↧
Alichokisema Baba yake Samatta Uwanja wa Ndege Dar!
↧
Nonga, Busungu hawa jamaa hatari
YANGA ina zaidi ya washambuliaji watano kwa sasa ila wanaotazamwa kwa sana ni Donald Ngoma raia wa Zimbabwe na Amissi Tambwe wa Burundi.

Lakini huo ni mtego kwani Yanga ina mastraika wengine wawili wazawa, Paul Nonga na Malimi Busungu, hao jamaa ni hatari na wote wameshafunga bao moja moja kwenye Kombe la Mapinduzi wakitokea benchi.
Huwa wanaingia kutoka benchi na wakiwa huko kazi yao huwa kusoma makosa ya wapinzani na wakiingia huonyesha uhai wakicheza sambamba.
Nonga aliyejiunga na Yanga Desemba mwaka jana akitokea Mwadui FC, alifunga bao moja dhidi ya Mafunzo akitokea benchi na Busungu alifunga dhidi ya Mtibwa Sugar pia akitokea benchi.
Kocha wao, Hans van Der Pluijm raia wa Uholanzi amebaki mdomo na kutoamini jinsi Nonga na Busungu wanavyofanya vizuri uwanjani.
Pluijm alisema kuwa hali hiyo inamfanya awe na amani zaidi kwani hata kama Ngoma na Tambwe wasipokuwepo ana watu ambao wanaweza kumpatia matokeo mazuri.
“Hakika Busungu na Nonga wamefanya kile ninachokita, nawaomba wazidi kujituma zaidi ya hapo, kwani pacha yao nimeikubali na nitaendelea kuwatumia kama ninavyofanya siku zote.
“Niliamua kuwapa nafasi ya kuwachezesha pamoja baada ya kuona kuwa Ngoma na Tambwe wamechoka na wanahitaji kupumzika, lakini kazi yao nimeibukabili,” alisema Pluijm.
↧
↧
Majungu yenu yatamtoa Kerr Simba
HAKUNA kitu kingine zaidi ya majungu. Kocha wa Simba, Dylan Kerr amesema anaipenda sana timu yake ila kuna kitu kimoja kinaweza kumtoa katika kikosi hicho, nacho ni majungu.
Kerr anayepambana kuhakikisha Simba inarudi katika makali yake, alisema pamoja na jitihada zake zote anazofanya, anachoka kwani majungu na maneno maneno ya baadhi ya watu wasiopenda mafanikio yake vimezidi.
Alisema tangu alipojiunga na Simba, amekumbana na changamoto nyingi lakini kubwa zaidi ile ya kuzushiwa mambo ya ajabu ambayo yanamfanya atumie muda mwingi kuyafikiria kuliko kazi yake.
“Kitakachoniondoa Simba si kitu kingine bali ni majungu ya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakinipiga vita ili nisifanikiwe.
“Wananizushia mambo mengi kuwa sijui kufundisha ndiyo maana timu haifanyi vizuri, lakini wote huo ni uongo, ukiangalia mimi na makocha waliopita takwimu zinanibeba lakini chuki tu ndiyo zimewazidi.
“Hata hivyo nitaendelea kuitumikia timu yangu mpaka dakika ya mwisho kwa sababu siyo wote wanaonichukia lakini mambo yakizidi, basi nitaondoka ila kwa sasa napambana kwanza,” alisema Kerr.
↧
Video mpya: Linah - Nia Yangu
↧
Pam D kuzindua Video ya Popo Lipopo kesho Maisha Basement
↧
↧
Mbwana Samatta alivyopokelewa leo jijini Dar
Mchezaji Bora Afrika Mbwana Samattaleo alizunguuka mitaa ya jiji la Dar kuanzia Hoteli ya Hyatt Regency Kempinsk kupitia samora,shule ya uhuru pale karume msafara ukapinda kawawa road mpaka Morocco ulipopinda tena Alli Hassan Mwinyi, mpaka njia panda ya Kawe Pale Lugalo na kuelekea Old Bagamoyo mpaka Escape One ambapo kulikuwa na hafla fupi ya kumpongeza.
↧
Muswada wa Habari Kurejeshwa Tena Bungeni
MUSWADA wa Sheria ya Habari ambao uliwahi kupelekwa bungeni kisha kuondolewa kimya kimya, sasa unatarajiwa kurejeshwa tena bungeni mwezi huu.
Uwezekano wa kurejeshwa tena bungeni kwa muswada huo, kunatokana na kuundwa kwa kamati ya wanahabari sita, itakayoshirikiana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (pichani) kupitia muswada huo kabla ya haujawasilishwa bungeni baadaye mwezi huu.
Akizungumza Dar es Salaam jana na wahariri wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Nnauye alisema serikali inathamini mchango mkubwa wa vyombo vya habari na watendaji wake, na kwamba itashirikiana nao kuhakikisha sheria bora ya habari inapatikana.
Kamati hiyo imeundwa baada ya mapendekezo ya Waziri Nnauye ambaye alitaka kamati hiyo iundwe na ikutane naye Januari 13 mwaka huu, kwa ajili ya kuanza kupitia muswada huo wa sheria ya habari.
Wanaounda kamati hiyo ni Naibu Mhariri Mtendaji wa kampuni ya TSN, Tuma Abdallah, Mhariri Mkuu wa gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu na Mhariri Mtendaji wa gazeti la Jamhuri, Deodatus Balile.
Wengine ni Mhariri wa Upendo Media, Mengda Johanes, Prudence Constantine wa Shirika la Taifa la Utangazaji(TBC1) na Joyce Shebe wa Clouds Media.
Awali, akizungumza na wahariri hao, Nnauye alisema vyombo vya habari nchini vina mchango mkubwa katika taifa na vinapaswa kuwa na sheria inayowasimamia, ili kuhakikisha uhuru wa habari unakuwepo na pia kuwa kuwa na mipaka yake.
Nape aliongeza kuwa yeye ni muumini mzuri wa uhuru wa habari nchini, hivyo atahakikisha anatekeleza wajibu wake kwa kuharakisha mchakato wa muswada wa sheria hiyo, kwa kuhusisha wadau watoe mapendekezo kabla ya kuupeleka bungeni.
Alisema nia ya serikali kutunga sheria hiyo ni nzuri kwa kuwa inaweka utaratibu wa kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya vyombo vya habari ili kuwa na mazingira mazuri na yenye tija.
Akizungumzia masuala ya vitambulisho vya waandishi (press card), Nnauye alitoa wiki moja kwa Idara ya Habari (Maelezo) kuangalia kanuni na utaratibu mzuri wa jambo hilo na kutoa mwongozo utakaotumika kwa ajili ya utoaji vitambulisho hivyo na kwa muda gani.
“Nawapa siku saba Maelezo, mkakae, muangalie kanuni na taratibu zikoje, ili mniletee ripoti juu ya jambo hili,” alisema Waziri Nnauye.
Kuhusu Muswada wenyewe
Katika Bunge la Juni mwaka jana, serikali iliuondoa Muswada wa Sheria ya Haki ya Upatikanaji Habari wa mwaka 2015, uliokuwa usomwe kwa mara ya pili.
Katika Bunge la Juni mwaka jana, serikali iliuondoa Muswada wa Sheria ya Haki ya Upatikanaji Habari wa mwaka 2015, uliokuwa usomwe kwa mara ya pili.
Ilieleza kuwa muswada huo utasubiri bunge jipya litakapokaa, baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka 2015.
Akitoa taarifa ya kuondolewa kwa muswada huo bungeni mbele ya Naibu Spika, Job Ndugai (wakati huo), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), kwa wakati huo, Profesa Mark Mwandosya alisema, “Uamuzi wa kuuondoa umeafikiwa na Serikali baada ya Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Huduma za Jamii kuishauri hivyo.”
Mwandosya alisema sheria hiyo ya upatikanaji habari ilichapishwa Februari 20 mwaka 2015 na kusomwa bungeni kwa mara ya kwanza Machi 12 hadi Aprili mosi mwaka huo.
Alisema muswada huo si wa dharura, kwa kuwa umepitia hatua mbalimbali, ikiwemo kujadiliwa na kamati hiyo Juni 22.
↧
Magazeti Ya Leo Jumapili ya Tarehe 10, 2016
↧
NYUMA YA MACHOZI - 15

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
“Siyo kuwasumbua, niligundua nilifanya kosa katika maelezo ya kuyapata hayo madawa, ndiyo maana nimepiga tena simu haraka.”
“Kwa hiyo tutakuwa basi tumechemsha.”
“Bado hamjachemsha.”
“Tusaidie jinsi ya kuyapata.”
“Mkoba wake mwekundu anao?”
“Ndiyo.”
SASA ENDELEA...
“Basi huo ndio wenye dawa hizo.”
“Mbona tumempekua hatujaona kitu?”
“Huyo dada ni muuzaji wa kimataifa wa dawa za kulevya, hata siku moja hamuwezi kumkamata kirahisi.”
“Tusaidie basi tujue ameficha wapi?”
“Huo mkoba wake umeshonwa maalumu kwa ajili ya kuvusha dawa za kulevya, una karatasi za lailoni ambazo haziwezi kuruhusu vipimo vyenu kuona ndani kuna kitu gani. Juu kuna manyoya hufanya mkoba huo mtu yeyote asiutilie wasiwasi. Kwa mtindo huo, umemfanya mwanamke huyu aendeleze biashara yake haramu ya dawa za kulevya bila kushikwa.”
“Kwa hiyo una maanisha mkoba alishonwa na dawa zake kabisa?”
“Ndiyo maana nikasema huyo dada ni muuzaji wa kimataifa, huzunguka sehemu zote bila kukamatwa na kumfanya aweze kujikusanyia fedha nyingi kila kukicha.”
“Una uhakika na unachokisema?”
“Kwa nini nimewapa picha jinsi alivyo na mmempata bila tatizo, kuna kitu nilichowaeleza akakataa?” “Mpaka sasa upo sahihi.”
“Basi pasueni mkoba wake mtanipa jibu, asante.”
Baada ya kusema vile alikata simu. Baada ya simu kukatwa, Deus alitumia dakika tano kutafakari maneno ya mtu aliyejiita msamalia mwema ili kutoa uamuzi ambayo kama utakwenda kinyume unaweza kumuhalibia sifa. Aliamuru yule mwanamke aingie, aliitwa na kuingia ndani na kukaa kwenye kiti. “Samahani,” alianza Mr Deus kumtaka radhi Teddy. “Bila samahani mkuu.”
“Naomba uniambie ukweli kuhusu sehemu ulipoficha dawa za kulevya.”
“Nimeeleza kila kitu, sasa mnataka nini? Sijui lolote juu ya dawa za kulevya nashangaa kunihusisha na biashara hatari kama hizo.”
“Naomba nifanye upekuzi kwenye mkoba wako.” “Huu hapa angalia,” Teddy alisema huku akiuweka mkoba wake juu ya meza.
“Kabla sijaupasua naomba uniambie ukweli juu ya kuficha dawa za kulevya.”
“Mkoba si huo hapo fanyeni muwezavyo utajua ukweli kuwa sihusiki japo kuwa watu wananipaka matope,” Teddy alisema kwa kujiamini. Mr Deus aliagiza kisu ili aupasue mkoba mbele yake, Kabla hajaupasua Teddy alimtaadhalisha.
“Kumbuka mkoba huu nimeununua pesa nyingi robo ya bajeti ya wizara moja kubwa katika serikali yako.” “Hiyo siyo juu yako.”
“Sema unataka shilingi ngapi ili usiharibu mkoba?”
“Sihitaji fedha yoyote zaidi ya kuupasua mkoba huu.” “Haya fanya uwezavyo lakini mwisho wa siku utaumbuka.”
Mr Deus hakumsikiliza alichukua kisu na kuanza kuupasua mkoba ili kupata uhakika kwa yale aliyoelekezwa na msamalia mwema. Alipoanza kuupasua mkoba Teddy aliomba asitishe zoezi. “Samahani mkuu.”
“Bila samahani,” Deus alijibu akiwa amesitisha zoezi la kuupasua mkoba.
“Naomba tuzungumze.” “Tutazungumza nikimaliza, fedha ya robo bajeti ya wizara hata mimi naweza kuilipa peke yangu wala usiwe na wasiwasi,” Mr Deus alijibu huku akinyanyua kisu kukididimiza kwenye mkoba.
“Naomba unisikilize kaka yangu,” Teddy alikuwa mpole ghafla.
“Juu ya nini?”
“Kuhusu huo mkoba.”
“Una nini?”
“Samahani kaka yangu naomba unisilize mdogo wako.”
Mr Deus aliacha kuuchana mkoba na kumgeukia Teddy aliyekuwa akitokwa na jasho japo ofisi ya Mr Deus ilikuwa na kiyoyozi kikali.
“Mhu! Unasemaje?”
“Najua nimepatikana, lakini naomba msaada wako?” “Umepatikana kivipi na unaomba msaada upi?”
“ Kila ulichoelezwa ni kweli?”
“Na nani?”
“Simjui, lakini inaonekana ananijua vizuri, sasa nifae kwa mvua nitakufaa kwa jua.” “Sijakuelewa,” Mr Deus alimshangaa Teddy.
“Ni kweli mfuko huu una dawa na kwa sasa nipo chini ya ulinzi na ukinifisha mahakamani nitafia gerezani, umri wangu bado mdogo. Nakuomba uniokoe kwa hili nipo radhi kukupa kiasi chochote ukitakacho hata ukiacha kazi unaweza kula miaka hamsini bila tatizo.”
“Lakini unajua dawa za kulevya ni haramu?” “Najua, na ndiyo maana nipo chini ya ulinzi.” “Sasa nikiwasikiliza wote tutamkamata nani?”
“Yaweza usione umuhimu wangu kwako leo, lakini kwangu mimi wewe ni mtu muhimu kama malaika mtoa roho aliyeahilisha kuchukua roho mama mzazi muda mfupi baada ya kujifungua.”
“Kwa ubinaadamu ni kweli nilitakiwa kukusaidia, lakini kwa vile ni dhamana niliyopewa na taifa sina budi kuwa na uso wa mbuzi.”
“Si kwamba nakulazimisha au nakufundisha kazi, hata hao wakubwa zako waliokutuma wanapokea mrungula. Amini usiamini kuna viongozi katika serikali yako hata viongozi wa dini mwenye heshima katika taifa hili wanaifanya biashara hii. Unaweza kunikamata na nikafungwa, lakini bado utakuwa umechota kikombe cha maji kwenye bahari hutapunguza kitu. “Nina imani msaada wako leo unaweza kukusaidia siku za mbele, mbegu ya wema siku zote haiozi.
Naomba unisaidie kwa leo nina imani nitakapotoka huwezi kujilaumu kwa msaada wako. Sema kiasi chochote ukitakacho hata kikipita fedha za mzigo huu nipo tayari kukupa tena muda huu.”
Kauli ile ilimfanya Deus alitulie kwa muda huku akiona sura ya yule binti ilivyoonesha kuomba msaada wake. Kila alilolizungumza alililona lina uzito kwake. Taratibu moyo ulilainika na kuona kuna umuhimu wa kumsikiliza yule msichana.
“Unajua binti unanipa wakati mgumu,” Deus alisema kwa sauti ya chini.
“Kivipi kaka yangu?”
