,” Kinape alikatisha ubishani wa mtu na mkewe.
Wote walinyanyuka kuelea nje kwenye gari, njiani wakiwa ndani ya gari kauli ya Deus kuhusiana na msichana aliyemshtumu kuvaa hijabu ilimshtua na kukumbuka jinsi alivyo mshangaa Kilole aliyekuwa amevaa usiku ule. Alijiuliza kama ni yeye aliyefanya mauaji yale alifanya kwa lengo gani. Alizidi kujiuliza kuhusu kifo cha Happy anaweza kuwa pia ni yeye?
*****
Msibani watu walikuwa wengi huku kila mmoja akizungumza la kwake, wengi walikuwa walionekana na huzuni hasa familia ya Happy baba, mama na dada yake ambaye alilia mpaka kupoteza fahamu. Mashoga zake nao walichanganyikiwa kwani walikuwa katika maandalizi ya harusi ambayo walipanga iwe ya kukata na shoka baada ya kuelezwa siku ile ndiyo ilikuwa ya kwenda kutambulishwa kijijini kwa mchumba wake. Kinape naye muda mwingi alikuwa amekaa chini kutokana na kutokuwa na nguvu za kusimama.
Deus alitumia muda wake mwingi kuwa karibu ya rafiki yake kumfariji kwani kila rafiki na ndugu wa Happy walipolia naye aliporomokwa na machozi. Kila aliyekuwepo msibani uso wake ulijaa simanzi nzito kutokana na kifo Happy msichana aliyekuwa bado mbichi pia mwenye malengo mazito katika maisha yake. Lakini ilikuwa tofauti kwa Kilole na wote waliokuwepo msibani, moyo wake ulijaa furaha kwa kutimiza lengo lake la kuweza kuuvunja uchumba wa Kinape na Happy ambao aliamini hautaunganika mpaka mwisho wa dunia.
Wakati watu wakiendelea kulia huku ibada ikiendelea kabla ya kuuchukua mwili wa Happy haujaenda kupumzishwa Kilole alijikuta akivuta kumbukumbu ya matukio ya kikatili aliyoyafanya jana.
Aliamini kabisa kwa Happy alifanya unyama wa hali ya juu, lakini kwa Jimmy na rafiki yake ilikuwa ni kulipa kisasi cha kubakwa kwani aliamini adhabu ya mbakaji Uarabuni au China ni kifo. Pia alikuwa kutimiza kile alichomuahidi Jimmy kama picha zake zitavuja basi angemfanyia kitu kibaya. Aliamini vifo vyao vilibakia simulizi ndani ya vinywa vya watu.
Alianza kukumbuka jinsi alivyotoka nyumbani baada ya kuhakikisha mume wake amelala fofofo baada ya kumwekea madawa kwenye chakula. Kwanza alimpigia simu Kinape ajue yupo wapi kwani alipanga na yeye siku ile naye angelishwa chakula kile na kulala fofofo ili aweze kutoka bila kutiliwa wasiwasi na mtu.
Lakini simu ya Kinape haikuwa hewani ile haikumsumbua sana japo wasiwasi wake aliwaza huenda wapo pamoja na Happy. Baada ya kuvaa vazi lake lililomziba mwili mzima, alichukua bastora ya mume ambayo aliikagua na kukuta risasi za kutosha.
Alichukua na kiwambo cha kuzuia sauti. (bomba linalowekwa mbele ya bastora au bunduki kuzuia sauti) Baada ya kuviweka vitu vyake vizuri alikwenda hadi kwenye bodaboda na kukodi. “Samahani kaka angu, Masaki shilingi ngapi?”
“Masaki ipi?”
“Mwanzoni kutokea Salenda?”
“Kwa vile usiku buku ishirini.”
“Naomba uniwahishe.”
