Quantcast
Channel: Rogers Linky - Sports Home
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live

Taarifa Kwa Umma Toka TCU Kuhusu Mgogoro wa Chuo Cha St. Joseph (SJUIT) Kampasa ya Arusha

$
0
0

 TAARIFA KWA UMMA
MGOGORO WA CHUO KIKUU CHA MT. YOSEFU TANZANIA(SJUIT) KAMPASI YA ARUSHA

1.  Tunapenda  kuuarifu  umma  kwamba,  Chuo  Kikuu  cha  Mt.  Yosefu  Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.

2.  Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.

3. Tume  inatambua  kuwa  kwa  nyakati  tofauti  kumekuwapo  na  matukio  ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo  Arusha na wanafunzi.
Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo. 
Katika kutekeleza azma hiyo, hivi karibuni Tume iliunda jopo la wataalam kufanya ukaguzi wa kina katika Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania Kampasi ya Arusha. Ripoti ya ukaguzi huo iliwasilishwa tarehe 22/02/2016.

4.  Kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa kisheria, ripoti hii inatakiwa kuwasilishwa na kujadiliwa na Kamati ya Ithibati ya Tume ya Vyuo Vikuu, ambayo itatoa mapendekezo kwa Tume kuhusu hatua stahiki za maamuzi. Kamati hii itakutana katika kikao cha dharura tarehe 25/02/2016 saa 3:00 asubuhi, na taarifa ya Kamati  hiyo  itawasilishwa  kwenye  Mkutano  wa  dharura  wa  Tume  tarehe hiyohiyo saa 9:00 alasiri.

5. Kwa mantiki hiyo, taarifa rasmi kuhusu maamuzi yaliyofikiwa juu ya hatma ya Kampasi hiyo ya Arusha ya Chuo cha Mt. Yosefu itatolewa siku ya Ijumaa tarehe 26/02/2016.

6.  Kwa taarifa hii, Tume inawaomba wanafunzi wote wa Chuo cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha kuwa watulivu wakati huu ambapo suala lao linashughulikiwa.

7. Tume inapenda kutumia fursa hii pia kuwaarifu wanafunzi wote wa vilivyokuwa Vyuo Vikuu Vishiriki vya Sayansi za Kilimo na Teknolojia (SJUCAST) na Teknolojia ya Habari (SJUCIT), kuwa orodha ya majina yao na vyuo walivyopangiwa inapatikana  katika   tovuti  ya  Tume  ya   Vyuo   Vikuu.  Hivyo  wanashauriwa kuondoka Chuoni  mara moja na kujiandaa kwa ajili ya kuripoti katika vyuo walivyopangiwa katika muhula wa pili.

Imetolewa na

PROF. YUNUS D. MGAYA

Katibu Mtendaji

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania

24 Februari2016

Taasisi ya TWAWEZA Yatangaza Matokeo Ya Utafiti Kuhusu Maoni ya Wananchi Juu ya Mabadiliko Kwenye Sekta Ya Elimu

$
0
0
1. Utangulizi
Mnamo mwezi Februari mwaka 2015, serikali ya Tanzania ilizindua sera mpya ya Elimu na Mafunzo. 

Sera hii imepanua wigo wa elimu ya msingi kwa kuiunganisha na elimu ya sekondari (hii ilikuwa ikitolewa bure na kwa lazima tangu mwaka 2001 baada ya kuanzishwa kwa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi {MMEM}).

Tangu kuchaguliwa kwa Rais John Pombe Magufuli mwezi Octoba mwaka 2015, utekelezaji kikamilifu wa sera hii imekuwa moja ya ahadi kuu za serikali yake. 
Rais Magufuli aliwahakikishia wazazi wenye watoto wanaosoma katika shule za msingi na sekondari katika hotuba yake ya ufunguzi wa bunge la kumi na moja kuwa hawatapaswa kutoa michango yoyote kuanzia mwezi Januari mwaka 2016. 
Rais Magufuli pia alibainisha kuwa fedha zote zitakuwa zikipelekwa moja kwa moja shuleni, na kuongeza kuwa “Nina uhakika fedha hizo zitatumika vizuri, ole wao watakao zitumia vibaya.”

Japokuwa dhamira hii ya kutoa elimu bure mpaka kiwango cha sekondari (kidato cha nne) kwa kila mtoto wa Kitanzania ni hatua kubwa katika historia ya nchi, lakini upatikanaji fursa za elimu siyo changamoto pekee inayoukabili mfumo wa elimu nchini Tanzania. Juhudi zote zitakuwa hazina maana kwa wananchi na taifa kwa ujumla iwapo watoto wanaenda shule lakini hawajifunzi.

Hivyo basi ubora wa elimu inayotolewa ni suala muhimu pia. Ripoti ya Uwezo ya mwaka 2014 inaonesha kuwa asilimia 19 pekee ya wanafunzi wa darasa la 3 ndiyo walioweza kusoma hadithi ya Kiingereza ya kiwango cha darasa la pili 4 .

Tukiangalia ufaulu wa darasa la 7 mwaka 2015, takribani asilimia 68 ya wanafunzi waliofanya mitihani walifaulu 5 . Japokuwa hii ni ongezeko la ufaulu kwa karibu asilimia 11, bado ni idadi kubwa ya wanafunzi wasiofaulu ipasavyo.

Kutokana na umuhimu wa elimu katika maendeleo, na ukizingatia mabadiliko katika sekta ya elimu yanayoendelea nchini hivi sasa, ni vyema kufahamu mitazamo ya wananchi kuhusu mfumo wa elimu ya umma.

Wananchi wana mtazamo gani juu ya hali ya elimu iliyopo hivi sasa? Wana maoni gani juu ya walimu wa shule za umma na ubora wa elimu wanayopatiwa watoto wao? Je wana matarajio yapi kuwa elimu ya bure itaboresha elimu?

Je wazazi wamekuwa wakichangia fedha kiasi gani huko mashuleni, na nini athari za kupigwa marufuku kwa michango yote ya wazazi katika elimu? Na je fedha hizo zimetumikaje?

Muhtasari huu umebeba maoni na uzoefu wa wananchi juu ya utolewaji wa elimu ya msingi ya umma. Tunatumaini matokeo haya yatakuwa mwanzo mzuri wa kupima mafanikio ya utekelezaji wa sera hii mpya kwa siku za usoni.

Takwimu kutoka muhtasari huu zimekusanywa na Twaweza kupitia mpango wake wa Sauti za Wananchi. Sauti za Wananchi ni utafiti unaofanywa kwa njia ya simu za mkononi, wenye uwakilishi wa kitaifa. Utafiti huu unawakilisha Tanzania Bara.

Mambo muhimu kuhusu matokeo haya:

• Asilimia 76 ya wananchi wanaamini kuwa utoaji wa elimu bure utaboresha elimu.
• Asilimia 89 ya wazazi wanasema wanatoa michango ya fedha kugharamia elimu ya watoto wao waliopo shule za umma.
• Asilimia 66 ya michango ya wazazi hulipia ulinzi, asilimia 57 majaribio na asilimia 34 madawati.
• Karibu nusu ya wananchi wanaamini michango inayokusanywa shuleni haitumiki kwenye malengo husika.
• Wananchi 8 kati ya 10 wanaamini kuwa walimu hawapendi taaluma yao.
• Nusu ya wananchi wote wanaona kuwa ubora wa elimu ya msingi umezorota ama kubaki pale pale wakati nusu nyingine wanaona kuwa imeboreshwa. Hii ni ndani ya miaka 10 iliyopita.