“Unajua vijana wangu wakiona nakuachia wakati mimi ndiye kiongozi wao watanielewaje?”
“Sikiliza mkuu hakuna hata mmoja anayejua huku ndani kipi kinaendelea, wengi wanajua ni mazungumzo ya kawaida.”
“Mmh! Sasa kwa kesi nzito kama hii unanipa kiasi gani?”
“Chochote ukitakacho utakachokiona kinalingana na kosa hili.” “Kwa vile wewe ndiye uliyetangaza biashara kusema ili nione kama kinalingana na kosa lenyewe.”
“Lakini huu mzigo si utaniachia?”
“Itategemea na kiasi cha mzigo utakaotangaza.”
“Milioni 50.”
“Hailingani na kosa lako, kumbuka hapa nauza kazi naweza hata kufungwa maisha ikigundulika.”
“75.”
“Okay, nisikuumize sana nipe hizohizo.”
“Na mzigo wangu?”
“Utaondoka nao, nitapataje mzigo wangu?”
“Kama una kijana wako nimuagize aende sasa hivi akachukue mzigo mimi nikiwa hapa akipata utaniruhusu niondoke.”
“Itakuwaje?”
“Nampigia simu mtu ukisikia kisha unanipa mtu wako nimuelekeze akachukue.”
“Okay, fanya hivyo.”
Teddy alichukua simu yake iliyokuwa mezani na kubofya namba kisha alisema:
“Haloo Tonny.”
“Eeh, Teddy.”
“Andaa milioni 75 kuna mtu atakuja muda si mrefu.”
“Hakuna tatizo, nitamtambuaje?”
“Nitakujulisha.” Teddy alikata simu na kumgeukia Mr Deus aliyekuwa akishangazwa na uwezo wa kifedha aliokuwa nao binti yule.
Alikubaliana na kauli ya mtu aliyejiita msamalia mwema kuwa binti yule ni mfanya biashara mzoefu pia mwenye utajiri mkubwa.
“Basi mjulishe huyu mtu wako ili nimwelekeze akachukue mzigo.”
“Hakuna tatizo ngoja nimpigie ili nikupe umuelekeze,” Deus alisema huku akichukua simu na kumpigia rafiki yake Kinape afuatilie dili lile.
“Haloo Kinape upo wapi?”
“Ndiyo natoka kazini.”
“Hebu zungumza na dada huyu akuelekeze sehemu akakupe mzigo wangu.”
“Hakuna tatizo,” Deus alimpa simu Teddy ambaye alimuelekeza sehemu ya kukutana ampe mzigo huo. Baada ya maelekezo Teddy alimgeukia Deus na kumuuliza.
“Nina imani utaamini kwamba mimi si mtu wa kubabaisha.”
“Mpaka tutakapo maliza kazi.”
Mr Deus alinyanyua simu na kumwita secretary wake, baada ya muda alifika na kukakamaa kikakamavu mbele ya mkuu wake.
“Abee bosi.”
“Mletee mgeni kinywaji.”
“Sawa mkuu.” Aligeuka na kuondoka, baada ya muda alirudi na sahani iliyokuwa juisi ya paketi na glasi mbili. Aliweka juu ya meza na kuwawekea wote kisha aliwakaribisha.
“Karibuni Juisi dada.”
“Asante,” alijibu Teddy huku akichukua glasi ya juisi moyo wake ukiwa umeanza kutulia. “Lete stori,” Deus alivunja ukimya.
“Ninalo kaka yangu, nakuahidi si leo si kesho msaada wako hutaujutia.”
“Kwa nini mnakaa na fedha nyingi kiasi hicho ndani?”
“Kaka yangu kazi yenyewe bila ya kuwa na fedha za haraka unaozea gerezani.”
Wakati wa mazungumzo simu iliingia toka kwa secretary, alipokea na kuzugumza.
“Simu ya Italia mkuu.”
“Niachie.”
“Haloo.”
“Ndiyo msamalia mwema?”
“Vipi mzigo umeuona?” “Kazi umeisha tupa tuachie tuifanye,” Deus alijibu kwa jeuri kidogo.
“Mkuu sina maana ya kukufundisha kazi bali kufanikisha kukamatwa kwa huyo malaya.”
“Asante kazi inakwenda vizuri.” “Mmeziona?” “Hiyo si kazi yako.”
“Sawa mkubwa mara hii nimekuwa adui?” “Siyo adui tunashukuru kwa msaada wako mambo mengine ni siri ya ndani hatakiwi mtu mwingine kujua.”
“Nakutakia kazi njema.”
“Na wewe pia.”
Baada ya kukata simu Teddy aliyekuwa akifuatilia mazungumzo yale alijua mbaya wake bado alikuwa akimuandama kwa kufuatilia mpango wake.
“Samahani mkuu.”
“Bila samahani.” “Naomba nimjue huyo mtu.” “Hapana ni siri ya jeshi.”
“Kaka yangu nipo radhi kukuipa pesa ile mara mbili ili nimjue tu.” “Ukimjua?”
“Basi tu nitakaa naye mbali.”
“Kwa kweli amekataa kutaja jina lake zaidi ya kujiita msamalia mwema.”
“Anatokea wapi?”
“Italia.”
“Asante kwa msaada wako.”
Mara simu iliita, Teddy aliipokea na kusema: “Eeh! Tayari hebu mpe simu nizungumze naye,” Baada ya kupewa alizungumza:
“Eeh! Umefika?” “Ndiyo.” “Hebu zungumza na mkuu hapa,” alimpa simu azungumze na Kinape.
“Eeh! Kinape umefika?”
“Ndiyo.”
“Ni yeye,” Deus alimgeukia na kumwambia Teddy.
“Nipe simu.”
Baada ya kumpa alimwambia mtu wa upande wa pili.
“Tonny mpe mzigo mpe ulinzi mpaka atakapozifikisha salama.”
“Hakuna tatizo.” Teddy alikata simu na kumgeukia Mr Deus na kumuuliza:
“Utazipeleka wapi?”
“Nyumbani.”
“Naomba uzipeleke benki ni nyingi sana sitaki upoteze nguvu zako bure,” Teddy alimshauri Deusi.
“Sawa nitafanya hivyo.”
“Deus alipigia Kinape simu na kumweleza azipeleke benki katika akaunti ya Kinape yeye angezichukua baadaye.
Tonny alimsindikiza Kinape mpaka benki ambapo aliweka fedha yote aliyopewa kwenye akaunti yake. Baada ya kuweka alimpigia simu Deus kumjulisha.
“Mkubwa kazi imekwenda vizuri.”
“Amekupa zote?”
“Ndiyo.”
“Shilingi ngapi?”
“Milioni 75.”
“Ooh, vizuri umeshaziweka benki?”
“Ndiyo natoka sasa hivi.”
“Basi tutaonana baadaye nyumbani.” “Hakuna tatizo mkuu?” Deus baada ya kupata uhakika kwa Kinape alimgeukia Teddy aliyekuwa akiendelea kunywa juisi taratibu bila wasi kama hakuna kitu cha hatari kilikuwa mbele yake.
“Teddy,” alimwita.
“Abee.” “Nafikiri kila kitu kimekwenda vizuri.”
“Hakuna tatizo, naheshimu sana kazi yako pia muda wako.”
“Asante lakini kumbuka umeniweka katika wakati mgumu sana.”
“Kawaida tu kaka yangu, nakuapia ulichokifanya leo hutakijutia maishani kwako, huenda leo usione umuhimu wake lakini ipo siku utayakumbuka maneno yangu.”
Itaendelea
↧
↧
NYUMA YA MACHOZI SEHEMU: 16

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Deus baada ya kupata uhakika kwa Kinape alimgeukia Teddy aliyekuwa akiendelea kunywa juisi taratibu bila wasi kama hakuna kitu cha hatari kilikuwa mbele yake.
“Teddy,” alimwita.
“Abee.” “Nafikiri kila kitu kimekwenda vizuri.”
“Hakuna tatizo, naheshimu sana kazi yako pia muda wako.”
“Asante lakini kumbuka umeniweka katika wakati mgumu sana.”
“Kawaida tu kaka yangu, nakuapia ulichokifanya leo hutakijutia maishani kwako, huenda leo usione umuhimu wake lakini ipo siku utayakumbuka maneno yangu.”
SASA ENDELEA...
“Basi wacha nikutoe ili ukapumzike na safari.”
“Na kweli muda huu ningekuwa nimelala, hata chakula ningekula jioni baada ya kuamka.”
“Pole sana ni harakati za maisha.”
“Tunaweza kwenda,” Deus alisema huku akinyanyuka na kuweka vitu vyake sawa kwenye meza. Teddy alinyanyuka na kuchukua mkoba wake wenye dawa za kulevya na kuuweka begani kisha alitangulia kutoka, alipofika kwenye korido la kutokea nje alisimama kumsubiri Deus kuogopa maswali kwa baadhi ya watu ambao angekutana nao njiani.
Baada ya kuweka ofisi yake sawa Deus alitoka na kumpitia Teddy kwa kumshika mkono, kwa mtu angewaona kwa mara ya kwanza angeamini wale ni marafiki wanaojuana muda mrefu.
Lakini kumbe muda mfupi walikuwa chui na paka. Walikwenda kwenye gari na kuondoka kumrudisha sehemu aliyofikia, lakini Teddy aliomba aachwe sehemu ambako ataingia kwenye gari litakalomfuata na kwenda kwake. Wakiwa njiani Teddy alianzisha mazungumzo.
“Nashukuru kwa ukarimu wako.”
“Japo unanishukuru, lakini kumbuka nimenilazimisha nimeisaliti nchi yangu kwa damana waliyonipa ya kulinda nchi yangu.”
“Huenda leo huijui faida yake lakini narudia kukuapia msaada wako hautakwenda bure, ila nilikuwa na wazo moja.” “Wazo gani?”
“Najua kazi hii umepewa na taifa lakini kuna maisha badala ya kazi.”
“Hayo najua, ulikuwa na maana gani?”
“Hivi ukistaafu utalipwa kiasi gani?”
“Kiasi cha kawaida.”
“Nina imani hakitaweza kuyaendesha maisha yako?” “Ni kweli kabisa.”
“Sasa unaona unafanya kazi ya mamilioni lakini mwisho wa siku unakufa maskini.”
“Ni kweli, lakini kazi yetu inalenga kujitolea na si kujitajirisha.”
“Wewe unasema hivyo wakati wakubwa zako wanaokutisha usichukue rushwa, wao ndiyo wanaongoza kuwa na utajiri wa kutisha.”
“Sasa wewe ulikuwa unanishauri nini?” “Nataka kupitia kazi yako uweze kufaidika ili mwisho wa siku ulie kivulini.”
“Kwa hiyo unanishauri nile rushwa.”
“Kula rushwa siwezi kukushauri nina imani hii si rushwa ya kwanza inawezekana umeisha kula nyingi, inaonesha kabisa unakula za kawaida mimi nilitaka tufanye biashara kwa muda mwaka mmoja uwe trionea.”
“Kazi hii ukiifanyia tamaa huchelewi kushtukiwa na mwisho wa siku unapigwa chini au unategewa mtego na ukinasa unafia gerezani.”
“Biashara hiyo nataka tufanye sisi wawili.”
“Kumbuka biashara hii mwisho wake mbaya kwa mfano ungekutana na mtu aliyekunywa maji ya bendera ya taifa si ungepotelea gerezani?” “Kabla ya kupotelea gerezani yeye kabla ya jioni jina lake lingebakia historia midomoni mwa watu.”
“Una maana ungemuua?”
“Siku zote kazi na dawa.”
“Nani angemuua wakati wewe umo ndani?”
“Mtandao ni mkubwa, miongoni mwenu kuna mtu angemuua.”
“Kwa nini mnamuua?”
“Kifo chake ni kupoteza ushahidi ili wakubwa wako wapate nafasi ya kunitoa kwa urahisi.” “Kama kuna wakubwa wanaweza kukutoa kwa njia hiyo, kwa nini hukuitumia kuliko kutoa fedha nyingi kiasi hicho?”
“Hii ni biashara kati yako na mimi hivyo lazima tukubaliane tukishindani lazima nitumie ya upande wa pili ambayo huwa sipendi kuitumia kwa kuamini kila mwanadamu ni muelewa wote tunatafuta kwa njia ya halali na haramu.”
“Kwa nini usiokoe fedha nyingi kuliko kutoa bila sababu.”
“Njia ya pili ina faida na hasara zake, faida ni kutoka salama lakini hasara zake kwanza kutoa uhai wa mtu ambao kwa kupitia uwezo wangu wa kifedha huwa sipendi kuutumia.
“Pili mara nyingi unaweza kutoka salama lakini mzigo wako ukapotea mikononi mwa dola, mara nyingi ukikamatwa kwanza taarifa zako zinafika katika vyombo vya habari hata kama ukitoka unakuwa umechafuka. Na mzigo nao unakuwa katika stoo kabla ya kuteketezwa hivyo inakuwa vigumu kuupata. Kama nitatumia njia ya kutoa fedha nyingi lakini ukiuza unarudisha faida japo kidogo.”
“Inaonesha una fedha nyingi, kwa nini usiachane na kazi hatari kama hii?”
“Hakuna mwanadamu anayetosheka fedha kila kukicha matajiri wanabuni miradi kuongeza kipato.”
“Lakini si kwa kazi kama hii.”
“Basi kwa taarifa yako kuwa watu wana fedha kufuru kwa kazi hii, kutokana na uwezo wao wamekuwa wakiwatuliza wenye viherehere. Hebu tuachana na hayo naomba tufanye kazi niliyokueleza awali, kwa muda mfupi nimeamini wewe ni mtu muhimu sana kwangu.”
“Kazi gani?”
“Kwa vile upo kwenye kitengo hiki naomba utumie cheo chako kufanikisha biashara hii. Nakuahidi kila safari yangu ikivuka salama una milioni 250.”
“Una sema?” Deus aliuliza kama hakusikia. “Nitakapopita salama, nikifika nyumbani nakukabidhi milioni 250 hata kabla sijafanya biashara.”
“Kwa mwezi utakuja mara ngapi?”
“Itategemea mara moja au mara moja kwa miezi miwili.”
“Naomba unipe muda wa kufikiria jambo hili.”
“Kama ningekuwa mimi wala nisingesubiri kwani kijua ndicho hiki, ila napenda kukuonya kitu kimoja.”
“Kitu gani?”
“Kama utakubali kuufanya mpango huu ambao nakuhakikishia kwa mwezi kupitia mtandao wangu utatengeneza bilioni moja.”
“Bilioni moja?”
“Ndiyo, watu wanne wakiingia kwa mwezi mmoja utakuwa na kiasi gani?”
“Nimekuelewa na nini ulichotaka kunionya?”
“Nakuomba chonde chonde mpango hatari kama huu usimshirikishe mkeo.”
“Kwa nini?”
“Wanawake nawajua mvizuri si waficha siri kwenye wakati mgumu, kosa lolote litalotokea kwenye ndoa anaweza kutumia kukuangamiza.”
Kauli ile ilimshtua Deus kwani mipango yote ya awali aliyofanya, mkewe ndiye aliyekuwa msiri wake. Lakini alikuwa mstari wa mbele kumshauri mambo ya kimaendeleo hata baadhi ya fedha za rushwa aliziweka kwenye akaunti ya mkewe.
