Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

Viongozi wa Simba Wakutana na Mohammed Dewji Usiku

$
0
0

UONGOZI wa Simba, jana ulitarajia kukutana na Mohammed Dewji maarufu kama MO, aliyeamua kujitoa katika suala la mchakato wa mabadiliko ya klabu hiyo kufuatia uongozi huo kuingia mkataba na Kampuni ya Mchezo wa Kubashiri ya SportPesa.

Hali hiyo ilionekana kumkasirisha MO kutokana na uongozi wa klabu hiyo kutomshirikisha licha ya kuwa na makubaliano naye ya kimkataba kwa baadhi ya mambo ya ndani ya klabu hiyo. Kutokana na hali hiyo, MO aliamua kujiweka pembeni na klabu hiyo lakini pia akiutaka uongozi huo umlipe gharama zake kiasi cha Sh bilioni 1.4 alizokuwa akizitoa kwa ajili ya malipo ya mishahara ya wachezaji wa timu hiyo. 


Akizungumza na Championi Jumatano mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu kabisa ya Simba ambaye aliomba kutotajwa jina lake alisema kuwa jana usiku walikuwa wakutane na MO kwa ajili ya kumaliza tofauti zao hizo ikiwa ni pamoja na kumuomba msamaha kwa yote yaliyotokea. “Tunatarajia kukutana na MO leo hii usiku (jana), kwa ajili ya kuzimaliza tofauti hizi zilizojitokeza hivi karibuni kwani kusema kweli baada ya kukaa na kutafakari tuliona hatukumtendea haki.

 “Hata hivyo nisingependa utaje jina katika habari yako hiyo kama mimi ndiye niliyekuambia kwa sababu tunataka kulifanya jambo hili kwa siri kidogo,” alisema kiongozi huyo na kuongeza kuwa. “Katika mkutano huo pia tutajadiliana na kuhusiana na mikataba ya baadhi ya wachezaji wetu akiwemo Ibrahimu Ajibu pamoja na Jonas Mkude ambao mara kwa mara wamekuwa wakihusishwa kutaka kuondoka. “Baada ya kikao hicho tutawajulisha wanachama wetu nini kilichoendelea kati yetu na MO lakini pia wachezaji hao,” alisema kiongozi huyo.

CHANZO: CHAMPIONI

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano Halotel ahukumiwa kulipa milioni 700 kwa Uhujumu Uchumi

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam imewatia hatiani, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mawasiliano Tanzania ya Viettel inayofanya biashara kama Halotel, Do Hong na wenzake wanane, kwa kosa la kuhujumu uchumi na kuwataka kulipa faini ya zaidi ya Sh. milioni 700.

Hata hivyo, Hong ameachiwa huru baada ya kulipa Sh milioni 479 ambazo kati yake, sh milioni 20 ni faini na sh milioni 459 ni fidia ya hasara anayodaiwa kuitia Serikali. 
Wenzake wamekwenda jela kwa kutolipa. Mbali ya Hong, washitakiwa wengine ni Dilshad Ahmed (36), Rohail Yaqoob (47), Khalid Mahmood (59), Ashfaq Ahmad (38), Muhamad Aneess (48), Imtiaz Ammar (33) wote raia wa Pakistan, Ramesh Kandasamy (36) raia wa Sri-Lanka na Viettel Tanzania Limited (Halotel) iliyoshitakiwa pia.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri alitoa hukumu hiyo jana baada ya washitakiwa hao kukiri makosa yao baada ya kusomewa upya mashitaka saba badala ya 10 waliyokuwa wameshitakiwa nayo kwa maelezo ya awali. 
Mashitaka waliyoshitakiwa nayo katika kesi hiyo ni kula njama kutenda kosa, kughushi na kuwasilisha nyaraka zilizoghushiwa. Hakimu Mashauri alisema katika kila kosa mshitakiwa atatakiwa kulipa Sh milioni tano na wanatakiwa kurudisha hasara yote walioisababishia serikali, ya Sh milioni 459.

“Washitakiwa hawa wamekuja kuwekeza nchini na lengo sio kuhujumu uchumi na miundombinu yetu. Ili iwe fundisho kwa wawekezaji wengine na kuonesha kwamba Tanzania ipo makini katika masuala haya, kila mshitakiwa atatakiwa kulipa Sh milioni tano na kuilipa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) fedha walizohujumu,” alisema Hakimu Mashauri katika hukumu. 
Pia Hakimu huyo aliagiza vifaa vyote walivyokutwa navyo washitakiwa wakifanyia biashara, vitaifishwe na serikali na akasema wanayo haki ya kukata rufaa Mahakama Kuu kuhusiana na adhabu pekee.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu, Wakili wa Serikali, Jehovaness Zacharia, alidai hawana kumbukumbu ya makosa ya zamani ya washitakiwa hivyo mahakama iwape adhabu inayostahili kulingana na makosa. 
Katika mashitaka yao, inadaiwa kuwa kati ya Novemba 2016 na Februari 2017, Jijini Dar es Salaam, walitengenezamfumo wa kutumia huduma za mtandao kwa lengo la kukwepa kodi ya kupokea na kusambaza simu za kimataifa bila kibali cha TCRA. Pia wanadaiwa katika kipindi hicho waliendesha hiyo mifumo ya kupokea na kusambaza simu za kimataifa bila ya leseni.

Inadaiwa Novemba 20, 2016 waliingiza vifaa vya kielektroniki bila ya kuwa na leseni ambapo katika tarehe isiyofahamika Novemba 2016, walisimika vifaa hivyo ikiwamo sim box yenye namba ya siri 1152000.8.n.t.n na Laptop mbili aina ya Dell bila ya kuwa na kibali cha TCRA. 
Katika kipindi hicho, washtakiwa hao wanadaiwa kuunganisha vifaa hivyo na huduma za mitandao kwa lengo la kupokea na kusambaza mawasiliano bila ya kuthibitishwa na TCRA itakavyo sheria.