2. Mambo sita kuhusu elimu nchini Tanzania

Jambo la 1: Wananchi wana matumaini na ahadi ya elimu bure
Asilimia 97 ya wananchi wanafahamu kuhusu ahadi ya Rais Magufuli ya kutoa elimu bure ya sekondari (kidato nne) kuanzia Januari 2016, kama ilivyoainishwa kwenye sera mpya na ilani ya chama tawala. Vilevile, asilimia 88 wana imani kuwa ahadi hii itatekelezwa kama ilivyopangwa.
Asilimia 76 ya wananchi wanaamini kuwa utolewaji wa elimu bure utaongeza ubora wa elimu kwa kuboresha mazingira ya kufundishia (asilimia 55).

Pamoja na imani hiyo, asilimia 15 ya wananchi walisema elimu ya bure haitaboresha elimu, kwa kuwa kuongezeka kwa uandikishwaji wa wanafunzi kutatumia rasilimali (fedha) nyingi 8.

Asilimia 49 walisema wanafunzi hawatafanya vizuri kutokana na kukatazwa kwa masomo ya ziada ambayo walimu waliyatumia kuwasaidia wanafunzi wasiofanya vizuri huku wakijipatia kipato cha ziada. Pamoja na hayo asilimia 22 wana hofu na upatikanaji wa vifaa vya kutosha vya kufundishia 9 .

Jambo la 2: Asilimia 89 ya wazazi huchangia elimu ya umma
Michango imekuwa ni sehemu ya mfumo wa elimu baada ya upanuzi wa Elimu ya Msingi kwa Wote. Asilimia 89 ya wazazi waliohojiwa walikiri kuchangia fedha kwenye shule za umma.

Wazazi walipoulizwa kuhusu kiwango cha fedha walichochangia, asilimia 80 walisema wamechangia TZS 50,000 ama pungufu kwa mwaka, huku asilimia 8 wakichangia zaidi ya TZS 100,000 .
Michango inayotolewa kwenye shule za umma hutumika kugharamia ulinzi (asilimia 66), majaribio (asilimia 57) na madawati (asilimia 34). Kiwango kidogo hutumika kwenye mahafali (asilimia 4) na safari za kishule (asilimia 4).

Utaratibu wa ugawaji wa fedha za ruzuku ni: asilimia 40 vitabu na nyenzo nyingine za kusomea; asilimia 20 kwa ajili ya vifaa vya kuandikia (kalamu, madaftari, penseli n.k.); asilimia 10 kwa shughuli za kiutawala na asilimia 10 kwa ajili ya makaratasi ya mitihani na uchapishaji. Hivyo basi, maamuzi ya kuwa ruzuku itumike vipi yanakuwa changamoto kwa upande wa shule zenyewe, na hata hivyo, inaonekana wazi kuwa michango hulipia vitu vingi zaidi kuliko ruzuku.

Jambo la 3: Asilimia 49 ya wazazi wanaamini michango ya wazazi haitumiki ipasavyo
Japokuwa wazazi wengi wamekuwa wakitoa michango ya ziada, asilimia 49 ya wazazi wanaamini kuwa fedha hizo hazitumiki ipasavyo. Wazazi wa mjini wana mashaka zaidi ambapo asilimia 57 wanasema hivyo ukilinganisha na asilimia 44 ya wazazi wa vijijini.

Vilevile asilimia 58 ya wananchi wanaamini kuwa michango hii haijaidhinishwa na serikali. Asilimia 89 wanaamini kuwa walimu wa shule za umma huchangisha fedha hizo kama chanzo cha kujipatia kipato cha ziada 11 .

Jambo la 4: Wananchi wanahusisha mafanikio ya ujifunzaji na juhudi za mwalimu
Wananchi walipoulizwa kuwa ni nini ambacho wanadhani kinachangia matokeo ya darasa la saba kwenye jamii yao (kuwa mazuri ama mabaya), nusu yao walihusisha matokeo na juhudi za mwalimu 12 . Asilimia 7 pekee ndio waliotaja changamoto zinazohusiana na wazazi au wanafunzi wenyewe 13 .

Cha kushangaza ni kwamba mwananchi 1 kati ya 3 hajui nini kinachangia matokeo ya kujifunza pindi watoto wanapohitimu elimu ya msingi.

Jambo la 5: Wananchi wanaamini kuwa walimu wanaona fahari juu ya taaluma yao lakini hawapendi kazi yao
Asilimia 93 ya wananchi wanaamini kuwa ualimu ni taaluma ambayo ndiyo msingi wa taifa. Japokuwa asilimia 79 ya wananchi wanaamini kuwa walimu wanaona fahari ya kile wanachokifanya, asilimia 80 wanaona kuwa walimu hawapendi kazi zao na hufanya tu kwa ajili ya kujipatia kipato. Je ni kwanini walimu wanaona fahari ya taaluma yao lakini hawapendi kazi yao?

Kwa mujibu wa baadhi ya wananchi, ni kutokana na mishahara pamoja na mazingira ya kufanyia kazi. Kwa ujumla asilimia 42 ya wananchi wanaamini kuwa walimu hawalipwi vizuri, na asilimia 34 wanaamini mazingira ya kazi ya walimu hayawapi motisha wa kufundisha.

Haya ni maoni ya wananchi wachache (wananchi wengi wanatoa kauli zinazokinzana), lakini yanaweza kutoa mwanga kwanini wananchi wanadhani walimu hawapendi kazi yao.

Wananchi walipoulizwa kuhusu vitu ambavyo vinaweza kuwaongezea walimu motisha ili kutoa elimu bora kwa wanafunzi, asilimia 56 walisema nyongeza ya mishahara na asilimia 19 walitaja uboreshaji wa mazingira ya kazi.

Jambo la 6: Maoni ya wananchi yanatofautiana juu ya ubora wa elimu ya msingi.
Wananchi walipoulizwa kuhusu ubora wa elimu, nusu yao waliamini kuwa ubora wa elimu ya msingi umezorota ama kubaki vilevile kwa kipindi cha muongo mmoja uliopita, huku nusu nyingine wakisema elimu ya msingi imeboreshwa.

Wananchi walio wengi wanaamini njia kuu ya kuboresha elimu ya msingi ni kwa kuweka mkazo kwa walimu. Ili kuboresha elimu wananchi wametoa ushauri ufuatao kwa serikali: kufuatilia utendaji wa walimu (asilimia 40), kuongeza mishahara ya walimu (asilimia 19), pamoja na kuongeza idadi ya walimu (asilimia 10). Asilimia 7 pekee ndiyo waliotaja ushirikiano kati ya
mwalimu na mzazi kama njia ya kuwawezesha watoto kujifunza.


3. Hitimisho
Serikali mpya imejikita kwenye utoaji wa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari na wananchi wamekuwa na imani kubwa juu ya suala hilo. Wananchi wanaamini kuwa utoaji wa elimu bure utatekelezwa katika muda ulianishwa, na ubora wa elimu utaongezeka.

Wasiwasi wa wananchi unaonekana kwenye uwajibikaji wa walimu katika kufikia kiwango cha juu cha elimu. Walipoulizwa kuhusu namna ya kuboresha elimu ya msingi, wananchi walitilia mkazo kwenye mishahara ya walimu, kuongezeka kwa idadi ya walimu mashuleni na zaidi ya yote uwajibikaji
wa walimu.

Siyo wananchi pekee wanaosisitiza uwajibikaji wa walimu. Kwa mujibu wa Davidson, ukosefu wa motisha kwa walimu ni moja ya sababu kuu inayoathiri ubora wa elimu nchini Tanzania 16 .

