Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

MMILIKI WA SALUTI5 AFIWA NA MAMA YAKE

$
0
0
 Marehemu Bi Desta Mohamed enzi za uhai wake.
 

Mmiliki wa mtandao wa Saluti5, Said Mdoe (kushoto) akiwa na mama yake.
MAMA mzazi wa mmiliki wa mtandao wa Saluti5, Said Mdoe - Bi Desta Mohamed - amefariki ghafla Jumatatu ya tarehe 31/3/2014 saa 1 za jioni.

Alipata homa kali Jumapili mchana, akapelekwa hospitali (IMTU) akapata matibabu na kuruhusiwa kurudi nyumbani. Hali yake haikuwa mbaya wala ya kutia mashaka.

Jumatatu akaamka vizuri na akashinda vizuri hadi saa 12 za jioni hali ipoanza kubadilika tena. Akafariki akiwa njiani kupelekwa hospitali.

Msiba uko Dar es Salaam, Mbezi Beach Old Bagamoyo Road kituo cha Zena Kawawa.
Mazishi yatafanyika Jumanne 1/4/2014 saa 10 alasiri kwenye makaburi ya Mbezi Beach (New Bagamoyo Road) mbele kidogo ya  Masana Hospital.
2jiachie.com tunapenda kuwapa pole Said Mdoe na wafiwa wote.
INNA LILLAHI WAINNA ILAYHI RRAAJIUN.


HARUSI YA MTOTO WA RAIS WA NIGERIA, WAGENI WAALIKWA WAPEWA IPHONE 5 KILAMMOJA

$
0
0
Hizi ni zawadi zaiPhone 5 ‘Gold plated customized’ walizopewa wageni waalikwa.Juu ya maboksi yaliyokuwa na zawadi ya simu hizo pameandikwa ‘Leeberry and her Prince wish you all the best for making our day beautifull. Thanx for coming and God Bless you’Maharusi Faith (katikati) na Godswill (kushoto) wakiwa na Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan.Kibongo bongo tumezoea mtu anapotaka kufunga ndoa lazima ipitishwe michango ya kutosha ili kuweza kufanikisha sherehe, na pia mchango wako ndio huwa kiingilio chako yaani bila kuchanga hupati mwaliko.
Mambo yamekuwa kinyume katika harusi ya mtoto wa kike wa Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria aitwaye Faith, ambaye katika harusi yake iliyofanyika April 12, 2014 wageni walioalikwa wamefanyiwa mshangao kwa kupewa zawadi ya simu za iPhone 5 ‘Gold plated customized’, zilizoandikwa majina ya maharusi hao Faith na Godswill.

CHANZO NI BONGO 5

KATIBU MKUU WA CCM,KINANA AWASILI SALAMA MKOA WA KATAVI USIKU HUU AKITOKEA KIGOMA

$
0
0

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia kwa ufupi wakazi wa mji wa Karema mkoani Katavi usiku huu mara baada ya kuwasili akitokea mkoani Kigoma kwa boti na kusafiri nayo ndani ya ziwa Tanganyika takribani kwa masaa kumi na manne.Kutokana na safari hiyo kuwa ndefu ya majini,inaelezwa kuwa kuna baadhi ya Watu wamedai msafara wa Katibu Mkuu huyo,Kinana umepotewa ziwa la Tanganyika,jambo amabalo si la kweli na la kizushi.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwapungia wenyeji wake (hawapo pichani) waliofika kumpokea usiku huu kwa boti akitokea mkoani Kigoma  katika bandari ya Karema mkoani Katavi,ambako amemaliza ziara yake ya siku tano na kuhamia mkoani Katavi ambako pia atakuwa na ziara ya siku nne.
 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanal Mstaaf Issa Machibya akishuka kwenye boti usiku huu kwenye bandari ya Karema mkoani Katavi akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,na Viongozi wengine wa Taifa,Mkoa na Wilaya tayari kwa kuanza ziara ya siku nne mkoani Katavi. 
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishuka kwenye boti wakati wenyeji wake (hawapo pichani) walipokuwa wakimsubiri kumpokea usiku huu akitokea mkoani Kigoma  katika bandari ya Karema mkoani Katavi,ambako amemaliza ziara yake ya siku tano na kuhamia mkoani Katavi ambako pia atakuwa na ziara ya siku nne.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa na Viongozi mbalimbali wa mkoa na Wilaya ndani ya Mkoa wa Katavi usiku huu,alipokuwa akiwasili kwenye bandari ya Karema mkoani humo usiku huu.Kinana ameongoza na Katibu Wa NEC,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye,Mjumbe wa NEC,Balozi Ali Karume,Mkuu wa mkoa wa Kigoma,Kanal Issa Machibya,Mwenyekiti wa CCM,Mkoa wa Kigoma ndugu Kabouru na wengineo.
 Kinana akipokelewa na Gwaride la chipukizi usiku huu ndani ya mkoa wa Katavi.

CHOMBEZO: MPANGAJI SEHEMU 21

$
0
0

“Okey.Nitafanya hivyo”.Nilimjibu na kuingia ndani na kumwacha yeye amesimama pale gizani.

Usiku huohuo nikiwa napanga nguo zangu ili kesho asubuhi na mapema niondoke,ndipo simu yangu ikaita.Nilipoangalia,alikuwa ni Gasper.
“Niambie Master P.Mtoto wa Vitoto”.Alianza Gasper kwa furaha.
“Dah! Huku mambo mwamala kaka”.Nilimjibu nikimaanisha mambo yameharibika.

“Kivipi kaka”.Naye aliniuliza.
Huku nikiwa naongea kwa sauti ya chini,nikamjibu.
“Eee bwana Shei ana mimba, kaka”
“Acha bwana,ya nani?”.Naye aliniuliza.
“Yangu kaka”.Nikamjibu.
“Hapo sasa kaka.Halafu nina taarifa mbaya zaidi kwako kuhusu kazi ya baba yake”.Naye akazidi kunipa mshawasha.
“Eheee,embu niambie”.
“Baba yake FBI”.Aliniambia.
“Una maana gani?”.Niliuliza.
“Baba ya Jasusi kaka.Jitu la CIA lile”.Alizidi kunipa hamasa Gasper ya kutaka kujua maana ya maneno yake.


FBI ni shirika la kipelelezi la Marekani huku CIA ni shirika la Kijasusi la Marekani pia.

Mashirika haya yanafanya kazi aina moja lakini katika majukumu tofauti.Kazi zikiwashinda FBI zinaenda kwa CIA,na kazi zikishindwa na CIA,zinapelekwa FBI.Sasa naambiwa kuwa baba wa Shei ni Jasus sijui FBI,halafu nimempa mimba mtoto wake.

“Bado sijakuelewa Gasper.FBI si huko Marekani kaka?”.Bado nilitaka kupata ufafanuzi halisi wa maneno yale.
“Kazi ya FBI si waijua?Au CIA si wajua kazi zao hawa?”.Aliniuliza Gasper.
“Ndio kaka.Hao ni wapelelezi”.Nikamjibu huku nikiwa na bonge la mtetemo.
“Basi na huyo dingi ni mpelelezi.Yupo usalama wa taifa huyo mzee wa hapa Tanzania.Hapo kanisani ni kujivalisha ngozi ya kondoo tu! Ili tusishtukie ishu.Ila ukweli dingi ni FBI”.Aliongea Gasper na nilijihisi mkojo kutoka baada ya kujua baba wa Sheila yupo usalama wa taifa.
“Kaka…..Kaka……Kaka mbona kimya?”.Sauti ya Gasper ilisikika lakini nilishindwa kuipa jibu na niliamua kukata simu tu!.
Baada ya kuikata ,nikaanza kupanga nguo zangu haraka haraka na kuweka vyeti na vitu vyangu muhimu mahala pake. Kisha nikakaa kitandani na kuvuta pumzi ndefu huku nikiomba kesho ifike haraka niondoke bila familia ile kuniona.
Baada ya mawazo na kusali sana,sala ambazo sijui zilikuwa zinaenda kwa nani,lakini nilikuwa naomba hadi mizimu ya mabibi inisaidie.Nilipitiwa na usingizi mzito ambao mwisho wake ulikuwa ni kesho yake saa kumi na moja asubuhi.

Ni kaka ndiye aliyekuja kuniamsha na kunitaka nijiandae haraka kwani gari linaondoka saa kumi na mbili,saa moja kuanzia pale nilipoamka.
Nilinyanyuka na kwenda bafuni ambapo sikutumia muda mwingi sana.Na hadi dakika kumi na tano zinaisha tayari nilikuwa mezani napata kifungua kinywa kwa mwendo wa haraka.

Baadae nilisikia kaka akigonga mlango wa baba mwenye nyumba. Dakika kama moja,tayari mlango ule ulifunguliwa na mzee yule alikuwa uso kwa uso na kaka.
Baada ya salamu,niliitwa na mimi ili niage kabla sijaondoka.
Mwili ulikuwa tayari ushaanza kulowa kwa jasho licha ya baridi kali iliyokuwa inapiga asubuhi ile.Macho ya mzee yule yalivyokuwa yananiangalia,waweza sema huyu mzee anataka kukurukia ili akutafune mzima mzima. Nilikuwa nimekaa kwenye kochi moja kumwelekea yeye,hivyo uso wake niliuona moja kwa moja.
“Kwa hiyo kijana unaondoka?”.Aliniuliza swali hilo mzee yule baada ya kuniona nimekaa sawia kwenye kochi mojawapo  la mle ndani.
“Ndiyo mzee,nadhani MUNGU akipenda tutaonana”.Nilimjibu kiuhakika huku nikiwaza itakuwaje kama tayari kishajua kuwa mimi ndiye mtuhumiwa anayenitafuta kwa muda sasa.
“Okey.Basi vizuri.Nashukuru sana  kwa yote tangu ulipokuja hapa.Na kama una cha kuongezea,huu ndio muda wake.Usiogope”.Mzee aliniambia maneno ambayo yalinifanya nikae njia panda nikijiuliza yana maana gani?.Ina maana mzee anajua ila anategea mimi nimwambie kuwa nimempa bend Shei?Au anataka kunitega ili nijitaje kuwa nimempa kitu mwanae.
Maswali hayo nilijiuliza haraka sana kichwani mwangu,na jibu nililolipata ni kwamba huyu mzee ananitega tu! Ili nijitaje.Sasa kaumia,sijitaji wala nini.

“Hapana mzee,sina chochote zaidi ya kukuomba uniagie kwa wengine”.Nilimwambia hivyo na kumfanya atabasamu kwa tabasamu la upande mmoja.Kisha akafungua kinywa chake.
“Mimi siwezi kukuagia bwana.Ngoja niwaite uagane nao”.Alisema mzee yule na kutaka kuwaita wanawe ili waniage.Lakini kwa kuwa kaka alikuwepo na anaenda na muda,alisimamisha zoezi hilo na kumwambia mzee yule kuwa tunachelewa.

 “Okey.Kama mnawahi,sawa.Ila ningependa huyu awaage hawa watoto”.Mzee yule bado alikuwa anasisitiza ombi lake.Lakini hadi muda ule tunaongea,tayari zilibaki dakika ishirini za mimi kuripoti kituoni kwa ajili ya kurudi zangu Morogoro.

Hatimaye nikabeba mizigo yangu kwa ajili ya kwenda kituo kikubwa cha mabasi pale Arusha.Kaka akiwa kwenye usukani na asiye na wasiwasi juu yangu,alikuwa anacheka sana jinsi mzee yule alivyokuwa anang’ang’ania niwaage watoto wake.
“Tuambiane dogo.Ndiyo baba mkwe nini?Maaana alivyokung’ang’ania,dah!Kama ruba vile”.Kaka alikuwa anaongea huku akifuta machozi kwa sababu ya kucheka.
Mimi nilikuwa na mashaka sana,na hata cheko yangu niliyoitoa ilikuwa na woga mwingi ndani yake.
“Hamna.Si wajua hawa wazee walivyowaswahili”.Nilimjibu kaka ila moyoni nilitamani sana nimwambie nini kinachoendelea.Sema sasa nilihisi ataniona wa ajabu na atakasirika sana kwa kitendo nilichokifanya kwa Sheila.Mtoto ambaye Mzee Donyo alimuona kama mkombozi wa familia ile hapo baadaye kwani dada mtu,tayari alishakubuhu kwa wanaume.
“Dogo sema bwana.Sisi ni kaka zako”.Kaka alizidi kunisisitiza lakini kwa utani mwingi hadi nikaona ni bora nifunguke tu!.Liwalo na liwe.
“Bro,pale bwana kuna matatizo makubwa tu!Ndo maana unaona mzee kanikazia niwaage wale watoto”.Nilianza hivyo kumwambia kaka huku bado macho yake yakiwa barabarani kuelekea kituo cha mabasi.
“Matatizo gani dogo tena”.Kaka aliniuliza.
“Ni Sheila”.Nikamjibu kifupi tu!.
“Sheila kafanyaje sasa,mbona hauwi spesific?”
“Sheila ana mimba yangu bro”.Nikamjibu na kugeukia dirishani ili nisione sura yake itakavyobadilika.
Kinyume na mategemeo,alionekana hata hajashtuka na zaidi alicheka sana.
“Nilijua tu!Utakuwa wewe.Ila nikawa nakusubiri nione na mimi kama utanificha,ha ha ha haaa.Dogo una kazi sana”.Alicheka kaka na kuniambia maneno hayo ambayo kwangu yalizaa mawazo mengine.
“Sasa na kazi gani Bro?”.Ilibidi nimuulize.
“Wewe unadhani unaweza kula vya watu na kuondoka mjini hivi hivi?”.Kaka aliniambia kwa mafumbo.
“Sijakuelewa kaka una maana gani”.
“Ukiondoka hapa Arusha bila tatizo,kweli mizimu yako itakuwa mikali sana.Niamini nachokwambia”.Kaka alinijibu na kuzidi kusababisha mimi tumbo la kinyesi kunibana hasa nikifikiria kazi ya mzee yule.
Nilipumua pumzi ndefu na kukaa kimya kwa mawazo ambayo sidhani kama alikuwepo wa kuyawazua muda ule.
“Tatizo lako wewe dogo hujali kitu hata kidogo.Hukuona shida kuwachanganya wale mabinti wote na mbaya zaidi kwako dhana ikawa shida kuitumia kwa huyu mtoto tegemezi wa Mzee Donyo.Sasa mimi sitaingilia masuala yenu,na ni bora palepale ungejitaja tu ili yaishe”.Kaka alizidi kunipa mawazo na kunifanya sasa kile kinyesi kugonga hodi kwenye boxer langu.
“Halafu wewe isitoshe ni mjinga sana tena sana.Mimi pale naheshimiana sana na yule mzee,ila kwa kuwa kwako ujana na maji ya moto,basi ukaamua kuwamwagia wengine.Sasa uaminifu kati ya mimi na mzee yule,hamna tena.Unadhani mimi kwa sasa nitahamia wapi?
Sijapanga kabisa kuhama muda huu.Embu fikiria dogo,kwa nini umenifanyia hivyo?”.Kaka sasa alibadilika na kuonesha wazi kuwa naye kachukia sana kitendo changu.Hakuishia hapo,akaendelea.
“Nyumba yangu ukaifanya nyumba ya ngono.Kitoto kidogo,miaka kumi na tisa.Kisheila,kinaingia ndani na kufanya unyambilisi na wewe.Eti mnajidai mmeoana wenyewe.Sasa kazi ni kwako.Mimi siingilii nakwambia”.Hadi kaka anamaliza kuongea hayo,mimi nilishalowa jasho kama nimtoka mazoezini.
“Na ninavyomjua mzee yule.Nadhani ukitoka hapo utakuwa umejifunza na umebadilika”.Kaka aliniambia hayo wakati gari linaingia pale kituoni.
Baada ya kuhakikisha nimepanda kwenye gari la wasafiri wa kwenda Morogoro,aliniaaga na kuniambia nisali sana.
***********
Baada ya dakika tano,gari lile lilianza kupiga honi likiashiria kuwa muda wake wa kuondoka umewadia.Mimi nilifumba macho na kumshukuru MUNGU kwani safari ilikuwa imeshaanza.
Tukatoka getini,na kuingia kwenye barabara tayari kwa safari ya kwenda Morogoro.

Amani ikanitawala kiasi chake baada kuona saa zima tunasafiri bila misukosuko.Usingizi ukanipitia kamanda na kuona kuwa tayari nimemaliza kazi.
************

Nilikuja kushtuka ghafla baada ya gari kupiga breki kali zilizofanya hata watu wengine mle kwenye basi kupiga kelele za hofu na hamaniko.
“Huyu dereva mshenzi nini.Anataka atuue wengine hapa?”.Aliongea mama mmoja mwenye mimba baada ya breki ile.

Unataka niwe nakutumia stori kama hizi na kila nyingine inayonifikia? jiunge na familia ya 2jiachie.com kwenye  facebook hapa LIKE PAGE YETU HAPA ==> 2JIACHIE


 Chombezo linazidikunoga hakikisha haikupiti hata siku moja.

 :: Endelea ku LIKE PAGE YETU na ku COMMENT chombezo hili kali na lakusisimua.

:: Kwa wale watakaokuwa waki SHARE 100 wa kwanza nitawapa kipaumbele kwa kuwa TAG chombezo hili kila litakapokuwa likitoka litakuwa katika wall yao



MPANGAJI sehemu ya 21 itaendelea tena kesho HAPA.

JANGA LA MAFURIKO: DAR SI SALAMA

$
0
0

ALFAJIRI ya Alhamisi ya wiki iliyopita haitasahaulika kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na viunga vyake ambapo maafa makubwa yalipoanza kufuatia mafuriko ya mvua zilizonyesha mfululizo na kusababisha vifo na uharibifu wa mali hivyo kuonesha wazi kuwa, kumbe Dar si salama.
 Daraja linalounganisha wilaya ya Bagamoyo na Mkoa wa Dar es Salaam likiwa limekatika baada ya mvua kubwa kunyesha.
Idadi ya vifo iliyoripotiwa mpaka juzi jioni ni kumi na mbili huku wanachi wengi wakikosa makazi na wengine kupotea kwa kusombwa na mafuriko.
UWAZI MZIGONI
Timu ya Uwazi ilizunguka sehemu tofauti za jiji zilizozizima na kushuhudia maafa hayo.
Tukio la kwanza ni kuonekana laivu kwa maiti ya mtu mmoja aliyezolewa na maji maeneo ya Jangwani wilayani Ilala.Mbali na kushuhudia uharibifu wa kutisha wa miundombinu na mateso ya watu walioathirika.
Helkopta ya Jeshi la Wananchi iliyokuwa imebeba viongozi wa serikali ikiwa imeanguka baada ya kupoteza mwelekeo.
BARABARA ZAFUNGWA, MADARAJA YAZOLEWA
Uwazi lilishuhudia baadhi ya barabara zikiwa zimefungwa kufuatia kujaa maji na madaraja kuvunjika na mengine kuzolewa. Barabara zilizofungwa ni pamoja na Dar es Salaam – Pwani kwa daraja la Mto Mpiji kubomoka.
Pia Barabara ya Dar- Kibiti ilifungwa na kufanya magari ya kwenda Kusini kutofanya safari kwa siku ya Jumapili iliyopita.
Daraja la Mto Ruvu lilifungwa kutokana na  maji kupita juu ya daraja hivyo kufanya usafiri wa kutoka Dar kwenda mikoani kuwa mgumu sanjari na kuingia jijini Dar.
MADARAJA YAFUNIKWA
Ndani ya Jiji la Dar madaraja mengi yalijaa maji ikiwa ni pamoja la Kinyerezi, Mlalakua, Mpiji Magoe kwenda Kidimu, Mbezi Mwisho, Msewe Kimara, Kijichi na Jangwani.
WAKAZI WAKOSA PA KUKAA
Baadhi ya maeneo ya jiji hasa Kigogo, Mwananyamala, Jangwani, Tandale, Mabibo na Tabata yalikumbwa na kadhia ya maji kujaa kwenye makazi ya watu na kusababisha wakazi wake kukaa kwenye mapaa kusubiri kuokolewa.
WAZEE, WATOTO, WANAWAKE WAKATI MGUMU
Makundi yaliyoonekana kupata wakati mgumu kwa mafuriko hayo ni wazee, wanawake na watoto waliokuwa wakishindwa kupanda juu ya mapaa ya nyumba, hivyo kusimama kwa kubebana kwenye maji kwa muda mrefu, waliopata bahati waliokolewa na watu wenye nguvu wakiwemo vijana.
MAITI, MAJERUHI WAKIMBIZWA HOSPITALI
Uwazi lilishuhudia miili ikipelekwa Hospitali ya Taifa Mubimbili kwa hifadhi huku ikiwa na dalili ya kuharibika.
Idadi kubwa ya majeruhi ambao hali zao zilikuwa mbaya walikimbizwa katika Hospitali za Amana, Mwananyamala na Temeke.
MAENEO HATARI ZAIDI
Maeneo mengi jijini yameathirika, lakini ambayo hayako salama kabisa ni mabondeni kama Jangwani, Kigogo Sambusa, Tabata ya Matumbi, Mikocheni na Msasani.
KOVA, MKUU WA MKOA WAPATA AJALI
Jumapili asubuhi, Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik walipata ajali ya chopa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ‘JNIA’ walipokuwa wakijiandaa kwenda kutembelea sehemu zenye mafuriko.
 