“Deus najua kabisa ulimshirikisha mkeo mambo yako ya nyuma, lakini kwa hili naomba iwe siri yako. Watu wengi wanaocheza michezo michafu kama hii huwaua hata wake zao pale wanapoona wamegundua kazi zao za hatari zinazoweza kuwapotezea maisha.
Lakini sikushauri umuue mkeo, ila nakuomba ili uweze kuwa tirionea kwa muda mfupi kwani mtando una watu zaidi ya kumi mwezi mmoja wote wakipitia katika mikono yako salama utajikuta ukitengeneza bilioni mbili na nusu kwa mwezi, unataka Mungu akupe nini?”
“Nimekuelewa nina imani ukiwa tayari nijulishe, tutaifanya kazi.”
“Nashukuru kuwa muelewa, huwezi kuamini wewe ni mtu wa kwanza kumueleza mpango huu wa hatari. Naomba usinigeuke unaweza kunishangaa pamoja na umbile langu dogo lakini nitakachokufanya hutasahau maisha yako yote.”
“Ondoa wasiwasi kazi itafanyika.”
“Niteremshe hapa watu wangu wamenifuata, mambo mengine tumia namba yangu hii ya simu ambayo ni watu muhimu tu wanayoijua.
” Deus alimteremsha Teddy ambaye aliingia kwenye gari lenye tinted na kutoweka kwa mwendo wa kasi na kumwacha Deus akilisindikiza kwa macho huku akiuona utajiri mbele yake.
Baada ya Teddy mwanamke hatari katika kuuza dawa za kulevya kuondoka, Deus alijikuta akipoteza ujasiri wa kulitumikia taifa na kujikuta akiota ndoto ya utajiri kwa kujiingiza kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Aliamua kurudi ofisini kumalizia kazi zake ili jioni akakutane na Kinape akiamini kabisa rafiki yake hawezi kumweleza mtu yeyote siri ile kama livyomkataza.
*******
Wakati akiwaza yale rafiki yake Kinape alikuwa na furaha ya ajabu moyoni mwake, alipofika nyumbani Kilole alitaka kujua furaha yake inatokana na nini.
“Vipi mwenzangu leo mbona una furaha umeongezwa mshahara nini?”
“Sasa hivi mimi ni milionea.”
“Una maana gani kusema hivyo?” Kilole alihoji. Alimpa picha yote ilivyokwenda, Kilole baada ya kusikiliza taarifa ile alimweleza kitu Kinape. “Mungu mkubwa.”
“Una maana gani kusema hivyo?” “Sasa mpango wetu utakamilika.”
“Una maana gani?”
“Sasa hivi ni wakati muzuri wa kumpotezea mbali Deus.”
“Tusifanye hivyo.” “Shauri yako akigundua atakumaliza wewe.”
“Kwa hiyo unanishauri nini?”
“Kwa vile benki kuna milioni 75 zinatutosha kwangu nina milioni 24 huoni milioni 99 zitatusaidia kufanya mambo mazuri baada ya kumuua tutauza majumba yake mawili na magari kisha tutafungua mradi wowote wa kutuendeleza kimaisha na kuuhama mji huu.”
“Hapana tusimuue.”
“Lazima Deus afe, ikiwezekana kazi ifanyike leo usiku.”
“Hapana tusifanye pupa tunaweza kuozea gerezani au hata kunyongwa kama ikigundulika sisi ndiye tuliyehusika na kifo chake.”
“Sasa tufanye nini?” “Hebu nipe muda.”
“Muda gani Kinape, mchicha umeisha kolea nazi fedha za kutosha tunazo tunasubiri nini?”
“Japo lolote zuri halihitaji haraka,” Kinape alimtuliza Kilole aliyekuwa na pupa. “Mpaka lini?”
“Nipe siku mbili.”
“Na ziwe siku hizo mbili, ukizidisha utakuta mzoga wa mtu ndani.”
“Unataka kujiua?”
“Nani afe, nitamnyongelea mbali Deus.”
“Punguza pupa kila kitu kitakwenda vizuri.”
“Lazima nikueleze ukweli Kinape hakuna mwanaume chini ya jua ninaye mpenda kama wewe.”
“Hilo nalijua lakini yote uliyataka wewe.”
“Lakini kukubali kwangu kuolewa na Deus huoni faida leo hii akaunti yako kuna milioni 75 hukuwahi kuota kuingiza fedha kama hizi.”
“Mmh! Na kweli.”
***
Deus baada ya kazi alirudi nyumbani na kupokewa kwa furaha na mkewe huku Kilole akionesha mapenzi mazito kwa mumewe ili kumfumba macho kabla kumtendea unyama. Baada ya chakula cha usiku Deus alimtoa nje rafiki yake ili ampe taarifa za utajiri wa ajabu unaokuja mbele yake.
“Unataka kuniambia kwa mwezi utakuwa unaingiza milioni 1000?”
“Ndio maana yake, nataka baada ya muda nipabadilishe kijijini kwetu pawe kama peponi.”
“Mmh! Mshiko mzito kauli ya yule dada kwa miaka mitano dunia utaishika mkononi.”
“Yaani naona kama ndoto.”
“Ungekuwa mnoko ungeishia na virushwa vya milioni kumi.”
“Basi naomba siri hii isimpe mtu mwingine, nimekupa wewe mtu wa karibu hata mke wangu sitamwambia ni siri ya hatari sana.”
“Hii ni siri nzito siwezi kumwambia mtu.”
“Hujui dhamira yangu kwako, katika kila fedha itakayo ingia asilimia kumi nitachukua wewe.”
“Unataka kuniambia katika milioni 1000 zangu ngapi?”
“Milioni 100.”
“Wachaaa, usinitie uchizi kwa furaha.”
“Lazima nikujali nataka nawe kijiji upabadilishe wajue kweli watoto wao tumekuja kutafuta maisha.” “Kweli nimeamini wewe ni zaidi ya ndugu.”
“Nathamini urafiki wetu tumetoka mbali kumbuka ndoto zetu tulipanga kufanya nini?” Baada ya mazungumzo walirudi ndani, Kilole hakuwa na haraka ya kujua walichokuwa wakizungumza kwa kuamini yote angeyajua kupitia kwa Kinape. Usiku nao ulikuwa wa raha kwa Kilole kuendelea kuonesha kumjali mumewe kwa kumpa penzi tamu ambalo lilimpagawisha Deus na kujikuta akimuahidi mkewe gari la milioni 20.
Kilole alijisemea moyoni kuwa asali ile aliyomlambisha ni chambo cha kumuingiza kwenye mtego wamlipue hakuwa na mapenzi tena na mumewe na kumuona shetani wa roho yake aliyetamani afe wakati wowote ili afaidi penzi tamu la Kinape.
Itaendelea
↧
NYUMA YA MACHOZI -17

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Kilole alijisemea moyoni kuwa asali ile aliyomlambisha ni chambo cha kumuingiza kwenye mtego wamlipue hakuwa na mapenzi tena na mumewe na kumuona shetani wa roho yake aliyetamani afe wakati wowote ili afaidi penzi tamu la Kinape.
SASA ENDELEA...
***
Siku ya pili Kinape alichelewa kutoka kwenda kazini kutokana na ishara aliyooneshwa na Kilole kuwa asiondoke ili wazungumze. Deusi aliondoka peke yake kuwahi kazini huku akijiona alichelewa kupata dili kubwa kama zile. Alipofika ofisini aliwasiliana moja kwa moja na Teddy mwanamke muuza unga. “Haloo Teddy.”
“Ooh! Brother za asubuhi?”
“Nzuri.”
“Nina imani una habari njema asubuhi hii?”
“Ni kweli, mimi nipo tayari kuifanya ile kazi.”
“Ooh! Vizuri sana, tena una bahati washirika wangu wote wapo hapa.”
“Kwa hiyo?”
“Basi jioni tukutane ili tuzungumze jinsi ya kufanya.”
“Hakuna tatizo.”
“Nakutakia kazi njema kaka yangu.”
Deus baada ya kukata simu alitabasamu kidogo kabla ya kuanza kazi. Wakati yeye anapanga mipango ya utajiri, nyumbani kwake pia kulikuwa na mipango ya kummaliza. Kinape baada ya kujiandaa kwenda kazini kabla ya kutoka chumbani Kilole alimfuata.
“Vipi mpenzi?”
“Safi.”
“Naona jana jamaa alikuita chemba alikuambia nini, au ndiyo anataka uwahi kumuoa Happy?”
“Walaa.”
“Alikuitia nini?”
“Jamaa anataka kututajirisha.”
“Kututajilisha una maana gani?” Kinape alimueleza yote aliyoelezwa na Deus pamoja na kukatazwa kuitoa siri ile nje. Pamoja na kusikia mpango ule wa mabiloni ya shilingi bado Kilole aliona wanamchelewesha.
“Kinape hiyo fedha itapatikana lini huoni kama tunachelewa, tuachane na mpango wake tummalize tufikiri mambo mengine.”
“Kilole zile ni fedha nyingi zitakazo tufanya tuishi kama peponi, tutakula mpaka tunakufa bila kufanya kazi.”
“Kwani huo mpango mwezi gani?”
“Wanamsubiri yeye tu watu waingine unga wakati wowote.”
“Mmh! Nitavumilia lakini kwa upande wangu naona zilizopo zinatutosha.”
“Ni kweli lakini tutafanya kosa kumbwa kuacha mabilioni ya fedha.”
“Mmh! Sawa.”
****
Wakati Kilole na Kinape wanapanga mipango ya kummaliza Deus, Jimmy mpiga picha naye alikuwa akipanga yake. Aliamini kupitia picha zile atajipatia fedha na penzi toka kwa Kilole mwanamke aliyempenda kupindukia. Aliamua kumtumia rafiki yake kumtisha ili wapate fedha. Kilole akiwa katika usafi wa kawaida wa nyumba simu yake iliita, namba ilikuwa ngeni kwake. Alibofya cha kupokelea na kusema:
“Haloo.”
“Haloo, nazungumza na Kilole.” “Ndiyo, nani mwenzangu?”
“Naitwa Simon, kumeokota picha zako ambazo zinaonesha unafanya uchafu kwa hiyo ili nisizisambaze nataka milioni tano.”
“Picha zangu?” Kilole alishtuka.
“Eeh, tena unafanya uchafu na ndugu wa mumeo, kabla picha hazijamfikia mumeo tunaomba huo mzigo.”
“Na..na..omba unipigie baada ya dakika tano,” Kilole alichanganyikiwa na kuona Jimmy amemgeuka. Kwa haraka alimpigia simu Jimmy kutaka kujua picha zake zimemfikiaje mtu mwingine. Alipopiga simu iliita kwa muda bila kupokelewa, hakukoma alirudia tena na kupokewa upande wa pili.
“Haloo Sister,” Jiimy alipokea upande wa pili. “Nazungumza na Jimmy?”
“Ndiyo Sister, lete stori.”
“Jimmy nilikueleza nini?”
“Kuhusu nini?”
“Kuhusu picha.”
“Kwani vipi?” “Kuna mtu kanipigia simu anasema ameokota picha zangu kwa hiyo anataka milioni tano la sivyo atazisambaza au kumpelekea mume wangu.”
“Ha!” Jimmy alijifanya kushtuka.
“Jimmy tulizungumza nini na umefanya nini?”
“Samahani Sister, wiki mbili zilizopita nilivamiwa ndani na kuibiwa vitu vingi, nina siku mbili tangu nitoke hospitali.”
“Taarifa ulifikisha polisi?”
“Niliogopa kwa vile kulikuwa na picha zako.” “Jimmy kwa nini umekaa na picha zangu, kama pesa yako nilikulipa yote?”
“Sister niliamini picha zile ulikuwa na umuhimu sana kwako hivyo ungeweza kuzipoteza ndiyo nikaamua kuzihifadhi nyingine kwangu.”
“Sasa umeona umenitia hasara?”
“Sikujua ingekuwa hivyo.”
“Sasa nitafanyaje, utawezaje kunisaidia?”
“Dada yangu kama fedha unayo ungempa kwa kweli picha zile siyo nzuri kuonwa na mumeo.” “Nampa lakini kumbuka umenifanyia kitu kibaya sana.”
“Najua lakini nia yangu ilikuwa nzuri tu.”
“Okay, imekwisha tokea sina jinsi, ila baadaye nitakupa kazi ya kunifanyia.”
“Hakuna tatizo dada yangu ila pole sana.”
“Bado sijapoa mpaka uifanye kazi yangu kwa asilimia mia.”
“Hakuna tatizo.”
“Basi baadaye.”
Kilole alikata simu na kumpigia aliyempa taarifa ya kuokotwa kwa picha zake. Baada ya kuita ilipokelewa upande wa pili.
“Ndiyo, sema.”
”Ulisema?” Kilole aliuliza.
“Kuhusu nini?”
“Si umesema una picha zangu?”
“Ndiyo.”
“Samahani kaka angu.”
“Samahani ya nini, fedha haipungui hata senti tano kama huna niifanye kazi yangu,” upande wa pili ulimtisha.
“Kaka yangu mbona unanifanyia ukatili kama huo, nimekukosea nini mpaka kushindwa kunisikiliza?” “Dada eeh, niambie utatoa mzigo au hutoi nijue moja sikuja kubembelezana.”
“Sio kwanza sitoi, nitatoa hata zaidi lakini nilitaka kujua hizo picha umeziokota wapi na zilikuwa kwenye nini?”
“Dada yangu eeh, sipo mahakamani kama mshiko upo nijulishe nina mambo mengi, hivi unafikiri nikimweleza mumeo kuwa nina picha hizo ningepata hata mara tatu ya fedha yako.”
“Basi naomba unielekeze nizilete wapi hizo fedha?”
“Unazo sasa hivi?”
“Hapana nakwenda kwenye mashine ya kutolea fedha.”
“Basi ukiisha kuwa nazo nijulishe nikuelekeze.”
“Nielekeze wala haichuki hata nusu saa.”
“Nitakujulisha baada ya dakika tano.” Jamaa baada ya kukata simu alimgeukia Jimmy aliyekuwa pembeni yake.
”Sasa mkuu fedha ndiyo hiyo atuletee wapi?”
“Mwambie Sea Green view hotel.”
“Poa.”
“Yule mwanamke anaonekana ana fedha za kuchezea lazima tumtumie kutengeneza maisha.” “Hakuna noma mkuu.”
Baada ya mazungumzo alimpigia simu Kilole. “Haloo Sister tukutane Sea Green view hotel.”
“Nje au ndani?”
“Aah! Jambo hili si la kitoto tunatakiwa tukabidhiane ndani.”
“Mmh! Sawa.”
“Mbona unaguna?”
”Si unajua mimi mke wa mtu naweza kuingia kwenye matatizo nikionekana katika mazingira ya kutatanisha.”
“Kuachika na kuonekana kipi kibaya?”
”Mmh! Sina jinsi kisu kimegusa mfupa.”
“Nikupe dakika ngapi?”
“Sidhani itachukua nusu saa, naomba basi nikukute kwani nina haraka.”
“Hakuna tatizo.”
Kilole alijikuta akiingia katika matatizo ambayo hakuyategemea, moyoni aliapa kumfanyia kitu kibaya Jimmy ambacho hatakisahau maishani mwake. Baada ya kutoka kwenye mashine ya kutolea fedha, alielekea Sea Green view hotel. Alipofika nje ya hoteli alimpigia simu mwenye picha zake.
