Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

MENINAH KUMWANIKA MCHUMB’AKE

$
0
0

BAADA ya kuandamwa na skendo kuwa anatoka kimapenzi na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, mkali wa Bongo Fleva, Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’ amesema yuko mbioni kumtambulisha mchumba wake.
 
Meninah Abdulkareem ‘Meninah la Divah’.
Akipiga stori, Meninah ambaye ni zao kutoka shindano la kuibua vipaji vya kuimba, Bongo Star Search ‘BSS’ 2012 alisema;
“Nimechoshwa kila siku kusikia Diamond, sasa ni bora nimtafute mwanaume yeyote tu kisha nimtambulishe ili ijulikane siko na Diamond,” alisema Meninah ambaye yupo mbioni kuachia ngoma mpya ya Kaniganda.
Hivi karibuni kulikuwa na tetesi kuwa Meninah anatoka kimapenzi na Diamond, pia Diamond ameshafika kwao kujaribu kutoa mahari ili amuoe.
  
A JOURNALIST IS BACK (MWANDISHI AMERUDI)
#SEHEMU YA 1-13 (MWANZO MWISHO)
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
Fungua hapa ===>http://bit.ly/1o4jyTc

WOLPER AMLIPUA PEDESHEE MAARUFU! NI MSHAMBA, LIMBUKENI

$
0
0

MTOTO mzuri Bongo Movies, Jacqueline Massawe Wolper, amemtolea uvimu pedeshee maarufu, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mwami Rajabu na kumwambia aache kumfuatafuata.
 
Mtotomzuri Bongo Movies, Jacqueline Massawe Wolper.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkongo huyo ambaye anajitapa kuwa ameshatembea na baadhi ya mastaa Bongo akiwemo Wolper, alikaririwa katika gazeti hilihili akidai ametembea na Wolper kisha kumwaga na sasa anammendea mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’ kwa gharama yoyote.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Wolper alisema anamshangaa mwanaume huyo amekuwa akimfuatafuata na kumzungumzia katika vyombo vya habari wakati hana hadhi ya kuwa na mtu kama yeye.
Jacqueline Massawe Wolper.
“Kwangu mimi huyo mwanaume siyo hadhi yangu, ni mshamba, limbukeni asiyeweza kuniweka mjini…kifupi nimwambie akome kunizungumzia mimi siyo taipu yake, atafute wa saizi yake,” alisema Wolper na kuongeza:
“Nilikutana naye Nairobi aliposema ana shida ya kikazi ndiyo akaanza kuleta mambo ya kunitongoza, nilipomfuatilia nikaona si mtu mzuri, hazimo kidogo. Huwezi kuwa mwanaume ambaye unaropokaropoka hovyo, mimi nina mtu wangu namuheshimu, akome kunizungumzia.”