DAR SI SALAMA
Imebainika kuwa, miundombinu ya maji jijini Dar ndiyo sababu ya kutokea kwa mafuriko makubwa kwa vile maji hukosa njia ya kupita na kutengeneza visiwa vidogovidogo kila mahali.
“Kama mnavyoona Dar si salama, iko siku jiji lote litafunikwa na maji. Mvua kidogo mafuriko, watu wanakufa. Yaani vifovifo njenje,” alisema mkazi mmoja wa Mwananyamala Kisiwani baada ya kunusurika na mafuriko.
WATAALAM WANENA
Wataalam mbalimbali wa masuala ya mabadiliko ya tabianchi wamebainisha kasoro kubwa katika mipango miji nchini kwamba haizingatii madhara yatokanayo na mabadiliko ya hali ya hewa na kuruhusu ujenzi holela mabondeni, milimani na kwenye mikondo ya maji, ikiwemo mifereji.
“Hatua ya kuruhusu makazi kwenye maeneo ya mabondeni na kwenye mapito ya maji huzuia mikondo ya maji hivyo mvua zinaponyesha maji yake hulazimisha njia na matokeo yake ni mafuriko yenye madhara makubwa kwa maisha ya watu na mali zao,” alisema mtaalam mmoja kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ‘TMA’ huku akiomba hifadhi ya jina lake.
SERIKALI KUENDELEA KUGHARAMIA MADARAJA
Kwa mujibu wa mtaalam huyo, ujenzi wa barabara na madaraja nchini pia hauzingatii suala la mabadiliko ya tabianchi ambalo ni ajenda kuu kwa sasa duniani na ndiyo maana mvua nyingi Tanzania hubomoa madaraja na barabara na kuigharimu serikali mabilioni ya fedha kwa ajili ya ukarabati.
CREDIT: GPL/GAZETI LA UWAZI

TUNDU LISSU ATIKISA BUNGE

$
0
0
Dodoma/Dar.
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu amesema Tanganyika ilikufa kwa amri iliyotolewa na Mwalimu Julius Nyerere na siyo kwa makubaliano katika hati ya Muungano.
Lissu alitoa kauli hiyo jana alipopata fursa ya kukamilisha dakika 16 za hotuba yake ya ufafanuzi wa maoni ya walio wachache iliyokuwa imekatishwa baada ya matangazo ya moja kwa moja ya Televisheni ya Taifa (TBC1) kukatika Jumamosi iliyopita.

Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu.
Huku akinukuu maneno yaliyopo katika vitabu vilivyoandikwa na Profesa Issa Shivji na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa, Lissu alisema Jamhuri ya Muungano ilizaliwa bila uhalali wa kisheria kwa kuwa hayakuwapo makubaliano ya kila upande wa Muungano.
Alisema Aprili 26, 1964 (Siku ya Muungano), Mwalimu Nyerere alitoa amri ya masharti ya mpito ya mwaka 1964 ambayo pamoja na mambo mengine iliifuta Tanganyika. Akichambua kitabu cha ‘50 Years of Independence: A Concise Political History of Tanzania’ (Miaka 50 ya Uhuru: Historia fupi ya Tanzania), kilichoandikwa na Msekwa na kuchapishwa Januari mwaka huu, Lissu alisema:

“Msekwa anasema katika kitabu hicho kuwa amri hiyo ilichapishwa katika Gazeti la Serikali la siku hiyo. Kwanza, iliwabadilisha waliokuwa watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika kuwa watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.”
Alisema hata Mahakama Kuu ya Tanganyika iligeuzwa kuwa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano na nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Tanganyika iligeuzwa kuwa nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano.

Alisema tarehe hiyohiyo, Mwalimu Nyerere alitoa amri ya Katiba ya muda ya mwaka 1964 na ilitangaza kuwa Katiba ya Tanganyika ndiyo iwe Katiba ya muda ya Jamhuri ya Muungano.
“Kifungu cha nne cha amri hii ndicho kilichoipatia Serikali ya Muungano majukumu kuhusu mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano yote na vilevile kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano kwa upande wa Tanganyika,” alisema Lissu huku akishangiliwa na baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo.

Alisema Juni 15, 1964, Mwalimu Nyerere alitoa amri nyingine iliyoitwa ‘Amri ya Masharti ya Mpito’ ambayo ilieleza kwamba mahali popote ambako sheria zilizokuwapo zimetaja jina la ‘Tanganyika’ basi jina hilo lifutwe na badala yake jina la ‘Jamhuri ya Muungano’ liwekwe.
Huku akimnukuu Msekwa, Lissu alisema kigogo huyo wa CCM katika kitabu chake amesema, “Uhai wa Tanganyika ulitolewa kwa njia hiyo ya amri. Athari za jumla za amri hizi ni kwamba eneo la kisiasa ambalo ndiyo ilikuwa Tanganyika lilitolewa uhai wake moja kwa moja kwa amri. Hii ndiyo sababu hata jina la eneo la kijiografia lililojulikana zamani kama Tanganyika ilibidi libadilishwe na kuwa Tanzania Bara.”

Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Lissu aliyoitoa jana, Msekwa alisema: “Kitabu kipo na ukikisoma kwa umakini utagundua kuwa alichokisema Lissu siyo ambacho kimeandikwa. Sasa umhoji kuhusu hayo aliyoyasema, muulize ameyapata wapi?”
Kuhusu Shivji

Akimnukuu Profesa Shivji katika kitabu chake ‘Pan Africanism or Pragmatism? Lessons of Tanganyika – Zanzibar Union’, Lissu alisema Profesa huyo ameeleza kuwa Muungano huo ulilazimishwa.

“Profesa Shivji amethibitisha kwamba kile kinachoitwa Sheria ya Kuthibitisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ya mwaka 1964 iliandaliwa na kuandikwa na maofisa wa sheria wa Tanganyika wakiwa Tanganyika,” alisema.

Alisema kuwa Profesa huyo ameeleza sababu ya ukweli wa kisiasa uliokuwapo wakati huo ambao Baraza la Mapinduzi kwa jumla wake halikukaa kuukubali Muungano.
“Profesa Shivji alisema hakuna shaka kwamba Muungano ‘ulilazimishwa.’ Hivyo, maofisa wa kisheria wa kigeni wa Serikali ya Tanganyika (waliokuwa pia marafiki wa Nyerere) walitumia mbinu ya kisheria ya kuchapisha Sheria ya kuthibitisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, mwaka 1964,” alisema huku akikatishwa mara kwa mara na wajumbe waliokuwa wakiomba miongozo ya mwenyekiti.

“Profesa ameeleza kuwa, kwa sababu utaratibu huo ulikiukwa, kitendo cha kuunganisha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika hakikupata baraka za Baraza la Mapinduzi na kuthibitishwa na kikao halali cha Baraza la Mawaziri la Zanzibar,” alisema Lissu na kuongeza: “Jamhuri ya Muungano ilizaliwa bila uhalali wowote wa kisheria kwa maneno ya Profesa Shivji.”
Alisema hata aliyekuwa Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Salim Said Rashid kati ya Januari 18 na Juni 1964, alitamka kuwa:

“Hakuwahi kupokea maagizo kutoka kwa Rais wa Zanzibar kwa ajili ya kuitisha kikao cha kujadili na kupitisha mkataba wa kuunganisha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika,” alisema Lissu.
Alisema katika kitabu hicho, Profesa Shivji alieleza jinsi Rashid alivyoeleza utaratibu wa kisheria uliotakiwa kufuatwa: “... Kwa mujibu wa amri ya mwaka 1964; kila jambo lilitakiwa kujadiliwa na kikao cha Baraza la Mapinduzi na Mwanasheria Mkuu kuarifiwa atayarishe ‘presidential decree’ kwa mujibu wa utaratibu.”
Alisema baadaye yeye (Rashid), akiwa Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Baraza la Mawaziri Zanzibar alitakiwa asaini na kisha Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na baadaye kutolewa katika gazeti la Serikali.
Alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa kauli hiyo ya Lissu kuhusu kitabu chake, Profesa Shivji alijibu kwa ujumbe mfupi wa maneno akisema: “Itakuwa vizuri ukisoma wewe mwenyewe.”
Mbowe: Takwimu za Tume zimetengenezwa na vigogo wa Serikali
Akichangia maoni ya walio wachache kutoka Kamati Namba Nane, Freeman Mbowe alisema kitendo cha wajumbe wanaotokana na CCM kubeza takwimu za Tume ya Jaji Joseph Warioba ni kuwakana Watumishi wa Serikali akisema ilikuwa na watumishi wa Serikali 190 wakiwamo wanasheria waandamizi.

“Tunapohukumu Tume imefanya kazi chafu ya kuchakachua takwimu hizi, mjue zimetengenezwa na watumishi waandamizi kutoka Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Zanzibar. Kwa hiyo wanaobeza taarifa ya Tume, wajue wanaikana Serikali, wanawakana watu ambao wana dhamana ya kusimamia nchi hii,” alisema na kuongeza:
“Tunapata wapi ujasiri wa kuwadhalilisha wajumbe wa Tume ya Rais iliyoongozwa na Warioba?... Tume iliyojaa viongozi walioitumikia nchi hii kwa uaminifu mkubwa, tunafanyaje jambo hili?”
Mbowe alisema Jaji Warioba aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za juu ikiwamo Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais na kuhoji wajumbe wanapataje ujasiri wa kuwadhalilisha. Aliwataja wajumbe wengine wa tume hiyo wanaoheshimika kuwa ni pamoja na Jaji Mkuu mstaafu, Agustino Ramadhan na Waziri Mkuu mstaafu, Dk Salim Ahmed Salim.
Mbowe pia alishangaa kiwango cha fedha kilichotumiwa na tume hiyo Sh68.88 bilioni kufanya utafiti ambao leo wajumbe walio wengi kutoka CCM wanaukana.
Alisema endapo wajumbe wanapuuza msingi wa Rasimu iliyotokana na Tume ya Jaji Warioba, ni vyema Bunge hilo lisiwepo ili CCM wakae upya na kutengeneza rasimu wanayoitaka ya serikali mbili. Alisema Tanzania haiwezi kupata Katiba Mpya kwa uongo na rushwa na kuzuia watu kujadili kasoro za muungano kwa uhalisia wake.
Jussa awabana mawaziri SMZ
Akitoa ufafanuzi kuhusu maoni ya wajumbe walio wachache wa Kamati Namba Sita, Ismail Jussa aliwabana mawaziri watatu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kwa kushindwa kueleza udhaifu wa muundo wa serikali mbili bungeni wakati kwenye semina ya Baraza la Wawakilishi kuhusu mchakato wa katiba walisema hivyo wazi.
Alisema mawaziri hao walilalamikia jinsi wanavyodhalilishwa na muundo wa serikali mbili wanapokwenda nje ya nchi.
“Kuna rekodi hata ya CD, siyo ya Hansard tu (kumbukumbu rasmi za Bunge), hata ukiitaka mheshimiwa mwenyekiti nitakupatia. Haya yalikuwa katika semina ya Baraza la Wawakilishi iliyoitishwa na Spika wetu, Mzee Pandu Ameir Kificho,” alisema.
Aliwataja mawaziri hao kuwa ni Dk Mwinyi Haji Makame, Haroun Ally Seleman na Omary Yusuf Mzee. “Walichofanywa Dodoma sijui mheshimiwa mwenyekiti, lakini wote pamoja na wengine walionyesha jinsi mfumo huu (serikali mbili) hautusaidii Zanzibar na umetukwamisha,” alisema.
Alitoa mfano mwingine kuwa kuna siku Zanzibar walikuwa wakijadili muswada wa utalii ambapo yeye alipendekeza waweke kipaumbele cha ajira kwa Wazanzibari kwa kuwa wizara hiyo si ya Muungano na kilikataliwa.
“Mimi na Asha Bakari tu wa CCM tulitoka nje na akalalamika kuwa wenzake wamemgeuka. Kwa tabia hii mheshimiwa mwenyekiti tunapokuwa Zanzibar, tunasema wengine tunapokuja Dodoma tunaufyata, Wazanzibari watatuhukumu,” alisema.

Awali akisoma maoni ya walio wengi, Mwenyekiti wa Kamati Namba Sita, Stephen Wassira alisema walio wengi walipendekeza muundo wa serikali mbili kwa sababu unatoa fursa kubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kwa pande zote mbili na kuondoa tabaka la ukabila na udini ndani ya Jamhuri.
“Mfumo wa serikali mbili ukifanyiwa marekebisho ya kikatiba utaondoa kero na manung’uniko ambayo yameelezwa kuwa msingi wa mapendekezo ya Tume ya kutaka mfumo wa serikali tatu,” alisema.
CREDIT: MWANANCHI

HII NDO HATI YA MUUNGANO..PICHA ZIKO HAPA

AZIZA WA FACEBOOK SEHEMU YA O3

$
0
0
Na Nyemo Chilongani.
ILIPOISHIA
MIMI: Yeah! Ni rafiki yangu ila kila kitu kinatakiwa kufanywa kimahesabu.
EDUADO: Usiniangushe basi Sharukh Khan.
MIMI: Hilo usijali.
 
Katika kipindi hicho nilikuwa nafikiria mambo mengi sana, huyu mtoto kwangu alionekana kuwa na pozi ajabu, yaani nilikuwa nikizipitia post za kizushi alizokuwa akiziweka, watu walikuwa wakicomment halafu yeye hatokei. Hata kama kaweka picha ya mdoli, watu walikuwa wakicomment halafu yeye hatokei na mbaya zaidi kulikuwa na watu wengi wanaolike na kucomment jambo lililonifanya kugundua kwamba kuna siku huyu msichana alikwishawahi kuweka picha na hivyo wanaume kujua ni mzuri na kisha kuzitoa.
Bado kiu yangu ilikuwa ni kuwasiliana na Aziza tu ambaye alionekana kuwa mtu wa mapozi sana. Sikujua ningeanzia wapi ila nilichokifanya ni kuanza kumtumia meseji nione kama angeijibu au kuipotezea.
MIMI: Mambo!
Niliituma meseji hiyo, siku ya kwanza, ya pili, ya tatu mpaka wiki hadi mwezi lakini meseji ile moja haikujibiwa, mbaya zaidi nilikuwa namuona yupo hewani. Sikukoma kidume mimi, bado nilikuwa nikimtumia meseji za kumsalimia lakini hali ilikuwa vile vile, hakujibu.
Mtu mzima nikaona naumbuka, kama nilikuwa naitwa Sharukh Khan basi ilibidi niwaonyeshe watu kwamba hawakukosea kuniita jina hilo, nilitaka kuwaonyeshea dhahiri kwamba mama yangu alikuwa mtu wa Tanga, kule ambapo mapenzi yalikuwa yamenogeshwa kwa kuwekewa makorokocho. Nilichoanza kukifanya ni kuanza kumtag picha. Hapa ni lazima ugundue, picha ambazo nilikuwa nikimtag ni zile ambazo zilikuwa na muonekano wa kimapenzi tu. Picha ambazo zilikuwa zikiwaonyesha wapenzi wakibusiana na kukumbatiana, ndizo ambazo nilikuwa nikimtag, tena yeye peke yake.
Hahaha! Ule ukaonekana kama ujinga vile kumbe kwa wakati huo nilikuwa na target zangu kichwani. Niliendelea na mtindo ule ule mpaka siku ambayo akaonekana kuchoka na kukasirika, kwa mara ya kwanza akaja inbox, ila sio kiamani kama nilivyotaka, alikuja kibifu.

AZIZA: Naomba usiwe unanitag mapicha yako.

Niliisoma meseji ile. Kwanza nikacheka, kilichonifanya kucheka ni kwa kumuona kwamba alikuwa msichana mjinga sana, kitendo cha yeye kuniandikia meseji kilionekana kuwa kama kosa kubwa sana, nilichokifanya, nikaanza kuandika meseji ndefu, meseji ambayo ingemfanya kunijibu, meseji ambayo isingemfanya kubaki kimya.

MIMI: Kuna vitu kadhaa Aziza itakupasa uelewe na ninatumaini vitakuongoza katika maisha yako yote. Jitahidi kuishi lakini kamwe usiwe mbinafsi. Unapopata kitu, usitake kukaa nacho, jaribu kuchangia pamoja na wenzako. Unapopata chakula, jaribu kumwangalia yule asiye na chakula na kumgawia, milele atakushukuru kwa ulichomfanyia siku moja tu alipokuwa na njaa. Unapomuona mtu hana nguo, mgawie nguo na ataendelea kukushukuru maisha yake yote. Unaniona mimi, mimi si mbinafsi hata mara moja, katika maisha yangu nimekuwa nikiwapa watu vitu fulani vitu ambavyo hawana katika maisha yao, nikakuangalia wewe, nikakuona kwamba u masikini sana, ukijiangalia, unajiona kuwa tajiri, mwenye fedha labda, lakini bado ni masikini, masikini wa kitu kimoja ambacho ulihitaji mtu mwenye kitu hicho akusaidie, nikakusaidia lakini unaonekana kuukataa msaada wangu. Kuwa makini Aziza, mara nyingine msaada huja mara moja na kupotea, unapoutafuta, inawezekana usiuone tena.


Kwanza nikashusha pumzi nzito, nikaiangalia meseji ile na kisha kuirudia rudia mara nyingi nyingi na kisha kuituma. Niliiona kuwa meseji kali ambayo isingemfanya kubaki kimya kwa kutaka kujua ni kitu gani ambacho alikuwa amekosa katika maisha yake, kilichonifurahisha, akatuma meseji. Kuna nini tena? Meseji ya pili hiyo, hakujua kwamba ndio mwanzo wa chating yetu.

AZIZA: Umemaanisha nini?
MIMI: Nimemaanisha kwamba wewe ni masikini. Tena yule fukara kabisa. Hiyo ndio maana yangu.
AZIZA: Sijakuelewa.
MIMI: Hebu isome vizuri hiyo meseji, utaielewa tu.
AZIZA: Nimeirudia zaidi ya mara tano, sijaielewa, naomba uniambie umemaanisha nini.
MIMI: Nikuulize kitu kimoja?
AZIZA: Niulize.
MIMI: Unaweza kugundua ni umasikini wa aina gani umekuwa nao?
AZIZA: Hapana na ndio maana nikauliza.
MIMI: Inawezekana ukawa na magari, nyumba na fedha ila bado ukawa masikini, unakubaliana nami?
AZIZA: Hapana.
MIMI: Kwa sababu gani?
AZIZA: Mtu ana kila kitu, atakuwaje masikini.
MIMI: Hahahah! Aziza. Ukisema hivyo unakosea. Kuwa na kila kitu haimaanishi kwamba wewe si masikini. Unaniruhusu nikuulize kitu?
AZIZA: Niulize
MIMI: Unaamini katika fedha?
AZIZA: Yeah!
MIMI: Fedha inaweza kukupa kila ukitakacho?
AZIZA: Yeah!
MIMI: Unakosea sana Aziza.
AZIZA: Unapokuwa na fedha unanunua gari ulitakalo, unanunua chakula, unanunua nyumba na mambo mengine. Kwani nimekosea?
MIMI: Umepatia. Ila unavyoona kila mtu mwenye fedha huwa na furaha?
AZIZA: Inawezekana.
MIMI: Umekosea. Umekwishawahi kuwasikia wale matajiri wanaojiua?
AZIZA: Yeah!
MMI: Sasa wamekosa nini wale katika maisha yao? Wana fedha, wanaweza kununua kila kitu, wana magari, wanaweza kwenda sehemu yoyote ile. Ila swali linakuja kwa sababu gani wanajiua?
AZIZA: Mmmh! Sijui.
MIMI: Hahaha! Jibu rahisi sana. Walikosa furaha, amani, wakakosa mapenzi na mambo mengine. Unapokuwa na fedha, utanunua gari ila kumbuka hautoweza kununua furaha, unapokuwa na fedha utaweza kumnunua msichana mtaani lakini ukashindwa kununua mapenzi. Umenipata hapo?
AZIZA: Kidogoooo.
MIMI: Yeah! Kila mtu hunipata kidogo, ila tukiendelea kuchati, utanipata sana tu. Utaniruhusu niwe nachati nawe kwa ajili ya kukuambia mengi usiyoyajua?
AZIZA: Yeah! Ila huwa siwi hewani muda wote.
MIMI: Hilo si tatizo. Unachotakiwa ni kunishtua kila unapokuwa hewani. Utakwenda kufahamu mengi ambayo haujayajua. Kwani unaishi wapi?
AZIZA: Nipo Masaki Dar es Salaam.
MIMI: Ndio maana.
AZIZA: Kwa nini?
MIMI: Usijali. Mtaa unaokaa ndio nitakaoanza nao siku tukianza kuchati. Kwa sasa nahitaji kusoma, naomba uniruhusu niondoke.
AZIZA: Ila pleeeaseeee naomba uniambie.
MIMI: Sijakataa. Nitakwambia tu wala usijali. Wewe ni rafiki yangu, pamoja kuwa na kila kitu, yakupasa kupata vitu vingine ambavyo haupaswi kuvinunua. Nitakwambia namna ya kuvipata na inawezekana hata marafiki zako wakakushangaa.
AZIZA: Mmmh!
MIMI: Usigune. Huo ndio ukweli. Usiku mwema Aziza.
AZIZA: Nawe pia.