“Haloo nimeisha fika upo wapi?”
“Njoo ndani ghorofa ya pili chumba namba 112.”
“Mmh! Mbona makabidhiano ndani ya chumba cha hotel?”
“Kwa vile wewe ni mke wa mtu.”
“Mmh! Sawa nakuja.
” Haikumpa shida kuingia ndani bila kujulikana kutokana na kujitanda kanga iliyomfunika kichwa na kujiziba na miwani nyeusi. Aliingia hadi ndani ya hoteli na kwenda moja kwa moja kwenye chumba namba 112, kabla ya kuingia alipumua kidogo na kugonga mlango.
“Pita mlango upo wazi,” sauti toka ndani ilimjibu.
Alizungusha kitasa na kusukuma mlango, mlango ulifunguka na kuingia ndani. Alimkuta kijana mmoja aliyekuwa amekaa kwenye sofa akinywa maji yaliyokuwa juu ya meza ndogo.
“Karibu,” alimkaribisha huku akitabasamu.
“Asante,” Kilole alijibu huku akikaa pembeni yake akiwa hajiamini. “Karibu soda.”
”Hapana nina haraka fedha hii hapa nipe picha zangu niondoke.” “Sikiliza dada yangu kufanya mambo yako kwa pupa utajikuta kila siku unarudia makosa.”
“Nimekuelewa kaka yangu ila naomba unipe kwanza hizo picha mambo mengine tutapanga siku nyingine.”
“Basi kunywa soda kidogo.”
“Hapana kaka yangu nina haraka.”
“Ina maana mimi ni mjinga kukununulia soda?” Jamaa alionesha kukasilishwa na kauli ya Kilole. “Basi wacha ninywe kidogo,“ Kilole alisema huku akichukua chupa ya soda iliyokuwa imekwisha funguliwa kabisa.
Alikunywa kidogo bila kujua alikuwa amepangiwa mchezo mwingine katika soda, aliona kama inamchelewesha alikunywa yote ili awahi kuondoka. Lakini hakufanya lolote baada ya kupatwa na kuzunguzungu na kujilaza kwenye kochi bila kujua. Joe alimpigia simu Jimmy aliyekuwa nje ya hoteli.
Itaendelea
↧
NYUMA YA MACHOZI - 18

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Alikunywa kidogo bila kujua alikuwa amepangiwa mchezo mwingine katika soda, aliona kama inamchelewesha alikunywa yote ili awahi kuondoka. Lakini hakufanya lolote baada ya kupatwa na kuzunguzungu na kujilaza kwenye kochi bila kujua. Jamaa alimpigia simu Jimmy aliyekuwa nje ya hoteli.
SASA ENDELEA...
Jimmy aliingia ndani ya hoteli na kumkuta Kilole amejilaza kwenye kochi hakiwa hajitambui. “Ooh! Kazi nzuri sana,” alimpongeza mwenzake.
“Mmh! Nilikuwa kwenye wakati mgumu unajua kazi kama hujaifanya hata siku moja lazima utakuwa hujiamini, wasiwasi wangu anaweza kuja na polisi.”
“Aje na polisi hajitaki, vipi mzigo amekuja nao?”
“Huu hapo,” Joe alimpa bahasha lililokuwa na fedha. Kabla ya kufanya lolote walihesabu fedha na kukuta milioni tano taslimu, Jimmy alimkatia Joe milioni moja kama malipo ya kazi aliyompa.
“Mzee nafikiri zinakutosha.” “Asante mkuu, nini kinaendelea?”
“Bado sinema inaendelea, sasa hivi tutafanya naye mapenzi kwa zamu huku tukipiga picha ambazo naamini zitazidi kututengenezea fedha.”
“Hakuna tatizo.”
Walimbeba Kilole aliyekuwa hajitambui na kumlaza kitandani kisha walimvua nguo zate na kuanza kumbaka kwa zamu huku wakimpiga picha za aibu. Baada ya kumaliza zoezi la aibu waliondoka na kumwacha Kilole akiwa amelala hajitambui.
********
Majira ya mchana Teddy alimpigia simu Mr Deus kutaka kujua kama ana nafasi waonane kutokana na baadhi ya washirika wake jioni ya siku ile kuwa na safari kufuata mzigo. “Haloo brother za kazi?” “Nzuri, sijui zako.”
“Zangu ziko poa, samahani tunaweza kuonana mchana huu?”
“Hakuna tatizo.”
“Basi njoo mara moja nikukutanishe na jamaa zangu ili tuianze kazi mara moja.” “Hakuna tatizo, tutakutana wapi?”
”Njoo na gari mpaka sehemu uliyoniacha siku ile.”
“Hakuna tatizo ndani ya robo saa nitakuwa hapo.”
“Okay, baadaye.”
Deus alikata simu na kujiandaa kwenda kuonana na kundi la wauza madawa ya kulevya. Baada ya kupanga vitu katika hali nzuri alitoka na kumuaga msaidizi wake.
“Happy natoka kidogo.” “Hakuna tatizo bosi.” Mr Deus alielekea kwenye maegesho kuchukua gari lake na kuelekea kwenye wito, alipofika eneo aliloelezwa alilipaki gari pembeni ya barabara kusubiri maelekezo. Baada ya muda simu yake iliita, alipoitazama alikuta ni Teddy, alibofya cha kupokelea na kuweka sikioni.
“Haloo.” “Haloo nimekuona, teremka kwenye gari lako na kupanda kwenye gari litakalo simama mbele yako.”
“Na gari langu?” “Liache tu litakuwa katika usalama wa hali ya juu, kwa hilo usihofu.”
“Okay,” Mr Deus alikata simu na kuteremkana kulifunga gari lake na kufuata maelekezo. Kabla hajapiga hatua Range Rover Vogue nyeusi yenye vioo visivyoonesha ndani ilisimama mbele yake na kufunguliwa mlango.
Hakupoteza muda aliingia ndani ya gari na kufunga mlango na gari liliondoka. Ndani ya gari kulikuwa na watu watatu Teddy aliyekuwa akiendesha gari na wanaume wawili waliokuwa wamekaa siti za nyuma.
“Habari zenu?”
“Nzuri,” Walijibu kwa mkato.
“Samahani brother,” Teddy alisema huku akipaki gari pembeni. “Bila samahani.”
“Naomba ufuate utaratibu wetu kabla ya kufika kwetu.”
“Hakuna tatizo.” “Utafungwa kitambaa usoni mpaka tutakapofika.”
“Hakuna tatizo mnaweza kufanya.”
Baada ya kukubali alifungwa kitambaa cheusi usoni na safari iliendelea bila kujua anapelekwa wapi. Baada ya dakika tano gari lilisimama na kuombwa
Mr Deus aliteremke, alitii amri na kuteremka kisha alishikwa mkono na kuongozwa hadi sehemu na kufunguliwa kitambaa usoni.
Baada ya kufunguliwa alijikuta yupo mbele ya sebule lililokuwa na kila kitu cha thamani. Ndani ya sebule ile kulikuwa na watu zaidi ya nane ukijumlisha watatu aliokuja nao wakawa jumla watu kumi na mbili pamoja na yeye mwenyewe.
“Karibu Mr Deus jisikie huru, ila samahani kukuleta kama mateka.”
“Kawaida tu wala hakuna baya.”
“Karibu kwenye kochi.”
“Asante,” alijibu huku akikaa kwenye kochi, baada ya kuketi aliwasalimia aliowakuta.
“Habari zenu.”
“Nzuri,” Waliitikia kwa pamoja.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu, huyo hapo ni Mateez anayefuata Sopas, Natalie, Suzy, Moops, Sweet, Pako, Flog, JMS na Poona, nina imani mimi unanifahamu?”
Mr Deus alikubali kwa kutikisa kichwa. “Waungwana huyu ndiye mtu niliyewaeleza ana umuhimu mkubwa kwetu, nimeweza kumwelewesha na kanielewa. Kwa vile kazi hii haihitaji kupoteza muda nina imani kuanzia muda wowote biashara ifanyike.
“Mr Deus hawa ndiyo washirika wangu niliokueleza kwa bahati nzuri tumekutana sehemu kubwa ya kundi letu. Wengine watatu utawajua kwa vile wiki ijayo wanaingia nimezungumza nao ili wapitie katika mikono yako salama japo wawili wamesema wataanza baada ya sisi ila mmoja atakuja na mzigo ndogo kujaribu.”
“Hakuna tatizo kazi itafanyika vizuri kila mmoja ataifurahia,” alisema Mr Deus baada ya kumsikiliza Teddy.
“Kwa hiyo kazi rasmi inaanza mwezi ujao kwa mwezi una uhakika wa kutengeneza zaidi ya bilioni mbili.”
“Hakuna tatizo nina imani mtafurahia kufanya kazi pamoja japo ni ya hatari.”
“Baada ya makubaliano hayo, tunakuonya tena kosa lolote la kizembe litagharimu uhai wako,” Teddy alitoa onyo lingine.
“Najiamini kuliko mnavyonidhania,” Mr Deus aliwatoa wasi.
“Kumbuka nilikukataza usimwambie siri hii hata mkeo.”
“Siwezi kumwambia mtu.”
Baada ya mazungumzo Mr Deus aliagwa na kupewa asante wa kukubali kufanya kazi na kundi lile ya milioni 55 kwa kila mmoja kutoa milioni tano. Baada ya mazungumzo yale alifungwa tena kitambaa na kurudisha hadi kwenye gari lake na kumkabidhi huku wakimuacha Mr Deus akiwa hajui alikuwa wapi.
******
Kilole alishtuka na kujishangaa yupo wapi baada ya kushtushwa na mazingira aliyoyaona mbele yake. Alijiuliza pale amefikaje na anafanya nini, kingine kilichomshtua ni kujikuta kitandani akiwa mtupu na pembeni yake kulikuwa na kondomu zaidi ya nne zilizotumika.
Alishtuka na kujishika sehemu za siri na kukuta kweli amebakwa, pembeni yake kulikuwa na bahasha mbili zilizokuwa imeandikwa jina lake. Kabla ya kuichukua ile bahasha alitulia na kuvuta kumbukumbu ya kufika pale. Alikumbuka alipeleka milioni tano ili apewe picha alizipiga akifanya mapenzi na Kinape. Aliendelea kuvuta kumbukumbu na kukumbuka baada ya kuonana na yule kijana alikaribishwa soda lakini kilichoendelea hakujua mpaka aliposhtuka na kujikuta akiwa mtupu kitandani huku ikionesha amebakwa zaidi ya mara nne kutokana na mipira minne ya kiume iliyotumika.
Alijipa ujasiri na kunyanyuka hadi bafuni na kuoga kisha alirudi chumbani na kuvaa nguo zake kisha alichukua bahasha mbili zilizokuwa na jina lake na kuziweka katika mkoba wake na kutoka nje ya hoteli kurudi nyumbani kwake.
Alipofika nje ilionesha kiza kilikuwa kimeingia, alitoa simu yake kwenye mkoba na kuangalia saa ilimuonesha ni saa mbili usiku. Alijikuta akishtuka na kujiuliza utamueleza nini mume wake, katika simu yake kulionesha kuna simu zilizopigwa zaidi ya mara kumi za mume wake pamoja na Kinape.
Japo roho ilimuuma kwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa na kuapa kulipa kisasi, lakini aliweka pembeni maumivu yale na kutafuta njia ya kukabiliana na mumewe nyumbani atakayetaka kujua alikuwa wapi. Lakini ilikuwa tofauti na alivyofikiria, alipofika nyumbani alishangaa kukuta mumewe hajarudi. Mfanyakazi wa ndani alipomuuliza alisema hajarudi, ile ilimpa nguvu na kumpigia simu mumewe. “Haloo sweet.”
“Ooh! Honey vipi mbona napiga simu hupokei mpenzi, kuna nini?”
“Nilikuwa nimelala kichwa kimeniuma ghafla.”
“Nilitaka kukujulisha kuwa nitachewa tuna kazi moja nzito.”
“Mmh! Mume wangu, siyo unanila kisogo,” Kilole alijifanya kulalamika.
“Mke wangu siwezi kutoka nje ya ndoa yangu nakupenda sana, hasa mwenetu ambaye ndiye mrithi wetu na yote nayafanya kwa ajili yenu.”
“Asante mume wangu, nashukuru kusikia hivyo.” “Nikimaliza tu narudi nyumbani.”
“Nakutakia kazi njema, nakusubiri kwa hamu,” Kilole alizidi kumtia ujinga mumewe. Baada ya kukata simu aliingia chumbani mwake na kuziangalia zile bahasha, bahasha ya kwanza ilikuwa na picha alizopiga akifanya mapenzi na Kinape. Bahasha ya pili kulikuwa na picha ambazo zilimmaliza nguvu lakini akijikaza na kuendelea kuzitazama.
Alijiona akibakwa na wanaume wawili, alishtuka na kukumbuka soda aliyokunywa ndiyo ilimfanya apoteze fahamu na kumfanya yule mwanaume na mwenzake wambake.
Roho ilimuuma kutoa milioni tano bado wamembaka na kumpiga picha chafu. Ndani ya bahasha kulikuwa na karatasi iliyokuwa na ujumbe usemao;
Kwa vile unapenda mchezo huo, baada ya kukupa picha zako na kutupa milioni tano, picha hizo zingine zinataka milioni kumi, la sivyo siri ilimfikia mumeo. Tutakupigia simu kujua utatupa lini na wapi?
Kilole jasho lilimtoka na kuona kama laana ya matendo yake ndiyo inayomtafuna, alijiuliza milioni kumi akiwapa lazima watatengeneza mpango mwingine. Wasiwasi wake huenda mpango ule Jimmy anaujua, lakini hakutaka kutumia pupa zaidi ya kutumia hata kishawishi cha fedha ili Jimmy amsaidie. Wazo lingine lilikuwa kumuwahi Deus kabla hajajua lolote kwa kumuua ili kuepusha aibu, lakini wazo la kuua bado hakulipa nafasi kutokana na Kinape kuweka pingamizi. Akiwa amechanganyikiwa simu yale iliita, aliipokea na kusema:
“Haloo.”
“Haloo, bahasha umeiona?”
”Wewe nani?” “Mdau wako, nina imani ujumbe umeuona nieleze hizo fedha nitapata lini?”
”Lakini kaka yangu nimekukosea nini mpaka kunifanyia unyama kama huo?” Kilole alilalamika huku akimwaga chozi. “Hujadhalilishwa na mtu, biashara umeianza wewe, sisi tunaiendeleza.”
“Kaka yangu milioni tano nimekupa leo, hizo kumi nitazipata vipi?”
“Kama huna pa kuzipata basi salamu utazikuta kwa mumeo,” sauti ya upande wa pili ilimtisha.
“Msifanye hivyo, nioneeni huruma.”
“Hukujionea huruma sisi tutakuonea vipi?”
“Basi nipunguzieni.”
“Tulikuwa tunataka milioni hamsini, lakini nimepunguza mpaka kumi bado huoni huruma yangu.”
“Basi nipeni muda wa muda ili nizikusanye.”
“Tutakupa siku mbili.”
“Mbona ndogo?”
“Kama ndogo utajuana na mumeo tena tuinampa na za mwanzo ulizopiga na shemeji yako.”