USIKU WA KIGODORO - 15

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com
ILIPOISHIA:“Mh! Mwenzangu, naona anakata,” alisema Lina akianza kulia.
Mara meseji ikaingia…
“Kuna nini umesahau kwangu we binti?”
Ilitoka kwa James…
SONGA NAYO…
“Mh! Hebu soma meseji hii,” Lina alisema akimpa simu Eg.
“Kuna nini umesahau kwangu we binti,” Eg aliisoma meseji hiyo kwa sauti huku akitingisha kichwa. Alipomaliza, alimwangalia Lina kisha akasema…
“Unajua kama angeandika meseji hii huku hujui shemeji Semi atasemaje hapo sawa. Lakini sasa, Semi naye kaonesha kukwazika, ndiyo nahisi pana tatizo hapo.”
“Sasa Eg hebu nishauri, nifanyaje sasa?”
“Aisee sina cha kukushauri shoga yangu. We cha kufanya ni kumwachia Mungu tu, yeye ndiye anaweza kulitatua tatizo lako lakini kwa akili zetu hakuna kitu. Unajua nini Lina?”
“Niambie…”
“Kama angetokea mmoja wao ndiye akawa amegundua kuwa upo kwenye ndoa nyingine, yaani awe Semi au James isingekuwa tatizo lakini sasa wamejua wote halafu kwa siku moja,” alisema Eg na kuzidi kumpa maumivu mwenzake.
Lina alilia sana, alifika mahali sauti ya kilio chake ilionekana kama amefiwa na mzazi wake.
“Lina shoga yangu, maisha yako hivyo, nilishakwambia mbona. Leo unalia, kesho utafurahi. Cha msingi we mwombe Mungu tu,” alisema Eg naye akisikitika. Lakini moyoni alijua alichokifanya Lina, yeye asingediriki kukifanya hata iweje!
“Unajua Eg maisha yangu yamebomoka?”
“Ni kweli Lina. Maana hali yenyewe ndiyo hivyo tena.”
“Da! Sijui nitafanya nini mimi Lina? Hivi, ni kwa nini nilikubali kuingia kwenye ujinga kama ule?”
“Ni shetani tu shoga yangu.”
***
James alikuwa ameweka laptop kwenye mapaja yake akiandika. Alionesha hana amani kivile, mfanyakazi wake mmoja wa ndani akamfuata na kusimama pembeni yake, akamuuliza…
“Bosi, shemeji vipi, jana uliondoka naye lakini hukurudi naye, kuna tatizo?”
 “Hebu waite wenzako wote niwaambie kwa pamoja,” James aliagiza.
Wafanyakazi wake wote, hadi wa getini walifika na kukaa kwa adabu…
“Jamani nataka kutoa tamko. Lina si mke wangu tena?”
“Umemfumania bosi?” waliuliza kwa pamoja.
“Hapana, ila imekuja kubainika kumbe ana mume wa ndoa kama mimi.”
“Eee?” waling’aka wote wakamtumbulia macho.
“Jana nilipoondoka naye tulikwenda kukaa Mlimani City ili tupate chakula cha pamoja, akaja bwana mmoja akasema amenifumania mimi na mkewe. Nilimwambia ni mke wangu akasema ni wake, tena wamefunga ndoa kanisani…”
“Ye Lina alisemaje?” mmoja wa wafanyakazi aliuliza.
“Hakusema kitu, alibaki analia. Kwanza alizimia, alipozinduka akaondoka mbio.”
“Aaa! Itakuwa kweli.”
“Siyo itakuwa, ni kweli. Nilikwenda hadi nyumbani kwa yule bwana, nilikuta picha yao ya harusi ukutani.”
“Mh! Hiyo kali. Sasa aliwezaje kuwa na wewe halafu ana mume nyumbani? Au waliachana?”
“Hawajaachana.
Kuna mchezo alikuwa akinifanyia Lina, anaaga anakwenda kulala hospitali kuna mgonjwa kumbe anakwenda kwa mume wake, kule nako anaongopa anakwenda kulala hospitali kumbe anakuja kwangu. Yaani sijui ni kituko gani hiki! Kuna mambo makubwa mengi tu. Alisema anasafiri kwenda kwao, hakwenda alirudi kwa mume wake…
“Sasa mbona amerudi na vitu?”
“Kanunua sokoni ili niamini ametoka safari. Nimejua kila kitu chake.”
***
Semi siku hiyo alishinda ndani tu, alikuwa akiwasiliana na ndugu zake mbalimbali na kuwapa taarifa ya alichokifanya Lina. Wengi walishtuka sana, wengine walisema hawajawahi kusikia achilia mbali kuona…
“Labda ungeniambia aliomba talaka kwako ili akaolewe na mwanaume mwingine, lakini kufunga ndoa nyingine na ya kwanza ipo na tena anaishi na wanaume wote kwa nyakati mbalimbali, sijawahi kusikia,” alisema kaka yake Semi, anaitwa Trela!
“Ndiyo hivyo kaka. Hivi hapa ninachotaka ni kufanya utaratibu wa talaka mahakamani,” alisema Semi…
“Hata mimi naunga mkono mdogo wangu. Kwani kuna kila dalili kwamba huyo mwanamke angeweza kukuua wewe ili abaki na mume mmoja.”
“Ni kweli kaka.”
***
Lina alikuwa ameduwaa, simu yake ikaita. Aliichukua haraka akiamini inaweza kuwa imetoka kwa mmoja wa waume zake. Kuangalia skrini lilijitokeza jina Boss!
“Mh! Eg bosi wangu anapiga simu.”
“Pokea.”
Lina akapokea…
“Haloo bosi…”
“Wewe uko wapi?”
“Nipo mahali bosi.”
“Upo mahali? Kivipi?”
“Bosi nina matatizo makubwa sana, siko nyumbani niko kwa rafiki yangu. Zile ndoa zote zimevunjika bosi wangu. Maisha yangu yameharibika bosi wangu, Lina si Lina tena,” alisema mrembo huyo huku akianza kulia tena.
“Ilikuwaje tena Lina?”
“Nilikuwa na James tumekaa Mlimani City tunakula, akatokea Semi…”
“Duu! Hiyo kali. Kwani hukujua kama Semi ataweza kuja?”
“Alikuwa Zanzibar kumbe akarudi bila kuniambia, ndiyo na yeye akaamua kuja Mlimani City…uuuuwi! Eeee! Najiua bosi,” alisema Lina huku akilia…
“Lina,” aliita bosi wake…
Abee bosi…”
“Kujiua si sababu wala dawa kwani wako waliokufa bila kukumbwa na mkasa kama wako. Mwombe Mungu akusaidie kwa namna yoyote ile,” alisema bosi huyo na kukata simu baada ya kubaini kwamba, Lina alikuwa akiendelea kulia.
“Mjinga sana huyu mtoto...ala! Yeye alitarajia nini sasa. Wenzake wakirubuniwa sana wanachepuka tu, sasa yeye mpaka kuamua kuolewa kabisa, hata kama ningekuwa mimi ndiyo mume wake nisingemwacha,” alisema bosi huyo huku akifikiria namna ya kumsimamisha kazi Lina.
***
Semi alikuwa safarini kwenda Korogwe, nyumbani kwa akina Lina kuweka wazi mambo ya mtoto wao. Safari yake hiyo hakumwambia Lina wala mtu mwingine yeyote yule.
Alifika saa kumi na mbili jioni na kukaribishwa kwa mshangao mkubwa maana mara zote anazoendaga, Lina huwajulisha kwanza…
“Karibu baba, za mjini? Mbona ghafla sana,” alisalimia mama Lina huku baba Lina akimwekea kiti.
Walichoona kimepungua au kuna jambo ni baada ya kumwona hajashusha zawadi yoyote kama walivyozoea kumwona akienda.
Baada ya salamu na mazungumzo mengine ya hapa na pale, Semi akaanza…
“Wazee kama mnavyojua, mshenga wangu alishafariki dunia hivyo kuna mambo yamenifanya nije mwenyewe hapa nyumbani…”
“Ndiyo ndiyo,” alisherehesha baba Lina huku mama akikaa vizuri…
“Nataka kuweka wazi kwamba Lina si mke wangu tena…”
“Eee!!” alishtuka mama mtu akamtumbulia macho Semi…
“Lina si mke wangu tena, iwe kwa talaka mahakamani au bila talaka. Nasema hivyo kwa sababu amefanya jambo moja la ajabu sana ambalo sijawahi kulisikia likifanywa sehemu nyingine hapa duniani.”
“Amefanyaje tena baba?” aliuliza baba mtu huku akianza kuhisi maisha magumu kwani msaada wa Semi kwao ni mkubwa sana tangu amemuoa binti yao…
“Lina amefunga ndoa na mwanaume mwingine, anaitwa James. Suala hilo halina ubishi kwake wala kificho, hajasingiziwa wala kuonewa…”
“Ngoja kwanza mkwe,” alidakia baba Lina…
“Eee…”
“Ina maana Lina amefunga ndoa na mwanaume mwingine wakati ndoa yake na wewe haijavunjika au imevunjika kwanza?”
“Amekwenda kanisani akiondokea kwangu, aliniambia anakwenda kwenye sherehe ya rafiki yake akaniomba alale hukohuko kumbe ndiyo wamekwenda kupumzika na huyo mumewe mwingine.”
Semi alihisi wazazi hao wa Lina hawataweza kumwelewa hivyo aliamua kuanika mkasa mzima mwanzo hadi mwisho na jinsi yeye alivyojua na alivyokaa na James na kumweleza ilivyokuwa.
Mama Lina aliangua kilio kikubwa sana kama amefiwa na huyo Lina, baba akachukua simu palepale na kumpigia Lina, ikawa hivi…
“Shikamoo baba,” Lina alisalimia baada ya kupokea simu…
“Lina,” aliita mzee huyo.
“Abe baba…”
“Una baba yako mwingine zaidi ya mimi?”
“Sina baba mwingine zaidi ya wewe baba, kuna nini?”
“Mumeo yuko hapa nyumbani. Sasa tambua mwenyewe kaleta habari gani kwetu?”
Lina alikata simu, akaizima kabisa…
“Vipi tena shoga?” Eg alimuuliza…
“Nimekwisha Eg…”
“Kivipi?”
“Semi yuko nyumbani Korogwe.”
“Mungu wangu! Kimenuka Lina, kila kitu sasa wazi hadi kwa wazazi, maskini shoga yangu wewe, utafanyaje sasa?”
“Eg mimi nakwambia sina namna, ni kujiua tu,” alisema Lina akasimama…
“Unakwenda wapi sasa Lina?”
“Nakwenda kujiua Eg, baki salama.
Niliipenda dunia na mambo yake lakini kifo nacho kimenipenda zaidi. Sina jinsi, simchukii Semi kwa kitendo chake cha kwenda kusema nyumbani wala simchukii James kwa kunitumia ile meseji bali najichukia mwenyewe kwa uamuzi wangu ulioshindwa kuangalia mbele ya safari.
“Nilidhani binadamu kuheshimika ni neema ya Mungu kumbe ni jinsi unavyoweza kutengeneza maisha  yako mwenyewe. Mimi si wa kuheshimiwa tena. Kwanza niheshimiwe kwa ajili ya kitu gani nilichokifanya. Nikifa Eg nakuagiza wewe nizikwe kokote kule na vyovyote vile.
Lakini pia kukwambia kwamba uwaambie ndugu zangu wamuombe mume wangu wa ndoa halali, Semi asimamie mazishi yangu,” Lina aliondoka kwa kasi Eg alimfuata nyuma akimzuia kuondoka.
Kwa vile Eg alikuwa ndani ya kanga moja tu, alishindwa kutoka hadi nje, akarudi kuvaa gauni na kutoka mbio lakini alikuta Lina ameshapanda Bajaj…
“Nipeleke Kijitonyama,” alisema Lina akimwambia dereva wa Bajaj.
Lina alirudi nyumbani kwake, akakuta mlango umefungwa kwa nje. Alilijua hilo baada ya kuambiwa Semi yupo kwako, Korogwe.
Alikwenda mtaa wa pili akamwita fundi na kumwomba auvunje mlango ili aingie ndani. Fundi hakuwa na maswali kwa vile anamfahamu Lina kuwa ni mke wa Semi, akauvunja, akapokea malipo yake, Lina akazama ndani.
Alichukua chupa tupu ya bia akaipasua na kusaga vipandevipande ili avinywe. Aliona ni vema akanywea maji, akafuata maji kwenye glasi.
***
Akili ilimruka Eg, kwamba Lina atakuwa ameshika uelekeo gani, akahisi nyumbani kwake, yeye akakodi bodaboda…“Please anko nikimbize Kijitonyama haraka sana,” Eg alimwambia suka.
ITAENDELEA KESHOOOOOOOOOO