Baada ya kupanda dereva aliondoa pikipiki kwa mwendo wa kasi kidogo, Alipokaribia nyumba ya kina Happy aliomba ashushwe mbali kidogo. Kwa vile muda ule magari hayakuwa mengi alitumia dakika kumi tu.
“Nina imani umewahi?” dereva wa bodaboda alimuuliza huku akipaki pikipiki. “Ndiyo ila naomba unisubiri hapa.”
“Dada mbona unanitisha?” aliogopa kukabwa.
“Hapana kaka yangu, bado kuna sehemu nakwenda, nafika nyumbani mara moja narudi sasa hivi.”
“Na fedha yangu?” “Chuku hii nikirudi tutapatana tena,” Kilole alipa dereva elfu arobaini.
“Poa wahi basi.”
Kilole alichepua mwendo kuwahi nyumbani kwao na Happy ambapo palikuwa na kipande chenye giza kutokana na nyumba za sehemu ile kuachana eneo kubwa. Alipokaribia alitoa simu yake ambayo aliiseti sauti ambayo muongeaji huwezi kuijua sauti yake mara moja hata laini alikuwa ameinunua siku ileile ambayo ilikuwa haijasajiliwa.
Baada ya kujipanga alipiga simu ya Happy ambaye alikuwa amejilaza kitandani akiwaza safari ya kesho yake ambayo alijiuliza sijui itakuwaje atakapo kutana na wazazi wa Kinape mwanaume aliyemkabidhi moyo wake. Happy aliichukua simu yake na kuitazama namba ambayo ilikuwa ngeni kwake, aliipokea. “Haloo.”
“Haloo Happy hongera shosti.”
“Ya nini?”
“Yaani kumbe kesho unakwenda kutambulishwa ukweni hujanijulisha.”
“Lakini hiyo si kwenda kutambulishwa lakini mambo bado, nikirudi kila kitu kitakuwa wazi, lakini mazungumza na wewe bado asijakufahamu sauti yako?”
“Mimi Betha,” Kilole alimdanganya.
“Betha yupi?”
“Happy hilo si muhimu kama hili ninalotaka kukueleza?”
“Lipi tena hilo?” Happy alishtuka na kujiweka vizuri kitandani. “Najua
naweza kuonekana mbeya lakini lazima niseme juu ya tabia za mchumba wako Kinape.”
“Tabia gani?”
“Japo kweli ni mchumba wako lakini si muaminifu, hivi ninavyozungumza yupo nje ya gari tulilokuja nalo na shoga yangu wakilana denda kibaya zaidi ni jirani na nyumba yenu kweli huu ni ustaarabu?” “U..u..unasema?” Happy aliingia kigugumizi.
“Tena kama unaweza wahi uwafumanie ‘live’ ukichelewa hata dakika kumi Kinape ataondoka.”
“Okay, nakuja.”
Happy bila kumweleza mtu alikurupuka kuwahi kumfumania Kinape, wakati huo Kilole alijiandaa kummaliza baada ya kujua anakuja.
Alitoa bastora na kufunga kiwambo na kumsubiri. Mara alimuona akitokeza kwao akiwa na gauni la kulalia bila hata ya viatu kwani aliamini angevaa kiatu angechelewa kufumania.
Kwa vile alikuwa kwenye giza alimuona Happy akisogea upande ule akipepesa macho, alitumia nafasi ile kumpiga risasi mbili za kifuani upande wa kushoto kama alivyoelekezwa na mumewe Deus jinsi ya kuua adui kwa risasi.
Alimuona Happy akiruka kwa nyuma hakutaka kuona kinachoendelea alichepua kwendo huku akiiweka bastora ndani ya hijabu. Alipofika alimwambia dereva wa bodaboda: “Tuondoke.”
“Tunaelekea wapi?”
“Mikocheni B.”
Itaendelea