Viettel Tanzania Limited (Halotel) na Do Hong, wanadaiwa kati ya Novemba 2016 na Februari 2017 maeneo ya ofisi za Halotel Victoria Kinondoni, walishindwa kuthibitisha taarifa iliyotolewa na Unex Company Ltd kusajili laini za simu 1,000. Pia inadaiwa washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kuisababishia hasara TCRA na serikali ya Tanzania ya Sh 459,000,000.

SAKATA LA MO KUJIONDOA SIMBA, KIMENUKA ZAIDI, WAZEE WAIBUKA WAWASHA MOTO

$
0
0
Sakata la mabadiliko ya katiba ya Klabu ya Simba ambayo yanatajwa kuwa yanaweza kuifanya klabu hiyo kuingia katika uwekezaji wa kununuliwa kwa hisa sasa yamefikia kwenye ‘moto’ mkali.
Baraza la Wazee la Simba, limeibuka na kusema mabadiliko ya katiba ya klabu hiyo yanafanyika kihuni. Simba ilikuwa katika mchakato wa kubadili baadhi ya vipengele vya katiba ili iweze kuuza hisa zake na tayari mfanyabiashara na mwanachama wa Simba, Mohamed Dewji ‘Mo’ alishajitokeza kununua hisa asilimia 51 akiwekeza shilingi bilioni 20.

Wazee hao wametaka mchakato kwa hatua sahihi ufuatwe badala ya uharakishaji wa mambo kama ambavyo inataka kufanyika sasa na wamemuandikia barua Rais John Pombe Magufuli.

Mratibu wa Baraza la Wazee la Simba, Felix Mapua amewaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kwamba wameamua kumuandikia barua Rais Magufuli, wakiomba kumuona.

“Tunaona mambo yanapelekwa haraka na kihuni, tumeamua kumuandikia barua Rais Magufuli kupitia kwa Waziri wa michezo, Dk Mwakyembe.

“Tunaomba kumuona Rais Magufuli, tunaona hata iwe kwa dharura. Hata kidogo hatukubaliani na mambo yanavyokwenda na hatufurahi hata kidogo.

“Simba ni kubwa sana, kubwa kuliko hata Mohamed Dewji. Hivyo hatuwezi kukubali mambo yaende namna hii,” alisema na kuongeza:

“Kuna wahuni wachache wanataka kupeleka mambo kibabaishaji, tunampa rais wetu Aveva kuwa aendelee na mwendo huu huu alionao, hapa kuna tatizo na ndiyo maana tayari tumesharipoti Takukuru juu ya hiki kinachoendelea.”

Baada ya hapo mwanachama mwingine wa klabu hiyo, aliyejitambulisha kwa jina la Bosi Matola mwenye kadi namba 080 alisema: “Kilichonileta hapa ni kumpongeza rais wangu Aveva kwa kuingia mkataba na kampuni hiyo ya mapesa, kijana wetu Mo amelipa mishahara kwa miezi nane tu anaidai klabu shilingi bilioni 1.4, sasa angekaa miaka mitano si angechukua jengo.”

Amber Lulu Acha Uchafu wa Mapicha, Fanya Muziki

$
0
0
                Lulu Auggen ‘Amber Lulu’.
NIANZE kumsh-ukuru Mungu kwa kila jambo katika maisha yangu na yako msomaji wa Barua Nzito, hasa baada ya kumaliza wiki ngumu na ya majonzi kwa Watanzania wote kupatwa na msiba mkubwa wa kufiwa na wanafunzi 32 kwa wakati mmoja.
Kama mwanajamii, nina kila sababu ya kutoa maoni yangu kwa jamii na wanajamii wenyewe katika kushauri juu ya mazuri au mabaya wanayofanya. Leo hii nimeandika waraka maalumu kwa rafiki na dada yangu mpendwa, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’ aliyeanza kutambulika kwenye baadhi ya video za wasanii wa Bongo Fleva kama ‘video queen’ ikiwemo Usimsahau Mchizi ya R.O.M.A, Inde ya Dully Sykes na nyingine kibao.


Kama ilivyo kawaida maisha ni kupanda na kuongeza kitu kila kukicha, nashukuru rafiki yangu, Amber Lulu ameongeza wasifu mwingine wa kuwa msanii wa Bongo Fleva, tayari ameachia ngoma ya Watakoma aliyomshirikisha mkali wa kurap, Country Boy. Inafanya vizuri, imepenya, ni ngoma ambayo inachezeka na kama unapenda kuicheza na hata ukitembelea baadhi ya kumbi za starehe utasikia inachezwa.


Simzungumzii Amber Lulu kwa kujifananisha na Amber Rose wa Marekani, simzungumzii kwa kufanana kiana na kuiga mtindo wake wa nywele, ‘kujibinua’ kama wanavyofanya watoto wa mjini kwa sasa, kwa sababu kuiga mtu si vibaya kama utaiga mazuri yake, ila ukiiga mabaya basi utaonekana wa ajabu sana.
Kiukweli Amber unakera dada yangu kwa tabia yako ya kupiga picha za ajabu, juzikati nimeona picha ambayo umechuchumaa mbele ya mwanaume kama unafungua sehemu ya zipu yake vile. Nikiwa bado natafakari kuhusu picha hiyo, ghafla naona picha nyingine ukiwa umemshika sehemu nyeti mwanamke mwenzako.
Nini tafsiri ya picha hizi mbili? Umelenga kufikisha ujumbe gani kwa jamii? Kwamba unashiriki mapenzi ya jinsia moja au umepinda kupindukia, au ndiyo ‘kitu cha Arusha’ kinafanya kazi yake.