JAMBAZI SUGU LILILOKUA LIKIUWA WANAWAKE ARUSHA LAUWAWA NA POLISI WANANCHI WASHANGILIA

$
0
0
Picha ya juu na chini  wananchi wa jiji la Arusha  waliojitokeza kuuangalia mwili wa  jambazi huyo atari aliowawa na polisi usiku wa kuamkia leo.
  Wananchi wakiendelea kushuhudia mwili wa jambazi hilo nje ya jengo la makao makuu ya polisi mkoani Arusha.


  Baadhi ya vitu vilivyokutwa kwa jambazi hilo zikiwemo silaha mbalimbali
  Kamanda wa polisi akionyesha moja ya kifaa cha kufanyia tageti kabla ya kupiga kijulikanacho kwa jina la Glock Fab Defence moja ambacho jambazi hilo lilikuwa likitumia.

Jambazi mmoja aliefahamika kwa jina la Ramathan Abudallah  alimaarufu kwa jina la Ramadhani Ndonga (37) mkazi wa  Moivo  ameuwawa baada ya kupigwa risasi katika majibizano na askari  wa jeshi la polisi.

Akizungumzia tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Arusha Liberatus Sabas Alisema kuwa tukio hilo limetokea October 10  mwaka huu majira ya saa nane na dakika nne usiku   katika  kijiji cha  Moivo  kilichopo ndani ya kitongoji cha  Enaboishu wilayani Arumeru.

Alisema kuwa marehemu  Ramadhan Abdallh  aliuwa anatafutwa kwa muda mrefu na jeshi la polisi kwa kuhusika na matukio mbalimbali ya uhalifu ambayo yameshawahi kutokea ndani ya  mkoa huu pamoja na katika maeneo mbalimbali ya nchi hiii.

Alibainisha  kuwa kuuwawa kwa jambazi hili kumetokana na  juhudi na kutumia mbinu za kisasa za kiyupelelezi na kufika  nyumbani kwa mtuhumiwa (marehemu) ambapo askari polisi walimwamuru  ajisalimishe lakini alikaidi amri na kuanza kuwarushia risasi hali ambayo ilisababisha askari kujibu mashambulizi na kumsababishia  umauti kumfika.

“Mara baada yakupiga jambazi huyo polisi walianza kumpekuwa  mwili wa marehemu na alipatiana akiwa ba bastola aina ya Glock 19 yenye namba RLU976 iliotengenezwa nchini Austria ikiwa na magazine yenye risasi (14) ambapo alikuwa ameishika mkononi pamoja na maganda matano yarisasi  na  mbali na hapo polisi pia  walifanya upekuzi katika chumba cha jambazi hilo na kukuta magazine ingine moja yenye risasi (15) na magazine zingine mbili zenye uwezo wa kubeba risasi thelathini kila moja ,Radio call moja  yeye nembo ya ITSS/UNICTR  pamoja na pikipiki aina ya toyo power king rangi nyekundu yenye namba za usajili T507 BSU  pamoja na kofia ngumu”alisema Sabas

Aidha alibainisha kuwa  pia katika upekuzi huo wa ndani ya nyumba ya jambazi hilo pia walifanikiwa kupata pingu moja ,plate namba ingine ya pikipiki yenye namba za usajili T 805 CVD  ambapo alibainisha kuwa jambazi hili lilikuwa likibadilisha plate namba ya pikipiki kila mara  pamoja na  chomba maalumu cha kuwekea magazine pamoja na kufanyia tageti kabla yakupiga risasi (Glock Fab Defence moja),kifaa cha kusafishia bastola pamoja na koti kubwa jeusi.

Kamanda Sabas alitaja baadhi ya matukio ambayo jambazi hili lilishayafanya  kuwa ni pamoja na tukio  lililotekea Augast 6  majira ya saa tatu na nusu usiku maeneo ya kwa iddi ambapo mtuhumiwa  akiwa na mwenzake ambaye ajakamatwa walimpiga risasi ya shingo mwanamke aliyefahamika kwa jina la Shamimu Rashid aliyekuwa mkazi wa sakina wakati akijiandaa kuingina nyumbani kwake  ,hu ku tukio lingine likiwa limetokea Augast 21 saa 19:00 maeneo yaoasiti ambapo jambazi huyo akiwa na mwenzake kwenye pikipiki walimjeruhi kwa kumpiga risasi yam domo na kutokea kichwani  mototo aitwaye Christen NIckson mwenye umri wa miaka mitatu na nusu na kisha kufanikiwa kumpora TSH 2000 na baadae majeruhi kufariki dunia akiwa anapatiwa matibabu.

Kamanda sabas alitumia nafasi hiyo kuwapongeza askari wake kwa kufanya kazi nzuri pamoja na kuwahaidi wananchi kuendelea kufanya uchunguzi na kuwabaini wahalifu wote na kuwachukulia sheria kali.

“arusha sio sehemu ya kuifadhi wahalifu ivyo tutajitaidi kwa hali na mali kuhakikisha tunawamaliza majambazi wote pamoja na wahalifu wote na napenda kuwaaambia wahalifu waache mapema maana sasa ivi tumejipanga vilivyo ,pia napenda kuchukuwa nafasi hii kuwaomba wananchi pia waendelee kuwafichua wahalifu  popote pale ili tuwaangamize kabisa”alisema Sabas

Mmoja wa wananchi ambaye alijitokeza kushuhudia maiti ya jambazi hilo Aliyejitambulisha kwa jina la Alaija Saro akiongea na libeneke blog hili alilipongeza jeshi  la polisi kwa kuweza kumuangamiza jambazi hilo kwani limekuwa likiwatia mashaka watu wengi na kuwanyima raha kwa jinsi walivyokuwa wanauwa watu.

Habari picha kwa hisani ya woindeshizza blog

YOUNG KILLER FT BANANAZORRO - UMEBADILIKA ( OFFICIAL VIDEO )

PAM DAFFA - NIMEMPATA FT. MESEN SELEKTA (OFFICIAL VIDEO)

SHINDANO LA REDDS MISS TANZANIA 2014 NDANI YA MLIMANI CITY JIJINI DAR USIKU HUU

MATUKIO YA REDDS MISS TANZANIA 2014 MLIMANI CITY DAR

$
0
0
 

Pichani ni Washiriki waliochaguliwa kuingia kwenye hatua ya tano bora katika shindano la Redds Miss Tanzania 2014 linaloendelea hivi sasa ndani ya ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar.
 

Mmoja wa Washiriki waliongia katika nafasi ya tanno bora shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakijibu maswali mbalimbali
 
Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz akitumbuiza jukwaani akiwa na Vanessa Mdee mbele ya wageni waalikwa (hawapo pichani),waliofika kushuhudia shindano hilo.
 