Kuna nini tena? Nilichokifanya ni kutoka hewani mpaka saa sita ndio nikaingia tena, Aziza hakuwepo, nikamtafuta Eduado, nikamuona, hata kabla sijamtumia meseji, akaniwahi.
EDUADO: Vipi Sharukh Khan. Imekuwaje au bado?
MIMI: Kwisha habari yake. Anacheza na mwanasaikolojia nini.
EDUADO: Imekuwaje tena?
MIMI: Wewe usijali. Cha msingi andaa zawadi yangu.
EDUADO: Umeanza kufanikisha?
MIMI: Ndio maana yake. Unajua ukimjua mpinzani inakuwa rahisi sana.
EDUADO: Dah! Wewe noma kaka. Yaani hii kazi nimewapa watu saba, naona wengine wanambwela tu, wananiambia kila wakimtumia meseji dogo hajibu.
MIMI: Hahahaha! Hata mimi ilikuwa hivyo hivyo. Nilivyoona anashindwa kujibu, nikatumia plan B. Hapo ndipo nilipompoteza na kuchati nae sana.
EDUADO: Kwa hiyo ulichati nae?
MIMI: Yeah! Tena mimi ndiye nimemkatisha. Chezea mimi wewe.
EDUADO: Hahahah! Ebwana wewe nomaaaaa....sasa hata kukutambulisha kwa mrembo wangu mwingine naogopa.
MIMI: Wewe si ulinipa kazi kaka? Hakuna tatizo. Kazi inafanyika taratibu.
EDUADO: Duh! Kaka nashukuru sana kwa kunisikiliza. Natumaini mtoto ataeleweka tu.
MIMI: Amekwishaeleweka. Dogo amekwishaeleweka.
EDUADO: Hahahah! Basi poa sana, nimefurahi sana.
MIMI: Usijali kaka...hug.
EDUADO: Poa.

Kila kitu kikaonekana kuwa juu ya mstari, meseji moja ambayo alikuwa amenitumia ikaonekana kubadilisha kila kitu. Ile meseji ndio ambayo nilikuwa nikiitaka kuiona na kweli aliituma. Chatting zikawa zimeanza, kwa Aziza, nilihitajika kuwa makini sana kupita kawaida kwani kwa kufanya vile nilikuwa na uhakika wa kumchukua ili kumuonyeshea Eduado kwamba nilikuwa Sharukh Khan.
                                                          ****
   Sikutaka kuleta shobo tena kwani tayari nilimuona kuku kuwa wangu kwa hiyo sikutakiwa kumshikia manati kwa kuamini kwamba jioni ikifika mwenyewe atarudi bandani. Nilipoingia hewani siku iliyofuatia, msichana Aziza alikuwepo, kajaa tele ila mtu mzima nikaamua kuchuna. Katika hili ngoja nikwambie kitu kimoja rafiki yangu hasa mwanaume kama mimi. Unapoona kwamba kuna msichana fulani unampigia sana misele facebook, hautakiwi kila wakati umuanze wewe tu, sometimes unamchunia uone je ataweza kukutumia meseji au la. Ukiona kwamba kakutumia, basi jua kwamba anautambua mchango wako na hata kwenye ile mishemishe yako anaonekana kuifurahia. Ila ukiona nae anakaa kimya, mtu mzima poteza kwani si unajua warembo wapo wengi! Inawezekana haujapangiwa kuwa na huyo.
   Nilipomuona Aziza hewani, nikamchunia kana kwamba sijamuona huku nikiamini kwamba yeye ndiye alipaswa kunitumia meseji. Ila katika kipindi hiki hasa siku ya leo, meseji zilikuwa zikiingia nyingi nyingi hasa kutoka kwa marafiki zangu wengine, bahati nzuri nilikuwa natumia kompyuta hivyo ilikuwa rahisi kuwajibu.

IBRA: Mambo vipi kaka!
MIMI: Poa. Ni aje mkuu?
IBRA: Kama kawa. Upo wapi?
MIMI: Nipo gheto aiseee nimesizi tu si unajua kijimvua nje kinazingua.
IBRA: Yeah! Hilo kweli kaka. Hivi unamuona mtu wangu hapo hewani?
MIMI: Nani?
IBRA: Tina.
MIMI: Dah! Hapa namuona kwa kuotea, mara anakuja mara anatoka. Kama vipi mcheki kwa whatsapp.
IBRA: Kwani yupo huko?
MIMI: Yeah!
IBRA: Dah! Basi nafikiri kule atakuwa kaniblock mtu mzima. Simuoni kabisa.
MIMI: Hahahah! Kaka pole sana. Umeblockiwa...hahaha! Tatizo lako uliremba sana kwa kujifanya umeoa, full mauhakika.
IBRA: Unajua nini kaka, kila siku naamini kwamba mwenda pole ndiye mla nyama.
MIMI: Usitake kuniambia hivyo. Wahenga wengine walikuwa wakizingua tu, kidogo naweza kumuamini yule aliyesema chelewa chelewa utakuta mwana si wako. Si kwamba unamuona kinyonga anatembea taratibu ukajua hata yeye anajua kwamba anatembea taratibu, mwenzako pale anajiona anakimbia kwa kasi sana. Hahahaha! Na bado...atakublock mpaka whatsapp.
IBRA: Akiniblock na huko tena, nitamuona katili sana kaka.

Huku nikiendelea kupiga stori na Ibra, mara Emmanuel Solo nae akaingia kwa inbox yangu. Sikuwa na jinsi, nilikuwa nachati nao huku nikimuona Aziza hewani ila nami nilikuwa nimemlia pini tu.

SOLO: Kaka.
MIMI: Niambie.
SOLO Upo wapi?
MIMI: Nipo gheto. Wewe upo wapi?
SOLO: Nipo Morogoro kama kawaida yangu.
MIMI: Duh! Wewe noma. Ndani ya wiki moja umetembea mikoa mitatu. Big Up mkuu.
SOLO: Kutafuta kaka. Maisha kutafuta. Si unamuona hata Ndimanga Hassan, anatembea zaidi ya mikoa kumi kwa mwezi, hatutakiwi kukaa sehemu moja. Hadithi imeishia wapi?
MIMI: Ipi? Zipo nyingi tu.
SOLO: Ile ya yule msichana mwimbaji wa kwaya aliyekuwa amepanga mauaji kwa mvulana ambaye alikuwa amemkataa kanisani na kuamua kutaka kumuua nchini Zambia.
MIMI: Bila shaka unaizungumzia HER HIDDEN FACE, si ndio?
SOLO: Yeah! 

ITAENDELEA SIKU YA KESHO

Unataka niwe nakutumia stori kama hizi na kila nyingine inayonifikia? jiunge na familia ya 2jiachie.com kwenye  facebook hapa LIKE PAGE YETU HAPA ==> 2JIACHIE

SAFARI YA MWISHO ZA MAREHEMU MUHIDIN GURUMO

RAY: SINA MPANGO WA KUMUOA CHUCHU

$
0
0
Makubwa! Kaka mkubwa kunako gemu la filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’ amefunguka kuwa hana mpango wa kumuoa mwanadada Chuchu Hans kama inavyodaiwa na baadhi ya watu.
Vincent Kigosi ‘Ray na Chuchu Hans wakiwa katika pozi.
Akijibu swali aliloulizwa na wanahabari wetu hivi karibuni, kuhusiana na kudaiwa kuwa baada ya mpenzi wake huyo kupewa talaka ana mpango wa kufunga naye ndoa kama ilivyokuwa inadaiwa ambapo alikataa katakata suala la yeye kufunga ndoa na Chuchu.
Diva wa filamu za Kibongo Chuchu Hans.
“Sina mpango wa kuoa ndugu yangu, hayo ni maneno ya watu ambayo yapo tu mitaani ila kwa sasa niko njiani naenda gym baadaye nitakutafuta tuongee.” alisema Ray.
 
Staa mkubwa kunako gemu la filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray The Greatest’.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa muigizaji huyo kufunguka kuhusiana na suala la ndoa na swali linakuja, je, Chuchu anafahamu kuwa anachezewa tu? Jibu analo mwenyewe moyoni mwake.
Ray na Chuchu katika pozi la mahaba.

VIDEO: MAZISHI YA MAALIM GURUMO KIJIJINI MASAKI, KISARAWE JANA

$
0
0
Mazishi ya Maalim Gurumo kijijini kwao Masaki, Kisarawe mkoani Pwani.

CHOMBEZO: MPANGAJI SEHEMU 22 ...MWISHO

$
0
0


Nilikuja kushtuka ghafla baada ya gari kupiga breki kali zilizofanya hata watu wengine mle kwenye basi kupiga kelele za hofu na hamaniko.
“Huyu dereva mshenzi nini.Anataka atuue wengine hapa?”.Aliongea mama mmoja mwenye mimba baada ya breki ile.


“Hamna mama.Kuna gari limekuja mbele ya basi letu na kumwomba dereva asimamishe na ndo maana imekuwa ghafla hivi”.Aliongea jamaa mmoja ambaye alikuwa amekaa dirishani.
Hadi hapo mimi nilihisi kama nataka kufa,lakini haikuwa hivyo.Nikatamani labda niwe ndotoni hivi,kisha nikafumba macho ili nione kama itakuwa ndoto.
Lakini nilipofumbua,nilisikia yule jamaa anasema kuna majamaa watatu pamoja na Mchungaji wameshuka na wanaongea na dereva.
Hapo sasa ndipo nilitaka hata kujitupa nje kupitia dirishani kisha nikimbie kwa nguvu zangu zote hadi sehemu ilipo salama.Lakini nilipoangalia nje,dah! Sijui hata tulikuwa wapi maana kulikuwa ni pori tupu.
Dakika kadhaa baadaye,niliona hao majamaa watatu wameingia mle ndani huku wamekamata picha mkononi.
Walipotua macho yao kwangu tu! Wala walikuwa hawana haja ya kuendelea hadi siti ya mwisho. Wakaja kwangu na kuniamuru ninyanyuke,nami nikatii. Wakataka nitoe na mizigo yangu yote.
Bila zengwe nikatii huku sasa lile tumbo la haja kubwa,likirudi katika hali ile ya mwanzo..
Baada ya kushusha mizigo yangu,waliniongoza moja kwa moja hadi kwenye Pajero waliyokuja nayo.Mizigo wakaitupia kwa nyuma,ma mimi wakaniweka kati huku Baba Sheila akiwa upande ule mwingine usawa wa dereva.
Safari ya kwenda nisipo-pajua ikaanza.
**********

ENJOY.
Hakuna aliyemsemesha mwenzake hadi pale tulipofika.
Kulikuwa kama ni kambi hivi ya jeshi au tuseme labda ya wakimbizi,au sijui niseme vipi.Kwani wapo waliokuwa wamekaa na wapo ambao walikuwa wanalinda usalama.
Baada ya kuingia pale ndani.Nikatolewa nje ya gari na moja kwa moja nikaanza kupelekwa kwenye jengo moja ambalo sifahamu hadi  leo lipo wapi na ni la nani.
Baba Sheila akiwa mbele,mimi na wale jamaa watatu tukiwa nyuma,tuliingia ndani ya jengo lile ambalo lilikuwa kama meli ya kivita hivi au nyambizi,zile meli za kivita zinazozamia kwenye bahari.
“Kijana umeingia sehemu mbaya sana.Heri ungeendelea na yule mwingine.Yule hata ungempa UKIMWI,kwangu si kitu.Alishanitoka moyoni.Ila huyu,aisee sikuachi”.Aliongea Baba Sheila baada ya kuingia chumba kimoja kilichokuwa na mitambo mingi-mingi,sijui hata ya nini.

Baada ya kuongea hayo,nilishtukia nguo zangu hasa tisheti ikivutwa kwa hasira na kuchanwa na wale jamaa.Kisha wakaja  kwenye jinzi langu nalo wakalivua kwa hasira.Nikabaki na kikaptula cha maua maua na singlend,ambavyo navyo vikanyofolewa pamoja na boxer langu la Man United.

Mzee  aliwaoneshea ishara wale jamaa kwa kidole.Na wao wakatii kwa kunipeleka sehemu moja ambayo ilikuwa kama ina senyenge.Wakanifunga pingu hapo kwa kunining’iniza huku mgongo wangu ukigusa zile senyenge.Baada ya hapo,wakaamuriwa waondoke wale jamaa.

Vya watu shida nyie.Mateso niliyopokea pale,nilisema nikitoka mzima,MUNGU atakuwa ngome yangu daima.Niliapa kuwa nitamrudia MUNGU na kuwa mfuasi wake.

Ile senyenge iliungwa kwenye umeme.Yaani pale wale jamaa walivyotoka,Baba Sheila alikuwa anabofya sehemu moja na kufungua kidude flani hivi kimeandikwa namba.Nadhani ni mita ya kupimia umeme.
Alipofungua kile kidude alisababisha zile senyenge kunipiga shoti mgongoni. Pale nilipolia,yeye alisema hata mwanangu atalia vivyo hivyo wakati anajifungua toto lako. Hapo alizidisha nguvu ya umeme na kuwa juu zaidi ya mara ya kwanza.
Kama haja kubwa na ndogo,zote zilitoka pale.Kilichofuata ni mimi kufumba macho nikigugumia kwa maumivu jambo lililiosababisha nipoteze fahamu.
************

Naweza kusema, kupoteza fahamu ilikuwa pona yangu  kwenye ule umeme.Lakini haikuwa pona ya mateso yangu.
Baridi isiyo kifani,ilikuwa imenishika hadi nikazinduka.Nilipoangalia,nilikuwa nipo sehemu moja kama swimming pool,lakini ndani yake kulikuwa na maji ya baridi hadi yanatoa mvuke.
Na kila baada ya dakika kumi,wanaweka barafu karibu ndoo sita za rita ishirini.Niliambiwa nitakesha humo kwenye baridi kama Sheila atakavyokesha na mimba yangu mtaani usiku na mchana akitafuta pa kujihifadhi.

Maswali mengi mengi nikajiuliza juu ya maneno yale.Kwanza nilijiuliza kwa nini Mzee yule alisema nitakesha kama Sheila atakavyokesha na mimba yangu mtaani.Ina maana Sheila katoroka kwao au huyu mzee kamfukuza aende huko mtaani.
Nilibaki na maswali hayo ambayo sikupata jibu lolote hadi leo.

Kama kupiga kelele za kuomba wanisamehe,nilizipiga sana.Na kama kulia nililia sana ili wanitoe mle kwenye swimming pool la mateso ya baridi.
Mwisho wa siku pumzi ilinikwisha baada ya muda mrefu wa mimi kukaa mle kwenye mibarafu.Miguu ikashindwa hata kusogea.Midomo ikabaki wazi na mikono nayo,ikakakamaa. Hapo napo niliona kama kuzimu kunaniita.
Wakanitoa kabla sijapoteza fahamu.Wakati huo ilikuwa mida ya saa mbili za usiku.

Nikapelekwa kwenye chumba kimoja ambacho mwanzoni nilihisi faraja kuingia mle.Kilikuwa kina joto balaa,lakini kwa kuwa nilikuwa nimeshikwa na baridi,niliona afadhari kuwemo mle.
Nusu saa mbele,nilianza kuona kero la joto lile.Na nilizidi kuona kero baada ya ubaridi ule kunitoka mwilini kabisa.Sasa jasho likavaa ngozi yangu,na kama kuwiva,sasa nilikuwa na wiva haswaa. Hapo spika za chumba kile nilisikia zikisema,eti navyojisikia joto lile, ndivyo na Sheila atakavyojisikia wakati jua litakapokuwa linamuishia mwilini kutafuta chakula.

 Mateso yalizidi kiwango,na kama kunyooka,nilinyooka sana kwa muda ule mchache.Nikazimia tena kamanda.
**********
Nilipozinduka ilikuwa ni asubuhi katika chumba kimoja kidogo sana.Ilikuwa ni faraja kwani hakikuwa na mateso kama ya jana yake.
Lakini baadae,walikuja jamaa wengine wawili na kuanza kunibana mbavu na zaidi waliporidhika na zoezi lile,wakachukua virungu fulani vya chuma na kuanza kunigonga kwenye ugoko na kwenye vile vinundu ambavyo ndivyo viungio vya miguu yangu .Hapo nilikuwa si mtu tena,bali mfu.Yale maumivu,kamwe siwezi kuyasahau na siyafananishi na maumivu yeyote katika maisha haya.
**********
Wiki nzima nilikaa nateswa pale,mateso ya kila aina,hadi kugalagazwa kwenye siafu. Na saa nyingine baada ya mateso wanakuletea mwanamke wanakwambia mpe mimba huyo,ukishindwa hata kusimamisha kichapo kinaendelea.Sikuweza zoezi lao hata moja,hivyo mateso kwangu yakawa ni kama chakula tu!.
Mwisho kabisa Mzee yule alisema anataka nisikie maumivu kama ambayo atayasikia mwanaye wakati anajifungua.Hapo alisema anataka amkate P wangu.
Daah! Kama kuomba msamaha ingekuwa ajira,mimi ningekuwa nalipwa mshahara mkubwa sana.
Niliomba msamaha hadi ulimi ukakosa mate nikabaki kukaa na kusubiri wafanye watakacho kwani nilikuwa sina uwezo wakukurupuka na kupambana nao.

“Sasa chagua moja.Tuchome haya mavyeti yako ya elimu uliyotafuta miaka sijui kumi na mbili au tukate huyo anayekupa kiburi”.Baba Shei aliniuliza.
Kwa wakati ule,vyeti vilikuwa si kitu.Ila hii kitu bwana muhimu.Niliwaomba wachome tu!Na bila kusita mbele ya macho yangu,nilishuhudia vyeti vikichomwa moto.

Mwisho kabisa,waliniminya sehemu ya shingoni ambayo ina mshipa mkubwa wa damu.Hapo nikapoteza fahamu.
*********
Nilipozinduka nilikuwa Morogoro tena nyumbani huku kaka yangu yule wa Arusha ikisemekana ndiye aliyenileta lakini aliondoka na kuacha ujumbe ulionipa pole lakini ukinitaka nisiwasiliane naye tena,yaani alikuwa kachukia.

Ni wiki moja lakini kwangu ilikuwa kama miaka.Sikuamini kama nimetoka salama.Nilimshukuru MUNGU japo ndugu yangu aliamua kunitenga.Najua ilikuwa ni hasira tu! Na mimi nimemsamehe kama alivyonisamehe.

Pale nyumbani,Stela na shangazi yake walikuwepo lakini Maimuna hakuwepo. Nilipomuulizia,walisema aliondoka baada ya kujigundua ana mimba,na mhusika nilikuwa ni mimi.Hawakusita kusema kuwa natafutwa sana baba yake.Hapo nikazidi pia kupagawa.

Mwezi ukakata na hali yangu ikatengamaa tayari kwa pirikapirika za maisha.
Hakuna aliyenijali kama hapo mwanzo.Kitendo nilichokionesha kwa kaka yangu kule Arusha,wengi kiliwagadhabisha hasa baada ya Mzee yule kumfukuza kaka nyumbani. Nashukuru kuwa mzee yule hakumdhuru kaka.Hiyo ni sababu kaka naye alikuwa ni mtu wa usalama kama mzee yule,fununu hizo nilizipata kwa baba yetu.