Najaribu kuvaa uhusika wa mimi kama baba, kaka au ndugu yako wa kiume halafu naona picha zako za utupu mitandaoni unadhani nitajisikiaje, nitawaza nini juu yako?
Hivi Amber kama una wazazi wako unahisi unawaweka kwenye wakati gani huko wanakoishi, mbaya zaidi picha zilizoko mitandaoni si kwamba zimepigwa kwa kuibia au bahati mbaya la hasha, si kweli kwamba zimepostiwa na wabaya wako kwa kusudi la kukuchafua ni picha ulizojiandaa kwa pozi za uchafu huo kisha ukaziposti mitandaoni.
Waswahili wanasema akili za kuambiwa changanya na za kujiongeza, Amber umekuwa ukifanya mambo ya ajabu kwa sababu ya kumuiga ‘role model’ wako, Amber Rose wa Marekani, lakini unasahau kuwa Afrika na Marekani ni vitu viwili tofauti, kuna mambo yakifanyika kule au kwingineko huonekani wa ajabu lakini mambo hayohayo ukiyafanya kwetu unaonekana ni mwendawazimu.


Rafiki yangu mbona unajiabisha hivyo, kwa nini usijikite zaidi kwenye kufanya muziki kuliko kupiga picha za uchafu na kutupia mitandaoni.
Nakukubali sana kwenye muziki lakini kwenye mapicha ya uchafu siko nawe, nikisema nakukubali namaanisha na hata siku za nyuma niliandika makala inayosema

VITA YA WAUZA SURA WA KIBONGO, ndani ya makala hayo nilizungumzia vita yako na Gigy Money na Lulu Diva kuanzia kwenye video queen hadi kuwa wanamuziki na nikachambua kuwa mtu ambaye nyota yake inaonekana kung’ara kwenye muziki ni wewe, sina nia mbaya ya kukupaka matope lakini kwa hili la mapicha ya ajabu acha tu nikupake.

Mapicha picha hayo si tu nimeyaona mtandaoni lakini hata maisha yako ya kawaida yamejaa ulimbukeni fulani hivi. Nakumbuka hata kwenye bethidei yako iliyofanyika Bunju nje kidogo ya Jiji la Dar ulikata mauno ya ajabu kwa kushika meza na kufanya kila aina ya mbwembwe.
Sikatazi usicheze ila cheza kwa staha, unachokifanya ni ushamba, ulimbukeni, ni kushindwa kufikiria nje ya boksi kuwa kuna maisha nje ya sanaa ya mapichapicha machafu.


Nilibahatika pia kusikilia mahojiano yako na kituo kimoja cha redio, Amber hata watangazaji waliokuhoji walikuambia kuwa kati ya video queen walioachia ngoma zao ni wewe tu ndiyo unaonekana kung’ara na una nafasi kubwa ya kutoboa kwenye muziki.
Ulikazia kile walichosema kuwa unashukuru Mungu kwa sababu umekuwa ukiongozana na baadhi ya mastaa wakubwa kwenye shoo zao za mikoani, hilo linajidhihirisha kwako kuwa nyota njema imeonekana asubuhi.
Kwa nini rafiki yangu usitumie nyota iliyong’ara kuing’arisha zaidi kuliko kupigania kufifisha bila kujua kama unaififisha?


Amber nakupenda ndiyo maana nakwambia lakini kwa kuwa umeshavurugwa na ukakubali kuvurugika si rahisi kunielewa lakini naamini siku zijazo utanilewa tu.
Kama kaka na rafiki yako nakushauri, kaa chini ujitafakari upya, achana na maisha ya mtandaoni, fanya muziki, jikite zaidi kwenye kuimba, unaweza rafiki yangu au unasubiri hadi msemo wa kusikia kwa kenge atokwe damu masikioni?



CHANZO: RISASI JUMATANO

Priyanka Chopra apata shavu kwenye Quantico Season 3

$
0
0

Staa wa Quantico, Priyanka Chopra ameongezewa episodes 13 za tamthilia hiyo katika Season 3.


Mrembo huyo wa India ambaye amafanya vizuri nchini Marekani amethibitisha hilo kupitia mtandao wa Twitter kwa kuandika, “So excited about the season 3 pick up for #Quantico congrats to everyone who made it happen! #AlexParrish will be back soon...”

Alhamisi ya mwezi Februari ya mwaka huu Chopra alikimbizwa hospitali baada ya kuumia wakati akiigiza kwenye tamthilia hiyo na kuteleza na kuangukia kichwa.

Quantico ambayo inaendelea kutayarishwa mjini New York, Marekani inaonyeshwa katika kituo cha runinga cha ABC. Kwa mujibu wa Nielsen umetangaza kuwa season 2 ya tamthilia hiyo iliyokuwa na episodes 21 ilifanikiwa kutazamwa na watu milioni 2.8 ikiwa ni idadi ndogo zaidi katika utazamwaji wa tamthilia hiyo..

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Mei 18, 2017

$
0
0



Hapa tumekuanikia kurasa za mbele na za nyuma za magazeti yote ya Tanzania leo, Mei 18, 2017. Ni yale ya Hardnews, Udaku na Michezo.

Rest In Peace Dogo Mfaume aliyefariki dunia jana mchana, Historia Yake

$
0
0


DAR ES SALAAM: Rest In Peace Dogo! Haya ndiyo maneno tunayoweza kusema baada ya kupata taarifa za kushtusha za kifo cha msanii maarufu wa nyimbo za Mchiriku na Mnanda, Dogo Mfaume aliyefariki dunia jana mchana wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Amani lina data za kutosha. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dogo Mfaume alikuwa akisumbuliwa na uvimbe kichwani na kwamba kesho, alikuwa katika ratiba ya kufanyiwa upasuaji baada ya tatizo hilo kumsumbua kwa miezi kadhaa.