NYUMA YA MACHOZI - 24

$
0
0

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’

ILIPOISHIA:
Baada ya msiba Kinape alibakia kwenye kaburi na mpenzi wake ambaye usiku wa jana yake alikuwa naye kabla ya kuagana kuonana alfajiri ya siku ile kwa ajili ya safari ya kijijini. Alibakia ameliinamia kaburi huku msiba kwake ukianza upya.
Deus na ndugu na jamaa walimbembeleza sana mpaka alipokubali kuondoka makaburini. Moyoni aliapa lazima atamshikisha adabu aliyehusika na kifo cha Happ. Mwanzo alikuwa na wasiwasi na Kilole, lakini kilio alicholia kumlilia mchumba wake aliamini kabisa hausiki kabisa.
SASA ENDELEA...
****
Usiku wakiwa nyumbani Deus katika kutafuta vitu kwenye kabati alishtuka kuona kiwambo cha bastola yake kipo kwenye nguo. Alishtuka kwani siku zote hukiweka mbali kutokana na kutotumia sana kutokana na matukio ya kijibizana kwa risasi na wauza madawa ya kulevya kupungua.
Alikichukua na kukinusa kilionesha kimetumika, alijiuliza mbona kinanuka baruti kama kimetumika. Wazo la haraka lilikuwa kuikagua bastola, alipofungua droo alishtuka kuona haipo kama alivyoiweka.
Aliitoa na kuifungua upande wa risasi, alizidi kushangaa baada ya kuzikuta pungufu ya risasi sita. Alijiuliza bila kupata jibu kuwa risasi zile zimekwenda wapi, alinusa mdomo wa mtutu wa bastora na kukuta umetumika.
Alijikuta akipata wasiwasi na kumwita mkewe aliyekuwa sebuleni akizungumza na Kinape ili amulize. Kilole aliingia chumbani bila kujua anaitiwa nini.
Alishtuka baada ya kumuona mumewe ameshikilia bastora na kiwambo chake. Mshtuko wake ulikuwa dhahili ambao ulionekana wazi kwa mumewe.
Mshtuko ule aliuona na kujua kuna kitu anachokijua mkewe kuhusiana na matumizi ya bastola ile. “U..unasemaje mume wangu?” alisita kidogo.
“Nani katumia hii bastola?” alimuuliza kwa sauti ya kiaskari.
Kilole aliamini kabisa akibabaika lazima atakuwa swali la kujibu, alitulia kwa muda akipanga la kujibu mume wake ambaye alionekana amekunja uso alilirudia swali lake la mwanzo.
“Nakuuliza mbona hunijibu nani katumia siraha yangu?”
“Si..si..jui.”
“Hujui ina maana mimi ndiye niliyetumia?”
“Kama hujatumi wewea nani mwingine anaweza kuitumia hiyo bastora, mimi niitumie kwa kazi gani?”
“Hujanijibu nani katumia hii bastola na kiwambo chake pia risasi zangu sita hazipo?”
“Sijui.”
“Mke wangu sitaki utani nieleze ukweli la sivyo leo utanitambua mimi nani, unaweza kuikodisha kwa watu wafanye uharifu ili mimi niingie matatizoni.”
“Mume wangu hiyo imeanza lini, niikodishe ili iweje, nina shida gani mimi?”
“Kama huna shida nani kaitumia, kumbuka vitu vyote vinakaa sehemu ya siri tunayojua mimi na wewe.”
“Kama unataka kufanya lolote juu yangu fanya lakini mimi sijui lolote.”
Kauli ile ilimuudhi sana Deus na kuamini kabisa mke wake anajua kila kitu juu ya matumizi ya bastola ile kutokana na kushtuka alipoingia ndani na kumuona ameshika ile silaha.
Alimsogelea mkewe kumpa kipigo ili aseme ukweli juu ya matumizi ya silaha ile kwa kuamini kabisa kama silaha ile ikikamatwa inatumika vibaya basi lazima yeye ndiye atakaye julikana anafanya mchezo ule na kufia gerezani. Wakati anamsogelea amzabe makofi, simu yake iliita, aliipokea na kuzungumza
“Haloo,” alizungumza huku akitoka nje kutokana na simu kuwa ya kikazi.
Taarifa iliyomfikia alitakiwa uwanja wa ndege mara moja kuna ndege iliyosemekana kuna mtu ana madawa ya kulevya hivyo ilitakiwa akamatwe. Taarifa ile ilikuwa inatoka kwa mkuu wake, alibadili nguo harakaharaka na kupitia vifaa vya kazi na kuelekea mlangoni, kabla ya kutoka alisema:
“Nakwenda nikirudi nikute jibu la sivyo leo humu ndani patachimbika.”
Deus alitoka kutokana na kuchanganywa na matukio ya ndani, alijikuta akimsahau hata Kinape aliyekuwa amejilaza kwenye kochi, alipofika mlangoni alikumbuka hajamuaga rafiki yake aligeuka na kumsemesha Kinape aliyekuwa kwenye dimwi la mawazo mikono kichwani.
“Besti...Besti,” alimwita zaidi ya mara mbili ndipo aliposhtuka. “E..ee.eeh,” Kinape alikuwa kama umeamshwa usingizini. “Unaonekana upo mbali sana?”