Utafiti usio rasmi uliofanywa na Twaweza kwa walimu 272 unaonesha kuwa asilimia 96 ya walimu hao hawaridhishwi na kazi zao. 
Pia, mwalimu 1 kati ya walimu watatu alisema asingechagua tena kazi ya ualimu, huku wakitaja mazingira magumu ya kazi (asilimia 34) na mishahara midogo (asilimia 26) kama sababu kuu. Hii inadhihirisha kuwa walimu na wananchi kwa ujumla wana mitazamo inayofanana.

Kwa kuwa uongozi mpya umeweka mkazo suala la elimu, ni vizuri pia ukaanza kutatua matatizo ya walimu na kuboresha mazingira ya ufundishaji Tanzania ili kwenda sambamba na kasi ya utoaji wa elimu.

Wakati utekelezaji wa sera mpya ya Elimu ukiendelea, ni vyema kufuatilia mabadiliko yaliyofanyika na mafanikio yaliyopatikana. 
Kumekuwa na kusitasita kuhusu dhana hii ya ‘elimu bure’ ambapo viongozi wa shule wana mashaka na jinsi ambavyo TZS 10,000 kwa kila mwanafunzi mmoja kwa mwaka inaweza kutosha. Mfano mmoja ni kuhusu suala la ulinzi.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, asilimia kubwa ya michango ya wazazi kwa mwaka 2015 imekuwa ikitumika kwenye ulinzi (asilimia 66); wakati ruzuku inayotumwa shuleni haihusishi suala la ulinzi. 
Iwapo fedha zote zilizotengwa zitapelekwa shuleni na kuwafikia wahusika kwa kiwango kilichopangwa, je kiwango hicho kitatosha kuhakikisha watoto wanajifunza?

Suala jingine la msingi ni kuhusu utunzwaji wa rasilimali. Ruzuku hapo awali zilikuwa zinapelekwa moja kwa moja shuleni mpaka mwaka kufikia mwaka 2002 zilipoanza kupelekwa kupitia kwa mamlaka zaHalmashauri za Wilaya na Miji. 
Kwa sasa mfumo umebadilika ambapo ruzuku zinapelekwa moja kwa moja shuleni. Tunaamini uamuzi wa kupeleka ruzuku moja kwa moja mashuleniumechangiwa na na kutokuwepo kwa ufanisi katika mfumo uliopita.

Kwa mfano, kati ya 2010 na 2013, kwa wastani ni TZS 2,202 pekee ndizo zilizofika shuleni kwa kila mwanafunzi.

Sera mpya ya kupeleka pesa za ruzuku moja kwa moja mashuleni unaibua maswali kadhaa. Tutahakikisha vipi upelekaji wa pesa moja kwa moja kwenye shule utatupa matokeo tofauti?

Je shule zina uwezo wa kusimamia rasilimali hizo vizuri; kuzuia ubadhirifu na upotevu na kuhakikisha zinaelekezwa kwenye matumizi ya vitu muhimu zaidi? Kuna mfumo gani uliopo kwenye ngazi ya shule, hususani katika kuhakiki maamuzi ya matumizi?

Ili kuhakikisha tunapata thamani halisi ya matumizi katika elimu, utoaji na matumizi ya fedha vinapaswa kuhakikiwa katika ngazi ya shule.

Kwa kumalizia, na la muhimu zaidi, utawala mpya umeonekana kuwa kimya kwenye suala la kuboresha matokeo ya ujifunzaji. Ongezeko la shule za msingi kwa mamilioni ya watoto wa kitanzania ni mafanikio makubwa.

Hata hivyo, baada ya miaka kumi ya sera hii, tunatilia shaka anguko la uandikishaji huo wa maelfu ya watoto pasipo kutoa fedha za kutosha, wala kutilia mkazo suala la ubora. Je kutakuwa na walimu wa kutosha kwa wanafunzi hawa? Tutahakiki vipi kama wanajifunza?

Kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita tumeshuhudia ongezeko kubwa la shule za sekondari pamoja na wanafunzi huku ikiambatana na ongezeko kubwa la idadi ya wanafunzi wanaofanya vibaya kwenye mitihani yao ya kidato cha nne. 
Je uongozi huu umejipanga kufanya nini cha tofauti kuhakikisha kuwa Tanzania haiendelei kutengeneza wahitimu mbumbumbu?

Tutahakikisha vipi mfumo wa elimu unawapa watanzania fursa ya kuishi maisha mazuri na kuchochea maendeleo ya nchi? Pamoja na nia njema na maelezo mazuri ya Rais yanayotilia mkazo kwenye elimu na kutoa matumaini mapya, ni muhimu kuzingatia kuwa ufanisi katika sekta hii muhimu utafikiwa kwa kutumia ushirikiano na wadau wote.

Aidha, panahitaji marekebisho mapana zaidi katika mfumo wa elimu ili kufikia malengo ya elimu bure na bora, na sio bora elimu bure!

Mfuko wa Habari Tanzania (TMF ) Wasema Uko Tayari Kutoa Msaada wa Fedha Ili Kuiwezesha TBC Kutangaza LIVE Mwenendo wa Bunge

$
0
0

KILIO cha ukosefu wa fedha za kuonesha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge la Tanzania kupitia Shirika la Utangazaji nchini (TBC) ambacho kimekuwa kikitolewa na serikali, sasa kimepata ufumbuzi.

Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF) umeeleza kwamba upo tayari kutoa fedha zinazohitajika ili kuhakikisha haki ya Mtanzania kupata habari kupitia TBC haiingiliwi wala kubughudhiwa kwa hoja yoyote.

Endapo serikali itakubali ombo hilo, wananchi wataendelea kunufaika na vikao vya moja kwa moja vya bunge tofauti na pendekezo la serikali la kunakili baadhi ya sehemu na kisha kuoneshwa usiku.

Ernest Sungura, Mkurugenzi Mtendaji wa TMF leo jijini Dar es Salaam amewaeleza wahariri wa habari na serikali kupitia mwakilishi wake Assah Mwambene ambaye ni Mkurugenzi wa Habari Maelezo kwamba, taasisi hiyo imejipanga kusimamia na kuhakikisha Watanzania wanaendelea kupata matangazo ya moja kwa moja kutoka bungeni kupitia TBC kwa kuyagharamia.

Sungura amesema kwamba miongoni mwa malengo ya mfuko huo ni pamoja na kuleta mabadiliko katika tasnia ya habari pia kuhakikisha wananchi wanapata taarifa.

Januari mwaka huu, Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alitoa ufafanuzi bungeni kuhusu hatua ya serikali kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya bunge kupitia TBC.

Miongoni mwa sababu alizozieleza ni pamoja na kuwepo kwa gharama kubwa ya Sh. 4.2 bilioni zinazotumika katika uendeshaji wa matangazo hayo ya moja kwa moja kwa mwaka pia watumishi wa serikali kushabikia bunge badala ya kuendelea na kazi ofisini.

Hatua ya serikali kusitisha matangazo hayo iliibua mjadala mkubwa bungeni huku Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) akilitaka bunge kusitisha shughuli zake ili kujadili taarifa hiyo ya serikali.

Nje ya bunge mjadala huo uliendelea bila kupatikana kwa ufumbuzi ambapo TMF imedhamiria kugharamia matangazo hayo ili kuruhusu wananchi kuendelea kupata matangazo hayo kupitia TBC.