KUTOKA SOBER HOUSE, KIGAMBONI
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Pilli Missanah Foundation, Pilli Missanah, Dogo Mfaume ambaye kwa muda mrefu alikuwa katika kituo hicho akipatiwa matibabu ya kuachana na utumiaji wa madawa ya kulevya, alikimbizwa hospitalini baada ya afya yake kuzidi kuzorota. “Dogo Mfaume alikuwa na matatizo ya uvimbe kichwani kwa muda mrefu, ingawa pia alikuwa akisumbuliwa na magonjwa mengine kiasi kwamba alifikia wakati akashindwa hata kuongea. “Ugonjwa wake ulimsumbua kwa muda wa miezi mitatu, baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya tukalazimika kumpeleka Muhimbili kwa matibabu zaidi na kesho (Ijumaa) alikuwa afanyiwe upasuaji huo,” alisema Pili.

DOGO MFAUME NI NANI?
Wakati vijana wenzake wakitamba na Muziki wa Kizazi Kipya maarufu kama Bongo Fleva, Dogo Mfaume aliibuka katikati ya miaka ya 2000 akiimba muziki wa mitaani, ambao ulionekana kama wa kihuni zaidi, wa Mchiriku na
Mnanda, ambako alifanikiwa kujitengenezea jina kubwa baada ya nyimbo zake mbili, Hereni na Kazi yangu ya Dukani kumfikisha kileleni. Mwaka 2009 akiwa katika ubora wake, Dogo Mfaume alitwaa Tuzo ya Msanii Bora wa Muziki Asilia kupitia kibao chake hicho cha Kazi Yangu ya Dukani.


INTERVIEW YA MWISHO NA GLOBAL TV Miezi michache iliyopita, Dogo Mfaume alifanya mahojiano na Global TV Online, akiwa katika kituo cha kusaidia kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya, Kigamboni jijini Dar es Salaam, ambapo alizungumza mambo mbalimbali kuhusiana na safari yake ya matumizi ya madawa ya kulevya.

JINSI ALIVYOANZA ‘KULA UNGA’ “Mimi nilikuwa navuta bangi tu, sasa siku moja nilikuwa nimekwenda kujiweni nikamkuta mshkaji anavuta, nikamgongea nikijua ni bangi tu ya kawaida. Sasa yule jamaa hakutaka kuniambia ukweli, aliogopa pengine ninaweza kwenda kumtangazia kwa watu na asingeweza kuninyima maana nisingemwelewa. “Kwa hiyo akanipa, nikapiga pafu tatu akaninyang’anya, akavuta tena mara kadhaa akanipa, nikavuta tena, nilipomaliza, nikaona raha f’lani ambayo sijawahi kuiona tangu nianze kuvuta bangi. Nikaanza kama kusinzia hivi kitu ambacho siyo kawaida.”
ATOA UJUMBE MZITO “Kusema kweli ile raha ilinifanya kesho yake nimtafute yule mshkaji nikamuuliza vipi ile kitu ya jana, akaniambia ili tuipate, inatakiwa buku (shilingi elfu moja) nikampa mia tano na yeye akatoa mia tano, akaenda kuchukua, tukavuta. “Hivyo ndivyo nilivyoanza kuvuta, hii kitu ukianza siyo rahisi kuacha, ndivyo hivyo ilivyokuwa.”
NIMETESEKA MIAKA SABA “Nimetumia madawa ya kulevya kwa muda wa miaka saba, mwanzo nilikuwa najifichaficha watu wasinione, lakini hali ilivyozidi nikajikuta sioni aibu tena, badala ya kwenda kununuliwa nikawa naenda mwenyewe.”
SIKILIZA SIMULIZI YAKE YA KUSIKITISHA
Wakati mamia ya mashabiki wa Mchiriku nchini wakiamini kuwa Kibao cha Kazi Yangu ya Dukani, kilimpa mafanikio makubwa msanii huyo kimuziki na kimaisha, ukweli kutoka mdomoni mwake ni kuwa wimbo huo ndiyo ulichangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka na hatimaye kuharibika kabisa kwa maisha yake.
“Nilikuwa nimeshaanza kutumia unga wakati natoa kile Kibao cha Kazi Yangu ya Dukani, kusema ukweli wimbo ule ndiyo ulichangia sana kuniangamiza, kwa sababu nilikutana na watu wengi na pia nilipata pesa nyingi, nilikuwa sina mke, sina majukumu, kwa hiyo kadiri nilivyopata pesa ndiyo kasi ya kubwia ilivyozidi

. VITU ALIVYOSEMA HATA VISAHAU KUHUSU UNGA
“Kuna siku tulikuwa tumealikwa kwenye shoo sehemu, ilipofika zamu yangu nikaitwa kupanda jukwaani, sasa nilivyoshika mic tu, mtu mmoja aliyekuwa karibu akaanza kupayuka kwa sauti, toa teja hilooo, toa teja hilooo, tumetoa hela yetu hatutaki mateja sisi…Dah! Jamaa alinitoa kabisa kwenye reli, sitakisahau kile kitendo. “Nilimuona jamaa kama ndiyo ananitangazia kwa sababu wakati anasema, alikuwa akisikika katika spika, nikajua Tanzania nzima watajua kama nakula unga maana hadi wakati huo nilitam
bua kuwa hakuna mtu aliyekuwa anajua,” alisema Dogo Mfaume.