“Wee acha tu, hata sielewi kama nitaweza kuidhibiti hali hii mpaka napata mawazo ya kijinga.” “Mawazo gani tena rafiki yangu.”
“Eti nami nijiue nimfuate mpenzi wangu.”
“Wewee! Mawazo gani hayo rafiki yangu, baada ya Happy kuna maisha mengine na farijiko lingine.”
“Ni kweli, siamini kama nitampata kama Happy, Deus yule mwanamke alinipenda mapenzi ya dhati toka moyoni mwake. Nina imani hata kifo chake kinatokana na kulilinda penzi letu.”
“Besti hebu tuache sheria ichukue mkondo wake.”
”Watamkamataje mtu ambaye hajulikani?”
“Mkono wa sheria ni mrefu atashikwa tu amini hilo best.”
Kauli ile ilimtisha Kilole aliyekuwa kwenye mlango wa chumbani akifuatilia mazungumzo. Wasiwasi kumjaa na kuamini kabisa mumewe kutokana na kazi yake ya kijeshi anajua siri nyingi, pengine hata tukio lile anajua yeye ndiye aliyefanya.
Alijikuta akitetemea na kujiona atafia gerezani au kinyongwa, lakini aliendelea kusikiliza kwa kuijificha. Alimuona mume akitoka nje na baada ya muda alisikia gari lake likiondoka.
Alirudi chumbani na kukaa kwenye kitanda kutafuta majibu ya maneno ya mume wake. Aliamini ile ni vita alitakiwa kumuwahi mumewe kabla hajafanya jambo lolote baya, wazo la haraka lilikuwa kwenda kwa wakuu wake hasa yule alimweleza hailewani naye baada ya kuzurumiana fedha za rushwa ya madawa ya kulevya.
Aliamini kupitia yule bwana atafanikisha mpango wake, kwa vile mumewe alisema akirudi akute jibu na yeye aliamini kabisa hakuwa na jibu la kumjibu hasa akizingatia siraha ile anayejua ni yeye na mumewe tu. Aliona kujiepusha na maswali yasiyo na majibu na mwisho wake kujulikana yeye ndiye muuaji ni kutoroka.
Aliamua kutoroka na kwenda kulala nyumba ya wageni ile kesho amtafute yule mkuu wa mumewe na kumweleza kuwa mumewe anajihusisha na dawa za kulevya.
Alijua yule bwana atataka kumkomoa na kuja kufanya upekuzi kwa vile atakuwa amwelekeza lazima atatiwa hatiani. Alichukua baadhi ya nguo za kuvaa kesho na kuziweka kwenye mkoba alimuaga mfanyakazi kwa kumwambia siri ile asimwambie mtu. “Marry hakikisha mtoto amekula vizuri.”
“Hakuna tatizo dada.”
“Na hizi utanunua chochote,” alimpa elfu ishirini.
“Asante dada.” Alitoka hadi sebuleni kumuaga Kinape.
“Shemu nakuja mara moja.” “Hakuna tatizo, wacha na mimi nikalale,” Kinape alijibu huku akielekea chumbani bila kuuliza safari ile ya wapi.
***
Siku ya pili Kilole alifika makao makuu ya kitengo cha kuzuia dawa za kulevya, alimuulizia yule mzee ambaye jina lake alikuwa analijua moja. Baada ya kuingia getini alikwenda mapokezi na kuulizia. “Samahani dada mzee Shamo yupo?”
“Wewe nani yake?”
“Mtu wake wa karibu.”
“Ameingia sasa hivi.”
“Naomba nimuone.” “Subiri,” yule dada alisema huku akinyanyua simu, baada ya kuzungumza alisema:
“ Nenda chumba namba sita.”
Kwa vile hakuwa mgeni sehemu ile alikwenda moja kwa moja chumba namba sita na kugonga mlango.
“Ingia,” sauti nzito toka ndani ilisema. Alizungusha kitasa na kuingia ndani, mbele ya meza kubwa kulikuwa na mzee mmoja aliyekuwa na mvi nyingi kichwani zilizompendeza.
“Karibu mrembo.”
“Asante, shikamoo.”
“Asante, nikusaidie nini?” Kilole alitengeneza uongo huku akiusema hata ugomvi wao, baada ya kumsiliza alimuuliza:
“Una uhakika na usemacho?”
“Mimi si ndiye mkewe sasa unataka uhakika gani zaidi ya huu?”
“Okay, muda si mrefu tunakuja kwako.”
“Asante mzee wangu.”
Kilole aliondoka moyo wake ukiwa mweupe kama seluji, moyoni alijisemea akuanzae mmalize.
Baada ya kuhakikisha kila kitu kimekwenda kama alivyopanga alirudi aliamua kurudi nyumbani kwake akiamini muda ule mumewe atakuwa kazini mpaka arudi jioni angekuwa amekwisha wekwa chini ya ulinzi.
Alipofika nyumbani alishangaa kumkuta mumewe nyumbani kumbe naye hakurudi jana alipoondoka na kurudi asubuhi ile. Japo alipatwa na mshtuko uliofanya haja ndogo imtoke kidogo alijitahidi kuuficha.
“Karibu mke wangu,” Kilole alishangazwa na hali ya mumewe ambaye hakuonesha hasira. Kilole hakujibu alikimbilia chumbani na kuangua kilio kitu kilicho mfanya mumewe amfuate na kumbembeleza.