Huyo Stela alikuwa kabadilika sana.Tabia za umalaya ndo zikawa zake.Shangazi yake alisema kamshindwa. Mbaya zaidi akawa ananitaka kimapenzi na wakati mwenzake sina hamu tena na hiyo kitu.
**********
Nilitoka pale Morogoro na  moja kwa moja nikaenda Kondoa kwa Maimuna kwa kutumia ramani niliyopewa na Shangazi wa Stella.
Nilipofika nilipiga magoti na kuomba msamaha kwa wazazi wa Maimuna huku nikiahidi matunzo na kumchukua Maimuna baada ya mambo yangu kukaa vizuri.
Mimba yake ilikuwa tayari kubwa na kwa kuwa baba nilikuwa mimi,hawakuwa na kipingamizi.Msamaha ukapita.

Baadae niliamua kusomea udereva.Nilipomaliza nikatafuta reseni  ambayo ilinifanya niajiriwe kwenye kampuni moja ya usafirishaji ambayo hadi leo nipo huko.
Mambo yalipokaa vizuri,nilimchukua Maimuna na kuanza kuishi naye tukiwa na mtoto wetu mmoja.Lakini baadaye tuliongezewa mwingine na Sheila ambaye alimbwaga mtoto yule siku moja asubuhi sana.Aliacha ujumbe tu! Wa karatasi kuwa yeye ndiye kamleta mtoto yule.
********
Maisha yakawa hivyo. Miaka sasa imepita tangu mkasa huu utokee. Sasa hivi nina watoto watatu,lakini ile tabia,imenitokea puani.

Sasa nimeokoka,na maisha yangu nimemkabidhi MUNGU.Namshukuru Mai,japo alikuwa Muislam lakini alikubali kufunga ndoa ya bomani ambayo ndio hadi sasa inadumu.
**********

Naamini mmejifunza mengi katika kuridhishana kimapenzi,kujikinga na magonjwa,kuwaheshimu wale wanaojiuza na kuwaona kama hawakupenda kuwa vile.Pia nadhani umejifunza kuwa cha mtu mavi na siku za mwizi ni 40.Mateso niliyoyapata,siwezi kuyasahau.

Chungeni sana vijana.


MWISHO.

Asanteni kwa sapoti yenu.
Komenti chochote kuhusu hadithi hii,usisite kukosoa.


Unataka niwe nakutumia stori kama hizi na kila nyingine inayonifikia? jiunge na familia ya 2jiachie.com kwenye  facebook hapa LIKE PAGE YETU HAPA ==> 2JIACHIE


BIFU ZITO: LULU, JACKLINE WOLPER NA MISS TANZANIA 2012 WAGEUKA PAKA NA PANYA

$
0
0
E LIZABETH Michael ‘Lulu’ anayetesa katika filamu za Kibongo, yupo kwenye bifu zito na mshiriki wa Miss Tanzania mwaka 2012, Husna Maulid ambaye anadai amempora bwana’ke.
Habari zinaeleza bifu lao limefikia hatua ya

kuanikana waziwazi hadi kumwagiana matusi kwenye mitandao ya kijamii, hasa Instagram lakini huondoa majibizano yao machafu kila baada ya muda mfupi.

Chanzo cha habari hizi kinapasha kuwa ugomvi wa Lulu na Husna ni juu ya mwanaume huyo ambaye anaishi jijini Arusha aliyetajwa kwa jina moja la Seki anayeelezwa kuwa na pesa za kutosha kusumbua mjini. “Hao wanamgombea jamaa fulani wa Arusha, anaitwa Seki, ana mawe (pesa) mbaya.

Lakini wa kwanza kuwa na Seki ni Husna na Lulu alijua, sema Husna na huyo jamaa walikuwa wanagombana na kumwagana mara kwa mara. Sijui sasa nini kilimfanya Lulu kwenda kutembea tena na huyo jamaa wakati anajua ni wa shoga yake, labda ni baada ya kujua wamemwagana,” kilipasha chanzo hicho.Baada ya kupata habari hizi, mwandishi wetu aliwatafuta Lulu na Husna kwa ajili ya kuthibitisha madai hayo. Lulu alikuwa wa kwanza kupatikana ambapo alisema: “Jamani mimi simjui kabisa Husna Maulid wala hata katika fikra zangu hayupo... yaani kifupi simjui.”

Husna alipopatikana na kuelezwa mkanda mzima, kwanza alishangaa Lulu kutomjua, akasema: “Hakuna mtu asiyejua kuwa Lulu kanipora mwanaume wangu. Lakini anajifanya mjanja, tutaoneshana tu. Anajidai sana, anajifanya wa mjini hanijui mimi, lakini mimi ni wa mjini zaidi yake.”

AZIZA WA FACEBOOK SEHEMU YA O4

$
0
0
Na Nyemo Chilongani.
ILIPOISHIA
MIMI: Duh! Wewe noma. Ndani ya wiki moja umetembea mikoa mitatu. Big Up mkuu.

SOLO: Kutafuta kaka. Maisha kutafuta. Si unamuona hata Ndimanga Hassan, anatembea zaidi ya mikoa kumi kwa mwezi, hatutakiwi kukaa sehemu moja. Hadithi imeishia wapi?

MIMI: Ipi? Zipo nyingi tu.

SOLO: Ile ya yule msichana mwimbaji wa kwaya aliyekuwa amepanga mauaji kwa mvulana ambaye alikuwa amemkataa kanisani na kuamua kutaka kumuua nchini Zambia.

MIMI: Bila shaka unaizungumzia HER HIDDEN FACE, si ndio?

SOLO: Yeah!

MIMI: Ile ipo sehemu ya tano. Inaendelea kama kawa.

SOLO: Basi poa. Ngoja niitafute niendelee kuisoma.

EDUADO: Kaka
MIMI: Niambie kijana.
EDUADO: Mtoto leo kaja chuo aisee kapendezaje!
MIMI: Acha utani.
EDUADO: Sure. Mtoto ni noma kaka. Mtoto mrembo mpaka anajishangaa. Namuona hewani, ushatupia mambo?
MIMI: Hapana. Nangoja anianze, asiponianza nampotezea tu kwani si lazima kivile kuchati nae na kumshobokea.
EDUADO: Ila kaka fanya mambo bhana. Huyu mrembo sitaki umkose kabisa.
MIMI: Usijali kaka. Huyu mdogo mdogo mwisho wa siku utamkuta gheto kapumzika. Chezea Tandale wewe.
EDUADO: Hahaha!

AZIZA: Mambo!
MIMIl Mabaya.
AZIZA: Ubaya wake?
MIMI: Naumwa.
AZIZA: Nini tena jamani?
MIMI: Maralia. Yaani mbu mmoja tu jana chumbani kwangu ndio alisababisha majanga yote haya.
AZIZA: umekunywa dawa?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Kwa nini sasa jamani?
MIMI: Naogopa sana dawa Aziza. Labda uje uninyweshe kinguvu.
AZIZA: Dah! Pole sana Ibra. Nitakuombea kwa Mungu akuponye.
MIMI: Asante sana. Nitafurahi sana.
AZIZA: Aya nishakushtua. Hebu niambie kuhusu vitu ulivyokuwa ukiniambia.
MIMI: Tatizo lako unajiamini sana Aziza halafu unafanya makosa sana kila unapoona kwamba fedha ndio kila kitu. Yaani haujifikirii kama kuna watoto wa matajiri ambao wanaumwa sana mpaka wanakufa, kama fedha ni kila kitu si wangepona.
AZIZA: Nafahamu.
MIMI: Basi kama unafahamu, fahamu pia kuna kitu ambacho ni kila kitu na si fedha kama unavyofikiria.
AZIZA: Kipi tena.
MIMI: Mungu ndiye kila kitu katika maisha yetu. Bila Mungu, huwezi kuwa na furaha hata kama una fedha, bila Mungu huwezi kupona ugonjwa wako hata kama una fedha na kutibiwa na madaktari wakubwa duniani. Umenipata?
AZIZA: Ndio nimekupata.
MIMI: Au hadi hapo unataka kubishana tena?
AZIZA: Hapana. Ila unaonekana kuwa na hekima sana Ibra.
MIMI: Yeah! Unajua wakati mwingine yatupasa kuutambua ukweli. Hatutakiwi kuamini sana katika fedha. Ila achana na hayo. Wewe ni mama wa nyumbani, mwanafunzi wa sekondari au mwanafunzi wa chuo?
AZIZA: Naonekaje?
MIMI: Profile picha yako ni ya mdoli, sasa nitajua unaonekanaje?
AZIZA: Hahaha! Usijali. Mimi ni mwanachuo.
MIMI: Unasoma wapi?
AZIZA: Mlimani
MIMI: Unasomea nini?
AZIZA: Sheria.
MIMI: Afadhali.
AZIZA: Afadhali ya nini tena?
MIMI: Uje kuwa mwanasheria wangu baadae katika kampuni yangu.
AZIZA: Hahahah! Utaweza kunilipa?
MIMI: Kwa nini nisiweze? Nitakuwa na fedha mbayaaaaaaa....nitamiliki magari ya kifahari na majumba makubwa sana....lol
AZIZA: Yote ni mipango ya Mungu ila napenda ulivyoongea kwa sababu unaonekana una imani ya kupata hivyo, cha msingi yakupasa kujituma tu na kumtanguliza Allah kwa kila kitu. Naomba nikuulize swali.
MIMI: Usijali. Uliza.
AZIZA: Unaishi wapi?
MIMI: Tandale kwa Mtogole.
AZIZA: Kule kwenye wezi wengi na wakabaji?
MIMI: Si wezi wengi tu, kule kunapodharaulika na watu wenye fedha kama nyie.
AZIZA: Hahaha! Usiseme hivyo bwana. Ila mbona umedanganya?
MIMI: Nimedanganya nini?
AZIZA: Kwenye profile lako. Umeandika unaishi Romania. Ulikuwa unataka kujipaisha nini upate wanawake?
MIMI: Hapana Aziza. Hiyo imekuja yenyewe tu.
AZIZA: Kivipi?
MIMI: Nilikuwa nataka kupatambulisha kama home kwetu ni Tandale. Ila nilipokuwa nikiandika Tandale, haikuwa ikitambulika kama ilivyokuwa sehemu nyingine. Matokeo yao wao kama facebook wakaniletea Tandalesti mji fulani kutoka Romania, nikaona sio kesi, nikakubaliana nao, ila ukiangalia kwa makini, Tandale imetokeza katika jina hilo.
AZIZA: Yeah! Nimeona. Hebu naomba uniambie mengi kuhusu Tandale.
MIMI: Kama yapi unataka kufahamu?
AZIZA: Mazingira, watu wa huko na mambo mengine.
MIMI: Tandale kama Tandale mazingira yake mazuri sana, watu full kuyafurahia maisha kama kawa. Kuna watoto wazuri, watoto ambao wanajitambua wao ni nani na kipi cha kufanya maishani mwao. Kuna mambo ya Rusha Roho usiku, yaani kwa kifupi kuhusu maisha, huku tunakula sana bata kuliko kwenu pa kulala saa moja.
AZIZA: Hahaha! Kwani huko kwenu huwa mnalala saa ngapi?
MIMI: Huwa nikiwa mgonjwa sana, nawahi kulala kama saa saba hivi.
AZIZA: Saa saba?
MIMI: Yeah! Ila nikiwa si mgonjwa, mpaka adhana iadhiniwe. Watu tunatransform usiku kuwa mchana na maisha yanasonga.
AZIZA: U must be kidding me Ibra.
MIMI: Huo ndio ukweli Aziza. Siwezi kukutania.

Unaona jinsi mawasiliano yetu yalivyokuwa yakienda? Hapo ndipo nilipokuwa napataka sasa. Nilikuwa namletea sana ucheshi lakini mwisho wa siku kuna kitu nilikuwa nakihitaji kutoka kwake, namba ya simu tu. Unajua katika maisha ya kuchati facebook huwa yanachosha sana, kuna kipindi fulani automatically unatokea kummisi mtu fulani na ungependa sana awe hewani lakini hayupo hewani, unapokuwa na namba ya simu, inakupa wakati mzuri wa kumsikia na kumjulia hali katika kipindi chochote ambacho ungependa kumsikia.
Ucheshi ndio ulikuwa kawaida yangu ila katika kipindi hiki nilikuwa nataka kuuleta ucheshi mpaka katika maandishi. Aziza akaonekana kulifurahia hilo, akaonekana kuanza kunikubali japokuwa hatujawahi kuonana hata siku moja. Nilikuwa bize na chatting na Aziza, sikutaka kuwasiliana na mtu mwingine katika kipindi hicho japokuwa nilimuona Eduado, Ibra Akilimia na Emmanuel Solo walikuwa wamenitumia meseji.
Nilikuwa nikijitahidi sana kumuingiza Aziza kwenye himaya yangu, yaani aingie bila kupenda na mwisho wa siku kila kitu kiwe poa sana. Sikujali alikuwa akiishi wapi, sikujali na mimi nilikuwa nikiishi wapi, kitu ambacho nilikuwa nikikiamini ni kwamba mapenzi wala hayakuwa na hiyana, yalikuwa hayabagui watu kama tulivyo wanadamu.

AZIZA: Nikuulize kitu.
MIMI: Niulize tu.
AZIZA: Unasoma?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Unafanya kazi?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Sasa unafanya nini?
MIMI: Nipo nipo nyumbani. Nilisoma kidato cha kwanza, sikuwa na fedha za kuniendesha kielimu, nikaachana nayo mpaka sasa hivi. Kuna kipindi nilipata vijisenti mara baada ya kubeba sana mizigo Tandale sokoni, nikaenda kusoma English Course.
AZIZA: Kwa hiyo haufanyi kazi?
MIMI: Yeah! Sifanyi kazi.
AZIZA: Unafanya kitu gani kingine?
MIMI: Sifanyi chochote kile.
AZIZA: Ila niliona kama unaandika hadithi! Au majina yamefanana?
MIMI: Yeah! Huwa ninazipost tu.
AZIZA: Hadithi zile huwa unaandika wewe?
MIMI: Hapana.
AZIZA: Sasa huwa anaandika nani?
MIMI: Anaandika baba na kisha mimi kuzichukua na kuziweka facebook.
AZIZA: Unanidanganya Ibra.
MIMI: Nikudanganye ili iweje? Kuna tuzo ya uongo wanapewa waongo? Huo ndio ukweli.
AZIZA: Mmmh! Basi mpe hongera baba yako.
Mimi: Zimefika.

Wakati mwingine haitakiwi kuwa mkweli kwa kila kitu. Tayari nilikwishaona kwamba kagundua kwamba sisi ni watu tunaoishi sehemu mbili tofauti, madaraja mawili tofauti na katika kichwa chake aliamini kwamba Tandale wanaishi watu masikini japo haikuwa hivyo. Nilichokuwa nikikifanya ni kuendana na akili yake alivyokuwa ameiweka, nami nikaanza kujifanya masikini ambaye sikubahatika kusoma kwa kuwa sikuwa na fedha ya kuniendeleza kielimu. Nikafanikiwa, kwa kiasi fulani aina ya maisha ambayo nilimpa yalimfanya kuamini kwamba kweli nilikuwa mtoto wa uswahilini, nilijivunia kuishi Tandale katika uwepo wake.

Maisha yalikuwa yakiendelea kama kawaida, kuhusu Aziza, wala sikuwa na wasiwasi kwa kuamini kwamba piga ua huyu mtoto ni lazima ningemchukua bila tatizo lolote lile. Kila siku nilikuwa nikiwasiliana nae, alikuwa akionekana kunikubali sana, chatting zangu zilizokuwa zikitabasamu zikaonekana kuuteka moyo wake. Nilikuwa na marafiki wengi facebook lakini nikikaa bila kuchati na Aziza sikuwa nikijisikia furaha kabisa.
Japokuwa Eduado alikuwa amenipa ishu ya kumfuatilia Aziza kama mchezo fulani lakini kadri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo nami nikazidi kufall inlove. Nilikuwa nikipenda sana Aziza, kila nilipokuwa nikiingia facebook na kumkosa, sikuwa nikijisikia raha kabisa.
Kuna nyakati za shida zikaingia, nyakati ambazo sikuweza kumuona Aziza hewani. Katika nyakati hizo maisha yalikuwa ya tabu sana, nilikuwa nikikosa furaha hata katika maisha ya kawaida. Nilimzoea sana Aziza, nilimpenda sana Aziza kwa hiyo kutokuuona uwepo wake machoni mwangu kilikuwa ni kitu ambacho kiliniumiza sana.

MIMI: Eduado vipi?
EDUADO: Poa. Inakuwaje?
MIMI: Kama kawa. Mbona Aziza simuoni siku hizi?
EDUADO: Tupo kwenye mitihani kaka.
MIMI: Sasa mkiwa kwenye mitihani ndio haruhusiwi kuwa hewani? Mbona wewe upo?
EDUADO: Mimi si unajua mbishi kaka.
MIMI: Dah! Nimemmisi sana Aziza. Nimemmisi ile mbaya kaka.
EDUADO: Usijali kaka. Mitihani ikiisha atakurudi hewani tu.
MIMI: Poa. Ila mnamaliza lini?
EDUADO: Wiki ijayo.
MIMI: Duh!
EDUADO: Nini tena kaka?
MIMI: Nahisi kama nitakufa kwa mawazo. Nahisi nitaweza kufa kaka.
EDUADO: Usijali kaka. Wewe vumilia tu utakula mbivu.
MIMI: Poa kaka.

Katika kipindi hicho ndicho nikajua kwamba moyo wangu ulikuwa ukimpenda sana Aziza. Huyu Aziza ndiye ambaye alinifanya niwaone wasichana wote kuwa wa kawaida sana, yeye ndiye aliyenifanya nimuone kuwa msichana mzuri kuliko wasichana wote duniani. Uwepo wake katika mtandao wa facebook bado nilikuwa nauhitaji sana, nilikuwa nikijisikia mpweke kupita kawaida. Aziza...Aziza...Aziza...upo wapi wewe msichana uje kuupoza moyo wangu ulio kwenye maumivu makali?
Siku zikaendelea kukatika na hatimae siku ambayo ilionekana kunifurahisha ikawadia. Siku hiyo nikawa kama nimepigwa na mshtuko mkubwa moyoni, sikuamini kile ambacho kilikuwa kikionekana machoni mwangu, Aziza alikuwa hewani. Sikutaka kupoteza muda, sikutaka kuleta pozi, kwa haraka sana nikamtumia meseji.