Hadi Amani linakwenda mitamboni kulikuwa hakuna taarifa zozote kutoka kwa familia yake, kuhusu msiba na shughuli za mazishi, lakini baadhi ya wasanii wenzake, kupitia mitandao ya kijamii, walizungumzia kifo hicho cha mmoja wa wasanii walioacha alama katika Mchiriku. Wasanii ambao walikuwa wameposti kuhusiana na msiba huo ni pamoja na Mr. Blue, Mheshimiwa Temba, Chegge Chigunda, Nay wa Mitego na Dulla Makabila walionesha kumlilia. Aidha, mitaani hasa uswahili ambako alikuwa na mashabiki wengi kufuatia aina ya muziki aliokuwa akifanya, simanzi imetawala hasa kufuatia taarifa kuwa, ilikuwa arejee kwenye game baada ya afya yake kutengemaa. Mungu ailaze mahali pema roho ya marehemu, Amina. (CHANZO: GAZETI LA AMANI)

Mume wa Zari hoi akisumbuliwa na Moyo

$
0
0
KAMPALA: Habari mbaya zilizotufikia zinadai kuwa, aliyekuwa mume wa staa wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Tycoon Ivan Ssemwanga yu hoi bin taaban akisumbuliwa na maradhi ya shambulio la moyo (Coronary Artery Disease). 
Aliyekuwa mume wa staa wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Tycoon Ivan Ssemwanga akiwa na zari.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya jijini Kampala, Uganda ambako ndiko maskani yake yalipo maeneo ya Munyonyo, pamoja na kwamba ana makazi Pretoria, Afrika Kusini, Ivan alionekana hadharani kwa mara ya mwisho akiwa amedhoofu na rangi ya ngozi kupauka, tofauti na alivyozoeleka kuwa na rangi nyeusi yenye mng’aro alipotinga kwenye Pati ya Blankets and Wine iliyofanyika Kampala hivi karibuni. Chanzo kilichomshuhudia Ivan kilitonya: “Sisi wenyewe tulipomuona kwenye Blankets and Wine Party akiwa na rafiki yake, Ed Cheune, kwanza hatukumtambua, lakini tulipomuangalia vizuri ndipo tukamjua ni yeye. Ukweli tulishtuka sana na tulijua anaumwa.



 “Tofauti na alivyozoeleka kuwa ni mtu wa bata, lakini siku hiyo alikuwa mpole sana. Alikuwa hanywi pombe kali na za bei mbaya kama alivyozoeleka. Badala yake alikuwa anakula samaki na kushushia na soda, tofauti na wadhifa wake unavyojulikana. Ivan linapokuja suala la starehe, huwa hana utani kwa sababu anajua kujiachia. “Nakumbuka tukio hilo lilikuwa Mei 11 (mwaka huu) na tangu siku hiyo hajawahi kurudi kwenye hali yake ya kawaida hadi tuliposikia amelazwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo,” kilikaririwa chanzo kimoja na mitandao ya Uganda. Hata hivyo, Amani lilizungumza na mtu wa ndani ya familia ya Zari kwa Bongo ambaye alibumburua kwamba, kufuatia ishu hiyo, Zari amekuwa akiangua kilio kumlilia mumewe huku akiwataka watu kumuombea ‘eksi’ wake huyo kwa Mungu ili apone haraka.

“Bi mkubwa hana raha kabisa, unaambiwa Ivan anamliza maana si unajua ni baba wa watoto wake watatu? ‘So’ na yeye kama binadamu lazima roho imuume kusikia mzazi mwenzake anaumwa,” alisema mtu huyo kwa ombi la kutotajwa gazetini. Juzi Jumanne, Zari kupitia ukurasa wake wa Snapchat aliandika: “Siku mbili kwangu zimekuwa ngumu, nawaomba tumuombee Ivan.” Baadaye mama huyo wa watoto watano alitupia picha akiwa amekwenda kumjulia hali Ivan katika Hospitali ya Steve Biko Academic huko Pretoria, Afrika Kusini ambapo jamaa huyo alionekana kuwa katika hali mbaya kiafya. Ndugu, jamaa, marafiki na watoto wake watatu aliozaa na Zari wamekuwa wakimuombea ili kurejea katika uzima wake

Kiongozi Mwingine Auawa kwa Kupigwa Risasi Rufiji – Pwani

$
0
0
Njwayo amesema kabla ya kuuawa kwa mwenyekiti huyo, pia wauaji hao walianza kumjeruhi kwa kumpiga risasi ya tumboni mtoto wa marehemu aliyetajwa kwa jina la Nurdin Iddy Kirungi.
Mganga wa zamu katika kituo cha afya Ikwiriri, Dk Rashid Omar alisema walimpokea Nurdin akiwa na jeraha kubwa tumboni mwake ambalo halikutokeza upande wa pili.

Alisema majeruhi huyo walimpatia rufaa kwenda Hospital ya Mchukwi kutokana na kuwa anavuja damu nyingi sana.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya LeoIjumaa ya Mei 19, 2017

Jay Z na Beyoncé wana mkwanja unaovuka Dola bilioni moja

$
0
0
WANANDOA wawili wakali wa wanamuziki wa familia ya Carters, ambao ni Jay Z na Beyoncé wana mkwanja unaovuka Dola bilioni moja.
Kwa mujibu wa jarida la Forbes, Hov (Jay Z) ana ‘mpunga’ unaofikia Dola milioni 810 na mkewe, Yoncé, ana Dola milioni 350 na hivyo kuwafanya wanandoa hao kuwa na Dola bilioni 1.16 kibindoni.
Pamoja na habari hiyo, kivutio zaidi cha utajiri huo ni kwamba huenda takwimu hizo zilizotajwa si za sasa.  Takwimu za Jigga (Jay Z) zinatokana na listi ya watu watano  iliyotolewa na Forbes kabla hata ya ziara iliyomwingizia mwanamuziki huyo Dola 20 milioni alipozunguka sehemu mbalimbali  Marekani kutumbuiza.
Utajiri wa Jay Z unatokana na vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na shampeni ya Roc Nation and Armand de Brignac.  Wakati huohuo, Malkia Bey (Beyoncé) huingiza mkwanja kutokana na vyanzo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kufanya maonyesho ya peke yake na  biashara ya nguo kupitia kampuni za Ivy Park na Parkwood.
Nyota hao wawili pia wanamiliki kampuni la huduma za muziki la TIDAL  ambalo linazidi kushamiri kwa kushirikiana na lile la Sprint.

Wanandoa hao matajiri wanaotegemea kupata watoto mapacha hivi karibuni, wanasaka nyumba ya anasa itakayogharimu mamilioni ya Dola huko Los Angeles kwa ajili ya familia yao ambayo inazidi kupanuka.