Msanii wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee 'V-Money' akitumbuiza kwenye shindano la kumsaka mshindi wa Redds Miss Tanzania 2014,yanayofanyika usiku huu ndani ya moja ya ukumbi wa Mlimani, jijini Dar.
 

Washiriki wa Redds Miss Tanzania 2014 wapatao 15 mara baada ya kuchujwa.
 
Baadahi ya Wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye shindano hilo la kumsaka Kinara wa Redds Miss Tanzania 2014
 

Washiriki wa Shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakicheza moja ya onesho lao la ufunguzi wa shindano hilo,ambapo mshindi atatangazwa usiku huu na kujinyakulia kiasi cha shilingi miloni 18 taslim.


SITTI MTEMVU ATWAA TAJI LA MISS TANZANIA 2014

$
0
0

Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu katika pozi na mshindi wa pili, Lillian Kamazima (kulia) pamoja na mshindi wa tatu, Jihhan Dimachk baada ya kutangazwa mshindi.
 
MREMBO Sitti Mtemvu kutoka Temeke ametwaa taji la Miss Tanzania 2014 na kujinyakulia kitita cha milioni 18 usiku huu katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Nafasi ya mshindi wa pili imekwenda kwa Lilian Kamazima ambaye amejishindia shilingi milioni 6 huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Jihan Dimachk. Dorice Mollel ameshika nafasi ya nne wakati Nasreen Abdul akichukua nafasi ya tano.
Kwa ushindi huo, Sitti atapeperusha bendera ya Tanzania katika mashindano ya Miss World 2015.