“Basi nitawapeni, nakuombeni msimpe mtu.”
“Hakuna tatizo timiza haja zetu.”
“Hakuna tatizo.”
“Kwa heri, usiku mwema.”
Baada ya kukata simu alijikuta akirudiwa na maneno ya mtu aliyetaka fedha kwa kusema alifanya mapenzi na shemeji yake ile ilionesha kabisa Jimmy huenda mpango mzima anaujua. Kilole pamoja na kutokewa na tukio zito la kumdhalilisha huku likizidi kumuingiza kwenye mazingira magumu. Lakini hakutaka kuyumba kwani aliamini vita ile ni yake na yeye ndiye anayetakiwa kupambana mpaka tone la mwisho.
Alizirudia zile picha na kuuona unyama aliofanyiwa ikiwa pamoja na kuingiliwa kinyume na maumbile. Moyo ulimuuma sana na kujikuta akidondokwa na machozi kutokana na udhalilishwaji kama ule. Aliapa kupigana nayo mpaka hatua ya mwisho hata kwa mtutu kwani alikuwa anajua kutumia vizuri chombo cha moto baada ya kufundishwa na mumewe na kujua kuitumia vizuri.
Alikumbuka visasi vingi ambavyo ameviona kwenye sinema hutendeka usiku kwa mtu kuingia sehemu na kufanya mauaji kisha kutokomea bila mtu kujua.
Wazo lake lilikuwa kwenda kumbana Jimmy ili amtaje mtu mwenye picha zake na alipanga kuhakikisha anamuua Jimmy na kijana anayemtumia kama mtaji. Wakati akiwaza vile alishtuka kusikia mlango ukigongwa, alificha picha kwenye kabati na kwenda kufungua mlango.
Alifuta machozi na kujirudisha katika hali ya kawaida kisha alipofungua akijua mumewe karudi, lakini kumbe alikuwa Kinape ambaye alionekana mwenye jambo zito kichwani mwake kutokana na mwonekano wake. Kilole alizidi kuchanganyikiwa na hali ile ambayo aliona huenda inafanana na yake.
“Kilole mbona hivyo?” alimuuliza kwa mshangao. “Kilole umeniweka katika wakati mgumu sana,” Kinape alisema huku akikuna kichwa.
“Mungu wangu! Amejua? Kwa nini tusimmalizie mbali?”
“Tummalizie mbali nani?”
“Si Deus.”
“Kwa kosa gani?”
“Si amejua.”
“Wala si hilo.”
“Picha ameziona?”
“Kilole hebu acha papala, yote unayouliza siyo.”
“Sasa nimekuweka kwenye wakati mgumu kivipi?”
Tukutane Jumatatu
↧
NYUMA YA MACHOZI -19

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
“Mungu wangu! Amejua? Kwa nini tusimmalizie mbali?” “Tummalizie mbali nani?”
“Si Deus.”
“Kwa kosa gani?” “Si amejua.”
“Wala si hilo.”
“Picha ameziona?”
“Kilole hebu acha papala, yote unayouliza siyo.”
“Sasa nimekuweka kwenye wakati mgumu kivipi?”
SASA ENDELEA...
”Happy hanielewi kabisa, kila kukicha naitwa na familia yake naichenga, nikienda nitawaelezea nini wanielewe.”
“Kinape unakuwa kama siyo mwanaume, mwambie kuwa humtaki kwani mapenzi ni lazima.”
“Si rahisi kiasi hicho, kuvunjika kwa penzi kuna sababu huwezi kuzima chuma cha moto na maji baridi lazima kitapinda na Deus nitamwambia nini mtu niliyempeleka kwa wazazi wa Happy kumtambulisha kama kaka yangu?”
“Yote uliyataka wewe, kwa nini hukuniuliza kabla ya kwenda huko?”
”Kilole, wewe ni mke wa mtu na Happy ni mchumba wangu hivyo nilikuwa na haki ya kufanya vile.”
“Sasa Deus atakulazimishaje umpende Happy wakati humtaki?”
“Nitaanzia wapi ikiwa nilimweleza mengi juu ya mapenzi yangu ya dhati kwa Happy huku akiniahidi kusimamia harusi yangu. Kibaya zaidi Happy na wazazi wake watakuja hapa jioni ya leo ili kujua hatima ya ndoa.”
“Kwani wewe ulimjibu nini Happy?”
“Nilimueleza asubiri kidogo mzazi wangu mmoja alikuwa na matatizo.”
“Sasa yeye anataka nini na ulikwisha mweleza ukweli?”
“Anataka kwenda kumuona kwa vile anajua na yeye ni mzazi wake, pia muda wa kuwa naye umepungua si kama zamani. Kingine majibu yako ya mkato yamemshtua kitu ambacho kimemetia wasiwasi huenda tuna uhusiano wa kimapenzi.”
“Sasa akijua atafanya nini? Tena mweke wazi ili ajue hana chake.”
“Kilole acha kujisahau wewe ni mke wa mtu, kibaya kosa tunalifanya ndani ya kinywa cha simba. Hivi wakija hapa nitamwambia nini Deus na kwa vile huu ni mwisho wa wiki huenda akasema kesho tunakwenda kijijini. Siyo siri tabia ya Happy ilimvutia sana Deus na kusema atanipigania hata kwa fedha kuhakikisha namuoa, hivi niseme simtaki Happy nitaanzia wapi?”
“Kinape, Deus hawezi kukulazimisha kuoa mwanamke usiyempenda.”
“Unasema tu lakini kauli hiyo kwa mtu mwenye akili timamu hawezi kuitamka.”
“Kwa hiyo unamuogopa Deus?” “Ndiyo.”
“Kwa nini tusimpoteze?”
“Kilole acha papara nimekueleza tutajipanga.” “Nataka kukueleza kitu kimoja Deus ni kikwazo kwa nini mnamlea?”
“Tukifanya kwa pupa tutakosa mwana na maji ya moto.”
“Sasa tutafanyaje?”
“Nimekueleza niache niangalie tufanye nini?”
“Na kuhusu Happy najua ndiye anayeweza kuharibu kila kitu kama ataonekana kijijini?”
“Kwa kweli la Happy ndilo linalonichanganya nashindwa nifanye nini, nilipokutana naye leo nimechanganyikiwa jinsi alivyokonda kwa muda mfupi niliokuwa karibu yako na amenitishia nikimuacha lazima atajiua.” “Sasa akijiua wewe utapungukiwa nini, kwanza ndiyo itakuwa safi tunakuwa na nafasi ya kuishi wawili baada ya kumpoteza na Deus.”
“Siwezi kufanya hivyo, kama Happy atafariki basi nitakuwa na dhambi kubwa sana ambayo itakuwa kama tone la rangi nyekundu kwenye nguo nyeupe haitanitoka mpaka nitakapo ingia chini ya udongo.”
“Mmh! Sasa tutafanya nini?”
“Ndiyo maana nikasema umenipa mtihani mzito ambao sikuwahi kuusoma hata siku moja kwangu naona kiza. Kwa nini tusiachane na wazo kama hili?” ”Wazo gani?”
“Ukaniachana nioane na Happy na wewe unakie na Deus?”
“Kinape huwezi kunivisha kitanzi kisha uniweke juu ya donge la barafu likiyenyuka lazima nitakufa. Heri nife mimi kuliko kuendelea kuishi kwani naamini maisha yangu baada ya zile picha hayana thamani.
Kwa hiyo ulitaka kunidhalilisha ili ufurahi kwa vile nimeolewa na Deus kama kweli ulitaka niishi na Deus kwa nini ulinitendea unyama kama ule?”
“Happy..Ooh! Sorry Kilole mbona umekosa subira.”
“Nimekuelewa Kinape, tutazungumza kesho.”
Waliachana na Kilole alirudi chumbani akiwa amechanganyikiwa na kushindwa afanye nini juu ya picha mpya na habari za Happy.
Kilole baada ya kuachana na Kinape alirudi chumbani kwake na kujifungia kwa ndani, kila dakika iliyokuja mbele yake ilikuwa na maumivu makali yaliyomfanya akose jibu la haraka afanye nini. Kubakwa hakuona tatizo zaidi ya kusikia habari za Happy kupigania penzi lake ambalo ndilo lililomfikisha katika maumivu yale makali.
Alijiona mtu mmoja ambaye alikuwa akipigana na watu wengi bila msaada wa mtu mwingine, alijiuliza atawezaje kumdhibiti Happy kuhakikisha anampata Kinape mwanaume ambaye aliamini ndiye wa maisha yake.
Alichukua bahasha na kurudia kuangalia picha alizopigwa akibakwa na wanaume wawili kwa mpigo ambao hawakuonesha sura zao zaidi ya yeye peke yake.
Picha zile zilimchanganya sana na kuamini kama zitamfikia Kinape zitamweka katika mazingira magumu ambao utakuwa kama fimbo ya kumpigia ili kumuoa Happy.
Alipiga ngumi kwenye godoro kwa hasira baada ya kujiona yupo njia panda asijue aanze na kitu gani ili aweze kuyazima yote na mwisho wa siku awe na Kinape.
Akiwa katikati ya mawazo mlango uligongwa, alijua ni Kinape amekuja na wazo jipya, alikwenda hadi mlangoni na kufungua lakini alikuta ni mumewe ambaye alimchanulia tabasamu pana.
Kwa mshtuko aliufunga mlango haraka na kufunga na komeo, kwa haraka alichukua picha zake na kuzificha kisha alitoka hadi mlango ambako mumewe alikuwa bado amepigwa na butwaa.
“Ha! Kumbe ni mume wangu?” Alijifanya kushtuka.
“Unaniona sasa mwanzo ulifikiria nani?”
“Mmh! Hata sijui niseme nini, wakati unagonga mlango nilikuwa nimejinyoosha kitandani na kupitiwa na usingizi na kuota nimevamiwa na majambazi. Ulipogonga nilikuwa bado na usingizi nilipofungua na kukuona nilifikiri ni jambazi mpaka uliponiita na kuitambua sauti yako nisamehe mume wangu.”
“Kawaida, pole kwa ndoto mbaya.”
“Asante mume wangu.”
“Vipi mbona kama haupo sawa?”
“Mume wangu si nimekueleza naumwa, hata ndoto zangu zilikuwa za kutisha.” “Ooh! Pole sana.”
Kilole alijikuta akiangua kilio kilichomshtua mumewe.
“Vipi tena?” alimuuliza.
“Aah! Basi tu.”
“Basi tu nini! Au umezidiwa?”
“Walaa, hata sijiui nalia nini.”
”Niambie kama umezidiwa nikuwahishe hospitali, utalia bila kujua unalia nini?”
“Nimemeza dawa naomba kitu kimoja.”
“Kipi hicho mke wangu?”
“Uniache nipumzike nisiamshwe na mtu yeyote na mtoto alale kwa msichana wa kazi.”
“Hakuna tatizo mke wangu.” Deus hakutaka kumsumbua mkewe alifanya yote aliyoelekezwa, alitumia nafasi ile ya mkewe kutotaka usumbufu kuzungumza na rafiki yake juu ya mpango aliozungumza na Teddy na wauza unga wenzake.
Baada ya kuoga na kupata chakula cha usiku kilichopikwa na msichana wa kazi alikwenda chumba cha rafiki yake. Alimkuta amejipumzisha, alipomuona rafiki yake alimkaribisha kwa furaha.
“Ooh! Best karibu.”
“Naona umejipumzisha.” “Nifanye nini baada ya mihangaiko ya siku nzima.”
“Basi leo tulikuwa na kazi moja nzito ya kukamata gari lililokuwa na madawa kutokana na taarifa za watoa habari. Wenye gari waligoma kufungua mpaka walipokuja wakubwa zetu ambao waliliruhusu bila hata kuuliza. Lakini taarifa zilisema gari lile lina dawa za kulevya.”
“Basi hapo kuna rushwa imetembea kwa wakubwa.”
“Umeona eeh!”
“Ukweli ni huo unafikiri ndani ya gari kulikuwa na mzigo kiasi gani, ndiyo maana walikuwa wabishi kuwafungulia gari kwa vile kuna watu wanawategemea.” “Kitendo kile kimenivunja nguvu kweli, siwezi mkupote muda wangu kwa upuuzi kama ule.”
“Nawe kula sehemu yako.”
“Sasa kuna dili moja nimeingia leo si mchezo.”
“Mmh! Dili gani tena mzee?”
“Si nilikueleza yule mwanamke alisema atanikutanisha na wenzake?” “Eeh, ndiyo.”
”Basi leo mchana alinipigia simu na kunikutanisha nao.”
“Acha utani! Ehe ikawaje?”
“Tumekubaliana kuinza mwezi ujao kwa hiyo mpaka mwezi ukikatika nitakuwa nimetengeneza bilioni mbili.” “Acha utani!”
“Ukweli sasa hivi najiona nimekwisha uaga umasikini, kweli! Umefikia wapi mambo yako na Happy?”
Swali lilikuwa kama pigo zito moyoni mwa Kinape hakuwa na jibu la haraka, Deus hakujua rafiki yake anawaza nini baada ya kumuuliza na kukaa kimya. “Ni hivi nina fedha kidogo nitakupa ili kuhakikisha unakamilisha harusi yako.”
“Kiasi gani?”
“Milioni ishirini ambazo nitakupa sasa hivi ufanye maandalizi yako na shemeji, umekwisha mpeleka kwa wazazi kijijini?”
“Bado.”
“Unasubiri nini? Fanya hivi kesho kutwa hakikisha unakwenda na Happy kwa wazazi ili tupange nipango mingine. Utatumia gari langu sawa pia tafuta nyumba ya milioni hamsini ili nikununulie kwa siri ili shemeji yako asijue kitu.”
“Hakuna tatizo nimekuelewa mkuu.”
“Mbona kama upo mbali au umechoka?”
Deus alimuuliza Kinape aliyeonekana yupo mbali kimawazo. “Ni kweli leo nimefanya kazi kama mbwa, hapa nilipo natamani kulala tu si kitu kingine.”
“Basi pumzika tutaonana kesho.”
“Usiku mwema.”
“Na kwako pia.”
Deus alitoka na kwenda sebuleni kutafuta mkanda wa filamu ili kuvuta muda kabla ya kupanda kitandani huku akiwa anaisikia harufu ya utajiri. Alipiga mahesabu hata kama wataingiza mara moja kwa miezi miwili kwa mwaka aliziona bilioni kumi na mbili mbele yake.
Alijikuta akicheka peke yake huku akisema kwa sauti ya chini: “Kumbe utajiri hauna njia ndefu.”
Wakati akiwaza yale chumbani mkewe alikuwa akigaagaa kitandani kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa kutokana na kuwa na maswali yasiyo na majibu juu vitu vilivyopo mbele yake alijiuliza aanze na lipi la Jimmy au la Happy.
Alipanga usiku atoroke na kwenda kwa Jimmy kumbembeleza kwa njia yoyote ili tu amjue nani aliyemfanyia mchezo mchafu kama ule tena kujua picha za awali akifanya mapenzi na shemeji yake. Pamoja hakuwa na usingizi alitulia kitandani akisubiri mumewe akilala atumie nafasi hiyo kwenda kwa Jimmy.