Lulu Amber AGOMA kufuta tatuu ya Young D, Kisa Kipo Hapa

$
0
0
VIDEO Queen anayesumbua Bongo, Lulu Augen ‘Amber Lulu’ ameweka wazi kuwa, pamoja na kwamba kwa sasa msanii wa Bongo Fleva, David Genzi ‘Young D’ hana mpango naye, hatafuta tatuu yake kwa kuwa inabaki kama kumbukumbu maishani kwake.
 
Akizungumza na Story Mix, Amber anayefanya pia Muziki wa Bongo Fleva akiwa na Ngoma ya Watakoma alisema, tatuu hiyo yenye jina la Young D iliopo upande wake wa kushoto ni kumbukumbu tosha ya maisha yake. 
 
“Sina mpango wa kuifuta tatuu ya mwanaume niliyempenda, hata mwanaume ajaye atalazimika kulifahamu hilo, siwezi kuifuta eti kisa hanitaki, hii itabaki mwilini mwangu daima,” alisema Amber Lulu.

Wema kwa hili la mihela, wa kukuoa humpati ng’o!

$
0
0
 
WEMA Sepetu, kwangu ni miongoni mwa wasanii waigizaji wa kike wanaojua nini wanafanya wakiwa mbele ya kamera. Na samahani, siyo peke yake, wapo na wengine ninaowakubali kama Irene Paul. Ni wasichana f’lan ninaowaona wanafanya vizuri linapokuja suala la uhalisia wa kile wanachoigiza, ukiachana na wengi wanaoigiza hadi mtazamaji anakereka. 
 
Hii siyo mara yangu ya kwanza kumzungumzia Wema katika safu hii na kwa maana hiyo, sitarudia kuzitaja sifa zake nyingi katika uigizaji wa fi lamu. Na siyo kwamba ninakutana naye hapa mara nyingi kwa sababu nina chuki naye, hapana, huwezi kuwa na chuki na mtu kama Wema, ambaye ni mkarimu kwa kila mtu, uongo? Huyu binti ni role model wa watu wengi sana, wake kwa waume na katika akaunti yake ya Instagram, ana wafuasi zaidi ya milioni moja. Hao ni watu wengi mno, ina maana akitaka kuhamasisha kitu, wanaweza kutoa ushawishi kwa idadi nyingine kama hiyo na kitu kikasimama.

 Kwa maana hiyo, mtu kama huyu ni rahisi kuweka mwelekeo anaoutaka, ndiyo maana akapata hata jeuri ya kuanzisha App yake na watu kibao wanaifuatilia. Juzi hapa nimeona kitu Wema ameandika katika akaunti yake ya Instagram, anawataka mashabikiwake wakubali ukweli kuwa yeye hivi sasa hana mpenzi, kwani uhusiano wa kimapenzi aliokuwa nao zamani, hivi sasa umeisha kwani kila mmoja ana maisha yake. Lakini aliponikosha ni pale aliposema anawaomba wamuombee kwa Mungu apate mwanaume mzuri wa kuweza kumuoa, tena mwanaume huyo awe na mihela miiiingi! 
 
Hapo kwenye mihela mingi ndipo paliponitatiza. Nimewahi kusema huko nyuma, kuwa Wema kwa kule majuu, unaweza kumfananisha na binti mmoja anaitwa Kim Kardashian, mtangazaji wa televisheni ambaye pia ni mke wa rapa mashuhuri duniani, Kanye West. Kuna watu wanamsema binti huyu wa Kinyaturu kuwa eti ‘ametoka’ na wanaume wengi.

 Kwa taarifa yao ni kuwa Kim, kabla ya kuangukia mikononi mwa West, alishatoka na mastaa zaidi ya 25, achilia mbali wale ambao hawaeleweki. Huu ni umri wa Wema kutafuta mume mwenye busara wa kumuoa na siyo mwenye fedha kwa sababu hawa wenye mkwanja mbona amesha-hag nao sana tu? Kila mmoja anajua kuwa ili kutoka na supastaa Wema ni lazima uwe na waleti iliyonona, siyo kwa ajili ya kumpa, bali kwa sababu ya gharama za kum-handle

Nilidhani angetumia nafasi ile kuwaomba mashabiki wake, wamuombee kwa Bwana Mungu wake, ampate mume bora wa kumuoa ambaye ni mwenye hofu ya Mungu, busara, hekima na upendo,
maana ndicho kitu cha msingi zaidi mwanamke anakihitaji kutoka kwa mwanaume anayempenda. 

Mwanamke anayetafuta mwanaume mwenye hela, hawezi kumpata wa kumuoa, bali wa kumchezea tu kwa sababu wenye hela hawajui kupenda, atapenda wangapi wakati kila mrembo anamhitaji? Wanaume wengi wenye hela huoana na wapenzi wao walioanza nao kuhangaika pamoja, hawa wengine wanaojitokeza huku juu, huwa ni wa kupotezea tu wakati. 

Hivyo nikupe ushauri mdogo wangu, kwanza umri wako wa kuolewa umeshafi ka, ni vyema na haki sasa ukatafuta mtu wa kutuliza naye mpira. Pili, usiwaze sana kuhusu hela, zinatafutwa na wewe unao uwezo wa kuzipata, ukazitumia na mumeo. Umekutana na wanaume wengi wenye nazo na wewe ukazitumia sana, hukuwekeza ili zikufae ndiyo  utampa wakati huu?

Ijumaa Figa Bomba Girl 2017: Sanchi, Wema Watifuana Kwa Kura

$
0
0
 
Jane Ramoy ‘Sanchi’ 
 HALI imezidi kuwa tete ambapo wiki hii modo, Sanchi ametifuana vilivyo na Wema Sepetu. Kwa mujibu wa kura mlizopiga zimepelekea wawili hao kutifuana nafasi za juu wakifuatiwa na Masogange na Sasha 
Wema Sepetu 

Je, ungependa nani aibuke mshindi kati ya hiyo tano bora iliopo? Jibu ni rahisi, Chukua simu yako, nenda kwenye sehemu ya kuandikiaSMS kisha andika neno SHEPU acha nafasi kisha andika namba ya mshiriki unayetaka abaki na utume kwenda namba 15542. 