ANGALIA VIDEO YA KUMTANGAZA REDDS MISS TANZANIA 2014

USIKU WA KIGODORO - 16

$
0
0

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ILIPOISHIA: Alichukua chupa tupu ya bia akaipasua na kusaga vipandevipande ili avinywe. Aliona ni vema akanywea maji, akafuata maji kwenye glasi.
***
Akili ilimruka Eg, kwamba Lina atakuwa ameshika uelekeo gani, akahisi nyumbani kwake, yeye akakodi bodaboda…
“Please anko nikimbize Kijitonyama haraka sana,” Eg alimwambia suka.
SASA JISUKUME NAYO…
Bajaj iliendeshwa kwa mwendo wa kasi kidogo hadi Kijitonyama nje ya nyumba ya Lina, Eg akashuka bila kulipa nauli na kukimbilia ndani ili kumuwahi Lina kabla hajajimaliza kama alivyoahidi mwenyewe kwamba anakwenda kujiua.
“Lina...Lina…” aliita Eg kwa sauti ya juu akikimbilia chumbani, alisukuma mlango na kumkuta Lina anaweka vipande vya chupa kwenye kikombe ili avinywe.
“Wee…weeee, acha hivyo Lina…Lina,” Eg alimrukia Lina wakaenda wote sakafuni…
“Lina noo! Usifanye hivyo tafadhali,” alisema Eg akimpokonya glasi Lina.
Cha ajabu Lina akaanza kulia kwa sauti ya juu kama vile amesikia habari za msiba wa mama yake mzazi.
Kusikia mayowe hayo, yule dereva wa Bajaj nje akawasha Bajaj yake na kutimua mbio. Haikujulikana mara moja kisa cha kukimbia vile wakati yeye alipeleka abiria pale.
Baadhi ya majirani walifika kutaka kujua kulikoni Lina akaangua kilio vile. Wengi walijua amepatwa msiba mzito, kama si baba, mama. Lakini ndani ya moyo wake, Lina ndiyo alianza kuingiwa na hisia za kitendo alichokifanya ndiyo maana akalia sana. Alipata hisia kali na kujilaumu kwa kumfanyia mumewe, Semi kitendo kibaya kama kile.
“Hodi wenyewe,” majirani walibisha hodi.
Eg akatoka akiwa ameshika glasi iliyokuwa na vipande vya chupa ndani ambapo Lina alitaka kuvinywa…
“Karibuni.”
“Jamani mbona tunasikia kilio, vipi tena?”
“Ah! Amepata taarifa si nzuri sana.”
“Kafiwa.”
“Ndiyo.”
“Na nani?”
“Shangazi yake kijijini. Ndiye aliyemlea.”
“Oh! Mpe pole, shangazi akishakulea huyo ni mama mzazi kabisa,” alisema mama mmoja jirani. Kwa ubinadamu, majirani hao walitoa michango mbalimbali. Wengine walifungua vitenge wakatoa elfu kumi, wengine elfu ishirini. Jumla zilipatikana laki moja, Eg akasema moyoni…
“Ama kweli kufa kufaana lakini huku si kufa kufaana bali wajinga ndiyo waliwao.”
Walipoondoka, Eg alimwaga zile chupa kwenye taka, akarudisha glasi mahali pake na kurudi chumbani. Hakuwahi kuingia chumbani kwa Lina ndiyo mara ya kwanza siku hiyo.
Kwa haraka sana Eg aliamua kutumia ufahamu wake kumpigia simu Semi ambaye muda huo alikuwa gesti amejipumzisha baada ya kumalizana na wazazi wa Lina. Baba wa Lina alikuwa akimtafuta kwa simu binti yake bila mafanikio baada ya kuzima simu.
“Shem…” aliita Eg…
“Ndiyo shem, mzima?”
“Mzima wapi bwana, kuna matatizo huku!”
“Matatizo gani?” alihoji Semi bila kuonesha dalili ya mshtuko.
“Mkeo ametaka kunywa vipande vya chupa.”
“Kisa?”
“Nadhani kwa yaliyotokea shem.”
“Sasa shem akinywa yeye ndiyo nimekunywa mimi? Na nikinywa mimi ndiyo amekunywa yeye sidhani kama ni shida.”
“Ni shida! Unajua tuko ndani ya nyumba yako?”
“Ndani ya nyumba yangu, mmeingiaje?”
“Sijui, mi nimemkuta ndani akiwa ameshika glasi ina vipande vya chupa tayari kwa kuvibugia.”
Kuna sauti ilipita kwenye kichwa cha Semi ikisema…
“Umefanya mangapi katika maisha yako ambayo ni machukizo kwa Mungu mbona umesamehewa? Jaribu kusamehe na wewe. Mbona Zanzibar una mwanamke. Morogoro una mwanamke. Tanga ulikwenda ukaishi kwa mwanaume siku saba nzima tena ukiwa na huyuhuyu Lina, samehe bwana.”
“Sikia shem. We si upo hapo?”
“Ndiyo.”
“Kwanza hebu niambie ukweli, Lina alilala kwako jana?”
“Hapana, nimekuja baada ya kumkosa kwenye simu ndiyo nikajua labda anaumwa, nikaja na kumkuta na glasi…
“Nilipomuulizia akanisimulia matatizo makubwa sana…”
“Ina maana ulikuwa huyajui shem?”
“Nilikuwa siyajui hata moja, nimeshangaa sana sana, tena sana.”
Kwa mbali, Semi alianza kumwamini Eg japo awali alijua ni mulemule tu. Aliamini zaidi baada na yeye kukumbuka kwamba akiwa na wazazi wa Lina, Korogwe alikata simu akazima.
Pia alianza kuamini alipobaini kwamba Lina hakuwa  kwa Eg lakini akaingiwa na wasiwasi kwamba kama hakuwa kwa Eg alikuwa wapi!
“Sasa sikia shem?”
“Ndiyo shem…ndiyo shem…nimekuelewa shem…sawa shem….eee, sawa shem….oke shem…”
Muda wote, Lina alikuwa akisikiliza baada ya kugundua kuwa, Eg alikuwa akiongea na mumewe lakini hakujua walikuwa wakiongea nini ila kwake yeye ilikuwa ni hatua kama kweli Semi amepoteza muda wake kumsikiliza Eg ambaye ni rafiki yake kipenzi.
Eg alipomaliza kukata simu tu, Lina akamuwahi hata kabla hajapumua…
“Naamini ni Semi huyo?” aliuliza kwa haraka Lina.
“Ndiyo mwenyewe.”
“Amesemaje? Niambie tafadhali…”
“Anasema mimi nisiondoke hapa nikuangalie mpaka yeye aje kesho,” alisema Eg na kumfanya Lina kuwa na matumaini kidogo kwamba huenda msamaha ukatembea kama si kupita.
“Anaweza kunisamehe kweli kwa jinsi ulivyoongea naye?”
“Anaweza. Tena uwezekano ni mkubwa kuliko unavyofikiria.”
“Mh! Ikiwa hivyo kweli Mungu ni mwema kwangu,” alisema Lina.
“Lakini Lina,” aliita Eg…
“Niambie.”
“Mimi nina wazo…”
“Lipi hilo Eg?”
“Kwa nini tusiende kwa yule padri aliyekufungisha ndoa ukatubu yote kisha yeye akamwita Semi kumpa maelekezo ya msamaha kwako?”
Lina aliangalia juu kama anayejiuliza jambo fulani. Alionesha kukubaliana na maneno ya Eg. Alimkumbuka padri huyo ambaye siku si nyingi zilizopita alikutana naye mjini akamuuliza…
“Ndoa yako inasemaje? Bado iko imara?”
“Iko imara Faza Denis.”
“Mungu awabariki sana.”
“Amina Faza Denis.”
“Eg ni kweli Eg. Mimi pia nakubaliana na wewe,” alisema Lina baada ya kuwaza kwa muda mfupi.
***
Ilikuwa jioni ya saa kumi na moja, walikwenda kanisani kuonana na Faza Denis ambaye aliwapokea kwa mikono miwili huku akimpongeza Lina kwamba amenawiri, mumewe anamtunza vizuri.
“Enhe, Lina nikusaidieni nini? Mwenzio anataka kufunga ndoa kama wewe?” aliuliza Faza Denis…
“Hapana Faza Denis. Nina matatizo makubwa sana sana sana tena sana…”
“Ndani ya ndoa? Maana sitarajii umeniletea matatizo ya kiofisi.”
“Ndani ya ndoa Faza Denis.”
“Mumeo Semi yuko wapi?”
“Yuko ukweni kwake, Korogwe.”
“Una maanisha kwa wazazi wako?”
“Ndiyo.”
“Haya, nakusikiliza,” alisema Faza Denis huku akikaa sawasawa kwenye kiti, kiganja cha mkono wa kulia akakitumia kushikilia kidevu…
“Huyu ni rafiki yangu mkubwa, anaitwa Agnes. Mimi nimezoea kumwita Eg, wengine wanamwita hivyo. Kanisindikiza hapa…
“Faza, kuna tukio nimelifanya ndani ya ndoa limeniletea hali mbaya sana pengine hata ndoa yangu kutaka kuvunjika…”
“Ni lipi hilo Lina? Unanitisha hata mimi kiongozi wako wa kiroho.”
Lina alianza kusimuliza kisa kizima cha James kwake mpaka kufunga naye ndoa nyingine.
Wakati anasimulia, kuna muda Faza Denis alitingisha kichwa kusikitika, wakati mwingine alitumbua macho. Pia kuna wakati alitumia kiganja cha mkono wa kulia kujifuta uso kama vile alikuwa na jasho.
Ilifika mahali Faza Denis alilaza mikono yake yote kwenye meza kama aliyekuwa akitaka kumsikiliza kwa karibu Lina. Kuna kipindi Lina alisema maneno yaliyomfanya padri huyo kumwangalia Eg kama anayemuuliza ‘eti ni kweli?’ Eg naye akawa anasema ni kweli kwa kutingisha kichwa juu, chini.
“…hayo ndiyo yaliyotokea Faza  Denis mpaka leo hii. Kama si huyu Eg ningekuwa mfu saa hizi. Nakuomba sana tena sana, natubu ni kosa lakini niombee kwa Mungu anisamehe na mume wangu pia anisemehe, nimekosa mnisamehe wote,” alimaliza Lina kisha padri akahema kwa nguvu…
“Lina!” aliita Faza Denis.
“Abee faza.”
“Pole sana. Najua mapito yako yote yalikuwa yamesimamiwa na shetani. Hukuwa na uwezo wa kumshinda kwa sababu ana nguvu sana kwako.
Wewe ukilala huombi, ukiamka huombi wala kumshukuru Mungu. Mara ya mwisho kukuona kanisani siku ile ulipokuwa umemsindikiza yule binti wa mzee Mchemsho aliyetaka cheti chake cha ubatizo hapa, sijakuona tena…
“Sasa kwa sababu umetubu ina maana umelijua kosa lako na Mungu anasema siku zote kwamba, kila mwenye kuomba msamaha asamewehe hata saba mara sabini kwa saa ishirini na nne.
“Nitampigia simu Semi ili akifika tu aje kuniona tuyaongee haya mambo.
Nitamwambia ulikuja kutubu kwangu. Ila kabla hamjaondoka niwaombee kidogo,” alisema Faza Denis huku akiweka mikono sawa kwa maombi. Alimshika kichwani Lina, akamwombea kwa dakika kama tatu kisha akampa mkono wa baraka aondoke.
***
Semi alikuwa amekaa kwenye kiti jirani kabisa na Faza Denis, Lina alikuwa pembeni, Eg naye pembeni lakini jirani na Lina, James hakuachwa nyuma maana aliitwa na faza huyo japokuwa walikuwa hawajuani lakini James aliitikia wito…
“Nadhani bwana James utakuwa unajua kisa cha kukuitia?” aliuliza padri huyo.
“Sikuambiwa, ila nilipokuta haya mazingira nimejua,” alijibu James…
“Asante sana kwa uelewa. Napenda vijana wenye uelewa kama wako…Semi unajua?”
“Na mimi kama huyu bwana James…”
“Nashukuru, lakini Lina na Eg mnajua kila kitu?”
“Ee tunajua kila kitu faza,” walijibu kwa pamoja wawili hao.
“Mimi sina maneno marefu, kesi iliyopo hapa ni ya ndoa mbili. Kesi hii imeletwa na Lina mwenyewe ambaye ndiye mhusika.
“James ni kweli mnamo mwezi mmoja uliopita ulifunga ndoa na Lina?”
“Ni kweli faza, tena ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule.”
“Unaposema ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule una maana gani?”     

Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma siku ya kesho.

MISS TANZANIA 2014 MSHINDI ALIJULIKANA MAPEMA?

$
0
0

Acha kabisa! Fainali ya lile shindano kubwa la mrembo wa Miss Tanzania 2014 limechukua nafasi usiku wa kuamkia jana, Jumapili ambapo Ijumaa Wikienda lilikuwepo ndani ya eneo la tukio kukukusanyia matukio yote yaliyojiri mbele na nyuma ya pazia hivyo lina full story.
 
Warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, wakionesha shoo ya kufa mtu.
WAREMBO 30
Baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko’ kukaribisha wageni waalikwa, warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, walionesha shoo ya kufa mtu kupitia kwa msanii wa nyimbo za asili, Wanne Star.
Vanessa Mdee akifanya makamuzi jukwaani
VANESSA AFUNIKA
Kabla ya mambo mengine kuendelea, Vanessa Mdee alifunika kwa bonge la shoo alilokamua , akisindikizwa na wacheza shoo wake wawili ambao walikamua ile mbaya.

MVUTO KWENYE PICHA
Aliyeibuka kidedea kwenye kipengele hicho ni Evelyn Bassah huku Kipengele cha Top Model, mrembo Jihan Dimach akijitwalia taji.

 
Warembo walifanikiwa kuingia Top Five.
KIPAJI
Katika Kipengele cha Miss Talent (kipaji), taji lilikwenda kwa Nicole Sarakikya, Elizabeth Tarimo akaibuka kidedea kwenye Kipengele cha mwanamichezo mwanamke (Sports woman) huku Miss Personality ikitwaliwa na Salama Saleh.

KIFUTA JASHO
Baada ya kuenguliwa warembo 15, wale top 15 waliosalia walilamba Sh. laki saba kila mmoja kama kifuta jasho.

TOP 5
Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye Tano Bora ni Jihan Dimach, Siti Mtemvu, Dorice Mollel, Nasreen Abdul na Lilian Kamazima.

 
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia shoo.
WAVALISHWA KAMA NDEGE TAUSI
Bila shaka unawajua ndege tausi hasa wale wanaoonekana pale Ikulu ya Magogoni. Warembo hao walioingia Top 5 walikuwa wamevalishwa kama ndege huyo isipokuwa rangi kwa namna walivyoonekana jukwaani.

MREMBO AMWAGA KIFARANSA
Wakati wa kipindi cha maswali na majibu, mrembo Siti Mtemvu aliwaacha watu midomo wazi aliposema atajibu kwa Kiingereza lakini baada ya kumaliza kumwaga ung’eng’e, akamalizia kwa kutema Kifaransa.

 
Meza ya majaji ikijipanga kutoa uamuzi wa mwisho katika kinyang'anyiro hicho.
MWINGINE ACHEMKA
Naye mrembo mwingine, Nasreen Abdul alijikuta akichemka kujibu maswali hivyo kuzomewa hasa pale alipochanganya kati ya maneno tourism (utalii) aliloulizwa na terrorism (ugaidi).

JIHAN ALA SHANGWE
Kwenye ‘segmenti’ ya maswali na majibu, mrembo Jihan alijikuta akipokea shangwe la kufa mtu kwa kujibu vizuri kwa ung’eng’e.

 
Siti Mtemvu (Miss Tanzania 2014 ) akiwa na anyedaiwa ni baba yake, Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu.
VITUKO VYATAWALA
Vituko vilivyojiri vilikuwa vingi kwa mfano katika shoo ya msanii Vanessa Mdee aliyetumbuiza katika shindano hilo, alijikuta akiachia  ‘nido’ moja nje wakati akicheza na kuchafua hali ya utulivu, akaibua zomeazomea ya ‘weweeeee’.
nyuma ya pazia

Kituko kingine ni cha mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash kutinga ukumbini akiwa ameongozana na kale kabinti ambako katika siku za hivi karibuni, amekuwa akionekana akiwa beneti nako bila Lady Jaydee kujua.
 
Ommy Dimpoz akipiga shoo katika fainali hizo
Baada ya shoo kali ya Ommy Dimpoz, washiriki walioingia fainali, walipanda tena jukwaani ambapo Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga naye  alipanda jukwaani na kuanza kuwatangaza washindi, kuanzia namba tano mpaka namba moja.
Nasreem Abdul alishika nafasi ya tano, nafasi ya nne ikaenda kwa  Dorice Mollel.

TOP THREE
Jihan Dimach alitangazwa kuwa mshindi wa tatu (second runner up) wakati Lilian Kamazima, alishika nafasi ya pili (first runner up).
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko' (kushoto) akisimamia shoo.
Nafasi ya kwanza, ilishikwa na Siti Mtemvu, mrembo kutoka Temeke ambaye alitawazwa kuwa Miss Tanzania 2014 na kuvalishwa taji na Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanya.
Pia Siti alijishindia shilingi milioni 18 za Kitanzania kama zawadi kwa ajili ya mshindi wa kwanza huku Lilian na akiondoka na shilingi milioni 6 za Kitanzania na Jihan akiambulia milioni 4.2.
MSHINDI ALIJULIKANA MAPEMA?
Swali kubwa ambalo wadau wengi wa mashindano ya umiss Tanzania walijiuliza usiku huo ni kwamba, je, mshindi alijulikana mapema?
 
Mashabiki wakipigia debe na kutoa sapoti kwa Mrembo Siti Mtemvu katika kinyang'anyiro hicho.
Viashiria vya mapema vilionesha kwamba, Siti ambaye inadaiwa ni mtoto wa Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu angeibuka mshindi kutokana na jinsi alivyokuwa akishangiliwa kwa nguvu huku wapambe wake wakiinua vipeperushi vyenye picha ya mshiriki huyo, hali ambayo haikuwepo kwa wenzake.
Waandishi: Issa Mnally, Gabriel Ng’osha na Musa Mateja

NDOA YABUMA BAADA YA BWANA HARUSI AINGIA MITINI

$
0
0

Aiseee! Ndoa ya binti aliyetambulika kwa jina moja la  Husna (16), imebuma baada ya bwanaharusi, Rahim (30), kuingia mitini muda mfupi kabla ndoa kufungwa.
 
Binti anayetambulika kwa jina moja la  Husna (16)(mwenye shela) , aliyetaka kuolewa na bwanaharusi, Rahim (30).
Tukio hilo la aina yake lilijiri maeneo ya Kitunda-Kati jijini Dar, wiki iliyopita ambapo chanzo makini kiliwajulisha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers kwamba, kuna ndoa ya mtoto inafungwa kinyume cha sheria.
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, OFM walitinga kwenye sherehe hiyo na kuanza kuwahoji baadhi ya ndugu ambao walikiri kwamba kweli ile ilikuwa ni ndoa ya mtoto aliyeacha shule akiwa kidato cha pili.
Akizungumza na OFM, Husna alisema aliamua kuolewa kwa sababu aliacha shule kutokana na kukosa ada.

 
Husna akilia baada ya ndoa kubatilika.
Alisema kwamba, darasani alikuwa haelewi chochote alichokuwa akifundishwa hivyo hakuwa na kazi yoyote.“Baba na mama yangu wameachana siku nyingi, sasa nilikuwa nalipiwa ada na mama huku kipato chake kikiwa ni kidogo.
“Niliamua kuachana na shule maana nilikuwa sielewi chochote kwa sababu niliugua mapepo, nimeamua mwenyewe kuolewa jamani maana sina kazi ya kufanya,” alisema Husna.Baada ya baadhi ya watu kuwashtukia OFM, walimpa taarifa bwanaharusi kwa simu na hakuonekana na ndoa hiyo ikaishia hewani kwani jamaa huyo hakufika kwa kuhofia hilo.
 