Katika mkutano huo, Mwambene amesema kwamba, serikali itafikiria namna ya kupeleka maombi TMF ya uwezeshwaji katika maandalizi ya miswada miwili ya sheria za habari ili kupitisha sheria zenye matakwa ya wadau.

Kuhusu hilo, Sungura amesema taasisi yake iko tayari kuisaidia serikali kwenye mchakato huo na hata kuitisha kongamano kubwa la wadau.

Rais Magufuli Akutana Na Rais Mstaafu Wa Awamu Ya Tatu Benjamin Mkapa Pamoja Na Mjumbe Maalum Wa Rais Wa Guinea Bisau Februari 25,2016

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati alipokuwa akizungumza na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa Ikulu jijini Dar es Salaam Februari 25,2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Benjamin Wiliam Mkapa Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz Ikulu jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine Mjumbe huyo alileta salamu za pongezi kutoka kwa Rais wa Guinea Bisau.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea barua kutoka Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau mara baada ya kupokea barua ya Salamu na pongezi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Genarali Omar Embalo mjumbe Maalum wa Rais wa Guinea Bissau Jose Mario Vaz Ikulu jijini Dar es Salaam

Magazeti Ya KENYA Ijumaa ya Leo Februari 26, 2016

Magazeti Ya TANZANIA Ijumaa Ya Leo Februari 26, 2016

Basi La Mashimba Express La Kahama- Mwanza Lagongana Na Gari Ndogo Na Kuua Watu Wanne

$
0
0
Watu wanne wamefariki dunia katika ajali baada ya basi la Mashimba Express lililokuwa linasafiri kutoka Kahama kwenda jijini Mwanza kugongana na gari dogo  katika eneo la njia panda kuelekea wilayani Kishapu  Mkoani Shinyanga

Ajali hiyo imetokea jana jioni ambapo mashuhuda wa tukio hilo wamedai kuwa ilisababishwa  na  gari ndogo iliyokuwa katika mwendo kasi ambayo ilipoteza uelekeo na kisha kuligonga basi hilo.Watu  wawili  waliokuwa  katika  gari  hilo  akiwemo  dereva  walifariki  dunia  papo hapo

Mganga mfawidhi wa hospitali ya  rufaa ya mkoa wa Shinyanga Dkt Albert George Masigati amesema kati ya saa 12 na saa moja usiku wa kuamkia leo  walipokea miili ya marehemu wanne katika hospitali hiyo ,wote wakiwa ni wanaume na majeruhi wanane,kati yao wanawake wanne na wanaume wanne.

Hata hivyo Dkt Masigati amesema huenda idadi ya majeruhi ikaongezeka kutokana na taarifa kuwa baada ya ajali hiyo kutokea baadhi ya majeruhi walikimbizwa katika hospitali ya Kolandoto na Kishapu.

Dkt Masigati amesema hakuna majeruhi aliye katika hali mbaya na kwamba bado wanaendelea kuwafanyia uchunguzi .

Sabby Angel: Kwa mauno yangu watakaa tu

$
0
0
Msanii wa filamu ambaye hivi sasa amejiingiza kwenye Muziki wa Mduara, Sabrina Omary ‘Sabby’ amefunguka kwamba anajiamini linapokuja suala la kukata viuno kiasi kwamba haoni msanii wa kike wa kumfunika.
 
Sabby ambaye ametoa kibao kinachokwenda kwa jina la Inahusu amesema anajua uwezo wa kuimba anao, ukijumlisha na uwezo wake wa kukata nyonga kana kwamba hana mfupa kiunoni anaamini atatusua kimuziki.
“Mimi najua ninaimba miondoko kama ya Shilole lakini niseme tu kwamba, yeye na wasanii wengine wa kike hakuna wa kunifikia kwa mauno,” alisema Sabby.

Zari Aibu Yake! atupia picha mtandaoni akiwa amelala na Diamond Platnumz

$
0
0
 
Stori: Mwandishi
Wetu, Ijumaa
Dar es Salaam: Aibu yake! Kitendo cha mwandani wa Mwanamuziki wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutupia mtandaoni picha ya nusu utupu akiwa amelala na jamaa huyo, kimetafsiriwa kuwa ni kulipa kisasi kwani miezi kadhaa iliyopita naye alimtundika akiwa anaoga bafuni.
Picha hiyo ya mapema wiki hii, inadaiwa Zari aliitupia kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Instagram kisha kuitoa muda mfupi bila kujua imeshachukuliwa na wapenda ubuyu na kurushwa kwenye meza ya Ijumaa.

DIAMOND FOFOFO
Katika picha hiyo, Zari anaonekana ndiye aliyeipiga ikiwaonesha wakiwa wamelala kitandani huku Diamond akiwa fofofo bila kujua kilichoendelea.
Picha hiyo iliibua gumzo kubwa kwa mashabiki wengi wa mastaa hao huku wengine wakidai kwamba inavyoonekana Zari aliamua kumfanyia Diamond hivyo kwani awali hakupendezwa jamaa huyo alipotupia video yake akioga.

MASHABIKI SASA
Hata hivyo, baadhi ya mashabiki hao walionekana kukerwa na kitendo hicho kwani mwanamama huyo ni kioo cha jamii na kwamba nyuma yake kuna rundo la mabinti ambao wanamuiga kwa kila anachofanya.
“Zari anapaswa kutambua kwamba yeye ni role model wa wasichana wengi ambao huwa wanamfuatilia na kutamani kuwa kama yeye hivyo anachowaonesha hakiendani na matarajio yao. Kwanza yeye ni mama wa watoto wanne, anatakiwa kuachana na mambo hayo,” ilisomeka sehemu ya maoni hayo.
TEAM WEMA NDANI
Kwa upande wao, kundi maarufu linalojiita Team Wema mitandaoni, lilitumia nafasi hiyo kumshambulia kwa kumuita ‘bibi’ anayependa mambo ya wasichana wakati ni mama wa watoto wanne.
“Hivi huyu bibi anajiona bado msichana? Amesahau ana watoto wanne lakini anataka kujilinganisha na Madam ambaye usichana unamruhusu kufanya hivyo,” ilisomeka sehemu ya maoni ya mmoja wa memba wa Team Wema.
KINYUME NA MAADILI
Wengine waliandika kuwa Zari hakupaswa kutumbukiza picha hiyo ya siri mtandaoni kwani kwa mila na desturi za Kibongo siyo sawa.
“Nooo…haya siyo maadili yetu (Watanzania). Kujiheshimu ni kitu cha bure kama mama wa familia. Kwanza anawafundisha nini wanaye na familia yake? Maana unajua sasa hivi Instagram kila mtu anaona kinachofanyika,” alisema shabiki mwingine.
DIAMOND ANASEMAJE?
Baada ya kuinyaka ishu hiyo, gazeti hili lilimsaka Diamond kwa njia mbalimbali ikiwemo kumtafuta katika WhatsApp na kumuuliza ishu hiyo lakini hakujibu.
NI TABIA YA ZARI?
Ukiacha tukio hilo, mara kadhaa Zari amekuwa akitupia picha mbovumbovu za utupu hivyo kuonekana ni hobi yake.
Mbali na yeye mwenyewe kujianika, Zari aliwahi kurekodiwa mkanda mchafu ambao ulidaiwa kusambazwa mitandaoni na aliyekuwa mumewe, Ivan Ssemwanga na swahiba wake, King Lawrence.
Kwa upande wake Zari amekuwa mtu wa kukaa kimya kwa maana ni mtu wa kupotezea (never mind).

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

Vigogo watatu wanusuru hekalu la Dk. Slaa

$
0
0

Vigogo watatu nchini wamejitosa kunusuru nyumba ya ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa kwa kumchangia Sh milioni 300.