Naye Kinape baada ya kutoka Deus alijikuta kwenye mtihani mzito wa kutoa uamuzi sahihi ambao hautaleta madhara kati ya Happy na Kilole. Lakini Happy kwake alikuwa muhimu kuliko Kilole ambaye tayari alikuwa mke wa mtu.
Swali ambalo kila kukicha lililokuwa likimla akili lilikuwa kuhusu picha alizopigwa akifanya mapenzi na Kilole nani aliyezipiga, alipata wazo la kumtafuta ili kupata ukweli wasiwasi wake huenda mtego ule ulipangwa na Deus.
Kingine kilichomkosesha raha kama picha zile zikivuja na kumfikia Deus angekuwa kwenye wakati gani. Wazo la kuua Deus au kumfanyia baya lolote alilipinga kwa nguvu zote japo hakuweza kumweleza ukweli Kilole. Taarifa za siku ya tatu kwenda kijijini kumtambulisha Happy zilizidi kumchanga kwa kujiuliza habari zile akimweleza Kilole atazipokea vipi.
Aliamua liwalo na lile lazima amweleze ukweli na hiyo kesho kutwa lazima ampeleke kijijini mengine yatakayotokea atakuwa tayari kukabiriana nayo. Alipuuza mkwara wa Kilole na kujilaza kuitafuta siku ya pili.
*****
Majira ya saa saba usiku baada ya kuona mumewe amelala na kukoroma, Kilole alijinyanyua kitandani na kumtazama mumewe aliyekuwa amepitiwa na usingizi hajitambui. Alinyanyuka taratibu kwa kunyata hadi pembeni ya kitanda na kuunyanyua mto aliokuwa amelalia mumewe taratibu na kutoa bastola ya mumewe.
Alikwenda hadi kwenye kabati na kuvaa kaptura na fulana, aliichomeka bastora kiunoni kisha alijifunga kanga zilizomziba mwili mzima na kutoka taratibu bila kumshtua mtu yeyote. Aliegesha mlango na kutoka kwa kunyata hadi nje ya geti na kuchepua mwendo kupitia barabara kubwa kuelekea kwa mpiga picha Jimmy ambako hapakuwa mbali sana na kwake.
Baada ya mwendo mfupi aliacha barabara ya rami na kuingia kwenye uchochoro ambao ungemfanya atokee nyuma ya nyumba anayoishi Jimmy pia ndipo palipokuwa na dirisha lake. Alishukuru Mungu muda wote hakupata kizuizi chochote alitembea kwa taadhari kubwa, shida yake kwenda kugonga dirisha la Jimmy ili azungumze naye na kutaka msaada wake. Alipokaribia alitembea kwa kunyata ili mtu wa ndani asijue nje ya nyumba kuna mtu anapita. Aliporikaribia dirisha la Jimmy alisikia sauti za watu wawili mwanaume na mwanamke.
Mwanaume alimtambua ni Jimmy lakini mwanamke hakujua ni nani, lakini alijua ni mwanamke wake japo Jimmy hakuwa ameoa. Alitulia akijifikiria amwite au afanyeje kwani wasiwasi wake huenda pakatokea tatizo kwa muda ule mwanamke wake akajua yeye ni hawala yake. Wakati akiwaza afanye nini, aliendelea kusikia mazungumzo yaliyokuwa yakizunguzwa ndani.
“Sasa mpenzi hiyo fedha utanipa lini?”
“Kuna dili moja litatiki muda si mrefu nitakupatia.”
“Kumbuka na mimi ninataka kuendesha gari.” “Nimekueleza nitakupatia hiyo fedha baada ya wiki kila kitu kitakuwa tayari.”
“Najua unanidanganya.”
“Mbona laki nane za kupangia nyumba nilikupa kisha laki nane zingine za kununulia sofa nimekupa nitashindwa vipi milioni nne?”
Kauli ile ilimshtua sana Kilole na kujiuliza Jimmy uwezo ya kutoa fedha kiasi kile ameutoa wapi, wakati maisha yake yalikuwa ya kubahatisha mpaka apige picha na muda mwingi alishinda kijiweni.
Wakati akijiuliza maswali yasiyo na majibu ndani mazungumzo yaliendelea.
“Ha..ha..lafu mpenzi siku hizi unafanya kazi gani maana fedha zimeibuka kama uyoga?”
Itaendelea
↧
↧
NYUMA YA MACHOZI - 20

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Kauli ile ilimshtua sana Kilole na kujiuliza Jimmy uwezo ya kutoa fedha kiasi kile ameutoa wapi, wakati maisha yake yalikuwa ya kubahatisha mpaka apige picha na muda mwingi alishinda kijiweni.
Wakati akijiuliza maswali yasiyo na majibu ndani mazungumzo yaliendelea.
“Ha..ha..lafu mpenzi siku hizi unafanya kazi gani maana fedha zimeibuka kama uyoga?”
SASA ENDELEA...
“Maisha kama kalata ukijua kuzichanga kila kitu kina kwenda kilivyopangwa.”
“Au unauza dawa za kulevywa?” “Kwani dia tatizo lako nini?”
“Naogopa nisije kukupoteza wakati nakuhitaji.” “Ungekuwa unanihitaji ungeridhika na nilivyokupa.”
“Sawa, hata kama unauza unga kuwa makini.”
Kilole alijikuta akijawa na maswali juu ya maneno ya Jimmy kuonesha ndani ya wiki ile atampatia yule mwanamke milioni tatu. Pia siku ile alimpa milioni moja na laki sita. Akili ya haraka aliamini fedha hizo huenda ndipo aliziombwa azitoe ili azipate picha zake.
Alikubaliana na wazo lake la awali kuwa Jimmy ndiye mhusika mkuu wa mipango yote. Wakati akiwaza vile alisikia simu ya Jimmy ikiita, alimsikia Jimmy akimwambia mwanamke wake.
“Samahani nakuja.” “Unakwenda wapi?”
“Sipendi maswali ya kijinga nimekueleza nakuja,” Jimmy alijibu kwa ukali.
“Najua na wanawake zako tu, “ alimsikia mwanamke akilia wivu.
“Wewe si unataka gari sasa kwa nini unapenda kufuatilia mambo yangu?”
“Sawa, basi nenda.”
Kilole alisikia mlango ukifunguliwa kuonesha Jimmy alikuwa akitoka nje kusikiliza simu. Kilole akiwa ametulia pembeni ya ukuta kwenye choo cha nyumba ya jirani.
Alisikia sauti za viatu zikielekea nyuma ya nyumba, kwa haraka alijificha nyuma ya choo. Jimmy bila kujua kuna mtu alisimama pembeni ya choo na kupiga simu iliyopokelewa upande wa pili.
“Sema Rich mbona usiku?”
“Aisee nina tatizo kubwa ya fedha,” kutokana na utulivu wa hali ya hewa Kilole alisikia mtu aliyekuwa akizungumza upande wa pili.
“Shida gani mzee, si leo nimekupatia mgao wa milioni?” “Ni kweli, si unajua nyumba za uswahili baada ya leo kununua sofa nimepandishiwa kodi ghafla na kutakiwa nilipe mwaka mzima na fedha yake anataka kesho. Sasa sijui utanisaidia vipi naomba basi unikope milioni ili kesho kama tukilipwa ile fedha nitakurudishia.”
“Sikiliza Rich leo nimempa shemeji yako milioni mbili kwa ajili ya sofa na kulipia nyumba, kwa sasa sina kitu ila jitahidi kumtisha yule mwanamke ili tupate hiyo fedha ikiwezekana hata kesho saa tano asubuhi.”
“Okay, nitajaribu kumsomesha.”
“Atakuelewa tu, jitahidi kesho tuzipate zote milioni kumi sawa?”
“Sawa nimekuelewa.”
“Basi usiku mwema, unajua umenitisha sana, wasiwasi wangu yule mwanamke kujua kama ni mimi ndiye namchezea mchezo huu.” “Walaa, nawe usiku mwema.”
Baada ya kukata simu Jimmy alirudi ndani na kumuacha Kilole akiwa amepata kitu ambacho mwanzo alikidhania lakini siku ile ukweli ulijulikana. Aliona hakuna haja ya kuendelea kuwa pale. Aliondoka na kurudi nyumbani huku moyo ukimuuma kwa kitendo alichotendewa na Jimmy.
Alifika kwake na kuingia ndani bila mtu yeyote kujua kama alitoka, alipanda kitandani na kujilaza. Kutokana na kutingwa na mawazo muda mwingi alifikiria jinsi ya kumuadabisha Jimmy. Moyoni aliapa kabla ya kuwapa hizo milioni kumi lazima wote wawe wamelamba udongo.
****
Teddy mwanamke hatari muuza unga baada ya kumaliza kuuza mzigo wake alimuaga Deus na kumweleza kila kitu kitakavyoendelea atamjulisha. Muda wote alikuwa na maswali juu ya mtu aliyemchoma katika kitengo cha madawa ya kilevya.
Alijiuliza nani aliyekuwa akijua kuondoka kwake zaidi ya mdogo wa marehemu mumewe ambaye alinyongwa China baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya. Tokea kifo cha mumewe mdogo wa mumewe alikuwa akimfuatilia na kumtaka kimapenzi. Lakini hakuwa tayari kutembea na familia moja kwa vile alikuwa na uamuzi wa kumchagua nani awe mpenzi wake. Muda mwingi kulikuwepo na kutoelewana kwa shemeji yake kulazimisha mapenzi na yeye kumkatalia. Mwanzoni alifanya kazi na mumewe ya uuzaji wa madawa na ndiye aliyemfundisha kuifanya kazi ile. Baada ya kifo cha mumewe alimshirikisha mdogo wa mumewe ambaye baada ya kupata fedha alianza nyodo na kuendelea kumtaka kimapenzi huku akimuahidi kumfanyia kitu kibaya kama ataendelee kumtolea nje.
Teddy bado hakutishwa na vitisho vya shemeji yake ambaye bado aliendelea kufanya naye kazi ya kusambaza dawa za kulevya kila kona ya dunia. Hata siku ya kuondoka mara ya mwisho aliyekuwa akijua safari ile ni yeye na washirika ambao wote walikula kiapo cha kuficha siri ya kazi yao na kuwa tayari kumsaidia mwenzao kwa gharama yoyote anapopatwa na tatizo. Wazo lake lilimpekeka huenda ni shemeji yake ndiye aliyefanya mchezo ule ili kumkomoa baada ya kumkataa kimapenzi.
Aliapa kumfanyia kitu kibaya kama ni yeye na adhabu yake ilikuwa ni kifo kwa vile nia yake ilikuwa ni kumpoteza. Teddy alipofika Italia alikwenda moja kwa moja kwenye nyumba aliyokuwa akiishi pamoja na shemeji yake.
Mara zote alipokuwa akisafiri na kurudi alikuwa akiwasiliana naye hata kumpokea, lakini siku ile alirudi kimya kimya. Alipofika nyumbani kwake aliingia ndani bila hodi, shemeji yake aliyekuwa na rafiki zake wakinywa na kujiachia na wanawake na muziki mkubwa alipomuona alishtuka sana.
“Ha! Teddy wewe si ulikamatwa?” “Wapi?” “Si..si.nilisikia umeshikwa Tanzania?” “Nani aliyekuambia?”
“Au alinidanganya?” “Nani mbona sikuelewi nani amekwambia mimi nimeshikwa?”
“Au umetoa rushwa?” “Ili?” Teddy alimuuliza huku akimtazama usoni kutafuta ukweli. “Tu..tu..achane na hayo, na..na mbona umekuja bila taarifa.” “Tatizo nini? kwa nini umegeuza nyumba yangu club?”
“Kwani tatizo nini?” “Mose unanitafuta huwezi kuigeuza nyumba yangu kama kilabu cha pombe ya kienyeji zinazouzwa Afrika.”
“Oya washikaji tutimke mambo yamekwisha haribika.”
“Sasa sherehe tunaihamishia wapi?” Mwanamke mmoja aliyekuwa amelewa sana na kuvaa nusu uchi aliuliza.
“Oya Rose, hii tunakwenda kuimalizia club Royal clasic.”
“Sasa kuna faida gani ya kupoteza muda, na huyu nani?” “Shemeji yangu.”
“Si ulisema umenyongwa au kafufuka?”
“Sitaki maswali hebu tuondokeni.”
Mose aliondoka na washikaji wake waliokuwa wamelewa na kwenda kumalizia starehe zao club.
Teddy alianza kufanya usafi ili kuirudisha nyumba katika hali nzuri. Macho yake yaliona simu kwenye kochi, aliacha kufanya usafi kuichukua simu ile na kuanza kuipekea kwenye sehemu ya ujumbe.
Jicho lake lilikutana na ujumbe ulioonesha shemeji yake alimtumia mtu aje kwenye sherehe ya kupotezwa kwake. Ilisomeka: yule fala nimemmaliza njoo tusherehekee njoo na demu wako. Palepale alipata picha kuwa shemeji yake ndiye aliyemtengenezea mtego ule. Aliapa kummaliza na kutoroka Italia na kwenda kuishi nchi yoyote kutokana na uwezo ya kifedha.
*****
Siku ya pili Kilole aliwahi kuamka ili aweze kuzungumza na Kinape kuwa asiondoke ili wazungumze. Kama kawaida Kinape alijichelewesha kwenda kazini. Baada ya Deus kuondoka alimfuata chumbani kwake ili apate muafaka wa jambo walilozungumza jana yake. “Mhu! Umefikia wapi?” Kilole alimuuliza Kinape.
“Kuhusu nini?” “Kuhusu huyo mwanamke wako.”
“Kwa kweli bado sijapata jibu, tena jana Deus ndio kaniachanganya zaidi.”
“Kivipi?”
“Amesema kesho niende na Happy kijijini.”
“Eti nini?” Kilole alishtuka kusikia habari zile.
“Mumeo kasema kesho niende na gari kanipa ili kuhakikisha sina cha kujitetea.”
“Wewe ulimjibu nini?”
“We unafikiri ningemjibu nini?”
“Si ungemwambia umebadili umamuzi kuwa hutamuoa tena Happy.”
“Ningeanzia wapi wakati kila siku nimekuwa nikiomba msaada wake kufanikisha ndoa yangu.” “Mmh! Kumbuka akiishafika kijijini mimi sina changu.”
“Lakini kwa nini tulazimishe mambo wakati yamekwisha onesha vikwazo?” “Kinape hunielezi lolote nikakuelewa, nimejitoa kwako sitarudi nyuma.”
“Sasa nitafanyaje maana leo jioni happy na mama yake watakuja kujua hatima ya uchumba wetu.”
“Lakini kwa nini tusimfutilie mbali Deus, huoni anatuwekea kivingu?”
“ Ni haraka sana kufanya mambo hayo, kuna kitu kimoja kizuri tukifanya haraka tutakipoteza.”
“Kitu gani?”
“Mwezi ujao kuna bilioni kama mbili hivi zinaingia kwa hiyo tukizipata tutakuwa na uwezo wa kuishi nchi yoyote tuitakayo.”
“Lakini kumbuka kila siku unaongeza siku mwisho wake picha zitamfikia na kuharibu kila kitu.” “Kilole tutakuwa wajinga kuziacha hizo bilioni mbili za bure.” “Tutazitoa wapi?”
Kinape alimueleza yote aliyoelezwa na Deus juu ya mpango wa kuhongwa na wauza dawa za kulevya. “Nimekuelewa.”