Mama akimfariji Husna
Baadhi ya ndugu wa bwanaharusi walikuja juu na kutaka warudishiwe mahari yao lakini mjomba wa mtoto huyo aliwasihi kwamba watakaa kama familia na watazungumza na wako tayari kurudisha mahari.
Baada ya ndoa hiyo kubuma, mtoto Husna aliangua kilio huku akisema kwamba anampenda huyo mchumba’ke huku mama yake naye akiangua kilio akidai anaumia kwani hajui atakapozitoa hizo fedha za mahari shilingi laki nne kwani kipato chake ni kidogo.

CREDIT:GPL

MNIGERIA AOZA PENZI LA JOKATE

$
0
0

Kutoka moyoni!‘Ubuyu’ mpya mjini ni madai ya staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’ kuoza akilitamani penzi la staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
 
Staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’ kuoza akiwa na staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
MNIGERIA ABEMBELEZA
Habari kutoka kwa vyanzo makini zilidai kwamba, Mnigeria huyo amekuwa akiwasiliana na kumbembeleza Jokate usiku na mchana akiomba wawe pamoja kwa jinsi moyo unavyomtuma.
Ilidaiwa kwamba hivi karibuni, Ice Prince anayekimbiza na ngoma yake ya I Swear amekuwa akitumbukiza vipande vya video kwenye ukurasa wake wa kijamii wa Instagram akimsifia Jokate ambaye anapendelea zaidi kumwita Kidoti.
ICE PRINCE: I MISS YOU KIDOTI!
Ilisemekana kwamba katika moja ya video hizo jamaa huyo anayefanya kazi na Jokate kwenye Runinga ya Chanel O nchini Afrika Kusuni ‘Sauz’ alisikika akimwambia mwadada huyo; ‘I miss you Kidoti’.
CHANZO CHATIRIRIKA
“Jamaa amemzimika Jokate ile mbaya. Unaambia anapiga simu na kumwita Jokate Sauz kila siku.
“Jamaa kafa kaoza. Kama unasikia mahaba niue ndiyo hayo sasa. Ishu ipo kwa Jokate tu kumkubali maana Ice Prince amekuwa akimuahidi kumpa maisha ayatakayo mtoto wa kike. Kazi anayo bidada, aamue kusuka au kunyoa,” alisema mmoja wa watu wa karibu wa Jokate.
 
Staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’
JOKATE ABANWA
Baada ya kunyetishiwa ‘mchele huo ulionyooka’ Ijumaa Wikienda, gazeti namba moja la mastaa Bongo lilimsaka Jokate ambapo aliulizwa juu ya uhusiano wake na mwanamuziki Ice Prince na iwapo anajua kuwa ana mapenzi na yeye na kama akimtamkia ndoa, je, atakubali?
Huku akionekana kushtushwa na habari hiyo, Jokate alisema kwamba iwapo Ice Prince atamwambia jambo hilo, atamchunguza tabia zake na kama zitamridhisha basi hana shaka atamkubalia.
MWANAMKE SHURTI APENDWE
Jokate alisema kwamba mwanamke kupendwa ni habari nzuri, ingawa hadi sasa bado hajaona wa kumuoa.
BOFYA HAPA KUMSIKIA KIDOTI
“Sijaona bado wa kunioa lakini kama Ice Prince ana nia, nitamchunguza kama anafaa ishallah,” alisema Jokate huku akicheka.
ATAKA MTOTO
Kwa upande mwingine staa huyo wa sinema na Bongo Fleva alisema kwa sasa matamanio yake yote anahitaji mtoto kutokana na umri wake (miaka 27) kuzidi kuyoyoma.
 
Staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
BABA BORA MPO?
Jokate alisema kuwa kama kweli akijitokeza baba bora (husband material) atazaa haraka.
Mwanadashoti alisema kwamba, yeye kama msichana, anatamani siku moja aitwe mama na kila akikaa anapata mawazo ya kuzaa lakini anashindwa kwa sababu Mungu bado hajamjalia mume ambaye atazaa naye.
“Natamani mtoto kiukweli basi tu ni Mungu anapanga ndoa lakini akinijalia tu mimi nitazaa mapema, sitasubiri ndoa yangu ikae sana kama wanavyofanya wanandoa wengine,” alisema Jokate.
KUKUTANA CHANEL O
Jokate mwenye mipango lukuki na bidhaa za Kidoti na Ice Prince wanatarajia kukutana kwenye kipindi kipya cha Runinga ya Channel O kinachokwenda kwa jina la Top Ten Most na huko ndiko kitaeleweka.
KWENYE ‘PROFAILI’ YA JOKATE
Huko nyuma Jojo aliwahi kuhusishwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mbongo ambaye ni staa wa Mpira wa Kikapu (NBA) nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka. 
Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

USIKU WA KIGODORO - 17

$
0
0

ILIPOISHIA: “Ni kweli faza, tena ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule.”
“Unaposema ilikuwa ndoa halali kabisa kwa wakati ule una maana gani?”
SASA JIACHIE MWENYEWE…

Nina maana wakati nafunga naye ndoa sikujua kama ana mume mwingine kabla yangu. Ila baada ya kutokea lililotokea ndiyo nimejua kumbe nilikuwa siko sawasawa,” alisema James na kuashiria ukomavu wa busara.
“Vema sana, sasa nilichotaka ni hicho, kwamba bwana James atambue kuwa ndoa haikuwa yake, kaingilia. Lakini pia napenda nijua kwako Semi, uko tayari kumsamehe mkeo? Maana kwa upande wake ameshalijua kosa lake na ndiyo maana alikuja kutubu kwangu na nikamfanyia maombi.”
“Kusema kweli baba paroko nampenda sana mke wangu lakini alichokifanya sijakubaliana nacho, nahisi ni zaidi ya usaliti. Kwa hiyo kusema nimsamehe hapana,” alisema Semi kwa sauti ya upole kabisa.
Lina alianza kudondosha machozi huku akionekana uso umevimba. Eg yeye, moyoni alisema…
“Kama anachomoa si James ajichukulie mke tu!”
“Kwa hiyo unataka kuniambia kwamba haupo tayari kwa ndoa?” aliuliza padri.
“Ndiyo, sipo tayari,” Semi alisisitiza.
Padri, Eg, Lina na James wakaangaliana huku nyuso zao zikionesha mshangao mkubwa lakini Semi hakuonesha kushangazwa na mishangao yao.
Ukimya ulitawala kwa muda, padri ndiye akaukata kwa kuuliza…
“Kuna mwenye nyongeza?”
James alikataa kwa kutingisha kichwa, Eg akataka kusema lakini akaacha, Lina yeye ni machozi tu. Semi midomo ilimchezacheza kwa hasira.“Basi sawa, nifunge kikao. Lina, pole sana, mimi sina jinsi tena, mumeo kaamua hivyo,” alisema padri huku akisimama.
James alikuwa wa kwanza kuondoka baada ya kumpa mkono paroko huyo, Semi akasimama, naye akampa mkono paroko na kuondoka, Lina na Eg walibaki. Lina kilio kama kawa huku akisema…
“Faza, ina maana kweli sina ndoa tena?”
“Ndoa ipo, maana alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitengue, ila mumeo hataki kuishi na wewe. Mimi nilichojifunza kwake ni kwamba bado ana hasira ya tukio, ngoja atulie lakini na wewe mwombe sana Mungu,” alisema padri.
“Ni kweli kabisa Lina, shemeji bado hayuko sawa. Unajua jambo lenyewe zito,” alisema Eg huku akitangulia kuondoka mbele ya Lina ambaye bado alikuwa anamwaga machozi.
Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Risasi, Jumatano ijayo.
Mama Kisamvu, mtoto Muhogo, ni shiida!