Hatua hiyo inaelezwa inatokana na maombi ya mmoja wa watu wa karibu wa Dk. Slaa, kuwaomba vigogo hao kunusuru nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Mtipwa, Mbweni jijini Dar es Salaam, ambayo iliuzwa kwa mnada.

Nyumba hiyo ilinunuliwa kwa mnada mwishoni mwa mwaka jana na mfanyabiashara Hussein Ndama, ambaye aliinunua kwa Sh milioni 110.

Baada ya kuuzwa kwa nyumba hiyo zilianza juhudi kutoka kwa watu waliokuwa karibu na Dk. Slaa kwa kutaka kuikomboa, huku mfanyabiashara huyo akigoma kuiuza kwa bei aliyonunulia na kutaka kuiuza kwa Sh milioni 500.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa, wakati vigogo hao wakijitosa, mawakili wa mke wa Dk. Slaa pia walifanya kazi kubwa, ili kurejesha nyumba hiyo mikononi mwa familia ya Dk. Slaa.

Chanzo cha kuaminika kimesema  kuwa, baadhi ya vigogo hao kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliamua kuingilia kati na kulazimika kuchanga fedha za kukomboa nyumba hiyo.

“Baada ya taarifa za nyumba kutoka kwa watu wa karibu na Dk. Slaa, viongozi watatu waliingilia kati na kuanza kutoa michango yao ambapo zilipatikana Sh milioni 300.

“Vigogo hawa watatu, wawili ni viongozi wa juu wa chama tawala na mmoja ni kiongozi wa ngazi za juu katika shirika la umma (jina linahifadhiwa), na kila mmoja alitoa shilingi milioni 100.

“… tena hilo halikufanyika hivi hivi ila nguvu kubwa ilitumika kuhakikisha hao viongozi wanawasiliana na Ndama (Hussein), ili kumwomba alegeze msimamo wake kuhusu bei ya nyumba aliyonunua. 
“Baada ya majadiliano marefu, Ndama alikubali ingawa kwa masharti zaidi.

"Wakati hilo likifanyika pia mawakili wa mke wa Dk. Slaa walifanya kazi kubwa ili kuweza kurejesha nyumba hiyo katika mikono ya familia ya Dk. Slaa,” kilisema chanzo .

Chanzo hicho kilisema jitihada za vigogo hao zilimfanya Ndama maarufu kwa jina la ‘Ndama mutoto ya ng’ombe’ alegeze masharti ya kiwango cha fedha alichohitaji na hivyo kukubali dau la Sh milioni 300.

Nyumba ilipotoka
Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Chadema, Dk. Slaa na mkewe Josephine Mushumbusi walinunua nyumba hiyo namba 74694, iliyopo katika kiwanja namba 117, kitalu ‘1’ Mbweni JKT.

Nyumba hiyo ilinunuliwa na wawili hao Mei 8, mwaka 2012 kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kwa gharama ya Sh milioni 117.859.

Dk. Slaa aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari Septemba 4, mwaka jana alipokuwa akitangaza kujitoa Chadema, akimshukuru Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa kumsaidia sehemu ya fedha za kununulia nyumba hiyo.

Licha ya sintofahamu hiyo, Dk. Slaa alisema hana ugomvi na Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

“Ninamuheshimu sana Mbowe, sina ugomvi naye maana hata nyumba ninayoishi amehusika kunichangia na hata kunisaidia mambo mengi,” alisema Dk. Slaa.

Jinsi Nyumba ilivyouzwa kwa mnada
Mfanyabishara huyo alinunua nyumba hiyo Desemba 27, mwaka jana kwa mnada uliosimamiwa na kuendeshwa na Dalali wa Mahakama, Bilo Star kwa ajili ya kufidia deni la mkopo wa Sh milioni 52.999 ambalo lilitakiwa kulipwa kufikia Novemba 26, mwaka jana katika Benki ya Equity ya jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa kwamba mke wa Dk. Slaa, Josephine Mushumbusi, ndiye aliyetoa hati hiyo ya nyumba kama dhamana ya mkopo huo uliochukuliwa na mtu anatajwa kwa majina ya Salehe Swedi Nehale wa Kampuni ya ujenzi ya T/A Nehale Building Material Supplies.

Safari ya Nje
Septemba 8, mwaka jana Dk. Slaa, alisema anakwenda Marekani pamoja na familia yake kwa mapumziko.

Akiwa nchini humo kwa ajili ya mapumziko na kujiendeleza katika kozi fupi katika tasnia ya Sheria na Lugha, Dk Slaa alisema nyumba yake itakuwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi.

Akizungumza katika mahojiano yaliyorushwa kituo cha televisheni cha Azam, mwanasiasa huyo, alisema akiwa mapumzikoni Marekani, nyumba yake itakuwa inalindwa na Jeshi la Polisi kutokana na vitisho ambavyo amekumbana navyo tangu alipoamua kuachia ngazi Chadema.

“Ninatishiwa maisha, ni lazima nichukue hadhari….., ninatishiwa kupigwa mawe.Ni kweli ninalindwa na usalama,” alisema Dk. Slaa akiwa anahojiwa na mwanahabari nguli, Tido Mhando.

Credit: Mtanzania

Makontena ya bilioni 6/- ya wakwepa kodi kuuzwa

$
0
0
MALI zenye thamani ya Sh bilioni sita za baadhi ya wadaiwa 16, waliokwepa kulipa kodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kutorosha kontena za mizigo yao kwenye Bandari Kavu (ICD) ya Azam mwishoni mwa mwaka jana, zimekamatwa jana na zinafilisiwa.


Aidha, mali nyingine za thamani ya Sh bilioni 7.4 zimebainishwa na muda wowote kuanzia leo zitakamatwa ili kufilisiwa kwa lengo la kulipa kodi inayodaiwa na TRA.
Hayo yalibainishwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Udalali ya Yono, iliyopewa kazi ya kufuatilia wadaiwa hao, Yono Kevella alipokuwa akizungumzia kuanza kwa kazi ya kukamata mali za wadaiwa hao na kufilisiwa.

Kevela alisema baada ya kuisha muda wa siku 14, walioutoa kwa wadaiwa 24 kulipa madeni yao ya Sh bilioni 18.95, hadi juzi ni wadaiwa nane tu waliweza kulipa, hivyo hao 16 hawakulipa na mali zao ndio zimeanza kukamatwa na kufilisiwa.
Aliwataja wadaiwa ambao mali zao zimekamatwa na wamekubali wenyewe zifilisiwe kulipa deni hilo kuwa ni Tifo Global Trading Co Ltd wanaodaiwa Sh bilioni 1.57 na Lotai Steel Tanzania Ltd wanaodaiwa Sh bilioni 5.47.

Alisema wadaiwa hao ni wawekezaji kutoka China na wamekubali kwa hiari yao mali zao zifilisiwe kulipa deni wanalodaiwa. Mali zilizokamatwa na ziko tayari chini ya kampuni hiyo ya Yono ni kontena tisa za mabati, zenye thamani ya Sh bilioni sita.

‘Nitumie fursa hii kuwaalika wananchi wote wanaohitaji mabati waje ofisi za kampuni yetu kununua mabati hayo, yako mengi ni kontena tisa, tunachofanya si kumuonea mtu, bali tunatekeleza wajibu wetu tuliopewa wa kuhakikisha kodi ya serikali inalipwa”, alisema Kevella.