“Mke wangu bado una yaleyale ya jana?” Deus alimuuliza mkewe kwa sauti ya upole. “Siku hizi hunipendi, nimekuwa mke mwema na muaminifu siku zote za ndoa yetu, lakini bado umekuwa huoneshi nina umuhimu kwako,” Kilole alisema kwa sauti ya kilio cha uongo.
“Mke wangu, kama kimetokea kitu cha tofauti ndani nimuulize nani kama si wewe mke wangu?”
“Ni kweli, lakini kama sijui mimi nitajibu nini, tena ulitaka kunipiga.”
“Ni hasira za mpito lakini baada ya kujua kosa langu niliamua kuliacha, lakini muhimu kuwa na uangalizi mzuri wa vitu vyetu usipovitunza wewe nani avitunze...Halafu lile gari lako linaingia mwisho wa wiki.”
“Usiniambie! Asante mpenzi wangu.”
Kilole alinyanyuka na kumkumbatia mumewe huku akiamini bado ni mshindi na muda si mrefu Deus ataionja joto ya jiwe. Wakati wao wanabembeleza kikosi maalumu cha kupambana na dawa za kulevya kilikuwa nje ya nyumba ya Deus na kugonga hodi. Deus alitoka nje kuwakaribisha alishtuka kumuona mkuu wake mzee Shamo:
“Ooh! Mzee karibu naona leo mmenitembelea.”
Waliingia wote ndani na kuketi kwenye kochi wakati huo Deus alimwita mkewe awahudumie wageni.
“Mke wangu kuna wageni hebu njoo uwasikilize wanatumia nini.” “Tunashukuru, hatuna muda tumekuja kufanya kazi moja hapa kwako.”
“Kazi moja! Ipi hiyo?” Deus alishtuka.
“Nina imani unaelewa vizuri kazi yetu ni nini?”
“Naijua, ndiyo maana hata mimi nimerudi alfajiri kufuatilia mtu mmoja aliyeingiza dawa za kulevya.” “Ni kweli, lakini huwezi kuwa msafi bila kujisafisha.”
“Una maana gani?”
“Kuna msamalia mwema mmoja amesema kuwa wewe unajishughulisha na uuzaji wa dawa za kulevya.” “Mimi?” Deus alishtuka kusikia vile.
“Unashtuka nini, sasa hivi upo chini ya ulinzi na kutuachia kufanya upekuzi.”
“Fanyeni tu, hizi ni njama za kuchafuana lakini kila kitu kitafahamika.”
Deus aliwekwa chini ya ulinzi na upekuzi ulianza mara moja, Kilole alijifanya kushtuka na kuuliza:
“Jamani kuna nini tena?”
“Siyo kazi yako,” Mzee Shamo alijibu kwa sauti kali.
“Jamani mume wangu kafanya nini?” Kilole aliendeleza usanii. “Wee waache, naona kila siku wananichokonoa lakini ukweli utajulikana,” Deus alisema bila kujua bomu lipo ndani litalipuka muda wowote.
“Hebu njoo hapa,” mzee Shamo alimwita Kilole kwa sauti ya ukali. Kilole alimfuata nakumwacha mumewe amekalishwa chini ya ulinzi, alipofika karibu alimuuliza kwa sauti ya chini.
“Kuna mabadiliko?”
“Hakuna kila kitu kipo vilevile.”
“Ipo sehemu gani?”
“Ndani ya kabati.” “Okay,” baada ya kusema vile alisema kwa sauti kali kupoteza lengo.
“Haya na wewe rudi kwa mwendawazimu mwenzako.
” Kilole alishikwa na askari mmoja na kwenda kukalishwa pembeni ya mumewe, upekuzi uliendelea huku Deus akisema kwa hasira: “Yaani mkikosa hicho mnachokitafuta walahi nitazaa na mtu.” “Mume wangu mbona wanakufuatafuata?” Kilole aliendelea kulalamika kiuongo.
“Wee waache, mwaka huu nitakufa mimi au mtu, nimechoka kuchezewa kama mpira,” Deus aliendelea kulalamika kwa hasira.
“Wee piga kelele utanyamaza muda si mrefu,” mzee Shamo alisema huku akiendelea kufanya upekezi wa uongo kabla hawajafanya kilichowapeleka pale.
Baada kutafuta sehemu nyingine mwisho waliingia chumbani na kufungua kila sehemu na mwisho walichukua briefcase iliyokuwa ndani ya kabati na kuifungua. Ndani ya briefcase kulikuwa na dawa za kulevya zilizokuwa ndani ya mifuko, mzee Shamo alisema kwa furaha:
“Amekwisha, hapa hata ateremke masihi kumtetea hatoki.”
Waliibeba na kutoka nayo hadi sebuleni na kuifungua mbele ya Deus.
“Nilikueleza mapema kuwa huwezi kuwa msafi bila kujisafisha.”
“Hiyo nini?” Deus alitaka kunyanyuka kwa hasira lakini alitulizwa na siraha zilizokuwa zimemtazama. “Deus umekwisha, nilikueleza toka zamani kuwa wewe mtoto mdogo huwezi kushindani na mimi, kwa hili utafia gerezani.” “Muongo mkubwa huwezi kuja kuniwekea madawa ili kunitia hatiani, lakini nikitoka nitakuua nakuapia,” Deus alipagawa kuona ndani briefcase yake kuna madawa ya kulevya.
Itaendelea