MIMI: Mungu wangu!
AZIZA: Nini tena.
MIMI: Umekuja at last.
AZIZA: Yeah! Nilipotea kwa kipindi fulani hivi, si unajua mitihani wangu.
MIMI: Pole sana. Mmekwishamaliza?
AZIZA: Yeah! Tumekwishamaliza. Ila nami nilikumisi sana.
MIMI: Nashukuru kwa kunimis, ila ulimiss nini kutoka kwangu?
AZIZA: Chatting zako, meseji zako zimekaa kitofauti sana na watu wengine.
MIMI: Kivipi?
AZIZA: Zipo kitofauti sana. Katika maisha yangu nimewahi kuchati na watu wengi sana, ila zako...dah!
MIMI: Bado haujaniambia kivipi.
AZIZA: Kwanza hauandiki kimkato kama neno ‘sijui kuliandika cjui’, yaani maneno ya mikato huwa hauitumii kabisa.
MIMI: Kwani hiyo nayo ni sababu?
AZIZA: Ngoja nikwambie kitu Ibra. Hii ni siri ambayo wanaume wengi wamekuwa hawaielewi na ndipo wanapofanya makosa kila siku.
MIMI: Siri gani?
AZIZA: Unajua unapochati na msichana yeyote ambaye haujawahi kuonana nae, unatakiwa kuonyesha nidhamu ya hali ya juu, hiyo ndio sifa moja kubwa ya kumteka msichana kwa sababu hisia zetu hazitekwi na mambo makubwaaa, hapana, hivi vitu vidogo vidogo ambavyo wavulana wanavipuuzia ndio vinatuteka.
MIMI: Kama vitu gani.
AZIZA: Cha kwanza salamu Ibra. Hivi unajua kwa sababu gani meseji yako ya kwanza kabisa uliyowahi kunitumia sijakujibu?
MIMI: Hapana. Sijajua kwa nini.
AZIZA: Salamu. Wanawake wengi wanalichukulia tofauti neno ‘mambo’. Unapomsalimia msichana kwa mara ya kwanza kwa kumwambia ‘Mambo’, wanaojibu ni wachache sana.
MIMI: Kwa nini sasa?
AZIZA: Kwa sababu mwanamke anapenda kufuatwa kinidhamu.
MIMI: Sasa nilitakiwa kukusalimia vipi ili ujibu?
AZIZA: Unapomfuata msichana yeyote duniani, anza kwa kumsalimia ‘Habari yako’ au salamu yoyote iliyokaa kinidhamu. Kidogo ukisalimia hivyo, kuna asilimia kubwa sana ya msichana kukujibu.
MIMI: Duh! Kumbeee!
AZIZA: Yeah! Hiyo ni siri ya kwanza Ibra, wavulana wengi huwa wanafeli hapo tu kitu ambacho kinawafanya kila siku kulalamika kwamba wasichana tuna mapozi kujibu salamu zao, hapana, hatuna mapozi bali wanakosea kusalimia, wanakosa nidhamu katika kusalimia.
MIMI: Nimekuelewa. Naomba siri nyingine.
AZIZA: Chatting. Unajua usipende kuchati na msichana kifupi kama nilivyokueleza toka mwanzo. Andika neno lote kwa ujumla, unajua unapoandika kifupi, unaupa kazi ubongo wa mtu kulifikiria neno na matokeo yake akili yake inachoka na kukatisha chatting na wewe.
MIMI: Ila mimi sijawahi kuchati namna hiyo Aziza.
AZIZA: Najua. Ila ninakumegea siri juu ya vitu ambavyo msichana anavipenda na vile asivyovipenda.
MIMI: Dah! Umeifungua akili yangu.
AZIZA: Ila wewe..dah! Wewe mtu noma.
MIMI: Kwa nini?
 ITAENDELEA SIKU YA KESHO
  
Unataka niwe nakutumia CHOMEZO watu 200 wa kwanza kulike PAGE YA 2JIACHIE Mtatumiwa imbox chomezo LIKE PAGE YETU HAPA ==>www.facebook.com/2jiachie

The Last Breath (Pumzi ya Mwisho) - 7

$
0
0
Na Eric Shigongo
NDEGE imeanguka, watu wote wamekufa isipokuwa Johnson na mwanaye Melania pamoja na watu wengine kadhaa lakini mbele ya safari wakati wakijaribu kujiokoa, watu wengine wote wanakufa na wanabaki Johnson na mwanaye, hata hivyo Johnson naye anazimika ghafla,  Melania analia akijua baba yake amekufa.
Muda mfupi baadaye, binti huyo mdogo anaingia mikononi mwa waasi wa Kundi la Congoleze Patriotic Front,  ambao wanataka kumbaka lakini kiongozi wao anamnusuru na kumpeleka moja kwa moja hadi kambini ambako hivi sasa anaishi akiandaliwa kuwa muasi akiwa amekabidhiwa kwa kijana aitwaye Paul.
Mke wa Johnson (Loveness) baada ya kupewa taarifa za kuanguka kwa ndege mshipa ulipasuka kichwani mwake, akapoteza fahamu na hata baada ya upasuaji uliofanyika Dar es Salaam, kumbukumbu zake zimepotea! Hakumbuki chochote kilichotokea na inawezekana akabaki hivyo maisha yake yote.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
MAKUBO Army Hospital  ilimilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Congo, ilikuwa ni hospitali kubwa yenye vifaa vingi kwenye kutibu majeruhi, Kaskazini Magharibi mwa Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Ndiyo iliyohusika sana na matibabu ya majeruhi wote walioumia katika mapigano kati ya Majeshi ya Serikali na Majeshi ya Waasi wa Kikundi cha Congolese Patriotic Front.

Asubuhi hiyo madaktari na wauguzi ambao pia walikuwa ni wanajeshi, walikuwa bize wakijaribu kuokoa maisha ya mgonjwa aliyeletwa na helkopta kutoka msitu wa   Kundelungu ambako mapigano kati ya jeshi na waasi yalikuwa makali kupita kiasi.

Alikuwa amevunjika mguu na mkono,  hakuwa na fahamu kabisa na kiasi kikubwa sana cha damu kilikuwa kimepotea. Kilichofanyika mwanzo ni kumwekea chupa za damu zisizopungua kumi, baada ya hapo akapelekwa chumba cha upasuaji ambako mifupa iliyovunjika ilirekebishwa ndipo akarejeshwa wodini na kuendelea na lishe kupitia kwenye mifupa yake, maana kiasi cha sukari katika mwili wake kilikuwa kimeshuka mno.
“He is terribly hypoglycemic, he needs 5% dextrose IV infusion, 30 drops per minute!”(ameishiwa sana na sukari kwenye damu, anahitaji  chupa za maji ya wanga 5%, matone thelathini kwa dakika!) Dk Linda Johnson kutoka Marekani ambaye alikuwa mfanyakazi wa shirika la madaktari wasio na mipaka alisema, alikuwa mmoja wa wafanyakazi kwenye hospitali hiyo wakiokoa maisha ya watu.
Maji yakaanza kuingia kwenye mishipa ya mgonjwa huyo kama daktari alivyoagiza, chupa zikawa zinabadilishwa kila moja ilipokwisha mpaka zikatimia chupa sita, damu yake ilipochukuliwa kwenda kupimwa kiasi cha damu kilionekana kuwa gramu 9.5, karibu kabisa na kawaida, daktari akaagiza chupa mbili zaidi ziwekwe.
Ghafla zilipomalizika hizo, mgonjwa akajitingisha na baadaye kufumbua macho, alichokifanya kiliwashtua watu wote waliokuwemo chumbani na hata waliokuwa kwenye ofisi ya wauguzi, alipiga kelele kwa nguvu kubwa akiita jina la Melania!
“Vipi?” Daktari mmoja aliuliza walipoingia chumbani.
“Ameita jina la Melania.”
“Labda ni mke wake?”
“Pengine, nashukuru angalau ameweza kuongea, hali yake ilikuwa mbaya mno, sikuwa na uhakika kama angeweza kufumbua macho na hatimaye kutoa neno, kwa jinsi sukari yake ilivyokuwa imeshuka, nilifikiri ubongo wake ungeweza kuwa umeharibika.”
“Mungu amemsaidia.”
“What is your name?” (jina lako ni nani?) daktari alimuuliza.
“Johnson!”
“Where are you from?” (umetokea wapi?)
“Tanzania.”
“What were you doing in the Congo forest? Are you a rebel?” (ulikuwa unafanya nini kwenye msitu wa Congo? Wewe ni Muasi?)
“No! I don’t know about that! The plane I was traveling with crashed, where is my daughter?” (Hapana! Sijui juu ya hilo! Ndege niliyokuwa nasafiri nayo ilianguka, binti yangu yuko wapi?)
“Who is your daughter?” (binti yako ni nani?)
“Melania.”
“She is not here, we found you alone in the forest, unconscious and dying, you have been here since yesterday!”(hayupo hapa,  tulikukuta wewe peke yako msituni, ukiwa hujitambui na unakufa, umekuwa hapa tangu jana!)
“Oh my God!”(Oh! Mungu wangu!) aliongea Johnson machozi yakianza kumlengalenga.
“What was your flight?” (ndege yako ilikuwa ni ipi?)
“Air Congo, flying from Kinshansa to Nairobi!” (ndege ya Shirika la Ndege la Congo,  iliyokuwa ikiruka kutoka Kinshasa kwenda Nairobi!)
Johnson akaenda mbele zaidi na kuwaeleza kila kitu kilichokuwa kimetokea, wote wakawa wameelewa kwamba ndege aliyokuwa akisafiri nayo ndiyo iliyoaminika na kutangazwa duniani kote kwamba ilidondoka baharini na kuzama mpaka kwenye sakafu ya bahari.
Zilikuwa habari mpya kabisa na zilipelekwa moja kwa moja kwa Mamlaka ya Anga ya Congo pamoja na shirika la ndege la nchi hiyo ambao walifika mara moja na kuonana na Johnson ambaye aliwasimulia kila kitu juu ya kilichotokea, hawakuamini!
Kilichofanyika ni kukubaliana kwamba apate nafuu ya afya yake kisha kabla hata hawajatangaza waende naye mpaka porini alikookotwa, huko ndiko angeweza kuwaonyesha mahali mabaki ya ndege yalipokuwa. Johnson akatuma taarifa zake Tanzania kuwajulisha juu ya kuwa kwake hai, ndugu, marafiki wakafunga safari kumfuata hadi kwenye hospitali hiyo iliyokuwepo katika Mji wa Marabakungu.
“Mke wangu yuko wapi?” alimuuliza kaka yake.
“Tanzania.”
“Mbona hamjaja naye?”
“Atakuja tu!”
“Au amekufa kwa mshtuko?”
“Hapana,”
“Nitaishije mimi? Bila mke na mtoto wangu?”
“Usiwe na wasiwasi, Melania atapatikana tu.”
“Wapi? Wakati tulikuwa naye pamoja porini? Lazima atakuwa amekufa.”
Wiki nne baadaye hali ya Johnson ilikuwa nzuri, kwa helikopta akarushwa mpaka katikati ya msitu wa Congo ambako helikopta ilitua, akashushwa na kubebwa begani mpaka eneo alikookotwa. Alipofikishwa hapo tu kumbukumbu zote zilimwijia kichwani mwake, akamkumbuka mtoto wake na watu wote waliokufa njiani wakijaribu kujiokoa.
“Unafahamu mahali ndege ilipoangukia?”
“Twendeni njia hii.”
Walitembea kwa saa tatu ndipo wakafika eneo hilo, mabaki ya ndege yalikuwepo na mifupa mingi ya watu, nyama zake zikiwa zimeliwa na ndege pamoja na wanyama. Kitu cha kwanza walichokifanya ni kukitafuta kisanduku cheusi, kikapatikana. Baada ya hapo wakaangalia sanduku lililokuwa na dhahabu pamoja na almasi, halikuwepo.

“Lazima waasi walifika hapa!” mmoja wa wapiganaji alisema:
“Inawezekana, wakachukua sanduku lenye mali na kuondoka.”
“Walipajuaje?”
“Inawezekana kabisa mtoto wa Johnson walimteka, baada ya mateso akasema ndege ilipoangukia.”
“Kwa hiyo mtoto wangu yuko mikononi mwao?”
“Kabisa, kama si hivyo basi inawezekana waasi waligundua tu kwa bahati na mwanao atakuwa ameliwa na wanyama wakali.”
“Hapana! Hapana! Usiseme hivyo, naumia moyo.”
Huku akilia machozi Johnson aliondolewa eneo hilo mpaka mahali helikopta ilipokuwa imetua, wakapanda na kuruka tena hadi Marabakungu ambako alirejeshwa hospitali kuendelea na matibabu, jioni ya siku hiyo Serikali ya Congo ilitangaza juu ya kupatikana kwa mabaki ya ndege iliyokuwa inaaminika kwamba ilizama katika bahari na mtu mmoja aliyenusurika alitajwa kuwa ni Johnson, picha yake ikionekana.

***
Loveness alikuwa wodini bado akiwa hajaweza kujitambua, muda wote alikaa na picha mbili mkononi mwake akiziangalia na kulia. Hilo lilionyesha kwamba kumbukumbu zake zilikuwa zimeanza kukaa sawasawa akili ndiyo ilikuwa bado haijatengemaa kama ilivyokuwa awali.
Ndani ya chumba cha wodi alichokuwa amelazwa, akiuguzwa na dada yake, kulikuwa na runinga kubwa ukutani, taarifa ya habari ya Shirika la Utangazaji la CNN ilikuwa hewani, mara ghafla taswira ya Johnson akihojiwa juu ya ajali ya ndege ilivyotokea ikaonekana.
“Johnsooooon! Johnsooon! My husband!”(Johnsoon!Johnsooon! Mume wangu!) kwa mara ya  kwanza baada ya muda mrefu kupita, Loveness alizungumza, dada yake aliyekuwa kando ya kitanda akanyanyuka ghafla akiwa katika mshangao na kutupa macho kwenye runinga.
“He! Ni yeye, umemtambua?”
“Ni mume wangu,  yupo Congo!”
“Kweli kabisa.”
Watu wakaingia wodini na kumkuta Loveness akiongea huku machozi yakimbubujika, kwa hali ilivyokuwa, daktari akihofia kwamba presha yake ingeweza kupanda, aliagiza achomwe dawa ya usingizi mara moja ili kupumzika.
Hilo likafanyika na akazinduka saa nne baadaye na kuelezwa kilichotokea.
“Nataka niende Congo, nikamwone Johnson, labda na mwanangu yuko palepale!”
“Haitawezekana kwa sasa.”
“Kwa nini isiwezekane?”
“Hali yako bado haijawa nzuri.”
“Lazima niondoke,  maisha yangu haya, maana ni kama sina watu wawili muhimu maishani mwangu; Johnson na Melania.”
“Tunaelewa.”
“Kama mnaelewa basi niacheni niende zangu.”
“Itabidi usubiri.”
“Siwezi kusubiri.”

Nisingependa kumaliza hadithi hii ya leo bila kukumbusha jambo muhimu la kutoa maisha yako kwa Mungu. Maisha tuliyonayo hapa duniani ni mafupi sana, yanapita kama maua yachanuavyo na kunyauka. Wengi unaowafahamu wamekufa lakini wewe unapumua, ni vyema basi kufikiria maisha baada ya kifo.
Kila siku jiulize: “Hivi nikifa leo nitakwenda jehanam au peponi?” Kila mmoja wetu analo jibu lake, bila shaka sote tungependa kwenda peponi. Kama hivyo ndivyo, basi tiketi ya kwenda huko ni matendo mema na kujiepusha na uovu.
Tukumbuke mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Je, nini kitaendelea?  Fuatilia siku ya Ijumaa kwenye gazeti la Championi Ijumaa.

VIDEO: WABUNGE WA UPINZANI WAKITOKA NJE BUNGE LA KATIBA LEO

$
0
0
Bunge Maalum la katiba linaendelea muda huu na leo wajumbe wataendelea kujadili sura ya kwanza na sita ya rasimu mpya ya katiba.

Mh. Sereweji

kutoka Zanzibar anasema kuwa muundo wa serikali mbili bado unatufaa,wazanzibar tuna kila kitu hapa Tanzania bara.

Anasema wapo bungeni kutafta katiba iliyo bora ya Tanzania na anawasihi wanaosema wataenda Zanzibar kuomba muungano wa mkataba kuwa watakuwa wanavunja sheria.

Anasema mapinduzi yamefanyika Zanzibar unguja ila pemba imepelekwa bendera tu baada ya mapinduzi.

Anaunga mkono hoja ya serikali mbili.


Mh. Gaudensia Kabaka,

Ameanza kwa kuipongeza tume kwa kazi kubwa iliyoifanya ila akaishauri ilete na yale maoni ya mabaraza ya katiba.

Kwa ujumla yeye anapendekeza muundo wa serikali 2 ambazo hazimo kwenye rasimu.

Anaongezea kwa kusema kuwa serikali ya shirikisho itakua serikali hewa.

Kwa ujumla msimamo wa Kabaka ni serikali 2.


Mh. Mohamad Sanya,

anaanza kwa kusema ni muumini wa serikal tatu na atatetea kwa busara muungano huo.

Anasema Lipumba alionesha jinsi usamehevu wa kodi ulivyo mkubwa hapa na kudidimisha maendeleo.

Anasema hataki huu muungano wa sasa,na wanataka muungano utakaoondosha kero kwenye muungano wa sehemu mbili.

Anasema wasilete kisingizio kuwa wazanzibar hawana mafuta na gesi ndo maana wanataka muungano ila wanaweza kujenga nyumba zao bila utegemezi.

Anasema wapo hapa kuzungumzia mustakabali wa muungano huu na sio vyama vya siasa.

Anasema wawape nafasi waone watakavyoinua uchumi na hata kusaidia upande huu mwingine wa muungano.

Anasema rada kijeshi na mawasiliano ni za muungano lakini baada ya chenji ya rada kurudishwa zanzibar hawakunufaika na chenji hiyo.Wazanzibar wamechoshwa na muungano huu na wanataka mamlaka kamili ili waweze kuamua mambo yao wenyewe.

Anasema kwa muungano huu ccm wataendelea kupoteza kura nyingi visiwani maana wanajali matumbo yao na sio wazanzibar.

Zanzibar wana matatizo makubwa lakini hayatatuliwi,anasema kuna watu wa tanzania bara wana uwezo wa kufungua vitega uchumi zanzibar lakini hawaji bali watu wasio na mwelekeo kama wauza karanga ndo wanakuja zanzibar.

Anasema zanzibar wakiwa na mamlaka kamili wanaweza kuibadili zanzibar kuwa Hong Kong ya afrika mashariki.

Anamalizia kwa kusema serikali tatu ipo na italeta maendeleo baina ya pande zote mbili.


Mh. Diana Chilolo,

Anaanza kwa kusema yupo kamati no 12,na anaamini serikali mbili bado zinafaa kufanya kazi katika muungano huu.

Anasema hayaelewa hii rasimu kila akiisoma na kuitafakari mpaka alkafika wakati akakasiri.

Anasema labda jaji Warioba kaweka utashi wake na kwanini aweke utashi wake kwenye maslahi ya watanzania kwa kuwaongezea watanzania mzigo wa serikali tatu.

Wizara ya muungano ipo chini ya makamo wa rais aliye mzanzibar,na anasema kweli watu hawa hawajui kero za muungano?Wanazijua ndo maana kati mya kero 27 zimebaki kero saba.

Anamshangaa tundu lissu kuwa alikuwa hawataki wazanzibar hata bungeni lakini anashangaa unafiki wake sasa ni rafiki wa zanzibar na kuwapigania.

Anasema kero ya watanzania sio serikali tatu bali huduma nzuri,mishahara iboreshwe na maendeleo mengine.

Anawashangaa cuf kwa kutaka kurudisha usultani zanzibar.

Anasema kinachotakiwa hapa ni kuboresha muundo huu wa serikali mbili.

Anamuomba makamu mwenyekiti kuwa kwanini hawa wanaowakashifu waasisi wetu kwanini wasisimame mbele ya bunge waombe radhi maana watanzania wana hasira na watanzania hawapo tayari waasisi wao kudharauliwa. Anasema watu kama hawa usishangae wakawakana wazazi wao.

Anamalizia kwa kutoa mfano kuwa Sitta alipomwoa Magreth alikuwa anaitwa Magreth Simwanza ila baadaye akaitwa Magret Sitta, hoja yake ni kuwa Magret hajamkana baba yake kwa hiyo Tanganyika haijakanwa.

Tunu za taifa anazungunzia kuingiza swala la jinsia maana ni tunu kwa taifa lazima lienziwe 50/50.


Mh. Sixtus Mapunda,

Anaanza kwa kusema kuwa hataweza kuikana kweli, anaendelea kusema kuwa ukizoea kusema uongo huwezi kusema kweli.

Kuna watu walisema hakukuwahi kuwa na hati ya muungano na kuwakashfu wasisi wetu. 25/4 baraza la wawakilishi lilikaa zanzibar na kambona alihudhulia na aliporudi alipokelewa kalimjee akasema yaliyo tokea.

Anaendelea kupangua hoja za Tundu Lissu kuhusu kutokuwepo kwa hati ya muungano, kuhusu kukutana kwa Baraza la Mapinduzi.

Anahoji uhalali wa takwimu za tume ambazo anaona hazikuwa na uhalali kutokana na namna zilivyokusanywa hasa kwa kuacha maoni ya mabaraza ya kata na wilaya.

Anamalizia kwa kusema Tunu za taifa zienziwe.


Mh. Ali Omar Makame:

Anazungumzia umuhimu wa kuweka haki za walemavu katika katiba.

Hii katiba tuliyonayo imerekebishwa mara 11 lakini mambo ya ulemavu hayamo. walemavu tunataka elimu afya mikopo na ajira na mazingira rafiki.

Mimi ni muumini wa serikali mbili. Mimi sikusoma, wasomi watatuelekeza. Je serikali tatu gharama zinakuaje?

Sisi walemavu tunataka huduma, kwanini hizi gharama za serikali ya tatu zisisaidie wenye ulemavu?

Tusaidieni tutoke hapa tulipo sisi walemavu halafu ndo mfikirie kuongeza serikali ya tatu na ya nne.

Watu wenye mahitaji maalum katiba itamke ni watu wenye ulemavu. Vipofu, viziwi viwete ni maneno ya kutudhalilisha.

Kubomoa kunasababisha wajane na yatima,mkibomoa watakaopata tabu sana ni sisi walemavu.

Anaunga mkono serikali mbili.


Mh. Hamis Mnondwa,

anaanza kwa kusema ni muumini wa serikali mbili na ana sababu zake.Anawashangaa wanaoshabikia serikali tatu na anasema kuwa hizi serikali mbili kama zina matatizo basi matatizo yote yanaweza kufanyiwa kazi.

Anasema kuna vijana wengi hawana ajira kwanini hizo gharama za serikali tatu zisiwasaidie vijana.

Anasema serikali tatu ni kuua muungano wa tanzania bara na Zanzibar.