Alisema kazi ya kukamata mali za wadaiwa wengine 14, zinaendelea na ndani ya wiki moja kazi hiyo itakuwa imekamilika na iwapo wahusika wote hawatapatikana, Kampuni ya SSB ambayo ndiyo mmiliki wa bandari kavu ya (Azam ICD) na kampuni ya wakala wa forodha ya Regional Cargo Services, watahusika kulipa deni linalobaki.

‘Kwa wale tutakaoshindwa kuwapata au kukamata mali za kutosha kulipa deni wanalodaiwa, mmiliki wa bandari kavu ya Azam ICD, na kampuni ya wakala wa forodha ya Regional Cargo Services, watapaswa kulipa”, alisisitiza Kevella.

Kevella alisema jana jioni walitarajia kukamata mali nyingine za Sh bilioni 7.4 za mdaiwa Tuff Tyres General Co Ltd, ambaye amekimbilia kufungua ombi mahakamani lakini Mahakama haijatoa uamuzi.
Alisema wameshazibainisha mali za mdaiwa huyo, ikiwa ni pamoja na jengo la ghorofa, matairi na nyumba iliyopo Msasani, ambazo zote kwa pamoja zikifilisiwa zitalipa deni la Sh bilioni 7.4 anazodaiwa.

CHANZO: HABARI LEO -  Imeandikwa na Ikunda Erick

Cannavaro arejea kwa mkwara kilo 200

$
0
0
Beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Dar es Salaam
BAADA ya beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kupewa nafasi kikosini juzi Jumatano tangu arejee kufuatia kupona majeraha, ametamba kuwa yupo vizuri na atamuondoa Mtogo, Vincent Bossou na kurejea katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
 

Tangu Novemba, mwaka jana, Cannavaro alikuwa nje ya uwanja akiuguza majeraha ya kisigino kabla ya kupona hivi karibuni na kupangwa kwenye mechi hiyo ya Kombe la FA dhidi ya JKT Mlale waliyoshinda 2-1.
 

“Naweza kukutolea mfano wa (Vincent) Kompany yule wa Manchester City, yeye ni nahodha kama nilivyo mimi hapa na ana uwezo mzuri, inajulikana hata akikaa nje kwa majeraha lakini akirejea na kufanya mazoezi kwa bidii anarejea kwenye nafasi yake.
 

“Mwamuzi wa mwisho katika hili ni kocha mwenyewe lakini kwa upande wangu nipo fiti, nitaendelea kujifua na ninaamini nitarejea kwenye nafasi yangu. Uzuri ni kwamba kikosi chetu ni kipana na hata nilipoumia wengine waliziba nafasi kama kawaida, nashukuru katika hilo,” alisema Cannavaro.
 

Awali, Bossou alionekana hana nafasi lakini ndiye ambaye alipata nafasi ya kucheza kwa kiwango kizuri katika kipindi chote ambacho Cannavaro alikuwa nje ya uwanja hasa katika mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Simba waliyofanikiwa kushinda mabao 2-0.

Donald Ngoma aondoka nchini, kukosa mechi ya Mouritius kwenye Uwanja wa Taifa

$
0
0


MSHAMBULIAJI wa Yanga, Donald Ngoma anatarajiwa kuukosa mchezo wa kimataifa kesho Jumamosi wakati timu yake itakapopambana na Cercle de Joachim ya Mouritius kwenye Uwanja wa Taifa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga inatarajiwa kuvaana na Cercle de Joachim baada ya awali kupata ushindi wa bao 1-0 nchini Mouritius, ambapo mfungaji alikuwa ni Ngoma.
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro amesema Ngoma amefiwa na mdogo wake, taarifa ambazo alizipata juzi Jumatano mara baada ya mechi dhidi ya JKT Mlale kwenye Uwanja wa Taifa na aliondoka alfajiri ya jana kuelekea msibani.
“Amefiwa na mdogo wake wa baba mmoja ambaye alikuwa kama mwanaye, Ngoma ndiye aliyekuwa akimlea, ameondoka leo (jana) alfajiri,” alisema Muro na kuongeza:
“Mdogo wake alifariki uwanjani wakati anatolewa kwa ajili ya kupelekwa hospitali, aligongana na mwenzake wakati wa kuwania mpira.
 “Tumempatia muda wa mapumziko wa wiki moja kisha akimaliza arejee nchini ambapo anatarajiwa kurejea kabla ya mechi dhidi ya Azam (Machi 5, 2016).”Aidha, Muro alisema kambi ya Yanga ipo kamili kwa ajili ya mchezo huo wa kesho, ambapo pia watawakosa Haruna Niyonzima na Salum Telela ambao ni majeruhi huku akisema kiingilio cha chini katika mchezo wa kesho kitakuwa shilingi 5,000.
Wakati huohuo, kikosi cha Cercle de Joachim kiliwasili jijini Dar es Salaam, jana saa 12 jioni. Akizungumza na gazeti hili mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kocha wa timu hiyo, Abdel Ben Kacem alisema:
“Tumekuja na wachezaji 21 na viongozi sita, tupo kamili na tunajua kuwa Yanga wameshinda mechi yao ya juzi. Tuna matumaini makubwa ya kupata ushindi, sisi kuwa ugenini siyo tatizo.”
CHANZO: CHAMPIONI



Kidoa adaiwa kutoka na mume wa mtu!

$
0
0
Asha Salum ‘Kidoa’ na anayedaiwa kuwa mme wa mtu wakiwa katika pozi.
Stori:  Hamida Hassan na Mayasa MaRiwata
Staa anayeibukia, Asha Salum ‘Kidoa’ wiki hii anatengeneza habari baada ya kudaiwa kuwa, hivi karibuni alikwapua mume wa mtu na kwenda kula naye bata huko Dubai.
Chanzo makini kilicho karibu na Kidoa kililitonya Ijumaa kuwa, Video Queen huyo kwa sasa amegombana na mpenzi wake aitwaye Mussa Masood ambaye alikuwa akimgharamia kila kitu kisa kikiwa ni safari ya Dubai ambapo alikwenda na mume wa mtu aliyefahamika kwa jina la Haidari.
“Hivi mnajua kuwa Kidoa na Mussa kwa sasa si wapenzi tena? Kama hamjui, habari ndiyo hiyo. Wamezinguana baada ya Kidoa kwenda kula bata na mume wa mtu anayeitwa Haidari,” kilidai chanzo hicho.
Kidoa (4)Baada ya habari hii kutua Ijumaa mwandishi alimtafuta Mussa ambaye alifunguka: “Dah! Sijui nianzie wapi lakini ukweli Kidoa amenikata stimu, sina hamu na mwanamke, nimemgharamia sana mpaka niliingia shoo room kununua gari kwa ajili yake lakini kumbe niliingia chaka.”
Musa aliongeza kuwa, siku kadhaa zilizopita walitofautiana kidogo lakini akashangazwa na taarifa kuwa, mchumba wake huyo alionekana akiwa na mwanaume aitwaye Haidari maeneo ya Sinza jijini Dar.
Kidoa (5)“Nilimpigia simu na alipopokea alikataa kuwa na mwanaume huyo, akanitajia msichana ambaye yuko naye wakati ni uongo.
“Sikujali niliendelea na kazi zangu lakini baada ya siku mbili niliona Kidoa akiwa ametupia picha yuko Dubai na hiyo ni baada ya kumpigia simu hapatikani, nilipopeleleza niliambiwa amekwenda na Haidari ambaye namjua ni mume wa mtu, nahisi mpaka sasa yuko naye,”  alisema Mussa.
Kidoa (3)
Baada ya Mussa kufunguka hayo, mwandishi wetu alimwendea hewani Kidoa ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Du! Huyo Mussa nilimuacha siku chache kabla sijaenda Dubai na huyo mwanaume anayenitajia simjui, nilienda na mtu mwingine,” alisema Kidoa.