Samahani, sijui mwenzangu unaitwa nani?”
“Juliana Anold.”
“Unaishi wapi?”
“Ilala.”
“Ilala kubwa, Ilala gani?”
“We tambua ni Ilala,” alijibu Juliana huku akimwangalia kijana aliyekuwa mbele yake kwenye foleni ya benki akimuuliza.
“Oke, mimi naitwa Bitungu, naishi Temeke, lakini Ilala huwa nafikafika sana ndiyo maana nikataka kujua wewe unaishi Ilala gani?”
“Mimi naishi Ilala tu.”
“Oke, tuyaache. Una boifrendi?”
“Ninaye ndiyo.”
“Anaishi wapi?”
“Temeke.”
“Temeke ipi?”
“Temeke tu.”
“Mh! Oke, tuyaache hayo, naweza kupata namba ya simu?”
“Ya huyo boifrendi wangu au?”
“Ya kwako, boifrendi wako mimi ya nini?”
“Nitajie zako, nitakubip,” alisema Juliana kwa sauti yenye utulivu maana ni eneo la benki.
Bitungu alimtajia Juliana namba zake za simu, baada ya hapo wakaendelea kutembea kwenye foleni.
Juliana ndiye aliyeanza kuhudumiwa, alipotoka akampa mkono wa bai kijana huyo huku akichia tabasamu la ‘nakuacha’.
***
“Juli,” mama yake alimwita siku ya pili yake tangu mrembo huyo kukutana na Bitungu…
“Natoka mara moja, lakini nitachelewa kurudi.”
“Hivi mama, kila siku unapenda kutoka muda huu, kurudi unachelewa mpaka unagombana na baba huwa unakwendaga wapi kwani?”
“Wee mtoto, acha maswali yako. Unapatia wapi ubavu wa kuniuliza maswali kama hayo mimi mama yako?”
“Nisamehe mama.”
“Tena koma kabisa, usirudie tena.”
***
“Baby, unajua nilikumisi sana? Hatujaonana tangu lini?” mama Juliana alimwambia mpenzi wake ambaye ni dogodogo.
Lina na Eg walitoka, ilibidi Lina aende nyumbani kwa Eg kuishi huko ambapo baada ya wiki mbili alipokea barua kutoka mahakamani ikimtaka afike kwa tarehe aliyopangiwa bila kukosa akiwa analalamikiwa na James.
Lina alifika tarehe hiyo akiwa na Eg, wakamkuta James amejaa tele. Malalamiko ya James kwa Lina mahakamani hapo ni kuamua kufunga ndoa batili na James huku akijua ana mume halali na hivyo kumsababishia hasara na kumchanganya akili mwanaume huyo.
Lina alikana mashitaka na kesi inaendelea huku Semi naye akimfikisha kwenye mahakama nyingine akidai talaka, nako kesi bado inaendelea. Kesi zote zimemkalia vibaya Lina, anakabiliwa kutoa talaka kwa Semi na kuamriwa kulipa gharama alizozitoa James kwa ajili ya ndoa yao.
Ama kweli, kabla ya kutenda fikiri kwanza, ikibidi hata mara saba mpaka kumi au kushirikisha watu wenye hekima zaidi yako.

MWISHO.

NORA: WEMA, LULU, WOLPER WANAWEZA, BATULLI, AUNT EZEKIEL, CHUCHU HANS HAMNA KITU!

$
0
0


Muigizaji wa filamu nchini, Nuru Nassoro maarufu kama Nora anaweza akawa ameshaongeza matatizo mengi kuyazidi 99 ya Jay Z.
Kwenye kipindi cha hivi karibuni cha Mkasi, Salama Jabir alimuuliza swali gumu kwake la kuwataja wasanii wa filamu wanaofaa na wasiofaa. Nora alikataa kutaja akijitetea kuwa hataki beef na mtu lakini watangazaji wa show hiyo walimrahisishia kazi na kuanza kuwataja ‘randomly’ waigizaji mbalimbali na kumtaka aseme tu kama wanafaa ama hawafai.
Hivyo ndivyo alivyojibu na kuwapa makavu live anaohisi wanafaa kurudi ‘kuflip burger’ na kuacha kuigiza.
Kajala – Hapana
Batulli – Hamna kitu
Steve Nyerere – Hapana
Wema Sepetu – Yeah anafaa
Rose Ndauka – Anafaa vibaya mno
Wolper – anajaribu… anafaa
Aunt Ezekiel – Hamna Kitu
JB – Anaweza
Hemed – Anaweza
Mlela – Hapana
Lulu – Ndiyo
Irene Paul – Anaweza
Chuchu Hans – Hamna Kitu
Unakubaliana na Nora?

SINTAHA AMPA MAKAVU LIVE MISS TANZANIA 2014

$
0
0

 
Miss Tanzania 2014: Decoration 100% okay
Stage Performance:20% 
Miss 2014 :Sitti Mtemvu ???? (nakuachia wewe)

Wanne Star ameboa watu, shindano la Miss Tanzania unafundisha music za ki Nigeria???

Hivi unafikiri kwanini watu wengi sana 90% hawamkubali Miss Tanzania 2014??? 

Ila Lundenga safari hii kaamua yake, yaani katukomesha kweli kweliiii tunasema havache 

je hundi imetolewa ya 10 mil na 8 jeeee?? kwakuwa hundi  si cash kwanini wasingemalizana hapo hapo mtoto wa watu akaenda ku deposit baada ya 2 days akapa chake?? kuna ulakini 

 Toa maoni yako kuhusiana na shindano hili, mshindi, na Team nzima ya Miss Tanzania

RED CARPET YA MISS TANZANIA 2014 MLIMANI CITY

STEVE RnB ALIVYOUAGA UKAPERA

$
0
0

Msanii wa Bongo Fleva, Steve RnB baada ya kufunga ndoa na Naimana Kuyangana juzi Jumamosi, Oktoba 11, mwaka huu.

Mke wa Steve, Naimana Kuyangana.
Msanii wa Bongo Fleva, Steve RnB juzi Jumamosi Oktoba 11, mwaka huu aliukacha ukapera kwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi, Naimana Kuyangana.

WAKILI DAMAS NDUMBARO ATUPWA JELA YA SOKA MIAKA SABA

$
0
0

Wakili Damas Ndumbaro.
Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la soka nchi TFF, imemfungia wakili Damas Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha pesa. Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na rais wa TFF, Ndugu, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam Tv.

Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa Shirikisho, Malinzi.

Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu. Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia, Bodi ya Ligi amekanwa ‘ hadharani’ na vilabu huku vikisema kuwa ‘ havikumtuma’ kuzungumza yale ambayo alisema mbele ya vyombo vya habari. Klabu zimesema alizungumza kwa ‘ utashi’ wake mwenyewe, na si wao walimtuma.

‘ Kilichomuhuku’ ni yeye kutaka kubadilisha maamuzi ya kamati ya utendaji ya TFF bila kuthibitishwa na wajumbe wa Bodi ya Ligi na kukubaliana. Kupingana maamuzi ya kamati ya utendaji ni kosa la kinidhamu. Ndumbaro amehukumiwa kutokana na makosa hayo na kama angezungumza kwa niaba ya klabu basi adhabu hiyo ingekwenda kwa kwao, lakini yeye alijizungumzia tu kama vile alivyotaka iwe.
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>