Tukiongeza serikali ya tatu ina maana tanzania bara na zanzibar bye bye.

Sasa hivi zanzibar wanajiuliza jeshi kubwa liko bara, hatuna hela za kugharamia uhamiaji wala hatuna mipaka. Tukiongeza serikali ya tau habari la muungano limekwisha.

Kwanini tusikae tukazungumzia mstakabari wa nchi? Muundo wa serikali tatu ni muundo ambao hauna shida,upo kwa ajiri ya kusimamia majeshi na madaraka.

Tanzania haina ardhi, Je serikali tatu itajenga wapi ofisi?

Je ni nini kitafuata kama sio mapinduzi?

Tutaliwa kodi mpaka ya kichwa na kodi ya kichwa itarudi.


Mh. Zainab Kawawa,

Nataka nizungumze na watanzania leo kwanini sikubaliani na serikali inayoitwa ya shirikisho. Nchi ndio inayozaa uraia na kutengeneza utaifa.

Jamhuri hiyo ya Tanzania haitoi huduma za afya, elimu na huduma zozote,haiwezekani.

Viongozi wa upinzani igeni mfano wa viongozi wa CCM, kwanini chama kimeendelea kuwa imara. Nyie hamna utashi wa kuvumilia na kukosoana.

Mna hadhi gani ya kuvaa koti linalofanana na wasisi wa nchi hii. Wajumbe wameonesha dhamira ya kuvunja muungano wetu.

Hivi ninyi mnaotaka serikali tatu kwa nia mbaya mnaonesha dhamira ya kuuvunja muungano huu,nani asiyejua CHADEMA haina wanachama Zanzibar?

Watanzania ndio wanaogawa uongozi,waroho wa madaraka ninyi na acheni njia za dezo.


Mh. Abubakar,

Anasema katiba ni nini? Katiba ni muelekeo wa baadae, katiba ni dira.

Katika hii katiba yetu kuna mambo mengi ni dhaifu kwa muungano.Katiba inaonesha ina mamraka tatu, ya Zanzibar, Tanganyika iliyotiwa kwenye mamraka ya muungano. katiba haina misingi ya muungano,ibara ya 98[1b].

Bunge inaweza kutunga sheria na kusema tu itumike Zanzibar, haiwezekani Zanzibar ina wawakilishi wake.

Mambo ya nje ina mabalozi kama thelathini kati yao Wazanzibar ni watatu tu, je wazanzibar hawafai.?

Kuna mbolea imetolewa na Japanyenye thamani ya billioni 10 lakini Zanzibar haijapelekwa hata mfuko mmoja,je huo ni muungano?

Lililopo hapa Tanganyika imevaa koti la Tanzania ndo maana ikiletwa mbolea inaenda Songea na Ruvuma. Sasa hili koti livuliwe.

Sisi Zanzibar tunataka serikali ya shirikisho, lakini lakini tumeimesema serikali moja mbili shirikisho hayafai inayofaa ni serikali tatu basi tumekubaliana nao.

Serikali tatu ndiyo zitatoa muelekeo wa swala hili. asanteni.


Mh. Ramadhan Abdallah Shaaban

anaongea sasa. Anasema kuwa mambo mengi yaliyoainishwa kama kero za muungano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba tayari yameshapatiwa ufumbuzi.

Anawataka wajumbe kutumia mjadala huu wa katiba kurekebisha kero zilizopo. Anasema kuwa wanachofanya wapinzani ni kama NDEKWA. kwamba wanatumia madai ya serikali tatu kwa ajenda wanazozijua wenyewe.

Kuhusu uwekezaji anasema kuwa wabara na wazanzibari wanawekeza kila upande. Amezitaja hoteli kama za Sea Cliff ya Subash Patel na Kiwonga inayomilikiwa na watu wa kilimanjaro.

Anapendekeza kurejesha mfumo wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa serikali ya Muungano na ugomvi utakuwa umekwisha.
Anaunga hoja mfumo wa serikali mbili.


Mh. Waziri Rajab Salum,

anasema ni muumini wa serikali mbili si kwa kufuata mkumbo au kubembelezwa na mtu. Mimi ni msomi nimefanya research na kuona serikali mbili ndizo zitatupeleka mbele.

Huwezi kutengeneza shirikisho bila kuwa na washirika. Zanzibar kukubali shirikisho ni kuigeuza Zanzibar kuwa kama Eritrea na Comoro.

Wapinzani wa Zanzibar hawakuanza leo,wapinzani wa uhuru wetu wa 1964 ndo hawa hawa vizazi vyao vinaendelea kuwa wapinzani.

Unapozungumzia Zanzibar unazungumzia Unguja na Pemba. Anasema kuwa wapinzani wa mapinduzi ni hawa hawa wanaopinga muungano hasa kupitia vizazi vyao.

Anasema kuwa Wazanzibari wanaotoka Unguja, wana muingiliano na watu wa bara huku wa Pemba hawana muingiliano wa kidamu zaidi ya ule wa kibiadhara. Wanaotaka Serikali tatu wanataka kuvunja muungano na kuchukua maduka yao na kupeleka Pemba.

Nature ya binadamu yoyote anapoambiwa ukweli lazima akasirike. Kwa vile naunga mkono serikali mbili napendekeza rais wa jamhuri na makamu na rais wa Zanzibar na makamu rais wa kwanza na wa pili wa Zanzibar washirikishwe kwenye jamhuri na watambuliwe kuulinda muungano wetu.

Tupo hapa kama taifa moja,tuache ushabiki tuambizane ukweli.


Mh. Issa Gafu,

Anasema Naunga mkono mapendekezo ya wengi ya kamati namba 11. Tuendelee kubaki kwenye mfumo wa serikali mbili.

Ulinzi na usalama zinahitaji fedha nyingi,usalama na ulinzi upo kwenye serikali ya tatu ya muungano ambao hauna vyanzo vya mapato.

Zanzibar imetuchukua miaka 40 bila hawa wanasiasa kuyatambua mapinduzi tukufu ya zanzibar. kama anaweza kubana uhuru wako hawezi kukupa uhuru wa kuuukubali muungano.

Tatizo la zanzibar sio mfumo wa serikali bali uchumi. vinginevyo tukitaka serikali tatu ina maana tunataka kuuvunja muungano jambo ambalo sipo tayari kufanya hivyo.

Faida za muungano zipo nyingi tu. Bila muungano kusingekuwepo na sherehe za mapinduzi, maadui wa mapinduzi bado wapo. Shindanisha maendeleo ya miaka 200 tuliyo tawaliwa na miaka 50 ya muungano.

Hatukua na mtaalamu hata mmoja lakini sasa hivi tuna wataalamu wengi.

Nawaomba wabunge tukisimama tujisemee sisi wenyewe sio kuwasemea watanzania eti wamewatuma.


Mh. Tundu Lissu

anasema, Naomba nianze kwa kujibu vihoja. Kuna kihoja kinasema Tundu Lissu amemtukana baba wa taifa.

1995 baba wa taifa alihutubia Mbea akasema, asiyekubali kukosolewa hawezi kuwa kiongozi bora.

Baba wa taifa alikuwa binadamu hakuwa Mungu wala malaika alikuwa binadamu na hajawa mtakatifu bado.

Baba wa taifa alishawahi kuunga mkono vita ya BIAFRA wakliotaka kujitenga na Nigeria.

Anasema kuna watu walikimbia ccm na kukimbila nccr Mageuzi na walirudi baada ya Mwl Nyerere kufariki.

Hati ya makubaliano ya muungano haupo.Tumeoneshwa sahihi nenda ulinganishe. Leteni hizo sahihi hapa tuwaonesheni mlivyo waongo.

Zanzibar haijawahi kuridhia muungano mpaka kesho kutwa. Kama mashariti ya muungano hayajatekelezwa kwa miaka 50 ni halali?

Muundo wa shirikisho wa serikali tatu kama ilivyopendekezwa na tume ya Nyalali, Kisanga, Walioba na wananchi ndo unafaa.

Ndivyo alivyo pendekeza Mwakyembe miaka 20 iliyopita. Rais wa Tanzania Kikwete sio mkuu wa Zanzibar. Katiba ya Zanzibar inasema rais wa Zanzibar atakua ndio rais mkuu, na mkuu wa vikosi maalum, Ibara ya 26(1) ya katiba ya Zanzibar.

Haya sio maneno ya Tundu Lissu ni maneno ya katiba ya Zanzibar.

Nani anaye weza kusema sisi ni nchi moja. Kikwete akienda Zanzibar anayepigiwa mizinga ni Shein, Kikwete akiwa mbali kabisa. Mkiwa na rais magogoni mwingine mmnazi mmoja wakipishana itakuaje?

Tutengeneze utaratibu mpya baada ya miaka 50 ya kudanganyana. Tusipochukua hatua za haraka mbele ni giza tupu.

Watakaoanzisha muda si hawa wanaoanzisha katiba mpya bali ni wale wanaofumba macho wakati mambo yakiharibika.


Mh. Benard Membe

anasema, Huu ni muungano wa pekee na wa pili duniani uliodumu ukifuatia ule wa Canada.

Tunaweza kuunda muungano wa nchi hizi mbili lakini serikali ya Tanganyika itaua serikali ya muungano na shahidi atakua serikali ya Zanzibar.

Tume ya Warioba italaumiwa kwa kupaga mauaji hayo.

Naungana na CCM kwamba jibu pekee ni serikali mbili.

1988-1990 huu ndo ulikuwa ubishi Urusi.

Kwanini tusijifunze kwa Urusi iliyokufa baada ya mwaka mmoja?.

Nawauliza mpo tayari mkubali Zanzibar na Tanganyika msikusanye kodi, kodi ikusanywe na jamhuri? {wabunge wameitikia ndio}

Serikali gani duniani inayoendeshwa bila kodi?

Mifano niliyoitoa ya Urusi, Spain na Ujerumani inatosha. Tukiunda serikali tatu itaua muungano.

Hakuna nchi duniani ambayo inatukana wasisi wake. Na bunge litakua wa mwisho kuwatukana waasisi. Tuna tatizo la kujifanya wajuaji.

Hakuna mtu mwenye akili timamu atakayeenda mbele ya hadhara na kuwakejeri.

Hati ya muungano nimeiona na ni halali na ndiyo mtakayoiona hapa na haikuchakachuliwa.


Mh. Khalifa Khalifa

anasema, Kwanini tumefika mahala kwenye chombo kama hiki baada ya kuleta hoja tunatukanana? woga huu wa nini?
Mimi tume ya Warioba naiunga mkono. Hawa walikua 30 sisi tupo 600 na kitu.

Warioba alisema tutenganishe mamraka ya muungano ya Tanganyika na Zanzibar yakae mbali.

Je ni halali mabolozi kutoka Zanzibar wawe wanne tu? je Zanzibar haifai kupata kiongozi mkuu jeshini? Tusikie humu ndani tukatukanana bure hadi kuwatukana viongozi wa nje.

Mtu anaongea ubaguzi wa Unguja na Pemba mnampigia makofi. mtu anakuja huku anajisifia kwa kabila lake mnampigia makofi -------- kama huyu.


Mh. Amon Mpanju anasema; Yanapotokea mafuriko kama haya walemavu tunataabika,yanapotokea mabomu walemavu tunataabika.
Sijapendezwa na kauri ya viongozi wanaosema kwamba kama serikali tatu haziruhusiwi tupo tayari kwa lolote. mimi ni mwenyekiti wa walemavu nina wafuasi pia, kuna wakulima wana wafuasi pia. Watanzania wenzangu hatunabudi kuwasusa watu wa namna hii. nawaomba sana vijana tusiwaunge mkono.

Jussa alinambia anapuuza taarifa na mimi ananipuuza. maneno haya yaliwaumiza walemavu. Tusimguse Mungu machoni kwani hakuna aliye amua kuwa mlemavu.

Ibara ya nne kuna mapendekezo yameletwa nami nayaunga mkono. ligha ya alama na lugha ya alama amguso itakua ni ligha ya alama kwa watu wasio ona. haya mabadiliko nayaunga mkono.

Nashangaa sana wanaanza kuhoji na kubeza uhalali wa huu muungano hasa tundu lisu. huu muungano sio wa wanasheria ,huu muungano unatambulika hadi UN. huu muungano una matatizo lakini tunaweza kuyatatua kwa kupitia muundo wa serikali mbili. uanasheria wenu usiwe kero.

Tuache kupotosha watanzania. serikali tatu ni kaburi la Muungano. tuache kuhubiri ubaguzi la sivyo zanzibar watagawana mikoba na huku bara tatagawana mikoba. Tuache kuwapa nafasi wazandiki na wanafiki wa nchi hii. wanasema wana watu wakati hawana watu kalenga na chalinze ilionesha.


Mh. Jussa

anasema, hawezi kujibu matusi kwani akili ndogo ndio inayojadili watu badala ya hoja.

Nasimamia matakwa ya Znz .. tunataka mamlaka kamili.
Anasema wanaosema kuwa serikali mbili zitaleta maendeleo Zanzibar mbona zimeshindwa kuyaleta kwa miaka 50?



tume ya Amina iliorodhesha matatizo lukuki ya serikali na wote walikuwa CCM

Mh. Yahya Kassim,

anasema katika upotoshaji huu kuna haja ya kuzungumza ili wapinzani waelewe.Wengine hawaelewi ukweli ulivyo.

Zanzibar imepatikana kwa mapinduzi na bara kwa kura na waliowaondoa hawapo.

Anasema zanzibar kweli wana uwoga,mana siku ya uchaguzi pia ni waoga kusema kuwa mwisho wa utawala wa weusi ni mwisho.

Kuja waarabu zanzibar wanakuja wanasema ardhi hii ya baba yangu anaitaka,je tutaishi wapi?

Anasema yeye ni muumini wa serikali mbili kwasababu katika rasimu hii hakuna mtu zanzibar aliyesema anataka serikali tatu,zanzibar walisema wanataka serikali mbili na ya mkataba.


Mh. Fathyiha Zahara Salum,

anasema kuwa wazanzibari walichoka kuuliwa ndo maana wakaamua serikali ya umoja wa kitaifa.

Kila siku watu wanauana na kuchinjana humu humu Tanzania chini ya s2.. tusitishane.


Mheshimiwa sana Zitto Kabwe,

Anasema kuwa mchakato huu ambao ulipaswa kujenga maridhiano, unajenga hali ya ubaguzi na kuna lugha na kauli za kibaguzi zinatoka huku watu wakishangilia.

Anasema kuwa tujadiliane kwa hoja, watu wajadiliane na wamue na kitakachoamuliwa ndicho kitakachoenda kwa wananchi

Anasema kuwa hakuna uhusiano wa muundo wa muungano na uimara wa serikali.

Muundo wowote wa Muungano, uwe wa serikali 1, 2 au 3 bila maridhiano utavunjika tu!

Hakuna utafiti wowote wa kitaalam unaothibitisha kuwa Serikali tatu zitaongeza gharama!

Tunaweza tukawa na rais mmoja wa Serikali kuu na wakuu wa nchi washirika.

Kuna jumla ya 2.3tril kila mwaka hazikusanywi kama mapato ya Taifa! Tunao uwezo wa kuendesha aina yoyote ya Muungano!

Anasema kuwa tunao uwezo wa kuendesha muungano wowote kama tukiamua kukusanya kodi ipasavyo.

Zitto anasema kuwa ikiwa muungano utavunjika, gharama za kuzilinda nchi zake ni kubwa zaidi kuliko gharama za mfumo wa serikali tatu.


Mh. Ritha Mlaki, Anasema anapendekeza S2

Mh. Serukamba, CCM Tunalo jukumu la kulinda Muungano huu. Muungano utakuwa salama mikononi mwa CCM!

Wapo wanaosema CCM tunang'ang'ania s2, ni kwamba sisi tuna dhamana.

serukamba:Lissu alisema uongo wa miaka 50 umefika mwisho..Mwl ameleta uhuru na amani na muungano

Mnataka kuudumisha Muungano gani ambao mnadai hati zake zimegushiwa?

Mnaotaka s3 mnasema mnataka muungano imara lakini mnataka kuvunja muungano.

Anasema Jussa anataka Zanzibar yenye Mamlaka kamili. Anamaanisha TUUVUNJE MUUNGANO!

===============

Makamu mwenyekiti anatoa matangazo ya wageni wa wajumbe wa bunge maalum la katiba pamoja na wageni wengine waalikwa.

Anasema amepokea hati ya makubaliano ya muungano na ni certified copy.

Anamkaribisha mh. Wassira aweze kutoa neno kuhusu hati hiyo.


Mh. Steven Wassira, anasema hati hiyo ipo na ni halisi na ipo katika hali nzuri hata baada ya kusainiwa miaka hamsini iliyopita.

Anasema kuwa Tundu Lissu na wenzake walikutana baada ya kujua hati ipo na wakakubaliana waseme saini ya Sheikh Karume sio ya kweli.

Anasema watanzania tujihadhari na mawakala wa shetani.

Anasema waasisi wetu wametukanwa sana mpaka kuitwa madikteta na hali hii haivumiliki kwa watanzania wote.

Anasema heshima ya waasisi wetu hailindwi na vyama bali inalindwa na italindwa na watanzania wote.

Makamu mwenyekiti,

Bunge litaendelea Saa kumi jioni.

Anasitisha kikao cha bunge maalum la katiba.


======== Bunge Maalum la Katiba, kikao cha jioni =======

Mh.

Anaanza kwa kuunga mkono maoni ya wengi ambayo inatambua uwepo wa serikali mbili.

Anasema zanzibar kuna makundi mawili yanayotaka mkataba na serikali mbili.

Sababu za kuunga s2 ni kuwa muungano huu ni kuna kero za muda mrefu na anasema kuwa kuna kero zishatatulika.

Serikali ya tatu ya nini wakati kero zinatatulika.

Anasema kuwa s3 haijaja lakini tayari ina kero 6,yanini kuwa muungano wa s3 ambayo tayari ina kero sita wakati kero za s2 zinatatulika.

Anasema cuf imefika bara na kumezwa na ukawa,wametoka zanzibar na asilimia 65 ya serikali ya mkataba lakini walivyofika bara wakamezwa na chadema.

Anasema chadema imewapa cuf majina tofauti na cuf wamejisahau kuwa chadema ndiyo inayoibomoa zanzibar.

Anasema amiri jeshi mkuu wa tanzania ni mmoja na ni rais wa JMT hivyo tundu lissu asipotoshe.

Anasema miaka hamsini hii ya muungano hawapaswi kustuka maana mtu mzima hatishiwi nyau.


Mh. Mch. Ernest Kadiva

Anaanza kwa kumshukuru Mungu.

Anasema wanatakiwa kuunda katika ya wananchi wote na yenye misingi madhubuti ya kusimamia nchi kwa muda mrefu.

Anasema taifa linaeza kuporomoka muda wowote kama haina msingi ulio imara na hivyo msingi lazima ulindwe.

Anasema kuwa ili taifa liweze kuvunjika lazima ikatwe mizizi imara ya msingi wa taifa hivyo taifa litatetereka.

Anapendekeza kuwa JMT ni nchi inayomtambua Mungu,Isiyo na dini na isiyoruhusu uchafuzi (kashfa) za kidini.

Anasema dini ni msingi imara wa ustawi wa nchi.

Anasema kama wosia wao bado una mantiki katika muundo huu wa serikali mbili basi bora uenziwe.

Wananchi wanataka kuona uchumi ulioimarika na mfumo watakaoutaka basi uhakikishe unazingatia na namna ya kuimarisha uchumi ambacho ndo wananchi wanachotaka kuona.


Mh. Prof Lipumba

Anasema yeye ni muumini wa dini ya mwenyezi Mungu hivyo ni muumini wa mapendekezo yaliyoletwa na tume ya Warioba.

Anamnukuu Lukuvi alivyoenda kanisani na kuwaasa waumini waupinge muundo wa S3 lasi hivyo nchi itataliwa na jeshi,anasema Lukuvi aliwasilisha maoni ya Waziri mkuu.

Anasema km zanzibar wangetaka muundo wa s1 moja basi wangekuwa na muundo wa serikali moja lakini wazanzibar hawati muundo huo,anasema wanataka muungano utakaokuwa na maridhiano.

Anasema wanahitaji katiba itakayokuwa sawa kwa wananchi wote maana ndo msingi ulioachwa na mwl Nyerere.

Anasema ni fedhea kwa waziri kwenda kusema kanisani kuwa cuf zanzibar wanataka muungano utakaoifanya zanzibar kuwa nchi ya kiislam.

Anasema watatumiaje bajeti kubwa kukarabati ukumbi wakato wanajua katika hawaitaki.

Anasema wamechoka ubaguzi na kudharau maoni ya wananchi.