Sabby: Mapenzi Kwangu No badala yake yeye atachapa kazi tu.

$
0
0




 MSANII wa Bongo movies Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ amesema katika kipindi hiki cha kasi ya Rais John Magufuli, hana muda wa kuhangaika na mapenzi, badala yake yeye atachapa kazi tu.
Akizu ngumza  msanii huyo alisema kumekuwa na wimbi kubwa la wezi wa mapenzi wanaotumia fedha, lakini kwake ni bora ajibidishe kivyake ili apate chake halali.
“Mimi naona kabisa hapa Bongo hakuna mapenzi, kuna usanii tu, kila mmoja anajidai yupo kwenye mapenzi kumbe utalii, ninachojua mimi hapa ni kazi tu mapenzi nchi za watu,” alisema.

Ndoa Ya Wastara Bond Nusu Afe!

$
0
0

DAR ES SALAAM: Zikiwa zimepita siku chache tangu staa wa filamu, Wastara Juma kufunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge,  Zanzibar, Sadifa Juma aliyekuwa mpenzi wake, Bond Suleiman nusu afe.
WASTARA24Wastara na Bond
Wakizungumza ndugu wa karibu wa kijana huyo ambaye pia ni muigizaji (jina linahifadhiwa) alisema siku moja kabla ya ndoa ya Wastara, Bond alitaka kujiua kwa kunywa sumu, lakini kaka yake aliyeingia chumbani kwake ghafla, akamuwahi kabla hajaibugia.
bond 
Bond
“Ni Mungu tu Bond kuwa hai mpaka sasa, japokuwa hayupo vizuri ni kama amepaniki kutokana na Wastara kuolewa, maana bado anampenda, ungekuta sasa hivi tunaongea mengine, kwani alikuwa ameshaweka sumu tayari anywe, lakini alisahau kufunga mlango ikawa ndiyo salama yake baada ya kaka yake kuingia chumbani kwake akiwa anahitaji kuzungumza naye ndipo akakutana na ishu hiyo na kufanikiwa kumuokoa.
wastara1Wastara 
“Ukweli hata sisi tumeumia sana Wastara kuolewa na mtu mwingine kwani tulikuwa tukimfahamu kwamba atakuja kufunga ndoa na Bond maana aliwahi kuletwa kutambulishwa kwa ndugu,” alisema ndugu huyo.
Gazeti hili lilimtafuta Bond ili kupata ukweli wa habari hizo, ambapo alikiri kuokolewa na kaka yake baada ya kutaka kunywa sumu kutokana na Wastara kuolewa.
“Nilikuwa nimeshaandaa sumu kabisa na Wastara nilimuaga kwa njia ya meseji na hii ni baada ya kuniambia siku inayofuata anaolewa, ukweli nilimpenda na najuta maana mimi ndiyo nilifanya makosa na kumkosea sana, lakini siku niliyoamua kuachana na mambo ya ufuska na kuwa mtu wa sala muda wote, naye naona ndiyo akasema basi hanitaki tena.
“Nilijitahidi sana kumuomba msamaha lakini akanikatalia na kusema amempata atakayempa faraja ya moyo, namtakia maisha mema ya ndoa na nitamsubiri kama ndoa itavunjika nitamuoa maana mwenyewe wakati anasubiri kufunga ndoa (Alhamisi iliyopita) aliniambia kwamba anaogopa ndoa hiyo,” alisema.