Alimkubalia ili kumaliza mazungumzo lakini moyoni alipanga wiki ile lazima afanye kitu ambacho kitakuwa simulizi midomoni mwa watu. Baada ya Kinape kuondoka kwenda kazini, Kilole alijikuta akizidi kuchanganyikiwa na kujiuliza aanze na nani kati wa watu wote watatu, mumewe, Jimmy na Happy mchumba wa Kinape.
Aliamini mtu wa kuanza naye alifaa kuwa Happy kwa kumzima usiku wa siku ile ili kuzuia safari ya kwenda kijiji, kisha Jimmy na mwisho alipanga kummaliza mumewe. Mpango ule aliufanya kwa siri ili mtu yeyote asijue kwa kuamini kama angemshirikisha Kinape angemuharibia kila kitu.
Wazo alilopata la kummaliza mumewe aliona anahitaji msaada wa mtu, na mtu wa karibu alikuwa Jimmy. Aliamini msaada wake ulikuwa muhimu lakini mwisho wa yote na yeye angemmalizia mbali. Baada ya kukubaliana na mawazo yake aliamua kumpigia simu Jimmy ili mpaka jioni mpango wake wa kummaliza mumewe ukamilike ibakie kuutekeleza. Baada ya kupiga simu ya Jimmy iliita upande wa pili na kupokelewa. “Haloo.” “Haloo Jimmy.” “Ndiyo sister.” “Samahani Jimmy nina shida na wewe.”
“Shida gani?” Sauti ya upande wa pili ilionesha kushtuka.
“Nitakueleza tukionana, sema tuonane wapi.”
“Njoo nyumbani kwangu.”
“Sawa nakuja.” “Nitakuwa nyumbani baada ya nusu saa.”
“Hakuna tatizo nitafika kwa muda huo.” Dakika tano baada ya kumaliza mazungumzo na Jimmy, simu ya Kilole iliita alipoitazama ilikuwa namba ngeni. Aliipokea. “Haloo.”
“Eeh! Umefikia wapi?”
“Kuhusu nini?” Japo sauti iliijua alijifanya kuuliza. “Hiyo milioni kumi ipo tayari?”
“Kesho itakuwa tayari.”
“Sihitaji kesho nataka leo.” “Okay, hakuna tatizo jioni ya leo nitatimiza kila kitu.”
“Na ufanye hivyo, kinyume na kauli yako kila kitu hadharani.”
“Wala usihofu, itanibidi nichukue fedha ya ujenzi wa nyumba nitazirudisha kesho.”
“Nakutakia siku njema.”
“Na wewe pia.”
Kilole baada ya kukata simu alishusha pumzi ndefu na kujikuta akili yake ikifanya kazi kama kompyuta kwa kupata jibu. Ilionesha muda alioweka Jimmy ulikuwa ni kuwasiliana na jamaa yake ili kutaka kujua fedha yao.
Alicheka kwa uchungu na kuamini siku ile mpaka inakatika itabaki kumbukumbu akilini mwake. Alikwenda kujiandaa kisha alitoka hadi kwenye mashine ya kuchukulia fedha na kuchukua milioni ishirini ambazo aliamini zingemsaidia kuifanya kazi yake vizuri.
Baada ya kuziweka vizuri fedha zake aliingia kwenye gari na kwenda moja kwa moja kwa Jimmy. Alimkuta Jimmy yupo nyumbani, kwa vile chumba alikuwa akikijua alikwenda kugonga mlango.
“Karibu,” Jimmy alitoka akiwa kifua wazi.
“Ooh! Sister karibu.”
"Asante nimekaribia,” Kilole alijibu huku akiingia ndani.
Ndani ya chumba cha Jimmy hakukuta mabadiliko makubwa zaidi ya tivii ya flati na friji ndogo. Alikaa kwenye kochi wakati huo Jimmy alikuwa akielekea chumbani kuchukua fulana. Macho ya Kilole yaliona kitu kilichomshtua, kiuoni kwa Jimmy kulikuwa na mchoro ambao ulifanana na mchoro aliouona kwenye kiuno cha mtu wa kwenye picha ya watu waliombaka.
Moja kwa moja ushahidi wake ulikamilika alijua Jimmy ni mmoja ya watu waliombaka, alijilaumu kwa kuondoka bila siraha ambayo ingemsaidia kumaliza kazi kwani ushahidi wa kutosha kuwa Jimmy ndiye mbaya wake ulikuwa umetimia. Lakini bado aliamini Jimmy alikuwa kiungo muhimu wa kufanikisha mpango wake kabambe utakaomuwezesha kutimiza lengo lake.
Itaendelea
↧
NYUMA YA MACHOZI - 21

MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
ILIPOISHIA:
Moja kwa moja ushahidi wake ulikamilika alijua Jimmy ni mmoja ya watu waliombaka, alijilaumu kwa kuondoka bila siraha ambayo ingemsaidia kumaliza kazi kwani ushahidi wa kutosha kuwa Jimmy ndiye mbaya wake ulikuwa umetimia. Lakini bado aliamini Jimmy alikuwa kiungo muhimu wa kufanikisha mpango wake kabambe utakaomuwezesha kutimiza lengo lake.
SASA ENDELEA...
Baada ya Jimmy kutoka chumbani akiwa amevaa fulana alikaa pembeni kidogo na Kilole.
“Ndiyo sister karibu sana.”
“Asante sana, mbona ndugu yangu umenitupa?” Kilole alijifanya kuchangamka japo moyoni alikuwa na hasira za kuua mtu. “Nikutupe wapi wakati kila kukicha mambo afadhari ya jana.” “Samahani sister unatumia kinywaji gani?” Jimmy aliuliza huku akinyanyuka kuelekea kwenye friji. “Walaa usisumbuke nashukuru.”
Jimmy alirudi kukaa kumsikiliza Kilole aliyeonekana na haraka.
“Sasa ni hivi nahitaji msaada wako wenye malipo mazuri sana.”
“Kazi gani tena sister?”
“Nina imani michongo ya mjini unaiju vizuri nilikuwa nahitaji unga.”
“Unga! Upi?” Jimmy alishindwa kumuelewa. “Kokeni.”
“Ha! Wa nini?” alizidi kushtuka.
“Dada yako najidunga muda mrefu lakini mtu aliyekuwa akiniletea amesafiri hivyo napata shida sana kubembea.”
“Mmh! Wa shilingi ngapi?”
“Kwa vile kuna watu wangu nao wana shida nilikuwa nahitaji wa milioni kumi.”
“Ha! Mbona mwingi?” “Tatizo mwingi au niupate, mbona kila kitu unashangaa.”
“Mmh! Ulikuwa unautaka lini?” “Leo hii na fedha ipo.”
“Na kamishina yangu kiasi gani?” “Wewe unataka shilingi ngapi?”
“Si unajua kazi za hatari hata laki mbili siyo mbaya.”
“Nitakupa milioni.”
“Ooh! Asante sana.” “Samahani Jimmy simu yako ina salio nataka nimpigie mtu wa tigo,” Kilole ambaye siku zote alijengwa uwezo wa kufanya mambo na mumewe Deus hata kumfundisha jinsi ya kutumia siraha kwa utimilifu tena kwa uhakika mkubwa.
Aliamini kupitia simu ya Jimmy ataweza kuipata namba ya mwenzake ambayo ingemsaidia kumfahamu na kuweza kumtia mikononi. Jimmy bila kujua alimpa simu yake, Kilole aliichukua na kujifanya anaingiza namba, kila alilofanya alimuangalia Jimmy ambaye hakuwa na habari naye.
Aliangalia simu iliyoingia jana yake usiku muda ambao yeye alikuwepo pale, baada ya kuiona ili kujiridhisha aliangalia iliyopigwa muda mchache baada ya Jimmy kutoka nje. Jina lilikuwa moja la Rich.
Baada ya kunukuu akilini ile namba alimrudishia simu yake, Jimmy naye bila kuhoji aliipokea simu yake. Kilole alinyanyuka kwenye kochi na kuanza kutoka nje. “Basi twende kwenye gari nikakupe hiyo fedha ili jioni nije niuchukue mzigo.”
Baada ya kusema vile Kilole alitangulia kwenye gari na kumsubiri Jimmy alipokuja alimuhesabia milioni kumi na moja kisha waliagana.
“Jimmy nakutegemea, basi usiniangushe kama zile picha ambazo ninanitia wazimu.”
“Ooh! Ina maana bado wanakusumbua?”
“Hawana lolote shida yao fedha sina jinsi nitawapa.”
“Ooh! Pole sana.”
“Ya kawaida, la muhimu nifanyie kazi yangu vizuri.”
“Hakuna tatizo sister kazi yako nitaifanya vizuri.”
Kilole baada ya kuondoka njiani aliwaza mengi huku hasira zikumpanda kichwani na kutamani kuwafanyia kitu kibaya. Lakini alikumbuka upumbavu wote anaoufanya ni kwa ajili ya kutetea penzi lake kwa Kinape. Hivyo alitakiwa kuwa makini kutekeleza mipango yake bila kumshirikisha mtu moja kwa moja hasa ya mauaji.
Kilole alirudi nyumbani kujipanga kuhakikisha kazi yake ya usiku wa siku ile anaifanya kwa umakini mkubwa japo moyo mwingine ulimshauri aachane na mpango ule wa hatari. Lakini upande wingine aliamini maji kaisha yavulia nguo lazima ayaoge na liwalo na liwe.
***
Wakati Kilole akipanga mkakati wa kummaliza Happy mchumba wa Kinape ili kuhakikisha haendi kijijini. Kinape naye alikuwa na mazungumzo na mpenzi wake sehemu tulivu waliyochagua, ambaye alikuwa akiteseka na mabadiliko ya mpenzi wake yaliyoonekana kutishia uhusiano wao.
Kinape pamoja na kujitahidi kuwa karibu na Happy lakini muda mwingi alibanwa na Kilole ambaye nia yake ilikuwa kuuvunja uhusiano ule.
“Kinape pamoja na kusema kesho unakwenda kunitambulisha kwenu bado siamini najua ni kunipoza moyo lakini hunipendi tena.”
“Happy kama kusingekuwa na umuhimu wa kwenda kukutambulisha kwetu ningekaa kimya usingejua nini kinaendelea?”
“Kinape lakini umegeuka kiasi hiki, nini nimekukosea?” Happy aliuliza kwa sauti ya kilio.
“Mambo yameingiliana tu lakini muda si mrefu kila kitu kitakuwa sawa,” Kinape alijitetea.
“Kuna kitu unanificha, Kinape una mwanamke mwingine.”
“Sina mwanamke mwingine zaidi yako.”
Kinape alijitetea japo alijua ana mtihani mzito kwa Kilole, moyoni mwake hakuwa tayari kumsaliti Deus rafiki yake kwa ajili ya mpenzi wake wa zamani.
Kilichomuumiza kichwa kilikuwa ni picha za kufanya mapenzi na Kilole ambazo kwake aliamini zilikuwa bomu ambalo kama lingepasuka kusingekuwa na usalama. Moyo alijipanga kuhakikisha anamfahamu aliyefanya mchezo ule, akiwa katikati ya mawazo Happy alimshtua.
“Ha..ha..lafu mbona simuelewi shemeji yako?”
“Umuelewi kivipi? Kinape alishtuka kidogo.
“Asingekuwa mke wa kaka yako ningesema mwanamke wako.” “Kwa nini unasema hivyo?”
“Kuna kila dalili za kuwepo siri nisiyojua kuhusu mustakabali wa penzi langu kwako. Mimi si wa kukatazwa kuingia ndani kwenu, hata kama haupo bado nina haki ya kuja kwenu.”
“Nimekuelewa lakini kila kitu kitakwenda vizuri, naomba uniamini na kesho ndiyo siku yako ya kuamini kuwa penzi letu lipo hai.”
“Mmh! Nitaamini mpaka nitakapokuwa mbele ya wazazi wako na kunitambulisha kuwa mimi ni mpenzi wako mkeo mtalajiwa.”
“Tena tumepewa lile lexus kwenda nayo kwa raha zetu.” “Usiniambie!” Happy alifurahi kwa kumkumbatia Kinape na kujisahau kama muda mfupi alikuwa akilaumu.
“Hii yote kukuonesha jinsi gani ninavyo kujali na ahadi niliyokuahidi ni ya kweli.” “Asante sana mpenzi wangu.”
“Si hilo tu, brother amenipa jana milioni 50 kwa ajili ya maandalizi ya harusi yetu.” “Jamani yaani matamani siku ifike niwe nisimame pembeni yako nikiulizwa: Happy Kinape unakubali kuolewa na Kinape kama mumeo?”
“Mmh! Utajibu nini?”
“Ndiyooooooo, tena mara mia.”
“Basi nikuache akajiandae na safari, kesho alfajiri nakupitia.”
“Sawa mpenzi wangu, katika siku ambayo nitakula chakula kiteremke sehemu zake ni leo, na siku tukifunga ndoa sijui itakuwaje bado naona ndoto ya mchana.”
“Nina imani kuanzia kesho utakula na kunywa kwa furaha baada ya kukuvisha pete ya milioni kumi.” “Haaaa!” Happy alishika mikono kifuani asiamini masikio yake.
“Nataka uamini ile ahadi niliyokuahidi inatimia.” “Kinape amini usiamini mabadiko yako kama yangeendelea kidogo nilikuwa nimewaza kufanya kitu kibaya.”
“Kipi tena mpenzi wangu?”
“Haki ya nani, leo isingepita salama nilipanga kunywa sumu nifilie mbali.”
“Aah! Happy mawazo gani tena hayo mpenzi wangu?”
“Hujui tu, nimeteseka sana, nimeumia sana, hebu nitezame mimi ndiye Happy unayemfahamu nimekuwa kama mti uliokauka.”
Happy alizungumza huku akiangua kilio ambacho kilikuwa sawa na kukamua uchungu wa moyo kutokana kuteswa na penzi la Kinape baada ya kutekwa na Kilole.
“Happy mpenzi wangu yote hayo yatakwisha hata mimi najua kosa langu lilikuwa wapi.” “Naomba usinitende nakupenda sana Kinape, sioni sisikii juu yako, bila wewe mimi sipo,” Happy aliendelea kusema huku akibubujikwa na machozi. “Basi mpenzi nimekuelewa nina imani nilikuumiza lakini nakuahidi kutuliza maumivu yako yote.”
Kinape alimpeleka Happy kwao na kuamua kwenda club ili aingie nyumbani usiku sana asionane na Kilole na alfajiri awahi kuamka na kuondoka ili kumkwepa.
****
Majira ya jioni akiwa amejipumzisha nyumbani kwake alipokea simu ikiulizia mzigo wao.
“Vipi umefikia wapi?” “Kila kitu kipo sawa ila sasa hivi nina wageni muhimu naomba univumilie kidogo.”
“Mpaka saa ngapi?”
“Sijajua ila lazima usiku huu nikupe mzigo wako wote kwa vile nimekwisha uandaa kabisa.” “Sasa tuambie saa ngapi?”
“Nimepanga baada ya mume wangu kulala nitoke mara moja, ila nilikuwa naomba uje karibu na nyumbani ili nikikukabidhi nirudi haraka kabla mume wangu hajashtuka kama nimetoka.”
“Kwa hiyo saa ngapi?” “Kuanzia saa sita usiku ila uhakika saa saba.”