Anasema watu wote wanaokubaliana na maoni ya wananchi wanaondoka bungeni na kuwaacha wao wajadili katiba wanayoitaka.


Wabunge wengi wameondoka ndani ya ukumbi wa bunge na makamu mwenyekiti anasema kuwa wakati wanaanza kikao cha bunge kolamu ilikuwa imetimia hivyo kanuni inawaruhusu kuendelea na kikao.


Mh. Nyangwine Nyambari,

Anasema kuwa tume ilikuwa ishapanga maoni yao binafsi na sio maoni ya wananchi.

Anasema wajumbe walioondoka ni wanafiki wakubwa na wamemsaliti mwalimu Nyerere.

Anasema historia ya zanzibar inapotoshwa sana kwa makusudi,ananukuu kitabu fulani na kusema kilichoandikwa ni uongo na kinapotosha historia ya zanzibar.

Anasema mwl nyerere amesaidia nchi nyingi kupata uhuru hivyo hawezi kuwa na njama hasi juu ya wanachi.

Anasema kwakuwa wapinzani wameondoka hivyo wao waliobaki waongozwe na utashi kuweza kufanya yaliyo mema kwa wananchi.

Anapendekeza kuwa alama za taifa waongeze nembo ya simba maana simba ni mkali na watoe ya twiga aliyekaa kizembe.

Anazungumzia pia kuhusu tunu ya taifa na kupendekeza vipengere vya kuongezwa.

Anasema wale wanaotishia kuwa bila serikali 3 hakuna utawala bora na wanatumia nguvu nyingi na ubabe basi wapuuzwe hawana jema kwa wananchi.


Mh. Ole Nasha,

Kwa ujumla anazungumzia masuala ya ardhi na wafugaji na ugomvi unaosababishwa na sera mbaya ya ardhi na kupelekea mauaji baina ya wafugaji na wakulima.

Anasema Tz imejaliwa rasilimali za wanyamapori lakini haziwasaidii wananchi walio wengi.


Mh.

Anaungana na walio wengi kwa kuendelea kuwepo serikali mbili.

Serikali mbili ndiyo imeleta amani na maendeleo ya Tanzania hivyo haungano na muundo wa s3.

Anasema wapinzani wanapotosha kwamba s3 ndiyo italeta maendeleo hapa hilo ni uongo.

Anasema kuimarisha muungano sio lazima kuwe na serikali tatu hizi mbili zinatosha.

Yapo mengi ya kuyafanyia mabadiliko ambapo kama wajumbe waliotumwa na wananchi kuibadili katiba itakayoleta maendeleo kwa wote.

Anasema wapinzani hawawatakii muungano na kuwatakia mema wananchi wa tanzania.


Mh. Mwagachi,

Anasema amesononeka sana wapinzani kutokaa kusikiliza mjadala huu hivyo hatendi haki kwa wale waliokuja kuwawakilisha.

Anasema waasisi wetu wanastahiki heshima kubwa pamoja na kuwa na mapungufu machache,ila walifanya yaliyo mema hapa.

Anasema ameshangaa kuwa kuna watu wanasema kuwa mwl Nyerere sio mtakatifu wakati dunia nzima ipo kwenye mchakato wa kumfanya kuwa mtakatifu.

Anasema waasisi wetu kwenye Berlin conference waliwasuta wale watu kuwa waafrika wanaweza kujitawala bila tatizo.

Anaunga mkono serikali mbili na washindane kwa hoja kutetea maoni yao na sio kwamba nataka serikali mbili au tatu bila hoja.

Anasema hawawezi kuwapa watanzania mzigo wa kuendesha mzigo wa watu miliono 43 alafu wawaongezee mzigo mwingine wa serikali tatu,yaani marais watutu,waziri wakuu watatu, makamu wa rais watatu pamoja na familia zao.

Katika mfumo huu wa vyama vingi vyama vinakwenda kwa wananchi kuomba sera zao na ndiyo wananchi wanazotaka na sio sera zitakazoleta mkanganyiko.

Viongozi imara wanatetea umoja siku zote,muungano na umoja umedumu kwa miaka 50 na tunaweza kuongeza miaka mingine mingi kwa kudumisha muungano huu wa serikali mbili.


Mh. Cyril Chami,

Anazungumzia kuhusu takwimu za watu watu waliotoa maoni katika tume ya Warioba.Anasema takwimu zilizotolewa zinaondoa uhalali wa kutumika maana kuna maoni ya watu wengi yameachwa. Badala Tume ikaja na takwimu kwamba watu walio wengi walipendekeza muundo wa s3.

Taasisi ya CCM yenye wanachama 6,500,000 wapo wengi na maoni yao hayajachukuliwa eti tume inakuja na watu 47 elfu eti ndio wamependekeza s3,haoni taasisi ya ccm ni kubwa kuliko hao wanaotaka s3.

anawaomba watu wote wanaopendea mema nchi hii kuwa macho na hao wapinzani wanaotaka kuharibu muungano huu kwa kupotosha.


Mh. Zainab Gama,

Anasema wapinzani walitaka kuondoka wakisingizia hati ya muungano hakuna,hati imekuja bungeni wamekosa kisingizio na kuamua kuondoka.

Anasema wao waliobaki baada ya wapinzani kuondoka wamebaki wengi hivyo anaomba wahakikishe muundo wa s2 unasimama.

Anazungumzia takwimu za maoni ya tume ya jaji warioba na kuyakosoa kuwa ni ya uongo hayana ukweli.

Anasema kuwa tume imedanganya kuwa watu wengi wanataka serikali tatu,anasema tume ina wasomi,majaji lakini wameshindwa kukotoa hesabu ndogo.

Anasema tume imekula rushwa hivyo inataka kusaritisha nchi hivyo isikubalike kamwe.

Anasema kuwa wao kundi 201 waliokuja kuwakilisha wananchi wanajua kuwa wamekuja kuwakilisha kweli.

Anaomba wakae na wabadilishe ili rasimu iwe na nguvu ili wavuvi,wakulima na wanawake wawe na nguvu.

Anamsihi rais Kikwete kuwa hawa waliotoka wasiende kwake kumpigia magoti maana wamemsaliti na posho wanyang'anywe.


Mh. Zena

Anasema yeye ni muumini wa s2 ya mapinduzi ya zanzibar na jamhuri ya muungano wa tanzania.

Anasema baada ya miaka hamsini pemba na unguja imepata maendeleo kama elimu bure,afya na barabara hivyo muungano huu kwake una maendeleo.

Anasema wapinzani wanasema wanabanwa kwenye hizi serkali mbili lakini wataendelea kubanana hapahapa kwenye muundo huu wa s2.

Muungano wa s2 ni halali kweli tena halali ya juu.

Anasema anayoitaka zanzibar yake ataipata huko lakini sio hii ya muungano.Rais Shein kafanya mambo mengi zanzibar imeng'ara.

Anawapongeza waasisi wote na wanaowatukana waasisi hawa hukumu yao ipo.

Anasema mh. Kikwete akija zanzibar sio kweli anapanga foleni,huo ni uongo anakuja ikulu kwa raha mstarehe na anafurahia.

Kikwete akienda kule kuna sheria zake na hata Shein akija bara kuna sheria zake hivyo upinzani waache upotoshaji.

Anasema pemba na unguja wote wanataka serikali mbili na huu mwaka wa 50 hakujatokea tatizo lolote.

Anasema zanzibar watatue matatizo yao na km wakishindwa basi waombe msaada upande wa pili wa muungano.


Mh. Faida Bakary

Anaanza kwa kusema wamewashinda kwa hoja wapinzani mpaka wakaamua kutoka.

Mimi ni muumini wa serikali mbili vile vile muumini wa CCM ambayo inaongoza muungano huu wa s2.

Anasema anaunga muungano huu maana una faida nyingi ambazo ameziona tangu azaliwe.

Muungano huu umeasisiwa na hayati Karume na Nyerere,umeleta muungano,amani na upendo eti baada ya miaka hamsini wanataka tuuvunje!!

Wazanzibar sasa wako bara na wabara wako zanzibar wamedumisha mshikamano tunataka nini tenaaaaa!!

Ananukuu kifungu kinachoupa uhalali muungano huu,uliondikwa na mwl Nyerere.

Anasema tume ya warioba ilipewa rejea sasa iweje leo waje na maoni yao na kuunyong'oa huu muungano?

Wapinzani pia walaaniwe kwa kutaka kuuvunja huu muungano na Mungu atawalipa.

Anasema kule pemba kuna miradi mingi mikubwa na yote hii miradi ya muungano iliyotuunganisha

Anasema anawakilisha wananchi wa pemba na wananchi wa pemba wanataka serikali mbili na sio tatuuu!!


Mh. Amina Mweta,

Anapendekeza kuwa uhujumu uchumi na ujangili pamoja na dhuruma zote ziondolewe nchini anapendekeza maneno haya yaingie kwenye katiba.

Anasema katika tunu za taifa liongezwe neno demokrasi na pia usawa wa jinsia.

Muundo wa muungano ni vizuri watanzania wakaelewa historia fupi ya tanzania hata tume kabla ya kuandika rasimu iliangalia historia taifa letu.

Anasema tume imekiri pia kuwa jina tanganyika tulikuja kupewa na wakoloni waliotutawala,hapo mwanzo tulikuwa pamoja na rwanda na burundi.Anashanga kuwabeza waasisi ambao walituletea muungano hu.

Anasema pia kuleta muundo wa s3 moja kwa moja ni kuuvunja muungano,hivyo anashangaa mapendekezo.

Anasema kuongeza s3 ni matatizo mfano maraisi wa tanzania,zanzibar na muungano watoke vyama vitatu tofauti kweli patakalika,mfano tukiangalia hapa bungeni jinsi ilivyo.

Anasema wananchi wanapenda serikali mbili ziendelee kuongoza nchi hii.


Mh. Jaji Simai Jaji,

Anasema serikali tatu ni misingi ya kuvunja muungano maana haamini kuwa hawa wote hawaamini kumwa s3 itavunja muungano

Anasema kuwa maoni ya serikali tatu sio ya wazanzibar bali wanasiasa waliowarubuni wananchi ambao hawajui wataenda kuzungumza kitu gani.

Anawashangaa hao wanasiasa kuja na mfumo wa s3 na huku wakijua chini ya mfumo huo mamlaka kamili ya zanzibar hayawezi kupatikana.Wamewadanganya wananchi.

Watu hao wamekuja na maono ya muungano wa mkataka na hilo limethibitishwa na mjumbe mmoja aliyeongea asubuhi.

Anasema hilo haliwezekani na wao ndio wazanzibar wenyewe.

Muungano wa s3 ni rahisi kuvunjika maana zanzibar haina uwezo wa kwenda kugharamikia serikali ya tatu,hawana uwezo huo kamisa na niz mzigo ambao hawana haja nao.

Anawashukuru wabara kwa uvumilivu pamoja na kuambiwa kuwa wabara wamevaa koti la muungano,anasifu wana haki hiyo maana wao wamechangia asilimia kubwa ya rasilimali.

Jusa alisema kuwa endapo s3 haitopita basi watawaambia wananchi kuandamana kudai muungano wa mkataba na anasema kama muundo huo wa s3 tatu kama umeshindwa kupita hapa bungeni basi hata huo wa mkataba hauwezi kufanikiwa.

Anamalizia kwa kusema s2 ndio suluhisho pekee la kuufanya muungano huu undelee kudumu.Bila s2 basi muungano huu tutauzika.


Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa,

Anasema ni mjumbe kati ya wajumbe 201 na ni mwakilishi wa taasisi ya Anglikana na ameagizwa na askofu kusema haya,

Muundo wa mamlaka kamili ya tanzania yawe ya muungano wa s2.

MATOKEO YAPO HAPA: Real Madrid vs Barca, Man city vs Sunderland

$
0
0


Ni game nyingine ambazo zilikua zinasubiriwa sana hasahasa hii ya hawa wa Hispania ambayo iliingia kwenye headlines mara kadhaa baada ya Ronaldo kutangazwa majeruhi ambae hatocheza.
Screen Shot 2014-04-17 at 12.50.17 AM
Screen Shot 2014-04-17 at 12.58.34 AM
Screen Shot 2014-04-17 at 1.06.35 AM

MAMBO YAMEBADILIKA UKIMYA ULITAWALA JANA UKAWA WASUSIA BUNGE... SOMA HAPA

$
0
0
Dodoma. 
Mambo yamebadilika. Ukimya ulitawala jana katika Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya wabunge zaidi ya 200 ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kususia vikao vya Bunge hilo.



Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Prof Ibrahimu Lipumba akizungumza katika kikao cha bunge jana ambapo alitangaza kujitoa kwa baadhi ya wajumbe kuendea na mchakato wa kupitisha Rasimu ya Katiba, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi 

Ilikuwa ni saa 10:31 jioni baada ya Mjumbe wa Bunge hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba alipohitimisha uchangiaji wake akisema: “Ukawa hatuwezi kuendelea kushiriki dhuluma dhidi ya wananchi kwa kupitisha Katiba ambayo ni kinyume cha matakwa yao.”


Baada ya kauli hiyo aliondoka akifuatiwa na Mwenyekiti wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia na wajumbe wao kutoka nje ya Bunge.


Ukimya ulitawala takriban dakika mbili hivi na baada ya wajumbe hao kutoka, Makamu 
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samia Suluhu Hassan aliwaelekeza makatibu kuhesabu wajumbe ili kuona kama akidi imetimia ili waendelee na kikao.


Baadaye aliliambia Bunge kuwa makatibu wamemweleza hawahitaji akidi kwa kuwa kikao kilikuwa kinaendelea wakati Ukawa walipotoka nje ya ukumbi.

Hotuba ya Lipumba


Profesa Lipumba alianza kwa kunukuu Gazeti la Mwananchi la Aprili 14, mwaka huu katika sehemu inayosema; “Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) ameanza kampeni kanisani kwa kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa serikali ya muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.”


Alisema yeye ni muumini wa dini ya Mwenyezi Mungu lakini anaafiki mapendekezo yaliyoletwa bungeni hapo na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoundwa na Rais.

“Hii ni kauli ya Waziri Lukuvi ndani ya Kanisa la Methodist wakati wa sherehe ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa Askofu na Waziri Lukuvi alikuwa anamwakilisha Waziri Mkuu.”


Alisema inasikitisha kwa sababu kauli hiyo inafanana na ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati akihutubia Bunge Maalumu.

Alisema kauli za Lukuvi zinatisha baada ya kusema Wazanzibari ambao wanataka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka wapate nafasi ya kujitangazia kuwa ni nchi ya Kiislamu.

“Waziri anaweza kusema hivyo ndani ya kanisa? Kawahamasisha mpaka yule kiongozi wa kanisa akasema ili kudumisha Muungano bora Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano,” alisema.

Alisema Lukuvi alikuwa akiwaaminisha kuwa mfumo wa serikali tatu ukipita kutakuwa na mapinduzi na nchi haitatawalika na hivyo watu watashindwa kwenda kusali makanisani.

“Kama ndugu zetu wa Zanzibar wangekuwa wanahitaji serikali moja tungekuwa na utaratibu mzuri tu, lakini siyo wanachama wa CUF, siyo wa CCM, Wazanzibari wote hawataki muungano wa serikali moja,” alisema.

Alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa mapendekezo ya serikali tatu kutokana na ukweli huo. “Hoja zilizoletwa hapa ni hoja za serikali moja, si hoja za serikali mbili lakini wenzetu moja hawataki, kwa hiyo tunahitaji Muungano ambao tutakuwa na maridhiano ya pande zote mbili,”

“Wengi wamenukuu makala niliyoitoa katika kituo cha TCD (Kituo cha Demokrasia Tanzania), ambayo iliunda Baraza la Katiba na mimi nilichambua mapendekezo ya Tume nikasema kwa mapendekezo yaliyomo ndani ya Rasimu ya Katiba hayatakidhi mapato ya shirikisho.”
Alisema wajumbe wanaomnukuu wanaishia hapo bila kwenda katika mapendekezo aliyoyatoa.

“Wamenisifu sana ni mchumi mahiri, basi waendeleze sifa hizo kwa mapendekezo niliyoyatoa ya mapato ya kukidhi uendeshaji wa serikali ya shirikisho.
“Nimeeleza katika hali halisi kuwa utaratibu mzuri ni mapato ya kila serikali kuchangia katika shirikisho na mambo haya yaandikwe katika Katiba. Katiba inaweza ikasema wazi asilimia 20 ya mapato yote yanayokusanywa Zanzibar au Tanganyika yataenda kwenye shirikisho.”

Alitaka pia kuwekwa kwa misingi mizuri ya kukusanya kodi na kutumia fedha za wananchi ndani ya katiba ya muungano ambayo ndiyo katiba mama.

“Lakini ndugu zangu mjadala wetu unavyokwenda utadhani kuwa Rasimu ya Katiba iliyoletwa imeletwa na CUF au na Chadema au na NCCR-Mageuzi, au Wapemba,” alisema.
Alisema ukurasa wa kwanza wa Rasimu ya Katiba unaeleza kuwa toleo hili la Rasimu ya Katiba lilichapishwa katika Gazeti la Serikali kwa mujibu wa Kifungu cha 20(2) ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83.

Alisema hiyo ni rasimu ya Tume ya Rais na si rasimu ya Wapemba.
Hata hivyo, alisema mjadala unaoendelea bungeni umekuwa na utaratibu wa ubaguzi... “Watu wamebaguliwa humu na viongozi wakubwa wanapiga makofi, Bunge hili limekuwa kama Bunge la Intarahamwe. Hii ni hatari kwa nchi yetu. Wapemba, Waarabu, Wahindi, Wakongo,” alisema.

“Hii hatuhitaji, tunahitaji katiba ambayo itahakikisha kila mwananchi anapata haki yake wote tuwe sawa bila kujali rangi zetu, jinsia zetu, makabila yetu, huu ndiyo msingi aliotuachia Mwalimu Nyerere tuenzi msingi huo.”

Alilalamikia kile alichokiita kuwa ni ubaguzi ndani ya Bunge na kwamba kama Serikali haikutaka Katiba Mpya kwa nini imepeleka wabunge Dodoma? Pia alihoji ni kwa nini ilitumia Sh70 bilioni katika Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

“Kwa nini mmetufikisha hapa? Jengo hili nimeambiwa limekarabatiwa kwa Sh8.2 bilioni hali hamuamini Rasimu ya Katiba ama ilikuwa ni utaratibu wa kupata hizo asilimia 10, ndiyo maana mmekarabati kwa gharama kubwa?” alisema.

“Tunataka CAG (Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali), akague matumizi ya fedha zilizotumika. Utatumiaje fedha nyingi wakati hiyo katiba iliyowasilishwa kumbe huitaki kabisa.

“Hakuna utaratibu wowote wa kupiga kura na kufanya maamuzi kuhusu sura hizi mbili. Tumechoka kusikiliza matusi. Tumechoka kudharau mawazo ya wananchi, tumechoka ubaguzi, hatuwezi kuwa sehemu ya kundi linalohamasisha ubaguzi ndani ya Tanzania hili hatukubali,” alisema.
CREDIT: MWANANCHI

MASSACRE (MAUAJI YA HALAIKI) SEHEMU 01

$
0
0
Na Nyemo Chilongani
Kila aliyekuwa akizisoma taarifa ambazo zilikuwa zimeandikwa katika magazeti mbalimbali yaliyokuwa yakitoka katika siku hiyo alibaki akishangaa tu. Watu wakashtuka kupita kawaida, habari ile ilionekana kuwasisimua kupita kawaida. Imani juu ya wachungaji ikaanza kuondoka katika mioyo ya watu, hasa waumini wa dini ya Kikristo.
  
 Kanisa likaonekana kupotea njia, kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea hasa katika makanisa mbalimbali kilionekana kuwa kama maigizo juu ya jukwaa au ndani ya luninga. Shetani akaonekana kuliteka kanisa na kulifanya alivyotaka kulifanya. Dhambi ambayo ilionekana kufanyika kwa kiongozi mmoja wa kanisa moja ikaonekana kama imetokea katika makanisa yote nchini Tanzania. Watu wengine wakataka kujitoa kutoka katika imani ya Kikristo kwa kudai kwamba shetani alikuwa amemzidi nguvu kila mtu.
 Wokovu wote ambao ulikuwa ukiendelea katika makanisa yote ukaanza kuyumba. Watu wengine wakaahidi kutokuhudhuria tena makanisani mwao kutokana na imani juu ya viongozi wao kuanza kupotea. Idadi kubwa ya watu wakaanza kupoteza uaminifu wao juu ya wachungaji wa makanisa yao.