Wema Hamjui Mwenye Mimba, Ampa Idris 50% na Mbunge 50%

$
0
0
Wema Sepetu ‘Madam’
Na Mwandishi Wetu, Risasi
DAR ES SALAAM: Habari zinazosambaa kwa kasi ya ajabu kama moto wa kifuu zinaeleza kuwa, mtoto mzuri ndani ya Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ mbali na taarifa za kuwa mjamzito, hadi sasa bado yupo kwenye wakati mgumu kuweza kutegua kitendawili cha nani mmiliki halali wa kiumbe kilichopo tumboni mwake, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili.

Hivi karibuni, magazeti tofauti ya Global Publishers ndiyo yalikuwa ya kwanza kuripoti kuhusu uwepo wa mimba ya mlimbwende huyo asiyechuja Bongo, ambapo awali, vyanzo mbalimbali vilieleza kuwa mhusika ni mbunge mmoja machachari ambaye ndiye anayemuweka Wema mjini kwa sasa.
WEMA 
Kitumbo cha Wema Sepetu
MAJIBU YA WEMA ALIPOBANWA
Kwenye habari ya awali iliyoripotiwa na gazeti la Ijumaa, Wema alipotafutwa kusomewa mashitaka yake kuwa ana ujauzito wa mbunge huyo, kupitia simu ya shosti wake, Aunt Ezekiel, staa huyo hakutaka kufunguka sana kuhusu mbunge huyo zaidi ya kusema; “ndiyo nina mimba, tena ya miezi sita.”
UBUYU MPYA SASA
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Miss Tanzania  huyo wa mwaka 2006 amejiridhisha kuwa ni mjamzito baada ya kupima kwenye hospitali moja maarufu (jina tunalo) na kuondoka na furaha ya ajabu lakini kitendawili alichoondoka nacho ni kuwa hamjui mhusika wa kiumbe hicho.
WOTE AWAPA ASILIMIA 50
“Madam alifurahi kweli maana suala lililokuwa linamnyima usingizi siku zote ni kutopata mimba. Baada ya furaha hiyo, ishu ikawa ni kumtambua mhusika kwani kwa nyakati tofauti ameshabanjuka kimalavidavi na mshindi wa Big Brother Hot Shot 2014, Idris Sultan na mbunge yule anayempa jeuri ya pesa kwa sasa, wote amewapa asilimia hamsini hajajua nani hasa ndiyo mhusika,” kilisema chanzo hicho.
WOTE WAWILI KAWAMILIKISHA
Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, baada ya kuona ameshachanganya madawa, Madam aliamua kila mmoja kumwambia kuwa ‘mzigo’ huo ni wake hivyo wote kwa pamoja na nyakati tofauti wanahudumia na kumjali staa huyo, tena kwa nguvu zote.
“Yaani kila mmoja kamwambia mimba yake. Wote wawili wamezipokea taarifa za ujauzito kwa bashasha huku kila mmoja akijiamini kuwa ni mhusika pasipo kujua Madam hajui nani hasa ndiye halisi.
MBUNGE, IDRISS ‘FULL’ KUHUDUMIA
“Yani ni full kuhudumia. Mbunge kwa wakati wake amekuwa akimwaga chapaa kama hana akili nzuri. Amelipia nyumba ile ya Ununio jijini Dar na kama hiyo haitoshi, amekuwa akisimamia shopping za maana tu mjini na hata ile ndiga aliyojizawadia Wema katika sherehe yake ya kuzaliwa, mbunge huyo alihusika katika malipo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Idris naye si haba. Anajitutumua kwa upande wake, anaamini kwamba mzigo ni wake bila kujua mimba hiyo ina figisufigisu.”
IDRIS ASAKWA, AFUNGUKA
Gazeti hili lilimtafuta Idris kupitia simu yake ya mkononi ambapo alipopokea, alitiririka hivi:
Risasi: Mzee tumepata habari kwamba wewe ndiyo mhusika wa mimba ya Madam, vipi unazungumziaje taarifa hizo?
Idris: Kwenye hilo kwa sasa siwezi kuliongelea, labda unipe mwezi mmoja. Kichwa changu hakijatulia.
Risasi: Lakini inasemekana unagharamia kila kitu kwa sasa, ukiamini mzigo ni wako?
Idris: Aaa! Acha kuniingizia hayo mambo bwana. Wewe subiri huo mwezi mmoja ukipita nitakueleza kila kitu.