CHANZO: GPL

MAWAZIRI WAPEWA MWISHO LEO KUJAZA TAMKO LA MALI NA MADENI, HATI YA UADILIFU

$
0
0
Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa  ofisi ya Waziri Mkuu wakati alipotoa maagizo ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kuhusu  mawaziri ambao bado hawajajaza fomu za  Tamko la Rasilimali na Madeni wawe wamejaza fomu hizo na kuzirejesha katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam ifikapo leo saa 12.00 jioni (Ijumaa, Februari 26, 2016).(PICHA NA JOHN BUKUKU- WA FULLSHANGWEDAR ES SALAAM)
kas2
Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa akiendelea kufafanua mambo kadhaa kwa wanahabari katika mkutano huo kushoto ni WAZIRI wa nchi,ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala bora, Mh Angella Kairuki

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amesema mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wawe wamejaza fomu hizo na kuzirejesha katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam ifikapo leo saa 12.00 jioni (Ijumaa, Februari 26, 2016).
Agizo hilo la Rais limetolewa leo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam.
“Mheshimiwa Rais ameelekeza mawaziri ambao hawajajaza tamko la rasilmali au hati ya ahadi ya uadilifu wafanye hivyo na kuzirejesha kabla saa 12 jioni na Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake,” amesisitiza Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu amesema wakati akifungua mafunzo ya Mawaziri na Naibu Waziri kuhusu Mwongozo wa Maadili ya Viongozi wa Umma na Utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu yaliyofanyika Ikulu jana (Alhamisi, Februari 25, 2016) alikabidhiwa majina ya Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao hawajawasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili.
Amewataja mawaziri wanaotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Bw. January Makamba. Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye anatakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye anatakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa  Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina anatakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma.

Rais Magufuli aagiza mawaziri wasiolejesha hati za tamko la mali na ahadi ya uadilifu kufanya hivyo kabla ya saa 12 jioni leo - la sivyo Watafutwa Kazi

$
0
0

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli amesema mawaziri ambao hawajajaza Tamko la Rasilimali na Madeni wawe wamejaza fomu hizo na kuzirejesha katika Ofisi za Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Dar es Salaam ifikapo leo saa 12.00 jioni (Ijumaa, Februari 26, 2016).

Agizo hilo la Rais limetolewa leo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika ofisini kwake, Magogoni jijini Dar es Salaam.

“Mheshimiwa Rais ameelekeza mawaziri ambao hawajajaza tamko la rasilmali au hati ya ahadi ya uadilifu wafanye hivyo na kuzirejesha kabla saa 12 jioni na Waziri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hili atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye nafasi yake,” amesisitiza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema wakati akifungua mafunzo ya Mawaziri na Naibu Waziri kuhusu Mwongozo wa Maadili ya Viongozi wa Umma na Utekelezaji wa Ahadi ya Uadilifu yaliyofanyika Ikulu jana (Alhamisi, Februari 25, 2016) alikabidhiwa majina ya Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao hawajawasilisha Tamko la Rasilimali na Madeni kwa Kamishna wa Maadili.

Amewataja mawaziri wanaotakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilimali pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Charles Kitwanga na Waziri wa Nchi (OMR – Muungano na Mazingira), Bw. January Makamba.
 
 Wengine ni Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa, Dk. Augustine Mahiga ambaye anatakiwa kurejesha hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako ambaye anatakiwa kutoa tamko la rasilmali na madeni.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa  Nchi (OMR – Mazingira), Bw. Luhaga Mpina anatakiwa kurejesha fomu za tamko la rasilmali na madeni pamoja na hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma
Tazama video hii kumsikiliza Waziri mkuu akuongea.

YANGA YAWANASA MATAPELI WAKITENGENEZA TIKETI FEKI MANZESE, YASITISHA UUZWAJI WA TIKETI ZA KESHO

$
0
0



Kazi imeanza na Yanga wanaonekana kuingia kwenye vita ya kuwakomesha wanaopenda "dezo".


Matapeli wengi hawapendi kufanya kazi na wanapenda vitu laini tu huku wakijua wengine wanahangaika.

Yanga wamepania kupambana nao na kukomesha hilo baada ya kuwanasa jumla ya washukiwa wanne ambao walikuwa wakitengeneza tiketi feki za mchezo wa leo dhidi ya Cercle de Joachim ya Mauritius.




Yanga itakuwa uwanjani kesho kesho kuwavaa Cercle katika mchezo ya pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya awali, huku Yanga ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 ugenini wiki mbili zilizopita.



Mkuu wa Kitengo cha Habari wa Yanga, Jerry Muro amesema katika oparesheni yao jana wamewakamata watu wanne maeneo ya Manzese jijini Dar es Salaam wakijaribu kucheza mchezo huo wa kitapeli na adui dhidi ya mali za klabu hiyo.
 

Amesema wanaendelea watu hao wako chini ya Jeshi la Polisi Tanzania ambalo limewashikiliwa wakiendelea kufanua uchunguzi kujua wahusika wakuu kabla ya ufikishwa kwenye vyombo vya dola.


Alisema kutokana na tukio hilo, mashabiki kuwa makini katika ununuaji wa tiketi.

Pia akasema hivi, jana walilazimika kusitisha baadhi ya vituo vya uuzaji wa tiketi hizo na kubakisha vituo viwili tu; klabuni na Karume wakati leo tiketi halisi zitakuwa zikipatikana kwenye Uwanja wa Taifa.

“Nianze kwa kutoa tahadhari kwa wadau wote kuwa makini, wajichunge na matapeli. Kuna  watu mitaani wanatengeneza tiketi bandia, leo (jana) katika ucunguzi wetu tumewfanikuwa kukamata watu wanne, wengine walivyotuona wakakimbia. Watu hao tunawashikilia na tuaendelea kuchunguza kujua akina nani wako nyuma yao, kisha tutawafikisha polisi," alisema Muro.

JUMA KASEJA SASA BABA WA FAMILIA, MAPACHAAAAAAAAAA

$
0
0

Familia ya Juma Kaseja, sasa imeongeza wageni wawili.

Mkewe Nasra Nassor amejifungua watoto wawili juzi, ni jambo la faraja kwa familia hivyo.

Kaseja ni kipa wa Mbeya City ambaye amepita katika timu kadhaa na mchango wake katika soka nchini ni mkubwa.

Kaseja alianza kutamba na Moro United kabla ya kujiunga na Simba, baadaye Yanga na baadaye Mbeya City ambako yuko hadi sasa.

Breaking News: TCU Yakifuta Chuo Kikuu cha St. Joseph Kampasi ya Arusha.......Wanafunzi Watahamishiwa Vyuo Vingine

$
0
0
1.Tunapenda kuuarifu umma kwamba, Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha ni mojawapo ya vyuo vikuu vilivyosajiliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ambacho kilianza kudahili wanafunzi kwa mara ya kwanza mwaka wa masomo 2013/2014.

2.Kwa mujibu wa kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Vyuo Vikuu, Sura ya 346 ya Sheria za Tanzania, Tume ina mamlaka ya kusimamia na kudhibiti ubora na usimamizi wa uendeshaji wa Vyuo Vikuu hapa nchini.
 