  MCHUNGAJI ATAKA KUMBAKA BINTI OFISINI’. Hicho kilikuwa ni kichwa cha habari ambacho kilikuwa kikisomekana katika magazeti mbalimbali jijini Dar es Salaam. Bado watu walikuwa wakiendelea kushangaa, hawakuamini kama mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge angeweza kufanya kitu kama kile ambacho kilikuwa kimeonekana kuandikwa katika magazeti mengi.

  Habari ile ilionekana kuwa habari iliyokuwa na furaha kwa watu wote ambao walikuwa hawawapendi Watumishi wa Mungu. Watu wakaanza kupeana taarifa majumbani mwao huku kila aliyepewa taarifa ile akaanza kuelekea barabani kulinunua gazeti moja ambalo lilikuwa na habari ile.

  Katika mwaka mzima, habari ile ndio ambayo ilifanikiwa kuuza nakala nyingi kuliko habari yoyote iliyowahi kuandikwa katika mwaka huo. Mpaka inafika saa saba mchana, hakukuwa na gazeti lolote lililokuwa na habari ile ambalo lilikuwa katika meza ya wauza magazeti.
  
 Kila mtu ambaye alikuwa akiyaona magazeti yale, aliyanunua. Siku ya mwisho ikaonekana kukaribia kutokana na shetani kuonekana kulivamia kanisa hasa kwa viongozi mbalimbali wa makanisa. Aibu kubwa ikaanza kulikumba kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge.
  
 “Haiwezekani hata kidogo. Mbona huyu Mchungaji ni Mtumishi mzuri wa Mungu! Tena kwa sasa anataka kuwa Askofu Mkuu. Hawezi kufanya hivi” Sauti ya msichana mmoja ilisikika ikiwaambia wenzake huku mkononi akiwa ameshika Biblia katika kipindi ambacho walikuwa wakitoka kanisani siku hiyo ya Jumapili.
  
 “Kwa nini isiwezekane kwa mtu kama huyu kufanya hivi? Tumemkaribisha shetani sisi wenyewe. Acha awatumie watumishi wa Mungu anavyotaka” Mwanamke mmoja alisikika akisema huku akishika vizuri Biblia yake.

  Habari hiyo ndio ambayo ilikuwa imeshika hatamu katika kipindi hicho. Kila mtu ambaye alikuwa akiiona habari ile na kuisoma, alishtushwa kupita kiasi. Picha kubwa ya rangi ya mchungaji Matimya ilikuwa ikionekana vizuri katika kila gazeti ambalo lilikuwa na habari ile.
                                                            ****
   Mchungaji Matimya alikuwa amekaa katika kiti cha nyuma kabisa ndani ya kanisa lake. Uso wake alikuwa ameuinamisha chini huku machozi yakimtoka. Mbele yake aliiona aibu kubwa ikiwa imemkuta, hakuelewa ni kitu gani ambacho alitakiwa kukifanya ili Watanzania waelewe kwamba hakuwa amekifanya kile kitu ambacho kilikuwa kikitangazwa sana na vyombo vya habari.
  
 Hakukuwa na mtu ambaye alionekana kumuamini Mchungaji Matimya, kila mtu kanisani humo alimuona kuwa kama Mwakilishi wa shetani ambaye aliletwa kanisani humo kwa ajili ya kulitia aibu kanisa. Ingawa ibada ilikuwa ikiendelea kanisani humo, macho ya washirika wengi walikuwa yalikuwa yakimwangalia Mchungaji Matimya.

   Machozi yale ambayo yalikuwa yakimtoka, yalionekana kuwa kama ya kinafiki machoni mwa washirika wa kanisa lile. Mchungaji Matimya hakuwa peke yake, familia yake ilikuwa pembeni yake. Mkewe, Bi Meriana alikuwa upande wake wa kushoto huku watoto wake wawili, Benedict na Angelina wakiwa katika upande wa kulia.

  Kilio cha chini chini kilikuwa kikisikika kutoka kwa Bi Meriana. Kila alipokuwa akikumbuka aibu ile ambayo ilikuwa imemkuta mumewe, alizidi kuumia. Hawakuonekana kufuatilia kitu chochote kilichokuwa kinaendelea kanisani mule. Vichwa vyao vilikuwa vikifikiria mbali.
  
 Ibada iliendelea kama kawaida. Mara baada ya muda wa matangazo kuingia, Askofu wa dhehebu hilo la Praise And Worship, Askofu Lugakingira akasimama na moja kwa moja kuelekea katika madhabau ya kanisa hilo na kuchukua kipaza sauti. Kabla hajaongea kitu chochote kile, alitulia kwa muda huku akiliangalia kanisa.
    
Kila mtu alikuwa kimya tayari kwa kusikiliza kile ambacho Askofu alitaka kukizungumza mahali hapo. Askofu alianzia mbali sana lakini huku lengo lake kubwa likiwa ni kufika katika kitu ambacho kilimfanya kuja katika kanisa lile katika siku hiyo ya Jumapili. Mara baada ya kutumia dakika kumi kuongea mambo tofauti tofauti, hapo hapo akamtaka Mchungaji Matimya kwenda mbele ya kanisa lile.
  
 Huku akionekana kuwa katika lindi la mawazo, Mchungaji Matimya akainuka kutoka katika kiti alichokuwa amekaa kule nyuma ya kanisa na moja kwa moja kuanza kuelekea mbele ya kanisa. Minong’ono ikaanza kusikika kutoka kwa washirika ndani ya kanisa lile, Mchungaji Matimya hakuonekana kujali, aliendelea kupiga hatua hadi mbele ya kanisa lile.
  
 “Nadhani hakuna mtu asiyejua kitu ambacho kimenifanya kuja ndani ya kanisa hili kwa siku ya leo. Lilikuwa ni suala ambalo lilihitaji kumuita Mchungaji Matimya. Niliongea nae kwa kirefu sana na kukiri kila kitu pasipo kuficha kitu chochote kile” Askofu Lugakingira aliliambia kanisa na kuendelea.
  
 “Ningependa kumpa nafasi ya kulieleza kanisa kama hiki kitu ambacho kimetawala kila sehemu ni kweli au kuna uongo wowote” Askofu Lugakingira alisema na kisha kumpa kipaza sauti mchungaji Matimya.

  Mchungaji Matimya hakuongea kitu chochote kile, alibaki kimya huku macho yake yakiangalia chini. Kila alipotaka kuongea kitu, aliuona mdomo wake kuwa mzito kufunguka, hakujua aseme kitu gani mbele ya kanisa na mbele ya familia yake. Kumbukumbu ya maisha yake ya nyuma ikaanza kujirudia kichwani mwake, katika hatua nyingine, alijuta kwa nini aliitwa kuwa Mchungaji.

  “Nalihitaji kanisa msamaha. Ni kweli nilitaka kumbaka Judith ndani ya of….” Mchungaji Matimya alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, akaanza kulia. Sauti ya kilio chake kilisikika kanisa zima kutokana na kipaza sauti alichokuwa amekishika. Wanawake wakashindwa kuvumilia, nao wakaanza kulia.
  
 Mtoto wake, Benedict hakuweza kuvumilia kubaki kanisani hapo akasimama na moja kwa moja kuanza kuelekea nje ya kanisa lile. Moyo wake uliumia kupita kiasi, maneno ambayo aliongea baba yake mbele ya kanisa yalionekana kumuumiza kupita kawaida.
  
 Mara baada ya kufika nje ya kanisa, moja kwa moja akalifuata gari lao na kuingia ndani na kisha kuliwasha. Kila mtu ambaye alikuwa nje ya kanisa alikuwa akimwangalia Benedict ambaye akaliwasha gari lile na kuondoka katika eneo lile la kanisa.

  Mchungaji Matimya akashindwa kuendelea, akakikabidhi kipaza sauti kwa Askofu Lugakingira ambaye alikuwa akimbembeleza kwa kumpiga piga mgongoni. Mchungaji Matimya akazidi kulia zaidi na zaidi, akapiga magoti chini huku uso wake akiwa ameuinamisha chini kwa aibu huku machozi yaliyokuwa yakimtoka kuloanisha sakafu ya pale madhabahuni.

  “Kila kitu kina sheria zake. Na hili kama dhehebu la Praise And Worship, mchungaji Matimya hatokuwa mchungaji wa kanisa hili tena. Tunamfungia kufanya huduma yoyote kwa muda wa mwaka mmoja na nusu” Askofu Lugakingira aliliambia kanisa.

  Idadi kubwa ya washirika ikaonekana kufurahia. Thamani ya mchungaji Matimya ikaonekana kushuka. Pepo la uzinzi likaonekana kumvaa mchungaji Matimya ambaye bado alikuwa pale mbele ya kanisa akiendelea kulia kwa uchungu. Kila kitu ambacho kiliendelea katika maisha yake kilionekana kuwa kama ndoto ambapo baada ya muda fulani angeamka kutoka katika usingizi mzito.
****
   Uchaguzi wa Askofu mkuu ndio ambao ulikuwa ukikaribia, siku tano tu ndizo ambazo zilikuwa zimebaki kabla ya uchaguzi huo. Wachungaji wawili, mchungaji Matimya wa kanisa la Praise And Worship la Mwenge lililoko jijini Dar es Salaam pamoja na mchungaji Mwakipesile wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Morogoro ndio ambao walikuwa wakiwania nafasi ya kuwa Askofu mkuu nchini Tanzania.
  
 Kila mtu alionekana kuwa na nafasi nzuri ya kuchukua nafasi hiyo lakini mchungaji Matimya ndiye ambaye alionekana kuwa na nafasi kubwa zaidi. Kila kanisa la dhehebu la Praise And Worship lililokuwa nchini Tanzania, jina la mchungaji Matimya ndilo ambalo lilikuwa likitajwa mara kwa mara.
   Wachungaji wengi walikuwa wakitamani Mchungaji Matimya achukue nafasi hiyo kutokana na huduma nzuri ambayo alikuwa akiitoa katika kanisa lake na makanisa mengine mbalimbali nchini. Hakuwa na roho ya majivuno kama aliyokuwa nayo mchungaji Mwakipesile.

  Kila mtu alivutiwa nae, kila mtu akatamani mchungaji Matimya achukue nafasi ile na kuwa Askofu mkuu. Asilimia zaidi ya themanini ya wachungaji wote wa dhehebu hilo walitamani mchungaji Matimya achukue nafasi hiyo ambayo ilitarajiwa kuachwa na Askofu Lugakingira siku chache zijazo.
   “Ni lazima nifanye kitu” Mchungaji Mwakipesile alijisemea huku akionekana kukasirika.
   Mbele yake hakuona dalili zozote za ushindi katika nafasi ya Uaskofu. Baadhi ya wachungaji ambao walikuwa katika upande wake, katika kipindi hicho walikuwa wamemsaliti. Kila kitu katika kipindi hicho kilionekana kwenda tofauti na matarajio yake ya nyuma.

  “Nitamtumia hata mshirika wake mwenyewe” Mchungaji Mwakipesile aliendelea kujisemea.
   Hakutaka kuendelea kubaki Morogoro, kitu alichokifanya siku iliyofuata ni kuchukua ndege na moja kwa moja kuanza kuelekea jijini Dar es Salaam. Hakutaka mtu yeyote afahamu juu ya safari yake hiyo ya ghafla, hakumpa taarifa hizo mtu yeyote zaidi ya msichana mmoja tu, Judith Simon ambaye alikuwa akiishi ndani ya jiji la Dar es Salaam.
*****
   Jina la Judith Simon wala halikuwa geni masikioni mwa washirika wa kanisa la Praise And Worship lililokuwa Mwenge. Binti huyu alikuwa na sifa zote ambazo msichana wa kisasa na mrembo alitakiwa kuwa nazo. Alikuwa na wembamba kama waliokuwa nao wasichana ambao walikuwa wakigombania nafasi ya kuwa mrembo wa Tanzania.

   Uso wake ulikuwa mwembamba, alikuwa akitembea kwa mwendo wa mapozi kana kwamba alikuwa hakanyag ardhi. Kila aliyekuwa akiuangalia mwendo wa Judith alikiri kwamba binti huyo alikuwa akitembea mwendo uliokuwa na mvuto kanisani hapo.
   Mashavu yake yaipendezeshwa na vishimo viliwili vilivyokuwa mashavuni mwake ambavyo vilikuwa vikionekana vizuri katika kila wakati alipokuwa akicheka au kutabasamu. Kila wakati Judith alionekana kuvutia.

  Uzuri wake ulikuwa ukionekana wakati wote. Haijalishi alikuwa amekarika, amenuna au ametabasamu, muda wote huo uzuri wake wa asili ndio ulikuwa ukionekana machoni mwa watu wengi.
  
 Judith alionekana kuwa mcha Mungu. Karama ya Uimbaji ambayo alikuwa nayo ndio ambayo ilimfanya kuzidi kukubalika katika kanisa hilo lililokuwa likiongozwa na mchungaji Matimya. Judith akaamua kujiunga na kwaya mojawapo iliyokuwa kanisani hapo. Kila mtu alionekana kubarikiwa katika vipindi vyote ambavyo Judith alikuwa akimsifu Mungu. Judith alikubalika na kila mtu kanisani hapo.

  Vijana hawakutaka kubaki nyuma kanisani hapo, harakati za kumtaka Judith zilikuwa zikiendelea kimya kimya kanisani hapo. Judith hakutaka kujirahisisha kwa wavulana kitu ambacho kiliwapelekea vijana wengi kusimamishwa huduma kanisani humo.
   “Watu wakijua?” Judith alimuuliza mchungaji Mwakipesile huku akionekana kuwa na hofu. Mchungaji Mwakipesile hakuongea kitu chochote, alibaki akimwangalia Judith na kisha kutoa tabasamu.
  
 “Utawaambia au?” Mchungaji Mwakipesile alimuuliza.
   Swali lile likaonekana kuwa gumu kwa Judith, alibaki kimya huku akimwangalia mchungaji Mwakipesile ambaye alionekana kumaanisha kile alichokuwa akikiongea kwa wakati huo. Alipoona Judith amekaa kimya, akachukua glasi iliyokuwa na juisi ya maembe na kisha kupiga fundo moja.
   “Kama hautowaambia nina uhakika hawatojua” Mchungaji Mwakipesile alimwambia Judith ambaye kwa kiasi fulani woga wake ukaonekana kupungua.
   “Na vipi kuhusu malipo?” Judith aliuliza.
   “Milioni tano baada ya kukamilisha kazi hii” Mchungaji Mwakipesile alijibu.
   “Sawa” Judith aiitikia na moja kwa moja kuondoka huku akijiandaa na kazi ambayo alitakiwa kuifanya.
****
   Alipomaliza kuongea na viongozi mbalimbali wa kanisa lake, mchungaji Matimya akaanza kuelekea katika ofisi yake iliyokuwa pembeni ya kanisa hilo. Alipoingia ofisini mwake, akaanza kuifuata kiti chake na kukalia, akaichukua Biblia ambayo ilikuwa mezani na kuanza kusoma baadhi ya maandiko.
  
 Alitulia kimya huku akiendelea kupitia baadhi ya maandiko. Mara kwa mara uso wake ulikuwa ukionyesha tabasamu kila alipokuwa akisoma andiko ambalo lilionekana kumvutia. Alitumia muda wa dakika thelathini kuyasoma baadhi ya maandiko ambayo alikuwa ameyadhamiria kuyasoma katika kipindi hicho. Alipomaliza kuyasoma maandiko hayo, akaifunika Biblia yake na kuanza kusali.

   Huku akiwa katikati ya sala, mara mlango ukasikika ukianza kugongwa kitu ambacho kilimpelekea kukatisha sala yake na kumkaribisha mgongaji. Mlango ukafunguiwa na msichana Judith kuingia. Mchungaji Matimya akaonekana kushtuka kwani halikuwa jambo la kwaida kwa mgeni kuingia ndani ya ofisi yake katika kipindi hicho ambacho alijiandaa kufunga ofisi yake.
  
 Judith akaanza kupiga hatua kukifuata kiti cha wageni na kisha kutulia huku kikiwa mbele ya meza ile pale ofisini. Judith hakuongea kitu chochote kile, alibaki akimwangalia mchungaji kwa kutumia macho ambayo yalionyesha mshtuo mkubwa kwa mchungaji Matimya. Mchungaji Matimya akasimama na kuanza kumsogelea Judith ambaye alibaki kimya akijifikiria namna ya kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati ule.
   
 “Kuna nini tena judith?” Mchungaji Matimya alimuuliza Judith.
   “Nina kiu mchungaji” Judith alijibu.
   “Kiu ya Neno la Mungu au?”
 Unataka niwe nakutumia CHOMEZO watu 200 wa kwanza kulike PAGE YA 2JIACHIE Mtatumiwa imbox chomezo LIKE PAGE YETU HAPA ==>www.facebook.com/2jiachie

ITAENDELEA KESHO HAPA HAPA

Zitto: Kitakachovunja Muungano si serikali tatu

$
0
0
Dodoma
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Zitto Kabwe amesema kuandikwa kwa Katiba isiyokubaliwa na pande zote kutasababisha gharama kubwa kuliko zile zinazotajwa za serikali tatu.
Akichangia hoja kwenye Bunge hilo jana, Zitto alisema kuna kila sababu ya kukaa na kukubaliana ili kupata Katiba itakayokubalika pande zote.


“Muundo wa Muungano una hatari ya kuvunjika iwapo hakuna matakwa ya dhati ya watu kuungana... Maneno ya kusema Serikali tatu zitavunja Muungano ni ya siasa na hayana msingi wa kisayansi. Urusi ilivunjika sababu haikuwa na demokrasia na siyo sababu ya idadi ya Serikali,” alisema.

Zitto ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), alisema hofu ya gharama inayotajwa katika uendeshaji wa muundo wa serikali tatu haina msingi wowote kwa kuwa hakuna ushahidi wa kitaalamu unaothibitisha gharama hizo.

“Nimesikia watu wanasema eti tutalazimika kujenga ikulu mpya, nani kasema lazima tuwe na marais watatu? Tunaweza kuwa na rais mmoja kwenye nchi na wakuu wa nchi washirika wawili… Ni jambo la makubaliano tu,” alisema.

Alisema bajeti ya mwaka huu ni Sh18 trilioni, kati ya hizo Sh5.3 trilioni ndizo zinazohudumia wizara za Muungano, lakini serikali ina uwezo wa kukusanya kodi zaidi ya Sh10 trilioni pamoja na mapato mengine.

“Kuna jumla ya Sh2.3 trilioni hatuzikusanyi kila mwaka kutoka kwenye kampuni kubwa, kwa uwezo wetu wa pato la ndani asilimia 17 tunao uwezo wa kuendesha serikali ya muundo wa idadi yoyote.
“Hofu ya Serikali ya Muungano kutokuwa na fedha ni sababu halisi, ni kweli kwamba ushuru wa bidhaa pekee yake hauwezi kutuendeshea serikali. Sasa nini kazi yetu, tunaingia hapa ili kuboresha hayo maeneo, kama hatuwezi tumekuja kufanya nini hapa?” alihoji.
Jussa akomaa

Mjumbe wa Bunge hilo, Ismail Jussa jana alisisitiza kwamba Wazanzibari wengi hawapo tayari kuendelea na mfumo wa serikali mbili kwa sababu unawatesa na kuwadhalilisha.
Jussa ambaye ni mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar kupitia CUF, alisema haoni haya kuzungumzia suala hilo kwa niaba ya Wazanzibari.
“Hoja nyingi zimetoka (kuhusu Muungano), lakini naendelea kuzungumza kwa niaba ya wananchi wa Zanzibar na katika hili sioni haya kwa sababu naamini kwamba wanakisimamia kile ambacho sisi tunasimamia nacho ni Zanzibar yenye mamlaka kamili,” alisema Jussa.

Alisema amekuwa akijiuliza kwa nini serikali mbili zinang’ang’aniwa na CCM licha ya kunung’unikiwa na baadhi ya wanachama wake kwa miaka 50?
“Hapa wala maneno hayo hayajasemwa na CUF, wala na mpinzani. Hapa ninayo Ripoti ya Amina Salum Ali ya Novemba 1992 ikiorodhesha matatizo lukuki ya mfumo wa serikali mbili na wajumbe wake hawa wote walikuwa ni kutoka CCM, mwenyekiti wake Amina Salum Ali, katibu wake Ali Juma Shamhuna ndiyo walioleta ripoti hii,” alisema Jussa huku akionyesha ripoti hiyo.
Kutokana na hali hiyo, alisema anaona ni kuwadanganya Wazanzibari kwamba serikali mbili zitatatua matatizo yao, hivyo kuwafanya wajiulize mbona hazikuyatatua kwa miaka 50 iliyopita?
CHANZO MWANANCHI
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>