Agness Gerald, maarufu Masogange  
    
Hii ni kwa wateja wa VODACOM pekee. Aidha, wadada hao unaowaona wana mapicha makali sana ambayo unaweza kuyaona kwa uzuri kupitia ukurasa wetu wa Facebook kwa jina la GAZETI LA IJUMAA. Tembelea na u-like!  

Picha za Masogange zawavutia wanainstagram wamwaga sifa


LIVE: Miss Ustawi wa Jamii, 2017 Kwenye Ukumbi wa King Solomon, Dar

$
0
0

KINYANG’ANYIRO cha kumtafuta Miss Ustawi wa Jamii, 2017 muda huu kwenye Ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga jijini hapa huku msanii wa Bongo Fleva, Ben Pol, Mgogosi na wengine kibao wataporomosha burudani ya ukweli.

Wema Sepetu Anaswa Akiwa karibu na AKIWA KARIBU mume wa mtu

$
0
0

Staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu.
DAR ES SALAAM: Kuna ishu! Ndivyo wasemavyo wapenda ubuyu kufuatia ukaribu wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu na mume wa mtu anayejulikana kwa jina la Daudi Mambya baada ya kunaswa wakiwa pamoja kwenye matukio kibao, Risasi Jumamosi linakupa habari kamili. Kwa mujibu wa watu hao, wawili hao wamekuwa wakionekana wakiwa ‘veri klozi’ kila anapokwenda Wema hasa mahakamani kwa ajili ya kesi inayomkabili ya kutumia na kukutwa na madawa ya kulevya.
Imeelezwa kuwa, mara zote ambazo Wema alitinga katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar kwenye kesi hiyo, aliambatana na Daudi hivyo watu kuanza kuhoji ‘sivii’ ya jamaa huyo kwa Wema ilihali kila mtu anajua ni mume wa mtu. 

Chanzo makini kililieleza Risasi Jumamosi kuwa, huenda wawili hao wana kitu nyuma ya pazia kwa sababu Daudi amekuwa mstari wa mbele kuhudhuria mahakamani tofauti hata marafiki wa karibu na Wema.
 
“Yaani huyu Daudi ambaye ni mume wa mtu, kila Wema akienda mahakamani lazima naye awepo pembeni yake kumsindikiza, jambo hili limezua maswali kwa watu kibao na kusema huenda anammiliki mwanadada huyo maana siyo kawaida kwa mtu mwenye kazi zake kupoteza muda kwenda kumsindikiza tu mtu ambaye hamhusu,” kilidai chanzo hicho.

Baada ya Risasi Jumamosi kunasa matukio tofauti ya Wema na Daudi wakiwa pamoja kwa siku tano tofauti, paparazi wetu alimtafuta Daudi ambaye alikiri kwenda mahakamani kila kesi ya Wema inapotajwa kwa kuwa ni rafiki yake na hawezi kumuacha akiwa na matatizo.

“Sina undugu na Wema ila ni rafiki yangu sana na sina uhusiano naye wa kimapenzi kama watu wanavyodai, unajua urafiki mzuri ni ule mnaosaidiana katika shida na raha hivyo siwezi kumtenga au kumuacha Wema wakati huu wa matatizo ilihali wakati wa raha tulikuwa marafiki.

“Wema kipindi hiki amejua kuwa hana marafiki wa kweli maana rafiki wa kweli ni yule mnayesaidiana katika shida na raha ndiyo maana mimi nikaamua kuwa naye kwani najua maana ya urafiki, anao wengi, lakini wapo wanaomjua wakati wa raha tu,” alisema Daudi huku Wema akigoma kupokea simu kila ilipopigwa.

CHANZO; RISASI JUMAMOSI

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Mei 20, 2017

$
0
0





Hapa tumekuanikia kurasa za mbele na za nyuma za magazeti yote ya Tanzania leo, Mei 20, 2017. Ni yale ya Hardnews, Udaku na Michezo.

Leo Ndiyo Leo Nay wa Mitego, Barnaba Kukinukisha Dar Live

$
0
0

Nay wa Mitego akiwarusha roho mashabiki katika Viwanja vya Karume jana.
BAADA ya kuliamsha dude katika shoo ya bure jana ndani ya Viwanja vya Karume jijini Dar, Mkali wa Ngoma ya Wapo, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ anatarajiwa kuungana na mastaa kibao katika bonge la shoo linalotambulika kama Wapo Concert leo (Mei 20), ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar.
Akizungumza na Mikito Nusunusu, Nay alianza kwa kuwapongeza mashabiki wote waliofurika jana katika Viwanja vya Karume na kuwasihi moto uendelee kuwa huohuo siku ya leo wajitokeze kwa wingi.
“Nimefarijika sana, vijana wengi bado wanatamani burudani kutoka kwangu na leo (jana) ile ilikuwa rasharasha tu mvua ya mawe ipo kesho (leo) ndani ya Dar Live.