3.Kwa muda mrefu na kwa wakati tofauti kumekuwapo na matukio ya migogoro baina ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha na wanafunzi. 
Kwa kipindi hiki chote Tume imekuwa ikifuatilia kwa karibu chimbuko la migogoro hiyo na kuchukua hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo kwa uongozi wa chuo kurekebisha kasoro zinazosababisha migogoro chuoni hapo.
Kwa sehemu kubwa migogoro hiyo imekuwa ikitokana na matatizo ya ubora, uongozi, ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji wa chuo kikuu kama zilivyobainishwa na Sheria ya Vyuo Vikuu. 
Hata hivyo jitihada za Tume ya Vyuo Vikuu kukitaka Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) Kampasi ya Arusha kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa katika Kampasi hii inakidhi viwango vya ubora vilivyowekwa na Tume hazikupewa uzito stahiki na uongozi wa chuo.
 

4.Hivi sasa Kampasi ya Arusha ina jumla ya wanafunzi 1557 wanaosoma programu za masomo ya ualimu wa sayansi zifuatazo:
5.Kutokana na yaliyobainishwa hapo awali, tunapenda kuuarifu umma kwamba, Tume imejiridhisha kuwa Kampasi ya Arusha ya Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania imepoteza sifa na vigezo vya kuendelea kutoa elimu ya chuo kikuu. 
Kwa kuzingatia ukweli kwamba wanafunzi ndio waathirika wakuu wa matatizo yaliyopo kwenye Kampasi hii, Tume imeamua kama ifuatavyo:
 

a)Imefuta kibali kilichoanzisha Kampasi ya Arusha ya Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Tanzania (SJUIT) na kuidhinisha uhamisho wa wanafunzi wote waliokuwa wanasoma katika Kampasi hiyo ya Arusha kwa gharama za Chuo Kikuu cha SJUIT. Orodha ya majina yao na vyuo watakavyopangiwa itatangazwa na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

b)Imefuta udahili wa wanafunzi wapya katika programu ya shahada ya miaka mitano ya ualimu wa sayansi. Na kwamba, wanafunzi wanaoendelea na masomo katika programu hii watahamishiwa katika Kampasi ya Luguruni, Dar es Salaam, na watalazimika kwanza kuhitimu katika ngazi ya Stashada (Diploma) kama ilivyokuwa imeidhinishwa na Tume hapo awali. Utaratibu wauhamisho wa wanafunzi wa programu hii utatangazwa hivi punde na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu.
 

c) Imeidhinisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza ambao hawakuweza kupata udahili katika vyuo vikuu vingine, kutoka katika kundi la wapatao 500 waliofukuzwa chuoni kutokana na migogoro iliyojitokeza katika Kampasi ya Arusha mwezi Juni, 2015 kuendelea na masomo katika vyuo watakavyopangiwa baada ya taratibu za uchambuzi wa taarifa zao kukamilika. Orodha ya majina yao na vyuo watakavyopangiwa itatangazwa na kuwekwa katika tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

6.Kufuatia uamuzi huu, wanafunzi wote wanaosoma katika Chuo Kikuu cha Mt. Yosefu Kampasi ya Arusha wanaarifiwa kuwa watahamishiwa kwenye vyuo vikuu vingine vinavyofundisha programu za masomo zinazofanana na masomo wanayosoma hivi sasa chini ya utaratibu na masharti yafuatayo:
 

 i)Wanafunzi wote wanapaswa kuondoka chuoni mara moja baada ya kukamilisha taratibu za kukabidhi mali na vifaa vingine vya chuo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.
 

 ii)Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti kwenye vyuo watakavyopangiwa wakati wa kufunguliwa kwa muhula (semester) wa pili. Tarehe halisi ya kuanza kwa muhula wa pili kwa kila chuo watakachopangiwa itatangazwa na kuwekwa kwenye tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.
 

 iii)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi katika masomo yafuatayo watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM):

     a)Bachelor of Science in Education with Mathematics & Chemistry;

   b)Bachelor of Science in Education with Physics & Chemistry, na

   c)Bachelor of Science in Education with Physics & Computer Science.
 

 iv)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi na Kompyuta (Bachelor of Science in Education with Mathematics & Computer Science) watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha (RUCU):
 

 v)Wanafunzi wanaosoma shahada ya miaka mitatu ya ualimu wa sayansi katika masomo yafuatayo watahamishiwa katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Mwenge (MWECAU):

  a)Bachelor of Science in Education with Physics & Mathematics; na

  b)Bachelor of Science in Education with Biology & Chemistry.

vi)Orodha ya wanafunzi waliohamishwa na majina ya vyuo vikuu walivyohamishiwa itatangazwa na kuwekwa kwenye tovuti ya Tume ya Vyuo Vikuu hivi punde.
 

 vii)Wanafunzi wote waliohamishwa ambao hawakukamilisha mitihani yao ya mwisho wa muhula wa kwanza, au hawakufanya kabisa mitihani hiyo, watatakiwa kufanya mitihani hiyo katika vyuo vikuu watavyohamishiwa kwa utaratibu maalum utakaondaliwa na chuo husika.
 viii) Kila mwanafunzi anawajibika kutunza kumbukumbu zake zote muhimu za maendeleo ya kitaalama kwa ajili ya matumizi ya baadaye, ikiwa ni pamoja na matokeo ya mitihani aliyokwishafanya.
 

ix)Wanafunzi wote ambao ni wanufaika wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, mikopo yao itahamishiwa katika vyuo wakapokuwa wamehamishiwa.
 

7.Kampasi nyingine za Chuo Kikuu cha SJUIT (Luguruni na Boko – Dar es Salaam; na Makambako – Njombe) zitaendelea na masomo kama kawaida.
 

8.Kwa taarifa hii, vyuo vikuu vyote nchini vinakumbushwa kufuata sheria na kuzingatia utoaji wa elimu inayokidhi viwango vya ubora vinavyokubalika kitaifa na kimataifa. Tume haitasita kuchukua hatua stahiki kwa chuo kikuu chochote kitakachobainika kutoa elimu isiyokidhi viwango vya ubora kwa kisingizio cha aina yoyote.
 

Imetolewa na

PROF. YUNUS D. MGAYA
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania 
26 Februari 2016

Orodha Ya Majina ya Wanafunzi wa St. Joseph Kampasi ya Songea Waliohamishiwa Vyuo Vingine Baada ya TCU Kukifuta Chuo Hicho

$
0
0
http://www.tcu.go.tz/images/pdf/Students%20from%20SJUCAST%20&%20SJUCIT%20%20to%20other%20institutions_25_02_2016.pdf

The Tanzania Commission for Universities (TCU) wishes to inform the general public and particularly students, who were undertaking their studies at St Joseph University College of Agricultural Sciences and Technology (SJCAST) and St Joseph University College of Information Technology (SJCIT) in Songea, that we have transferred the respective students to other universities. 

These students are required to report to the receiving institutions upon the opening of the second semester.

The dates for opening of the second semester for each receiving institution will soon be communicated through TCU website and websites of respective institutions.
 
Meanwhile, TCU hereby releases the list of names of the transferred students, which contains receiving institutions and the programmes they have been transferred to.
 
TCU would also like to inform respective students including those with Diplomas that there are names of some students, which are yet to be posted as we are continuing with the verification of their data. 

These names shall be posted as soon as the verification exercise is completed.
 
For further information or clarification please contact the Tanzania Commission for Universities through the following numbers;
 
Landline: +255 (0) 222 772 657 
Hotlines : +255 (0) 683 921 928
                +255 (0) 675 077 673
Viewing all 12768 articles
Browse latest View live




Latest Images