“Hakikisha muda huo unatupa mzigo wetu ukifanya ujanja wowote picha zako zitasambaa kila kona ya jiji.” “Walaa usitie hofu nilichowaeleza kitakwenda kama nilivyopanga, naomba usikae mbali na simu yako ili nikikupigia utokee na kuchukua.”
“Nimekuelewa baadaye.”
Kilole baada ya kukata simu alicheka na kuuapia moyo wake usiku wa siku ile utabakia historia nzito moyoni mwake. Majira ya saa moja na nusu usiku Kilole alipigiwa simu ya Jimmy kumjulisha kupatikana kwa mzigo, walielekezana pa kuonana.
Alikwenda eneo la tukio na kupewa unga wake wa shilingi milioni moja. Baada ya kuupata aliamini kabisa utamsaidia kuifanya kazi yake kwa uhakika mkubwa. Aliagana na Jimmy na kurudi zake nyumbani na kuuficha sehemu ambayo mumewe hawezi kuiona.
Baada ya kuweka mzigo vizuri alichukua bastola ya mumewe na kuichunguza kama risasi, alikuta za kutosha aliamini zitafanya kazi yake ya usiku ule aliiweka vizuri kwa kazi ya usiku ule. Alichota unga kidogo na kuuweka kwenye chakula cha mumewe ili akila alale na yeye aweze kutoka usiku ili akafanye kazi yake nzito ambayo ilimpa mtihani mzito. Baada ya kuipanga mipango yake vizuri, alitulia kusubiri muda. Mumewe baada ya kutoka kazini alimuandalia chakula.
Baada ya kula alimuomba waende wakazungumzie chumbani. Waliingia chumbani huku Deus akikisikia kichwa kizito. Hata wakuwahi kuzungumza usingizi mzito ulimpitia. **** Ndani ya jiji Sicily nchini Italia, jiji linalosifika kwa uuzwaji wa dawa za kulevywa,Teddy bado alikuwa na hasira baada ya kugundua shemeji yake ndiye aliyemchoma kwa kitengo cha kuzuia dawa za kulevya Tanzania. Kwake alimuona ni adui mkubwa asiyefaa kuendelea kuishi.
Alipanga usiku wa siku ile amuulie mbali na yeye kutimka zake kwenda mji mwingine wa Turin kuanzisha maisha mapya kwa kuamini uwezo wa kifedha ungemwezesha kuishi sehemu yoyote duniani bila tatizo.
Baada ya kugundua kuwa shemeji yake ndiye mbaya wake hakutaka kumuonesha kukasilishwa na kitendo kile. Ili kumvuta adui yake alijifanya kubadilisha msimamo kuwa amemkubali kimapenzi. Asubuhi ya siku ile baada ya kifungua kinywa alimwita Mose na kumweleza kitu:
“Mose my sweet.”
“Teddy kauli hiyo imeanza lini?” Mose alishtuka kusikia anaitwa vile.
“Leo mpenzi, nimetafakari na kuona hakuna umuhimu wa kulikataa penzi lako kwa vile wewe ni mwanaume kama wanaume wengine pia kuwa na wewe sawa na kuwa na marehemu kaka yako.”
“Umeona eeeh,” Mose alifurahi kusikia vile bila kujua aliyekuwa anazungumza naye si Teddy aliyemzoea bali malaika wa kifo.
“Unajua Mose nimekuwa sipati jibu kila nilipojiuliza kwa nini nisikukubalie uwe mpenzi wangu, lakini ujio wa safari yangu Italy ilikuwa kuja kukueleza nimekufungulia moyo wangu kwako.”
“Ooh! Asante sana, siamini kwa kweli lazima nikueleze ukweli Teddy nimeteseka kwa muda mrefu juu yako. Nina imani sasa hivi moyo wangu utapoa.”
“Najua umeumia kwa muda mrefu, nina imani kama uliteseka juu yangu basi penzi letu litakuwa lenye upendo wa dhati. Mose mpenzi naomba usinitende.”
“Teddy amini nitakupa mapenzi zaidi ya kaka, hutajutia kunikubali kuwa mpenzi wako.”
Siku ile ilikuwa yenye furaha kwa Mose lakini moyoni kwa Teddy ilikuwa ngumu sana kwake kwa kujipanga kuhakikisha kujirahisi kule kutamlahisishia kummaliza kwa urahisi. Teddy hakuona hiyana kuutoa mwili wake kwa Mose japo alikwisha muapia labda atafanya naye mapenzi akiwa marehemu asiye na fahamu.
Siku ile alijitoa ili kumvuta karibu na kuamini kabisa anachokitafuta muda mrefu atakipata. Majira ya mchana Teddy alibuku tiketi ya ndege ya kuelekea Turin saa tatu usiku, baada ya kurudishiwa taarifa ya kupatikana kwa nafasi katika ndege ya usiku ule.
Alijipanga kuhakikisha mipango yake inakwenda kama alivyopanga na saa tatu awe kwenye kiti cha ndege akihamia jiji wa Turin kuanza maisha mapya baada ya kummalizia mbali shemeji yake Mose aliyetaka kumpoteza kwenye ramani ya dunia.
Baada ya mambo yake kwenda alivyopanga alirudi kwa Mose na kuendelea kunywa katika mahaba mazito. Mose baada ya kulewa sana Teddy alitumia nafasi ile kumpeleleza kupata ukweli. “Mose mpenzi wangu kwa nini ulinichoma?” Teddy alijifanya kulalamika katika mahaba mazito.
“Teddy ulinichanganya kimapenzi kwa kweli nilichokifanya hata sielewi nilifanya nini, nilikuwa sawa na mfa maji.”
“Lakini usirudie tena, ona sasa kama ningefungwa penzi tamu kama hili ungelipata wapi?”
“Nisamehe mpenzi wangu.”
Kauli ya Mose ilizidisha machungu moyoni kwa Teddy na kuamini wazo lake na ushahidi aliopata lilikuwa sahihi.
Alijitahidi kutengeneza tabasamu la uongo ili kuvuta muda wa kummaliza Mose. Muda wote alionesha mapenzi mazito yaliyomziba masikio asijue nini kilichokuwa kikiendelea.
Itaendelea
↧
Amazing photos of the Day
↧
Wastara kathibitisha kuolewa na Mbunge wa Zanzibar... Picha 12 zipo hapa
Wastara kafunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge Zanzibar, Sadifa Khamis Juma. ambae pia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama cha CCM (UVCCM).
PICHA ZAIDI BONYEZA
HAPA ===>bit.ly/1nbgRjn
↧
↧
Simba yatupwa nje Mapinduzi Cup, SIMBA 0, MTIBWA SUGAR 1
MPIRA UMEKWISHAAAA+5Dk 90, Banda anapiga shuti kali katikati ya mabeki wa Mtibwa, Nduda anaokoa tena
Dk 89, Nduda anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa kichwa wa Ajibu
Dk 86, Nduda anaokoa vizuri kabisa mbele ya Kiongera, analala chini ili kupoteza muda na kupunguza presha
Dk 83, Ajib anapiga mpira mzuri wa faulo lakini nduda anaokoa vizuri kabisa
SUB Dk 80, Vicent Barnabas anaingia kuchukua nafasi ya Jeba
Dk 78, Jeba anatolewa nje baada ya kuumia mwenyewe, anapatiwa matibabu
SUB Dk 76, Paul Kiongera anaingia kuchukua nafasi ya Dani Lyanga
Dk 72, Kipa Nduda anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa kichwa wa Lyanga, inakuwa kona lakini haina matunda kwa Simba.
Dk 70, Jeba anaingia vizuri lakini anapiga mpira unatoka juu ya lango
Dk 66, Tshabalala anachonga krosi safi lakini Mbonde anaruka na kuokoa
KADI Dk 64, Issa Rashid 'Baba Ubaya' analambwa kadi ya njano
Dk 60, Jabir anaingia katika nafasi nzuri lakini anashindwa kuitumia
Dk 55 hadi 59 Inaonekana mpira unachezwa katikati zaidi na Simba kila wakifika kwenye lango la Mtibwa Sugar wanaonekana hawana mipango kabisa
DK 50, Ajib anaingia vizuri kabisa, lakini anakuwa mchoyo anashindwa kutoa pasi nzuri, anapiga shuti nyanya kabisa
Dk 46, Simba inafanya mabadiliko kuwaingiza, Said Hamis Ndemla, Brian Majegwa na Ibrahim Ajib Migomba na kuwatoa Awadhi Juma, Emiry Nimubona na Mussa Hassan Mgosi
MAPUMZIKO
Gooooooooo Dk 45 Jeba anaifungia Mtibwa bao la kuongoza, ilikuwa ni baada ya shuti kali la Kichuya kutemwa na Manyika na Jeba akawahi na kumalizia.
Dk 43, Jeba anapata nafasi nyingi nzuri katika eneo la Simba, lakini anaipoteza kwa kumpasia Manyika mkononi
Dk 35, KAzimoto anawatoka mabeki wawili wa Mtibwa Sugar, lakini kipa Said Mohammed Mduda anatokea na kuudaka mpira huo vizuri kabisa
Dk 34, Mgosi anaingia eneo la hatari na kuiwahi krosi safi na Nimubona lakini kipa Saidi Mohammed anaokoa.
Dk 29, Hassan Isihaka anafanya uzembe kwa kushindwa kuuwahi mpira, hata hivyo anaugusa na kuwa kona inayochongwa na Kichuya lakini haina madhara
Dk 26, Tshabalala anachonga krosi safi lakini Mkude anashindwa kuuwahi
Dk 23, Jeba anapata nafasi nzuri kabisa katika eneo la 12 la Simba akiwa na kipa Peter Manyika wa Simba lakini anapaisha juuuu.
Dk 7 hadi 18, timu zote zinaonekana kucheza katikati ya uwanja zaidi huku kukiwa hakuna mashambulizi langoni.
Dk 6, Nimubona anaangushwa tena na Baba Ubaya, mwamuzi anamuonya
Dk 3, Simba wanaanza kurejea taratibu, Emiy Nimubonaa anaingia vizuri lakini anaangushwa. Inapigwa faulo lakini haina faida.
Dk 1, Mtibwa Sugar wanaonekana kuwa watulivu, wanaingia katika lango la Simba, lakini Peter Manyika anadaka kwa uzuri kabisa.
↧
Magazeti ya Leo Jumatu ya Januari 11, 2016
↧
Askofu Kanisa La Anglikana Atimuliwa kwa Ufisadi wa Mamilioni ya Pesa
KANISA la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Victoria Nyanza (DVN) lililopo jijini Mwanza, limemtimua rasmi Askofu kanisa hilo, Boniface Kwangu, kutokana na ubadhilifu wa zaidi ya Sh. 600 milioni.
Askofu huyo ni wa pili kutimuliwa na uongozi wa kanisa hilo baada ya mwaka 2007 aliyekuwa Askofu wa dayosisi hiyo, John Changae na yeye kufukuzwa kutokana na matumizi mabaya ya madaraka kitendo ambacho kinaonesha taswira mbaya kwenye kanisa hilo.
Pia Askofu Kwangu aliyedumu kwenye nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minane, katika uongozi wake alishawahi kutuhumiwa na waumini wake kuwa anajihusisha na dini ya Freemasons huku wengine walikuwa wakimtuhumu kwamba anatumia nguvu za giza.
Askofu Kwangu na wenzake wanne wanatuhumiwa na kanisa hilo kwa ubadhilifu wa zaidi ya Sh. 600 milioni pamoja na kuendesha kanisa hilo bila kufuata kanuni na taratibu za kanisa hilo kitendo ambacho kimesababisha kutimuliwa kwake.
Askofu Kwangu, anatuhumiwa na upotevu wa Sh. 500 milioni ya shule ya kimataifa ya Isamilo, kuuza gari la dayosisi hiyo, kufukuza wafanyakazi wa kanisa hilo na kusababisha wadaiwe Sh. 60 milioni, kujipatia kiasi cha zaidi ya Sh. 15 milioni kutoka kwa Mhasibu wa kanisa, Sam Wisa, bila kibali.
Akisoma tamko la kumfukuza kazi, Mwenyekiti wa Nyumba ya Wadumu kutoka DVN, Andrew Kashilimu, amesema askofu huyo ameisababishia hasara kanisa hilo zaidi ya Sh. 600 milioni, kutokana na kufanya kazi bila kufuata kanuni na taratibu.
Amesema kuwa askofu Kwangu amekiuka viapo vya uaskofu, katiba ya jimbo, katiba ya DVN na amekiuka maadili na kanuni, kuendekeza matabaka ndani ya wahudumu na waumini, kutoa ajira ndani ya DVN kinyume na taratibu za kanisa.
Amesema katika kikao kilichoketi Septemba 1 mwaka jana, kilithibitisha mambo hayo na kukubaliana kwamba Askofu huyo ajiuzulu kwa afya ya kanisa la Mungu lakini alikaidi maagizo hayo mpaka kutoka kwa tamko hilo.
“Askofu (Boniphace Kwangu) ametumia vibaya madaraka yake na alikuwa anatumia vibaya mali na fedha za kanisa, kwa hali hiyo tusingeweza kuwa na kiongozi wa namna hiyo,” amesema Kashilimu.
Mmoja wa waumini ambaye alikumbwa na fagio la Askofu, Kwangu, Edwar Kibiti, amesema kwamba kutimuliwa kwa kiongozi huyo wa kiroho katika kanisa hilo kutasaidia kurudisha matumaini kwa waumini walio wengi.
Kibiti ambaye pia ni Mchungaji amesema kuwa walipokuwa wakijaribu kuhoji sababu za Askofu Kwangu kuuza mali za kanisa ikiwamo gari alilochangiwa na waumini alikuwa akiwafukuza watu waliotaka kufahamu suala hilo.
“Tulipokuwa tunahoji matumizi ya mali za kanisa tulichokuwa tukiambulia ni kwenda polisi na wengine wafukuzwa, huyu (Askofu Boniphace Kwangu) alikuwa anafanya kazi kwa majungu na mpaka anaondoka alishafukuza wachungaji 19,” amesema Kibiti.
Amesema kuwa baada ya askofu huyo kuona wachungaji wazawa wanaanza kumfuatilia alianza kutafuta wachungaji wengine kutoka nchi mbalimbali hususani kutoka Rwanda, ili kuficha maovu yake anayoyafanya.
Mmoja wa Waumini, Joycelyn Juma, amesema kilichomgharimu askofu huyo ni upungufu wa mambo ya kiuongozi ambayo yamechangia kusababisha kuwepo kwa mwanya wa wizi wa mali na fedha za kanisa hilo.
“Kiufupi nimefurahi sana kwa sababu mambo ya ufisadi ama wizi wa fedha haviendani na mambo ya Mungu na nimefurahi kuona suala hili limefikia mwisho na sasa tutakuwa na amani,” amesema Juma.
Sanjali na kufukuzwa kazi ya Uaskofu DVN, pia uongozi wa kanisa hilo limemfungulia kesi Askofu Kwangu na wenzake wanne, Katibu wa Bodi, James Mtaritinya, Mhasibu wa Shule ya Isamilo, Sam Wisa, Samson Maganga na John Magawa.
Kesi iliyofunguli ni Januari 10 mwaka huu, Mw/Rb/265/2016 ambalo ni jalada la uchunguzi kwa watuhumiwa.
↧