“Kwa zaidi ya miaka mitatu sijafanya shoo ya kishindo na safari hii itakuwa kiboko maana nimejiandaa vya kutosha kuwapa mashabiki kitu wanachopenda.
Nitapiga ngoma zote kuanzia Itafahamika, Helo, Muziki Gani, Muda Wetu, Pale Kati Patamu, Uko Kwenu Vipi hadi Shika Adabu Yako na Wapo,” alisema Nay.
Naye Mratibu na Meneja wa Dar Live, Juma Mbizo aliongezea kuwa usiku huo unaotambulika pia kama Usiku wa Wabishi, watakuwepo wakali kibao wanaotikisa katika vichekesho na Muziki wa Bongo Fleva.
Kala Jeremiah
“Tutakuwa na mabingwa wa vichekesho wanaotikisa kwa sasa Bongo, Mkali Wenu na Ebitoke, tutakuwa pia na Shilole wengi mmezoea kumuita Shishi ambapo atakamua ngoma zake kibao bila kusahau inayobamba kwa sasa ya Hatutoi Kiki, atakuwepo pia Barnaba Classic, wengi mnamtambua kwa sauti tamu aliyonayo, basi atawaburudisha kwa ngoma zake nyingi ikiwemo Milele, Magumegume, Lover Boy, Nakutunza, Mapenzini na Lonely huku pia mkali mwingine Kala Jeremiah akitinga na ngoma zake kali kama Dear God, Waambieni, Usikate
Tamaa na Wana Ndoto,” alisema Mbizo na kuongezea; “Mashabiki wasiwaze kabisa kuhusu kiingilio kwani lengo ni kutoa shoo sawa na bure hivyo watalipia hela ya mboga yaani kiingilio kiduuuuuchu sana cha shilingi 5,000 tu kitakachomuwezesha kila mpenda burudani aweze kuhudhuria na kuimba Wapo pamoja na Nay jukwaa moja,” alimaliza Mbizo.

Wengi wanapishana na ndoa, tengeneza njia kwa muda sahihi!

$
0
0


RAHA ya uhusiano wa mapenzi, ni kumpata mwenza sahihi na kwa wakati muafaka. Unapopishana na muda, unachelewesha maendeleo yako maana mapenzi ni chachu ya maendeleo. Ili uingie kwenye familia, inakupasa uingie katika muda sahihi na mtu sahihi. 


Kinyume chake utaishia kuchezewa, ukija kushtuka umri unakuwa si rafiki. Utaingia kwenye uhusiano na mtu ilimradi tu na wewe uwe na mtu. Kwa sababu tu unataka na wewe uwe na familia. Lakini kama ungeingia mapema, pengine ungekuwa mbali. Wengi sana wanajuta kwa kupoteza muda. Wengi wanalia kwa kuingia kwenye uhusiano na mtu ambaye si sahihi. Ukitaka kufanikiwa kwenye uhusiano, hakikisha unaingia na mtu sahihi na katika muda muafaka. Ukisikiliza simulizi za wanaume wengi kwa sasa, watakuambia wamechoka kuishi maisha ya ubachela. 

Wanataka kuwa na wenza wao ili kwa namna moja au nyingine, washirikiane katika kutengeneza maisha na wapate maendeleo kabla uzee haujawanyemelea. Wanakiri kwamba kwa kuishi maisha ya ubachela, wanajikuta wakiwa kwenye matumizi makubwa yasiyokuwa ya lazima. Wanalazimika kutumia fedha nyingi kwa kununua vyakula hotelini, kuwapeleka wanawake baa, gesti au hoteli pamoja na mambo mengine mengi ya starehe. 
 
Kifupi unafika wakati wanayachoka hayo maisha. Wanayaona hayana tija katika suala zima la maendeleo. Hapo ndipo wanawasaka wenzi wa maisha kwa udi na uvumba. Bahati mbaya sana, wakati wakiwa wanawasaka wenzi, wanakutana na changamoto ya wale ambao wanawahitaji. Mwanaume anakuwa yuko tayari kuingia kwenye uhusiano lakini mwanamke anakuwa bado. Anataka kuula ujana na yupo katika kile kiwango cha ‘kunguru hafugiki’. 

Mwanaume hata afanye nini, yeye si kutulizwa akatulia. Si wanaume pekee, hata wanawake nao wanakutana na kisanga hiki. Unakuta mwanamke yupo tayari kwa lolote, amechoshwa na maisha ya kuhangaika na dunia, anataka kuingia kwenye uhusiano wenye tija lakini wapi. Anaambulia patupu maana kila anayekutana naye, hana huo mpango. Huu ndiyo ulimwengu ulivyo. Mwanaume aliye tayari, anahaha kumpata mwanamke aliye tayari bila mafanikio. Vivyo hivyo mwanamke aliye tayari, naye anahangaika kila uchwao kumsaka mtu ambaye atakuwa baba wa watoto wake lakini naye anapishana naye. 

USIKURUPUKE Linapokuja suala la kumsaka mwenzi wa maisha, hupaswi kukurupuka. Unapaswa kufanya tathmini ya kina ili uweze kumpata yule ambaye ni sahihi. Usiendeshwe na tamaa ya mwili. Kwamba huyu mrefu, huyu mfupi huyu ana hiki, tazama mahitaji sahihi ya mtu unayemtaka. Unayetaka kuingia naye kwenye uhusiano, ana tabia njema? Ana hofu ya Mungu? Hofu ya Mungu, ni chachu ya mafanikio Mwenye hofu ya Mungu ana tabia njema. Mwenye hofu ya Mungu ni mvumilivu. Ana hekima, ana busara na anaweza kusamehe pale inapobidi. Mwenye hofu ya Mungu si mtu wa visasi. Si mtu wa kukaa na chuki au kuwa na kinyongo. Anapoombwa msamaha wa jambo alilokosewa, akasema amesamehe basi ujue limeisha. Hutalisikia tena! 

MUDA NI KITU CHA THAMANI
 Tunashauriwa tusipoteze muda. Pale unapoona upo na mtu sahihi, mwenye malengo sahihi tunapaswa kupashikilia. Muda haumsubiri mtu. Usiseme eti utaingia kwenye ndoa baadaye, safari ya ndoa inaanza na uchumba. Hakikisha unaujenga kwa muda muafaka na uweze kuingia na mtu sahihi. Kuchelewa kuingia, wakati mwingine ni kujikuta unaingia na mtu ambaye si sahihi. Utajikuta umeingia kwa sababu tu unaona umri unakutupa mkono. Yeyote atakayejitokeza ni halali yako. Tengeneza njia sahihi katika muda sahii.
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>