SHOGA ZAKE WAMSHANGAA!
Mashosti wake waliozungumza na Gazeti hili ambao hawakutaka kutajwa majina yao, walisema ni jambo la kushangaza kwa mwanamke kushindwa kumjua mwanaume aliyempa ujauzito.

WEMA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilifanya jitihada za kutosha kumsaka Wema kwa kumpigia simu na kumtumia ujumbe mfupi lakini hakupokea wala kujibu ujumbe huo.
KUTOKA KWA MHARIRI
Mimba ni jambo la kheri hivyo kwa kuwa Wema ameziona simu za wanahabari wetu zikimuuliza juu ya mhusika wa kiumbe hicho, ni vyema akawapigia na kuanika kila kitu kuhusu habari hii.

CHANZO: Global Publishers (GPL)

pichaz za Party ya Samatta na zawadi aliyopewa na Serikali kwa kutwaa tuzo

$
0
0
IMG_20160112_232125
Zawadi ya Samatta kwa Waziri mkuu ikipokelewa na waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi
Headlines za Mbwana Samatta kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani ya Afrika, bado inazidi kuleta furaha kwa wapenzi, mashabiki, watanzania na viongozi wa serikali kwa ujumla. Usiku wa January 12 Mbwana Samatta alifanyiwa party iliyopewa jina la Samatta Party. Party ilifanyika na serikali kutangaza kumpatia zawadi ya kiwanja Kigamboni na siku kadhaa mbele atakabidhiwa hati.
IMG_20160112_232228
Mkuu wa idara ya Vodacom kanda ya Pwani Harrieth Koka akiwa katika picha ya pamoja na Samatta
IMG_20160112_232252
Mshindi wa Big Brother Afrika Idris Sultan akiwa na Samatta
IMG_20160112_231625
IMG_20160112_231648
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zacharia Hans Pope kushoto na mwandishi wa habari za michezo Saleh Ally
IMG_20160112_231728
IMG_20160112_231754
Samatta katikati, kushoto waziri wa michezo Nape Nnauye na waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi
IMG_20160112_231815
IMG_20160112_232012
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akithibitisha serikali kumzawadia fedha na kiwanja maeneo ya Kigamboni.
IMG_20160112_231838
IMG_20160112_231857
Samatta akiwa na waziri Nape na Lukuvi pamoja na mama na baba yake.
IMG_20160112_231916
IMG_20160112_231936
Thomas Ulimwengu alikuwepo pia kumsapoti Samatta

Taswira za sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akikagua gwaride la Vikosi vya Ulinzi liliandaliwa rasmi katika kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar,zilizofanyika jana katika Uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi wakati wa kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Salim Ahmed Salim.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein mara alipowasili katika kilele cha sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete alipowasili katika kilele cha sherehe hizo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akisalimiana na Rais Mstaafu wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Pichani kutoka kushoto Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi,Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein,Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange.
Baadhi ya Wananchi na Maafisa mbali mbali wa Serikali wakiwa katika sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akisalimiana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu wakati alipowasili katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja katika Kilele cha sherehe za Mapinduzi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi walioshiriki katika kilele cha Sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 katika Uwanja wa Amaan Studium jana akiwa katika gari maalum.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi walioshiriki katika kilele cha Sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 katika Uwanja wa Amaan Studium jana akiwa katika gari maalum.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteremka katika gari maalum alilopanda wakati akiwasalimia wananchi katika kilele cha Sherehe za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 katika Uwanja wa Amaan Studium.

Baadhi ya Maafisa mbali mbali wa Vikosi vya Ulinzi na Taasisi za Serikali wakiwa katika sherehe za kilele cha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kutimia miaka 52 zilizofanyika katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Vijana wa Chama cha Mapinduzi wakibeba Picha la Marehemu Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Karume wakati wa Maandamano ya kusherehehekea Kilele cha Mapinduzi Kutimia miaka 52.
Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mjini wakibeba mabango yenye ujumbe tofauti kama yanavyoonekana wakati wa Maandamano ya kusherehehekea Kilele cha Mapinduzi.
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>